Reader Settings

Baada ya wote kumwangalia Afande Mdudu  na Mshauri  pia alimwangalia  Mdudu akionekana anahitaji maelezo na kumfanya afande huyo sura yake kuzidi kuwa nyeusi.

“Afande   naripoti kwako.. mimi ndio nimemkamata”

Afande Mdudu hakuona haja ya kujificha  muda huo   hivyo aliamua kuuvaa ujasiri na kusogea mbele.

Ukweli ni kwamba hata alipoomba  ruhusa kwa mkuu wake  wa misheni  Afande Msuya alipewa maelekezo  ikitokea  ameshindwa kumkamata Hamza basi   ajisalimishe kama  alichukua maamuzi peke yake , ijapokuwa ilikuwa kweli Msuya alikuwa akitaka kumkamata Hamza lakini alipingana na wazo hilo kwa kuhofia  kile ambacho anaweza  kufanya lakini  Mdudu alilazimisha.

“Afande nimemkata kwasababu mpaka sasa ameua watu wengi , tulikuwa na wasiwasi ataende…”

“Haina haja ya kuendelea kuongea”Aliongea Afande Himidu akimkatishia njiani .

"Mdudu   kama niko sawa wewe ni mtoto wa pili wa 

Mkuu wa Majeshi aliepita  Afande Mbwana?”

“Ndio afande  , babu yangu pia ni waziri mkuu mstaafu”Aliongea kwa kujiamini.

“Huna haja ya kuendelea kuelezea vyeo  vya wanafamilia yako ,  japo ni kweli familia unayotokea ni ya watu maarufu lakini  haitoshi katika hali kama hii”Aliongea  na kumfanya Afande Mdudu kuonyesha hali ya kuchanganyikiwa.

Ukweli  alikuwa akijiamini katika sehemu nyingi , sifa za jina la familia yake lilikuwa likimtangulia katika  maeneo mengi , sasa alijiuliza inakuwaje  jina lake hapo lisitoshe au  Afande anajaribu kuongea kitu gani.

       

“Afande umeulizia kuhusu familia yangu , hili swala lina uhusiano?”Aliuliza.

“Unaweza kufikiria unachoweza  , ila  itakuwa vizuri kama ukiongea na   baba yako  kwanza umwelezee kilichotokea leo, pengine inaweza kukusaidia”Aliiongea lakini kauli yake ilizidi kumchanganya Mdudu kwani hakuwa akijua ni  kitu gani  amekosea..

Hata upande wa Afande Wazo na Maningi hawakuelewa Mshauri anachojaribu kumaanisha.

“Acha kuonyesha  dalili za kuchanganyikiwa , ninachomaanisha hapa fanya kila namna kuokoa maisha ako”Aliiongea.

“Lakini Afande baso sielewi , sijui kama kuna kosa lolote nimefanya kiasi cha kutaka kunipa adhabu”

“Una uwezo mdogo wa kufikiria   na sijui aliekupatia uongozi wa hii kesi alikuwa akilenga nini , ninachomaanisha  yule mtu akitoka unaweza usiwe salama  na  akiamua kukuua  sitoweza kumzuia”Aliongea na mara baada ya kusikia maelezo hayo alijikuta akitetemeka.

“Lakini Afande huyu si mfungwa , kwani tunamuachia atoke?”

“Afande anachoongea  ni sahihi , sidhani kuna haja ya kumuachia huru , ana siri  juu ya kitu kinachoitwa Ankh  na  inaonekana ni siri ya thamani kubwa  mno inayofuatiliwa na watu wengi kiasi cha kuhatarisha usalama wa  nchi”

“Ndio  Afande Hamza yupo pale  na hakuna namna anaweza kutoka  kwa hiari yake labda tumuachie  bila ya kujali uhalifu  wake”Alikazia  Afande  Mdudu.

Lakini  Afande Himidu hakuwa akiwasikiliza kwa maneno yao, macho yake yalikuwa yamemkazia Hamza ambae alikuwa ashasimama tayari na kusogelea kioo huku akijivuta.

Japo   kwa  ndani ya chumba hicho ilikuwa ngumu kuona anaengalia nyuma ya kioo lakini  muda ule ni kama Hamza alikuwa akiangaliana na  Afande Himidu kwani alitoa tabasamu  la ishara ya salamu na kumfanya hata Afande Himidu kutabasamu pia, huku macho yake yakionyesha ishara  ya heshima  kwa Hamza.

