Reader Settings

“Kazi yangu nyingine , kwanini ghafla tu unaniuliza kitu kama hicho?”

“Najua  utadanganya  lakini nimesikia taarifa  unafanya kazi  chini ya mtandao wa kihalifu  wa Chatu”Aliongea Prisila  na pale sasa  Hamza alielewa ni kipi kilikuwa kikimfanya mrembo huyo kuwa na wasiwasi.

“Unaujuaje mtandao wa Chatu?”Aliuliza Hamza.

“Niambie ukweli  kama  unafanya kazi  kwenye mtandao huo au hapana , napatwa na wasiwasi  maana mimi ndio nimekukutanisha na bosi Regina”Aliongea .

“Prisila   huna haja ya kuwa na wasiwasi hivyo , sio kama unavyofikiria  ni kwamba tu  nina ukaribu na bosi wa huo mtandao lakini  haimaanishi kama  nafanya hizo kazi , lakini pia huo mtandao sio wa kihalifu kama unavyofikiria wewe”Aliongea Hamza.

“Najua habari  juu  za huo mtandao na imekuwa  moja ya topiki kwenye kampeni  za viongozi wa chama  cha wapinzani, najua pia  kiongozi unaemzungumzia  una ukaribu  nae ni Dina , mwanamke Smrembo,  kwahio wewe ndio mpenzi wake ndio maana mnafanya kazi pamoja?”Aliuliza na  kumfanya Hamza asijue acheke ama  alie.

“Nani kakuambia hayo yote”

“Nime mfollow Instagram  ana wafuasi kibao  , wengi wanamjuia  japo haijulikani  kama   ndio mmiliki wa mtandao  wa Chatu, baada ya kusikia una ukaribu nae nikajua moja kwa moja   mnafanya wote kazi , wasiwasi wangu sio wewe kufanya kwake kazi maana siwezi kukupangia ,  kama yanayozungumzwa ni sahihi basi  hupaswi kuwa karibu na  Bosi Regina, chochote kitakachomtokea mimi ndio nitalaumiwa kwa kutokuwa makini”Aliongea  huku akionekana kuwa siraisi.

Hamza hakujua   nini Prisila  aliambiwa  na nani lakini  alijua kwa mwanamke kama huyo  anajali sana kitu kinachoitwa  sheria.

“Unaonaje tukifika Dar  twende wote ukajionee mwenyewe   na ndio utajua kwanini nashirikiana nao”Aliongea Hamza , aliona ndio namna  pekee ya kuondoa wasiwasi wa Prisila  na mambo mengine yaendelee.

“Wewe niamini mimi tufika  twende wote?”Aliongea Hamza mara baada ya kuona   Prisila anasita na  kutokana na msisitizo wa Hamza Prisila aliamua kukubali,  hata hivyo aliona  kama Hamza ni mhalifu   kwanini atoe kiasi chote kile cha pesa kwa ajili ya kusaidia watoto  Yatima, ukweli ni kwamba tokea aambiwe juu ya hilo swala alikuwa na wasiwasi na alitamani kumwambia Regina  lakini aliona ni busara kuongea na Hamza kwanza.

Baada ya masaa  mawili kupita hatimae waliweza kufika  mjini Dar es salaam na Hamza alinyoosha moja  kwa moja mpaka  Kijichi   unapopatikana  mgahawa   wa chai wa Dina.

Hamza mara baada ya kusimamisha gari alishuka na Prisila  na kuingia ndani  na   mhudumu  alivyomuona Hamza alitingisha kichwa kumkaribisha kwa adabu.

Muda  huo  waliweza kusogelewa  na Lawrence ambae alionekana kuwa   na haraka.

“Bro  karibu sana  ila  Madam ameenda  kwenye  kikao  tokea asubuhi   ila naamini atawahi kurudi”Aliongea Lawrence  na kumfanya Hamza kushangaa kidogo.

“Kwenye kikao?!”

“Ndio  , ni juu ya lile swala la usiku  ule”Aliongea Lawrence  na kumfanya Hamza kuelewa.

