Reader Settings

Mzee huyo  alionekana kuwa na haraka  , japo Hamza  alikuwa hamjui lakini kuna kitu ambacho  alikiona kutoka kwa huyo mwanaume   , ilionyesha alikuwa akimfahamu  japo hakujua kivipi.

“Daddy!!”

Sauti ya Irene ilisikika nyuma ya Hamza ,  ilionekana hata yeye alishituka baada ya mlango kugongwa na alimwangalia baba yake kwa macho yaliojaa hasira.

“Irene  naomba unisamehe binti yangu , nimekukosea jana , Dadd amekosea  na  hatorudia tena ..”Aliongea huku akimpotezea hata Hamza na kwenda kumshika mikono Irene.

“Ulinifokea jana na kunitolea lugha chafu..”

“Nilikuwa  nimechanganyikiwa   na pombe zilinipanda kichwani…”Aliongea  kwa kujitetea , ukweli kama mwanaume Hamza alimuonea huruma mwanaume mwenzake  kusalitiwa.

Waswahili wanasema ‘kugongewa’ kusikie kwa jirani tu, halikuwa jambo  jepesi na aliona hata kwa Irene ni swala ambalo  litamuathiri sana.

Irene hakuwa na sababu ya kumkasirikia baba yake , isitoshe  alikuwa akimpenda na alimchukia mama yake kwa kumsaliti baba yake  na waliishia kusameheana.

Lakini ndio muda ambao  mzee huyo  alianza kushikwa na wasiwasi kama hakuna kitu kilichomtokea binti yake ,  Irene  ilibidi amhakikishe hakuna kilichomtokea na alipatwa na ahueni japo sio kwa asilimia mia.

Ukweli licha ya kumfukuza  Irene hakujua hata alimfukuza  saa ngapi maana alikuwa amelewa chakali  na alikuja kukumbuka asubuhi akimfukuza  Irene na  alivyoenda kuangalia  chumbani kwake na kutomkuta ndio alipatwa na wasiwasi na mtu  wa kwanza kumkumbua alikuwa  mdogo wake , alijua  Irene ataenda Bunju  kwa mjomba maana ndio mtu aliemzoea lakini alivyopiga  na kuambiwa  yupo Dosam V Hoteli  ndio  alikimbia mkukumkuku huku akiwa na wasiwasi baada ya kugundua mvua ilinyesha sana  jana, japo ya kupokea lawama kibao  kutoka kwa mdogo wake hakujali tena.

“Mr Hamza  asante sana   kwa kumfanya binti yangu kuwa salama”Aliongea.

“Usiwaze mzee , Irene ni mwanafunzi wangu nisingemuacha ananyeshewa na mvua”

“Hivi ni kweli  umekuwa  mwalimu wa Irene , nimesikia leo  ila sikuamini?”

“Ndio ila nilipatwa na ubize  ndio maana sikuonekana tena”Aliongea  na kauli ile ilimfanya  bwana huyo kumwangalia Hamza kwa macho yaliojaa wasiwasi.

“Hamza  nakushukuru  kwa  yote uliomfanyia binti yangu na kuhakikisha yupo  salama , yalikuwa makosa yangu kumfukuza nyumbani hivyo siwezi kumlaumu mtu , lakini  kwanzia sasa naomba ukae  nae mbali , bado ana safari ndefu ya kimasomo…”Alitaka kuongea zaidi lakini Hamza alimzuia.

“Mzee kwanza kabisa niseme mimi nimeoa ,  pili  hatuna ukaribu wala  mimi sio mwanafunzi wako  kiasi cha kutaka kuanza kunifundisha cha kufanya kilichotokea kuwepo hapa  ni ukarimu  tu na kujali usalama  wa msichana mdogo kufukuzwa na baba yake nyumbani”

“Ah , kumbe umeoa?”Aliuliza  huku akionyesha mshangao na Hamza aliishia kutingisha kichwa.

