Reader Settings

Hamza  mara baada ya kuingia eneo la  sebuleni aliweza kumuona  Yulia  alievalia blazia ya rangi nyeupe na  jeans ya rangi ya bluu bahari  na  Regina upande wake alikuwa amevalia  gauni la rangi ya bluu na visendo manyoya, wote walikuwa wamekaa  ki upande upande kwenye masofa.

Kwa mwanaume yoyote angeburudishwa na muonekano wa warembo hao wawili  , maana  licha ya kuwa na  rangi tofauti lakini walikuwa wakivutia  macho  mno.

Lakini upande  wa Hamza ilikuwa  akifikiria tofauti muda huo , kitendo cha kuwaona wanawake hao wamekaa sehemu  moja aliona kuna kitu ambacho hakipo sawa.

Muda ule  Yulia mara baada ya kumona Hamza akiingia  uso wake ulipambwa na tabasamu   mwanzoni na  kugeuka  kuwa hali ya mshangao kana kwamba ni mtu ambae hakutarajia kumuona hapo.

“Hamza unafanya nini hapa?”Aliuliza  Yulia huku  akishangaa.

 Regina  mara baada ya kusikia Yulia anamwita Hamza   macho yake yalijawa na mshangao pia , alionekana kushangaa  Yulia kumfahamu  Hamza.

“Na wewe unafanya nini hapa?”Aliuliza Hamza huku  akikunja ndita.

“Nimetoka kumtembelea  leo  Bi Mirium   ni mfanyabiashara  ambae  namuheshimu , nafahamiana  pia  na  Regina ndio maana nimekuja kumsalimia”Aliongea  Yulia  akiwa  na utulivu.

“Yulia  unafahamiana  na Hamza?”Aliuliza Regina na Hamza alitaka kujibu hilo swali haraka lakini  Yulia alimuwahi.

“Namjua ndio , nimekutana nae miaka saba iliopita  nikiwa nje ya nchi na ndio  alieniokoa kwenye mikono ya watekaji , siku kadhaa zilizopita nilikutana nae  hapa Dar ,  kukutana  kwetu kumenifanya  nione imepangwa tuje kuonana tena”Aliongea huku akiwa na  tabasamu zito.

Regina alikuwa akijua swala la  wazazi wa Yulia kupoteza  maisha  wakiwa nje ya nchi baada ya kutekwa na katika tukio hilo  aliesalia  alikuwa ni Yulia pekee yake , sasa hakujua kwamba tukio la  kipindi kile  Hamza alihusika kwa  kumsaidia mwanamke mrembo kama Yulia.

Isitoshe  pia  pengine wakati  huo Yulia alimchukulia Hamza kama raia wa  nje ya nchi, hivyo kukutana nae  nyumbani hapa Tanzania lazima  kuwe na hisia tofauti zilizojijenga kwake kama mwanamke , maana sio rahisi kupata msaada kwenye ardhi ya  ugenini.

“Mbona hujawahi kuniambia?”Aliuliza Regina huku akimwangalia Hamza.

“Nilisahau ndio maana ,  kwangu halikuwa tukio kubwa sana kiviile ndio maana sikuona haja ya kuliweka wazi”Aliongea Hamza huku akilazimisha tabasamu.

“Tukio la namna hio unaliita  dogo! , huwa najiuliza ni  tukio lipi ni kubwa kwako?”Aliongea Regina  na kumfanya Hamza kumeza mate  huku akiona aibu kidogo  baada ya kuhisi kuna zaidi ya maana kwenye kauli ya Regina

“Regina  unafahamiana vipi na Hamza  ni rafiki yako au?”Aliuliza  Yulia  na kwa namna ambavyo alikuwa mpole utadhani ni mpole kweli kumbe ni mtukutu.

Regina aliishia kudharau  ndani  kwa ndani kwenye moyo wake ,  alikuwa na akili sana , ijapokuwa  kihisia alikuwa slow  haikumaanisha  hakuwa  akijua  kinanachoendelea kwa  Yulia.

Isitoshe  Yulia  hata yeye alikuwa  na cheo kama chake ijapokuwa Yulia alitambulika kama Managing Director(MD) , yaani Mkurugenzi mtendaji na Regina  kama Chief exucutive officer(CEO) yaani Afisa Mtendaji mkuu lakini  wote  ni wafanyabiashara  wenye vyeo vinavyolingana  kimajukumu  kwa kiasi flani ndani ya kampuni  wanazoongoza.

Ukweli ni kwamba mwanzoni  Regina alikuwa akijiuliza   kwanini  Yulia Mkurugenzi wa makampuni ya Prima Tanzania  kumtembelea hospitalini   bibi yake  na hata kuja  nyumbani kwa ajili ya kumpa faraja.

Lakini  baada ya  ujio wa Hamza na namna ambavyo alikuwa akiongea ilimpa nafasi  Regina ya kujua nia yake  halisi  ni ipi , alijua  yote aliofanya Yulia  ilikuwa kisingizio  tu cha kutaka kumuona Hamza.

Katika moyo wa Regina alianza kushikwa na hali ya kupaniki , hakujua ni kwanini  lakini  alikuwa  na wasiwasi Hamza anaweza kuwa na uhusiano wa ndani  kabisa na  Yulia.

