Reader Settings

Hamza hata hakujua ndoto iliisha saa ngapi na saa ngapi alipata usingizi lakini kitu ambacho alikuwa akikumbuka usiku aliota na  katika  ndoto aliishia  akiwa anamwita mchungaji kwa ajili ya  kudili  na mzimu.

Alijikuta akikaa kitandani na kufikiria  juu ya uhalisia wa ndoto , ukweli ni kwamba  ashawahi kusikia  aina za ndoto ambazo mtu huota huku wakati akijua kabisa alikuwa akiota , ndio kilichokuwa kikimpata Hamza , alikuwa akiota yupo ulimwengu mwingine huku akijua kabisa alikuwa akiota.

Maneno ya  kile kimemo ambacho kiliachwa  kwake  juu ya  ndoto hizo  kilikuwa kikijirudia rudia katika akili yake.

“The history of  your past life in onother  world has already begun  to echo , if  you fail to inherit  your history ,it will be the end of your life  in this world , your greatest enemy  has already awakened”

Hamza alijikuta akikumbuka  maneno  hayo , lakini ajabu licha ya kwamba ni swala ambalo lilikuwa likimpa wasiwasi kwa kiasi  flani lakini alijikuta akianza kupatwa na hamu ya kujua kinachoendelea , kwake ilikuwa ni kama anaangalia  sinema ya  karne za kumi  na tano katika  nchi za  Ulaya.

Hamza kabla hajatoka kitandani  aliona  siku hio  anapaswa kwenda kuonana  na  Frida , sababu ya kutaka kuonana nae ni kwamba  alikuwa na uwezo wa kuota bila kutumia mshumaa wa nuru ambao alipewa , alikuwa akitaka maelezo kama kuna shida yoyote  ya yeye  kuota  bila ya mshumaa huo , maana ukweli ni kwamba  katika maisha yake ya nyuma hakuwahi kuota ndoto  za maajabu   namna hio , zimeanza   muda mfupi tu  baada ya kufahamiana na Regina.

Kwasababu alikuwa na namba ya Frida aliamua kumtafuta  muda uleule na  simu yake ilipokelewa na alimwambia waonane  siku hio  na Frida upande wake  ni kama alikuwa akiisubiria simu ya Hamza  kwa hamu zote.

Alikuwa  na mpango wa kwenda sehemu mbili  kwa wakati mmoja mpango wake wa kwanza ilikuwa ni kwenda kuonana na Frida na kisha achukue  safari ya kuelekea Morogoro..

Kwasababu alijua ilikuwa ngumu kwa Regina kupika chochote alitoka na kwenda jikoni.

“Jiandae nataka twende wote   kwenye kampuni”Aliongea Regina  baada ya kumaliza kifungua kinywa.

“Leo ni jumamosi   na kazini sina kazi  hivyo sitoenda”Aliuongea Hamza maana alikuwa na mipango yake kichwani  tayari.

“Sio huna kazi  ni kwasababu  hujatafuta kazi ya kufanya , unataka kwenda wapi kama huendi kazini?, au  ni chuo  si likizo inaendelea?”

“Sio  chuo , kuna maswala yangu binafsi naenda kuyafuatilia”Aliongea Hamza na kumfanya Regina  kumwangalia   na muonekano   usiosomeka  na alionekana kuna kitu anataka kusema lakini anasita.

“Jana usiku umesema tupeane muda wa kufahamiana na kuelewana , nimefikiria  kwa  umakini na nimefanya maamuzi , mwanzoni sikutaka  kuolewa lakini  kwasababu  tushafunga ndoa   naamini tutakuwa na mwisho mzuri , sitaki yanayomkuta baba yangu kunikuta na mimi  wala kuwa kama  mama yangu ambaye  ameishia kuwa mpweke…”Aliongea Regina na kauli ile ilimfanya Hamza kufurahi mno.