“Kama ni hivyo basi  nimeridhika  na maneno ya Irene , sisi  wanaume ni waaminifu sana ndio hivyo tu  , kwa mtu kama wewe  unaefahamiana  waziri  Mulumbi sio mtu wa kukurupuka”Aliongea na kumfanya Hamza kujua sasa  wasiwasi umetokana na nini.

Mulumbi ni Waziri wa ulinzi ambae alikutana nae jana wakati akiwa na Afande Himidu katika viwanja vya bata.

Upande wa Irene mara baada ya kusikia kauli hio ya Hamza kuoa  uso ulijikunja  na alimwangalia  Hamza kwa macho yaliojaa machungu.

Ilikuwa ni  Jumatatu hivyo Hamza aliagana nao haraka haraka na  kuianza safari ya kwenda kazini.

Kutokana na foleni kubwa barabarani alichelewa kufika kwa zaidi ya nusu saa  na  mara baada ya kupeleka gari kwenye  maegesho aliweza  kuona Aud Q8  nyeusi na   moja ka moja alijua Regina ashafika.

Hamza mara baada ya kuingia ofisini kwake hakupewa  kazi nyingi sana kama mwanzo na ilimfanya kushangaa maana sio kawaida ya Linda  na alijiuliza nini kimetokea mpaka mwanamke huyo kubadilika , sio hivyo tu hakuonyesha ile hali ya dharau aliokuwa nayo mwanzo bali ni kama alikuwa akimuogopa.

Asichokijua Hamza Linda alifokewa  mara baada ya kumwagiza  kwenda  kudai mkopo makao makuu ya kampuni ya Dede.

Mchana   ulipofika Hamza alishuka chini kwa ajili ya chakula cha mchana  na aliweza kumuona Yonesi akiwa amekuja kazini na alikuwa amekaa  sehemu yake ile ile ya siku zote.

Alikuwa amevalia suti nyeusi  ,  rangi ambayo ndio sare kwa  watu wa usalama   ndani ya jengo hilo lakini kutokana na suruali yake kumbana  ilifanya  wanaume kumwangalia kwa macho ya tahadhari, walikuwa wakimtanani na kumuogopa kwa wakati mmoja.

Yonesi ni kama alikuwa ametarajia Hamza atafika kwenye meza yake  maana  hakuonyesha kushangaa zaidi ya kuinamisha kichwa chake chinni akiendelea kuwa bize na  kula.

“Kapteni hatimae naona umekwisha kupona kabisa  na  ari ya kufanya  kazi imerudi”Aliongea Hamza lakini Yonesi hakuongea kitu.

“Kapteni  mbona kimya tena , leo sijakuchokoza  ila kwanini unanipotezea?”

“Wewe ni  mume wa bosi, hata kama wafanyakazi wote hawajui   napaswa kujiweka mbali na wewe”Aliongea kwa kauli  hafifu na  hata bila ya kumaliza chakula chake alisimama akitaka kuondoka lakini Hamza alimzuia.

“Kapteni umeongea kitu ambacho hakipo sahihi , kwani  kuna kosa lolote kukaa kama hivi , ukinikimbia kama hivi  si itamaanisha kuna kinachoendelea kati yetu , Au Kapteni ushaanza kunipenda nini?”Aliuliza Hamza.

“Sijaanza chochote , unaongea ujinga gani?”Aliongea  huku akishikwa na aibu na kugeuza  uso wake  pembeni.

“Hutaki hata kuniangalia usoni, najuaje kama kweli hujaanza?”

“Haya nimekuangalia sasa , umefurahi?”Aliongea Yonesi huku akimkodolea  Hamza  macho  kwa hasira lakinni Hamza hakuchukulia upande wa hasira bali aliangalia uzuri wa  mjeda huyo.

“Kama ni hivyo  basi kaa chini , umalizie kula  tena kama vipi uongeze kabisa maana umetoka hospitalini na kama mgonjwa unatakiwa kula ushibe”Aliongea  na kweli Yonesi hakuwa ameshiba  na kutokana na kwamba  alikuwa mtu wa mazoezi  alihitaji kula  sana tofauti na wanawake wengine.

