Reader Settings

Hamza  akiwa ndani ya gari na   Dina alimwambia  kile ambacho kimetokea  mpaka namna alivyojiandikisha na Regina  na kuwa wanandoa kisheria.

Ijapokuwa Dina alikuwa mtulivu wakati wa kumsikiliza  Hamza , lakini mara baada ya kusikia Hamza alikuwa amesajili ndoa   na mwanamke mwingine alijikuta akishikwa na huzuni.

Lakini hata hivyo aliona  haiwezekani  yeye kuja kuwa mke wa Hamza kwani hakuwa na vigezo hivyo.

“Kwahio kwanzia sasa  utakuwa chini ya ulinzi wa mke wako na kuwa ngumu kwetu kuonana ,  sijui  mimi  Dina nimekosea wapi  katika ulimwengu huu”Aliongea  na kumfanya Hamza  asijue alie au acheke.

“Hapo ndio unapokosea , kasema licha ya kuandikisha ndoa niharakishe kutafuta mwanamke na  ataachana na mimi baada ya  nafasi yake katika kampuni kuimarika”Aliongea Hamza

Dina  mara baada ya kusikia hivyyo alijikuta  akimuonea huruma  na kumdharau kwa wakati mmoja Regina.

“Regina ni mwanamke asiejua  ana bahati kiasi gani lakini anachezea, kuolewa na mtu kama wewe ni zaidi ya  faida ya vizazi na vizazi”Aliongea Dina.

“Dina huwezi kurahisisha  mambo , kwa  nafasi yake  huwezi kumlaumu yeye sio kama sisi  tuliozea kuona damu , nadhani baada ya kugundua nimeua mtu  jana  ameona hata swala la kuandikisha ndoa  amekurupuka”Aliongea Hamza lakini upande wa  Dina alimuona Hamza kama anatafuta sehemu ya kulalamikia.

“Naona unafikiria sana , sio kawaida yako,  kwa haraka haraka unaonekana kumpenda, ni kitu gani cha pekee ambacho  kimekuvutia kutoka kwake?”

“Ushaanza kujilingansha  sasa , hebu acha kufikiria mbali kwangu mimi wewe ni  mtu muhimu ambae siwezi kukupoteza.. Regina sijafahamiaa nae kwa muda mrefu na kuna uwezekano pia naweza nisiendelee kuwa nae muda wowote  lakini angalau  najua wewe huwezi kunikimbia”Aliongea  Hamza na kumfanya Dina kujisikia utamu.

“Sawa , ila acha sasa kufikiria  maswala ya  Regina , mimi naamini   anakupenda pia  na muda wowote atazielewa hisia zake , leo ngoja ukapoteze mawazo  yako Club”

“Ni Club gani tunaelekea?”

“Tanganyika Club  ushawahi kuingia?”Aliuliza  Dina.

“Naionaga sijawahi kuingia”

“Sasa Tanganyika ndio moja ya Club ya kifahari  hapa  nchini yenye kila aina ya  starehe  kuna hadi sehemu ya  kujifunza kutumia bunduki  halisi  kulenga shabaha,  kiingilio cha chini kwa mwezi ni milioni therathini na tano  na pia lazima upendekezwe na  mwanachama, wanaoingia  humo ni wa hadhi ya juu  mno”

“Mbona kama unapanga  kunipeleka kulenga shabaha na  bunduki?”

“Ni mpango wangu pia, nimekuona  mara kadhaa ukipigana lakini sijawahi kukuona ukitumia bunduki , nataka nione kama unanizidi”

“Dina  unajua unazidi kuwa tofauti na wanawake wa kawaida  kutokana na hobi zako”

“Kwahio unamaanisha  hupendi.. kama ndio hivyo  turudi”Aliongea Dina na Hamza aliishia kutingisha kichwa chake kukataa na kuendelea kuendesha gari.

Dakika kadhaa mbele waliweza kufika  Posta na kuingia kwenye jengo kubwa ambalo halijaenda sana hewani  , lilikuwa limejengwa kwa  kuigiza muundo  wa meli , sehemu hio ndio ilikuwa ikipatikana Club na hoteli maarufu ya matajiri  ya Tanganyika.