“Hebu fanyeni haraka  , mfungulieni atoke”Aliongea  kwa sauti  kubwa iliojaa ubabe.

Kundi hilo  la wanajeshi waliishia kusita kupokea maagizo hayo , hawakujua  wamuachie Hamza au  wasimauchie , isitoshe  kwao walimuona kama mhalifu na Mshauri anataka kuvunja sheria.

Lakini sasa kilichotokea  baada ya hapo kiliwafanya  kuganda kama vile wamegeuka mawe ya barafu.

Hamza alikuwa akipiga piga  kuta za  eneo  hilo  la ndani kana kwamba anajaribu kuona ni wapi  kuna udhaifu  na uimara, baada  ya kuonyesha kuridhika  na kugonga gonga  alisogelea kioo na kuweka kiganja cha mkono huku akionekana kufumba macho.

“Anajaribu kufanya nini , au amepatwa na uchizi wa ghafla?”Mmoja aliongea  kwasababu  waliamini kioo alichoshika Hamza kilikuwa ni  kioo kigumu mno ambacho ni kipana   kiasi kwamba hakiwezi kupitisha risasi wala   kupasuka kwasababbu ya mlipuko.

Afande Maningi palepale wasiwasi ulimwingia na alibonyeza kitufe ambacho kinasafirisha sauti.

“Mr  Hamza   tunakuomba  utulie tutakuachia muda si mrefu”Aliongea , alijua kama kweli Hamza anafahamiana na  Afande  Himidu basi kuna uwezekano asiwe wa kawaida.

Isitoshe walikuwa ni wanajeshi wa kitengo cha kupambana na nguvu za ziada na kupitia  uzoefu na  stori nyingi walizosikia juu ya mafunzo mbalimbali ya maajabu walipatwa na hisia za hatari wakiamini Hamza anaweza kuwa na hayo mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi.

Hamza aliendelea kushikilia kile kioo kwa nguvu  na alioekana kama mtu ambae  anasali kwani  midomo ilikuwa ikicheza kwa kuongea  na  kabla hata  wale wanajeshi hawajachukua hatua ya kumfungulia eneo hilo   lilianza kutetemeka kama vile ni mtikisiko wa ardhi.

Kitu kile kiliwafanya watoe macho washindwe kujua nini kinakwenda kutokea. 

Wakati wakishangaa  ghafla ule mtikisiko ulipotea   lakini Hamza bado alikuwa  ameshikilia kile kioo huku akiwa amefumba macho na kuendelea kuongea maneno.

Ghafla  tu  macho yaliwatoka mara baada ya  kile kioo walichoamini hakiwezi kupasuka hata kwa nyundo kikianza kutengeneza  nyufa taratibu kana kwamba kinapata kiwango cha juu cha moto ,hazikupita sekunde  kumi kioo chote kama vile  ni glasi imedondoshwa  chini kwani kilipasuka vipande vipande.

Bahati ni kwamba   kioo hakikuwa kimoja pekee kulikuwa  na layers angalau  tatu za vioo  vinavyofanana.

“Afande wazo  si umesema hivi  vioo haviwezi kupasuka hata kama vipigwe na bomu?”Aliuliza Afande Mdudu  huku akitetemeka. “Inawezekana vipi  kupasua kioo bila ya kutumia nguvu?”Afande Wazo aliekuwa kwenye bumbuwazi.

Ilikuwa ngumu   kukubali maana walitumia kiasi

kingi cha pesa kwa ajili ya ujenzi wa hilo eneo , lakini namna ambavyo Hamza alikuwa akividondosha  sio uwezo wa kawaida.

Hamza kabla hajafikia kioo cha mwisho  Afande Wazo alishikwa na hasira , alitaka kujihakikishia kama ni kweli vioo hivyo vilikuwa vigumu au kuna tatizo , hivyo mara baada ya kushika  bunduki alianza kuvimiminia risasi. Lakini hakuna risasi hata moja  ilioacha hata ufa   kwani zilidunda  tu na kudondoka chini.

“Hakuna haja ya kufanya majairibio ,  hakuna tatizo   kabisa na ujenzi  wa hili eneo, Shida ni kwamba   ana uwezo  mkubwa mno na wa ajabu”Aliongea Afande Himidu huku macho yake ni kama  amefurahi kuona  tukio kama hilo.

