CHANGE 2
A Story by Elton Tonny
Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA NNE
★★★★★★★★★★★★
Draxton anafumbua macho yake na kujikuta yupo ndani ya chumba chake kidogo. Kabla hajajiuliza ni jinsi gani alifika hapo, anavuta harufu nzuri sana kwake anayoifahamu vyema, naye anafumba macho kuisikilizia vizuri zaidi. Anafumbua macho yake na kugeuza shingo yake upande mwingine wa kitanda, na hapo anamwona Namouih, akiwa amelaza kichwa chake kitandani karibu kabisa na chake, na akiwa amesinzia kwa kile kilichoonekana kuwa uchovu. Kiganja cha mwanamke huyo bado kilikuwa kimeshika kitambaa chake alichotumia kumkandia, naye Draxton alipojitazama mwilini akaona ni taulo tu ndiyo iliyokuwa imemsitiri.
Akatazama juu tena na kubaki kutafakari vitu. Mwanamke huyu hakutakiwa kuwa hapo. Ni kwa nini alikuwa na king'ang'anizi sana? Na kama ni jambo lingine lililomchanganya ilikuwa ni wakati alioamka. Kwa uzoefu wake alitambua kwamba bado haikuwa imefika alfajiri, ikimaanisha ni muda mfupi tu ulikuwa umepita tokea alipobadilika mpaka kufikia sasa. Ni nini kilichokuwa kimefanya awahi kurudia hali ya kawaida kabla ya asubuhi kufika kabisa? Namouih alikuja huku wakati gani? Maswali hayo kichwani kwake yalimpa wazo fulani, wazo ambalo hakutaka kabisa liwe ndiyo sababu ya haya yote kutokea. Ikamfanya akumbuke vitu vingi mno, naye akaingiwa na simanzi.
Akaanza kusikia sauti za kuguna kutoka kwa Namouih, na alipomtazama akagundua kwamba alikuwa anaota, tena ndoto mbaya maana uso wake ulionyesha kutatizika. Ikambidi Draxton ajinyanyue na kuketi, akihisi maumivu mwilini kama ya mtu aliyeanza kufanya mazoezi ya viungo, naye akaifunga vizuri zaidi taulo kiunoni halafu akarudi kulalia ubavu wake mmoja ili amwamshe mwanamke huyu mrembo kwa ustaarabu. Akawa anapitisha kiganja chake nyuma ya kichwa cha Namouih huku akimpuliza usoni taratibu, na hisia ambayo mwanamke huyu alipata ikaanza kusaidia ndoto imwondoke na yeye kuanza kurejesha ufahamu wake kwa kuamka.
Akafumbua macho taratibu, akiwa bado na kumbukumbu ya ndoto mbaya ya muda mfupi nyuma, lakini hakuhisi msisimko wa hofu. Kufumbua kwake macho kulimkutanisha na uso wenye kujali wa Draxton, na kwa sekunde chache akabaki kumtazama tu kwa umakini. Kwa sasa Draxton alikuwa amerudia hali yake ya kawaida, lakini nywele zake kichwani zilikuwa nyeupe bado na ndefu, zilizofunika pande za kichwa chake kufikia mbele ya paji lake la uso kwa njia fulani utadhani alikuwa amevaa wigi.
Namouih akanyanyua kichwa chake na kufikicha macho yake kisha kuendelea kumtazama, naye Draxton akazirudisha nywele zake nyeupe upande mmoja wa bega ili uso wake uwe wazi zaidi, na wakati huu alikuwa akimwangalia Namouih kwa njia fulani kama anasubiri aseme ni kwa nini alikuwa sehemu hiyo kwa wakati huo.
"Umeamka zamani?" Namouih akauliza kwa sauti ya chini.
Draxton akabaki kumtazama tu.
Namouih akachukua simu yake pembeni kuangalia muda, naye akakuta ni saa tisa usiku. Akamtazama Draxton tena. Yaani alionekana kama mvulana mdogo usoni kwa jinsi ambavyo nywele zake zilipendezesha kichwa chake, na Namouih alielewa kwamba bila shaka zingehitaji kunyolewa baadaye.
"Mbona unaniangalia hivyo?" Namouih akauliza baada ya kuona amekaziwa macho tu.
"Nilikwambia nini Namouih? Na wewe umefanya nini?" Draxton akauliza.
"Hiyo ndiyo asante ya kukutoa msituni usiku ukiwa uchi?"
"Sikuhitaji msaada wako. Namouih... inapokuja kwenye suala hili nakuomba ukae mbali na mimi. Unajihatarisha bila sababu yoyote ile ili iweje? Kuonyesha kwamba unanijali sana au?"