Licha ya Club  hii kuwa ndani ya Tanzania lakinni ni asilimia   kumi  tu pengine  pungufu zaidi ya  walioingia  ndani ya Club  hio kuwa watanzania, ukiachana na kwamba matajiri wa kibongo  huingia ndani ya  club hio  ila ni wachache sana,  raia wengi wa Kigeni ambao walikuwa  wakiingia  nchini kwa ajili  ya kufanya anasa  lazima wafikie katika hio Club , ilikuwa  maarufu Afrika mashariki na kati yote.

Taarifa ambazo  hazikuthibirishwa ilisemekana  inamilikiwa na familia moja ya kitajiri  kutoka Scotland  maarufu kama Keswick  kupitia  asset zao ndani ya Mandarlin oriental luxury

hospitality,Uwekezaji huo mkubwa ulitekelezwa

kipindi cha uongozi wa Mheshimiwa Mgweno.

Mara baada ya kuingia  ndani ya  lango la  hoteli na Club hio  Hamza alikabidhi funguo  kwa  Valet  na kutokana na  Dina pia kuwa moja ya  wanachama  ndani ya Club hio  alikuwa akiruhsiwa  kuingia na tafiki.

Mara baada ya kuingia katika Korido ndeefu  Dina alikunja kulia kwake na kuhamia katika Korido nyingine  na  hapa ndio  Hamza alijua ni kipi kinaendelea ,  ndani ya  eneo hilo kulikuwa na  skrini zilizofungwa ukutani kama TV na zilikuwa zikionyesha kila aina ya Bunduki inayopatikana kwa ajili ya  kulengea shabaha. 

Kila mtu alikuwa na starehe  yake na hili lilizingatiwa ndani ya hoteli hio , wengine starehe yao pengine ni kuzima shauku zao katika matumizi ya  siraha na sio kuishia kuziona kwenye filamu tu  na hiki ndio kilichokuwa kikipatikana ndani ya  club hio , ukitaka kuwa  Mdunguaji ama kujifunza kuwa Mdunguaji basi hio ndio sehemu yenyewe.

Upande wa Hamza kila bunduki alioweza kuona  alikwua ashaitumia hivyo  ni kama hakuwa na ile shauku kubwa.

“Dina!!”

Ghafla tu sauti  ya kiume iliita kutoka nyuma yao  na kufanya wageuke.

Alikuwa ni bwana mmoja  mwenye muonekano wa kipole  alievalia suti nyyeupe  pamoja na miwani. “Huyu mwanaume ni nani , usiniambie ndio boyfriend wako?”Aliongea mara baada a kuwakaribia  na alimwangalia Hamza kwa macho yasiokuwa na ishara ya urafiki, alikuwa hajapenda kabisa namna ambavyo  Hamza na  Dina   walivyoshikana mikono. 

“Robert  umekuwa  na shauku ya kumjua , huyu sasa ndio mpenzi wangu”Aliongea Dina na kisha alimtambulisha Hamza.

“Hamza huyu ni Robert  mtoto wa Eliasi  mheshimiwa raisi anaemaliza  muda wake, ni  Mbunge na msimamizi mkuu wa  mahoteli yote  ya Tanganyika”Aliongea Dina.

“Hello Mr Robert!”Aliongea Hamza na kunyoosha mkono kusalimiana nae.

“Sijaona ubora wowote  uliokuwa nao tofauti na mimi , ukiachana na muonekano wako wa kuchanganya rangi, nimemfuatilia Dina kwa mwaka sasa  lakini kila siku ananikataa , nataka kujua ni kipi ambacho  kinakufanya kuwa bora zaidi yangu”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kucheka.

“Sijajua anachonipendea labda ni kwasababu  mimi ni handsome zaidi kuliko wewe”Aliongea na kumfanya Dina  kumpiga Hamza na kiwiko  akimwambia atulie.

“Haiwezekani ,  kinachokubeba ni huo muonekano wako wa kuchanganya rangi lakini  kimavazi na kila kitu nimekuzidi “

“Labda nikwasababu namridhisha kwenye sita kwa sita  wanawake hawajawahi kueleweka wanachopenda kwa  mwanaume”Aliongea Hamza.

“Hebu  acha kuongea , unamaanisha nini?” Dina hakutaka  Hamza aendelee kuongea maana  alijikuta akishikwa na aibu.