“Hii sehemu  nilikuwa napita tu ,  sijawahi kuelewa wanachouza hapa”

“Wanauza Chai”

“Sehemu kubwa hivi  wanauza chai  tu?”

“Sio chai  ya kawaida Prisila,  ni chai inayotumia aina  nyingi ya mimea , ushawahi kusisikia Gisaeng tea?”Aliuliza  Hamza akiamini  Prisila atakuwa anaangalia filamu za  kikorea.

“Ndio nishawahi kuona   kwenye filamu  wakorea wanashabikia, unasema na hapa wanauza!!?”

“Sio  Gisaeng  tu , hapa wanauza kila aina ya chai maarufu zote  duniani ikiwemo  Panda Dung  kutoka China , Gyokoro , Yellow Gold  na aina nyingine nyingi za chai”Aliongea na kumfanya   Prisila kushangaa  na alishangaa baada ya kuona kuna wateja wengi tu wakionekana kufurahia chai.

Hawakuchukua muda mrefu kuwa peke yao  Dina aliweza kurejea na alishangaa kumuona  Hamza akiwa na mwanamke mwingine , tena mrembo.

Upande wa Prisila  pia alishangaa kumuona Dina kwa urembo wake , ijapokuwa  Prisila alikuwa amemzidi  Dina lakini   muda huo  mwonekano wa kujiamini wa  Dina umemfanya kuona amezidiwa  vitu vingi.

“Hamza huyu  msichana mrembo ni nani ,  mbona hunitambulishi?”Aliongea Dina  huku akiwa na wasiwasi.

“Huyu  anaitwa Prisila  ni mfanyakazi  mwenzangu lakini vilevile nimegundua leo ni rafiki yangu wa utotoni”Aliongea Hamza na kauli ile ilimfanya Dina kujiona  mdogo mbele ya  Prisila maana licha ya kwamba alikuwa amevalia mavazi ya kawaida lakini alikuwa ni mrembo haswa.

“Hello ! Naitwa Dinaq , ndio bosi wa hapa”Aliongea.

“Nimefurahi kukuahamu  Dina”Aliongea Prisila  huku akimpatia mkono lakini alionyesha hali ya wasiwasi.

“Prisila unaonaje  sasa , huyu Dina unaemuona anafanana na  mtu  mhalifu?”Aliuliza  Hamza lakini upande wa Prisila  ni kama  alianza kukosa utulivu , ukweli ni kwamba  alikuwa akizidi kujiuliza inakuwaje Hamza anakutana mara kwa mara na wanawake warembo warembo na  wote wanaonekana kana kwamba wanampenda.

Dina mara baada ya kusikia kauli ya  Hamza ni kama sasa alielewa kwanini  amekuija na mrembo huyo hivyo alichukua nafasi ya kujielezea.

“Prisila , ijapokuwa  kwa nje tunaweza kuonekana kama wahalifu lakini biashara zetu hazihusiani  na maswala ya kihalifu, tofauti ya biashara zangu na za  kawaida  ni kwamba tunamalizana na wateja wetu kibiashara bila kuhusisha sheria”Aliongea.

Prisila alimwangalia Dina kwa wasiwasi , lakini tabasamu la Dina lilimfanya kushindwa kujizuia  kumuamini.

“Ni kweli?”Aliuliza.

“Unadhani nakudanganya, kama  kweli sisi ni wahalifu unadhani ingekuwa rahisi kwa serikali kutuangalia  tu bila kuchukua hatua yoyote , ijapokuwa wapo wengi wanaotusemea mabaya kama wahalifu lakini  tunacheza nafasi  kubwa ya usalama ndani ya nchi hii, kama huniamini mimi unaweza kumuamini Hamza , unadhani ni  mtu mbaya ukimwangalia?”Aliuliza  Dina na kauli yake ilimfanya   Prisila kukumbuka  Hamza muda  mchache uliopita alikuwa ametoa kiasi kikubwa cha fedha kwa ajili ya watoto   yatima, tena wakati ambao kituo hicho kilikuwa kikihitaji  msaada  kwa  kuwa nje ya bajeti.

