Reader Settings

Hamza mara baada ya  kuonana na Eliza, mrembo huyo alionekana kama amechoka mno licha ya kwamba ilikuwa asubuhi, ni kama vile  alikuwa ameachwa na mpenzi.

“Eliza kwanini unaonekana kuchoka hivyo?”Aliuliza  Hamza na mara bada ya Eliza kukutanisha macho na Hamza alionyesha kulazimisha tabasamu.

“Labda ni kwasababu nilikosa usingizi  jana , vipi kwanini umekuja ofisini kwangu?”

“Linda kasema kuna hela za malipo unazokwenda kukusanya  leo , ameniambia  niende na wewe kama mlinzi”

“Kwahio tunaenda pamoja?”

“Ndio”

“Nikweli  nilikubali kwenda lakini  pamoja na  Kapteni Yonesi kama  mlinzi wangu”Aliongea  Eliza.

Ombi la  kampuni hio kutaka  Eliza kwenda kuchukua hayo malipo lililetwa kabla ya  Yonesi kupatwa na matatizo mpaka kulazwa.

“Hivi hii kampuni ya Dede inatisha namna hio , nimewahi kusoma mtandaoni kuna mdau  analalamika  ndugu yake kupoteea ndani  ya kampuni hio”Aliongea Hamza.

“Kumekuwa na taarifa nyingi  kuielezea lakini haijulikani kama ni za kweli ama za uongo, polisi pia hawajawahi kukanusha  ndio maana wafanyakazi wengi wanaogopa , lakini  wana wateja wengi tu wapenda starehe”Aliongea Eliza , ilionekana hata yeye hakuwa na uhakika kama hio kampuni ina shida.

“Kama kampuni haijulikani uendeshwaji wake  kwanini mnafanya nayo biashara?”

“Mteja  huwezi kumkatalia  kumhudumia kwasababu umesikia tetesi ni mtu  mbaya , labda kuwe na ushahidi wa  wazi  unaothibitisha hayo madai , vinginevyo kama amekidhi vigezo ukimkatalia lazima umpe sababu ya kuelezeka,  Kampuni  ni  taasisi  na haikopeshi  wateja kulingana na tabia zao, inaangalia vigezo”Aliongea Eliza na kumfanya  Hamza kutingisha kichwa kukubaliana nae.

“Kama ni hivyo  angetafutwa  mtu mwingine wa  kwenda , kampuni ina watu wengi wa kudai madeni sio lazima  wewe?”

“Mara ya mwisho  alienda  mtu kwa niaba yangu lakini hakuweza kukutana kabisa  na  mkurugenzi wao, lakini ilisemekana   alikuwepo   na  baada ya kuwatishia kuwachukulia hatua za kisheria  ndio bosi wao akasema anataka mimi  niende  nikapatiwe  cash”

“Huoni sasa  kuna mtego?”

“Najua ndio maana sikutaka kwenda mwenyewe ,  nilipanga kwenda na Kapteni Yonesi”Aliongea Eliza.

Mara baada ya wawili hao kutoka nje  ya lift  sehemu ya  maegesho  , Eliza alisogelea gari ya mjerumaini  Porsche Macan ya rangi nyekundu , ilionekana ile  gari  ya  Toyota ambayo  ilipata ajali ilibadilishwa na kupewa gari nyingine.

“Eliza  ni lini umenunua gari kali namna hii?”Aliuliza Hamza kwa mshangao maana ilikuwa ni gari ya hadhi  mno na kwa haraka haraka alijua sio chini ya milioni mia thamani yake.

“Sijanunua  mimi , hii ni zawadi kanipa  Regina  kutokana na kufanikisha dili la  ile kampuni kutoka Morogoro?, ni gari ya bei sana najua lakini nilishindwa kuikataa maana  mwenyewe ndio kanipa”Aliongea Eliza na kumfanya Hamza kushangaa , ilionekana  Regina alikuwa akimjali mno  Eliza lakini bado ni kama kuna kitu kilimpa ishara  tofauti , ilionekana   kulikuwa na zaidi ya sababu kwa  Regina kumpatia Eliza gari  ya bei ghali namna hio.