Hatimae vioo vyote vilipasuka chini bila ya kupigwa ngumi  zaidi ya kuwekewa kiganja  cha mkono tu. “Kuna mwenye sigara kati yenu?”Aliuliza Hamza mara baada ya kutoka  nje lakini kila mtu alikuwa amemkodolea  macho kana kwamba wameona mnyama.

“Mnashangaa nini sasa ,  au hamhawahi kuona  kioo kikipasuka?”Aliongea Hamza na  Afande Himidu ndio aliekuwa  wa kwanza kushituka.

‘”Inamaana hamjamsikia , hakuna mwenye sigara  kati yenu?”Aiuliza na Afande Wazo kwa kutetemeka aliingiza  mkono kwenye mfuko wake wa kombati na kuchomoka na sigara na kibiriti.

Upande wa Afande Himidu hakushangaa Hamza kuhitaji sigara , kwa mtu wa  kawaida anaweza kuona Hamza hakutumia  nguvu  kupasua vioo hivyo lakini kwa uelewa wake alijua Hamza ametumia nguvu nyingi tu  japo sio zote, kutengeneza resonance pacha  kwenye kitu kigumu kama hicho haikuhitaji  tu nguvu lakini matumizi makubwa ya ubongo ili kupatia hivyo hufanya akili  kupata hali  ambayo inaweza kuondolewa na sigara au kilevi.

“Kijana naona una mabadiliko makubwa mno , umepata mke nini?”Aliongea Hamza akimshika  bega Afande Himidu huku wakiwa na tabasamu .

Kwa namna ambavyo Hamza alianzisha mazunguzo na afande wa heshima kama huyo iliwafanya  Mdudu na wenzake kuzidi kushikwa na wasiwasi.

“Kama ningekuwa nimeshaoa  wewe ungekuwa wa kwanza kujua , yaani nifunge ndoa  bila ya kukualika   mlevi kama wewe”Aliongea Afande  Himidu huku akicheka,

“Haha……utaachaje kunialika na  unavyopenda  vitu   vya mteremko , sidhani bila kutoa mchangao wangu utataka kuoa wewe”Aliongea na kumfanya Afande Himidu kujikuta akicheka mpaka  mabega  yanamtingishika.

Muda huo Hamza akipata muda wa  kuangalia watu waliokuwa ndani ya eneo hilo na aliweza kuona kila mtu alikuwa akimwangalia kwa wasiwasi.

“Nyie  watu haina haja  ya kujenga  upya  hivyo vioo , ni kujitia hasara tu”Aliongea Hamza  huku akiwa na tabasamu la kejeli  lakini  Afande  Wazo na Afande Maningi walikuwa na wasiwasi mno.

“Ndio  Afande tumekuelewa” Aliongea  Afande

Maningi huku hana uhakika kama   kumuita   Hamza  afande ni sawa , alijaribu kubahatisha   kwa namna yoyote  ile ili  kumtuliza asichukue hatua.

Muda ule Hamza macho yake yalitua  kwa  Afande Mdudu ambae alikuwa akijificha ficha kana kwamba anatamani kuikimbia hilo eneo.

“Afande Mdudu unajua  umefanya kosa  gani  leo?”Aliongea Hamza na Afande Mdudu alijikuta akitetemeka  kwa hofu.

“Sikupaswa kukukamata  .. naomba msamaha wako”Aliongea  

“Kunikamata halikuwa kosa kwasababu ulikuwa ukifuata  sheria  na   ulikuwa na ushahidi , mtu kushurutisha  watu kutii sheria sio kosa hata kidogo”

“Basi kosa langu itakuwa ni

kutokukuheshimu?”Aliongea  huku aking’ata meno kwa hasira , mpaka dakika hio ameshindwa kujua kabisa Hamza ni mtu wa aina gani mbona anatisha.

“Mimi  sio mtu wa kukasirika kwa   vitu vidogo  vidogo kama hivyo , hata  mimi nisingekuongelesha kwa upole, kosa lako kubwa  ni ni kujaribu kunitengenezea udhaifu  mbele ya mwanamke  huku  ukiwa na uhakika  mimi ni  mhalifu, umeshindwa kunikamata nikiwa  Kijichi na kuniwekewa mtego  njiani, mpango wako haukuwa kunikamata ila kujaribu   kunidhalilisha”Aliongea Hamza huku akionyesha  hali ya  ukauzu na swala lile lilimfanya Afande Himidu kuingiwa na wasiwasi.

