Reader Settings

 

SEHEMU YA 82.

Waandishi wa habari walianza kujiuliza maswali wao kwa wao wakitaka kujua mwanamke alieshuka kwenye gari ya kifahari na kupendeza sana ni nani.

Prisila hakuzoea maisha ya Kamera hivyo aliishia kuinamisha kichwa chake chini kwa namna ya kutotaka sura yake kuonekana.

Hamza hata yeye hakujua ndani ya eneo hilo kungekuwa na vyombo vya habari namna hio  ,lakini yeye hakuwa na wasiwasi hata kidogo ,  kama  ni  matukio makubwa  alikuwa  ashashiriki  mara kibao  hivyo  alitembea kwa kujiamini.

Hamza na Prisila hawakusimama kwenye Zulia jekundu, Dina aliishia kuwakabidhi kadi zao mwaliko na kisha kuzionyesha na kuruhusiwa.

Baada ya kuingia kwenye ukumbi Prisila mwili ulimsisimka , kulikuwa  na watu wengi ndani ya eneo hilo   wengine wakiwa  ni watu wazito ambao  aliwajua lakini hakuwahi kuwa  na ukaribu nao huku eneo lilkiwa limependeza mno.

Wanaume kwa wanawake walimwangalia Prisila kwa macho  ya matamanio  na wivu , licha  wanawake wengi kupendeza waliona wivu kufunikwa na  Prisila mrembo ambae  sio maarufu.

Muda huo kabla hawajaelekea kwenye sehemu zao kukaa  sauti   ililiita jina la  Prisila.

“Kwaho wewe ndio  Prisila?”Ilikuwa sauti ya mwanamke

Kauli ile ilimfanya Hamza na Prisila wote kugeuka na macho kwa macho waliweza kukutana na Salma , Hamza alikuwa akimjua  ila upande wa Prisila alionekana kutomfahamu.

“Ni wewe tena?”Aliongea Hamza  huku akikunja sura.

“Hamza  huyu ni nani , ananijua lakini  mimi simjui”Aliuliza Prisila.

“Jina lake anaitwa Salma  ni mpenzi wake Saidi”

“Oh  kumbe! , mambo Salma”Alisalimia Prisila kwa upole  lakini upande wa  Salma  alionekana kutompenda waziwazi  Prisila.

“Sitaki salamu yako , nakupa onyo kaa mbali na  Saidi”Aliongea Salma  huku akiweka mwonekano wa kejeli mbele ya Prisila

“Hakuna kinachoendelea kati yangu na Saidi , hakikisha taarifa zako”Aliongea Prisila huku akishindwa kuamini  siku yake inaingia  dosari kwa kuanza kusingiziwa.

“Kwahio uaniona mjinga , Saidi  ametokea nyumbani kwenu  kwa ajili ya kukuchukua na ameenda mbali mpaka kukuandalia gauni . halafu unasema sina taarifa, huna aibu kuchanganya wanaume wawili kwa wakati mmoja?”Aliongea Salma akimjumuisha na Hamza na kauli yake ilimfanya Prisila kupaniki.

“Sina mahusiano yoyote na Saidi, ni ukorofi kuwaza kitu ambacho huna  uhakika nacho”Aliongea  Prisila huku akianza kutokufurahishwa na tabia  ya  Salma , lakini alijizuia maana  eneo hilo lilikuwa na watu wengi ambao walionekana kusikiliza mazungumzo yao.

“Salma unafanya nini?”Aliongea Saidi ambae alionekana kusogea  eneo hilo kwa spidi na alimwangalia Salma kwa macho makali mno kiasi cha  kumfanya  kuingiwa na wasiwasi kidogo

“Saidi naomba unisamehe , najua nilikukosea  usinifanyie hivi , huyu mwanamke hajui  kipi ni kizuri kwake na  hana thamani ya  kukupoteza muda wako”

“Sikia Salma usinikasirishe , nishawambia mimi na wewe basi , ondoka”Aliongea kwa hasira.

Salma uso wake ulikuwa na hasira mno , ijapokuwa Salma hakuwa maarufu sana lakini   alikuwa akitokea familia ya  matajiri kuliko hata Saidi  ambae  ni Mkurugenzi tu ndani ya shirika la mitandao ya simu.

Lakini licha ya mwanamke huyo kufokewa na Saidi hakukasirika  zaidi alimwangalia  Prisila kwa macho ya hasira mno.