“Hata mimi naona hukuwa na haja ya kukataa , isitoshe unahitaji  usafiri”Aliongea  Hamza.

“Ndio , bosi ananijali  ndio maana sitaki kumwangusha”Aliongea Eliza huku akiwa na muonekano usioweza kuelezeka ni wa furaha au wa huzuni.

Kwa namna ambavyo Eliza alikuwa akiongea ilizidi kumpa  wasiwasi  Hamza na kujiambia kuna kitu ambacho hakipo sawa  kabisa  lakini hakuelewa  nini kinaendelea, isitoshe Eliza pia alionekana kutokuwa na raha kabisa.

Kwasababu Hamza ndio aliekuwa akiendesha  Eliza alisema analala  kidogo.

Kampuni  hio ilikuwa maeneo ya  Msata-Bagamoyo hivyo ilikuwa ni safari ya kama masaa mawili hivi.

Kutokana na Eliza kulala  Hamza aliendesha gari kwa spidi kubwa  ya wastani na ndani ya muda mfupi  aliweza kufika na kuingia kwenye barabara inayokunja kushoto  akipishana na kituo cha kujazia mafuta cha Lake oil.

Dede  licha ya kwamba ilikuwa ikiitwa kampuni lakini  ilikuwa ni kama hoteli tu.

Tajiri  Laizer mara baada  ya kupata madini makubwa yaliompa zaidi ya utajiri wa dolla milioni  kumi za Kimarekani ndio alijenga  katika eneo hilo ambalo  ilikuwa   ni shamba lao kabla hata ya  kutajirika.

Hamza mara baada ya kuegesha gari  Eliza aliweka nywele zake vizuri  na wote wakashuka  na kuanza kutembea kulisogelea geti na mara baadaya kufika  getini hawakuweza kuigia maana  lilikuwa limefungwa na  waliishia kugonga.

“Mnaenda wapi?”Sauti ya mmasai ilisikika kupitia kijidirisha  kidogo.

“Tunatokea  kampuni ya Dosam , tuna miadi na Mr Laizer ”Aliongea Eliza.

“Dosam?, hebu subiri kwanza tutoe taarifa”Aliongea   yule mlinzi na kisha kidirisha kilifungwa , walionekana kuwa makini kama vile wanafanya biashara haramu humo ndani.

Mpaka dakika  tano zinaisha ndio  mlango wa geti dogo  ulifunguliwa na mwanamke  alievalia  sare za  uhudumu.

“Nadhani utakuwa unaitwa Eliza  meneja kutoka kampuni ya Dosam , unaweza kunifuata”Aliongea  yule mwanamke na  Hamza na Eliza waliingia ndani.

Lilikuwa eneo kubwa  mno   lenye bustani zilizotengenezwa na kuvutia , kulikuwa hadi na sanamu kubwa ya ng’ome  katikati  ya bustani.

Jengo la  kampuni hio  lilikuwa limeenda hewani kwa floor kama nne hivi  na pana.

Ukweli  licha ya kuambiwa hio ni kampuni lakini alishindwa kuelewa ni kampuni ya aina gani , Hamza alijiambia pengine ni  biashara ilioandikishwa kama  kampuni pekee lakini sio kampuni.

Walimfuata  yule mhudumu ambae aliwaingiza katika korido ndefu iliokuwa na kila aina ya michoro ya  wamasai  ikiwemo Morani  na  viongozi wakubwa wa kimasai waliowahi kutamba katika historia , kulikuwa hadi na picha za  baadhi ya tamaduni zao ikiwemo vinyago na mengineyo.

Licha ya michoro hio, jengo hilo lilinukia harufu ya kitajri  , ni aina   flani ya harufu   hata benki unaweza kuweza kuinusa.

Waliweza kupishana na watu tofauti tofauti ikiwemo wanawake na wanaume na walikuwa wamevaa  na wakapendeza mavazi ya pesa nyingi  na kuna  hata wale ambao  Hamza aliweza kuona walikuwa na mafunzo ya mapigano.

