Reader Settings

 

SEHEMU YA 65.

Wakati Hamza akiwa amembana yule mwanaume mlevi chini na mguu wake, yule mhudumu ambae aliwakalisha hapo aliingia kwa haraka huku akiwa na hisia mchanganyiko ilikuwa ni kama hakuwa ametegemea tukio hilo au hata kama alitegemea hakuwa na jinsi ya kulizuia kutokana na maagizo ya bosi wake.

“Samahani kaka , nini kimetokea?”Aliuliza yule mwanamke  na Hamza aliacha kumminya na kumpiga teke.

“Huyu  bwana amekuja hapa na mapombe yake na kutaka kumdhalilisha Meneja,hili  eneo inaonekana lina usalama mdogo sana kwa watoto wa kike”

“Mr Hamza najua amekosea kweli , naomba umwachie  kwanza”Aliongea yule mwanamke huku akimwangalia yule mwanaume wa miraba minne alivyodhbitiwa na Hamza na ilimfanya kuonyesha hali ya mshangao.

“Sio kirahisi, huyu mtu alitaka  kumdhalilisha  meneja na kwa ninachoona hapa  pengine sio tukio la kwanza , hivyp napanga kupiga simu polisi waje hapa wafanye uchunguzi”.

Yule mhudumu mara baada  ya kusikia kauli hio alijikuta akikakamaa , sio kwamba alikuwa akiogopa polisi, ukweli ni kwamba  yametokea matukio mengi ya polisi  kuja eneo hilo lakini hawakufanya chochote zaidi ya kuzuga, bosi wa hilo eneo alikuwa ameliweka jeshi la polisi  mfukoni mwake, kilichomuogopesha ni kwamba swala hilo linaweza kumfanya kupoteza  kibarua chake.

“Naona samahani kwa kile kilichotokea, lakini kabla ya kuwasiliana na polisi naomba kwanza niwasiliane na bosi wangu ili  nione kama ananipa maagizo gani”Aliongea na kwa haraka sana alikimbilia nje kufanya mawasiliano.

“Vipi ushawahi kupitia  tukio kama hili?”Aliuliza Hamza na El,iza alitingisha kichwa kukataa.

“Sijawahi  nimeshangaaa Mr Laizer  kupanga kitu kama hichi kwa ajili ya kutotaka kulipa”Aliongea  Eliza.

“Kuna  kitu  hakipo sawa hapa ,  hata mimi sidhani yote haya ni kutotaka kulipa  kama ni mfanyabiashara kwanini  akatae kulipa”Aliongea Hamza.

“Unataka kumaanisha  pengine kuna sababu nyingine zaidi ya kulipa  deni?”Aliuliza Eliza.

“Kwasasa hatuwezi jua , lakini kwasababu nipo, wewe usiwe  na wasiwasi , nina hamu ya kuona ni kitu gani wanapanga”Aliongea Hamza na muda huo yule mhudumu alirudi mbio  mbio.

“Naomba  mnifuate tafadhari bosi yupo vyumba vya ardhi kwenye Kasino”Aliongea na  kauli ile ilimfanya Hamza kushangaa  kidogo na kujiuliza inamaana hii sehemu ina vyumba vya ardhi.

Hamza alimpa ishara  Eliza kutokuwa na wasiwasi  na palepale alitoa tabasamu akimwangalia yule mhudumu.

“Hakuna shida  tangulia tuelekee huko”Aliongea Hamza na yule mhudumu  aligeuka na kuanza kutembea  kuwapeleka vyumba vya ardhi.

Walitembea  mpaka mwisho wa Korido na mwishoni kulikuwa kumejengwa kijumba kidogo  kama kabati kubwa  kilichopakwa rangi nyeupe , kwa kuangalia tu ungegundua ni  kijumba ambacho hutumika kama mlango wa kuingilia kwenye lift kuelekea upande wa chini.

Eliza ndie ambaye  alionekana kushangaa zaidi kuliko hata ya Hamza ,  katika eneo hilo kulikuwa na eneo kubwa mno  ambalo katikati ya eneo hilo kulikuwa na ulingo  takribani ukubwa wa mita sitini za mraba.

Ulingo huo wa mzunguko ulikuwa umezungukwa  na viti virefu ambavyo vilikuwa vimekaliwa  na wanaume , wanawake  na hata  watoto walikuwepo.

Kwa haraka haraka tu utaweza kusema watu hao wote ni wale wenye  uchumi wa juu sana, yaani watu walioyapatia maisha.

Ililikuwa ni eneo la kushangaza mno  tena kuwepo ndani ya ardhi ya nchi kama  Tanzania.

Kitu ambacho kilimshangaza Hamza na Eliza  ni kwamba  watu hao wote waliokuwa hapo ndani walikuwa wamevalia  vinyago usoni  kana kwamba walikuwa wakiogopa  sura zao kuonekana.

Ijapokuwa ni eneo  ambalo  lipo chini ya ardhi lakini  mwanga  wa taa za  rangi tofauti  tofauti zilimulika na kufanya  eneo  lote kuonekana kupendeza zaidi.

“Huu ni uwanja wa mapigano unaitwa NunguNungu ,Bosi yupo pale  upande wa VIP , mimi naruhisiwa kuishia tu hapa”Aliongea yule mhudumu  na kwa ukauzu  aligeuka na kuondoka akiwaacha Hamza na Eliza.

Hamza na Eliza waliinua vichwa vyao upande ambao  walielekezwa na yule mhudumu  na waliweza kuona pande zote nne za steji  kulikuwa na viti virefu , masofa  na  aina nyingine za thamani.

Kulikuwa na  wanaume kadhaa ambao ndio pekee hawakuwa wamevalia vinyago  na mmoja kati yao alikuwa ni bosi Laizer  ambaye amevalia mavazi ya kitamaduni ya kimasai , alionekana kuwa na uso uliozeeka kidogo, licha ya umbali na mavazi yake  ya kitamaduni lakini saa ya  Luis Dantoni ya  rangi ya  almasi ilikuwa ikionekana.

Sekunde ambayo Hamza na Eliza walitaka kusogelea eneo lile sauti   zilianza kusikika  upande wa  uliongo  watu wanaopigana.

“Kill him , Kill him!”

Zilikuwa ni sauti za kingereza  zilizokuwa zikitoka kwa watu, ilimpa Hamza uelewa kwamba inawezekana wengi wambao wapo ndani ya eneo hilo walikuwa ni  wageni na sio raia  wa Kitanzania, ni kweli kwamba kati ya watu waliovalia vinyago walikuwa   wana ngozi  nyeusi na za kizungu lakiini ilikuwa ngumu kuwatofautisha wala kuwafahamu.

“Tumia nguvu,  Yess!, kata sikiio  lake  la kulia kwanza , yeah yeah safii”Zilikuwa ni kelele za kutisha  na kwa  jinsi  ambavyo walikuwa wakiongea  ni dhahiri kabisa  watu hao wote walikuwa na roho za kikatili mno , yaani wanashangilia mtu  kuulizwa kwa  ukatili mkubwa.