"Kwani ni dhambi kukujali?"
"Uliniambia nibaki nikusaidie... masuala mengine yaache kama yalivyo, nitadili nayo mwenyewe. Kaa mbali na mimi Namouih!"
"Kwa nini unakuwa mkali? Shida ni nini Draxton?"
"Shida ni kwamba...."
Draxton akaishia hapo na kubaki amemwangalia tu mwanamke huyo machoni. Namouih aliweza kutambua kwamba kuna kitu kilichokuwa kinamfanya mwanaume huyu aogope sana kumuumiza, kumaanisha alimjali pia, lakini akawa anataka kujua hicho kitu ni nini hasa.
"Niambie. Nielezee ni kwa nini hutaki niwe karibu yako kukusaidia hata ingawa... hata ingawa ninajua hautaniumiza," Namouih akasema.
"Usiwe na uhakika kwamba sitakuumiza Namouih, ni kwamba bado tu sijakuumiza, na wewe unavyoendelea kujisogeza kwangu ndiyo unalikaribisha hilo," Draxton akamwambia.
"Ni nini kilitokea Draxton?" Namouih akauliza kwa upole.
Draxton akabaki tu kimya.
"Niambie... tafadhali... ninataka kukuelewa vizuri zaidi Draxton..."
Draxton akajivuta kutoka kitandani huku akisema, "Hautakiwi kuelewa lolote... na ilikuwa makosa mimi kubaki huku."
Akazifata droo na kutoa T-shirt moja nyeusi ili avae.
Namouih akanyanyuka kutoka kwenye kiti na kumsogelea huku akisema, "Draxton usiseme hivyo. Niambie tafadhali. Huu woga wako wa kuniumiza unatokana na ile kauli kwamba sikuzote ni lazima tatizo litatokea ukianza kumjali sana mtu, si ndiyo? Lakini haliwezi kutokea endapo kama huyo mtu hajui kuhusu siri yako, na kwa hii instance ni mimi ndiyo ninayejua na si Blandina. Kinachofanya ufikiri utaniumiza ni kwamba nimeendelea kujiweka karibu nawe, lakini mbona hata ulipokuwa umegeuka kuwa mnyama mara ya kwanza nakuona vile haukuniumiza? Kuna jambo lingine Draxton... jambo lingine linalokusumbua. Na nafikiri ni kwa sababu yangu. Tafadhali niambie..."
Namouih aliongea kwa hisia sana. Draxton akawa anamwangalia tu kwa umakini huku mwanamke huyo akionyesha hamu ya kutaka kujua ukweli.
"Niambie. Ni kwamba... unanijali mimi zaidi hata ya unavyomjali Blandina?" Namouih akauliza swali hilo moja kwa moja kabisa kuonyesha ni jambo alilokuwa ameshafikiria mapema.
Draxton akamwangalia kwa umakini sana, akiona hapa hakukuwa na haja tena ya kumficha mwanamke huyu ukweli. Akavaa T-shirt yake na kuangalia chini kwa sekunde chache, kisha akatikisa kichwa chake kukubali na kusema, "Ndiyo... uko sahihi. Lakini siyo MIMI."
Jibu hilo likamchanganya Namouih kiasi. "Unamaanisha nini?" akamuuliza.
"Ni upande wangu wa pili ndiyo unakujali namna hiyo Namouih," Draxton akasema.
"Excuse me?!" Namouih akashangaa.
Draxton akaifunga droo taratibu huku akionekana kuingiwa na huzuni. Pamoja na kwamba jambo hilo lilimshangaza, Namouih alijua kulikuwa na kisa cha kina zaidi kilichofanya liwe baya kwa mwanaume huyu, naye akamshika mkononi taratibu.
"Draxton... nieleweshe. Hilo linawezekanaje? Yaani... huyo mnyama ana hisia kwangu?" Namouih akauliza.
"Ni jambo gumu lakini... huwa inatokea... imeshatokea," Draxton akamwambia.
Namouih akaendelea kumwangalia kwa umakini, naye Draxton akaegamia kabati yake ya droo huku akionekana kuwa na simanzi usoni.
"Ilianza na mama. Mama yangu... mama yangu ndiyo pekee aliyeweza kuzoeana na huu upande wa pili kwa sababu nilikua nikiwa naye kwa miaka mingi... kwa hiyo upande huu ukajifunza kumjali pia... kama tu mnyama wa kufugwa. Kuna vitu nilikuwa navitamani maishani hasa kama kijana, niwe natembea, niwe na marafiki, michezo, kwenda shule pamoja na wengine... na hata kuwa na girlfriend pia..."
