Reader Settings

 Regina mara baada ya kuulizwa swali hilo ni kama moyo wake uliingia katika hali ya mkanganyiko na akili yake , lakini mara baada ya kufikiria kwa umakini alionekana kupata jibu.

“Kabisa bibi, yaani simpendi”Aliongea na kumfanya  Bibi Mirium kuonesha hali ya kukata tamaa.

“Hata iwe hivyo hakikisha  huachani nae , ukihisi  kutaka kuachana nae kumbuka maneno ya bibi yako ,  ukiona  huko mbeleni  umeshindwa kumpenda kabisa  basi jifanyishe unampenda . mchukulie  kama kete , mtumie   kwa faida yako  huku ukihakikisha haondoki”Aliongea  Bibi Mirium na maneno yale yalimshangaza mno   Regina.

“Bibi wewe….”Aliongea lakini muda huo  Bibi Mirium alionekana kuwa siriasi na kile abacho anaongea.

“Mjukuu wangu unadhani   mimi bibi yako ni  kipofu na sionni kinachoendelea kati yenu , lakini sitaki kuongea sana kuhusu hayo , hakikisha  unamshikilia hata kama huna hisia nae”

“Lakinni bibi kwanini…”

“Hakuna cha kwanini Regina , nataka uniahidi   hutoachana na Hamza”Aliongea  na kumfanya Regina kuishia kung’ata lips zake.

“Bibi nimekuelewa”Aliongea na kumfanya Bibi  kucheka  kicheko cha  ahueni.

“Mjukuu wangu  wewe ni mwanamke  mrembo sana , umewazidi wengi  kwa uzuri , ukiongeza mbinu  kidogo  tu unaweza kumfanya Hamza kufa kuoza kwako  na kumfanya akutii kwa kila kitu , mimi bibi yako nakuamini sana”Aliongea na kumfanya Regina mwili wake kusisimka.

Alijiuliza inamaana  ndoa hudumu  kutokana na kudanganyana ,  Regina alijikuta akijihisi  vibaya  kwenye moyo wake , kadri alivyokuwa akiangalia swala hilo ni kama  bibi yake alikuwa na sababu kubwa

Bibi Mirium alionekana  kama vile ni  mtu ambae amekuwa na amani ghafla  na  ki uchomvu sana aliegamia mto wake.

“Nimechoka sasa , nenda kamtafute Hamza , haina haja ya kuendelea kuja kuniona”Aliongea

Regina alijikuta akishikwa na huzuni   baada ya kuona  bibi yae anazidi kuwa mdhaifu , alijikuta pia akishikwa na mshagao  akijiuliza kwanini bibi yake alionekana kuwa  na ahueni lakini ghafla tu  hali yake inabadilika.

“Bibi   unajisikiaje , mbona ghafla tu  umekuwa…”Regina alitaka  kuongea lakini alizuwa na Shangazi Mariposa.

“Regina  kwasasa  nendeni nyumbani kwanza na umuache apumzike”

Regina licha ya kuwa na wasiwasi mwingi  alijikuta akitii na kugeuka   na kutoka nje , moyo wake   ulikuwa mzito mno kuondoka.

Baada ya Regina kutoka Shangazi alijikuta akivuta pumzi nyingi na kuzishusha kwa ahueni na alinyoosha mkono wake  na kushika mkono wa Marium na  macho yake  ni kama yamebadilika   ghafla na  kutoa miale kama ya jua.

Alimwangalia  Bibi yake Regina kwa  namna ambavyo ni kama anamsindikiza huko aendako.

*******

Regina  mara baada ya kutoka nje aliweza kumkuta Hamza akiwa ameegamia boneti ya gari  huku akionekana kama mtu ambae anafikiria kitu,  aliishia kuangalia pete ambayo amevaa kidoleni kwa  sekunde kadhaa na  macho yake yalionyesha kutoridhika.

“Tunza hio pete vizuri , ni mali ya familia yetu”Aliongea na kumshitua Hamza.

“Unaonaje nikikuachia uitunze”

“Sitaki , kwasababu bibi ndio kakukabidhi kwasasa siwezi kukupokonya , isitoshe haina maana hata nikiichukua”Aliongea na kumfanya Hamza asijue alie ama acheke , ukweli ni kwamba alikuwa akiwaza kama kweli  pete hio   ni kama ambavyo anafikiria  basi  kuendelea kuivaa ni kujitafutia matatizo.