Katika steji ya ulingo wa mapigano  alionekana mwanaume wa miraba  minne  mweusi  ambaye damu  na jasho vilikuwa vimemloanisha  na alikuwa amemshikilia mwanaume mwingine mwenye ngozi  nyeupe shingo  yake huku akiwa na kisu alichokielekezea  shingoni.

Yule mwanaumne alieshikiliwa alionekana  kujitahidi kuhangaika ili kujitoa katika  mikono ya yule mwanaume wa   miraba minne , lakini   alikuwa ameshikiliwa vyema  kiasi kwamba  hakufurukuta.

Dakika  ileile kilichosikika ni shingo ya yule mtu kuvunjwa na kupoteza uhai palepale huku akiwa hana masikio kwani yalishakatwa.

Kitendo cha  bwana yule kuondoka  chini na kupoteza maisha ilifanya  kundi  la upande wa kulia kuanza kushangilia kwa furaha kubwa.

“Tumeshinda , tumeshinda …!!”Ilikuwa ni kama wote wamepandwa na ukichaa  na  walianza kurusha  maburungutu ya hela pamoja na  vito vya thamani kwenye  ulingo.

Jambo lile lilimfanyua Eliza  kutetemeka  kiasi cha kujificha nyuma ya  Hamza.

“Hamza  please naomba tuondoke , hii sehemu inatisha mno”Aliongea  Eliza kwa sauti ya kuomba.

Upande wa Hamza  alijua Tanzania  pia kuna  matukio ya ulimwengu wa giza  lakini hakutegmea  ingekuwa hatari namna hio, ukweli ni kwamba alishasikia tetesi  za kitu kama hiki ,  kipndi ambacho alikuwa mtu wa kuperuzi sana mitandaoni alisikia malalamishi kibao kutoka  kwa watu  wakisema baadhi ya ndugu zao wamepotelea katika jengo hilo , sasa kile ambacho anaona  ilionekana ilikuwa ni kweli kabisa,  pengine waliongia hapo ndani  waliingia kupigana na kilichowatokea   ni kupoteza maisha na maiti zao  kutoweshwa.

“Usiogpe Eliza ,ukiondoka  si ndio kitu ambacho  Laizer anataka  kitokee, hili eneo linaonekana kuwa siri lakini kafanya makusudi kutuleta hapa ili tumuogope na  uache kumdai”

“Lakini…”

Hamza ilibidi amtulize , ijapokuwa kwa mwanamke kama  Eliza kwake  eneo hilo lilikuwa likitisha lakini kwa watu wengine ilikuwa ni burudani  ya aina yake na hata kuingia hapo   pengine walilipia  pesa nyijngi sana.

“Kama ushawahi kusikia Black Boxing Market  ndio hii sasa , zipo  nyingi duniani  na zinaendeshwa kwa siri , ndio mahali ambapo  matajiri  wanatafuta   msisimko wa furaha ya tofauti , haya matukio yote yanayoendela hapa yanarekodiwa  na kuonyeshwa kwenye mtandao wa DeepWeb kama njia ya matangazo  kujiingizia pesa zaidi , ndio maana  hapa wentgi wanaonekana sio  raia wa kitanzania”Aliongea Hamza.

“Lakini huu ni ukatili unaofanyika”Aliongea Eliza.

“Katika Dunia hii furaha inatafutwa kwa  njia tofauti sana, kuwa  na kila kitu hakumfanyi mtu kuwa  na furaha ndio maana   kuna starehe  za namna hii,   wewe  nifuate mimi na  tufanye kile kilichotuleta kisha tuondoke”Aliongea  Hamza  na kumfanya  Eliza kumwangalia  kwa macho  ya kusita , kwa namna ambavyo Hamza alikuwa akijiamini aliona ni kama vile ni mtu ambae ashaingia kwenye maeneo kama hayo mara kibao.

Mara baada ya kufika eneo  la VIP yule bwana alievalia  kitamaduni alionekana kuwaona.

“Nimefurah kuwaona  nyie wageni wetu wa heshima kutoka kampuni ya Dosam , mniwie radhi  kwa  kutokuja kuwapokea kwasababu ya ubize”Aliongea  Laizer  huku  akifurahishwa na namna ambavyo Eliza alionekana kutetemeka.

“Mr Laizer tupo hapa kwa ajili ya kukusanya malipo ya mwisho ya tenda, lakini mazingira ya hapa yanaonekana kutokuwa mazuri kuongea”Aliongea Eliza

“Hili eneo ni zuri kabisa kuongelea  maswala ya hela , hivi unajua  wageni wangu wote unaowaona hapa wamelipia zaidi ya milioni mia  kama kiingilio, kwasababu mmefika  ngoja mliwekee  baraka kidogo hili eneo”Aliongea  na muda uleule alimwangalia mwanaume alievalia kinyago alionekana kama mhudumu na kumpa ishara ya kusogea.

“Leta mvinyo huo kwa ajili ya wageni wetu”Aliongea na  Mvinyo wenyewe haukua mbali, mhudumu yule  alimimina mvinyo kwenye glasi  mbili  na Bosi Laizer aliinua glasi yake juu kama ishara  ya kuwakaribisha.

“Meneja mnapaswa kunywa huu mvinyo kama ishara ya heshima  kwa ajili ya hili eneo”Aliongea na muda uleule  alikunywa  mvinyo uliokuwa kwenye glasi yake huku akitoa tabasamu lililojaa uovu.

“Samahani Mr Laizer situmii mvinyo wenye kilevi”Aliongea Eliza akijitetea.

“Kama nilivyosema sio swala  la kunywa ama kutokunywa  ni ishara ya heshima ndani ya hili eneo”Aliongea huku akiwa na muonekano usiokuwa na furaha.

“Macallan ni moja ya mvinyo  bomba sana hasa huu wa miaka ishirini na tano , unaonaje  nikinywa kwa niaba ya Meneja nadhani  maana ni ileile”Aliongea Hamza.

“Unaonekana upo vizuri sana  Mr Hamza  likija swala  la Mvinyo mpaka umejua jina lake”Aliongea Laizer na Hamza hakujali sifa  zake, alichukua  kile kilevi cha  Eliza pamoja na cha kwake na kunywa vyote kwa mikupuo miwili.

“Mr Laizer tunaweza kusogea  sehemu iliotulia, ili kwenda  moja kwa moja kwenye  lengo letu”Aliongea Eliza akiwa tayari ashatoa karatasi kutoka  kwenye mkoba wake.

“Mbona haraka hivyo”

“Mr  Laizer bado nipo kazini na  nina kikao  baada ya hapa , kwanini tusiongee  haya makabidhiano ya hela kwanza , kampuni yetu…”

“Eliza..”Laizer alimkatia  hewani asiendelee kuongea.