Draxton akasema hayo na kutabasamu kidogo, naye Namouih akatabasamu pia lakini kwa njia ya huruma.
Draxton akaendelea kusema, "Ilikuwa ngumu sana kwangu kuishi kwa kujificha, nilijiona kama mfungwa ingawa nilikuwa na company yake, na kwa sababu ya kutoridhika nikajaribu kutoka nje siku moja ili nikajifurahishe... nikajichanganye na watu yaani.... ikaanza kuwa zoea. Muda si muda nikawa simsikilizi mama kwa kujiona nina control nzuri.... usiku mmoja nikaondoka tulipokuwa tunaishi na kwenda mbali sana bila kumwambia chochote. Nilikoenda.... nilipoteza control na kuua watu 26 Namouih... watu 26!"
Namouih akatikisa kichwa kwa kusikitika.
"Vifo vya watu wengi namna hiyo... sababu ikiwa ni mnyama mkali, oh labda ametoroka zoo, labda kaingia town kutoka milimani, hivyo ndivyo wengi walivyowaza lakini hawakuweza kumpata huyo mnyama kwa sababu haikuwa mnyama kwa asilimia zote. Ilikuwa ni mimi. Mimi ndiyo niliyewaua..."
"Hapana Draxton, usiseme hivyo..."
"Kama tu ningebaki ndani... na mama yangu... nisingeamka sehemu ya mbali nikiwa na damu za watu midomoni mwangu..."
Namouih akafumba macho na kuinamisha uso chini.
Draxton akavuta pumzi na kuishusha kwa nguvu, kisha akaendelea kusema, "Kwa hiyo... ikiwa kama muujiza tu kwamba sikukamatwa, nikarudi kwa mama... muuaji. Haijapita muda mrefu nikagundua kwamba alikuwa na cancer kwenye ini... stage 4... na hakukuwa na njia yoyote ya kumwokoa tena maana hata hospitali alizojaribu kuulizia uwezekano wa transplant kwa hali yake ilishindikana. Sikutaka aniache, lakini akaniacha. Mtu pekee aliyeweza kunitunza vizuri nikiwa na hali yangu akaniacha. Hata damu yangu haikuweza kumsaidia. Sikutaka kuendelea kuishi tena. Nilijaribu kujiua mara nyingi, na kila mara upande wangu wa pili ulipotoka kwa sababu ya mimi kufanya hivyo ningesababisha vifo. Haikuwa rahisi kunitia hatiani kwa sababu kilichofatiliwa ilikuwa ni mnyama na siyo mtu ambaye wangekuja kukuta amelala tu barabarani. Katika kufanya hayo yote nilikuwa navunja ahadi ambayo nilimpa mama kabla haja.... nilimwambia ningeendelea kuishi kwa siri na kujitahidi nisimuumize yeyote, lakini nikaivunja!"
Draxton akiwa anasema "nikaivunja" alikuwa anajipiga kwa nguvu kichwani, naye Namouih akaushika mkono wake ili kumzuia. Mwanamke akaendelea kumtazama kwa hisia sana, akielewa kwamba bado kuna mengi aliyotakiwa kujua.
"Kila sehemu niliyokwenda... yaani... ikawa wazi kwangu kwamba hakuna kitu ambacho kingeweza kuniondoa duniani, na sikutakiwa kujipeleka kwa watu kwa sababu only God knows wangeitumia vipi damu yangu ikiwa ningejionyesha kwao. Mama alikuwa ameniambia niendelee kutafuta sababu ya kuishi hata kama nitabaki kuwa mwenyewe... kwamba ipo sehemu fulani inanisubiri... na baada ya muda fulani Namouih... niliipata. Niliipata nilipokwenda Venezuela. Nilikutana na mwanamke mwenye moyo mzuri sana. Na ilikuwa kwa bahati mbaya tu lakini nilimpenda. Nilimpenda sana. Ila kilichokuja kunifanya nitambue kwa nini nilimpenda sana ni kujua kwamba upande wangu wa pili ulimpenda pia. Ulimpenda the same way kama ulivyokuwa unampenda mama, kwa hiyo mbele yake... upande wangu wa pili ungekuwa dhaifu. Ah... Namouih sijui hata ikiwa unaelewa nayokwambia...."
"Ndiyo naelewa Draxton... tafadhali endelea..." Namouih akasema kwa hisia sana.
