Reader Settings

“Sijui kuhusu katiba yao inachosema , ila nina uhakika   mgombea Mwenza ndio atachukua nafasi, kwanini unauliza?”Aliuliza tena Dina maana alijua Hamza hakuwa mtu wa siasa.

“Nawaza  kuna mchezo unaochezwa hapa na kuna nguvu mbili kubwa za kisiasa , nataka kujionea mwenyewe”Aliongea  Hamza na Dina  alitingisha kichwa , kwasababu Hamza alitaka kwenda hakuona haja ya kumzuia , isitoshe  ilimpelekea  kujiamini zaidi kudili na  hali kama hio.

Upande wa Dina alijua lazima kuna mchezo unaofanywa na kama Mzee Seif atakubali kuhusika moja kwa moja  itaaminika  mtandao wake ndio umekamilisha  swala hilo , jambo ambalo hakautaka litokee.

Nyumba ya Mzee Seif ilikuwa Kigamboni Mbutu B  na gari mbili ziliendeshwa kuelekea huko  ya mbele akiwemo Hamza  na  Dina na ya nyuma ilikuwa Noah iliowabeba Lawrence na kundi lake.

Kitendo cha kufika eneo la tukio  waliweza kuona  watu walioizingira nyumba ya  Mzee Seif , jambo ambalo liliwashangazwa hakukuwa na uwepo wa polisi hata mmoja ni kama Hamza alivyotarajia.

“Mbona sio polisi kama taarifa ilivyosema?”Aliuliza  Dina kama  kwamba Hamza alikuwa na majibu.

Hamza alichunguza  eneo lote hasa wale watu walioshikilia siraha  na alijikuta akikunja sura mara baada ya kuona  wazungu wawili  ndani ya eneo  lile wakiwa ni sehemu ya  watu waliozunguka  nyumba hio.

“Ni kama nilivyotarajia kuna kinachoendelea hapa”Aliongea  Hamza.

“Lakini  kama kweli  walikuwa wakimshuku  Mzee Seif kulipua gari ya mheshimiwa Jongwe kwanini hawajaja polisi?”Aliuliza.

“Tutapata majibu yote mara baada ya kuongea nao”Aliongea Hamza huku akitangulia kutoka nje ya gari.

Wale  watu  kama walinzi walioshikilia siraha wakiwa wamezingira nyuma hio waliongeza umakini kwa  Dina na kundi lake.

“Kama  tabia yako ya siku zote,  Dina mrembo wa kujiamini , naona umekuja  na watu wachache mno tofauti na nilivyotegemea”Sauti ya mwanaume ilisikika kwasababau ilikuwa kuna giza hawakumuona vizuri na mara baada ya kusogelea taa za mwanga wa gari ndio Dina aliweza kumuona.

“Pancho!, unafanya nini hapa?”Aliongea Dina  na muda huo ni kama sasa  alishaanza kupata  picha ya kile kinachoendelea.

“Nimekuja kukusalimia kwa mara nyingine mara

baada ya kukataa pendekezo ya  dili

nono”Aliongea na muda ule alitoa ishara na  baada ya kupita   dakika mmoja tu wanaume wanne walitoka  katika nyumba hio   na moja wapo ya wanaume wale alikuwa ni Mzee Seif  alieshikiliwa  na wanaume wawili weusi waliojazia mwili , mtu wa mwisho kutoka alikuwa  ni Mzungu- Mjapani , yaani  mtu aliechanganya rangi ya mjapani na Mzungu.

Kilichomfanya Dina kuanza kupandwa na hasira alijua  mpango wote huu ulisukwa na Pancho.

Pancho alikuwa ni moja ya wasimamizi  wa   mtandao wao upande wa Congo   na siku kadhaa  nyuma  Dina  alipokea dili  kupitia kwa Pancho kutoka kwa  Wacanada ambao walitaka kuingiza siraha za kivita  Congo kupitia Bandari ya Mtwara.

Dili hili liliungwa mkono na Mheshimiwa Mgweno  lakini  Dina aliona  halikuwa na maslahi na  kama angelikubali ni kama kujipiga risasi mguuni, ikizingatiwa siraha hizo zilipaswa kufikishwa kwa kundi  lingine  la waasi ndani ya Congo  tofauti na lile ambalo wanashirikiana nalo kwa muda mrefu. “Mzee Seif nini kimetokea ,  kwanini taarifa  nilizopokea ni wewe kuhusika na  kumuua  Mzee Martini  na mheshimiwa  Jongwe?”Aliuliza Dina akimpotezea Pancho.