“Upo sahihi ,  kwanzia sasa hivi  tunapaswa kufikiria  mazuri yenye uelekeo mmoja”

“Umeongea ki usahihi hivyo naamini  utaanza kufanya  kazi kwa bidii  na kupunguza uzembe , najua  una koneksheni kubwa  jambo ambalo ni zuri  lakini hii ni Tanzania, nataka siku ambayo nikikubali watu wakujue kama mume wangu nijivunie kwa kile  ambacho unafanya  na sio kuongelewa vibaya na watu”

Hamza alielewa  alichokuwa akimaanisha  Regina  na aliishia kukuna kichwa  na  hakujali  kabisa  msisitizo wa huyo mwanamke.

“Regina wewe mwenyewe unanijua vizuri , kwasasa nasoma lakini mpango  wangu  nikimaliza hata nisiwe na cha kufanya  ili mradi niwe na hela ya chakula basi , sitojali  watu  wanachoniongelea”

“Sawa unaweza usijali lakini vipi  kuhusu mimi, siwezi kuwa na mwanaume ambae hana  malengo wala  ndoto za kukamilisha , wanaume ambao hawana malengo  wanachukiza  zaidi ya wanaume  wachepukaji”

Regina alikuwa siriasi , alionekana hakuwa akitania hata kidogo , alithamini sana Career yake  hivyo alihitaji mtu ambae atakuwa sambamba nae.,

“Vipi kuhusu Eliza  sasa , unaweza kukubali  niendelee nae  bila kuleta shida?”

“Inamaana hukuelewa pointi yangu  au unajitoa ufahamu?”Aliongea  huku  hasira zikianza kumvaa.

"Hivi  kwenye kichwa chako wewe  malengo yako ni wanawake na sio kitu kingine ,  wanaume wengi wa umri wako  wanafikiria namna ya  kutengeneza pesa , kuanzisha biashara  na kufanya kazi kwa bidii , ukiachana na  wanawake ni kitu  kipi kingine unataka kufanya  au kukamilisha kwenye maisha yako?”Aliongea Regina  akiwa siriasi.

“Kufanya kazi kwa bidii  na kupata hela  sio  malengo yangu kwasasa naona ni kama kujishughulisha tu , kama ni hela  tunazo za kutosha , kwani  unataka kuwa na shilingi ngapi  ili uridhike?”

“Unakwepa majukumu yako, hela zangu sio zetu , halafu wewe  si ndio jana ulisema  mwanaume anapaswa  kujua kuwajibika ,  kwahjio kutofanya chochote na kupoteza muda   ndio unaita  uwajibikaji?”

“Regina kwanini unaweka vigezo vikubwa hivyo, mimi  nipo mwaka wa mwisho chuo   na sasa hivi umenipa kazi kama mfanyakazi wako wakati wewe ukiwa ndio CEO , kazi zote ninazopewa kufanyia kazi   nazifanya kwa usahihi  na nazidi kuwa bora siku hadi siku , nimeweza kushinda  tuzo  kwa ajili ya kampuni na mengineyo , kipi  kingine  napaswa kufanya?”

“Ninachomaanisha sitaki mwanaume anaeridhika na  kitu kidogo  au wewe unadhani hela ulizopata zinakutosha  kabisa?”Aliuliza na kumfanya Hamza kutoa tabasamu la uchungu.

“Labda  ndio zinanitosha , nimepitia mengi  mpaka kufika hapa  na  malengo yangu ni kuishi maisha ya  amani na utulivu  na kuwa na furaha”

“Umepitia mengi!, unamaanisha kuua watu?, mimi nataka  kujua ni mafanikio  gani umefanikisha ,  kama ni kupitia  mengi kila mtu anapitia hayo mengi , wewe baada ya kupitia mengi mafanikio yako ni yapi?”

“Sijasema mafanikio yangu ni kuua watu na  sio kweli kama nimeaua watu?”

“Kama sio hivyo ni mafanikio gani  unayo?”Hamza alijikuta akishindwa kujibu swali lile.