Kama ingekuwa ni mwanamke mwingine pengine asingejisikia hivyo   lakini  Yulia , ukiachana na kwamba amemzidi kimwonekano  na yeye kuwa na umri mdogo ,lakini hakuwa  na kitu kingine  cha ziada cha kujivunia , kwa ufupi ni kwamba alikuwa akijihisi  amekutana  na mtu anaeweza kumletea ushindani , ndio hisia alizokuwa akijisikia muda huo.

Muda uleule Regina alikumbuka maneno ya bibi yake  akimuonya  juu ya kutoruhusu Hamza kuondoka kwenye maisha yake  na  kuhakikisha kumbakisha  hata kama ni kwa kumuigizia ,  maneno yale ni kama  sasa yametoka  kwa bibi yake na yanaanza kutafuta nafasi  katika   moyo wake na kujiambia  kwa vyovyote vile  hawezi  kumuacha Hamza kwenda kwingine.

Sasa Regina anaanza kuelewa  nini amabcho bibi yake alikuwa akilenga , kama Yulia alikuwa anafanya juhudi za namna hio kwa ajili ya  kumkaribia Hamza hata kwa kujifanyisha mkarimu  kwao  basi  ni mtu ambae  ana kitu.

Mrembo huyo ni kama alianza kuchanganyikiwa , hakujua kama  moyo wake ulikuwa ukitaka  Hamza  abaki kutokana na thamani ambayo  inaweza kuwa mchangao kwake au moyo wake na hisia zake ndio vilivyokuwa vikimtaka Hamza kubakia  upande wake.

Lakini  kwa muda huo hakutaka kujali ni hisia gani ilikuwa kweli na ipi  ni uongo,  maamuzi ni kwamba Hamza hapaswi kuondoka kwenye maisha yake anapaswa kummiliki hata isiwe  kimapenzi, kwanza tayari alikuwa na pete ya ukoo.

‘”Umekosea sisi sio marafiki  Yulia”Aliongea Regina  na kumfanya  Yulia kushangaa kidogo.

“Oh! , kama sio marafiki  ni bodigadi wako au Houseboy?”

Baada ya  Yulia kuuliza vile,  Regina alitoka kwenye Sofa na kusogea upande aliopo Hamza na kisha alipitisha mkono wake kwenye kiuno chake na kumwegamia.

“Hamza ni mume wangu”Aliongea.

Hamza alishitushwa na kauli hio  na kumwangalia  Regina kwa mshangao, ilikuwa ni mara ya kwanza  kusikia sauti  ya upole  na yenye heshima kutoka kwa Regina  ikionyesha  kweli walikuwa na mahusiano.

Sauti ya Regina ilifanya mapigo  yake kwenda  kwa kasi  mno huku damu za kutosha zikimwagwa na moyo wake kushangilia  kauli hio.

Regina   hata yeye uso wake ulikuwa umepata moto kidogo lakini hakuwa amemuachia Hamza, muda huo alikuwa akimwangalia Yulia  kwa namna  ya kujivunia kuwa na mume kama Hamza na kumpa ishara kwamba hana nafasi na amechelewa.

“Sikujua kabisa  kama CEO Regina ameolewa , kama ningejua  ile siku tulivyokuwa kwenye gari tusing.. tusinge..” baada ya kufikia hatua hio alijifanyisha kuziba mdomo  kama vile  anajutia kutamka kauli hio.

“Regina naomba unisamehe , sijui nataka kuongea nini, nilikuwa najaribu kumaanisha kitu kingine…”

Regina aliishia kumwangalia Hamza , alikuwa na hasira  ndani kwa ndani,huku akijiuliza inamanaa huyu mpuuzi tayari  ashafanya  kitu na  Yulia.

“Siwezi kufikiria chochote kibaya ,  kwanza namwamini  sana mume wangu , pia  naijua tabia yako  bosi Yulia”Aliongea Regina akimuwahi Hamza ambae alitaka kuanza kujitetea  lakini hata hivyo asingeongea kile ambacho alimfanyia Yulia kule Bagamoyo.

Regina pia alijua huo sio muda wa kuanza kugombana, vinginevyo angempa Yulia ushindi, hivyo aliendelea kukazia.

“Honey utakuwa umechoka na mihangaiko ya siku, nenda kaoge na upumzike, muda umeenda”Aliongea Regina kwa namna ya kupembeleza.

Hamza alijiambia kama maneno ya Regina yangetokea moyoni basi angekuwa anajisikia ni kama anaogelea angani.

Lakini kwa wakati huo kwasababu alikuwa akijua anaigiziwa alianza kukosa utulivu na alichotaka kufanya ni kuondoka ndani ya hilo eneo haraka.

“Sawa Wife natangulia kwenda chumbani” Aliongea Hamza maana muda huo alijihisi kama ni kama Refa kwenye uwanja wa vita.

Regina aliishia kutoa tabasamu la kumkubalia kama vile alikuwa ni   wanandoa wapya ambao wanatokea  kula fungate.

Baada ya Hamza kuondoka  ndani ya eneo hili hali ilirudi katika ukimya wake.

Yulia aliishia kushika shika nywele zale kimapozi ambazo siku hio hakuzisuka kama alivyozoeleka na kisha alisimama.

“Regina  muda wangu wa kuondoka umewadia ,  naamini hotochukulia vibaya kilichotokea kati yangu na Hamza.”

“Wala usijali , najua  hakuna kibaya kilichotokea , kwa cheo chako  Yulia   huwezi  kujikosea heshima mbele ya mume wa mtu”Aliongea Regina akiwa na macho makavu.