"Angalau kufikia wakati huo niliweza kujichanganya na watu, na nilikuwa nimeanza kuzoea tabia za upande wangu wa pili kwa hiyo niliweza kuwa mwangalifu. Vitu, au tabia za watu zingeonekana kuwa kawaida kwangu, lakini ilipokuja kwa Ramona, kila kitu kumhusu kilikuwa kizuri kupitiliza. Aliitwa Ramona... alikuwa... special. Na yeye alikuja kugundua kuhusu hali yangu lakini sikumuumiza kama nilivyohofia. Alikuwa tayari kuwa nami licha ya hilo, na alinisaidia sana kila mara ambapo ningebadilika ili watu wengine wasijue. Alikuja kufikiri kwamba ningeweza.... kulala naye bila kumuumiza, akiniambia imani yake kwangu ina nguvu nyingi itakayonisaidia kuweza ku-experience jambo hilo zuri kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu... lakini nilijua wazi hilo lisingewezekana. Nilimwambia sana tusifanye hivyo lakini akanitia moyo kwamba angeweza kunisaidia.... Namouih... nilimuua kwa sababu ya jambo hilo... nilimtafuna Ramona, Namouih!" Draxton akasema hayo huku machozi yakijaa machoni mwake.
Namouih sasa akawa ameelewa. Kumbe hiki ndiyo kitu ambacho huu muda wote kimekuwa sababu kuu ya mwanaume huyu kujichukia sana na kuogopa kumuumiza Blandina. Bila shaka alikuwa akimaanisha kwamba katika harakati ya kutaka kupeana mapenzi na mwanamke, ilikuwa ngumu kwake kuziongoza hisia za upande wa pili endapo kama ungetoka jambo hilo likiwa linaendelea. Ndiyo kitu ambacho kilimfanya amkimbie Blandina mara ya kwanza na kuendelea kumkatalia kushiriki naye mapenzi. Hilo Namouih alilielewa. Lakini ikiwa Draxton alikuwa anampenda Blandina, ni kwa nini upande wa pili wa mwanaume huyo umjali yeye Namouih zaidi badala ya rafiki yake?
"Draxton.... I am so sorry. Pole sana kwa kupitia mambo mengi magumu mno," Namouih akamwambia huku sasa akimshika begani.
"Blandina ni mwanamke mzuri Namouih. Ananipenda sana bila kujua mimi ni nini, na ninakuwa mnafiki kwake kwa kuendelea na uhusiano wetu bila kumwonyesha upendo namna anavyostahili. Naogopa kwamba itafikia wakati nitapaswa kumwambia ukweli, na kwa jinsi alivyo, yeye pia anaweza kufikiri kwamba ataweza kunisaidia. Sitaki kurudia historia Namouih. Roho huwa inaniuma sana... tokea Ramona, sijawa na mwanamke mwingine kwa sababu hiyo. Lakini bado natumaini labda maneno ya mama kuhusu kuwepo kwa sababu ya mimi kuendelea kuishi ni kweli, ndiyo maana najipa nafasi kwa Blandina. Ila... kila nikifikiria kujaribu... naogopa Namouih... nitamuumiza...."
Namouih akaangalia chini kwa huzuni.
"Ni suala la mimi kutoweza kuji-control vizuri inapokuja kwa Blandina. Nimempenda yeye... lakini upande wangu wa pili umekupenda wewe. Nahofia naweza kuja kukosa control mbele yako, na upande wangu mbaya ukikushika Namouih... hautakuachia," Draxton akasema.
"Ahh... sielewi Draxton. Unasema upande wako wa pili umenipenda, halafu utaniumiza? Ikiwa hilo jitu liliweza kumzoea mama yako, basi hata na mimi...."
"La Namouih, mambo hayako hivyo. Mama iliwezekana vile kwa sababu alikuwa nami toka nipo mdogo. Hata Ramona nilikaa naye kwa miaka kadhaa, na ndicho kilichonifanya nidhani kwamba ningeweza kuji-control... au labda upande huu wa pili. Ila sikufikia hata hatua ya kuwa mnyama kikamili na nikamuumiza... nikampoteza milele kwa sababu ya imani yake kwangu. Jinsi unavyonionyesha kuniamini ni kama Ramona tu. Na jinsi unavyoendelea kujiweka karibu yangu ndiyo unafanya upande wangu wa pili uvutwe nawe hata zaidi, na hilo linaniathiri mimi pia. Sijui kama unaelewa uzito wa hili jambo Namouih?"
Namouih akaendelea kumwangalia tu usoni kwa hisia.