Hamza mara baada ya kuona tukio hilo  alijiambia siku zote matajiri hawakosi cha kuchukia  kwa watu waliowazidi kipato.

“Saidi  mimi na wewe   hayajaisha bado”Aliongea  Salma kwa hasira na kisha aliondoka  na kuwaacha.

“Prisila umependeza  sana”

“Asante sana Saidi”

Hamza hakutaka kuendelea kusimama  na Saidi  maana ashaanza kumchoka  hivyo mara baada ya kuangalia upande ambao Dina yupo alimpa ishara ya kusogea.

Saidi licha ya kuonyesha kutoridhishwa na   Prisila kuwa karibu na  Hamza lakini hakuwa na chakufanya  kwa usiku huo.

Dina ndio ambae alionekana  kufahamiana na watu wengi mno  na ndio pekee aliekuwa bize huku Hamza na Prisila wakiwa wametulia wakisubiria  ratiba nzima kuanza.

Saa tatu kamili  karibia  wageni wote walioalikwa walikuwa wamekwisha kufika mpaka wale  wa  muhimu zaidi ambao walikaa viti  vya mbele ,  upande wa  Hamza wao walikaa  mstari wa tatu kutoka vilipo viti va VIP.

Hamza  hakuwa hapo kwa ajili ya  uzindunduzi huo wa albamu kabisa , alichokuwa akitaka ni kumuona huyo mwanaume ambae  inasemekana anajihusisha na  shirika la Utatu Giza.s

Dina upande wake alitaka kumsaidia   kwa namna yoyote Hamza lakini mpaka  uzinduzi unaanza  Dina  hakuonyesha ishara yoyote ya  kumuona mtu ambae alimtarajia na aliishia kumtingishia kichwa Hamza kumuashiria hayupo jambo ambalo  lilimfanya  kidogo  kutoyafurahia  matokeo maana alitaka kumaliza swala hilo  usiku huo huo.

Prisila upande wake hakuwa akijua hata kinachoendelea kutokana na umakini wake kuuelekezea jukwaani.

Wakati Hamza akijishawishi kuangalia uzinduzi huo  muda uleule simu yake ilianza kunguruma  ikiashiria ilikuwa ikiita , Hamza aliitoa haraka haraka  na kuangalia nani anapiga na namba ilionekana  ngeni  na  kumfanya akunje ndita.

“Prisila naenda msalani  mara moja”Aliongea Hamza  na Prisila aliekuwa amenogowa aliishia kutingisha kichwa.

Hamza mara baada ya kuingia msalani hakuchelewa kupokea   simu ile .

“Hello”

“You are Hamza?”Sauti    ya kingereza iliojaa  lafudhi ya kizungu ilisikik.

“It’s me”Alijibu  Hamza akimaanisha ni yeye.

“Not bad , its took me so long  to find out what the hell you are”

“Unataka nini kwangu na wewe ni nani?”

“Niite Van Bridge , najua  una mahusiano  na mwanamke anaeitwa Eliza  na upo ndani ya huo ukumbi kwa ajili ya kutafuta  watu  wanaohusika na Utatu , nimekupigia kukurahisishia misheni yako”Sauti ya majigambo ilisikika na kumfanya Hamza  kukunja sura huku akitoa tabasamu la kifedhuli.

“Ongea unachokitaka?”

“Kama unataka kumuona  baba mkwe  wako akiwa  hai ,  ndani ya msaa mawili yajayo  nikuone mjini Morogoro”

“Morogoro!”

“Ndio Morogoro  ndani ya masaa mawili”Sauti  hio iliongea na palepale simu ilikatwa.

Hamza aliishia kusimama kwa sekunde kadhaa  akififikiria cha kufanya , lakini alionekana kupatwa wazo hivyo alirudi alipomuacha Prisila na Dina.

“Prisila mimi nitatangulia , utaondoka  na Dina”Aliongea Hamza na Prisila alishangaa kidogo.

“Hakuna shida , mimi nishanogewa hapa”Aliongea na Hamza alitabasamu huku akimwangalia Dina.

“Nenda , usijali kuhusu Prisila nitahakikisha anarudi nyumbani salama”Aliongea Dina bila ya kuuliza Hamza anaenda wapi ila tu alijua atakuwa na haraka.