“Regina wapi tunaenda?”

“Naenda kumtembelea Yonesi  hospitalini”Aliongea na kumfanya Hamza pia kukumbuka  alimuacha  Yonesi hospitalini , hivyo aliona sio mbaya kama ataenda kumuona pia.

Muda ambao  Hamza anafika   ndani ya hospitali ambayo  Yonesi amelazwa  alijikuta akimwangalia Regina na kujiangalia na kuona hawakuwa wamebeba chochote.

“Regina  tunaenda kumuona mgonjwa lakini hakuna tulichobeba?”Aliongea na kumfanya  Regina  kushangaa na kuona  ilikuwa ni kweli hakuna walichobeba.

“Ila tungebeba nini?”Aliuliza  na kumfanya Hamza kufikiria kidogo  na baada ya kugeuza macho upande wa kulia waliweza kuona  kijana ambae anauza maua  na kadi.

Hamza alisogelea na kisha alinunua  ua na kadi ya kumtakia Yonesi kupona haraka na kisha waliongozana kuingia  hospitalini  upande wa wodi.

“Hili  ua nikiliangalia vizuri naona kama linakufaa   mno  mke wangu”Aliongea Hamza.

“Halafu huelewi tu , nishakuambia usiniite hivyo”Aliongea huku akizidi kuongeza ukauzu   lakini alikuwa akihema kwa nguvu kiasi kwamba alihisi   kutokana na udogo wa lift Hamza atasikia mapigo yake ya moyo yalivyokuwa yakidunda.

“Acha wasiwasi , sina mpango wa kukupa zawadi ya ua”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kuzidi kuwa kauzu.

“Bora  ufanye hivyo , siku ukijipendekeza na  vimaua maua  hupati mshahara”Aliongea  na kumfanya Hamza kuishia  kutingisha mabega, ilionekana Regina kutaja mara kwa mara neno  mshahara ni kumkumbusha kwamba  uhusiano wao ni wa kikazi pekee na  hakuna zaidi.

Wakati  Hamza akiwaza  hilo  lift ilifungukka  katika  wodi ya daraja la   watu muhimu   na walitembea mpaka kwenye  wodi  namba  nne , kitendo cha kusukuma mlango na kuingia ndani Hamza alijikua sura yake ikikunjamana mara baada ya  kuona  ndani  kuna  mtu tena akiwa amevalia  Kombati za jeshi zilizochafuka kwa vyeo.

******

Ni muda wa saa  tisa  za  jioni alionekana  Kanali  Dastani akiingia makao makuu ya kitengo cha MALIBU, huku  kwa kiasi flani hatua zake zikionyesha alikuwa  na haraka.

Muda huo baadhi ya wafanyakazi walikuwa wakianza kutoka  kazini  wakipisha  zamu za jioni.

Mara baada ya kuingia kwenye lift alibonyeza kitufe cha floo ya juu zaidi,  floor ambayo   ofisi za  wakuu  zaidi yake  zilipatikana.

Yeye alikuwa akiendesha idara yake kama Kanali  na ofisi yake ilikuwa  floor   ya  kumi  na tisa huku ya bosi wake ikiwa  floor ya  ishirini.

Kitendo cha kutoka katika  floor hio  mtu wa kwanza kukutana nae alikuwa ni  Afande Msuya  mkuu msaidizi wa kitengo cha MALIBU,licha ya kwamba kivyeo wote walikuwa ni makanali lakini  Msuya yeye alikuwa ni  mwandamizi  hivyo  Dastani ilibidi kumpa heshima yake.

“Jambo afande”Alisalimia  Kanali.

“Dastani hivi  unajua katika hiki kitengo wewe ndio  unaonekana  kuwa bize sana , nimeshauriana na  Afande Doswe na  kuona pengine tukupunguzie majukumu”Aliongea Msuya huku akionyesha hali ya kutoridhishwa na  Kanali.

“Sio kweli Afande ,  nilikuwa nje ya ofisi kikazi  ndio maana nimechelewa kuripoti”Aliongea

“Vizuri kama  ulikuwa nje ya ofisi kikazi ,  sasa  niambie ni kazi  gani hio  ambayo  timu yako hata  hawaijui”Aliongea  na kumfanya  Afande Dastani wasiwasi kumvaa.