“Una hisa ndani ya kampuni ya  Dosam?”

“Sijafanyakazi kwa muda mrefu ndani ya kampuni , ni vigumu kuwa na hisa”

“Kama hisa huna kwanini unafanya kazi kwa juhudi kiasi hiki, ni faida gani kubwa unapata tofauti na mshahara?”

“Haijalishji napata  kiasi gani cha mshahata hii ni kazi na napaswa kuichukulia siriasi”

“Hivi katika  dunia ya leo kuna  sababu  nyingine ya kufanya kazi kwa bidii tofauti na kupata hela?”Aliongea na muda huo alionekana kuchukua cheki kutoka kwenye mikono ya  msaidizi wake.

“Nitakuandikia cheki ya milioni ishirini  hapa  na hela zinataingia kwenye akaunti yako binafsi , kuhusu   malipo mengine  mnaweza kunishitaki tu”

“Mr Laizer unajaribu kunipa rushwa?”

“Sio kukupa rushwa  ninachofanya hapa ni kukununua”

“Kuninunua!?”Eliza hakuamini maneno ya Laizer  na aliishia kukunja ngumi kwa hasira.

“Meneja wewe ni mwanamke mrembo sana ,  na nimekupenda  ghafla tu , unaonaje ukichukua milioni ishirini  na kuwa na mimi kwa mwezi mmoja, hii ni hela  rahisi  mno  kuliko  mshahara unaopata  kwa jasho jingi”Aliongea na kauli ile ilimfanya Eliza kubadilika na kujawa na hasira   na ukauzu kwa wakati mmoja , ni kweli ametokea familia  ya kimasikini lakini hakuwa tayari utu wake kushushwa thamani.

“Mr Laizer  ukiongea tena , nitakushitaki  kwa kosa la  unyanyasasi””

“Unishitaki .. hahaha.. huu ni utani ambao sijausikia kwa muda mrefu ,  mwanamke wa kariba yako ya kukutokuchangamka  umewezaje kuwa meneja  wa kampuni kubwa?”Aliongea huku akiendelea kucheka, aliamini  mwanamke mrembo kama Eliza ili kuwa  meneja lazima atumie uzuri wake na alitaka kutumia njia hio hio kumhonga.

Eliza alikuwa na hasira mno na kwa ilivokuwa ikionekana Laizer hakuwa na mpango wa kulipa na  aliona swala hilo lishakuwa la kisheria tayari.

“Hamza tuondoke tu”Aliongea lakini Hamza alikataa palepale.

“Hatujapata hela tulioijia hapa , tunaondokaje kirahisi?”Aliongea na kumfanya Eliza kushangaa maana hakujua Hamza alikuwa akipanga nini.

“Kwahio unasema  bila hela hapa huondoki?”Aliuliza  Bosi Laizer.

“Mwanzoni sikuwa nikijali  swala  la hela na nilitaka kuona nini kinaendelea hapa ndani, lakini nimebadilisha mawazo”

“Nini kimekufanya kubadili mawazo?”Aliuliza Laizer.

“Hakuna sababu kubwa ,  cha kwanza umetufanya tusubirie muda mrefu  na kisha ukatuma mtu wa kuja kutuogopesha , lakini sasa hivi unaanza  kuongea uchafu wako  kumtania meneja wetu ,  hatuwezi kupoteza muda wote  huo tuliokuja hapa  na kuondoka mikono mitupu , kingine nimekuja hapa kama mlinzi wa meneja ,  unadhani nitaonekana vipi  ikisikika kwamba  niliangalia tu  bosi wangu akidhalilishwa?”Aliongea Hamza na kumfanya  Bosi Laizer macho yake kuchanua.

“Hivi unajua  muda mwingine muonekano wa mwanaume unaweza kumfanya   kupoteza maisha hata kama hana kosa?”

“Acha kujaribu kuniogopesha ,  nakushauri   tulipe kilicho chetu tuodoke kwa amani na sio kutupotezea muda , sisi wote ni watu wazima  michezo kama hii ya kitoto ishapitwa na wakati”Aliongea  Hamza huku akikaa chini kabisa  na  kauli yake ilimfanya Laizer kushangaa maana siku zote vijana ambao  alikuwa akiongea nao walionyesha   kumuogopa, palepale alijikuta  akisimama na kuangalia mbele kwenye ulingo.

“Ukiangalia hili eneo lote  ubunifu wake ni  wa Kirumi,  hii inakupa hisia gani?”Aliuliza akionyesha kuwa siriasi.

“Ninachoona   hapa ni ushenzi tu unaendelea ,  muda mchache uliopita nimeona mtu akipoteza   maisha kwenye ule Ulingo , huwa miili yao unapeleka wapi , vipi kuhusu waliojeruhiwa wanatibiwa wapi?”Aliongea Eliza.

“Meneja Eliza  unadhani  anaeingia  ulingoni  ni kwa ajili ya kutoka  bila  majeraha au kufa , hapa hakuna cha daktari ukiumia umeumia , ukifa umekufa”Aliongea.

“Hizi sio Karne zilizopita , hii  ni Tanzania inayoendeshwa  kwa sheria na haki za binadamu na watu sio watumwa wako , inakuwaje  unawachukulia binadamu kama vile ni wanyama, sijawahi kuwaza  ndani ya nchi yetu iliojaa amani  kuna vitu kama hivi vinafanyanyika , huu ni  ushenzi”Aliongea  kwa  kufoka lakini  Laizer hakuonyesha kukasirika hata kidogo na alinyoosha kidole chake kuelekea ulingoni.

‘”Wale  unaowaona pale  nimewanunua kwa pesa nyingi  na unajua  alieniuzia ni nani? , hawa wote ni wafungwa wenye vifungo aidha vya maisha au  wamehukumiwa kuonyongwa, wengine wamejileta  wenyewe  kwa ajili ya kutafuta  hela ,  hebu chukulia wewe ni mfungwa  adhabu yako ni ya kifo  na kuna njia kama hii ya kuweza  kupigana aidha kufa katika ulingo au kushinda na kupata hela na kisha kujiokoa na adhabu ya kifo  ni kipi utachagua?,  wewe utaniita kila jina baya lakini  wao wananiita Mwokozi niliewapatia tumaini, hebu kwanza waangalie  wanavyopigana , unadhani kuna wakulazimishwa pale?”Aliongea  na kisha aligeukia wageni wake.