"Nathamini sana jinsi unavyoonyesha kunijali, lakini unajiweka hatarini. Wewe ni mke wa mtu Namouih, na mawazo yangu ya upande wa pili kukuelekea hayafai. Kila mara nikivuta harufu yako...." Draxton akaishia hapo tu na kubaki amemwangalia.
Namouih, akiwa amekwishaelewa kila kitu kwa asilimia zote sasa, akainamisha uso wake na kufumba macho kwa huzuni.
Draxton akasimama vizuri na kufungua droo nyingine, na mkono wa Namouih uliokuwa bagani kwake ukashuka. Mwanaume akatoa bukta ndogo ya samawati na kuifunga droo tena, kisha akainama na kuvuta boksi lile kubwa pembeni ya kabati hiyo, na humo akatoa blanketi kubwa lenye rangi mbili mchanganyiko wa pink na maziwa (cream), naye akakisogelea kitanda na kuanza kukivalisha vizuri blanketi hilo. Namouih alikuwa akimwangalia tu sasa, kwa hisia sana, kwa sababu kisa chote cha mwanaume huyo kilijaa magumu mengi mno yaliyofanya atie huruma kuwa mtu aliyeyapitia. Fikira za kufanya lolote ili kumsaidia alikuwa nazo bado, lakini baada ya kujua haya yote sasa angemsaidia vipi? Ikaonekana kwamba kweli msaada wa kumpatia mwanaume huyu ilikuwa ni kukaa mbali naye, kwa sababu Draxton hakutaka kujipa sababu nyingine ya kuwa na hatia kwa makosa ambayo angeyafanya bila kudhamiria.
Draxton sasa akawa amemaliza kulitandika blanketi kitandani, naye akachukua shuka lingine jepesi na jeupe, kisha akamwangalia Namouih na kukuta bado anamtazama sana.
"Nashukuru kwa kuja kunisaidia... na... samahani kwa kusema baadhi ya vitu kwa ukali. Ni ngumu kiasi kukwambia nachotaka na wakati huo huo akili yangu ikipingana nami..." Draxton akaongea hivyo na kutabasamu kwa mbali, akiwa anajaribu kutania yaani.
Namouih akaanza kulengwa na machozi bila hata yeye mwenyewe kuelewa ni kwa nini.
"Tafadhali nakuomba urudi kulala. Me nitalala huku kwenye sofa. Hilo saa moja au mawili yaliyobaki kwa ajili ya kupumzika yatasaidia kukupa nguvu kukikucha. Natumaini tu niliyosema hayatakufanya uote ndoto mbaya tena..." Draxton akawa amejaribu kuongea kwa njia ya utani tena, naye Namouih akaangalia chini tu kwa huzuni.
Mwanaume akainama na kuvuta droo ya chini kabisa, kisha akatoa kiboksi kidogo chenye mashine ya kunyoa nywele na kuibeba na ile bukta, halafu akafunga droo kwa mguu wake na kuliweka shuka lile kwenye kitanda hapo kisha kutoka ndani ya chumba hicho hatimaye. Namouih akatikisa kichwa chake kwa kusikitika sana na kuketi kitandani kama amejitupia kwa nguvu. Akawa anatafakari kila kitu alichoambiwa, na kiukweli kuna sehemu fulani ndani ya moyo wake iliyotamani sana kuweza kufanya jambo fulani ili kumsaidia hasa kwa sababu alimjali zaidi baada ya kumwelewa kwa kina. Akawaza sijui ingekuwa busara kumwambia Blandina? Lakini hapana, kwa sababu ni kitu ambacho Draxton hakutaka.
Akajilaza tu kitandani na kuendelea kuwaza na kuwazua kuhusu njia ya kumsaidia mwanaume huyo mpaka usingizi ulipomchukua kwa mara nyingine tena. Kwa upande wake Draxton, yeye hangeweza kupata usingizi kabisa baada ya jambo lililokuwa limempata usiku huo, hivyo aliendelea tu kukaa kwenye sofa akitafakari vitu vingi sana hasa baada ya kukumbuka mambo mengi yenye kuumiza aliyopitia kwenye maisha yake.
★★★
Namouih alikuja kufumbua macho yake muda fulani baada ya kusinzia kitandani pale, na kulikuwa na sauti ya kelele nzito kutokea juu ya nyumba hii iliyomwambia kwamba mvua ilikuwa inanyesha. Draxton alikuwa ameitengeneza vizuri sana sehemu hii kwa sababu hakuna hata tone moja la maji lililopita ndani, naye Namouih akajinyanyua taratibu na kuichukua simu yake. Bado alikuwa na wenge zito la usingizi, hivyo akafikicha macho yake na kutazama saa kukuta ni saa mbili ya saa tatu asubuhi.
