Reader Settings

“Sogea uone kama  sitochangua ubongo wako”Aliongea Mdudu  huku akiwa hana  ishara ya  utani kwenye macho yake.

Regina  na  Yonesi mara baada ya mara baada ya kuona  Hamza kawekewa bunduki  kwenye paji  la uso  mioyo ilitaka kuwatoka,

“Hamza  naombeni tuishie hapa , Mdudu haina haja ya kwenda mbali hivyo”Aliongea Yonesi kwa  namna ya kubembeleza.

“Huoni kama sio vizuri kutoa siraha eneo la hospitalini ?”Aliongea Regina.

“Kwahio ikiwa hospitalini ndio nini ,  ninaweza wa kumuua hapa na hakuna wa  kufanya chochote”

“Kapteni kwanini tusimkamate tu na kumpeleka kituoni?”Aliongea   Afande Diksoni  ambae muda wote alikuwa ametulia  pembeni.

“Upo sahihi , huyu tunaondoka nae hapa pamoja na Yonesi , nitakuwa nimepiga  ndege wawii kwa jiwe moja”Aliongea Mdudu mara baada ya kujifikiria kwa dakika chache, lakini dakika ambayo anamaliza kauli hio  bunduki  yake  ilikuwa ishachukuliwa kiustadi  kabisa  na kutua katika mikono ya Hamza na  ilichukua dakika chache tu risasi zote kutolewa na Hamza na  kumwagwa chini.

“Umeitunza  vizuri hii bastora”Aliongea Hamza huku akiichunguza chunguz.

Mdudu na mwenzake walikuwa wameshikwa na butwaa maana hawakujua ni kwa namna gani  Hamza aliweza kuchukua hio bastola , kilikuwa kitendo cha  spidi sana kutokea.

Hamza mara baada ya kuhakikisha bunduki hio haikuwa na risasi hata moja alimrushia  Afande Diksoni ambae aliidaka.

“Mnaweza kuondoka sasa , hapa ni hospitalini na panapaswa kuheshimiwa , kama hutaki ugomvi na mimi basi acha kumsumbua Kapteni”

Wajeda hao  walijihisi   kudhalauliwa kwa kile ambacho kimetokea , yule bwana ambae alikuwa ameambatana na  Mdudu alionekana mtu wa shari kwani palepale  kwa hasira alimsogelea Hamza kwa nia ya kumshambulia, lakini hata hivyo mbele ya Hamza ilikuwa ni kujitafutia matatizo tu kwani sekunde ambayo ngumi yake inamkaribia Hamza alishadakwa mkono na kilichosikika ni mifupa ya mikono yake  kupishana.

Lakini  licha ya  maumiivu makali alionekana alikuwa na uwezo mkubwa wa kuyavumilia kwani aliinua mguu wake kutaka  kupiga teke na buti la kijeshi  lakini Hamza alikuwa mwepesi kwani alimkwepa na kumpiga  ngumi ya mbavu  iliomfanya  kudondoka chini  kama gunia kutokana na maumivu.

Mdudu mara baada ya kuona   mjeda mwenzake ameweza kudhibitiwa na Hamza kwa mashambulizi mawili tu hali ya hofu  ilimvaa palepale  na aliona ilikuwa bahati kwake hakumshambulia.

Muda huo  Yonesi na Regina walijikuta wakishangaa na  kufurahi kwa wakati mmoja.

“Sogea , si ulitaka kuondoka na kapteni , ukinishinda  nitakuruhusu kuondoka nae”Aliongea Hamza akimpa ishara  Afande Mdudu , lakini bwana huyo aliishia kumeza mate mengi huku akionyesha  hali ya kusita .

“Nitakuchunguza kwa umakini na kukujua wewe ni nani  na baada ya hapo  nitakukamata kulingana na sheria”Aliongea na kumfanya Hamza kucheka.

‘Yamekuwa maswala ya kisheria tena, sekunde chache nyuma ulikuwa ukiongea kana kwamba hujali sheria lakini sasa hivi unaonekana kutii”

“Sitaki kuendelea kubishana na mtu kama wewe”Aliongea  akionyesha kabisa  amenywea na muda ule alimgeukia Yonesi.

“Yonesi  wewe ni mchumba wangu ukubali ukatae na ni swala la muda tu utakuwa mke wangu”Aliongea kwa hasira na  kumpa ishara mjeda mwenzake na   kuondoka.

Mara baada ya wajeda hao kuondoka hatimae hali ya ukimya ilirejea , Regina na Yonesi walimwangalia Hamza  huku wakiwa na mwonekano usioelezeka.

“Mbona mnaniangalia hivyo kama ndio kwanza mnaniona?”

“Ni bora  kama usingenisaidia , Mdudu namjua vizuri  ni mtu wa kuweka chuki moyoni  na kwa sapoti ya  cheo cha baba yake utamsababishia tu matatizo  mkurugenzi”Aliongea Yonesi.