“Ni mtoto wa pili wa mkuu wa majeshi Afande Mbwana, babu yake pia alishawahi kuwa  Waziri mkuu”Aliongea.

“Nishayajua hayo yote tokea muda tu ,  lakini kuwa  mtoto wa nani haimaanishi  ndio tiketi ya  kuachwa afanye atakavvo”

“Unapanga kumuua?” Aliuliza. Afande  Himidu akiwa na wasiwasi  na Afande Mdudu  kwa woga alipiga magoti mbele ya Hamza.

“Hamza naomba unisamehe  , nilikosea kweli”Aliongea   lakini Hamza  ni kama hakuwa  hata na hio hasira ya kumuua kama alivyoulizwa , alitaka kumtishia kidogo  tu.

“Nikikuua mtu kama wewe  nitaonekana kama  mtu ambae naonea  dhaifu, onyo langu  kwako  usije kumsumbua  Yonesi  tena”Aliongea Hamza na mara baada ya Mdudu kusikia kauli hio alijikuta akipatwa na ahueni   huku akijiambia   kwa muda huo ataacha kumsumbua  Yonesi lakinin sio kama atamwacha kabisa.

“Asante sana Hamza” Aliongea  huku  akijifuta , licha ya kwamba  alikuwa mwanajeshi lakini ukweli ni kwamba alilelewa kimayai sana kutokana na  utajiri wa familia yao hivyo kumfanya kuwa mjivuni  sana.

Sababu ya Hamza pia kutomfanya kitu chochote 

Afande Mdudu  ni  kwa ajili ya  Afande  Himidu,   alikuwa  ni rafiki yake hivyo hakutaka kumuingiza  kwenye matatizo.

“Mnaweza kutoka nje sasa ,   nataka kuongea na  Hamza, hakuna anaeruhusiwa kusogelea hapa”Aliongea   Afande Himidu mara baada ya hali kutulia.

Wote baada ya kutoka  nje  Afande Himidu  ghafla tu  alipiga  goti kwa mguu mmoja huku akiongea  kwa  unyenyekevu

“My Prince!!”

“Inatosha  Bro , kwanini unafanya hivi kama  watu wengine bwana , hatujaonana kwa zaidi  ya miaka sita   lakini naona bado  hujasahau  hizi  itifaki, nakumbuka kipindi kile   ukiwa kambini ulikuwa  mjeuri mno lakini baada ya kuimarika ukawa humble”Aliongea Hamza.

“Hakuna mtu yoyote ndani ya  Tanzania hii  naweza kumpigia magoti , hata awe raisi , kwangu  hii ni ishara ya kukuheshimu kama  mwalimu wangu na bosi wangu”Aliongea Afande Himidu huku akiwa na tabasamu.

“Haha. Vizuri , lakini  naona sasa hivi unaitwa Himidu Mshauri , jina lako la Murphy Stopphilius umelitelekeza , huwa na kukubali sana maana hubadiliki sio kama rafiki yako Mameni”Aliongea  Hamza.

Kitu ambacho  hawakukijua   wakina  Afande Wazo na wenzake ni kwamba Murphy halikuwa jina  la Hamza bali  ni  la  Afande Himidu.

“Ukweli   miaka miwili iliopita niliposikia  umestaafu  mwanzoni sikuwaza ni wapi  utaenda , lakini  nikikumbuka kipindi kile ulivyokuwa ukinisumbua  kufahamu  kiswahili nilijua tu lazima  utakuwa hapa nchini  na hisia zangu zilikuwa  kweli ,  nimefurahi kukuona sana  bosi”Aliongea.

“Mwaka wa kwanza wakati nafika hapa  nchini nilikuwa nikijiuliza nikutafute au  nipotezee , isitoshe  kati ya marafiki zangu wote wewe ndio ulikuwa mtanzania pekee, lakini  mara baada ya  kupata taarifa  umejipenyeza kwenye jeshi la Tanzania  niliona nisikusumbue  , isitoshe mpango wangu  ulikuwa ni kuishi maisha ya chini chini” “Bosi hata usiwe na wasiwasi  naelewa..”Aliongea  huku akimwangalia Hamza kwa namna ya kumchunguza..

“Lakini bosi  kwanini  naona kama umebadilika  sana , mbinu uliotumia kupasua  vioo haifanani kabisa na ile  niliokuzoea nayo?”Aliongea  na kauli ile ilimfanya Hamza kucheka.