Baada ya kufikriia aliona hakuna kibaya ambacho amefaqnya na Hamza  hivyo  haitokuwa vizuri kuonyesha kana kwamba kuna kilichotokea , hivyo alikaa chini na kuendelea  kula.

“Halafu nimekumbuka , hivi  Afande Mdudu  hajakusumbua tena?”Aliuliza Hamza na kumfanya Yonesi kumwangalia usoni.

“Kwannini unauliza?”

“Nina rafiki yangu jeshini ana cheo kikubwa kuliko  Mdudu na nilimiomba amwambie Mdudu asikusumbue tena, ila sijajua kama kweli  anaweza kumtii”Aliongea Hamza kawaida lakini  kauli yake ilimwacha Yonesi na mshangao.

“Wewe ndio  umefanya hivyo?”

“Nimefanya nini?”

“Jana  mchana  nilipigiwa simu kutoka nyumbani  , ni mara ya kwanza kunipigia tokea nilivyokuja  Dar”

“Oh, na wamesemaje?”

“Baba amesema  hakuna ulazima wa ndoa na Mdudu tena  maana wametengua posa”Aliongea na Hamza aliishia kutabasamu na kuona pengine Mdudu alikuwa mtu mzuri kama ameweza kutii mara moja  kauli yake , aliona hayo yote ni kutokana na rafiki yake Himidu  na pengine anapaswa  kumtafuta na kumshukuru , isitoshe alikuwa akijua bado yupo mjini.

“Nadhani sio ishara nzuri kwangu ,   napaswa kuwa makini kwanzia sasa”Alitania Hamza.

“Ukweli nilijua baba alikuwa akinipigia kwa  ajili ya kunifokea maana toka nikimbie  hakuwahi  kunipigia na kuniuliza chochot, lakini  tofauti yake alianza kuniuliza maswali ambayo haya eleweki?”

“Amekuuliza nini?”

“Ameniuliza tu , yupo  Dar huyo anaekutana na  Mshauri mkuu?”

Baada ya kumaliza sentensi hio  Yonesi alimwangalia Hamza kwa umakini mkubwa kana kwamba kuna kitu anakitafuta

“Kwahio nini cha kushangaza hapo?”

“Cha kushangaza kipo , nimeingia jeshini  muda sana , lakini mpaka leo sijawahi kukutana na Mshauri mkuu , wanajeshi wengi wa  vyeo vya chini hatukuwahi kumuona  zaidi ya kumsikia tu”Aliongea  na Yonesi alijua pengine Hamza ndio  Mshauri mkuu.

Ki ufupi hata kwa Afande Mdudu kumjua  Mshauri mkuu ni kwasababu  alikuwa katika mfumo wa jeshi  kitengo cha siri.

“Mshauri mkuu ni rafiki, naweza sema ni kama ndugu yangu”

“Mshauri mkuu  amejiunga jeshi miaka sita iliopita na  alipitia  mafunzo makali  na kushinda kwa maksi ambazo hazijawahi kufikiwa na mwanajeshi yoyote kihistoria  na ndio  ilivyokuwa rahisi kwake kupandishwa  mpaka kufikia cheo cha  Luteni Jenerali  na inasemekana ametokea nje ya nchi kama wewe na  ni mdogo  kwa umri , ndio maana nikahisi  niwewe”Aliongea  na kumfanya Hamza aone  kumbe  rafiki yake Himidu amekuwa shujaa kwa mwanamke  kama Yonesi, lakini hata hivyo hakupenda..

“Unaonekana kumkubali sana?”