“Hawa ndio wahusika , wameiteka  familia yangu na wanataka nikiri kuhusika  kwa kushirikiana na wewe kumuua Jongwe  au turejee mezani  na kuanza mazungumzo ya kuingiza siraha  Tanzania kwenda Congo”Aliongea Mzee Seif aliekuwa na hali ya hofu na kumfanya Pancho  kutoa tabasamu.

“Pancho unajaribu kufanya nini , nani yupo nyuma yako?”

“Dina hakuna  ambae yupo nyuma yangu?”Aliongea  Pancho kwa kejeli.

“Kwa kumuua  mgombea wa uraisi kupitia chama tawala, unasema hakuna  ambae yupo nyuma yako?”Aliongea  Dina kwa hasira na kumfanya  Pancho kutoa tabasamu la kifedhuli.

“Nilitaka hili swala angalau ulichukulie kwa uzito  wake, ushahidi wa wewe kuhusika katika  shambulizi  la kulipua bomu  gari ya mgombea wa uraisi  kupitia chama tawala upo , unaweza ukawa wa kutengeneza lakini jeshi la polisi lipo tayari  kuuamini na kama likitoka uraiani , kitengo cha  TISA  kitakufanya  mbuzi wa kafara, lakini  huko kote  ni  kujisumbua kama upo tayari kuchagua chaguo zuri kati ya matatu  alioongea Mzee Seif?”

Hamza muda huo alikuwa  akiangalia mazingira yalivyo  na  watu wote waliokuwa hapo walikuwa na siraha za bunduki  na   haraka haraka  kwa sheria ya Tanzania ilikua ngumu   kwa watu hao kumiliki hizo siraha  labda iwe kuna mtu  ndani ya  serikali ambae alikuwa  akihusika.

Isitoshe safari yao  kutoka kijichi mpaka kufka hapo  , kama kweli  jeshi la polisi lilikuwa sirasi kukamata watu hao  waliomsababishia ajali mgombea wa kiti cha uraisi basi wangeshafika  labda tu iwe kuna maagizo ambayo yamewafanya kuchelewa.

“Hizo siraha mnaotaka kuingiza  Tanzania  mnazitoa wapi?”Aliongea Hamza.

“Oh!, ahsante kwa kuuliza bwana  mdogo , kidogo tu nimesahau kumtambulisha bosi wetu hapa ,  huyu ni  Bosi Keita  na ndio msingi wa haya maungumzo , kuhusu wapi siraha zinatoka   ni juu yake”Aliongea  Pancho kwa kujigamba.

“Pancho kama nilivyosema  mtandao wetu haudili na maswala ya siraha  bila ya  utaratibu maalumu, kama unataka dili hili lipite lisimamie wewe mwenyewe na hela zako na sio  za mtandao wa Chatu”Aliongea Dina na yule bwana  mwenye asili ya kizungu na  Kijapani alimpa ishara  Pancho ya kuongea yeye.

“Miss Dina kama  alivyoongea Pancho  tunaweza kulimaliza hili swala kimya kimya na kusiwe na athari zozote  kwa kila upande”Aliongea kwa Kingereza.

“Unamaanisha unaweza  kuzima kesi ya kulipua gari  ya mgombea wa Uraisi  pamoja na  Martini?”Aliuliza Lawrence.

“Itategemea  na   maamuzi ya Miss Dina?” “Kwanini nahisi hata  waliompendekeza  Jongwe kupeperusha bendera ya Chama ni kama wanashangilia kifo chake?”Aliongea Hamza huku wakati huo  Dina akiwa ametulia.

“Tunafanyaje?”Aliuliza Dina akimegemea  Hamza , isitoshe ndie aliesema wasije na watu wengi.

“Wana siraha na hata kama tukishambuliana bila siraha  hatuwezi kushinda bila kushitua  raia ,  hawa watu wana mafunzo  ya mapigano”Aliongea Hamza na kumfanya Dona kuwa na wasiwasi.

“Usiwaze hili naweza kulimaliza  kwa amani  na kisha utadili nao kujua nini kinaendelea  kuhusu mgombea wa uraisi kulipuliwa”Aliongea  Hamza    na japo Dina alikuwa na wasiwasi aliamua kumwamini  Hamza.

“Bwana Keita  kwa ninavyojua  huwezi kudili na siraha pasipo kuwakilisha  shirika la giza unalotokea”Aliongea Hamza akitaka kujua Black Association ambayo  Keita anatokea.