Mwingine angeona  Regina ana masharti makubwa lakini ukweli ni kwamba  alikuwa ni  bosi wa kampuni kubwa ambayo imeorodhshwa katika masoko makubwa ya hisa dunani , kama  ataolewa inamaanisha na mume wake atakuwa  katika rada za watu.

“Najua unashindwa  kuongea ,  wewe ni mwanaume usie na malengo   na uliepoteza tumaini ,  nenda kapoteze muda huko unakoenda , mimi naenda kazini”Aliongea  na kisha kwa hasira alishika mkoba wake na kutokomea nje.

Hamza aliishia kuvuta pumzi tu  na hakuongea chochote , sio kwamba  hakuwa na mafanikio , alikuwa nayo lakini hayakuwa yakielezeka.

Yeye  alijichukulia kama mtu ambae ameishuhudia Tsunami  tayari  na hawezi kuogopeshwa na mawimbi madogo madogo.

Lakini hata hivyo  alijiambia sio  muda sahihi wa kumwambia Regina chochote , isitoshe  licha ya kwamba ni kweli alitamani maisha ya amani ambayo hayana usumbufu , lakini vilevile alikuja Tanzania kwa lengo moja tu , lengo la kumfahamu Mzee ni nani.

Siku zote wanawake wanajivunia kuwa na mwanaume ambae ana mafanikio kumzidi , hilo Hamza alielewa lakini aliona sio muda sahihi wa kumuonyesha chochote  Regina, isitoshe  sio yeye tu kama sehemu ya familia yake.

Kwasababu   alikuwa na mzunguko mrefu hakuchelewa kuondoka nyumbani  na hakutoka na gari  bali aliona atumie usafiri wa  uma , isitoshe  Regina alimnanga vya kutosha hivyo  hakutaka kushobokea magari yake.

Ilimchukua dakika kama  arobaini hivi  kufika Madale kwa ajili ya   kuonana na Frida.

Na baada ya kugonga ni Frida ambae alitoka  kuja kumfungulia  mlango .

“Mlinzi wako leo hayupo?”Aliuliza Hamza.

“Kwasasa sina mlinzi,  uliemkuta kipindi kile amerudi nyumbani  kwao  Singida”Aliongea  na Hamza alitingisha kichwa.

Frida alikuwa mwanamke mrembo   lakini  Hamza aliweza kuona mabadiliko   Frida  alionekana kupungua mwili.

“Naona  umepungua mwili ,  ndio  kutokana na adhabu nini?”Aliuliza Hamza maana alijua mara ya mwisho wakati alipoongea na  Frida alimwambia   alikuwa akienda kuhojiwa.

Kitendo cha Frida kumsikia Hamza akimwambia amekonda alijisikia  faraja , japo ukweli ni kwamba sababu za kukonda   ni juu ya kazi yake na misheni yake kwa Hamza.

“Niliweza kutoka  bila ya   kupatiwa  adhabu  ndio maana nimewahi”Aliongea  huku akimkaribisha  ndani.

Eneo la sebuleni kulikuwa na makatarasi kibao  pamoja na vitabu , ilionekana mwanamke huyo alikuwa bize  kusoma kama sio kuandaa ripoti.

“Oh !, nilikuwa bize kidogo na ripoti ndio maana  unaona makaratasi mengi”Aliongea.

“Wana taaluma  hamjawahi kupumzika, kila saa mpo  na mavitabu mnasoma na kufanya uchambuzi”

“Watafiti   wa   kisayansi hawajawahi kupata usingizi  kwa muda mrefu , hata  wakati  wakulala tunawaza kile kilichokwama, ukiachana na  kutambulika  kutokana na kukamilisha kitu kikubwa lakini haya yote tunafanya kwa ajili ya faida  ya dunia”Aliongea na kumfanya Hamza kutingisha kichwa kumwelewa.

“Nina safari ya Morogoro ,  hivyo sitaki kukaa hapa muda mrefu”Aliongea Hamza.

“Ukweli ni kwamba nilitaka kukutafuta pia leo tuonane kama nilivyokuambia kwenye simu , nianze  mimi au uanze wewe kuongea  sababu ya kutaka kuonana?” Aliongea Frida.