“Yonesi usiongee hivyo , ijapokuwa  ni kweli Hamza  ni mtu wa kukurupuka lakini  nisingeweza kukuangalia tu  ukichukuliwa kwa nguvu,maana haina tofauti na kutekwa”

“Huna haja ya kuwa na wasiwasi , nakuhakikishia hakuna matatizo yoyote yatakayotokea , halafu Kapteni unaonekana umeshapona  tayari , kwanini  usiende kukaa kwenye apartment za kampuni ili isiwe rahisi kwa yule mtu kukusumbua”

“Namfahamu Mdudu kwa muda mrefu tokea tukiwa   kambini , kwa kilichotokea leo hatokuja kunisumbua tena mpaka apate mbinu ya kudili na wewe”Aliongea  lakini Hamza haikufanya  kuwa na wasiwasi  kabisa.

“Yonesi  nadhani itakuwa vizuri kama ukiwahi kurudi  kazini , usifanye mazoezi magumu , nikikuona kazini  itakuwa rahisi kwangu  kutokuwa na wasiwasi”Aliongea  Regina  na Yonesi alitingisha kichwa kukubali.

“Regina  hujawahi  kuniuliza chochote kuhusu familia yangu au hutaki kujua?”Aliuliza  Yonesi huku akionyesha kusita  sita.

“Hata nijue ama nisijue  haimaanishi kwamba nitabadilisha   maamuzi yangu  wala kukataa ukweli kwamba tumekuwa  marafiki kwa  muda wa miaka mitatu , ila kama unataka kuniambia nipo tayari kusikiliza”Aliongea Regina.

“Usiwe na wasiwasi, nyumbani kwetu Kongwa natokea familia ambayo inaheshimika kwa mchango  mkubwa jeshini, niliondoka nyumbani kuja  Dar kwasababu ya kuepuka usumbufu wa  Mdudu na maswala yake ya ndoa  maana simpendi,  hivyo usiwe na wasiwasi familia yangu haiwezi kukuletea shida”

“Nakuamini Yonesi , isitoshe  wewe  ni msichana jasiri ambae unapenda haki sijapata ona”

“Usiseme  hivyo mkurugenzi , ni kwasababu   tu sipendi  kuonewa”Aliongea Yonesi huku akitabasamu kwa furaha.

Ukweli licha ya kwamba muonekano wa Yonesi na Regina ni kama wanalingana  ki umri  lakini  Yonesi alikuwa akimheshimu mno Regina , pengine  ni kutokana na tabia zao kuendana.

Upande wa Hamza  aliishia kukunja sura tu , kuna kitu alihisia na kujiambia  kuna uwezekano   Yonesi ni mtoto wa  mwanajeshi mwenye cheo kikubwa kama  anavyohisi kwa Mdudu..

****

“Damn it”

Kitendo cha Mdudu kuingia kwenye Jeep ya jeshi  alijikuta akigonga usukani  kwa  hasira.

Diksoni  mjeda mwenzake ambae alikuwa ametenguliwa mkono na Hamza aliishia kujikaza kisabuni ili  aweze kufika hospitali ya jeshi kwa ajili ya matibabu .

“Kapteni huyu Hamza anaonekana sio  wa kawaida kabisa ,  ndio maana Norbert licha ya uwezo wake ameweza kudhibitiwa kirahisi”

“Wewe ni mjinga ndio maana umepigwa kirahisi , ole wako  uruhusu  taarifa ziwafikie watu wengine kwenye  kikosi changu”Aliongea huku akisugua meno kwa hasira na kumfanya Job kutulia.

Muda huo huo  Mdudu alionekana   kupokea simu kutoka kwa vijana wake.

“Afande   taarifa kutoka TISA  wale wawindaji kutoka ufilipino wameingia nchini”Sauti ilisikika upande wa pili na kumfanya Afande Mdudu macho kuchanua.

“Wameingia  nchini lini ,mmeweza kupata uelekeo wao??”

“Ndio Afande wameingia jana nchini  na  wamefikia  katika hoteli ya Sunset Kigamboni ,  wana Visa  kama  watalii lakini taarifa kutoka kwa majasusi  ubalozi wetu Ufilipino wametuhakishia ndio wenyewe”

“Lazima wapo hapa nchini kwa ajili ya kufuatilia   kupotea kwa wenzao ,  hakikisha hawaondoki kwenye rada zetu , hii ndio njia rahisi ya kujua  walikuwa wakitaka nini  kutoka kwa Hamza”

“Sawa Afande”

Kitendo cha Afande Mdudu kukata  simu tabasamu lilichipua kwenye uso wake ,  tokea tukio la Hamza kuua kundi lile kikatili kule Bagamoyo , kitengo cha Malibu kikiongozwa na Afande Msuya walikuwa  katika uchunguzi wa kutaka kujua  walifuata nini nchini Tanzania mpaka kujaribu kumteka Regina.