“Jungle Army Merchant ndio  ninatokea”Aliongea  bila  ya kusita sita.

“Kumbe ni Jungle , hebu subiri kwanza nipige  simu, nikimaliza  utaamua cha kufanya”Aliongea.

“Umpigie  nani?”

“Utajua  nikimaliza’Aliongea Hamza.

“Mr Keita  haina haja ya kupoteza muda na hawa watu ,  swala  ni moja tu wachague  chaguzi moja kati ya tatu tumalizane”Aliongea Pancho akionekana kukosa uvumilivu.

“Kimya! , sitaki unifundishe namna ya kufanya biashara”Aliongea Keira kwa kingereza na kumfanya   Pancho kukaa kimya , isitoshe alikuwa akijua Jungle  Army Merchant walikuwa  wafanyabiashara wakubwa   ndani ya Black Market kwa kuuza  siraha za  kila namna.

Muda huo Hamza alikuwa ashapiga simu tayari bila ya kuwa na wasiwasi kabisa.

*****

Magneto, Las Vegas- USA

Ni ndani ya jiji  la  Las Vegas , jiji ambalo kwa  wacheza kamari  hawakuhesabu muda , Usiku ni kama mchana na Mchana ni kama usiku tu ndani ya hili jiji.

Katika moja ya hoteli ya kifahri ya nyota tano  ndani ya chumba cha hadhi ya raisi ,  alionekana  mtu bonge mweusi mwenye kitambi akiwa amelala chali.

Alikuwa mrefu wa mita kama  moja  nukta tisa hivi , vidole vya mikono yake vilikuwa vimevishwa pete za madini ya  almasi  , Dhahabu  na madini  mengine ya thamani ,  shingoni alikuwa amevalia mikufu ya  bei ghali.

Mtu yule bonge  alijikuta akitandaza miguu yake vizuri huku akifumba fumba macho  na

kuyafumbua , katikati ya eneo   la mapaja yake alionekana mwanamke  mzungu mwenye nywele nyeupe(blonde) akiwa bize  kumhudumia.

“Mr Mamen are you comfortable?”Aliuliza yule mwanamke kwa sauti tamu huku akiinua kichwa chake akimwangalia  kwa macho malegevu , akimuuliza  Big kama  ni mwenye kuifurahia huduma.

Mwanaume  yule bonge udenda ulikuwa  ukitaka kumwagika kutoka  kwenye  midomo yake , alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine wa raha.

“Comfortable..!?, Deeper the better .”Aliongea  akimaanisha azame chini zaidi ndio  itakuwa vizuri.

“You’re so annoying , I’m realy tired ..”Aliongea yule mwanamke akimwambia anachukiza kwani amekwisha kuchoka.

Bonge  yule mweusi kama  msanii RickRoss alifungua  droo ya meza pembeni na kitanda chake  na kuchomoa maburungutu ya pesa   za dola  na kumtupia.

“Hakikisha najisikia vizuri mpaka kisogoni , nitakupa kiasi chochote cha pesa unachotaka”Aliongea Big na yule mwanamke  uchomvu uliisha  palepale na alijkuta akiongeza mashambulizi ya kuhakikisha Big anajisikia vizuri.

Dakika  hio hio simu yake ilianza  kuita ,  hata simu yake tu ilikuwa  imetengenezwa kwa   housing  ya madini  ghali sana na kuifanya ionekane kama kitu kisichokuwa cha kawaida kutokana na uthamani wake 

“F*ck , kama ningejua ningeizima   hii simu , nani ananipigia muda huu”Big alilaani  huku akichukua ile simu na kuipokea  maana namba ilikuwa mpya tena  haikuwa ya   taifa hilo 

“Big naona kama kawaida yako  sasa hivi unaringa , kwahio unaona sipaswi kukupigia  hata  kama ni swala linalohusu vita ya tatu ya dunia”Sauti ya  kiume ilisikika  katika simu ya Big.

Kitendo cha Mameni kusikia ile sauti  mwili wake ulitetemeka na macho yake yalibadilika na kuwa mekundu  na  hata ule msisimko aliokuwa akisikia ulipotea.

Yule mwanamke aliekuwa   bize kuhakikisha Big anafurahi alijikuta akipiga kelele mara baada ya  kadudu kabig kupotea   na kuwa kabamia.