“Dina kwahio ndio  sababu ya kunikataa , kwanini usingeongea  tu , niko vizuri  pia kwenye sita kwa sira  na kama usingeridhika ningetumia  hata mkongo kwa ajili yako”

“Robert usimsikilize Hamza anakutania tu , sijakukataa kwasababu huna vigezo ni kwasababu  kazi  yangu  haieandani vyema na  kazi yako  na ya baba yako, sidhani pia  kama natosha  kwako , isitoshe hili ni swala la kihisia zaidi”

“Hilo sio tatizo Dina , nilikupenda siku ya kwanza nilipokuona  ndani ya mgahawa wako…”

“Robert  naomba unisamehe lakini  sitaki kuendelea na haya mazungumzo mbele ya Hamza”Aliongea na kumfanya  Robert kuonekana kutoridhika hasa alipomuangalia Hamza.

Upande wa Hamza  aliona  huyo bwana anafurahisha , alikuwa ni kama mtoto  ambae amekasirika  baada ya kunyimwa hitajio lake , kariba  ambayo kwa bahati mbaya haikuendana na Dina kabisa.

Muda huo Wenza wengine waliingia ndani ya eneo hilo na kumfanya Hamza kuwashangaa baada ya kuwajua .

Alikuwa ni bosi Side Mkrugenzi wa Vodocum Tanzania  alieambatana na Salma ambae  alidhalilika  mbele ya Fellini wa kamapuni ya  kimavazi ya Zara..

“Mr Hamza?”Aliita Saidi.

“Bwana Saidi  kumbe  na wewe ni mhudhuriaji hapa?”Aliongea Hamza huku akitoa tabasamu la utulivu.

“Side unamfahamu?”Aliongea Salma akijifanyisha eti hamjui  Hamza.

“Ndio namfahamu , mbona kama na wewe unamjua?”Aliongea Saidi   na kumfanya  Salma mwili wake kukakamaa , alihitaji kujizuia kadri awezavyo asije kuongea upuuzi kama wakati ule.

“Ndio nilifahamiana nae katika harakati za kazi”Aliongea Salma.

“Kumbe mnafahamiana ne , Hamza  huyu  ni Side rafiki yangu , Salma ni mpenzi wake na rafiki yangu pia”Aliongea  Robert  na kumfanya Hamza kuishia kujisemea  Side hakuonekana  mzembe , Salma alikuwa mwanamke matawi pia na mrembo na kwa kuangalia tu ilionekana Salma ndio kapenda zaidi ya Side.

“Robert  si ulisema ulimfukuzia Dina kwa zaidi ya 

mwaka , inamaana huyu ndio mtu aliekubia?”Aliongea Salma hakukoma  tu.

Hata kwa Side aliweza kuona ukaribu uliokuwepo kati ya Dina na Hamza  na alizidi kujawa na hisia mchanganyiko , siku ile  Prisila alimtambulisha kama mpenzi wake  lakini leo hii  Hamza  yupo na Dina , wanawake hao wote kwake ni ngumu kuwapata licha ya cheo chake kazini .

“Salma haina haja ya kusema hivyo , bado sijakubali kumpoteza  Dina , lazima  nimuonyeshe  mimi ni zaidi ya  Hamza”Aliongea na muda uleule alimgeukia Hamza.

“Si mmekuja upande huu  kulenga shabaha na  bunduki , kwanini tusishindane , kama kweli  wewe ni  mwanaume tucheze pambano moja  na atakae shinda rasmi atatoka kimapenzi na Dina”

“Robert!, mimi sio tuzo kwamba nitajikabidhi kwa yoyote anaeshinda , kwanini unanigeuza  kuwa kifaa?”

“Dina  usinifikirie vibaya , nadhani utanipa nafasi angalau ya kukupigania , kama wasemavyo huwezi  kuona ubora wa kitu  pasipo ya kukilinganisha na kingine , siwezi kukubali kushindwa bila ya kuijua sababu”

“Lakini mimi sitaki kushindana”Aliongea Hamza  

“Wewe sema hujui  kutumia bunduki acha kuzunguka, Dina  ni mwanamke  anaeweza kulenga shabaha kwa kiwango kikubwa unaweza vipi  kuwa mpenzi wake  kama hata kutumia bunduki hujui?”

“Najua lakini sitaki kushindana”Aliongea Hamza akionyesha kukereka.

“Kama unajua  tushindane acha kuwa mwanamke , jiamini bro kama nikishinda utaachana na Dina kama  ukishinda nitaacha kumsumbua Dina , unaonaje hapo?”