Eliza alikuwa mwanamke mrembo  na  kitendo cha kuingia eneo hilo ilikuwa ni kama anaingia kwenye  shamba lililojaa mbwa mwitu, kila mwanaume aliekuwa akimwangalia alionekana kumtamani.

Hata Hamza aliweza kuona namna ambavyo Eliza alikuwa na wasiwasi lakini hakuongea chochote , ili kumuondolea wasiwasi aliamua kumshika mkono

Eliza mara baada ya kushikwa mkono na  Hamza alishituka kidogo lakini kwa wakati mmoja alionekana  kujisikia vizuri kwenye moyo wake , lakini  macho yake alipokuwa akimwangalia Hamza ni kama alikuwa akionyesha hisia za mwanamke mpweke, ni kama zile hisia ambazo  michepuko wanakuwa nazo wakati  wakiwasindikiza kwa macho waume za watu wakirudi nyumbani kuonana na familia zao.

Mara baada ya kutembea kwa   takribani dakika saba  waliweza kufika katika   eneo ambalo lilikuwa kama sebule , kulikuwa na kila aina ya samani za  bei  ghali na kulikuwa hadi na kitanda  chembaba cha kupumzikia.

“Mtasubiri hapa  chumba cha mapokezi  kwa dakika chache , bosi kwasasa  yupo bize   na baadhi ya  kazi”Aliongea yule mhudumu na kisha akaondoka na  kuacha  ukimya ndani ya eneo hilo, kulikuwa na runinga pekee ambayo ilikuwa ikionyesha  habari za kifo cha mgombea  wa  uiraisi wa chama tawala ambazo  hazikumvutia  Eliza kwa muda huo

“Hili eneo ni kama vile tupo Ikulu , ndio maana kuna malalamishi mengi kuhusu hili eneo”Aliongea Hamza  maana ukimya wa hilo eneo ni kama vile hakuna kinachoendelea.

“Nimepitia mengi na kuna  kila dalili zinazoniambia kuna kitu hakipo sawa , tunapaswa kuwa makini”Aliongea Eliza na kumfanya Hamza atake kumuuliza swala   ambalo aliambiwa na Dina kutaka kutengenezwa na mheshimiwa Mgweno  kama shushu wao  wa karibu na Regina.

“Una hisi  hivyo?”

“Ndio , unaweza ukawa hujapitia changamoto  nyingi lakini  kama meneja wa idara ya mauzo nimekutana na kila aina ya  wateja  kukamilisha  mauzo ,hatujaambiwa hata ni muda gani tunakutana na Mr Laizer hii inaonyesha wametukalisha hapa makusudi kuvuta muda”Aliongea na kumfanya Hamza kutabasamu.

“Eliza wa  nyumbani ni tofauti sana na wa kazini  unaonekana kuwa makini mno”Aliongea  Hamza.

“Sina utofauti wowote nyumbani na kazini  nipo makini”Aliongea  Eliza  kwa kulalamika lakini kitendo cha  kulainisha midomo  na mate ni kama ilimpa hamasa Hamza kutaka kumkisi  hapo hapo baada ya kuona  wapo wenyewe tu na alichowaza ndio alifanya , alimshika kiuno Eliza  na kumsogelea.

“Ah , wewe unafanya nini?”Aliongea  lakini alionekana kulegea mbele ya Hamza  na  ilikuwa ni kama ishara nzuri kwa Hamza na kuzidi kumsogelea ili  kumkisi lakini Eliza aliwahi kumziba Hamza  mdomo  na kiganja chake.

“Hamza usiwe hivi bwana , hatuwezi..”Aliongea Eliza akijitahidi kuwa siriasi na muda huo ni kama Hamza na yeye alikumbuka kuhusu swala la ndoa  kwamba bado hajamuambia ukweli.

“Sorry Eliza ,  shida ni kwamba tukiwa wenyewe hivi nashindwa kujizuia  kukuangalia unavyovutia”Aliongea Hamza.

“Kwasasa  tuwe  bize na kazi kwanza”Aliongea Eliza kikauzu huku akisogea mbali kidogo na Hamza na kitendo kile kilimfanya Hama kuona huyu sio Eliza aliemzoea.