“Ndio sijatumia kabisa mbinu ya  nishati za  mbingu na ardhi maana nishaachana nazo?”

“Kama ni hivyo umetumia mbinu  gani sasa?”Aliuliza  huku akiwa  anashangaa , ukweli ni kwamba hakujua kabisa ni kitu gani kinaendelea kuhusu Hamza.

“Usiwaze sana   nimeachana na mbinu zote  zilizozoeleka sasa hivi  nipo  kwenye kitu kingine kabisa”

“Boss kila siku unaonyesha wewe sio mtu wa kawaida , yaani umepata mbinu mpya  na umeweza kujifunza ndani ya muda mfupi tu na sasa unaonekana kama mtu mwingine , yaani

unatufanya sisi   binadamu wa kawaida tukose  kabisa hata  tumaini”

“Hehe.. unawaza nini sasa,  kama  tungefanana unadhani ningekuwa bosi wenu  wewe mshenzi, huna haja ya kuwaza sana labda kama unataka kunipindua”

“Hamna bosi  bado  najichukulia  nipo chini ya himaya  yako  mpaka sasa. halafu sio kama nina cheo kikubwa  tokea nirudi kuliko kule”

“Huko nako ndio kujihusha , ndani ya miaka saba uliorudi  nchini  umeweza  kuingia ndani ya  kitengo cha  Malibu na baadae kuwa mshauri  wa vitengo vyote  vya usalama na ulinzi  na kupanda cheo  mpaka kuwa jenerali , sio  kazi ndogo  kulingana na umri wako”

“Mafanikio yangu ni   kama kichekesho nikijaribu kulinganisha na yako , isitoshe  kwa  kujilinganisha na  wenzangu  niliowaacha sidhani  napaswa kusema nina mafanikio ya juu”

Hamza aliona alichoongea kinaleta maana , isitoshe kwa kipindi kirefu  walichokuwa chini  yake, alikuwa  kama kikwazo kwa mafanikio yao , lakini  wengi baada ya kuwaachia  na kurudi   kwenye mataifa  yao  waliweza kupata mafanikio makubwa ndani ya muda mfupi.

Walijikuta wakiongea kwa muda mrefu kidogo mpaka muda ambao Afande Himidu alikumbuka  swala la Ankh.

“Bosi vipi kuhusu  hili swala la Ankh , kwannini watu wanakufualitia  nalo sana au ulikuwa mtego wa Genesha?”

“Genesha  aliiniingia kwenye majaribu ni  kama ananiambia  hata kama nimekufa  huwezi kuishi kwa amani ,  unadhani ni nani kajua kuhusu hii siri kama sio yeye alieisambaza , mtu ananipa kitu halafu anawapa watu taarifa ili waanze  kuniwinda , huyu  alichotaka ni   kuona sipati  amani.

Hivi unajua ndio alinirudisha hapa  Tanzania , baada ya kunitumia  ujumbe wa kila aina kwamba anakaribia kufa na yupo hapa   hivyo nionane nae kwa mara ya mwisho , lakini sikujua  kama  aliacha  anuani kwenye maabara yake  ili ijulikane nipo Tanzania.

“Nini! , kwahio unamaanisha Dokta Genesha alifia  hapa  nchini, maiti yake..”

“Nilimtupia  baharini  , aliniambia mwenyewe niifunge maiti yake na jiwe zito na kisha nimtupe”Aliongea Hamza huku akiwasha kwa mara nyingine sigara na kuvuta moshi kidogo.

“Kama ni hivyo  bosi , vipi kuhusu hii Ankh , ni siri  gani , maana kwa  ninavojua kama nipo sahihi  Ankh maana yake ni alama ya msalaba  ambayo  ilikuwa ikiwakilisha uhai   ndani ya Misri ya kale , si ndio?”

“Upo sahihi Ankh  ni  ishara ambayo alitengeneza Nekhbet  mungu  wa Misri ya  kale kama  ishara   ya zawadi ya uhai   kwenda kwa  Farao, sababu ya   dokta Genesha  kuipa siri hii Ankh  ni kwasababu  ni siri  ambayo inahusianisha na uhai wa binadamu, ushawahi kusikia mtu yoyote anasema  simulizi ya njiwa juu ya mti wa Uzima?”Aliongea Hamza. “Nakumbuka nilishawahi kusoma hiki kitu kwenye Deep web , nilichukulia kama uzushi lakini   walisema  kuna Dokta  kagundua  siri  juu ya kwanini binadamu anakufa  mapema?”