“Dastani unanipotezea muda”Sauti nyuma yao  ilisikika  na kumfanya  Afande Msuya bila kugeuka   kukunja ndita.

“Nakuja  afande”Aliongea  na kisha  alitoa ishara ya heshima  kwa Msuya na kisha kupita huku akonekana  kuvuta pumzi ya   ahueni.

Ukweli ni kwamba  licha ya Afande Msuya kuwa mkubwa wake kazini lakini  hakuwa akimuamini   ni moja ya Ma’Afande ambao   walijaa rushwa  na hata nafasi yake hio ya umakamu aliipata kutokana na kuwa  mkwe  kwa  Makamu  wa raisi.

Kwake  mtu aliekuwa akimheshimu   alikuwa  Afande Doswe, lakini  kutokana na mara nyingi  kujihusisha na maswala mengi yanayomuhusu Mheshimiwa  Mbilu, Kanali Doswe alikuwa  akimuweka pembeni  katika misheni  nyingi na watu waliokuwa wakiaminiwa ni kama  Amosi na  wengineo.

“Jambo  Afande”.

“Kaa chini Dastani, muda umeenda nina kikao sehemu nyingine”Aliongea kwa kuamrisha na  Dastani alikaa chini.

“Nimeitikia wito  Afande”

“Dastani naungana na  Msuya , upo  bize sana  kama nisingekuwa na Siwalima  katika  idara yako  mambo mengi yangekuwa hayaendi ,  kwasasa umegeuka kuwa  Field  officer  tofauti  na Command  officer , kama unataka   naweza kukuondoa ofisini”Aliongea  Afande Doswe na kumfanya Dastani kuanza kukuna kichwa akikosa jibu.

“Nadhani umezipata   taarifa  za kifo cha  Jongwe huko ulipokuwa umejichimbia mpaka simu yako  kutopatikana hewani”

“Ndio  Afande , nimezipata tokea jana usiku”Aliongea.

“Jana usiku ya saa ngapi?!!”Aliuza Afande Doswe huku akionyesha  mshangao kidogo.

“Usiku wa saa  tano  kwenda sita hivi”Aliongea huku akionyesha hali ya kuchangahyikiwa kidogo.

“Mimi mkuu wa kitengo taarifa nimepatiwa saa nane usiku, wewe umezipata saa  saa tano, kwanini hukutoa taarifa mapema?”

“Afande  taarifa sikuzipata”

“Unamaanisha nini?”

“Nilikuwa eneo  la tukio  wakati ajali inatokea”Aliongea Dastani  na kauli ile kidogo ilimshangaza  Afande Doswe.

“Inamaana ulishuhudia wakati   ajali inatokea , ilikuwaje mpaka ukawa aneo la tukio?”Aliongea na kumfanya  Kanali kukuna kichwa huku akionyesha hali ya wasiwasi.

“Ongea kanali una dakika  kumi  tu za  kunielewesha  la sivyo  nakubadilishia majukumu”

“Afande  nilikuwa nikiendelea  na uchunguzi  wa  kesi namba 99”Aliongea  na kumfanya  Afande Doswe  sura kujikunja.

“Hii  kesi si imetolewa chini ya idara yako  na kupatiwa  Amosi?, hukupaswa kuigusa mpaka  tuhuma zinazokukabili  kuthibitishwa ,  inamaana muda wote ulikuwa bize kuvunja utaratibu wa  Kitengo?”

“Afande  najua ni kweli nilikuwa nikivunja utaratibu  lakini  yote  ni kwasababu ya  faida ya   Kitengo chetu”

“Faida kivipi?”

“Afande nadhani   hata wewe unajiuliza mpaka sasa Amosi  yupo wapi,  kesi namba tisini na tisa  ni nyeti sana na  inahitajika kutafutiwa ufumbuzi wa haraka , lakini mpaka sasa  hakuna taarifa yoyote kutoka kwa  Amosi , tokea mwanzo niliona hii ni kesi ambayo  naweza  kuitatua”Aliongea na kumfanya  Afande Doswe kuvuta pumzi na kuzishusha   na kisha akaangalia saa yake ,  ilionekana maneno   ya Dastani  yalikuwa na ukweli, mpaka muda huo   Amosi hakujulikana alipo.

“Muda umeenda , niambie   kwanini  ulikuwa eneo la tukio?”