“Robert huwezi  kuzipangia  hisia zangu nani wa kumpenda  kupitia mashindano?”AliongeaDina akionekana kuanza kukasirika lakini Hamza alimzuia huku akitoa tabasamu lililojaa kejeli. “Sio mbaya muda mwingine  wanaume kwa wanaume  kushindana  japo huwa sipendelei , kama hili  ni swala la kuonyesha nani mwanaume zaidi kati yetu basi nipo tayari”

Hamza hakutaka kuonekana  mdhaifu mbele ya  Dina hivyo alitaka kuuonyesha   Robert nini maana ya kulenga shabaha.

Side na Salma walioneysha hali ya  dharau  kwa Hamza , walikuwa wakimjua  Robert  Eliasi likija swala la kulenga shabaha alikuwa fundi  kuzidi hata wanajeshi wa vikosi maalumu.

“Hamza upo   tayari kushindana na Robert kweli! , ngoja umpoteze bosi Dina kwa Robert”Aliongea Salma.

“Hatujaanza kushindana lakini ushaanza  kuleta dharau zako  kama siku ile?”Aliongea Hamza na kumfanya Salma  kupandwa na hasira,  bado alikuwa  na kinyongo na Hamza kwa kumsababishia kukosa ushirikiano wa kibiashara kati ya  Kampuri yao ya S Corporation  na Zara Group kwa Hamza  kuleta habari zake za  Mshona nguo kutoka Ulaya.

“Dina usiwe na wasiwasi , huwa sijawahi kushindwa”Aiongea  Hamza akimtoa wasiwasi.

Dina hakuwa na cha kumfanya Hamza kutokana tayari ashaafanya maamuzi , licha ya kwamba alionekana kama anatania  lakini aliamini Hamza hawezi kufanya kitu ambacho  hajiamini nacho.

Wote kwa pamoja walisogea mpaka eneo la Shooting Range.

“Tutatumia  bastora ya Smith & wesson  toleo la tatu , yenye uwezo wa kuachia risasi ukubwa wa Kaliba arobaini  na tano, kila mtu raundi kumi , mita hamsini kutoka kwenye shabaha , tutashinda kwa kuangalia nani  ana maksi kubwa”Aliongea Robert na kumfanya Hamza kuchukua bastora na kuanza kuipima uzito wake  na aligundua ilikuwa  ni orijino kutoka  kiwandani kabisa na sio feki  na alijiambia  hii hoteli sio ya kawaida.

Eneo hilo lilikuwa na  soundproof kiasi kwamba hata ukifyatua  bunduki sauti yake inamezwa  na haiwezi kufika floor za juu  kwenye  makasino na vyumba vya kulala lakini pia bunduki nyingi zilikuwa na mfumo wa Suppressor wa kuzuia makelele.

“Hakuna shida, nani anaanza?”

“Yoyote  yule , mimi niko freshi”

“Kama  ni hivyo wewe anza”Aliongea Hamza na Robert hakujali zaidi ya kutoa tabasamu lililojaa kejeli  na aliijaza bunduki na risasi na kisha akaiweka katika usalama  na kuanza kulenga  shabaha  za duara zilizokuwa  mita hamsini  umbali.

“Bang , Bang , Bang..”

“Bahati mbaya kwako umenikuta nikiwa  na  hali nzuri ya kulenga , alama hizi ni  karibia na  alama zangu za juu katika ulengaji , kama utaamua kukata tamaa  mapema naweza kukuelewa”

Alikuwa  ameweza kulenga duara  namba nane na namba saba , kwa umbali wa mita hamsini  ana uwezo wa  kulenga kiganja cha mkono wa mtu , ni uwezo wa juu ambao mtu wa kawaida hawezi kufikia kabisa, lazima uwe na  mafunzo  ya miaka mingi , maana msukumo wa nguvu inayokurudisha nyuma  ulikuwa mkubwa mno  bila  kusahau bastora aliokuwa akitumia  ina mdomo(Calliber au Kaliba) mkubwa hivyo  kuwa na msukumo mkubwa.

Dina hata yeye aliingiwa na wasiwasi , licha ya kwamba  uwezo wake wa kulenga shabaha ni mzuri lakini  ilikuwa  ni mara chache sana kufikia alama alizopata  Robert  kwa kufyatua risasi mara kumi mfululizo  na aliona Hamza anaweza asimfikie. 