Na kauli yake ile ilimfanya Yulia kumkazia  Regina macho ,  muda huo ni kama wawili hao wanaonyeshana kwamba  hakuna ambae yupo tayari kukubali kushindwa bali  ni half time na raundi ya pili itaanza.

Yulia ndio aliekuwa wa kwanza kucheka kana kwamba kuna kitu ambacho amekumbuka.

“Regina , nadhani sasa naelewa  kwanini umeamua  kukubali kuolewa na Hamza, nikiri kwamba sikukujua vizuri  lakini  unaonekana  kutokuwa  mwanamke mwepesi”

Maneno yale yalimfanya Regina kidogo kuwa na wasiwasi lakini hakuuonyesha kwa macho.

“Asante  kwa sifa , ila  mimi najiona mwanamke wa kawaida tu ambae  ni  bosi kazini  na mke nyumbani , najijua vizuri kuliko mtu yoyote yule, ukiachana na kuchukulia kama mfanyabiashara  mzuri leo nimegundua upo vizuri pia  kwenye maeneo mengine, nipo tayari kujifuza kutoka kwako”

“Oh kama nini vile?” Aliuliza na kumfanya Regina kuwa kimya kwa sekunde kadhaa.

“Kwa mfano   Bosi Yulia unajua sana kuwa na shukrani kwa muda mrefu,nichukue nafasi hii kwa niaba ya mume wangu kukushukuru na  na kukuombea  siku  zijazo  usije  kuingia kwenye mtatizo  kama uliopitia”

“Nimefurahi  kusikia hivyo , kwasababu  Hamza  anaishi hapa  mjini  naamini siku za usoni  nitakapokuwa kwenye hatari  hatokataa kunisaidia, naamini pia  wakati huo Bosi Regina  hutokataa kuniazima mume wako, najua ni ombi dogo ambalo huwezi kukataa, si kweli?”

Regina alijikuta  akishindwa kujua namna hata ya kujibu , ilikuwani kama  Yulia anamwambia   muda sio  mrefu ataingia kwenye matatizo  na Hamza ndio mtu atakaekuja kumsaidia.

“Kuhusu hilo itategemea na tutakavyokubaliana na mume wangu”Aliongea Regina .

“Natanguliza shukrani  zangu za dhati kwako Bosi Regina”

“Huna haja ya kunishukuru.  Nadhani sina haja ya kukusindikiza, nakutakia Usiku Mwema” Aliongea Regina  na  Yulia alitoa tabasamu na kutoka nje.

Baada ya Regina kuhakikisha ameondoka na gari yake  kwanza alisita  kidogo lakini alirudi ndani na kupandisha mpaka  juu na kwenda moja kwa moja kwenye chumba cha Hamza.

Dakika ambayo alitaka kugonga Hamza alikuwa ameshafungua mlango na alimwangalia kwa tabasamu.

“Regi Babe ,  kumbe  una wasiwasi mno juu yangu , sikujua hapo kabla”Aliongea  Hamza.

Regina alitaka kukataa  lakini aliona   haitokuwa vizuri ,  aliamini kufanya hivyo ni kama kumwambia Hamza aende kwa Yulia kitu ambacho hakutaka kitokee, hivyo  haraka  haraka alibadilisha topiki.

“Kwannini jana hukurudi?”

“Ah.. jana nilikutana na rafiki yangu wa kitambo , hivyo tulitumia siku nzima kusherehekea  na kujikumbushia, sikukumbuka kukuambia , nadhani unajua  ni kwa muda mrefu  nimeishi peke yangu”

“Unaweza kuendelea na mazoea yako tu , isitoshe nina kazi nyingi za kufanya na   napata amani zaidi ukiwa haupo”Aliongea  na kumfanya Hamza kukamaa mwili baada ya kujihisi kumbe ni mzigo.

Muda huo  hakuna aliongea neno na kufanya hali kuwa kimya , Regina aliishia kumwemwesa lipsi zake , hakujua cha kuongea lakini kwenye moyo wake bado alikuwa na wasiwasi juu  ya  Yulia.

“Regina  bado una wasiwasi juu ya Yulia?”

“Nini kilichotokea kati yenu , haijawahi kutokea akajali kinachoendelea kwenye  familia yetu ,  unaonaje ukinipa maelezo”Aliongea

“Anachopenda ni kuniona nikipigana , sina mahusiano yoyote  nae, kwa mudu sasa  alikuwa akinibembeleza  niwe bodigadi wake , usimzingatie   Yulia ni mwanamke mjanja sana na  muda wote anapanga  kutega watu na hajawahi kuona hasara yoyote  ya kile anachokifanya hata kiwe kibaya ,ana  mawazo  juu ya vitu visivyowezekana hivyo usije kumruhushu akakuingia kichwani”

“Yulia familia yake anayotokea sio ya kawaida , ijapokuwa mpaka sasa hivi sijui kwanini familia yake imekuwa tishio sana  lakini  ni  ngumu mwanaume wa kawaida kukubalika ndani ya familia yake , usianze kucheza cheza huko  nje   na kusababisha matatizo maana sitokusaidia”Aliongea kwa kuonya huku akiweka  maneno ya  kumtishia kidogo  Hamza akitarajia ataogopa  lakini baada ya kumwangalia usoni  aligundua hakukuwa na wasiwasi wowote kutoka kwa Hamza

“Hii ni mara ya kwanza  kuwa hivi ,  kwahio siku hizi unajali  sasa ni mwanamke gani natoka nae , usiniambie  unaona wivu?”Aliongea Hamza na  Regina uso wake ulianza kuwa yai  na kujiambia  kwanini anapenda sana hizo topiki.