Hamza haraka haraka hakusubiri kuendelea kukaa ndani ya eneo hilo , baada ya kutoka nje alimpigia Eliza simu  wakutane  kituo cha Treni  ya Mwendokasi Posta, Eliza aliuliza kuna nini ila Hamza alimwambia atamwambia  akifika.

 Baada  ya kumaliza  kuongea alimtumia   Regina ujumbe wa meseji akimwambia ana dharula  na hatorudi nyumbani  na   upande wa Regina licha ya meseji kupokelewa haikujibiwa , ikionekana bado ana hasira juu ya kilichotokea mchana, ila Hamza aliona sio kipaumbele kumbembeleza  Regina kwa wakati huo , alihitaji kumsaidia Eliza kadri awezavyo ili asiwe na mawazo ya kukimbilia nnje ya nchi.

Nusu saa baadae Hamza aliweza kukutana na Eliza  akiwa tayari amekwisha kukata  tiketi na kwa bahati nzuri  walipata treni hio ya mwendokasi inayoelekea Dodoma.

“Kuna nini Hamza?”Aliuliza Eliza akiwa na wasiwasi huku akiangalia tiketi zilizokuwa kwenye mikono yake.

“Inaonekana baba yako hayupo hapa Dar kama ulivyofikiria , bali yupo Morogoro”

“Baba yupo Morogoro!!?”

“Ndio , waliomshikilia wamenipigia simu ,sijajua hata namba yangu wametoa wapi, tuingie kwanza tutaongea mbele ya safari”Aliongea Hamza  maaana ndio waliokuwa wa mwisho mwisho na Treni inataka kuondoka.

Kutoka  Dar es salaam mpaka Morogoro  ulikuwa mwendo wa   dakika sabini pekee.

Hamza na Eliza mara baada ya kutoka katika kituo hicho cha Treni  vijana watatu waliokuwa wamevalia suti waliwasogelea  na kuwaziba kwa mbele , kitendo kile kilimfanya Eliza kumwangalia Hamza.

“Mr Hamza tupo hapa  kukuchukua kwa maelekezo ya bosi”

“Bosi wenu  ndio  Van Bridge sio?”Aliuliza Hamza na wale wanaume  ambao walionekana ni mabodigadi walitingisha kichwa bila kuongea neno na kuwapa ishara   Hamza na Eliza wawafuate.

Mita kama miatatu  mbele walikuja kusimama  pembeni ya gari nyeusi Toyota Landcruiser  na  kumpa ishara Hamza kuingia.

“Hamza tunajiendea tu bila kuchukua tahadhari?”Aliuliza Eliza   akiwa na wasiwasi.

“Usiwe na wasiwasi,  lazima tufanye hivi kama tunataka kumuokoa baba yako”Aliongea na Eliza alitingisha kichwa kukubali.

Gari ile iliondolewa ndani ya maeneo hayo bila ya kuwa na maongezi yoyote kutoka kwa wale waliowachukua na safari ilitembea kwa muda mrefu  mno na kwakua Hamza hakuwa mzoefu sana wa mji huo hakuwa akijua ni  ueleko gani wanaelekea , kitu pekee alichokuwa akijua  wamekwisha kutoka  mjini tayari na  muda huo walikuwa kwenye mashamba ya mikonge ambayo barabara yake ilikuwa  ni ya  lami pia

Baada ya dakika kumi na tano mbele hatimae Hamza alielewa kinachoendelea, ilionekana walikuwa wameletwa hotelini.

Ilikuwa ni hoteli ya  hadhi ya nyota tatu  iliofahamika kwa jina la Troitsa na  mara baada ya Hamza kusoma jina hilo alijikuta akitoa tabasamu na kumfanya hata Eliza kushangaa kwanini Hamza  anatabasamu.

Baada ya  kushushwa nje ya gari  waliingia ndani ya hoteli hio wakitangulizana na wale mabodigadi mpaka eneo la  mapokezi.

“Mtapumzika hapa kwa usiku  na kesho  tutakuja kuwachukua na kuwapeleka kwa bosi”Aliongea mmoja ya wale mabodigadi huku akimkabidhi Hamza  ufunguo wa chumba.

“Kama alikuwa na mpango wa  kuonana na sisi kesho, kwanini  ametuharakisha kuja  kote huku  usiku usiku?”Aliuliza Hamza huku akionyesha hali ya  kukasirika kutokana na kuchezewa na watu hao ilihali wenyewe ndio walionekana kuwa wagomvi, ila Hamza  aliona avumilie tu aone  nini kinaendelea.

