Reader Settings

Hamza  aliona ni kama  Dina anaonngea kimafumbo mafumbo na alitaka aende moja kwa moja.

“Unakumbuka  nilimwambia  Prisila leo  kuna tukio la  ufunguzi wa  Albam ya msanii mmoja mkubwa hapa nchin na niende nae?”Aliongea  Dina na Hamza hapo hapo alikumbbuka  ndio.

“Nakumbuka vizuri?”

“Basi  huyu msanii ni mkubwa mno na  huyo mtu ambae namzungumzia  lazima atakuwa mmoja   wa wageni wa heshima wa tukio hili , nina uhakika hata mstaafu  Mgweno atakuwepo , unaonaje  tukishiriki wote watatu?”Aliongea Dina na Hamza hapo hapo aliona  ni  pendekezo zuri.

“Itakuwa vizuri nikishiriki,  nitaenda kumpitia 

Prisila nije nae”

 “Vizuri , mimi nitatangulia na kukuwekea utaratibu wa kupata  kadi ya mwaliko”Aliongea   Baada ya Hamza kukata simu  alimtumia ujumbe Prisila kwamba atampitia kwa ajili ya  kwenda kwenye sherehe za ufunguzi wa Albamu  na Prisila  alijibu  dakika hio hio  kwamba atamsubiri.

Muda alikuwa nao wa kutosha  na alitamani kurudi kwenye kampuni  lakini  aliona sio chaguo sahihi hivyo alipeleka gari mpaka  fukwe ya Coco  na kisha alishusha kiti  na kusinzia.

Saa kumi na mbili  hivi aliwasiliana   na Prisila na alimtajia  anapoishi na Hamza mara baada ya kuijua Anuani inaelekeza wapi alichoma mafuta kwenda huko na ilimchukua dakika kama kumi na tano  mpaka kufika nje ya  nyumba  kubwa yenye ukuta na  Geti jeusi lililonakshiwa na rangi ya shaba.

Lakini sasa muda ambao Hamza anasimamisha gari pembeni kwa ajili ya kugonga  geti , gari  nyingine ilisimama kando yake, ilikuwa ni moja ya gari ya kifahari  na ilionekana pia uelekeo wake  ni ndani ya  nyumba hio.

Hamza  mara baada ya kufungua mlango na kutoka na  gari ile aina ya   Cadillac S series toleo jipya ya  rangi ya bluu  ilifunguliwa mlango na palepale Hamza alimfahamu bwana huyo  ambae alionekana kupendeza mnno.

Alikuwa amevalia suti ya Armani  na suruali ya Zegna , mtu yoyote angemuona kwa macho ya  haraka angeweza kumfahamu ni mtu muhimu kwenye jamii.

“Bosi Side  naona  ni bahati nyingine tunakutana”Alisalimia Hamza huku akikunja ndita  “Hamza!, unafanya nini hapa?”Aliuliza  Side huku akikunja sura kama amelishwa  pilipili.

Kabla hata ya  Hamza kujibu hilo swali mlango wa geti ulifunguliwa na alitoka Prisila  ambae  alionekana  ameshavaa makeup lakini  mavazi bado ,  urembo wake uliongezeka maradufu.

“Hamza umewahi mno , nilikuambia uchelewe chelewe”Aliongea Prisila huku akitoa tabasamu. , lakini  alionyesha mshangao  mara baada ya  kumuona  Side , ilionekana alifika hapo bila   taarifa.

“Side unafanya nini na wewe hapa ?”Aliuliza.

Muda ule Side hakumjali tena Hamza na  alitoa tabasamu  lake la kimauaji  huku  akitoa  ua  la Rose kutoka kwenye gari.

“Prisila najua wewe ni shabiki  kindaki  ndaki wa msanii Almasi  na leo ni siku ya  kuzindua rasmi albamu yake , nina mwaliko nataka  tutangulizane wote”Aliongea  kwa   swaga nyingi mno kama vile ni  mwanamfalme.

Prisila  alijikuta akiyaangalia maua  na kisha  bila hata ya kujielewa macho yake aliyaelekeza kwa Hamza  huku akionyesha hali ya kusita.

Baada ya kujifikiria kwa sekunde aliishia kupokea  lile ua kwa ajili ya kutoonyesha ujeuri.