Hamza hakuongea neno na  taratibu alichukua risasi moja moja na kuijaza kwenye bunduki.

Ni kweli aliona Robert alikuwa na uwezo  mzuri  wa kulenga   kwa kugusa duara namba  8 na 7 , wasiwasi wake mkubwa ni   kupata  maksi za  juu kabisa ambazo sio za kawaida na kufanya  hao watu kumshitukia.

Baada ya kuwaza hivyo aliona kidogo   aonyeshe ubinadamu kwa kujikosesha.

Bang , Bang , Bang

Hamza aliishikilia bunduki kwa mikono miwili kana kwamba alikuwa akimuigiza  Robert lakin ukweli ni kwamba  hakuangalia hata anapolenga, kwa umbali huo aliiona anaweza kupata maksi mia ya mia hata kama amefumba macho yake.

Mara baada ya kukamilisha mizunguko  kumi , haraka sana Robert alibonyeza kitufe cha kuonyesha alama  Hamza alizopata.

“”Nane .. tisa ,,, nane , nane  , nane!!”Robert alijikuta akishikwa na hasira huku akisaga meno  akiwa haamini macho yake 

“Samahani mkuu  nimeshinda”Aliongea Hamza.

“Wewe .. unaonekana kuwa na bahati sana”

“Kwahio  bado hujakubali nimeshinda”

“Turudie tena ,  tufanye iwe mbili    kwa tatu”Aliongea Robert akionyesha kutokukubali kushindwa.

“Tulikubaliana  atakaepata maksi kubwa ndio mshindi  lakini sasa hivi unaanza kubadilisha sheria, siwezi kushindana na mtu ambae  anaenda kiunyume na ahadi yake”

“Sio hivyo…”

Kilichomfanya  Robert kukasirika ni kwasababu alijua  angekosa nafasi ya kuombata tena tunda kutoka kwa Dina.

Salma alimwangalia  Saidi na kisha  alimgeukia Hamza na  alionekana kuna kitu alichokiwaza.

“Mnaonaje tukifanya hivi, kama marafiki  Saidi atashindana kwa ajii ya  Robert , akishinda  tutafanya  shindano la mwanzo ni suruhu”Aliongea huku akishika mkono wa Saidi akiupangusa kwa mapozi.

“Side naomba umsaidie  Robert , naona kama   haki haijatendeka”Aliongea lakini  Side alionekana kutofurahishwa na alichosema Salma.

“Hili ni wazo zuri  Salma , vipi upo tayari kupambana na saidi?”Aliongea Robert akimwangalia  Hamza 

“Bado hatujamaliza tu hili   na mnataka tena, sidhani kama  kuna faida yoyote”Aliongea Hamza lakini  Side alionekana kulifikiria lile wazo. 

“Unaonaje tukifanya hivi kama  nikishinda, pambano kati ya Hamza  na  Robert ni batili  na kama Hamza akishinda  nitampatia  dola laki  moja , Robert chukulia hio hela kama ufadhili wangu kwenye  uchaguzi wa kutetea jimbo lako”Aliongea  Side.

“Haha… Side ndio maana nakukubali sana rafiki yangu , hili  limepita”

Hamza  alijikuta akiishia kutingisha kichwa kwa masikitiko , ilionyesha  Side alitaka kushindana nae  kwa kiasi kikubwa mpaka kuweka rehani kiasi kikubwa hivyo cha pesa.

“Kuwa makini , Saidi  uwezo wake wa kulenga shabaha sio wa kawaida , ndio  mwenye rekodi ya juu tokea  kuanzishwa kwa hii club, huwa hashuki chini ya pointi tisini”Aliongea Dina lakini Hamza wala hakujali.

“Unaonekana  kuwa na nia ya dhati kabisa kupambana  na mimi  hivyo sio vizuri kukukatalia , tuanze mechi”Aliongea Hamza  na  Side alitingisha kichwa na kisha alisogea na kuanza kuload  risasi na kuanza  kushuti.

Baada ya awamu   kumi kuisha  Side hata hakujali kuangalia matokeo  kwani alisogea pembeni  na kazi hio ilifanywa na Robert.

“Side umevunja rekodi tena ,  umepata  pointi tisini  na nane umekosa mbili tu”Aliongea  Robert   ikimaanisha  amelenga kwenye  duara  namba  kumi mara nane  na  tisa mara moja.