“Hamza  hatuwezi kulala kwenye chumba kimoja , tuchukue chumba kingine ili nikalale”Aliongea Eliza mara baada ya kuingia ndani ya chumba  walichopewa ,  Eliza alidhania kutakuwa na angalau vitanda viwili lakini  kilikuwa chumba cha kitanda kimoja pekee

“Eliza  tunapaswa kulala pamoja, unajua kabisa tupo  kwenye misheni hivyo  unapaswa kuwa karibu yangu kwa usalama ,isitoshe  hii hoteli  nina mashaka nayo”Aliongea Hamza huku akimshika Eliza  mkono.

Kwa kuona usiriasi aliokuwa nao Hamza , Eliza alishindwa kujua kama  kuna nia nyingine  ambayo  Hamza anakusudia  au ni sababu  tu ya kutaka kumlinda.

“Eliza unapaswa kuniamini?”Aliongea.

“Hapana nakuamini”Aliongea Eliza  huku bado akionyesha kuwa na wasiwasi  na  hali ya hewa ilionekana kuwa ya  ubaridi hivyo  hakuna ambae alienda  kuoga na waliishia kupanda kitandani na kulala.

Lakini licha ya muda kuwa umeenda,  Eliza alikosa usingizi kutokana na kuwa na mambo mengi kichwani kwake, hata Hamza hakutaka kulala moja kwa moja  , aliona atumie hio nafasi kuongea na Eliza.

“Eliza sikupata nafasi ya kukuuliza ,  ulijuaje  kuhusu ndoa yangu na Regina?”

“Ni Madame , bibi yake Regina alieniambia ..”Alijibu  Eliza kwa sauti ya chini  na Hamza  aliweza   sasa kuamini kile alichokuwa akifikiria ni kweli.

Ilionekana  Bibi Mirium alikuwa akifanya yote hayo kwa ajili ya Regina hivyo hakutaka kuongeza neno.

“Wakati tunaingia ulionekana  kutabasamu , sababu ilikuwa nini?”Aliuliza  Eliza.

“Ah!,mliniambia waliomkopesha baba yako  ni shirika linaoitwa Utatu , hii hoteli pia inaitwa Utatu ila wameamua  kutumia lugha ya Kirusi  ya  Troitsa”Aliongea Hamza.

“Unamaanisha Utatu kwa kirusi ni Troitsa?”

“Ndio”

“Kwanini mchana uliongezea  neno Black Trinity , maana mimi ninavyojua  Utatu ni  kama sehemu ya mafundisho ya kikristo?”

“Ndio , ila kama ninachodhania ni sahihi  ni tofauti na unavyofikiria , Black Trinity ni shirika la  ulimwengu wa Giza , lilianzia  kama Band  ya mziki na baadae likakua na kujitransform”Aliongea Hamza.

“Kwanini unaamini  hawa waliomchukua  baba ni hili shirika , kuna sababu yoyote  ya kuamini hivyo?”Aliuliza Eliza.

“Labda nikuambie kwa  njia hii pengine utaelewa ,katika dunia ya kawaida kuna sababu nyingi  za mtu  kufanya mapenzi  lakini katika ulimwengu wa giza kuna sababu  kuu  nne, Burudani , biashara, kuzaa  na kisha inakuja  sababu ya kuvuna  nguvu za  kiroho”Aliongea Hamza.

“Kuvuna nguvu za kiroho inakuwaje kuwaje?”Aliuliza Eliza akionekana kushangaa.

“Muunganiko wa ulimwengu wa kiroho  na ulimwengu wa nyama  ni kupitia hisia, kwa lugha nyepesi unaweza kusema hisia ni mlango wa kuingia kwenye ulimwengu wa kiroho, kitendo cha  mwanaume na mwanamke  kukutana kimwili  kuna matokeo mengi yanatokea   katika nafasi zao  kwenye ulimwengu wa kiroho , kuna  mafunzo maalumu ya kuvuna  nguvu za kiroho , ziwe nguvu za giza ama  za nuru kupitia kufanya mapenzi”

“Kwahio unaamini kama  ni huyu mbaba aliefanya haya yote kwa ajili ya kunitaka , unamaanisha  ni kati ya hizi sababu  unazoongelea?”Aliongea  Eliza akiwa  na mshangao.