“Asante  sana Saidi , lakini umejuaje namshabikia   Almasi na sio King?”

“Nimekufollow instagram  na  mara nyingi naona maoni yako  ya kumkubali Almasi” “Oh kumbe “Aliongea huku  akionyesha  kutofikiria sana  isitoshe hata yeye  alikuwa akiona maoni ya Saidi mtandaoni.

“Saidi  nilikuwa nikijiandaa  kwa ajili ya kuelekea   huko  ndio maana Hamza yupo hapa kwa ajili ya kunichukua”

“Ulikuwa  na mwaliko , wewe na  Hamza!!?”Aliongea  Saidi  huu akionyesha mshangao.

Lakini side muda huo alikuwa  akijiuliza inamaana Lea hakumwambia  Prisila juu ya  Hamza kujihusisha na magenge ya kihalifu.

Aliishia kumwangalia  Prisila   kwa namna  anavyomwangalia  Hamza na kila kitu kilijionyesha  na ukauzu ulimvaa palepale   lakini alijitahidi kujionyesha kuwa kawaida , alitamanni  bora hata angekuwepo  Chriss  kidogo angeweza kuonyesha ukichaa wake waziwazi lakini aliupotezea  mara moja.

“Prisila   nataka leo uwe partner wangu  usinikatae, sikukutaarifu  moja kwa moja  maana nilijua huna wa kwenda nae”Aliongea .

“Side kama nilivyosema  nishakubaliana na  Hamza kwenda nae  na  tuna mwaliko , ni kosa lako kuchelewa, Hamza naenda kuchukua mkoba  wangu  tutapitia Malkia Stylish  nivae gauni langu”Aliongea Prisila na bila ya kusubiri alirudi ndani  na hazikuchukua sekunde nyingi aliweza kutoka na  kumpa ishara  waondoke.

“Bosi Side naomba utuwie radhi  tutatangulia  wa kwanza”Aliongea Hamza  na muda ule Saidi  alijihisi ni kama atapasuka  kwa hasira. 

“Prisila  fikiria mara mbilimbili , ukienda na mimi utakutana na watu wazito  na itakuwa faida kwako”

“Asante Side  naenda kumshuhudia msanii ninaemshabikia na sio kukutana  na watu  wazito” “Prisila kwanini  hutaki kunielewa tokea tukiwa  shuleni mpaka sasa najitahidi kukuonyeshea   ninavyojisikia , lakini kwanini hujawahi kunisikiliza”

“Saidi kwanini ghafla tu unaongea yote hayo..”Aliongea Prisila huku hasira zikianza kumvaa na Saidi  hakutaka kumsababishia hasira zaidi. 

“Usikasirike  Prisila , sijaja  kwa ajili ya kukasirisha  hivyo naondoka, Hamza hakikisha

Prisila anakuwa salama”

“Usiwaze bosi , Prisila ni mwanafamilia  , hawezi kupatwa na tatizo lolote chini ya himaya yangu”Aliongea Hamza lakini kauli ile ilimfanya Side kumwangalia  Hamza kwa macho makali  bila kuongea neno.

Upande wa Hamza  alijikuta akikunja ndita , sekunde hio kuna kitu ambacho alihisi   na sio cha kawaida  ni msisimko  wa ajabu ambao ulimtoka Saidi.

Lakini sekunde  kadhaa tu  msisimko ule ulipotea na hakuweza kuhisi kitu chochote tena  na alijikuta akijiuliza nini kimetokea au amehisi vibaya.

“Hamza hakuna kinachoendelea kati yangu na  Saidi na haitokuja kutokea hivyo usije kunidhania vibaya , nimepokea zawadi yake ya ua kwasababu  sikutaka kuonekana nina jeuri”

“Usiwe na wasiwasi , mwanamke kama wewe kufuatiliwa na wanaume wengi  inamaanisha  ni mzuri , sio jambo  baya”Aliongea Hamza  akiwa na tabasamu  huku akijiuliza kwanini  rafiki yake huyo wa utotoni  anajitetea mno kwake au ashampenda.

Prisila aliishia kutoa tabasamu  baada ya kuona Hamza  hana ishara yoyote ya kumdhania vibaya na muda huo huo walianza safari.