“Unadhani nimeanza kukuelezea juu ya Nekhbet 

ili ulichukulie hili swala  kama hadithi za kale?”Aliuliza Hamza.

“Kwahio  Bro  unasema  Ankh  ni kitu   cha  enzi ya  Farao au unamaanisha nini?”

“Kama nilivyokwisha kusema Ankh kama Ankh  ni  ishara tu  ambayo imetumika kuficha  siri  juu ya  hatua za uhai wa binadamu ulivyo , chukulia ni kama  maandiko ya  enzi hizo yameonekana sasa hivi  kwa ligha ngumu isioweza kutafsirika” 

“Kwahio  bosi kama ulichoshikilia ni kanuni , si inamaanisha umeshika siri  ya dunia , sidhani   ni  makundi ya kihalifu tu ambayo yanaweza kupigania, hata nchi  zitajiingiza katika vita za kupata hiki kitu”

“Enzi  ya kale watu walikuwa tayari kusafiri kwa kuvuka bahari kwa ajili ya kutafuta namna ya kurefusha maisha  lakini sasa hivi  sio kutafuta  bali sayansi imeendelea   na wanasayansi wanakaa tu maabara  kufanya  tafiti za kutengeneza madawa , lakini mtu yoyote ukimwambia kama  kuna uwezekano maisha  yakarefushwa na dawa atakuona kichaa  tu”Aliongea Hamza na kumfanya  Himidu kutingisha kichwa kukubaliana nae.

“Kwahio bosi kama ulichoshikiria ni   kanuni   juu ya siri ya uhai wa binadamu ,   je   imewezwa kufanyiwa utafiti?”

“Hapana ,  Genesha alijaribu kufanyia utafiti  ili kuweza kuitafsiri  lakini alishindwa , kulingana na maelezo yake  ana uhakika kabisa  ni kitu ambacho  kinaweza kubadilisha mtazamo wa binadamu juu ya uhai , lakini kutokana na   msongo  wa mawazo juu ya mke wake  yalimshida  hivyo  aliniachia kila kitu  na kisha akajiua , nadhani unajua  nisingeweza kumzuia kama alitaka kujiua  mwenyewe”

Afande Himidu alijikuta akivuta pumzi ya ahueni ,ukweli  kulingana na mtazamo wake  anaomba  isiwe kweli , aliona kama kweli  binadamu atajua namna ya kurefusha maisha , basi atakuwa kiumbe hatari zaidi kuliko hata siraha za nyuklia.

“Mimi kwangu naona hizi ni kama  stori  tu na uwezekano huo haupo?”Aliongea Himidu.

Hamza licha ya kuamua kumwambia ila hakutaka kumpa ukweli wote , isitoshe kuna misheni ilikuwa ikiendelea kuhusu  yeye chini chini 

“Ukweli  ni kwamba  Ankh  ni ni nadharia  ambayo  wanasayansi wanayo tayari”Aliongea Hamza.

“Kivipi?”

“Kwanza unajua namna mwili unavyofanya kazi , mfano tu chukulia  seli ambazo zinazunguka utumbo  zinajigawa  kila baada ya siku tatu mpaka tano na  kuweka  nyingine , sio hivyo tu   kila baada ya miezi miwili  seli za  kibofu  cha mkojo zinajiondoa  na  kuwa  zingine , seli za damu  zenyewe zinabadilika  kila baada ya  miezi minne , maana yake ni kwamba  asilimia tisini na nane  ya seli  zote  zilizopo ndani ya mwili wetu zinaondolewa  na  hewa na chakula kwa  mwaka , kwa  ligha nyepesi ni kwamba  kila mwaka mmoja  ukipita mwili wako umebadilika  vitu vingi sana, sasa  kadri mwili  unavyoendelea kwa kasi kuzalisha seli mpya na kuhamisha zile zilizokufa  huo mchakato unazuia mwili  kuzeeka , , hivyo kama mchakato huu ni endelevu  bila kupungua nyakati zote basi  binadamu asingekufa mapema, ukichana na swala la kuugua  na  kupata ajali”

“Kama ni hivyo  sasa  kwanini sisi binadamu bado tunaendelea kuzeeka?”Aliuliza   Afande.