Walikuwepo matajiri wengi ambao walikuwa na uwezo wa kuchangia zaidi ya milioni mia tisa   lakini  wengi wao michango yao haizidi hata milioni  mia nne , isitoshe  kwa mwonekano wa Hamza alionekana kama mtu ambae anauhitaji wa  hela , kama sio hivyo  kwanini akubali kuajiriwa na Regina  kwa ajli ya mshahara wa laki saba .

Baaada ya kufikiria hayo yote  aliona  wasiwasi wake ulikuw bure tu na hakupaswa kumshuku hata kidogo.

Dakika ile ile  ni kama  sasa ndio anaanza kumuona Hamza kama rafiki yake wa utotoni  ambae alikutana nae  kituoni ,ile furaha ya kumjua Hamza kama mtu aliepotezana  nae  ilianza kuchipua.

“Hamza Sorry kwa kukushuku , ningejua nisingemsikiliza Lea   na ujinga wake, wote mnaonekana kuwa watu wazuri”Aliongea  Prisila.

“Lea ndio nani na kwanini akuambie mambo yangu ?”Aliuliza Hamza akiwa amekunja sura.

“Lea ni jirani yetu  na ni kama rafiki yangu   wa muda mrefu , alikuja  nyumbani  na kuniambia alikuwa Tanganyika Club  na aliwaona wewe  na  Dina mkiwa pamoja , amesema wewe ni  mhalifu  hivyo nichukue tahadhari”Aliongea na kumfanya Hamza kumgeukia Dina.

“Ile siku  kulikuwa na mwanamke yoyote alieitwa Leah?”Aliuliza.

“Sijasikia  jina la Leah , halafu ile siku ilikuwa ni  tofauti  na  watu wanazopendelea kuja kuchukua mazoezi hivyo hatukutana na watu wengi”Aliongea Dina .

“Prisila  nadhani umejionea mwenyewe  licha  ya kwamba ni kweli Chatu inachukuliwa kama   mtandao wa kihalifu ,  sio swala la kumfanya mtu awe na aibu  kama sheria zinafuatwa hivyo usiwe na wasiwasi sasa”Aliongea na kumfanya Prisila mzigo wa wasiwasi  kuutua

Maana  swala hilo lilikuwa likimuumiza kichwa sana , kama  mwajiri aliona amemwingiza  bosi wake kwenye  hatari na kutafuta namna ya kumuondoa kwenye hatari lakini  baada ya kuongea  na Hamza na kuonyeshwa  hali halisi  wasiwasi ulimtoka.

“Haya yameisha sasa , Prisila unaonaje tukiwa dadaz , njoo nikuonjeshe  radha ya chai tofauti tofauti”Aliongea Dina kwa furaha  huku akiagiza chakula pia maana Hamza alikuwa na njaa.

Dakika chache mbele walijikuta washazoeana na kuanza kupiga soga na kucheka.

Prisila alijua vitu vingi sana kuhusu  chai na faida zake mwilini  na  mwisho wa siku aliona ni kheri kunywa chai kama njia ya kujichangamsha kuliko mvinyo uliojaa pombe.

Dina alidhamiria  kumfanya  Prisila  rafiki yake pengine ni kwasababu ya Hamza na ili  kukazia alimwalika  Prisila kwenda nae kwenye sherehe ya uzinduzi wa Albamu  ya msanii maarufu , Dina alikuwa amealikwa hivyo alimchagua  Prisila kwenda nae , kwasababu Prisila alikuwa akijua juu ya uzinduzi huo alikubali.

“Naona amani imerudi  sasa maana ulikuwa ukiniangalia kwa wasiwasi mno?”Aliongea  Hamza  wakati akimsindikiza Dina kuelekea nyumbani.