“Hamza vipi  ile siku walikutoa saa ngapi?”Aliuliza  Prisila.

“Ukweli nilienda kama kutalii tu  na kurudi , sikukaa muda mrefu”Aliongea Hamza na Prisila alitingisha kichwa kukubali.

“Vipi Regina  anaendeleaje , sijawasiliana nae muda mrefu?” “Kama kawaida yake , nadhani unamjua rafiki yako alivyo”

‘”Wee unaongea kama vile  una ukaribu nae  sana siku hizi”

“Ndio ukaribu wetu ni mkubwa”Aliongea Hamza  na kumfanya Prisila kutoa tabasamu lililojaa maswali.

Dakika chache  tu  Hamza alisimamisha katika moja ya duka kubwa la nguo za  kike  na ilionekana   wauzaji walikuwa wamejipanga kwa ajili ya kumhudumia , licha ya kwamba muda ulikuwa umeenda lakini walionekana uwa na ari kubwa.

Dakika chache tu  lilitolewa gauni la  rangi nyeupe  na  nyeundu kama main tone , ambalo limedariziwa  shingoni na Velvet , Chiffon  na vitambaa vingine vya rangi ya  dhahabu  na kutengeza shingo yenye upo la Almasi.

Baada ya Prisila kwenda kulivaa na kurudi wahudumu wa duka hilo walitoa macho kutokana na kupendeza kwake.

“Jamani  hilo gauni limekupendeza , ni kama vile  limetengenezwa kwa ajili yako  pekee”Aliongea muhudumu huku  akimuonea Prisila wivu kwa urembo wake.

“Prisila nakukumbusha  hili gauni ni kwa ajili ya matangazo ya duka letu”Aliongea mdada mmoja mweupe hivi  mwenye uso wa duara na mwanya.

“Hilda mbona unakumbushia sana  wakati naelewa , isitoshe hata kama  nataka kulinunua ni  bei  kubwa sana”Aliongea  Prisila na Hamza mara baada ya kusikia kauli ile alitoa simu  yake  na  aliingia  kwenye internet na kupiga  simu  kwenda nje ya nchi na  ndani ya dakika chache tu alianza kuongea  Kifaransa.

Na kitendo kile kilimfanya  Prisila kumshangaa Hamza   kwani  licha ya kwamba hakuwa akijua lugha ya kifaransa lakini kwa kusikia tu alikuwa  akiijua lugha hio ,  sasa  alishangaa  kuona Hamza anaongea tena kwa ufanisi mkubwa.

“Hamza  hicho ni kifaransa?”Aliuliza Prisila. “Ndio  ni kifaransa”Aliongea na  Prisila alionyesha ushangaa.

“Kumbe unajua  kuongea kifaransa tena unaonekana unaongea kwa usahihi kabisa ,  ulikuwa ukiongea na nani?”

“Nitakuambia baadae”Aliongea Hamza  huku akionyesha tabasamu , ndani ya dakika chache tu  walitoka ndani ya eneo hilo na kurudi kwenye gari kwani kila kitu kiliuwa kimekamilika kwa  upande wa Prisila.

Kutoka Malkia EmpireStylish  mpaka Mlimanni City  tukio linakofanyikia iliwachukua dakika  kumi   na mbili hivi na baada ya  Hamza kuiingiza Maybach ndani ya eneo hilo  Kamera za waandishi  zilianza  kumulika upande wao.

Hamza akiwa kwenye gari aliweza kumuona Dina akiwa ameshafika na alikuwa   juu ya redcapert.

Watu walionekana kuwa wengi ndani ya eneo hilo na ulinzi pia ulikuwa sio wa kawaida na haraka haraka ilionyesha kuna  kiongozi  mkubwa ambae  anakwenda kuhudhuria hilo  tukio.

Hata Prisila licha ya kwamba alikuwa na  hamu zote za kushiriki tukio hilo lakini baada ya kuona idadi hio kubwa ya watu maarufu mabimbali pamoja na Kamera  za Redcarpet wasiwasi ulianza kumwingia  , kwake ilikuwa ni mara ya kwanza kuhudhuria tukio kubwa la namna hio.

Previoua Next