“Hebu angalia na watazamaji, angalia  walivyocharukwa na akili kutokana na furaha ,  kukurahisishia  ukishakuwa mfungwa muda mrefu na  ukapewa nafasi kama hii , watazamaji hawatakuonea huruma , watakuona kama  mambwa tu wanaojaribu kushindana ndio maana wanafuraha  hio”

“Hawa watu ni kwamba tu huwezi kuona sura zao, lakini unadhani hawa wanatokea wapi ,  hapa kuna  wanasheria ,  wanasiasa ,  wanajeshi,  wajasiriamali  wakubwa tu  mpaka  watu wa dini wapo hapa,  ndio watu ambao wapo  katika ngazi za juu kimaisha kwenye jamii zetu , watawala wetu,  lakini wapo tayari kulipa mamilioni ya pesa kwa ajili ya kumuona  Mfungwa akimuua mfungwa mwenzake  kama sehemu ya starehe”Aliongea Laizer bila ya kubadilisha muonekano.

Eliza aliishia kukamaaa mwili bado hakukubaliana na maneno yake lakini  alishindwa pia  kujua namna ya  kupinga.

Hakuelewa kwanini watu  kama hawa ambao  walionekana   kuheshimika katika jamii  na kuwa na elimu kubwa kuja kulipa kiasi kikubwa cha pesa kwa ajili ya kumwangalia binadamu akimpiga mwenzake mpaka kufa   na kisha kushangalia.

“Meneja inaonekana  bado hujanielewa tu , mimi sio mkatili . unachokiona hapa ndio asili  halisi ya binadamu  akiwa  nje ya sheria  na haki ,  binadamu ni mnyama hatari zaidi ya wanyama wote  tena zaidi ya mkatili  ukimwondolea vifungo vya sheria, haya sio maneno yangu  ni kutoka  kwa  mwanafalsafa  mkubwa wa kihistoria Aristotle,  na   alikuwa sahihi  maana unachokiona ndio uhalisia wa maneno yake”Aliongea Laizer na aliinama na kuchukua Whiskey  na kupiga pafu mbili na kisha akaendelea.

“Hili eneo ndio sehemu pekee ndani ya Tanzania hii   ambalo hakuna sheria , wala mfumo wa aina yoyote ile , Sheria ya msituni pekee ndio inatumika hapa, uwezo  na nguvu ndio kitu pekee chenye  maana hapa  na mimi  Laizer Kayole  ndio mungu wa hili eneo”Aliongea  huku akitoa  tabasamu la kujivunia  hasa pale alipomuona Eliza amekosa neno la kuongea lakini  alishangaa kuona  Hamza hakuwa na  mabadiliko yoyote   na macho yake yalionyesha ukauzu  usiokuwa wa kawaida.

“Mr Hamza naona ni kama hujakubaliana na mim”

“Nafikiria kwanini  unangea pumba zako  kutupotezea muda na huna mpango wa kulipa”

“Kwahio unaona naongea pumba?”

“Ndio, unaongea pumba , nishasema unachokifanya ni mambo ya kitoto  na huwa sipendelei  michezo ya namna hii”Aliongea na kumfanya Laizer   uso wake kucheza.

“Mr Hamza nimesikia umemuumiza kijana  wangu aliekuwa amelewa , najua ana kiu ya damu lakini bado ni mtoto  kwako  lakini haogopi chui”

“Mini natokea ukoo wa farasi  na  nina uhakika  wewe sio Chuii”Aliongea Hamza

“Haha.. kumbe unajua kuongea utani , sio mbaya nimependa  kujiamini kwako , kama nilivyosema  uwanja huu wa mapambano wa Nungunungu kinachoangaliwa ni nguvu  pekee  na uwezo , kama kweli unataka kuondoka na  milioni  mia nane  zote basi  onyesha kama  uwezo unao”

“Oh , na ndio naonyeshaje sasa?”

“Hii sehemu ukiingia lazima  ulipie kama sio hela basi ni mwili wako”

“Kwahio unamaanisha kama nikiingia ulingonni na kupambana  kama mwanaume na kushinda ndio nitaweza kulipwa deni?”

“Hamza nini ,  hapana.. ni hatari sana tuondoke tu”Aliongea  Eliza kwa kupaniki lakini upande wa Hamza alikuwa na tabasamu na kumwambia apunguze wasiwasi.

Upande wa Laizer aliishia kutingisha kichwa kwa tabasamu akionyesha kukubali.

“Haitokuwa fair sasa , sisi tupo hapa kwa ajili ya kukusanya madeni yetu  na haina haja ya kupambana kwani ni haki yetu  , kama nikipambana na nikishinda sitofaidika  kwa chochote”Aliongea Hamza.

“Mr Hamza upo sahihi , unaonaje tukifanya hivi, kama ukishinda sitotoa milioni  mia nane  pekee mnazonidai  bali nitatoa kiasi chote cha pesa  kilichopatikana leo hii”

“Ndio shilingi ngapi?”Aliuliza na bosi Laizer alimgeukia  bwana aliekuwa nyuma yake.

“Mpaka sasa tumeingiza  milioni mia tisa bosi”Aliongea  na kumfanya Hamza kushika kidevu , zilikuwa ni pesa nyingi mno kwa mahesabu ya Kitanzania ambazo zimeingizwa kwa siku moja tu.

“Deal!!”

Aliongea Hamza akikubali kuingia kwenye ulingo  na kumfanya Laizer kutoa  tabasamu  la kikatili  wakati huo  Eliza akiwa  na hofu kiasi kwamba  mwili ulianza kumtetemeka , alijiuliza  Hamza katoa wapi tamaa ya pesa kiasi hiko.

Baada ya  kukubaliana na Hamza  Laizer alionekana kujawa na furaha na alichukua  maiki yeye mwenyewe na kisha kutoa tangazo.

“Mabibi na mabwana  tunakwenda kuanza mechi ya kipekee ambayo  mshindani wetu hatopitia  raudi   ya kwanza , tunaye  Hamza hapa kutoka jijini  Dar es salaam  na ataingia  kwenye ulingo moja kwa moja  na kupambana na Maddog nambetia  kiasi chote cha pesa kilichopatikana tokea asubuhi”Aliongea na kauli ile ilifanya watu washangilie  kabla hata  hajamaliza.

Muda huo Hamza alikuwa ashapanda kwenye Steji tayari na kufunguliwa mlango kuingia kwenye Arena na mara baada ya mashabiki  kumuona mtu mwenyewe anaenda kupambana na Mad Dog  walijikuta wakianza kumdharau.

“Huu ni utani , yaani hata  hajatuna mwili  anataka kupambana na  Mad Dog”

“Mad Dog  hajawahi kuwa  na mpinzani tokea  kufunguliwa kwa hili eneo, huyu  binadamu anakwenda kung’atwa mpaka afe”

“Nitambetia  kama ataweza  kumshida  Mad Dog”Aliongea  mzungu mmoja alievalia kinyago  na wengine walianza kubeti  kati ya mpiganaji  aliepewa jina la Mad Dog  na Hamza , wengi walichagua upande wa Mad Dog kushinda.

Eliza mara baada ya  kukaa chini na kuangalia  kile kinachoendelea moyo wake ni kama ulikuwa  umehama upande.