“Wasiwasi wangu haukuwa  wewe kufanya wapi kazi ,  wasiwasi wangu  ulikuwa juu ya  Regina   na Kampuni”

“Unamjali  sana Regina , sijui kama na yeye anakujali kama unavyomjali?”

“Sina  mashaka  kabisa na Regina , alivyosiriasi utadhania  hajali  lakini ukimiuona anaweka hisia zake wazi kukuonyesha kujali  huwa inagusa sana , nimekuwa nae namjua vizuri”Aliongea na Hamza hata yeye  alijua hilo  maana hata Eliza aliongea.

“Vipi  yule mtoto mwenye mashavu kule Morogoro niliekutana nae miaka zaidi ya ishirini iliopita?”Aliuliza Hamza na kumfanya Prisila kuona aibu ilionekana udhaifu wake ni kuambiwa alikuwa na mashavu makubwa akiwa mdogo.

“Wakati nikiwa mtoto nilitelekezwa  na mama  kule kituoni kwa Baba Hizza na sikuwahi kumuona mpaka leo”Aliongea  Prisila na kauli ile ilimshangaza  na kumgusa Hamza.

“Mama yako alikuacha kule kituoni , ilikuwaje?”

“Ni stori ndefu  ila nikipindi  ambacho  baba alikuwa  nje  ya nchi  kwenye mafunzo ya kijeshi , mama  alionekana kutompenda  baba , pengine ilikuwa ni kutokana na kusafiri safiri  kwake ndio maana alipoteza hisia  na  baba  mpaka  akaamua kunitelekeza  kituoni , Baba Hizza ni  ndugu  wa baba upande wa bibi ,  baada ya  baba kurudi nchini  ndio  aliambiwa nipo kituoni na kuja kunichukua”

“Na mama yako sasa hivi yupo  wapi?”

“Mama sijui alipo   mpaka sasa , ila tetesi  zinasema itakuwa anaishi nje ya nchi maana alikuwa  na mahusiano  ya siri na mtalii, sijui labda baba anajua anapoishi ila  sijawahi kumuuliza”Aliongea  na kumfanya  Hamza kumuonea huruma.

Kila mwanamke aliekuwa nae  alikuwa na matatizo upande wa mama  lakini ilionekana  Prisila alikuwa na uchungu  zaidi , kutelekezwa  lazima  itakuwa  anajihisi mama yake hakumpenda.

Hamza wakati akifikiria namna ya kumfariji  muda huo wakiwa  mkabala na chuo cha TIA  walisimamishwa na Traffic.

Dakika hio hio baada ya  Hamza kusimamisha gari  pembeni,  gari mbili  ziliongezeka  kutoka nyuma yao  na  mbele yao  moja  kati ya hizo ikiwa ni Diffenda  ya  kijeshi jambo ambalo lilimfanya akunje sura na kujiambia kumekucha.

Wapita njia pia walivutiwa maana ni mara chache sana kuona    jeshi la ulinzi   kuzingira gari  mbele na nyuma kama kwamba wanakamata mhalifu maana wengi walizoea kazi hio  hufanywa na jeshi la polisi.

Muda ule  mlango wa gari aina ya Jeep ulifunguliwa na alitoka   mwanajeshi alievalia kombati za jeshi , alikuwa ni Afande Mdudu akitanguliwa na wanajeshi wengine na wote walizingira  gari ya Hamza huku wakimwamrisha atoke.

Prisila alijikuta akitetemeka mno kutokana na tukio lile  na alimwangalia Hamza na kushangaa alikuwa katika hali ya utulivu.

“Hamza nini kinaendelea?” Mrembo huyo aliuliza  huku akiamini pengine  ni kutokana na Hamza  kujihusisha na mtandao wa kihalifu.

“Prisila  usiwe  na wasiwasi najua wanachotaka  ngoja nitoke wewe utatangulia  nyumbani  tutawasiliana”Aliongea  Hamza lakini kauli yake haikutosha kumtoa Prisila   kwenye wasiwasi na   Hamza  baada ya kutoka na yeye alitoka.