“Nitaanza mimi”Aliongea Hamza na Frida alitingisha kichwa akimpa ishara ya kuongea.

“Kilichonileta ni swali  moja tu ,  wakati unanipatia ule mshumaa ulisema umetoka kwa Dokta  Genesha  na   kazi yake ni kuamsha ndoto,  je una kazi zaidi ya kuamsha ndoto?”Aliuliza Hamza  na swali lile kidogo lilionekana kumshitua  Frida lakini alijizuia.

“Kwanini unaongea  hivyo , kuna  kitu kingine ambacho  kimekutokea kwasabu ya  Mshumaa?”

“Hakuina kilichonitokea , ukweli ni kwamba sijawahi kuutumia tokea  unipatie , ila katika kipindi chote nimekuwa nikipatwa na ndoto kama kawaida, kama mshumaa ni  wa kuamsha ndoto  na  naota bila ya kutumia mshumaa kuna haja ya kuutumia?”Aliuliza Hamza na swali lake lilimfanya Frida kupumua kwa ahueni.

“Unachokiona kupitia  ndoto sio  ndoto kama ndoto bali  ni uhalisia wa kumbukumbu zako, kuna kitu nilisahu kukuambia kuhusu mshumaa , licha ya kwamba ni kweli  kazi yake ni kuamsha ndoto lakini pia  ni kuifanya akili yake isichukulie kile ambacho unakiota kama ndoto”Aliongea na kumfanya  Hamza  sura kuchekza kidogo .

“”Unamaanisha nini?”

“Umesema  unaonta ndoto kama kawaida,  kama umeota zaidi ya mara mbili au mara tatu  lazima kuna tofauti ambayo umeweza  kuona?”Aliongea Frida na kumfanya Hamnza kushangaa.

“Umnejuaje kuna tofauti?”

“Umesahau mimi ni  mwanafunzi wa  Dokta Genesha, ukiachana na  Profesa   Frola rafiki yako”Aliongea na kumfanya Hamza kukunja ndita.

“Unamfahamu  Dr Ronicas  kama mwanafunzi  wa Dokta Genesha?”

“Kila mtu anamfahamu Dr Ronicas , najua pia alikuwa hapa nchini Tanzania , wakati  nikiwa  kama Ajent  miaka  saba iliopita  niliweza  kumfahamu Dr Ronicas  lakini ni kupitia maandishi tu”.Aliongea na Hamza  hakushangaa sana maana mzunguko wa Dokta Genesha haukuwa wa kawaida.

“Licha ya kwamba  ndoto  zote utakazoota  una husika moja kwa moja wakati wa matukio lakini utofauti  unakuja  pale  ambapo unaota lakini hujui unaota  na  muda mwingine utakuwa unaota huku ukijua kabisa unaota”Aliongea Frida na kumfanya  Hamza kutngisha kichwa.

“Upo sahihi  mara ya kwanza niliota  bila kujua naota , lakini jana  nimeota huku  akili yangu ikiniambia nipo ndotoni”

“Ndoto  unayoota unajiona kuwa na sura ya tofauti si ndio?”Aliuliza .

“Hivi nilikusimulia  , mbona ni kama unajua  kila ninachoota?”Aliuliza Hamza na kumfanya Frida kutabasamu.

“Kwasababu  wewe ni  mteja wangu wa tano”

“Unamaanisha kuna watu wanaota kama ninavyoota mimi?”

“Ndio wapo   licha ya kwamba  kuna utofauti  lakini wote  wanaota wakiwa na sura tofauti , ni kama wamezaliwa katika miili mingine  kwenye ndoto zao , utofauti ni kwamba  kwa maelezo ya Dokta Genesha  wewe  ndoto zako zina upekee”

“Upekee!  Unamaanisha nini ?”