“Jana    usiku wakati nikitokea Mpiji  nilitumiwa ujumbe  kwenye simu yangu  ukinitaarifu Chendezi  ametolewa   Gerezani”Aliongea.

“Chendezi!”

“Ndio Afande , mfungwa  wa kesi ya Ajenti  Sedekia”

“Endelea”

“Wakati  nikitafakati  namna ya kudili na ujumbe huo nilipokea simu kutoka kwa Afande Norbert  na kunipa  habari  juu ya  ujumbe  aliotumiwa  na yeye”

“Unamaanisha Norbert na yeye katumiwa ujumbe kama wako?”

“Ndio katumiwa ujumbe lakini  tofauti na wangu?”

“Wa kwake  unasemaje?”

“Jongwe  yupo  hatarini”Aliongea na kumfanya  Afande  Doswe macho yake kucheza.

“Norbert aliniambia yupo hospitalini  hivyo hawezi kutoka na  alinipigia kuuliza maoni yangu juu ya ujumbe huo  na nilimwambia  kuhusu ujumbe wangu na  ndipo tulipokubaliana mimi nifuatilie kwa undani kama ni taarifa ambayo ni sahihi”

“Kwahio   ulianza kumfuatilia  Jongwe”

“Ndio Afande”

“Baada ya hapo nini kilitokea?”

“Afande  nilienda nyumbani  kwa  Jongwe  baada ya kuambiwa  yupo kwake  lakini  wakati nafika niliambiwa  mheshimiwa alikuwa na kikao na  Mzee Martini na  kuambiwa   kama nataka kuonana nae nije kesho, ila nililazimisha  ni jambo  muhimu  sana nataka kuonana nae  usiku huo hivyo nitasubiri  ,  lakini baada ya kuonyesha msimamo wangu  mtoto wa Mzee Jongwe  alinipa taarifa mheshimiwa  hana mgeni, bali ametoka  kwenda kwenye kikao cha siri nyumbani kwa Mzee Martini , baada  ya taarifa hio kuipata  machale yalinicheza na  haraka nilianza safari ya  kwenda  nyumbani kwa Mzee Martini ,  lakini wakati nakaribia  kiwanda cha Binsulm ndio nilishuhudia gari  ikilipuka”Aliongea Kanali na kumfanya  Afande Doswe kupatwa na utulivu wa kutaka kusikia zaidi.

“Kama ni hivyo kwanini hukutoa taarifa?”

“Sikuwa  na muda,  mwanzoni sikujua  gari  ile  ilikuwa  ni ya mheshimiwa Jongwe , umakini wangu  niliuelekeza katika  pikipiki   iliokuwa nyuma ya gari hio , kwa namna gari ilivyolipuka niliweza kugundua ni bomu mara moja  kutokana na uzoefu wangu na mtu aliekuwa kwenye pikipiki nilimtilia mashaka kushika rimoti  mara baada ya kuigeuza na kurudi alikotokea uzuri tulikuwa uelekeo sawa”

“Kwa maana hio   ulianza kumfukuzia?”

“Ndio Afande”Aliongea na kumfanya  Afande Doswe  uso wake kucheza kidogo.

“Hilo lilikuwa swala la kutaarifu polisi  na  hata kama  ulitaka kuhusisha kitengo ungempigia mkuu wa TISA, Wewe na Norbert  kama mlipata ujumbe wa namna hio mlipaswa  kuwasilisha makao makuu ili kuchakatwa, huo ndio  utaratibu,  Dastani huu nin muda wa kikao   na sina muda wa kusikiliza mpaka mwisho , andika   ripoti ya tukio zima na kisha  unitumie  kwenye barua pepe  yangu, hata kama nikujirekodi fanya hivyo   na unitumie kabla sijafika makao makuu ya TISA”Aliongea na kusimama.

“Ndio afande”.

“Usishahu  na kuandika  vifungu vya  sheria ulivyovunja,  asubuhi naitaka barua yako  hapa na nitajua namna ya kudili na wewe”Aliongea akiwa kauzu  na kisha alitoka ofisini.

Lakini kitendo cha  kufungua mlango  atoke  alijikuta akisimama  mara baada ya kuona sura aliokuwa akiitafuta.

“Amosi!!”

“Jambo Afande!!” Alisaluti Amosi.

Previoua Next