“Kwasababu  inafikia hatua  ule mchakato wa seli  kugawanyika ndani ya mwili na kutengeneza mpya  hupungua  kabisa , huu mchakato wote unadhibitiwa na DNA, Chukulia  urefu wa uhai wako ni kama kamba ya kiatu, kadri  unayotoka mwanzo  wa kamba  kueleleka mwisho wa kamba ndio  namna unavyopunguza  siku za uhai wako kutokana na seli za mwili kutojigawa na kutengeneza mpya , ukifika mwishoni mwa kamba unakutana  na kile kichopoo ambacho kimeifunga kamba  kuonyesha ndio mwisho, sasa  pale ndio mwisho wa  seli za mwili kujitengeneza upya ,  ukizungumzia  kisayansi  sasa DNA  ina muundo kama  wa kamba  kwani mwishoni mwa urefu  wake  kumefungwa  kitu kama kichopoo ambacho  kisayansi  kinaitwa Telomere.

Sasa  chukulia   kitendo cha kutaka kuongeza urefu wa kamba  ndio kuongeza urefu wa  maisha ya binadamu , utakachofanya ni kuondoa kile Kichopoo na kutafuta   kamba inayofanana kwa asilimia mia moja na ulokuwa nayo  kisha kutafuta namna ya kuunganisha ile kamba bila  kubadili  muundo wake na mwisho wa siku utafanikiwa kuiongezea  urefu,  ukichukulia huo mfano   katika  muundo wa DNA  utakuwa umeongeza urefu wa maisha yako, hiki ndio kitu ambacho  Genesha anaamini kipo katika  siri ya Ankh”Aliongea Hamza.

Ijapokuwa  hakuwa  mwanabailojia lakini  kwa kiasi kidogo alihisi kuelewa alichokuwa akitaka kumaanisha juu ya itu kinachoitwa Ankh. 

“Inaonekana nadharia yake inaleta maana kwa kiasi flani , lakini kwasababu haikukamilika na  kanunni   imeshindikana kutafsirika kutokana na lugha yake si inamaanisha ni kitu ambacho hakitowezekana, kwanini akaamua kukupatia wewe   hii  siri ya Ankh?”

“Kwasababu anaamini kazi kubwa amekwisha  ifanya , kwa maelezo yake anaamini kuna  elementi moja ambayo haijagundulika bado na  inaweza isigundulike  kama tu  kutakosekana tafsiri  ya Kanuni ya Ankh , elementi hii ameitaja kama  Elementi  ya Nuru na kama ikipatikana basi kila kitu kitabadilika”

“Kwahio  bosi Dokta Genesha anaamini   fumbo la

hii elementi litapatikana katika   tafsiri ya  kanuni hio ya Ankh?”

“Uwezekano huo upo ila sina uhakika , kuna uwezekano  hii elementi isiwepo kabisa  hapa duniani  au hata angani katika sayari nyingine”

Ilikuwa  ni siri nzito sana juu ya Ankh aliopata  kuisikia  Afande Himidu ,ijapokuwa  aliona  Hamza  hakuwa ameielezea vizuri   kueleweka lakini  aliona pengine kuna sababu ya Dokta Genesha  kumpatia  Hamza,  hata hivyo alijiuliza kwanini  maana Hamza sio mwanasayansi.

“Bosi  hiki kitu ni kama kiazi  cha moto  ni kheri ubakie nacho tu , sitouliza tena  kuhusu hili  , kuna kila sabababu ya  Dokta Ganesha  kutotaka   tafiti zake zipotee , lakini  hata hivyo   swala hili likijulikana kwa watu wachache  ni bora zaidi”

“Ndio maana nilitaka kuongea na wewe ,  ili uweze kutuliza shauku wanayoanza kuipata   wanajeshi wenzio  , siku zote watu wakinifuata niliishia kuwaambia   simulizi ya   njiwa juu ya mti wa uzima   ni  uzushi tu, nafanya hayo kwasababu nataka watu wasahau, vyovyote vile  hata kama ikitokea  kanuni yote nimeijua  nitaenda nayo kaburini , sioni kama kuna faida  ya binadamu kuishi muda mrefu, hivyo  hakikisha  uchunguzi wowote unaendelea kuhusu mimi  uachwe  mara moja , sio salama watu  wengi kuanza kuulizia kuhusu Ankh , wakikusumbua wewe waonyeshee dole”Aliongea Hamza na kufanya Afande Himidu kucheka.