“Kabisa , kipindi  hicho kila mtu alipokuwa akimzunguzia  hakuna ambae alikuwa akiamini , unapaswa kuelewa  sio rahisi mwanajeshi kupanda cheo ndani ya  miaka mitatu kutoka  kuwa Meja  mpaka kuwa  Jenerali  na hatimae kuwa mshauri mkuu”

“Mna mpa misifa kibao  , unadhani  kapanda cheo kwasababu  ya juhudi zake tokea karudi ,  kama sio uzoefu wake aliokuwa nao nje ya nchi  isingekuwa rahisi  kiasi hicho  mpaka kuwa mshauri mkuu , kapitia hatua za kawaida  tu ,  alikuwa  jeshini nje  ya nchi na kuna ambao walikuwa wakimzidi vilevile , hebu acha kumfikiria sana   kwangu ni wa kawaida sana”

Hamza sio kama alikuwa akimuonea wivu   Himidu  kuwa shujaa kwenye macho ya Yonesi , alikuwa akiongea  ukweli mtupu licha ya kwamba ingeonekena kama ana wivu.

Yonesi pia aliliona hilo na kujiambia kwanini  Hamza anaongea kama vile  ana uchungu.

“Mbona povu  wakati namuongelea Mshauri mkuu? , kwahio umekosa furaha kisa nimemsifia?”

“Kwannini nikose furaha wakati naongea ukweli , yeye ni mtu wa kawaida tu hivyo  sikutaka uende mbali”

“Nimesikia  ni mtaalamu wa levo ya mbingu , kwahio unataka kusema umemzidi?”

Hama alijiambia ndio Himidu yupo levo ya  mbingu kama sio hivyo angewezaje kurudi  bongo.

“Kama ni hivyo inawezekana vipi , maana  huna   nguvu za nishati yoyote ya mbingu na ardhi?”Aliendelea kuuliza Yonesi.

“Kwenye huu ulimwengu kuwa  na nguvu  sio kujifunza tu  maswala ya nishati za mbingu  na ardhi , kama umezaliwa na kipaji na  uvumilivu , unaweza kuwa na nguvu hata bila ya kujifunza mbinu ya nishati ya mbingu na ardhi na ukamshinda hata mtu ambae yupo levo ya juu ya mafunzo hayo”Aliongea Hamza na kumfanya  Yonesi kushangaa.

“Kama ni hivyo kwanini  usinielekeze  namna  ya kuweza  kuwa na nguvu?”Baada ya kusikia hivyo  Hamza alijiona amekuwa mropokaji na kuongea vitu ambavyo hata hakupaswa.

“Basi tufanye  hivi  saa nane twende  kwenye  vyumba vya mazoezi  na nitakufundisha kitu”Aliongea.

“Kwahio unaniambia  naweza kuwa na nguvu  bila  ya kujifunza mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi?”

“Ndio , ila itategemea  na jinsi unavyojifunza , ninachoweza kusema kama  utazingatia nitakachokuelekeza , unaweza  kuwa zaidi hata wavuna nishati”Aliongea  Hamza na kumfanya  Yonesi kushangaa.

“Wewe ni nani?,  kwanini mtu ambae unafahamiana na Mshauri mkuu  kuwa na mafunzo ya ajabu namna hio?”

“Kama  unataka kujua  , nikiss  kwanza”Aliongea Hamza akiwa na tabasamu.

“Kafie mbali” Aliongea akionekana kuurudia  uhusika  wake , Hamza hata hivyo alimtania tu maana alijua ni ngumu sana kwa  Yonesi kufanya hivyo.,

“Umeoa tayari , kuwa makini na mimi la sivyo nitaenda kumwambia  mkeo ujinga wote unaofanya”Aliongea na  palepale alichukua sahanu yake na kisha akaondoka.

Hamza mara baada ya chakula  alichukua matunda  kwa ajili ya kumpelekea Regina na kumsalimia pia , lakini alivyokumbuka ana siku nyingi hajamuona  Eliza wala kuwasiliana nae  aliona aanze kupitia huko kwanza na kumpelekea na yeye matunda.

Dakika ambayo alitaka kuingia  ofisini kwa Eliza sauti ya Asha kutokea nyuma ilimwita

“Hamza unamtafuta Eliza?”Aliuliza huku akionyesha kuwa na ari  kubwa.

“Ndio , yupo wapi?”

“Meneja  ameomba likizo ya   muda mrefu , hatorudi mapema”Aliongea na kumfanya  Hamza kushangaa.