“Hamna .. siwezi kuwa na wivu nakutahadharisha tu… Ahhhh!.. unafanya nini”

Hamza  hakutaka hata kumsubiria Regina kumaliza kuongea  kwani alimshika kiuno  na kumbeba juu juu na kumwingiza ndani ya chumba chake.

Baada ya kumfikisha bila ya kumjali kama ni bosi wala  nani alimrushia kitandani na kisha kumpandia kwa juu  huku akiwa amemshika mikono  na  kumzuia kurusha miguu kwa kwa miguu yake.

Akiwa  ameinama walijikuta wakiangaliaana  kwa jiuu na chini  huku  pua  zao zikiwa zimepishana  sentimita chache.

Regina aliishia kuchezesha kope za macho yake  kwa haraka haraka akionekana  kutetemeka ,  alijua ilikuwa ngumu  kujichoropoa  hapo kwa kutumia nguvu  zake pekee.

Hamza aliishia kumwangalia  mrembo huyo na tabasamu lililojaa  nia ovu  na alimsogelea  sikioni na kumnong’oneza.

“Wife  ongea ukweli wako , una wivu mimi kuwa na wanawake wengine”

“Sio wivu, niachie”

“Usipokubali kuongea sikuachii”Aliendelea kupigilia msumari huku akicheka  kifedhuli akinusa  shingo  ya Regina.

“Wife umejipulizia  marashi sasa hivi ni nini , kwanini unanukia sana”Aliongea Hamza lakini Regina muda huo aliona yanakwenda kumshinda.

“Hamza niachie bwana… sipendi hivyo…”

“Usifanye chochote” Aliongea Hamza huku akimsogezea uso wake karibu kabisa kiasi cha pua zao kugusana.

Kitendo kile kilimfanya Regina kuwa mwekundu kama yai huku  macho yake akionekana kutaka kulia.

“Wewe endelea kunifanyia hivi.. nita.. nita …” Hakujua hata aongee nini.

“Unataka kuongea nini , unataka kusema utanikata mshahara , nikiendelea na ninachopanga kwa   usiku huu mmoja sitojali hata unikate mshahara”Aliongea.

“Usiku mmoja!!?”Aliongea huku   akili yake ni kama  ukichaa uliopotea unaanza  kumvaa.

“Unashangaa nini , sisi ni mume na mke kisheria , sidhani  litakuwa kosa  tukilala pamoja?”

“Kama tukiendelea nini kitatokea kati yetu?”Aliuliza.

Hakuelewa kwasababu alijua ndoa yao ni ya mkataba  tu , pengine   kwa kinachofanyika  muda huo alipaswa kukasirika lakini alijishangaa alishindwa kabisa  kushindana na Hamza.

Lakini muda huo ni kama  wazo  lilimwingia  na kujiuliza au nimsikilize bibi kile alichoniambia , aliamini ili  kuweza kumfanya Hamza kuwa upande wake kama bibi yake   alivyomwambia basi  anapaswa kulipa  gharama hata kama ilimaanisha kuutoa mwili wake.

Muda huo aliiona   jambo la msingi sio  swala la   hisia zake kwa Hamza wala mahusiano yao.

“Sipo  tayari kumuona Yulia akimchukua Hamza”Aliwaza mwanake huyo,kwa haraka haraka alipima faida  na hasra  na kuona hata kama ikitokea akifanya kwa mara ya kwanza na Hamza  isingeleta picha  mbaya   kwani  licha ya mkataba wao  lakini  kisheria ni mume na mke.

Baada ya kufikiria kwa haraka juu ya jambo hilo aliamua  kujilegeza na kuacha kushindana nguvu na Hamza na palepale alifumba macho yake kusubiria  chochote kila kitakachomkuta kama tu ndio njia pekee ya kumbakisha Hamza kwake.

Lakini licha  ya kusubiri  kwa dakika mbili zote  hakuweza kuhisi kitu chochote kinachoendelea   na kumfanya afumbue macho yake  na  alijikuta akimwangalia Hamza kwa mshangao.

Lakini muda huo Hamza alikuwa akimwangalia mrembo huyo na macho yaliojaa  upole.

“Wewe.. shida nini?”Aliongea Regina akionekana kushangazwa na  Hamza mbona haendelei.

“Kaoge  upumzike , naamini utakuwa umechoshwa na kazi”Aliongea Hamza huku akimwachia na kumfanya Regina  awe ni kama haamini kama Hamza amemuacha salama.

“Kwanini?”Aliuliza  kwa shauku , hakujua ni sababu gani ambazo zimemfanya Hamza kuishia njiani na alitaka kujua.

“Kwa kilichotokea   kule chini nishajua tayari  unanipenda  ila  unaona aibu ya kukubali, lakini bado unaonekana haupo tayari kwa hili   maana ghafla tu umegeuka kuwa  kama sanamu juu ya kitanda , hakuna ushirikiano wowote na  siwezi kufanya kitu ambacho haupo tayari kufanya”

Regina  aliona ilikuwa kweli maana  hata yeye hakujua moyo wake ulikuwa  katika upande upi kwa wakati huo , isitoshe hajawahi kupenda na hakujua kama hisia zake  ni za mapenzi  au ni hisia za kutotaka  kuwa mpweke.