Walikaa kwa zaidi ya dakika ishirini   bila ya  mtu yoyote kufika na hawakukaribishwa hata kinywaji , Hamza alijikuta akianza kuchoka na kuanza kupiga miayo na walisubiri kwa nusu saa nyingine lakini hakutokea mtu  na muda wa  chakula cha mchana  ulifika na kumfanya Hamza kuhisi  njaa.

“Inaonekana  wanataka kuendelea kutukalisha hapa”Aliongea Hamza

“Tusubiri kidogo?”

“Mimi naona tunapoteza tu muda , kwanini tusiende kumtafuta   wenyewe,tunaweza hata kuuliza  wafanyakazi watuambie ofisi yake ilipo”Aliongea

“Unafikiri itakuwa rahisi wafanyakazi kutuambia?”Aliongea  Eliza  na  muda huo huo mlango  ulifunguliwa  na alionekana  mwanaume aliejazia mwili alievalia singlend tu kama  mcheza basketball.

Mwanaume huyo alikuwa akinuka pombe tu  na  alikuwa ameshikilia  chupa ya  Whiskey mkononi  na macho yake yalikuwa kwa Eliza muda wote kama vile anamtathimini.

“Mrembo nilieandaliwa leo naona   hana ubaya mwenye , kazurii..”Aliongea huku akitabasamu kifedhuli  na  kauli yake ilimfanya Eliza kubadilika.

“Wewe ni nani?”Aliuliza  Eliza na swali lile ni kama lilikuwa kichekesho kwa yule mwanaume kwani alianza kucheka kwa sauti huku akimsogelea Eliza.

“Unauliza nini wakati umeletwa kwa ajili yangu , halafu kwanini umevaa nguo nyingi namna hii au ndio  unatunza joto , hii  mbinu  nimeipenda”Aliongea kilevi  huku akinyoosha mkono kutaka kushika kola ya shati la Eliza lakini  Hamza alikuwa ashamkinga Eliza kwa mbele tayari.

“Bro , nadhani umekosea chumba?”Aliongea Hamza  na kumfanya yule bwana kumwangalia Hamza kwa macho yaliojaa  ukauzu.

“Dogo   wewe ni nani , kwanini unanizuia kuigusa mali yangu?”

“Narudia tena , Bro umekosea chumba “Aliongea Hamza na kumfanya yule mlevi   kukasirika na aliinua chupa  yake na kutaka kumpiga nayo Hamza ya kichwa na kitendo kile kilimfanya  Eliza kupiga kelele , lakini  Hamza aliweza kuidaka kabla hata haijampiga na  ni pombe  tu ilioishia kumwagikia  usoni  na aliishia kulamba  maji maji yaliomfikia mdomoni.

“Sijui nafanya nini , hata mimi naona nishalewa”Aliongea Hamza.

Lakini yule mlevi alijikuta akikasirika zaidi na aliinua mkono kutaka kumpiga Hamza kibao lakini kabla ya kumfikia  Hamza alikuwa ashainua mguu na kumpiga nao tumboni.

“Bang!!”

Yule mlevi alijikuta akishindwa kuhimili nguvu iliomsukuma na kwenda kuvaa  pot  ya maua na kudondoka nayo

“Fuc*k you”

Bwana yule alijkuta akitukana  na alisimama kwa tabu na kumsogela Hamza kwa mara nyingine  huku akiwa amekunja ngumi , lakini Hamza alisimama katika eneo moja na baada ya kumkaribia alimpiga ngumi ya kifuani  iliomfanya yule bwana kudondoka tena chini huku  akiwa amepiga magoti  na kuanza kutapika pombe iliochangayikana na damu.

Eliza aliekuwa nyuma aliweza kuona  Hamza alikuwa amemuadhibu yule mlevi kwa  mashambulizi mawili tu mpaka kutapika damu , alishindwa kujizuia  na kuishia kushikwa na hofu asijue cha kufanya.

Hamza  alimsogelea yule  mwanaume na kisha alimkanyaga mgongoni  na kumfanya  alale kifundi fudi.