Mvua hiyo ilisikika kwa nguvu sana kumaanisha ilikuwa kubwa mno, hata sauti za radi nzito zilisikika, naye Namouih akajitoa kitandani na kuanza kuuelekea mlango. Wakati huu hakuwa na viatu miguuni, hivyo akatembea taratibu na kuifikia kingo ya mlango na kuchungulia sehemu ya sebule ile ndogo. Macho yake yakatulia sehemu moja tu, na hapo ilikuwa ni mlangoni kuingilia ndani ya nyumba hiyo, ambapo Draxton alikuwa amesimama kwa kuegamia. Mwanaume huyo alionekana kwa nyuma, akiwa amevaa T-shirt yake nyeusi na bukta ile ya samawati, na kichwa chake sasa hakikuwa na nywele zile nyeupe kumaanisha alizinyoa na kupaka dawa nyeusi kichwani kwenye nywele ndogo alizobakiza.
Namouih akaendelea kumwangalia tu kwa umakini, akiwa anakumbuka vyema mambo yote aliyoambiwa masaa kadhaa nyuma, naye akatoka sehemu hiyo na kuanza kumfata taratibu. Aligundua haraka kwamba bila shaka Draxton alivuta harufu yake kwa kuwa mwanaume huyo aliacha kuegamia sehemu hiyo na kugeuka nyuma kumtazama. Namouih akasimama kiufupi na kuangaliana naye machoni, na ulikuwa ni utizami uliobeba hisia nyingi sana kutoka kwa wawili hawa, kisha mwanaume huyo akarudi kutazama tu nje. Mwanamke akaendelea kumfata taratibu na kufika usawa wake, kisha naye akasimama kwenye kingo ya mlango akitazama nje.
Maji mengi yalionekana kuelekea upande mmoja wa msitu, na Namouih akatambua kwamba gari lake lilikuwa limeacha kutoa mwanga wa mbele, ikimaanisha ni Draxton ndiye aliyekwenda kuzizima muda fulani nyuma. Maji ya mvua hayakuwafikia hata tone kwa upande huo wa mbele kwa sababu nyumba ilijengewa kama dari la mbao zililoziba upande wa mbele kwa kutokeza sana, kama kofia kichwani inavyoziba uso kwa mbele. Hakukuwa na neno hata moja lililosemwa kutoka kwa wawili hawa, na mara kwa mara Namouih angemwangalia Draxton kwa jicho la chini, lakini hakukuwa na chochote kilichotendwa na wanasheria hawa.
Ndipo Namouih akaanza kukisogeza kiganja chake taratibu kuelekea mkono wa Draxton, na kidole chake kidogo kikagusa kidole kidogo cha Draxton pia. Macho ya Draxton yakashuka chini kidogo, lakini hakuitazama mikono yao kabisa. Namouih hakusita kuendeleza jambo hilo, kwa sababu akakiingiza kabisa kidole chake kidogo kwenye kidole hicho cha Draxton na kuvifunganisha, kitu kilichofanya Draxton amtazame usoni taratibu. Namouih akamwangalia pia, sura yake ikionyesha hisia sana, naye Draxton akakaza macho yake kiasi; kama anamuuliza kitu fulani. Namouih akaendelea tu kumwangalia, ikiwa kama anamwambia jambo fulani bila kunena, naye Draxton akawa amemwelewa.
Mwanaume huyu akaendelea kumwangalia kama vile haamini kabisa mawazo ya mwanamke huyu, naye Namouih akaviingiza vidole vyake zaidi kwenye kiganja cha Draxton huku mapigo yake ya moyo yakikimbia kwa kasi sasa. Draxton akatikisa kichwa kwa njia ya kuonyesha kwamba kile ambacho Namouih alikuwa anafikiria hakikuwa sahihi, na jambo hilo lilimshtua sana. Lakini Namouih akamgeukia vizuri zaidi, kisha akaanza kumsogelea huku akimwangalia kwa hisia sana, naye Draxton akafumba macho yake na kuinamisha uso wake baada ya harufu nzuri ya mwanamke huyo kumwingia vyema puani kwa ukaribu huo.