Hakujua imekuwaje hali ikafikia hatua hio , alitamani kupiga simu kuelezea kile kinachoendelea lakini  tokea waingie hilo eneo  simu zao hazikuwa zikisoma mtandao kabisa.

Muda huo kitu pekee ambacho aliona anaweza kufanya ni kumuombea Hamza kushinda na si vinginevyo.

Upande wa Hamza alikuwa na utulivu wa hali ya juu  akimwangalia  Eliza kwa namna  ya kumtuliza.

Muda huo huo  makelele yaliweza kusikika , kwa jinsi  watu walivyokuwa wakishangalia utadhani ni  michezo ile ya mieleka inayoonekana kwenye  runinga , hata taa za  manjonjo zilimulika eneo  ambalo anatokea  bwana ambae alijibatiza jina la Mad Dog.

Licha  ya kwamba  yanayofanyika hapo ni mambo ya kikatili lakini  ukweli ni kwamba yalikuwa na msisimko mkubwa mno  hasa namna ambavyo  Mad Dog   anaimbwa na watu  kwa furaha kubwa.

Mwanaume huyo  alikuwa amejengeka  mno mwili kimazoezi, alikuwa sio mwafrika kama ambavyo  Hamza alitegemea bali alionekana kuwa mzungu ambae amenyoa kipara huku akiwa amefunika uso wake na kinyago.

Mad Dog alionekana ni kama vile hakutaka kujulikana  yeye ni nani kwa sura  lakini licha  ya hivyo watu waliendelea kumshangalia.

Ukimlinganisha Hamza na yule bwana  ilikuwa ni kama vile ni mtoto na anakwenda kupambana na  mtu mzima.

“Hahah… huyu  mtoto  hajaanza kujikojolea  bado tu”

“Hey! Mad Dog  kill him , nitakulipa dola laki tano ukimuua huyo dogo”

“Nitatoa  Dolla laki sita Cash nikiona umeunyofoa mguu wake”

“Mimi  nne  ukinionyesha uume wake ulivyo kwa ndani”

Makundi ya watu kwa watu ni kama walikuwa wakishindana  kuonyesha nani analipa zaidi   lakini masharti yao yalikuwa yakikatili mno.

Kitendo cha Mad Dog kuahidiwa kiasi  cha pesa ni kama mzuka ulianza kumvaa na  licha ya kuwa na mwili mkubwa  miguu yake ilianza kucheza cheza kwa wepesi, licha ya kwamba alikuwa amejifunika na kinyago lakini  macho yake yalionyesha hali ya ukatili.

Mara  baada ya kipenga cha pambano kuanza  Mad Dog alimsogelea Hamza kwa spidi huku akiwa amekunja ngumi  na alipomfikia aliirusha kumlenga eneo   la kichwa.

Hamza  kwa wepesi kabisa alisogea pembeni na ngumi ile ilipiga hewa  kiasi cha kumfanyaMad dog  akose mhimili na kutaka kudondoka maana alikuwa ametumia nguvu  kubwa.

“Unatumia nguvu kubwa , unaendana vyema na jina lako la mbwa kichaa”Aliongea Hamza,

“Damn huyu chalii ana bahati , kama ile ngumi ingempata ingekuwa ndio mwisho wake”Mmoja ya watazamaji aliongea.

Mad Dog alianza kumshambulia  Hamza kwa spidi kubwa , licha ya kuonekana kutumia nguvu kubwa lakini alionekana kuwa na mafunzo  na hili kidogo lilimshangaza  Hamza na kutaka  kumuona sura yake.

Lakini licha ya Hamza kushambuliwa ilikuwa rahisi kwake kukwepa  mashambulizi lakini alijua kama ni mtu ambae hana mafunzo ya uhakika basi   ni rahisi kushindwa  pambano.

Upande wa Hamza sio kama hakuwa akitaka kupigana , alikuwa  akimkwepa  Mad Dog huku macho yake yakiangalia watazamaji , kuna kila hisia  zilizokuwa zikimwambia  kinachoendelea hapo  ni tukio ambalo limepangwa ili alifanye.

Ukweli hakuona kama kuna haja ya  Laizer kupitia kampuni yake ya Dede kushindwa kulipa  kiasi  cha pesa wanachodaiwa  na hata kama hawataki kulipa haikuwa  haja  ya kutengeneza uadui na  wadeni wake na pia kutoa siri  za uwepo wa  hili eneo.

Hivyo Hamza aliamini lazima kuna mkono wa mtu mwenye nguvu zaidi ya Laizer  katika swala hili  na si vinginevyo.

Lakini  kadri alivyokuwa akiangalia   watazamaji  hakuweza kumhisia  yoyote na   alijiambia pengine  mtu aliepanga huo mchezo hayupo kwenye kundi la watu waliovaa Vinyago.

Hadhira hio ni kama ilikuwa na chuki ya muda mrefu na Hamza , walikuwa wakizunguka huku na huko wakimlaani  Hamza na maneno ya kila namna, wakitaka apigwe .

Hamza alijikuta akisimama  bila ya kusogea tena  na  palepale MadDog  aliona hio  ni  nafasi  adhimu ya kummaliza kabisa Hamza na alimsogelea kwa kasi   akiwa amekunja ngumi lakini Hamza   alikuwa amejiandaa kwani baada ya kukaribiwa palepale   aliinua mguu na kumpiga Mad Dog  kwenye makagari  na kutokana na uzito wa teke Mad  Dog alidondoka chini  mpaka nje ya ulingo.

“Haaaaa…!!”

Hadhira ilijikuta ikishikwa na mshangao , kwasababu hawakutegemea Hamza angeweza kumshinda Mad Dog kwa shambulizi moja tu

Eliza alijikuta akifurahi mara baada ya kuona Hamza ameshinda , alikuwa na wasiwasi mno.

Mad Dog  aliugulia  maumivu ya kupigwa teke lile  kwa sekunde kadhaa huku akijiuliza imekuwaje amepigwa kirahisi namna hio.

“Kama umeshindwa  tayari  , tuishie hapa”Aliongea Hamza  kwa kingereza  akimwangalia Mad Dog.

Mad Dog bado alionekana hakuridhika kushindwa na alitambaa na kurudi  ndani ya ulingo.

“Kwenye ulingo wa  Nungunungu  ni swala la kifo  au  uhai , kama hujafa hutakiwi  kushindwa , simama na endelea kupigana”Aliongea  Laizer kwa   kingereza kwa nguvu na  Mad Dog mara baada ya kusikia kauli ile  alisimama haraka.

Hamza aliishia kukunja sura ,   lakini kwa wakati mmoja akitaka kuangalia sura ya Mad Dog , dakika ileile bila kumpa nafasi ya kurudiwa na nguvu aliruka teke na kumpiga kifuani.

Bam!

Teke lile lilikuwa zito kiasi kwamba lilimchomoa Maddog  kutoka kwenye ulingo  na kwenda kudondokea  mashabiki huku  akitema damu nyingi , alijitahidi  akasimama lakini  ghafla tu alidondoka chini na kuzimia.