“Kwanini kaomba likizo ghafla tu?”

“Kuhusu hilo sina uhakika , lakini nadhani kuna kinachoendelea nyumbani kwao , pia nimesikia ameomba  nafasi ya kwenda kufanya kazi nje  ya nchi kwenye  kampuni tanzu , sijui sababu  labda utuambie wewe Hamza”

Muonekano wa Hamza ulibadilika  hapo hapo , alikumbuka mara ya  mwisho alivyoachana na  Eliza na wasiwasi ulimvaa palepale na kuanza kujilaumu kwanini hakumtafuta hata kwenye simu.

“Ngoja  nitakucheki nikifahamu lolote”Aliongea Hamza na kukimbilia kwenye lift  akipanga kwenda  ofisini kwa Regina.

Regina  alikuwa bize  na tarakishi yake  ikionekana kuna kitu alichokuwa akisoma , siku hio alikuwa amevalia  shati  la  mikono mirefu kitambaa cha saatini  na  suruali  ya kitambaa ya rangi ya pink.

Kwa kumwangalia kwa ukaribu usingedhania alikuwa CEO , alikuwa kama msichana wa  miaka kumi na nane ambae   anajiandaa na mtihani wa chuo , lakini usiriasi wake ulimfanya kuonekana mtu mzima.

“Mbona umeleta maboksi mawili  , siwezi kumaliza yote”Aliongea Regina maana alishazoea Hamza ana utaratibu wake wa kumletea matunda.

“Regina  nasikia Eliza ameomba kufanya kazi nje ya nchi , unajua kuhusu hili?”Aliuliza Hamza na  swali lake lilimfanya Regina kuganda  kabla  ya kutingisha kichwa kukubali.

“Ndio  nimepokea maombi yake kutoka ofisi ya rasilimali watu , kwanini nisijue wakati ndio naidhinisha”Aliongea.

“Tangu lini tokea atume hio barua,halafu kwanini hujaniambia?”Aliongea Hamza huku akionyesha kuwa  na mawazo  na  ilimfanya Regina kuongeza usiriasi zaidi.

“Mimi ndio  Mkurugenzi  na yeye ni mfanyakazi wangu  kama mfanyakazi katuma maombi napaswa kuwasiliana na Idara ya  HR  kwanini  nikuambie  wewe?”

“Regina unajua sijamaanisha hivyo , kama hili swala linatuhusu sisi  napaswa kujua , huoni sio sawa  kwa mtu ghafla tu kutaka kwenda nje ya nchi?”

“Kwahio unaona ambacho hakipo sawa kwake , kwangu ndio kipo sawa , kwanini kila kinachomtokea  Eliza unahisi  mimi ndio Mkandarasi mkuu nyuma yake?”

“Regina  unajua  sijamaanisha unachofikiria , ninachotaka kujua sababu ni nini basi”

“Kwahio unadhani nimekuficha makusudi sio ili kuwatenganisha , kama una wasiwasi  sana kwanini usimtafute alipo na kumuuliza sababu niini ,  hujiulizi  kwanini hajakwambia?”Regina alikuwa na hasira mno hasa  baada ya kuhisi anasingiziwa kitu ambacho hajafanya.

“I was wrong , usiwe na hasira  hivyo  , nimekosea  nilipaswa kujiuliza mwenyewe na sio  kukuuliza wewe”Alijitetea Hamza.

“Halafu ukitoka hapa unaanza porojo ooh sijui  ni wanandoa kisheria  na ujinga mwingine huku unaempenda  ni  Eliza. At least on the surface,  you should show me respect

Hii ni mara yako ya  pili unanisingizia  kitu cha namna  hii , ushawahi  kujiuliza najisikiaje?”Regina  alikuwa na hasira kiasi kwamba kifua chake kilipanda  na kushuka kwa kasi mno, huwa ni mara chache sana kumkuta  akichanganya kingereza na kiswahili na akifanya hivyo  ni kweli hasira zimemfika  kooni.

Previoua Next