Lakini hata hivyo alijikuta akijisikia vizuri  na kufanya damu  yake kuchemka, ilionekana Hamza alikuwa akijali hisia zake kuliko kitu chochote, maana kwa mwanamke mrembo kama yeye  mbele ya mwanaume katika mazingira kama hayo  asingekuwa salama hata kidogo.

“Basi naenda kulala , pumzika mapema  kesho jumatatu”Aliongea Regina  na kisha alitoka ndani ya chumba cha Hamza.

Baada ya  Regina kuondoka Hamza aliishia  kujilaza kwenye  kitanda kivivu  akionekana kama mtu ambae anaweza, ukweli  aliona alikuwa na safari ndefu kwa Regina , japo  mwanamke huyo alionyesha  hisia za wivu lakini haikumaanisha alikuwa  akimpenda moja kwa moja na  kujikabidhi kwake  kwa hiari.

Isitoshe pia  alijua  Regina  alikuwa mgonjwa na  bado hakuwa na uelewa  na  ugonjwa wake ulivyo maana hakumuuliza,   kutouliza sio kwamba hakutaka kujua  bali  aliamini  ni Regina mwenyewe ambae anaweza kuchukua jukumu hilo la kumwambia.

Lakini  kwa namna moja aliona  Yulia  ni mwanamke ambae  muda wote anamtafutia matatizo ,  maana kama sio hivyo asingekuja nyumbani kwake kutangaza vita, ilikuwa bahati tu Regina hakuwa mwanamke wa kawaida la sivyo  asingeweza kumshinda mwanamke mwenye hila nyingi kama Yulia.

Muda ambao Hamza anataka kuvua mavazi yake kwa ajili ya kwenda kuoga simu yake ilianza kuita na alishangaa  kidogo maana muda ulikuwa umeenda.

Baada ya kuangalia namba  inayompigia alishangaa kidogo maana ni  muda hawajawasiliana.

Alikuwa ni Irene mwanafunzi wa  Advance shule ya Alpha   ambae alikuwa akimfundisha tuwisheni  miezi kadhaa iliopita kabla ya kuacha,  Hamza alishangaa kwanini    msichana huyo anampigia ila hakutaka kujiuliza sana kwani alipokea palepale.

Kitendo cha Hamza kupokea simu tu  alichoweza kusikia ni sauti ya kilio  cha mwanamke.

“Irene kuna nini!?”Aliuliza Hamza kwa mshangao.

“Hamza where are you ? ,  I feel so  terrible …”Sauti ya   kike ilisikika  huku ikiambatana na kilio.

“Nipo nyumbani , nini kinakufanya ulie?”Aliuliza  Hamza  huku akijaribu kumsikiliza kama msichana huyo anamtega kama siku zote.

“Sina pakulala…, Sina pakwenda Hamza”Aliongea na kumfanya Hamza kushangaa.

“Hebu nyamaza kwanza  uniambie nini kimetokea , kwanini unasema huna pakulala wakati  una nyumbani kwenu”

“Baba kamfukuza  mama  na mimi  anasema  hataki kuniona pia..”Aliongea  mrembo huyo na kumfanya Hamza kufikiria kidogo.

Ukweli ni kwamba tokea aanze kwenda nyumbanni kwa Mama Irene hakuwahi kukutana na baba yake  Irene hata siku moja ila hakuwahi kuuliza pia.

Hamza alijua pangine ni  mgogoro ya kindoa imeibuka, lakini bado hakumuamini Irene moja  kwa moja  , lakini hakutaka kupotezea pia, aliishia kujikuna kichwa huku aking’ata meno kwa uchungu wa  kuharibiwa  ratiba yake ya usingizi.

“Niambie uko wapi?”

“Nipo  Masaki Karnitas  Restaurant  mkabala na CCBRT  hospital’Aliongea na kumfanya Hamza kuanza kukuna kichwa tena  maana kutoka Kigamboni mpaka  Masaki ilikuwa mbali japo si mbali sana kwa usafiri binafsi.

“Kaa hapo hapo usiondoke nakuja” Aliongea  Hamza na kisha  hakujali kubadilisha tena mavazi alishuka mpaka chini  na  aliona akienda  na usafiri wa uma angechelewa hivyo  aliiba ufunguo wa  Maybach  ya Regina  na kisha kuliwasha na kuondoka .

Muda  huo na mvua haikuweleka imetokea wapi ghafla lakini ilianza kunyesha mfululizo.

Hamza  alichukua maamuzi ya kwenda kwasababu ya  Mama Irene  , kipindi ambacho  anaanza kumfundisha  Irene   alitendewa  wema sana na mama huyo ikiwemo kumlipa hela kubwa  tena hata kabla ya  muda na hata kuacha kwake kazi  ya kumfundisha  Irene ni kwasababu ya heshima aliokuwa amejenga kwa  mama yake , alijua msichana huyo alikuwa akimtega  kimapenzi  na hakutaka kumgusa kutokana na  kuaminiwa na  mama huyo.