“Babe  upo vizuri sana  ndio maana nakupenda”Aliongea Salma  akimwangalia Side na macho yaliolegea. 

Dina alimwangalia Hamza  na  aliona ni ngumu kwa  Hamza kuzidi hizo  maksi mbili tu ambazo  Side alikosa. 

“Unaweza kukubali kushindwa hakuna atakae kucheka”Aliongea Side.

Hamza aliona yupo kwenye hali ngumu na hawezi kuigiza tena , isitoshe iwe tisini na tisa au mia hakuna ambae ataona kama anadanganya. 

“Usiwaze , ngoja nijaribu na mimi”Aliongea Hamza na kisha alisogea na kuanza kujaza bastora na risasi na kisha aliinua  mkono mmoja wa kushoto  na kuanza kupiga , hakupumzika hata kwa sekunde ilikuwa ni mfululizo  wa risasi  kutoka.

Dakika  ambayo Hamza aliweka  bunduki chini , kwa haraka  sana Robert aliangalia matokeo  na mara baada ya namba nyekundu kuonekana   wote na Dina ambao walionekana kuwa na shauku macho yaliwatoka , huku  Side na Salma wakimwangalia Hamza kwa mshangao mkubwa.

“100!?”

Robert alikuwa akiangalia namba  hio kwa muda mrefu kana kwamba  alidhania macho yake yanamdanganya.

“Wewe ni binadamu kweli!?”Aliuliza Robert  maana hakuamini mfuatano wa  risasi zile  zote zimegonga shabaha kwa asilimia mia.

“Leo inaonekana nina bahati sana”Aliongea Hamza akicheka , ijapokuwa  watu wote waliokuwa wakimwangalia hawakuwa wajinga , lakini ilikuwa ni uhalisia Hamza hakutumia uwezo wake wote.

“Kupoteza ni kupoteza tu , ikitokea mtaalamu zaidi yako utaishia kushindwa , Hamza nitajie namba za 

akaunti yako  ya benki nikuingizie kiasi nilichoahidi”Aliongea Saidi.

“Potezea , Side sisi sio wageni  kwetu , chukulia kama tulikuwa tukicheza”Aliongea Hamza hakutaka kufanya mambo kuwa magumu kwa

Saidi.

“Huwa sichukulii kiwepesi ahadi zangu , nikisema ni laki  ni laki , nimekubali kushindwa  hivyo usinifanye kwenda kinyume na  ahadi” “Babe nitampatia mimi”Aliongea Salma.

“Haina  haja”

Salma alionekana kujutia kupendekeza  shindano lile na  kumfanya Saidi kuingia hasara  na aliona hasira ya  Side kabisa, lakini alipendekeza vile kwani hakuamini kama Hamza anaweza kumzidi 

Saidi.

Hamza mara baada ya kuona Side anataka kukasirika aliona asiikatae ile hela.

“Dina  mtajie akaunti yako ya benki akuingizie hela , chukulia kama malipo ya  siku zote nilizokula na kunywa bure kwenye mgahawa wako”

“Ni hela  yako hio , sioni kama ni vizuri kuitumia kama malipo”Aliongea Dina lakini hata hivyo alimtajia  Saidi akaunti yake ya benki na alichukua sekunde kadhaa muamala ulisoma milioni mia  mbili hamsini, ijapokuwa aliahidi atalipia kwa dola lakini alilipa kwa hela za kitanzania na baada ya hapo alionekana hakuwa  hata  na mudi   kwani aligeuka na kuondoka  na kumfanya  Salma kumkimbilia.

“Side  inaonekana kakasirika, sio  kwasababu ya kupoteza hela ila kwasababu ya kushindwa”Aliongea  Robert 

Wewe vipi hujakasirika, siku nyingine unapaswa kutimiza wajibu  wako wa kutumikia wananchi na sio kumsumbua  mpenzi wangu”

“Nimekubali kushindwa Bro , kama nilivyoahidi nitatekeleza’Aliongea Robert  kisha alimsogelea Hamza  na kumpatia mkono.

“Hamza unaonaje  tukishikana mikono kama ishara ya kuwa marafiki kwanzia sasa?, natumaini utamfanya Dina kuwa na furaha”Aliongea na kumfanya Hamza amuone kweli bwana huyo ni mwanasiasa  lakini hata hivyo aliishia kunyoosha mkono   kumkubalia.