“Ndio”

“Lakini wanawake  wapo wengi tena wazuri zaidi yangu , kwanini mimi ?”

“Katika ulimwengu wa kiroho kigezo cha  uzuri wa mwanamke  sio muonekano  ni ile nguvu ya kike unayozaliwa nayo , kuna  majina mengi sana  jinsi ya kuiita hii nguvu, Wewe ita ukike na Ukiume ,sasa kila mwanamke anakuwa na kiwango tofauti , kuna wanaozaliwa na kiwango kikubwa cha nguvu hii ya  Ukike  na  aina hii ya wanawake unaweza kuwatambua katika ulimwengu wa kawaida kwa bahati zao  na  mvuto, hujawahi kuona mwanamke ni wa kawaida lakini  wanaume wanapanga foleni au mwanake ni mzuri  lakini  hana mvuto mkubwa?”Aliuliza Hamza na Eliza alitingisha kichwa kuitikia kama ni kweli.

“Hivyo kwa upande wako wewe , umezaliwa  na kiwango kikubwa   cha nguvu ya kiroho  na  pia nguvu yako haijapotea kwa kukutana na wanaume wengi kimwili?”

“Kwahio  nguvu unazaliwa nayo lakini inapungua kadri unavyokutana na  mwanaume kimwili?”Aliuliza Eliza huku akionyesha kushangaa mno maana ni kama anajifunza kitu kipya.

“Sio lazima lakini  ni kweli nguvu inapungua , inategemea unakutana kimwili na  mwenza kwa malengo yapi , kama unakutana nae  kwa ajili ya  kunyonya nguvu zake  basi  wewe utafaidika kwa kuimarisha nguvu zako ,  kama mnafanya kwa ajili ya kujinufaisha wote wawili  basi  nguvu zenu zinabakia palepale ,ila kama  unaefanya nae ana malengo ya kunyonya nguvu yako ya  kiroho basi za kwako zinapungua,  mwanamke hata ajiweke msafi  vipi , hata  afanye upasuaji mara ngapi kuongeza urembo  kama  amekutana na wanaume wengi na wakamtumia kwa ajili ya kujiimarisha kiroho mvuto wake utapotea na  ataishia kukosa soko , umoja   huu wa siri wa Black Trinity   wanachama wake  wanafanya mapenzi kwa  ajili ya kujiimarisha kiroho na wanawake hao  wanapimwa  kiasi cha nguvu  wanachokibeba kabla ya kuwa shabaha , hivyo kama  huyo mbaba  ni mshirika basi moja  kwa moja anakutaka kimapenzi kama host , hii haipo kwa mwanamke ipo , yote niliokuelezea yanatokea pia kwa upande wa  wanaume

Eliza wewe  licha ya kuwa mrembo  una mvuto   mkubwa mno wa  nguvu ya kiroho ndio maana  wanaume wanakuwinda  , ikitokea ukiwa na ukaribu na mwanaume mwenye  nguvu   za ukiume  hafifu  itaonekana ni kama umemuwekea Limbwata..”Aliongea Hamza huku akicheka.

“Hee! , Kumbe  dunia ina mambo mengi namna hii?”

“Dunia ina mambo mengi sana Babe ,Unadhani  watu mashuhuri wanaoandamwa na kesi za kulawiti watoto  na kubaka  ni kwasababu wamekosa wanawake , kila kitu  kinatokea  kwasababu  maalumu, zipo ‘organisation’ nyingi za  kiroho kama hii  ambazo zinalea watu mashuhuri ikiwemo   viongozi  wakubwa wa kidini”Aliongea Hamza na Eliza alijikuta mwili ukimsisimka , alijifikiria maisha yake ni kama  kila alichoongea Hamza kina ukweli ndani yake.

“Vipi kama ukipendana  na mtu bila ya kufanya mapenzi?”

“Unaongelea True love ,  au  love with no reason ,  unajikuta  mnapendana  sana lakini hakuna sababu yoyote kati yenu ya kufanya mpendane , huu muunganiko wa  kiroho wa  namna hii ni ngumu kuuvunja katika ulimwengu wa kiroho ,  penzi hili linaweza  kupitia  misuko suko na hata  wenza kutengana na kuendelea  na maisha mengine  lakini  kama mmefungwa na  Nira  za  kihisia  ,mkitakana tena ni ngumu  sana kujizuia”

“Wewe na Regina penzi lenu ni la aina gani?”Aliuliza Eliza.