Lakini sasa teke lile pia  lilimfanya kile kinyago chake kumtoka usoni  na Hamza mara baada ya kumwangalia kwa umakini alijikuta akishangaa  na kutabasamu kwa wakati mmoja.

Alikuwa ni yule mfungwa ambae  inaaminika ndio  kamuua Jongwe  mgombea wa kiti cha uraisi  kupitia chama tawala  na kisha kutoweka.

Hamza aliishia kutabasamu na kujiambia  ni kama alivyofikiria , hakuwa ameenda mbali lakini  kumbe  alikuwa amejichimbia  ndani ya hili eneo.

Ilionekana hisia zake  zilikuwa sahihi  bwana huyo hakuwahi kukaa   kwenye gereza ambalo halina fursa , ilionekana kipindi chote akiwa Gerezani  hili ndio eneo lake la kujiingizia kipato  na  hata baada ya kumuua  mtu mzito  bado hakupanga kukimbia maana ni sawa  kukimbia utajiri , kwa nchi  kama  ya Tanzania ilikuwa rahisi kwake kujitengenezea kipato  bila ya kuwa na mshindani.

Hamza aliona  mtu ambae alikuwa akimchezea  alikuwa amefikiria mbali , pengine aliona ni  bwana huyo pekee ambae anaweza kumletea ugumu katika uwanja wa  mapambano ndio maana  zikachewa hila mpaka kumfanya kupanda  kwenye ulingo, aliishia kutoa tabasamu na kutaka kumjua adui yake.

Upande wa  Laizer uso wake ulikuwa umejikunja  kama vile amekula pilipili  ya kuwasha sana , alikuwa na uhakika asilimia mia moja   Hamza hawezi kumzidi Mad Dog  na  kujiamini huko kumetokana na kwamba Mad Dog kwa  kipindi kirefu sana hakuwahi kuwa na mpinzani  ndani ya hilo  eneo  na  ndio mpiganani ambae amempatia pesa nyingi sana kwa  kurekodi matukio yake  na kuyauza kwenye mtandao wa Black Web.

Sasa alijiuliza inakuwaje Hamza kuwa na uwezo wa ajabu namna hio na kumshambulia  kwa mapigo mawili Mad Dog  na kisha kuzimia.

Eneo lote lilikuwa kimya , macho katika vinyago yalionekana kumwangalia Hamza  kwa wasiwasi , zile dharau na kejeli zote zilikuwa kwisha.

Kwao  kupatikana kwa mpinzani wa Mad dog sio tatizo  , kilichowashangaza ni pale  ambapo  Mad Dog alishambuliwa na mashambulizi mawili tu  mpaka kuzimia ili hali wamembetia kiasi kikubwa cha pesa kushinda.

“Takataka  hii!1”

Aliongea  Laizer kwa hasira akisahau ni zaidi ya miaka minne sasa tokea afungue hilo eneo ni Mad Dog ambae hakuwahi kupigwa, hata wapiganaji kutoka maeneo mengine duniani walifika kushindana  nae  na wote wakapigwa na kufanya watazamaji wengi kusafiri kuja kumuona.

Muda huo  mara baada ya kuangalia uelekeo wa Hamza aligundua ni kama hakuwa na nia ya kurudi   alipo ili kupata hela yake  badala yake aliruka ulingo na  kutokomea  nyuma  eneo ambalo  Mad Dog alitokea.

“Anafanya nini?”Aliuliza Laizer.

“Inaonekana ameenda nyuma ya ukumbi”Aliongea  kijana  msaidizi.

“Pumbavu unadhani  mimi ni kipofu , Seba hebu   peleka mtu akaangalie anafanya nini”Aliongea  Laizer na Seba  kiongozi wa  mabodigadi alikusanya watu kwa ajili ya  kwenda kuangalia  Hamza anafanya nini  lakini  muda uleule Hamza alionekana  akirudi  kupitia kwenye  ulingo  huku akiwa na utulivu wa hali ya juu.

“Kumradhi , nilienda  toilet  mara moja, Bosi Laizer nadhani umeshuhudia mwenyewe ushindi wangu , hivyo andika  cheki  ya pesa  tuna njaa sisi “Aliongea Hamza huku akijifuta mikono yake kwa tishu.

“Umeumia , mbona unatoka damu?”Aliuliza  Eliza na palepale aliishika mikono ya Hamza kuangalia kama alikuwa ameumia.

“Sijaumia sana nimejichubua kidogo  tu”Aliongea Hamza  huku akicheka lakini dakika hio meneja  wa eneo la  nyuma  ya ukumbi alichomoka akija eneo la VIP huku akiliita jina la bosi wake..

“Bosi, bosi…”

“Nini  kimetokea , mbona umepaniki?”

“Dakika hii  huyu  mtu amekuja  kwenye vyumba vya wapiganaji wetu na kuwashambulia , zaidi ya   wapiganaji wetu ishirini  wamekuwa vilema”Aliongea

“Pumbavu, kivipi?”

“Ni kweli bosi ,  baada ya kuja  alianza kutupiga sisi  na  kisha  akafuatia wapiganaji “Aliongea huku akionekana anatetemeka.

“Hamza  inamaana hiki ndio ulichofanya?”Aliongea Laizer huku  hasira zikiwa zimempanda kiwango cha juu.

“Kama nilivyosema nilienda kutafuta choo lakini sikukiona lakini hao watu wako wakanizuia  nisiondoke , sikuwa na jinsi zaidi   ya kuwashikisha   adabu”

Moyo wa Laizer  ulikuwa ukivuja  damu , milioni mia nane  pamoja na mia tisa alizoahidi haikuwa kitu sana kwake,  lakini hao watu ambao Hamza  amewageuza viwete amewanunua  kutoka  magerezani kwa zaidi ya mamilioni ya hela ,  hata kama wakifa ulingoni   angeendelea kujipatia hela lakini kama wakifa  bila ya kuingia kwenye ulingo  ni hasara.

Kwa mahesabu ya haraka haraka  alikuwa amepata hasara zaidi ya   bilioni ishirini .

Ili kupata wapiganaji kama hao kwake ilikuwa ni kama uwekezaji ,ilimbidi kwenda hadi nje ya nchi katika magereza kuangalia wafungwa ambao  anaweza kuwaingiza kwenye ulingo , lakini hao wafungwa  hata akiwapata hakuwachukua  bure, lazima  viongozi wa kisiasa walipwe kuidhinisha  na kisha jeshi la polisi kuwaziba midomo , sasa  kwa mlolongo  wote huo zilikuwa ni pesa nyingi sana , alikuwa akinunua  mpiganaji mmoja mpaka kufikia  Dolla laki  moja na nusu  sawa na  milioni mia  nne  na  bado hapo hajawalisha  virutubisho vya kutunisha misuli.

