Reader Settings

Teri meri, meri teri prem kahani hai mushkil

Do lafzon mein yeh bayaan na ho paaye

Ik ladka ik ladki ki yeh kahani hai nayi

Do lafzon mein yeh bayan na ho paaye

Yours and mine, mine and yours, love story is difficult,

can't tell it in two words,

This story of a girl and a boy is new,

can't express it in two words..

Teri meri, meri teri prem kahani hai mushkil

Do lafzon mein yeh bayaan na ho paaye

Ik dooje se hue juda Jab ik dooje ke liye bane

Yours and mine, mine and yours, love story is difficult,

can't tell it in two words,

Separated from each other when made for each other..

Tumse dil jo lagaya toh jahaan maine paaya

Kabhi socha na tha yoon meelon door hoga saaya

Kyun khuda tune mujhe aisa khwaab dikhaya

Jab haqeeqat mein use todna tha

When I loved you, I got the world,

but never thought (even) your shadow will be miles away,

O god why you gave me such a dream,

when you had to break it in reality..

Ik dooje se hue judaa, jab ik dooje ke liye bane

Teri meri, meri teri prem kahani hai mushkil

Do lafzon mein yeh Bayaan na ho paaye

Teri meri baaton ka har lamha sabse anjaana, 

do lafzon mein yeh bayaan na ho paaye

Every moment of your amd my talks is unknown to all else

can't express it in two words..

Har ehsaas mein tu hai har ik yaad mein tera afsaana

Do lafzon mein yeh bayaan na ho paaye

You're in every feeling, and your story in every memory

can't express it in words..

Sara din beet jaaye, Saari raat jagaye

Bas khayal tumhara lamha lamha tadpaye

Yeh tadap keh rahi hai mit jaaye faasle

Tere mere darmayaan hai Jo saare

 The entire day passes, all the night I am awake,

Your thought troubles me day and night,

this longing is saying that the distances should go

which exist between you and me..

Ik dooje se hue juda Jab ik dooje ke liye bane

Teri meri baaton ka har lamha sab se anjaana

Do lafzon mein yeh Bayaan na ho paaye

Har ehsaas mein tu hai har ik yaad mein tera afsaana

Do lafzon mein yeh bayaan na ho paaye

Teri meri, meri teri prem kahani hai mushkil

Do lafzon mein yeh bayaan na ho paaye

Ni moja ya wimbo bora sana kwenye historia ya mapenzi duniani, ni muziki ambao unapatikana kutoka kwa moja ya waigizaji bora sana kutoka bara la Asia ndani ya taifa la India, anaitwa SALMAN KHAN (THE BIG BOSS) pamoja na Himesh Reshammiya japo waimbaji wa wimbo huo ni Rahat Fateh Ali Khan, Shreya Ghoshal. Jina la wimbo unaitwa TERI MERI unapatikana kwenye movie ya BODYGUARD yakwake SALAMAN KHAN wakati akiwa anamwimbia mtoto wa bosi wake ambaye alimpenda Kwa siri muda mrefu sana bila SALMAN KHAN mwenyewe kujua kwa sababu yeye alikuwa ni mlinzi wa mtoto huyo wa kitajiri.

Huo wimbo haukuja tu bali zilikuwa ni kumbukumbu nzito ambazo zilikuwa zinakisumbua kichwa cha mwanaume mmoja akiwa ndani ha gari yake akiwa anamuwahi yule nyonga mkalia ini wake, Markvelous Japhary ndiye mwanaume ambaye alikuwa anayakumbuka maneno matamu sana ya kwenye huo wimbo yalimpeleka mbali sana na kumfanya afute machozi yake usoni.

Miaka kadhaa iliyopita nyuma alikuwa akiyasikia hayo maneno kutoka kwenye kinywa cha mtu ambaye alikuja kukiri mbele ya dunia kwamba alimpenda sana mwanamke huyo, alijitahidi sana kuweza kuficha lakini bahati mbaya sana ulimwengu ulitaka kumuumbua na maradhi yake hakuweza tena.