“Afande Mdudu nini tena tatizo?”Aliuliza Hamza mara baada ya kutoka  nje ya gari.

“Hamza Mzee , Naitwa Meja Mdudu , kapteni  kikosi namba mbili  kitengo cha usalama wa nchi ,  rasmi kwanzia  sasa hivi  upo chini ya ulinzi  kwa tuhuma za mauaji , kusababisha Ghasia na  Utekaji”

Baada ya kuongea hivyo alitoa nyaraka na kumuonyeshea  Hamza mbele yake, ilionekana kweli ni  nyaraka ya  kukamawa kwake iliosainiwa na wakubwa.

Hamza macho yake yalisinyaa , ilionekana  hawa wanajeshi walikuwa wakimfuatilia kwa muda mrefu na hawakutaka kumkamata mbele ya Dina wakijua kuna uwezekano angemkingia kifua ndio maana wakamuwekea mtego wa kumkamatia njiani.

Japo Hamza hakupenda kukamatwa mbele ya kadamnasi ya watu  na  mbele ya  Prisila ambae ndio kwanza anatoka kumtoa hofu   ili aendelee kumuamini  lakini   hakuwa na jinsi zaidi ya kutii shuruti.

“Naona  mnaniwinda sana  kama mizimu”Aliongea na kumfanya Afande  Mdudu kucheka kwa furaha.

“Unadhani nilikuwa  nikikuogopa , kabla  ya kuwa mwanajeshi mimi ni raia wa hii nchi  na kabla ya kuchukua hatua lazima niwe na ushahidi wa kisheria  , kwa mtu hatari kama wewe ushahidi  wa uhalifu wako ninao hivyo ninakukamata”

“Kwahio unajiona   raia unaetii sheria , lakini sio wewe juzi  ulietaka   kumfosi  mwanamke  kwenda kumuoa , na hio  pia ni sheria ya hii nchi?”Aliuliza Hamza na kumfanya  Kamanda kunywea

“Haina haja ya kubadilisha topiki , nipo hapa  kikazi  na  sina muda wa kuongea ujinga na wewe , kama unajua kuwa mtii na tuondoke pamoja”Aliongea Kamanda  Mdudu maana alijua  kama Hamza akitaka kuwakimbia   wanaweza wasimzuie , lakini   mbele  ya mwanamke  kama Prisila walijua ndio  njia rahisi ya kumkamata na kumfanya atii shuruti , ulikuwa ni mpango.

 

 

 

Hamza aliishia kutoa tabasamu la uchungu na aliona Mdudu alikuwa na akili kidogo kwa kutaka kumkamatia mbele ya  Prisila.

“Hamza..!!”

Prisila alitaka kuongea neno lakini  jicho alilokatwa na wanajeshi hao lilimfanya kukosa  nguvu ya kujiamini.

“Sikia Prisila usiwe na  wasiwasi  na  usifikirie mbali, nitakupigia simu hili likishaisha  nakuhakikishia sijafanya kosa lolote  hivyo hawatonifana  chochote”

“Mhalifu hebu  acha majigambo kujsafisha mbele ya  mwanamke uwe  umefanya au hujafanya sisi  ndio tunajua”Aliongea Mdudu

Kwa jinsi wajeda hao walivyokuwa siriasi  Hamza aliamua kutii amri  na alimwangalia  Prisila  kwa macho ya wasiwasi.

“Nitakupigia  simu , nakuahidi nitakupeleka  kwenye sherehe aliokuwahidi  Dina mimi mwenyewe”Aliongea Hamza.

“Hio ni ahadi??”

“Ndio ni ahadi , hivyo acha wasiwasi”Aliongea Hamza na  kishingo upande Prisila alikubali  na kumfanya Hamza kuvuta pumzi.

Mdudu palepale alitoa  ishara kwa  mwanajeshi mwenzake na  Hamza alaivishwa pingu na kuingizwa ndani ya gari  na  kuondolewa kwa spidi kuelekea mjini”

Previoua Next