“Kapteni   hii ni njia nzuri ya kukamilisha uchunguzi  wetu”

“Haha..hili lazima lifanikiwe , njia pekee ya kuja  kufanya kazi hapa makao makuu ni kuonyesha uwezo wa juu kuliko Norbert, isitoshe pia  nina hamu ya kujua  ni  kwasababu ipi kundi  kama hili linatoka mbali hivyo kwa ajili ya  Hamza tu”

*******

Upande  wa  Hamza aliishia kushika simu yake  akiendelea kuperuzi wakati  Yonesi  na  Regina wakiongea  kwa kucheka, kwasababu stori hazikuwa  hazimhusu  hakushiriki katika maongezi.

Baada ya kuachana na Yonesi, Hamza na Regina  walianza safari ya kruudi nyumbani  maana muda ulikuwa umeenda, ilikuwa inakarbia saa moja na nusu za usiku.

Regina  baada ya kuingia kwenye gari alionekana hakuwa na  mudi ya kuongea  kwani aligeukia kioo na kuangalia mandhari ya usiku ya mji.

Hamza alijua lazima Regina bado atakuwa na hasira juu ya swala la Eliza  hivyo hakutaka kumsumbua na kuendesha gari kimya kimya huku akiwaza namna ya kumchangamsha.

Ambacho  hakujua , Regina alikuwa akiyawazia maneno ya bibi yake, na kujiuliza au bibi yake ameongea vile kutokana na  ugonjwa  wake wa akili  au kuna maana nyingine Zaidi .

Regina  hata hivyo  aliona  kama ni swala la shida yake ya akili  ni kwa muda mrefu sana  hajaugua na kuna siku alikuwa akisahau kumeza mpaka dawa  na hakuna shida yoyote  iliokuwa ikimpata.

Kwake aliona sio sababu ya bibi yake kumwambia kumshikilia Hamza hata kama hampendi.

“Nitaenda kuonana na Dokta , pengine anaweza kuwa na ushauri mzuri Zaidi”Alijiwazia Regina mara baada ya kuona  akili yake ni kama imechoka kufikiria , isitoshe kwanzia asubuhi alikuwa akifikiria mpaka muda huo,  kutokana na uchomvu alijikuta akipotelea usingizini.

Hamza mara ya kufika nyumbani  na  kuegesha gari  na kugeuka nyuma ndio  alikuja kugundua Regina  alikuwa amelala muda mrefu na kujikuta akianza kukuna kichwa.

Hamza aliona  ni swala la kumbeba  na kumpeleka ndani , hivyo alishuka na kufungua mlango mwingine , lakini  wakati anataka kumpakata udenda ulianza kumtoka mara baada ya  kuona  lipsi  nyororo ya  Regina kwa ukaribu Zaidi.

“Hivi jamani  si nimefunga nae ndoa  huyu , inamaana siruhusiwi hata kumkiss japo kidogo”Alijiuliza Hamza swali la kipuuzi akijisahaulisha  yupo kazini.

Kulikuwa  na kasauti kalikuwa kakimwambia anaruhusa kwa asilimia mia moja na  aache   uoga la  sivyo atadhalilisha uanaume wake.

Kitendo cha kuweka pua zake karibu na kupatwa na harufu nzuri kutoka kwa mrembo huyo pumzi yake ilianza kuwa nzito.

“Huu  ni ufala , ngoja nipige  hata  kakiss kakuibia ibia”Alijiwazia  huku   akianza kuinamisha  mdomo wake kuzisogelea lipsi za Regina.

Lakini  sasa kabla hata hajazifikia  Regina  usingizi ulimzidia  na kutaka kudondokea upande mwingine , sasa  ile Hamza   anamzuia ili  asidondoke mdomo wake  uliojaa udenda  ulivamia  nyonyo  la  Regina ambae alikuwa amevaa  blauzi nyepesi tu.

Shida haikuwa mdomo wake kugusana na nyonyo  la watu , tatizo ni kwamba mate mengi yalimtoka na kuloanisha ile sehemu .

Hamza macho yalimtoka lakini alipatwa na ahueni mara baada ya kuona Regina bado hajashituka.

“Bro endelea hapo hapo acha woga..”

Hamza hakuelewa sauti hio ya ushawishi inatokea wapi lakini aliamu  kuitiii na kujaribu  tena huku akifurahia  marashi ya  mrembo Regina.

Hamza  hisia zilianza kumpata kwa kiwango cha  SGR ,  na kutokana na kukosa tendo kwa muda mrefu ilimfanya  ashindwe  kujizuia na kutoa ulimi kama paka.

“Arghhh..!”

Regina alijikuta akishituka mara baada ya kuhisi kitu kikimuwasha  upande wa kulia wa  kifua chake.

 

Previoua Next