Kuna sababu fulani kwa wakati huu iliyomfanya Namouih apende sana kumwona Draxton akifanya hivyo tofauti na ilivyokuwa mwanzoni, na ilikuwa kwa sababu sasa alimwelewa vizuri zaidi. Hakujua ni nini tu kilichokuwa kinamsukuma kufanya kitendo hiki lakini alikuwa ameridhia kwa asilimia zote kujiweka karibu zaidi na Draxton, na kiukweli, alikuwa anaogopa. Lakini bado akawa anataka kuizima hofu yake, hofu ya mawazo ya vitu vibaya ambavyo vingeweza kumpata, kwa kuwa hii haikuwa kwa sababu tu alitaka "kumsaidia" Draxton, bali ni kwa sababu alitaka KUWA na Draxton.
Mwanamke huyu akaushika uso wa Draxton kwa kiganja chake kingine, naye Draxton akawa ameinamisha uso wake bado na kusema, "Namouih.... nini unafanya?"
Ilikuwa ngumu kiasi kusikia alichosema kutokana na sauti kubwa ya mvua, lakini Namouih alielewa kile ambacho mwanaume huyo aliongea. Akaunyanyua uso wa Draxton ili watazamane, na kwa ukaribu huo Namouih alipendezwa sana na macho ya Draxton. Hakuwahi kuyaangalia vizuri sana lakini wakati huu aliweza kuona jinsi yalivyokuwa mazuri mno.
"Sijui ninachotaka kufanya... lakini moyo wangu unataka nikifanye," Namouih akasema kwa hisia.
Draxton akaanza kutikisa kichwa chake kukataa. "Hukuelewa chochote kati ya mambo niliyokwambia? Namouih... nakuomba... nakuomba ukae mbali na...."
"Hapana.... sitafanya hivyo," Namouih akamkatisha.
Draxton akaushika mkono wake na kuutoa usoni kwake, kisha akasema, "Usinifanye nijute kukujua Namouih."
Namouih akatabasamu kwa hisia, kisha akamwambia, "Najua Draxton. Lakini bado sitaondoka upande wako. Nimekuelewa vizuri sasa. Nafikiri najua jinsi ya kukusaidia."
"Sitaki uni.... si... sitaki unisaidie... kaa mbali na...."
"Kilichompata Ramona ilikuwa ni kwa sababu aliweka imani kwako tu!" Namouih akasema kwa hisia.
"Unamaanisha nini?"
"Hhh... aliweka imani kwako tu Draxton... kwamba hautamuumiza... lakini hakukufundisha namna ulivyopaswa kumwamini YEYE... ndiyo sababu imani yake kwako ikamfanya adhani ungeweza kila kitu mwenyewe hata ulipoanza kubadilika...."
"Unaweza vipi kuongea namna hiyo kama vile ulimwona... au kumjua?"
"Mimi ni mwanamke Draxton, lakini pia nimekuelewa kwa njia tofauti. Sitafanya hivi ili kukusaidia tu... ni ili na mimi unisaidie pia," Namouih akamwambia.
"Sielewi chochote unachojaribu ku... aagh!" Draxton akasema hivyo na kuonyesha kama anaumia kichwa.
"Nini Draxton?" Namouih akauliza kwa kujali.
"Naomba uende chumbani Namouih... kaa mbali na mimi..." Draxton akasema hivyo na kuanza kumsukuma taratibu kwa mkono mmoja.
"Draxton.... mwachie..." Namouih akasema.
"Nini?"
"Let him come out," Namouih akasema.
"Namouih!" Draxton akashangaa.
"Please nakuomba uniamini...." Namouih akasema.
Draxton akaonyesha kukasirika na kuamua kwenda chumbani ili ajifungie huko kutafuta utulivu. Hisia zake kumwelekea Namouih zilikuwa zinalazimisha kutoka kwa njia ambayo alijua ingesababisha atende vibaya, hivyo akaona kumwepuka ndiyo suluhisho zuri kwa sababu hakuelewa hata mwanamke huyo alikuwa anatoa wapi mawazo hayo. Alikuwa ameanza kuelekea upande ule wa chumba lakini mkono wake ukashikwa na Namouih, aliyekuwa amemfata na kumfanya Draxton amgeukie.
"Draxton please nisikilize...."
"Namouih this is wrong. Siwezi kufanya hivi, mbali na hii kuwa jambo baya na kukuumiza, ninaweza kusababisha uka...."
Draxton akaishia hapo na kubaki amemwangalia mwanamke huyo machoni. Namouih akaendelea kumwangalia pia kwa hisia, na ikawa kama vile Draxton anatafakari kitu fulani. Namouih akasogea karibu yake kidogo na ile anataka kusema kitu fulani, Draxton akamvuta ghafla na kuubana mwili wake kwake kwa nguvu, kisha akaanza kumpiga busu mdomoni moja kwa moja!