“Sina maelezo ya kutosha,  ninachojua unachoota ni kitu cha kipekee  ambacho kitakufanya  kutafsiri Lugha iliowashinda  binadamu kutafsiri”Aliongea  na Hamza alikuwa akielewa  Frida alikuwa akimaanisha nini kuhusu lugha.

“Kwahio ni ipi sahihi , kuota nikiwa najua  naota ama kuota  nikiwa sijui  naota?”.

“Swali lako   nikilirudia naweza kuliweka hivi , je  ni ndoto ya  aina ipi unaweza kusahau  haraka, kati ya ndoto ambayo unajjihisi  unahusika moja kwa moja au ndoto ambayo unajua  unaota?, jibu la swali hili kitaalamu ni kwamba ndoto  ya kawaida ambayo hujui unaota  ndio ambayo  haisahauliki haraka , lakini kwa swala  lako wewe  ndoto yako sio kama ndoto zingine , ubongo wako sio wenye kutengeneza  matukio  ambayo unaona  kama msingi mkuu wa ndoto bali  unachoota ni koneksheni ya kimawasiliano baina ya Dimension mbili tofauti  hivyo  kwa swala hili unapaswa kujua  unaota  lakini pia uwe na uwezo wa kukatisha ndoto  muda wowote”Aliongea  Frida.

“Kwa  kukuelewesha  kwa urahisi  wakati ukiwa ndotoni  si unajua unaota, lakini  ghafla ukakutana na tukio la kutisha  na  kutamani ndoto iishie palepale  na ikaisha  hapo utakuwa umefanikiwa , kati ya wagonja wangu ambao nishawahi kupata wengi walikuja  kwasababu wanaota vitu vya ajabu ambavyo vinawafanya kushindwa kulala,hakuna  dawa  ya kumpa   mtu kuzuia ndoto bali  namtengenezea mazingira ya kuifunga ile ndoto na  njia pekee  ni  kumfanya aote wakati akijua anaota  kwa njia ya hypnosis”

“Kwahio   napaswa kutumia mshumaa kama njia ya kunifanya niote wakati nikiwa naota  si ndio?”

“Ndio , unapaswa kuota  wakati ukijua unaota   na wakati huo  hisia zako zote zikiwa katika ndoto , hata baada ya ndoto isitokee ukasahau  kitu chochote kile ambacho unaota , kama nilivyosema  unaota ukiwa umetawala  mwili mwingine, lakni nafsi ya  mwili huo bado inafanya kazi, mshumaa wa nuru utakusaidia  kuwa  na uwezo wa kutumia akili yako  na  ya mtu ulietawala mwili wake kwa wakati mmoja  na kila unachoota hakitasahaulika  hata baada ya ndoto”Aliongea Frida.

“Kwahio  unaamini  kwamba  kupitia hii  ndoto  nitaweza kutafsiri kitabu alichoniachia Dokta  Genesha”

“Ndio kwasababu kupitia hio ndoto utajifunza lugha mpya ambayo hukuwahi kuijua hapo kabla na itaendana na lugha ambayo binadamu tumeshindwa kuitafsiri”

“Kuna uhakika gani kwamba nitaweza  kujifunza lugha  mpya  na je   ninachoota mnajuaje kama ni sahihi  au  ni ndoto tu  ambazo hazina mpangilio”Aliongea Frida  na kumfanya  Frida kutabasamu kidogo .

“”Nadhani ni muda wa kukuambia na mimi kwanini nilitaka   kuonana na wewe . ndio njia rahisi ya kujibu swali lako”Aliongea Frida na kisha  alimwambia Hamza asubiri anarudi.

Dakika   moja tu alitoka chumbani  akiwa ameshikilia picha  na kumpatia  Hamza.

“Hii ni picha ambayo aliniambia nikupatie Dokta , huwezi kuita picha ni kwasababu ni  mchoro  tu  lakini nadhani umebeba maana ambayo utaweza kuitambua”Aliongea  Frida  na Hamza aliingalia ile picha na macho yake yalichanua .

“Red moon!!”Aliongea Hamza akimaanisha mwezi mwekundu.

Previoua Next