“Sema wapi alipo Laizer”Aliongea Hamza

“Unajitafutia kifo , mimi ni mgeni hapa unathubutu vipi kunishambulia?”Aliongea  kijeuri na kumfanya Hamza  anyanyue mguu na kumkandamiza kwa nguvu kwenye bega  lake  na kumfanya  apige mayowe kwa maumivu makali.

“Ongea  wapi alipo  Laizer?”Alirudia Hamza.

“Sijui  alipo , mimi sijui kweli”Mtu yule wa miraba minne alijikuta  akianza kuingiwa na woga .

“Unaendelea kujifanya   mtiifu sio , mpaka muda huu bado unaigiza?”Aliongea Hamza huku akizidi kumkandamiza kwenye bega lake.

“Nilikuwa nikifuata maagizo  tu , mimi sijui  kweli alipo”Aliongea yule bwana na muda huo ni kama Eliza alishituka.

“Hamza anasema ametumwa na  Mr Laizer?”.

“Kuna haja hata ya kuuliza , huyu katumwa kuja kukuigizia hapa  kukuogopesha ili usahau hata  kuulizia hela”Aliongea Hamza.

“Mbona wameenda mbali hivyo , sidhani Mr Laizer anaweza kukosa milioni themanini iliobaki”

******

Upande wa makao makuu,  Regina akiwa ndani ya ofisi  yake alijaribu kumpigia  Hamza lakini ajabu alikuwa akiambiwa simu yake haipatikani.

Na alianza kushikwa na wasiwasi  kutokana na  bibi yake alimsisitizia  kupitia simu  anataka  kuonana na Hamza siku hio  bila ya kukosa ,  sasa kwa mtu ambae alikuwa  siku za mwisho mwisho ombi lake  lilipaswa kutimizwa bila ya kuchelewa  ndio maana Regiina  alikuwa na wasiwasi.

Lakini anajaribu kupiga simu yake sasa haipatikani , muda uleule aliamua kumuita  Linda ofisini kwake.

“Mkurugenzi kuna maagizo yoyote?”Aliongea Linda.

“Hamza yupo wapi?”Aliuliza na kumfanya Linda mwili kumkakamaa.

“Ametoka nje ya ofisi kikazi?”

“Kwenda nje kikazi ,  nje ya wapi na  ni kazi gani?”Aliuliza Regina  kutokana na kwamba hata yeye alishangaa kusikia kauli hio.

“Kuna  zile  pesa zilizobakia za tenda kutoka kampuni ya  Dede Bagamoyo , mkurugenzi wao alipiga simu   na kusema atafanya malipo ya  Cash na Meneja Eliza anapaswa kuyafuata  leo , ilipangwa Eliza kwenda na  Kapteni Yonesi kama mlinzi wake  lakini bado hajapona kabisa , hivyo nilimpa kazi hio  Hamza  kwenda nae  ,  maana anaonekana kuwa na nguvu zaidi ya  Kapteni..”Aliongea Linda na kumfanya Regina  ukauzu kumvaa.

“Nani kakuambia umpangie kazi ya namna hio?”

“Lakini bosi si ulisema nimpe kazi  asikae bure”

“Hebu  nyamaza , Hamza ni msaidizi wangu mimi , inakuwaje atoke hapa aende kuwa bodigadi wa  meneja wa idara ya  mauzo , nimekwambia mpangie kazi na sio  kumhamisha idara ,  akili yako inawaza nini?,  hivi unadhani  mimi nimekuwa kipofu , hata kama una wivu kutokana na uwezo wake  kwenye baadhi ya mambo  hupaswi kuonyesha wivu wako kwa  kufanya maamuzi ya namna hii ,  yaani umefanya kazi  na mimi kwa zaidi ya  miaka mitatu lakini unashindwa kukua kimawazo” Regina alibadilika na kuwa mbongo na kuanza kumfokea sekretari wake.

Linda macho  yaligeuka  kuwa mekundu huku akiinamisha kichwa  kwa hofu  kubwa.

“Nisamehe   bosi , nimekosea.. , nitampigia mara moja arudi’Aliongea  Linda akijitetea.