“Nadhani  huwezi kunilaumu katika  hili , isitoshe wapiganaji wako  wamejaza misuli tu ila kupigana hawajui , hasara uliopata chukulia kama  riba ambayo ulipaswa kuilipa Dosam kwa kuwazungusha muda mrefu na deni lao”

“Kwannini ulienda kupiga watu tena?”Aliuliza   Eliza.

“Ni kheri kuwavunja miguu  kuliko wakaingia  kwenye ulingo  na kuishia kupoteza maisha, wewe unaona kipi bora?”Aliuliza  Hamza na kumfanya  Eliza kushindwa kujua cha kuongea.

“Mr Laizer  unapaswa kulipa maana haitokuwa taswira nzuri kwako ilihali watu kibao  wamesikia  kwa masikio yako ukiahidi”Aliongea Hamza  na  muda huo  masikio ya  Laizer yaliokuwa yametobolewa    ni kama yamegeuka ya Sungura kutokana na hasira, aliishia kuchukua cheki  na kisha aliandika kiasi cha pesa anachodaiwa na Hamza alichoshinda na kisha kwa kusaga meno alimkabidhi.

Tokea aanze biashara siku hio ndio mara ya kwanza kupata  hasara kubwa namna hio.

Hamza  mara baada ya kupatiwa cheki mbili moja alimkabidhi  Eliza na  ile yake alichukua na kuikagua kama masifuri  yapo sawa   na alijikuta akitoa tabasamu lililojaa uzembe huku akijiambia hajapoteza muda wake kuja  ndani ya eneo hilo.

Eliza mara baada ya kushika  ile cheki ya milioni mia  nane   alijikuta akishikwa na hisia mchangayiko , hakuamini deni hilo lingelipwa., sio kwamba hio ni  pesa  kubwa ambayo ashawahi kukamilisha , alikuwa  akikamilisha madili ya zaidi ya bilioni kumi, kilichomfanya  kushikwa na hisia mchanganyiko ni kutokana na kwamba alikuwa na hofu ya  muda mrefu deni hilo haliwezi kulipwa na alijutia  kuwahudumia  Dede bila ya kulipa malipo yote.

“Asante sana  Mr Laizer deni lako na  kampuni yetu limeisha, sisi tunaondoka sasa”Aliongea Eliza huku akionyesha hamu ya kutoka hilo eneo.

Lakini sasa wakati  wanataka kuondoka   Seba  akiwa ameambatana na kundi la wanaume waliovalia mavazi ya kibodigadi waliwazingira Hamza na Eliza huku wakiwa wameshikilia bunduki za shoti.

“Mr Lazer hiki ni  nini tena ?”Aliuliza  Hamza baada ya kugeuka

“Niliahidi nitakulipa lakini sikusema unaweza kuondoka hili  eneo , tutakuacha uondoke baada ya   kuchukua hizo hela ,  utalipia hasara uliosababisha”Aliongea Laizer.

“Mr Laizer  huko ni kukosa aibu, huna thamani  watu wanayokupa”Aliongea Eliza.

Laizer licha ya kuonekana anafanya biashara za kihalifu lakini alikuwa pia ni maarufu sana  kwa watu  , alikuwa amejenga shule kadhaa  ambazo wanafunzi wanasoma bure na  pia alikuwa akitoa misaada , licha ya  kampuni yake kuhusishwa na skendo  ambazo  nchi haijawahi kudhithibitisha licha ni kweli baada ya Eliza na Hamza kushuhudia lakini  aliheshimika na hata viongozi wakubwa walikuwa wakimwalika kwenye matukio makubwa makubwa Ikulu.

“Kimya wewe mwanamke , unadhani najali thamani  watu wanayonipa , ninachojali ni biashara zangu kufanya vizuri na si vinginevyo.”

“Ni kheri kwanzia leo nimekujua tabia  yako , siwezi kuwa gizani na  kumpa  mtu sifa asizostahili, kwangu wewe huna tofauti na  jambazi”Aliongea Eliza na kumfanya Hamza kumwangalia Eliza  kwa mshangao , alijiambia  kumbe hata  panya  anaweza kung’ata  akizidiwa.

“Mwanamke mpumbavu wewe usiejua nini uongee na kipi usiongee, Seba nataka kumuona huyo  kijana akiwa chini  na mwanamke  anafaa sana kwa filamu za  kutuingizia pesa”Aliongea

“Yes Sir!!”Yale  majambazi ya  Bosi  Laizer yaliitikia kwa nguvu  kama misukule  na  kumzingira  Hamza kwa ajili ya kumshambulia.

…………

Dakika  chache mbele  wale mabodigadi wote walikuwa chini wakiugulia maumivu , Abasi  ambae alikuwa  ndio kiongozi wa mabodiadi aliishia kupiga yowe mara baada ya Hamza kutegua kiganja chake cha mkono  na kudondoka chini.

Eliza ambae alishuhudia tukio zima  alijikuta  akikamaa mwili  , alikuwa akitamani kutoa kilio  kutokana na  kile alichokuwa akiona , Hamza alimtia wasiwasi mno.

Hamza mara baada ya kugeuka nyuma aligundua  Laizer alikuwa amekaa  sakafuni kwa woga, tukio hilo lilimfanya kuhisi kudhalilishwa kwa karne  na kwa muda huo  hakuwa na mtu mwingine wa kumwambia apigane  na Hamza kwani  aliokuwa  akiwategemea walikuwa chini wakiugulia maumivu.

Upande  wa Hamza mpaka anakuja kupumua  na kuona kundi la watu wakigalagala chini  hata yeye hakujua  amewezaje kuwashughulikia kwa  dakika chache hivyo , maana hakutumia uwezo wa ziada kudili nao , ulikuwa ni uwezo wake  wa mafunzo mbalimbali  ya mbinuu za sanaa za kimapigano.

Hamza mara baada ya kutulia kidogo alimsogelea  Mzee huyo wa kimasai ambae ni kibukta tu kilichokuwa kikionekana  kutokana na rubega yake kupanda juu.

“Unataka nini  kwangu?”Aliongea  Laizer akijitetea maana hakujua Hamza alikuwa na  mpango gani.

“Nataka hio saa , gharama za kumpiga mad dog  ilikuwa ni  milioni mia tisa, ukaniletea  kundi  la mabodigadi  nipigane nao lazima niongeze hela kidogo , sitokufanya chochote  wewe nipatie  tu hii saa yako”

Wageni  ambao walishuhudia tukio zima  la Hamza kupiga mabodigadi mara baada ya kusikia   hitajio la  Hamza walijikuta  wakiduwaa , ni kama  sasa waliona Hamza anajaribu  kujitajirisha kupitia Laizer.

“Unajua hii saa inauzwa shilingi  ngapi?”Aliuliza  Laizer huku akirudisha mkono wake nyuma.