“Boss!! , ni wewe  kweli  , naona hatimae umenipigia , nimekumisi sana”Aliongea Big huku sauti yake ikiwa imebadilika.

“Unafanya nini hapo , lazima utakuwa na m*laya kitandani , yaani ndio kwanza kunakucha  wewe unahangaika na wanawake , kuna siku utafia  kwenye kifua cha mwanamke”

“Hehe..Bosi wewe mwenyewe unanijua vizuri , isitoshe wewe ndio mtu pekee ulievunja rekodi yangu”Aliongea. “F*ck you!”Alitukanwa.

“Bosi  nasikia upo Tanzania , habari za siku nyingi , vipi naweza kuja huko?”

“Nina mambo mengi ya kufanya siku hizi  tutaona kama unaweza kuja , nyie watu  ni wasumbufu sana mkisikia nipo mahali mnataka kuja tu , sitaki  usumbufu wenu nahitaji kutulia kwa sasa”

“Bosi  kwa uwezo wako  na  ushawishi wako unaweza kuomba chumba  mapumziko Ikulu na ukapatiwa  na  warembo kabisa ,  hayo sio mapumziko ila  ni kujitia stress  tu , mapumziko ni yale  wafariji wanakuwa  wanabadilika badilika  kila siku kwenye kuusisimua mwili”

“Sterehe za kutumia  hela hizo nishazichoka , hata  nikikuambia ni namna gani nafurahia maisha ya sasa hivi hutonielewa Big”

“Kama ni hivyo bosi kwanini umenipigia simu , kuna dili  jipya?”

“Hakuna dili  lingine , nishastaafu hayo mambo”

“Sababu ni ipi sasa Bosi , au kuna sehemu nimekosea?”Aliuliza  Big kwa upole.

“Kwenye biashara zako unamfahamu bwana anaefahamika kwa jina la  Keita?”

“Ndio  mwaka juzi niliingia dili na  kundi moja linalofanya shughuli zao ndani ya Afrika  kuiba  madini Adimu na kuyauza kwenda kwenye moja ya kampuni ya maswala ya kiteknolojia nchini Ufaransa , linaongozwa na   bwana Keita”Aliongea Big.

“Huyu bwana wako naona ana juhudi mno , muda huu  nimeelekezewa mitutu ya bunduki  ndio maana nimekupigia simu kuthibitisha , Big kwahio sasa hivi umeshaanza kuwa mkubwa kiasi cha kunisaliti kisa  tu nnimetoka kwenye uringo?”

Big mara baada ya kusikia kauli hio  kutoka kwa  Hamza alijikuta mikono  ikimtetemeka kiasi kwamba simu ilitaka kudondoka.

“Bosi , subiri kwanza , nitampigia simu sasa hivi , naomba kwanza nimfokee baada ya hapo unaweza kumuua”Aliongea Big na dakika ileile alikata simu  na kuitafuta namba ya Keita.

“Mamen Babe! , unafanya nini sasa mbona imepotea!?”Yule   kahaba  wa kizungu aliongea  lakini Mameni  alimpotezea  na mara baada ya kuipata namba ya Keita aliipiga palepale.

Mara baada ya Hamza kumaliza kuongea na simu  hakuongea neno na alitulia  akiangalia matokeo.

Ijapokuwa Keita hakujua Hamza alikuwa akiongea na nani kwenye simu lakini alihisi kuna kitu hakipo sawa.

Dakika ileile simu yake ilianza kuita  na  alisogea pembeni na kupogea  lakini muda huo huo alianza kuonyesha ishara za kupaniki.

Upande wa pili ilikuwa ni sauti ya  Big kutukana  kimarekani  kwa mara nyingi mfululizo kadri alivyoweza.

“Bosi nimefanya kosa gani?”

“Unataka kumuua nani sasa hivi?”

“Bosi umejuaje nataka kuua mtu?”

“Unaetaka kumuua ni bosi  wangu”

“…”

Keita alijikuta akikosa neo , alishangaa mno  kwa zaidi ya sekunde kumi , ni kama alikuwa akisharabu yale maneno.

“Ah!”

Alijikuta hofu ikimwingia na vigoti vya miguu yake vilianza kumlegea  na alijikuta akigeuka na kumwangalia Hamza.

Upande wa Hamza alikuwa akimwangalia Keita tu kwa mbali na kwa jinsi alivyoonyesha kupaniki na woga alitamani kucheka. 

“Mr Keita ,  Mr Keita , what happened?”Pancho  aliuliza  mara baada ya kuona mabadiliko.