Ilikuwa usiku wa saa   tatu  hivyo  hakukuwa na foleni kubwa  na ndani ya nusu saa tu aliweza  kufika  Masaki  na kwa kutumia  GPS aliweza kuufikia mgahawa wa Karnitas na kusimamisha  gari pembeni.

Kulikuwa na mvua na Hamza hakutaka kushuka kwenye gari hivyo alimpigia simu na kumwambia atoke aingie kwenye gari.

Zilipita  kama sekunde kadhaa Hamza aliweza kumuona msichana akitoka nje ya mgahawa ule , kulikuwa na magari kadhaa kando kando ya barabara ikiweo gari yake.

Irene alikuwa mwanamke mrembo mno , pengine kutokana na uzuri wa mwanamke huyo ndio maana Hamza aliachaga kumfundisha maana alijua asingewea kuhimili mitego yake.

Hamza alimwangalia tu namna anavyohangaika  na kujiuliza kuna wazee ni wakatili  wanafukuzaje mtoto wa kike  nyumbani usiku usiku tena mzuri  namna hio , si ni  kama kumwambia  aende akajiuze.

Hamza mara baada ya kuona  Irene anashangaa shangaa ilimbidi kupiga honi huku akiwasha taa za gari   na kufungua kioo upande wa dereva akimpungia mkono.

Mrembo huyo mara baada ya kuangalia gari aliokuja nayo Hamza ni kama alishikwa  na mshangao ,  ilikuwa  ni usiku lakini  gari  aina ya  Mercedenz Benz Maybach  ni chache sana barabarani  kwa  Tanzania na pengine hakuna kabisa hivyo mtu yoyote angeijua.

“Unashangaa nini unanyeshewa na mvua , ingia kwenye  gari?”Aliongea Hamza , alijua kwanini  msichana huyo alikuwa akishangaa  , isitoshe  tokea aache kwenda kwao  maisha yake ni kama yamebadilika.

Irene mara baada ya kurudi katika hali yake ya kawaida hakuongea  kingine na aliingia   kwenye   gari huku akiliita jina la Hamza  kana kwamba hakutegemea angekuja  na kumkumbatia  kwenye shingo  huku  akianza kulia kwenye kifua chake.

Na Hamza alivyomshika  nguo zake aligundua alikuwa ameloa  karibia nguo zote, ilionekana alikimbia kwao  mvua ikiwa inanyesha.

“Irene tulia , nipo hapa kwa ajili ya kukurudisha nyumbani kwenu na si vinginevyo”Aliongea Hamza.

“Siendi nyumbani nyumbani hata kwa fimbo , baba  hataki  kabisa kuniona”

“Irene acha utoto ujue , mama yako alishawahi kuniambia  ulitoroka nyumbani na kwenda kuishi Mwenge  wewe kisa ulifokewa”Aliongea Hamza.

“Sitaki kwenda nyumbani wala kwa ndugu  yoyote , haiwezekani  makosa ya  mama  anibebeshe mimi kwa kuniita Mal*ya”Aliongea na kuanza kulia upya.

“Nini  kimetokea !?”

“Mimi sijui ila  Baba nimesikia akisema   mama anamsaliti na jirani yetu ambae ni msanii wa Bongo Movie…Hamza sitaki kuzungumzia hili  please naomba unipeleke unapoishi , sitaki kurudi nyumbani..”

Hamza mara baada ya kusikia  ombi  hilo  hakutaka  kuvuta picha muonekano wa Regina utakavyo  kuwa , licha ya  Irene kuwa  mwanafunzi tu wa High School  lakini   asingekubali kirahisi wakae nyumba moja.

“Nyumbani  ninapoishi hapana.. nitakupeleka   hotelini”Aliongea.

“Hotelini!?”Aliuliza  kwa mshangao  na  Hamza alitingisha kichwa akiwa siriasi huku akigeuza gari.

“Okey , nipo tayari kwenda popote , ili mradi isiwe nyumbani”Aliongea  na Hamza alikubali  na  kuondoa gari.

“Nitakupeleka  hoteli za karibu , shule unaendaje bila  sare?”

“Tupo likizo, twende hoteli ya mbali’Aliongea na Hamza upande wake  hakutaka kumwitikia kwa kila anachoongea ila alishachagua hoteli ya kumpeleka.

Dakika chache Hamza  alikuwa ameshamfikisha  Dosam V hoteli, hoteli ambayo ndio  kwa mara ya kwanza alikutana  na Regina , hoteli hio alikuwa pia akijua  ni  mali ya kampuni ya Dosam.

Baada ya kwenda mapokezi  Hamza alitoa  kadi yake ya benki, alikuwa na kitita cha kutosha alichopata katika mashindano ya  Baskatball hivyo  kwake kulipia chumba kwenye hoteli ya hadhi kama hio halikuwa  tatizo.

Wakati Hamza anatoka  mapokezi  ndani ya hilo eneo  kama angeongeza umakini angegundua kuna mtu aliekuwa akimfahamu alikuwa akimwangalia kwa macho ya mshangao na shauku.

Mtu huyo alikuwa  ni  mwanafunzi mwenzake , msichana ambae alimkataa baada ya kuziweka hisia zake hadharani  kwenye kadamnasi ya watu, alikuwa ni Anitha  na alitaka kunyanyuka kumkimbilia  lakini  alisita kufanya hivyo mara baada ya kumuona Chriss anasogelea eneo hilo.