“Haina haja  nishampigia mara kadhaa na simu yake haipo hewani , nadhani kaizima au  hakuna mtandao”

“Lakini bosi  wanazimaje simu , wameenda  Msata  makao makuu  ya Dede kwanini  mtandao usipatikane”Aliongea Linda na muda ule ni kama  Regina anasikia vizuri  sasa.

“Dede si wana ofisi yao  Posta  na  ndio tulikubaliana  makabidhiano ya malipo yatafanyikia hapo , kwanini wameenda Msata?”Aliuliza Regina  ni kama  aliona kuna taarifa ambazo hajaletewa.

“Ndio walivyotoa maelekezo ,  mara  ya mwisho siku yao ya kulipa waliomba kuongezewa siku mpaka leo  na  Eliza ndio afuate Cash, idara ya  mauzo ndio walifanya makubaliano na  Dede na  ofisi ya  Finance wameipa siku kumi idara ya  sales kukamilisha hesabu  la sivyo wataripoti  idara ya sheria…”

“Kwahio wamemwambia Eliza aende na akakubali kwenda ,  hivi ni habari ngapi mmesikia kuhusu   mambo yanayofanyika huko  Msata , ukute hata hizo Cash wanazotaka kutoa ni kwa ajili ya  kutakatisha hela , mlipaswa kuwakatalia na sio kwenda kichwa kichwa ,si walikubaliana wakutane  Posta kwenye makabidhiano?”Aliuliza  Regina lakini  Linda hakuwa na jibu zaidi ya  kukaa kimya

“Dede wanafahamika kwa  kutapeli  watu kupitia madeni yao , wakikataaa  deni lao Eliza  ana  uzoefu wa kutolazimisha na kuacha sheria ichukue mkondo wake , lakini wewe umemjumuisha Hamza ambae anapenda kujichukulia sheria mkononi , unataka akaibue matatizo mengine?”Aliongea  Regina huku akimwangalia Linda  kwa  macho ya kukatishwa tamaa.

“Nisamehe bosi sikufikiria mbali”Alijitetea lakini Regina  hakuwa na mudi  kabisa ya kuendelea kumuona.

“Unaweza kuondoka , unapaswa kuomba  yasitokee matatizo na warudi  wakiwa salama  la sivyo jiandae kuandika barua  ya kuacha kazi”Aliongea Regina kikauzu  na kumfanya  Linda kuinua uso wake  huku akimwangalia bosi wake kwa  kutoamini.

“Bosi , kwani Hamza  ni wa muhimu sana?”Aliuliza Linda.

“Ndio ni wa muhimu”Aliongea kikauzu na kauli yake ilimfanya Linda kutetemeka  na aliishia kuondoka kwa hatua hafifu  na kufunga mlango.

Ukweli ni kwamba  Regina hakujua  kwanini alikuwa na wasiwasi Hamza angesababisha matatizo huko Msata ,  kulikuwa na mambo mengi yanaendelea nchini  ikiwemo taarifa za mgombea wa uraisi kuuliwa  na mengineyo  na  aliona  Hamza anaweza kutibua zaidi hali.

Baada ya kukaa akiwaza cha kufanya palepale  alichukua simu yake  na kuitafuta namba  ya  Meneja wa hoteli yao ya nyota tano   Bagamoyo  mjini.

“Mkurugenzi  habari za mchana , kuna  maagizo  yoyote?”Sauti  ya mwanaume ikiongea kwa heshima ilisikika.

“Hebu  tuma  mtu yoyote  kutoka hotelini  aende  Dede  kuangalia kinachoendelea, Meneja Eliza na  msaidizi wangu  wapo  huko  na hawapatikani hewani”Aliongea

“Sawa  Mkurugenzi nina mtu yupo maeneo ya  Msata  nadhani itakuwa rahisi  kwenda kuangalia nitakupa majibu muda si mrefu”Aliognea mkurugenzi na  Regina alikata simu.

Hamza ametengenezwa  mpango wa kwenda  Dede bila  kujua , ngoja uone.

Previoua Next