Dina macho yake yalichanua  alijua kabisa mabadiliko ya  Keita ni kutokana na  Hamza alipopiga simu   na kwake  aliona mwanaume Hamza alikuwa akimshangaza  kila siku.

“Nini tatizo Mr Keita , mbona huongei?”Aliuliza Pancho  kwa wasiwasi 

“Hivi unajua  mimi na  vijana wangu tutakufa sasa hivi  kutokana na ujinga wako na wale wanasiasa wapuuzi?”Aliongea kwa hasira.

“Unamaanisha nini  Mr….”

Keita  hakuchelewa alichomoa Desert Eagle kutoka kwenye kiuno chake na kumchapa  risasi tatu  Pancho palepale.

Mpaka Pancho anadondoka chini muonekano wake  ulikuwa na shauku ya kutaka kujua kwanini   Keita  anamshambulia.

Keita mara baada ya  kumalizana na Pancho alitoa maagizo kwa vijana wake kuwashambulia watu wa Pancho na  walionekana kuwa shapu kweli kwani ndani ya sekunde wote walikuwa chini.

Baada ya   Keita kuituliza hali alijikuta akimdondokea Hamza kwa magoti huku akiwa na wasiwasi mwingi  akitia huruma.

“Prince Rich.. Bosi wangu ameniambia kila  kitu , naomba unisamehe kwa ujinga wangu  , sikubahatika kukutana na wewe ana kwa ana zaidi  ya kusikia   habari zako  ndio maana  nimekukosea…”

Kitendo kile kiliwashangaza mno  Dina , Lawrence na  wenzake , waliishia kujiuliza Hamza ni nani mpaka  bwana yule kuwa na hofu namna ile  kiasi cha kupiga magoti.

“Nipe bastora yako”Aliongea Hamza akiwa siriasi  na kumfanya Keita kukakamaa mwili lakini alimpatiia.

‘Tafadhari naomba uwaache  vijana  wangu waondoke , walikuwa wakifuata maelekezo  tu kutoka kwangu  na  wanazofamilia zinawategemea”Aliongea Keita lakini Hamza hakumjali  na muda ule aliinua ile bastora na kujielekezea kwake kana kwamba anataka kujipiga risasi.

Tukio lile lilimshangaza kila mtu  wakishindwa kuelewa Hamza anataka kufanya nini 

“Hamza unataka kufanya nini  , usipaniki..”Aliongea Dina lakini kabla hata hajamaliza  Hamza alikuwa ashaachia risasi.

Bam!

Mlipuko ule wa bunduki ulimuogopesha mpaka Keita  na wote walimwaangalia Hamza kwa mshangao  na walishangaa  zaidi baada ya kuona  hakuna kilichotokea.

Risasi ambayo  ilitoka katika ile bunduki ilikuwa katika vidole vya Hamza , haikueleweka amefanyaje  lakini ilionekana  aliikamata kabla ya kumfikia, tukio lile lilimfanya  Keita  kushindwa kuendelea kupiga magoti na  kukaa chini kwa  kunyoosha  miguu huku mapigo yake ya moyo yakidunda kwa kasi.

“Kabla sijafanya chochote nataka muelezee kila kilichotokea… sababu ya kwamba  umepiga magoti sio kwasabau ya bosi wako bali ni kwasababu yangu  hivyo nataka majibu”Aliongea Hamza.

“Serafii.!!, nipo tayari kuongea”Aliongea  Keita huku akipiga  kichwa chini kiasi  cha kutoka damu kwenye paji  la uso.

“Anza kuelezea , kwanini  kifo cha  Mgombea wa uraisi  na nani  kahusika”Aliongea Hamza.

“Hatujahusika   katika kumuua mtu , tupo hapa nchini kwa ajili ya mazungumzo ya biashara ya kupitisha Siraha Kwenda Congo  kupitia bandari ya Mtwara , kitu pekee ambacho  nafahamu  kuhusu muhusika tulipewa kazi ya kumtorosha  hapa nchini kupitia boti yetu”Aliongea na kauli ile ilimfanya  Dina kusikiliza kwa umakini.

“Imekuwaje mkajiingiza , sitaki kuuliza maswali mengi elezea kila kitu ninachotaka kujua?”