“Babe Eliza  ya Regina yamekujaje hapa , hebu sogea karibu kidogo nikukumbatie basi”Aliongea Hamza huku akisogea lakini Eliza alimkwepa.

“Sitaki , wewe ni mume wa bosi wangu , hatuwezi  kukumbatiana , sitaki unitumie kiroho mimi?”Aliongea Eliza  na kumfanya Hamza kutamani kulia na kujiambia umbea wake unamkosesha fursa.

“Kama  Bibi  yake ndio aliekuambia  kuhusu swala la ndoa yetu , basi utakuwa unajua pia   tumeandikisha ndoa mimi na Regina kwa ajili ya hisa za kampuni ,  sikatai ni kweli nampenda Regina  lakini hata wewe nakupenda”

“Kama  umemuoa  bosi Regina huwezi kunipenda na mimi”

“Kwanini ,  unataka kusema binadamu anaweza kuuzuia moyo wake uliongezeka ukubwa kwasababu ya mtu?”

“Huo moyo unaemuongezekea ukubwa ndio unaemuoa ,  ipo hivyo”Aliongea  Eliza huku akijikunyata  kwenye ukingo wa kitanda.

“Labda iwe  hunipendi  ila sitokukatia tamaa , nishakuambia kuhusu hili au umesahau?”Aliuliza Hamza lakini  Eliza hakujibu kitu zaidi ya kukaa kimya.

Hamza  aliwaza namna ya kumsogeza  karibu  Eliza bila ya kutumia nguvu na baada ya kupata mbinu   alitoa tabasamu.

“Ngoja nikusimulie  simulizi moja ya kusisimua”

“Simulizi gani?”

“Wewe sikiliza itakufanya ulale kwa  haraka”Aliongea Hamza huku akijiambia ngoja tuone baada ya hii simulizi utaendelea kujikunyata au utakuja kwenye kifua changu.

“Kuliwahi kutokea  wanandoa wawili ambao  walikuwa wakigombana kila siku kwa kufokeana , siku moja  ugomvi wao ulikuwa mkubwa  mno kiasi cha kuanza kupigana, mume alichukua kisu  na bila kudhamiria  alijikuta akimuua mke wake kwa kumchoma nacho  tumboni ,  baada ya  tukio hilo ili mume kuficha kile alichokifanya alimbeba  mke wake  kimya kimya na kwenda kumzika msituni , lakini hata bado alikuwa akiogopa  mtoto wake  wa kiume atauliza ni wapi alipo mama yake  akisharudi nyumbani  hivyo hakujua ni namna gani atamjibu mtoto , lakini sasa baada ya yule baba kurudi nyumbani  siku ya kwanza  ilipita , hatimae siku ya pili  mpaka ya sita  yule mtoto  hakuwahi kuuliza  mama yake  yuko  wapi , kitu kilichompelekea yule mume   kuona kuna kitu hakipo sawa , hivyo  alichukua jukumu la kumuuliza mtoto wake”

“Mtoto wangu  hujamuona mama yako kwa  muda mrefu , kwanini  huulizi alipoenda?”Aliuliza yule baba lakini ajabu yule mtoto alimwangalia  baba yake kwa namna ya kushangaa  lakini alijibu.

“Baba kwanini unaniuliza mama alipoenda wakati umembeba mgongoni na hutaki kumshusha…”Kitendo cha Hamza kufikia hapo  Eliza alijipeleka mwenyewe kwenye mwili wa Hamza kwa kuanza kuhisi woga.

Hamza aliishia kutoa tabasamu la ushindi  kana kwamba ameokota  embe chini ya  mparachichi.

“Hehe .Eliza  najua unanipenda sana..”Aliongea huku akinusa harufu ya marashi  kutoka kwenye nywele zake.

“Umenifanyia makusudi  kunisimulia simulizi ya kutisha..”Aliongea Eliza kwa sauti nyororo.

Hamza aliishia kuinamisha kichwa chake na kumbusu kwenye paji la uso, kitendo kilichomfanya  Eliza ajihisi yupo kwenye mikono  salama na hakuna kitu ambacho kinaweza kuuogopesha tena.