LOVERS DREAM LOUNGE

Ilikuwa ni lounge moja ya kisasa Kwa aina yake ambayo haikuwa mbali sana na barabara kubwa ambayo ndipo magari mengi sana yalikuwa yanapita, siku moja kijana mmoja baada ya kumaliza elimu yake ya kidato cha sita alikuwa na kazi nzito sana ya kumpambania mdogo wake wa damu ambaye naye alikuwa akimsomesha mwenyewe, licha ya kusubiri majibu yake ya kuweza kwenda kuendelea na elimu yake ya chuo kikuu alikuwa anapambana na mtaa ili kuweza kumuandalia mazingira mazuri mdogo wake ambaye alimpenda sana kwenye maisha yake, hakuna kitu kingewekwa mfano wa kulinganisha na namna alivyokuwa akimpenda na kumjali ndugu yake wa pekee. Usiku mmoja akiwa.anatoka kwenye moja na mbili za kutafuta chochote kitu ili mdogo wake aamke na furaha ya aina yake ndipo alipo bahatika kupita kwenye lounge hiyo ambayo ilikuwa ni maarufu sana kwa sababu ilikuwa ndiyo njia ya yeye kupita kila siku.

Leo ilikuwa ni tofauti kidogo alivuka Ile sehemu lakini nafsi yake iligoma kabisa akaamua kurudi hatua mbili ili aamini kama masikio yake yalikuwa yanamdanganya au yalikuwa yapo sahihi kama.alivyohisi, baada ya kurudi zaidi hatua kama kumi nyuma ndipo alipopata bahati ya kukithibitisha kile ambacho alikisikia. Ni moja ya sauti nzuri sana ambazo hakuwa na uhakika kama aliwahi kuisikia mahali popote pale tangu ujio wake kwenye huu ulimwengu, ilikuwa ni sauti ambayo ilimfanya ayafumbe macho yake kwa hisia nzito sana ilimpenya vilivyo alijikuta mpaka machozi yanamtoka, lakini mpaka muda huo alikuwa hata hajajihangaisha kugeuka na kumuangalia ambaye alikuwa anaimba huo wimbo.

TERI MERI ndio wimbo ambao alikuwa anausikia kutoka kwenye sauti moja nzuri sana na ndio wimbo ambao ulimfanya atoe machozi Kwa namna ulivyoweza kuziteka hisia zake za ndani kabisa, aliyafumbua macho yake na kugeuka ile sehemu ambayo alikuwepo mtumbuizaji japo alikuwa nje ila ndani palikuwa panaonekana vizuri sana, bahati mbaya ilikuwa kwake alishuhudia tu gauni moja la kisasa sana kutoka kwenye mwili ambao bila shaka MUNGU alitenga muda wa kutosha kuutengeneza kwa hicho kiumbe, gauni lilikuwa linaishia kwenye chumba ambacho ni wazi kilikuwa ni cha kubadilishia nguo, alijikuta anatabasamu na kutamani sana kuweza kumjua mwanamke huyo ila alijua hicho kitu hakiwezekani Kwa sababu alikuwa ameshachelewa tayari.

"Princes prisca atakuwepo hapa kwa wiki nzima hapa kwa ajili ya kuwapatia burudani hivyo kesho muda kama huu atakuwa yupo live tena mwambie na mwenzako hakikisha haukosi" ni sauti kutoka kwa mwanaume mmoja ambaye bila shaka hakuhitaji maelezo mengi kutambulika kama ni MC wa ile lounge. Hayo ni maneno ambayo yalimuingia vizuri sana kijana huyo akijiapia kesho yake lazima awahi hilo eneo ili aweze kufaidi kwa umakini sauti hiyo pamoja na kuitazama sura ya mwanamke huyo ambaye hakufanikiwa hata kumuona.

Markvelous alijifuta tena machozi akimhitaji dereva wake aongeze zaidi kasi ya gari ili aweze kuwahi nyumbani kwake alikuwa na wasiwasi mno.

Huenda umesha unganisha doti kinacho fanyika, unahisi hizi nyimbo zimeingiaje kwa huyu mwanaume?

Najua huenda imekugusa sana ila nadhani muda utaamua kukupatia kisa hiki cha kusikitisha sana chenye mapigano ya hali ya juu mno.

Usikose kutoa like na comments ili niweze kuleta mwendelezo, bila likes na comments mimi mwenyewe naona uvivu wa kuleta hadithi ndiyo maana muda mwingine zinachelewa sana kama ulikuwa unajiuliza nini tatizo nadhani utakuwa umenipata.

Bux the story teller

Previoua Next