“Mara ya mwisho nilivyokuja hapa nchini  niliweza kukutana   na mstaafu Mgweno kwa ajili ya kuingia dili la  kupitisha siraha , lakini  kutokana na  usafirishaji wote wa Kimagendo kuwa chini ya Chatu  hakutoa maamuzi  badala yake  aliwasiliana na  Miss Dina  ambae mara baada ya kuelekezwa kuhusu dili hili  alikataa, Mstaafu   baada ya ombi hili kukataliwa alituambia hana namna ya kutusaidia  kwani  njia pekee ya kupitisha  siraha hizo ni moja tu  ambayo ni Mtwara kutokana na bandari zote kuwa chini ya mwekezaji”

“Nini  kiliendelea”

“Wakati  tukifikiria  namna  ya kutafuta njia nyingine ya kukamilisha dili hili nilipokea  simu kutoka kwa mtu ambae alijitambulisha ni msaidizi wa raisi”Aliongea.

“Unamaaniisha Mheshimiwa Eliasi Mbilu?”

“Ndio na alisema anataka kuonana na sisi kwa ajili ya mazungumzo  ya namna ya kukamilisha kile tulichokuwa tukihitaji , kutokana na kuwa na haraka ya kufanikisha  hili dili  nilikubali  na  kupitia  msaidizi wake alinipa maelekezo niwaache vijana  na boti yetu nchini  Tanzania  kwa muda  na nikutane nae  jijini Kual Lampur nchini Malaysia   ndani ya tarehe alionitajia wakati akiwa ziarani”

 

Tokea tuzungumze  kuhusu hili dili imeshapita mwezi miwili , inamaana huu mpango  ulikuwa wa muda mrefu?”

“Inawezekana  Miss Dina , kabla  ya  siku moja ya tarehe  kufika , niliweza kufika  Malaysia na nilikutana na mheshimiwa kwa siri sana  kupitia  msaidizi wake na nilitambulishwa  kama mwekezaji”Aliongea Keitani kwa kutetemeka.

“Alitaka kuongea nini kwa siri namna hio?”Aliuliza  Dina , ijapokuwa Keitani alijua alikuwa  akitoa siri  kubwa lakini hakuwa na jinsi.

“Aliniambia siku ya leo  saa nne kamili za usiku  mgombea wa  kiti cha uraisi  kupitia chama  chake  atafariki kwa  ajali ya   gari  na  atakaesababisha ajali hio  napaswa kumtorosha nje ya nchi  na kama ikishindikana nimuue kabla ya  kukamatwa na polisi, kisha nitumie ushahidi feki wa tukio hilo  kuhakikisha  nakamilisha dili  la kupitisha siraha”

“Ushahidi feki ni  kutusingizia  sisi ndio wahusika, si ndio?” ‘Ndio”

Ameenda mbali mpaka kutengeneza ushahidi feki

, yeye anafaidika nini  katika hilo?”Aliuliza Lawrence.

“Kila kitu kipo wazi , naamini  Jongwe sio chaguo lake  na pili alitaka kujitengenezea njia za kupata  maslahi  hata akiwa amestaafu kupitia hili dili”Aliongea Hamza.

“Ndio , alitaka asilimia ishirini ya  faida itakayopatikana na wakati huo huo Mgombea  wa uraisi akiwa  ni chaguo lake baada ya  chaguo la Mgweno kufariki”Aliongea keita na kumfanya Dina sura kujikunja 

“Mgweno na  Eliasi wanataka kupinduana , madaraka huwa ni matamu sana”Aliongea Dina lakini upande wa Hamza hakujali nani anampindua nani.

“Vipi kuhusu muuaji  ni nani?”

“Kuhusu mfungwa  hatuna taarifa nyingi kuhusu yeye , tulipatiwa picha  pekee  na tuliambiwa ni mfungwa  wa kidiplomasia  aliefungwa kwa  muda mrefu kwa siri”

Yuko wapi kwasasa?”Aliuliza Hamza.

“Ametoweka mara baada ya tukio, tunaamini alikuwa na mpango wake binafsi wa  kujitorosha baada ya kukamilisha misheni”Aliongea  na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.

“Picha yake ipo wapi”Aliuliza Hamza na Keita alimpa ishara  bwana moja wa kizungu na alimsogezea Hamza simu  na ilionekana picha ya mfungwa kwenye kioo cha simu na mara baada ya kuiangalia  alijikuta macho yake yakichanua.

“What the f*ck!!”

Hamza alijikuta akitoa tusi  na kumfanya Dina kusogea kuangalia  picha  hio ili kujua kwanini  kashangaa.

Previoua Next