“Lala sasa , nitahakikisha baada ya kesho kila kitu  kinakuwa sawa  na utaishi kwa amani”Aliongea  Hamza huku akimpeti peti na hatimae mrembo huyo alipotelea usingizini muda mchache tu.

Asubuhi kulivyokucha  bwana alieitwa Van Bridge hakutuma  watu kuja  kwa haraka  jambo ambalo lilimfanya  kuona ni kama anacheleweshwa  , hivyo bila ya kujifikiria mara mbili mbili alitumia ile namba iliompigia jana  na kupiga.

“Hamza wewe ni kijana jasiri sana  mpaka kukikipigia kifo simu , yaani mimi  hata sitaki kukuua lakini wewe unanipigia?”

“Mmekuja, mmeniweka kwenye hoteli yenu bila  maelekezo ya kutosha  kwanini nisipige , kama unaniogopa kuwa  muwazi”Aliongea Hamza.

“Unaongea ujinga , yaani nikuogope wakati nazungukwa na mabodigadi zaidi ya mia, kama nisingekuwa  bize  ningeshatuma watu  kukuua”

“Wewe sema uko wapi?”

“Unataka kujileta kwenye  mdomo wa mamba?”

“Wewe sema unapatikana wapi , mimi nitakuja  na kukutafuta , kama unaniogopa  basi chukulia sijaongea chochote , nitatumia njia nyingine za kukupata”

“Afraid! , I, Van Bridge  have been  out here for thirty  years  and I don’t know how to write  word ‘fear’, kama unakitaka kifo  fanya uone”Aliongea kwa ubabe  na simu ilikatwa palepale.

Hamza alijikuta akishangaa , inamaana hao watu wamemleta hapo kumchoresha, lakini hata hivyo hakutaka kuwaza sana.

Muda huo huo mlango  wa chumba chao uligongwa na Hamza mara baada ya kwenda kufungua alikuwa ni mhudumu aliemwagiza  kifungua kinywa.

Lakini  bila kutarajia yule mhudumu wa kike alimpatia Hamza  kikatarasi  mkononi na  baada ya kukifungua aliweza  kusoma  neno ambalo hakulielewa mara moja na ilimfanya  na Eliza kuwa na shauku.

“Kimeandikwa Shamba la Mzungu”Aliongea Hamza na Eliza  alionekana kuelewa neno  lile mara moja.

“Ninavyojua mimi Shamba la Mzungu  ni  hospitali  ya kuhudumia  wagonjwa wa muda mrefu wasiojiweza”Aliongea Eliza.

“Unamaanisha ni Sanatorium?”

“Ndio , miaka  kadhaa iliopita sehemu hio ilivuma  kwa  kashfa ya  kuiba viungo vya  wagonjwa waliofariki , lakini   serikali ilikuja kukanusha baadae”

“Umesema kuiba viungo?!!”Aliongea  Hamza na swali lile  lilimfanya Eliza na yeye akili kumkaa sawa.

“Baba..!!!”

Eliza alishituka huku akiamini kinachoendelea huko pengine ni baba yake kuondolewa figo  au moyo  kulipia deni.

Hamza na yeye ni kama sasa  anaamka  , mwanzoni  akili yake ilijua pengine  ni mchezo wa kumfanya Eliza akubali kutumika lakini hisia zingine zilimwingia mara baada ya kujua  pengine  mchezo uliochezwa ni  kwa ajili ya Mzee Mlowe kuuza kiungo cha mwili kulipia deni.

“Eliza usiwe na wasiwasi , ngoja tuwahi”Aliongea Hamza akimtuliza Eliza na  kwa haraka sana walichukuana na kutoka nje ya  hoteli hio  na kisha waliita taksi iwapeleke Shamba la Mzungu

Hamza alijiambia kama wamevuna viungo vya baba mkwe wake atalipua eneo lote.

Baada ya  kupanda taksi iliwachukua  saa moja na  dakika kadhaa kufika , ilikuwa ni sehemu ambayo ipo ndani ndani, licha ya barabara yake kuwa nzuri

Kwa mbali tu Hamza aliweza kuona majengo mengi ya ghorofa yaliokuwa ni kama  chuo  hivi  na   mazingira kusogelea eneo hilo yalikuwa  safi kabisa na kulikuwa hadi na kibao kiliochoandikwa  Bridge Sanotarium.

Previoua Next