“Bosi usiwe na wasiwasi , hii ni siri yagu na wewe kwanzia sasa , hata  taarifa  azitake Mfalme Nyoka” “Haha.. halafu huyu Mfalme Nyoka  sijamuona kwa muda mrefu , unadhani   atakuwa amenipita ki uwezo kwasasa?”

“Kama ni kipindi cha  mwanzo  ningeweza kusema unamuweza , lakini sasa  hivi naona  umeua  nguvu zako zote za nishati , hivyo ni ngumu kutabiri chochote”

******

 Waliongea mambo mengi mno  mpaka  juu ya  Hamza kuoa, na  Afande Himidu alitaka kujua  imekuwaje kuwaje  Hamza akaoa lakini Hamza alimwambia ni  stori ndefu.

Alimwambia kama ni stori ndefu basi amtambulishe kwa shemeji, Hamza aliona sio mbaya kumtambulisha kwa Regina , hivyo  alimwambia wakitoka  hapo watafute  sehemu   kwa ajili ya chakula cha usiku  na ampigie  simu  Regina kufika.

Afande Himidu  alitoa maagizo kwa  makamanda waachane  na uchunguzi  wote unaohusiana  na Hamza kwanzia dakika hio na wiki inayofuatia atafika makao makuu kutoa maelekezo zaidi.

Kwasababu  maneno yake ni sheria  wote walikubali na kisha waliondoka huku  bado wakiwa na maswali mengi , kati yao ambae hakuwa ameridhika kwa kiasi kikubwa alikuwa ni  Afande  Mdudu.

Baada ya   Hamza kuingia  kwenye V8 ya Afande Himidu ili kutafuta sehemu kwa ajili ya  kupata chakua cha usiku , Hamza alitumia nafasi hio kumtafuta  Regina na kumuuliza kama yupo free wakapate Dinner lakini Regina alisema  yuko bize  na kazi  hivyo Hamza  hakujishughulisha nae  zaidi.

Japo Himidu alitaka kujua   Hamza kashikika kwa  nani lakini  mara baada ya Hamza kumwambia haiwezekani  kwa siku hio kukutana na shemaji yake  aliamua kuridhika . Hamza hakumwambia  kama ni Regina mmiliki wa makampuni  ya  Dosam , alitaka kuweka cheo chake pembeni na kutambulisha Regina kama Regina.

Hamza kwasababu alikataliwa na Regina kutoka  wote Dinner  aliona haina  haja ya kwenda mjini  kwa ajili ya chakula bali walichukua barabara ya kuelekea  Kijichi  kwa  Dina.

Himidu alishangaa kuona Hamza alikuwa na mahusiano na Dina , alikuwa akimjua sana Dina  kutokana na faili  nyeti la mtandao wa Chatu alikuwa amekwisha kulisoma.

Kwa Hamza  ilikuwa kama sherehe ya kukutana na  rafiki yake  na kwasababu  ilikuwa  wikiend walijiachia  mgahawani kwa Dina na  baadae wakabadilisha   kijiwe na kwenda  mjini  zaidi.

Himidu aliamua kutumia pesa zake  kuhakikisha Hamza anayafurahia  maisha na Hamza hakuona shida.

Hamza upande wake hakusahau kumpigia simu 

Prisila na kumpa taarufa alishatoka , taarifa ambayo ilikuwa  nuri kwa Prisila.

Hamza  hakufanikiwa kurudi nyumbani kabisa  siku hio  na kuishia kulala nyumbani kwa  Dina mpaka asubuhi na  kulivyokucha  aliendelea  kukaa mpaka  muda wa jioni ndio alivyoanza safari ya  kurudi nyumbani.

Ilikuwa muda wa saa kumi  na moja kama  na nusu hivi ya jumapili ndio aliingia  nyumbani   na kitendo cha kuingia getini  aliweza kuona gari  ambayo sio ya Regina ikiwa katika  maegesho ya muda  mfupi.

Hamza  palepale kwa kuichunguza tu hio  gari  aliikumbuka vizuri.

“Hii  gari si  ni ya Yulia hii, anafanya nini hapa nyumbani”Aliwaza   Hamza huku hisia zikimwambia huyo mwanamke kamfuata mpaka  hapo  zikimvaa.

Previoua Next