Ki ufupi ni kwamba Chriss na  Anitha walionekana kuwa wapenzi na wapo eneo hilo kula bata  pamoja , Hamza angegeuza  uso wake Chirss angemuona.

“Mbona umekodolea macho upande ule , kuna nini?”Aliuliza Chriss huku akiangalia  upande ambao  Anitha alikuwa akiangalia  lakini aliishia kuona  mgongo wa mwanaume  ukitokomea kwenye lift na hakuweza kumtambua kama ni Hamza.

“Hakuna tu , kuna mtu  nilidhani nilimfanananisha”Aliongea  Anitha huku akijitahidi kulazimisha tabasamu.

“Huyu  Hamza kwanini ajitokeze sasa  hivi , ashanipotezea mudi tayari”Ndio kitu ambacho alikuwa akiwaza huku kwa namna moja akishangaa pia.

Ijapokuwa hakuwa mshamba wa  kuingia hoteli za hadhi ya juu kama hizo lakini  kwa Hamza ambae alimjua  chuoni kama masikini  sio mtu wa kuingia kirahisi na kulipia  hapo tena akiwa na mwanamke mrembo na mbichi kuliko yeye.

Ndio Irene alikuwa mrembo kuliko Anitha na alionekana mbichi mno  kuliko yeye ambae ashaanza kuvaa sidiria.

“Nenda kaoge sasa, nishamwambia  mhudumu akusaidie upate nguo zingine za kubadilisha”Aliongea Hamza mara baada ya kuingia ndani ya  chumba.

“Sawa”Aliongea Irene huku akimwagalia Hamza  kwa macho ya kusita sita

“Lakini si  huondoki , unalala hapa hapa?”Aliuliza.

Hamza alitaka  kusema  kwamba anaondoka  lakini muonekano wa kutia huruma wa Irene ulimfanya aone pengine kubakia inaweza kuwa  vizuri zaidi   na asubuhi  ampeleke  kwao.

“Nipo usiwe na wasiwasi”

Baada ya kuongea   kauli hio  Irene ni kama  alipatwa na uhakika wa jambo flani  na kimya kimya aliingia bafuni na kumuacha Hamza akiwa amekaa kwenye kiti na kutoa simu yake ili kufanya mawasiliano.

Mpango wake ulikuwa ni kumpigia mama yake  Irene ili  kumpa taarifa alikuwa na mtoto wake ili asije kujibebesha kesi ambayo haimuhusu.

Hamza mara baada ya kupiga simu   kwa bahati nzuri ilipokelewa na alimweleza Mama Irene juu ya binti yake na Mama huyo alionekana kushangaa sana huku  akimlaumu  mume wake  kwa kusema hata kama alikuwa na hasira na yeye asingezitolea  kwa Irene, aliishia kumshukuru mno Hamza.

Mama Irene alimwambia Hamza atawasiliana na  shemeji yake yaani mdogo wake mume wake ili ikiwezekana asubuhi amchukue[DI1]   Irene  kwenda nyumbani kwake kwani yeye yupo Morogoro.

Muda huo alivyokata simu mlango wa chumba chao uligongwa na mhudumu alifika akiwa  na nguo  za aina tofauti ikiwemo za ndani na nje  na Hamza alitingisha kichwa kuridhika na alipokea na kwenda kuweka  kwenye mlango wa bafuni.

“Irene nguo   nimekuwekea mlangoni  vaa ukimaliza”Aliongea Hamza  na Irene aliitikia  na kumfana Hamza kurudi kwenye sofa  na kuegamia.

Lakini  dakika mbili mbele  Irene  alitoka bafuni  akiwa hana nguo hata moja mwilini  na kuja kusimama mbele ya Hamza, kitendo cha kunyanyua kichwa  na kumuona hana alichovaa alijikuta akishangaa  mno.

“Wewe unafanya nini?!”Aliuliza  Hamza  maana hakuelewa  au hakutaka kuelewa na Irene muda huo alikuwa na aibu za kike ziliozoambatana na ujasiri,

“Ni.. nipo tayari”

“Upo  tayari kwa ajili ya nini?”

“Inamaana huelewi , kwanini unaniuliza Hamza wakati wewe ni mwanaume”Aliongea  na sasa Hamza alielewa kilichokuwa kikiendelea.

Kwa picha iliokuwa ikiendelea pengine Hamza angemrukia Irene na kufanya nae , ijapokuwa aliona kakomaa lakini  hakuwa mwepesi hivyo kufanya  mapenzi na mwanamke kisa tu amemkalia uchi  mbele yake , kama ni hivyo angekuwa ashafanya mara kibao na  Dina ambae  usiku wa jana alilala nae akiwa nusu uchi.

“Kwahio ulidhani nimekuleta hotelini kwa ajili ya  kufanya mapenzi?”

“Kama sio  hivyo   maana yake nini?”Aliongea.

Haikuwa mara yake ya kwanza kwa Irene kumkukalia uchi  kama hivyo ,  wakati anamfunndisha ilikuwa  hivyo hivyo kutegwa.

Muda huo  hakujua alie ama acheke maana aliona ni kama  msichana huyo bado hajabadilika na pengine hata kupiga simu  na kutokwenda kwa ndugu  hio ndio sababu.