“Najua ndio ,  imetengenezwa kwa  madini ya platinum ,  mkanda wake ni wa ngozi ya mamba , kioo cha  Yakuti , mashine yake  lazima itakuwa ni CA,  kama nitakuwa sahihi lazima  itakuwa  si chini ya   dollar laki sita”Aliongea Hamza.

“Hizi saa zipo kumi na tano duniani ,  unadhani nakuogopa mpaka nikupatie kitu cha thamani namna hi?”Aliongea na kauli yake ilimfanya Hamza kuinama na kumwangalia bosi Laizer usoni kwa macho ya kichawi na  ndani ya sekunde  Laizer alijikuta akianza kutetemeka  mwili mzima ,  alikuwa akihisi mtu ambae yupo mbele yake ni jini ama kiumbe ambacho hakuwahi kukutana nacho.

Hamza haikueleweka alimfanya nini na palepale alisimama na kumwangalia akiwa na tabasamu la uchokozi.

“Nitakuuliza tena , upo  tayari kuivua mwenyewe au nikate mkono ndio  niichomoe?”Aliuliza  Hamza na kumfanya Laizer kuangalia watu waliokuwa wakimwangalia kupitia  vinyago,  aliona aibu mno  lakini kutokana na kumhofia Hamza aliishia kuivua.

Hamza alimkwapua kwenye mikono yake na alisogea mpaka kwenye meza na kisha alichukua  chupa ya mvinyo ambayo imebakia nusu na kuimalizia yote mara moja.

“Mvinyo mtamu sana huu , huwa muda wote nikinywa Wine namkumbuka mwandishi wa vitabu  Willium Faulkner huyu jamaa alisema: ‘Human civilization starts with distilling technology’ kama unamjua Aristotle basi utakuwa unasoma soma vitabu na utaona sikudanganyi , kama  mwanaume unapaswa kustaarabika hela unazo lakini  unafanya vitu ambavyo   fukara  anafanya”Aliongea Hamza na   Mzee Laizer hakuongea kitu , alijua Hamza alikuwa akimdhihaki ila hakuna kingine.

“Leo  ilikuwa siku nzuri , nimepata hela , nimekunywa mvinyo wa bei  ghali na  nimechukua mazoezi kidogo , Mungu akijaalia Bosi  Laizer pengine tutaonana tena , Binadamu sio milima”Mara baada ya kuongea alimshika Eliza mkono na kuingia kwenye lift.

Bosi Laizer mara baada ya Hamza kupotelea kwenye macho yake alisimama na kisha alimsogelea Seba ambae  kamasi linamtoka kwa maumivu na kumpiga teke  kwa hasira  na kisha  alisogelea  mlango uliokuwa ni kama lift  na alibonyeza, mara  mlango ule ulipofunguka ilionekana  eneo kama jukwaa la  vioo , ukiwa kwa  ndani unaona upande wa eneo  lote la Ulingo  ila kwa aliekuwa kwenye Ulingo  hawezi kuona  watu ndani ya eneo hilo.

Eneo hio  walikuwa wakikaa  VVIP yaani watu  muhimu zaidi, yaani sio muhimu tu , wale muhimu zaidi ndio walikuwa wakikaa hapo ikiwemo wanasiasa wakubwa  na  wafanyabiashara  wakubwa.

Sasa ndani ya eneo hilo kwenye Masofa alionekana  mwanamke mrembo  wa kuvutia sana akiwa ameketi kimapozi , alikuwa amevalia  gauni la rangi ya bluu  na viatu vya high heels.

“Madam Yulia ,  nadhani unapaswa kuniambia  huyu Hamza ni nani haswa?”

“Mzee Laizer kwanini unaniuliza mimi?”

“Kwahio  hata wewe hujui , kama ni hivyo kwanini  uliniambia nimlete Eliza hapa  na kumwandalia mtu wa kudili nae, inamaana mpango wako haukuwa  Eliza bali Hamza kwasababu ulikuwa ukijua ni wapenzi?”

“Ndio , mwanzoni nilijua tutapata mkanda mzuri wa filamu lakini bahari haikuwa kwetu Hamza amekuja na kuharibu mpango mzima”Aliongea lakini Laizer  alikuwa na hasira.

“Yuia unapaswa kunielezea vizuri , nimepoteza  wapiganaji wangu  na  zaidi ya  mabilioni ya hela  , halafu unaniambia hujui chochote?”Aliongea kwa hasira lakini mwanamke huyo alionekana kutokuwa na hisia zozote , alisimama kimapozi  na muda uleule  alitoka kuwa mwanamke mrembo na  kuwa mwanamke kauzu.

“Laizer  nilikuambia udili na Eliza pekee  lakini sio kutafuta ugomvi na Hamza , yaani hasara kidogo  tu unabweka , wakati nakupatia kazi ulijaa ujivuni  kwamba utaiweza lakini sasa hivi umeingia kwenye mikono ya  Hamza unalalama , kwahio unataka nikulipe hasara uliopata?”Aliongea na kisha alimsogelea  Laizer karibu kana kwamba anajaribu kunusa jasho lake.

“Kama shida yako ni pesa naweza kukuandikia cheki …  lakini  je ujasiri wakuipokea unao?”Aliongea kikauzu na kumfanya  Laizer kugwanya ,  alikuwa na hasira  mno wakati akija hapo lakini sekunde hio hio alikuwa  akimuogopa huyo mwanamke.

“Sijamaanisha hivyo   Madam , kwanini nikudai?”

“Unapaswa  kujijua wewe ni nani ,  ijapokuwa  kwa nje unaonekana mtu muungwana lakini  wewe ni mhalifu namba  moja ndani ya nchi hii , nikiamua  huwezi kuliona jua tena, Mimi Yulia ndio mrithi  wa nguvu ya familia yangu yote  na hakuna  mtu yoyote ndani ya taifa hili anaweza kuondoa  mizizi yangu, kuja kwangu hapa  unapaswa kujivunia , kwanzia sasa unapaswa kuanza kufikiria  nafasi yako  na sio kujilinganisha  na  mimi , aliekuwa anakupa  kiburi nishamkata miguu na  amekuwa joka la kibisa”Aliongea na kumfanya  Laizer jasho kumtoka maana alielewa Yulia alikuwa akimaanisha nini.

“Nimekuelewa Madam , naomba unisamehe”Aliongea  Laizer huku akiinamisha kichwa chake chini lakini kitendo kile kilimfanya  Yulia kuanza kutoa kicheko ,  alikuwa akicheka vizuri  mno  na kufanya uzuri wake kuzidi kuonekana.

“Vizuri , napendaga mbwa mtiifu ..oh sorry namaanisha mtu mtiifu  haha…”Aliongea na kisha alizipiga hatua kimaringo kutoka  hapo ndani.

Laizer aliishia kumwangalia mwanamke huyo akiondoka huku macho yake yakiwa yamefunikwa  na  uovu mkubwa.

Previoua Next