Upande wa maegesho ya magari mara baada ya   bosi Side kuingia ndani ya gari yake  Audi R8  aliweza kumuona  Salma akiwa ameshaingia tayari.

“Shuka!”Aliongea kikauzu na kumfanya  Salma kutia huruma.

“Side naomba unisamehe mpenzi wangu , sikujua kama Hamza angekuwa na bahati kiasi kile , naomba usikasirike”

Eti bahati , kuna bahati ya namna ile  mtu kuweza  kulenga shabaha eneo moja kwa mara zote kumi  au unaongea upuuzi?”

“Lakini kwanini upo hivi Side , kuna kingine tofauti na hiki kilichotokea , tumekuwa wapenzi  kwa zaidi ya miaka minne  sasa na  nimeamua kurudi  kwa ajili yako , lakini kwanini kadri siku zinavyosogea unazidi kuwa mkali kwangu?”

“Kama unadhani nimekuwa mkali  kwako , basi rudi China ukaendelee na mambo yako sikukuambia urudi  kwa ajili yangu”

“Sirudi tena China, awamu hii  nimerudi ili unioe”

“Nani kasema nitakuoa , hebu toka kwenye gari yangu kabla sijakufanya kitu kibaya”Aliongea  na kumfanya  Salma kuzidi kuona Side anamkosea na alishuka  kwa hasira na kuondoka  lakini  hata hivyo Side hakujali , mara baada ya kuingia katika gari yake alianza kutafuta majina katika simu yake na kuweka sikioni  ikionyesha anapiga simu.

“Side , naona leo  umepata muda wa kunipigia?”Sauti ya kike ilisikika.

Lea hebu acha  maneno yako , kuna kitu  nataka unisaidie nitakulipa hela”

“Kila unapoongelea hela ujue una stress , haya niambie ni kipi unataka nikusaidie?”

“Leo nimegundua siri   ambayo Hamza anaificha , nataka umwambie Prisila…”Aliongea Saidi huku akiwa na tabasamu lililojaa uovu.

******

Upande mwingine ndani ya makazi ya mrembo na Daktari , Frida Franklin  katika chumba cha Master alionekana mrembo huyo akiwa amejilaza  na  kukoroma kabisa , alionekana  alikuwa amechoka  kwa namna alivyokuwa  amelala.

Taa ya kitandani ilionekana haijazimwa  na pembeni yake kuna kitabu  kilichokuwa kimefunguliwa , ikionyesha alipitiwa na usingizi wakati akiwa anasoma.

Zilipita sekunde chache tu  muda ule hali ya hewa ya kile chumba ilibadilika , ilikuwa ni kama upepo umeongezeka  na kumfanya  Frida kuanza  kujinyoosha kitandani.

Mara ghafla  tu  chumba kile kilirudi katika hali ya  utulivu wa hali ya juu na kumfanya Frida  kujigeuza na kulala chali , lakini utulivu  ule uliambatana na maajabu yake  kwani  ghafla tu kilionekana kivuli kikitokea  kwenye pembe  ya chumba hicho.

Ajabu  ni kwamba  kifizikia ili kivuli kitokee kinahitaji mwanga  lakini kivuli hicho kilitokea bila ya  kuwa na chanzo cha mwanga.

Kile kivuli  kilikuwa na umbo la mtu lakini  kwa namna moja ama nyingine kama ni mtu  katika uhalisia basi angekuwa akitisha kutokana na eneo lake la kichwa kukosa mpangilio mzuri.

Wakati Frida akiwa hana hili wala lile mkono wa kivuli kile cha mtu wa ajabu ulinyooka ni kama ulikuwa ukirefuka kutoka eneo  kilipo mpaka kwenye kitanda  , mkono ule ukimlenga  Frida katika shingo yake.

Ghafla tu ni kama Frida alishituka  lakini  alianza kurusha miguu kama  mtu ambae amekabwa

shingoni , alijikuta akirusha  Miguu huku akijitahidi kuvuta hewa.

Lakini   mwanamke mrembo huyo alionekaa kushindwa kabisa kupambana na mkono ule wa Kivuli cha mtu na ulionekana ni kama umedhamiria kumuua.

Frida alijikuta kadri sekunde zinavyoenda ndio  ambavo  alikuwa akikosa nguvu  kutokana na   kutoweza kuvuta pumzi ,aliishia kurusha rusha miguu huku akionekana muda wowote atakata roho.

Previoua Next