“Hey! Nimekuja kukusaidia na sijafikiria mbali hivyo , au  kwenye macho yako unadhani mimi ni mnyama  nitakupalamia tu bila kufikiria, Irene nadhani nishakuelekeza  mara nyingi juu ya hili”

“Lakini kipindi kile ulikuwa ukikataa kwasababu  ni nyumbani na leo tupo wenyewe   tu  na umesema huondoki na kitanda  ni kimoja… au nimekuelewa vibaya?”Aliongea  na Hamza  hakutaka kumwangalia zaidi akiwa uchi mbele yake na alienda  bafuni na kuchukua zile nguo na kumpatia.

“Vaa kwanza nguo zako  na acha kufikiria ujinga , nishakwambia soma kwanza  umalize  ndio mambo mengine yaendelee , kwanini huelewi tu?”Aliongea  Hamza  na kauli ile ilimfanya  Irene machozi kuanza kujitengeneza kwenye mboni za macho yake  alihisi ni kama anaonewa ilihali anajiona mtu mzima.

“Kama hutaki ungesema  mapema , nimekuonyesha kila kitu kwnaini unanikataa?”

“Irene ukiendelea na ujinga wako nitakuacha ulale mwenyewe?”

“Wewe sema tu uvumilivu unaanza kukushinda  kwa kuniona hivi?”

“Ni mara ya ngapi hii unanionesha. hebu nenda kavae nguo huko”Aliongea Hamza akiwa siriasi na kumfanya Irene  kwa hasira kwenda kuvaa nguo  na ndani ya dakika chache tu aliweza kurudi huku akiwa mwekundu , alikuwa mweupe kama mama yake.

“Nishaongea na mama yako,Uncle wako  kesho asubuhi  atakuja kukuchukua”Aliongea Hamza na Irene alimwangalia tu bila kuongea chochote, licha ya kukataliwa  na Hamza   bado hakukata tamaa.

“Sasa si uande kitandani  au unataka kukesha kwenye hilo sofa?”

“Wewe huogopi naweza kugeuka Simba na kukurarua”Alitania Hamza.

‘Kama ningekuwa naogopa ningetoka uchi bafuni na kukuonyesha kila  kitu?””

“Unaonekana bado upo bikra , kwannini unataka  kupoteza ulichotunza kihasara hasara namna hio?”

“Kama Baba  yangu Mzazi   ananiita Kahaba  na kunifukuza nyumbani kwanini  nijali , si bora  nikutafute wewe ambae  naweza kukutegemea, Hamza nipo tayari kukupa chochote sio kwasababu mimi ni Ma*ya nakupenda  ndio maana…”

“Sijasema wewe  ni M*laya na hata baba yako hajamaanisha pengine ni hasira tu”Aliongea .

“Baba ana hasira kweli ,  kamfumania  mama  mara mbili  na yule Mgosi, ila mara zote amesamehewa”Aliongea na kumfanya  Hamza kushangaa  kidogo ukweli hakuwahi kudhania Mama Irene anaweza kuchepuka , lakini hata hivyo alikuwa mwanamke  haswa  na bado hajazeeka ilikuwa sahihi kupata  vishawishi , kingine  kwa  muda wote ambao alifundisha nyumbani kwake  hakumuona mume wake ikimaanisha  alikuwa mpweke kwa muda mrefu.

“Baba yako anafanya kazi gani?” Aliuliza Hamza.

“Baba  anafanya kazi kitengo cha usalama wa  Taifa , wakati ule unaanza kuja kwetu alikuwa Jamhuri ya Czech  kikazi , sasa hivi amerudishwa  Ikulu”Aliongea na kumfanya Hamza kuona ndio maana  kagongewa,hakuna kazi  ambazo zinawafanya wanaume kuwa bize kama za vitengo vya usalama.

“Hamza kama  nikikupa bikra yangu siku moja si hautoniacha?”

“Nishakuambia ukiendelea kuongea ujinga  nitaondoka”

“Unajifanyisha hunipendi lakini umekuja nilivyokupigia simu?”

“Nimekuja kwasababu wewe ni mwanafunzi wangu  hakuna sababu nyingine ,  kama  unataka kunitunuku maliza Form Six  kwanza na faulu kwenda chuo  nitakufikiria upya

“Jamani mpaka nimalize  Form Six, mimi ni mtu mzima tayari , nina marafiki wana wanaume hadi watatu watatu  halafu wewe unanina mtoto,unanikasirisha”

“Wewe ni mtoto kwa macho yangu , hebu  lala huko?”Aliongea.

Hamza hakuwa na mpango wa  kulala kitanda kimoja na  Irene alimjua hashindwi  kuamka usiku  na  kumkuta yupo bize na kiungo chake hivyo alijiegamiza kwenye sofa kuutafuta usingizi.

Asubuhi  ilipoingia kilichomtoa Hamza  usingizini  ni mlango wa chumba  kugongwa kwa nguvu na  ilimfanya Hamza kushituka haraka haraka  na kwenda kuufungua na  mtu wa kwanza kumuona alikuwa ni mhudumu wa kike  nyuma yake  kukiwa na mwanaume mrefu mweusi alievalia suti na alivyomuona ni kama alionyesha hali ya kushangaa  kidogo.

“Irene yupo wapi?”Aliongea

“Kaka samahani , huyu baba anamtafuta  binti yake  na tumeshindwa kumzuia , tunaomba radhi..”Aliongea  akianza kujitetea ila Hamza alimpa ishara asiwe na wasiwasi na anaweza kuondoka.

 [DI1]

Previoua Next