Ingawa Namouih alikuwa ameshtushwa kiasi na jambo hilo, akafumba macho taratibu na kuanza kuisikilizia vizuri busu hii kutoka kwa mwanaume huyo kwa sababu ilifanya hamu yake ya kimahaba ipande sana. Draxton akaunyonya mdomo wake kama mara tano kwa namna hiyo huku Namouih akiwa amelegea kiasi kwa nyuma, kisha akajitoa mdomoni mwake na kumwangalia machoni. Alikuwa amekishika kichwa cha Namouih kwa nyuma na kiuno chake, akiwa amemshikilia kama vile anataka kumbatiza kwenye maji mengi, kisha akamwambia....
"I love you."
Maneno hayo yalimfanya Namouih amwangalie kama amezubaa kiasi kwa sababu yalikuja ghafla sana bila matarajio yoyote kabisa, kisha Draxton akaanza tena kumbusu kimahaba mwanamke huyu. Wakati huu alimbusu taratibu na kwa hisia sana, naye Namouih akawa anarudisha busu hiyo kwa kuonyesha hamu kubwa pia. Akainyonya midomo yake huku sasa Namouih akianza kusimama wima, naye akawa analishika kalio lake na kuliminya kwa nguvu, kitu kilichofanya Namouih aanze kuguna ndani ya mdomo wake katikati ya busu yao tamu. Halafu Draxton akamgeuza, na sasa Namouih akiwa amempa mgongo kwa ukaribu, jamaa akaanza kuibusu shingo yake kwa nyuma huku mikono yake akiitumia kuyasugua matiti ya Namouih ndani ya nguo aliyokuwa amevaa, na mwanamke huyu akawa amefumba macho huku ameachama mdomo wake na kupumua kijuu-juu.
Baada ya sekunde hizo chache za kupandishiana hamu, Draxton akamwachia na kurudi nyuma kabisa, naye Namouih akamgeukia na kumwangalia machoni kimaswali kiasi. Draxton alionekana kupumua kwa nguvu sana, naye akausogelea ukuta wa hapo na kuuegamia huku akiendelea kupumua kwa nguvu, na Namouih akamfata taratibu na kumshika shingoni kwa mikono yake. Ilikuwa ya moto kweli, lakini Namouih hakuitoa mikono yake hapo.
"Draxton.... mwachie..." Namouih akasema.
Draxton akatikisa kichwa kukataa huku ameinamisha uso wake.
Namouih, akimwangalia kwa hisia sana, akaita kwa sauti ya chini, "Max..."
Draxton akanyanyua uso wake na kumtazama machoni kwa mkazo.
"Mwachie..." Namouih akasema hivyo na kupitisha viganja vyake mashavuni kwa mwanaume huyu.
Draxton alikuwa akiendelea kumtazama sana, huku bado akijitahidi kujikaza, na ni jambo moja tu lililokuwa limeteka hisia zake. Ilikuwa ni kitendo cha Namouih kumwita "Max" ndiyo kilichomfanya ahisi ni kama ana ukaribu mkuu sana na mwanamke huyu, kama jinsi ilivyokuwa kwa mama yake tu. Hakuna yeyote aliyemwita hivyo kwa kipindi kirefu sana. Bado alikuwa anaona mambo kama Draxton lakini nguvu zake zilikuwa zinatoka kwa njia ya mnyama mkali, kwa hiyo alikuwa anahofia kumuumiza Namouih. Alielewa kwamba mwanamke huyu alichotaka ilikuwa yeye kutojikaza, na kwa sababu ya kuhisi udhaifu fulani hivi mbele ya Namouih, Draxton akaamua kujiachia. Akafumba macho huku akiendelea kupumua kwa nguvu kiasi, na viganja vya Namouih bado vikiwa vimeushikilia uso wake huku mwanamke huyo akimwangalia kwa hisia sana.
Ndipo nywele za Draxton zikaanza kuota taratibu kichwani kwake, zikirefuka na kuanza kubadilika rangi, naye Namouih akawa anamtazama kwa umakini. Draxton akafumbua macho yake ghafla na kumtazama Namouih, na mwanamke huyu akaingiwa na msisimko wa kushtuka kiasi kwa sababu yalikuwa yale macho ya blue yenye kutisha. Lakini Namouih hakuuachia uso wa mwanaume huyo, ambaye sasa alikuwa anapumua kwa njia fulani ya hasira, na ngozi yake ikaanza kuwa nyeupe. Lengo la Namouih lilikuwa kuhakikisha Draxton hapitilizi, na kama alivyomwambia muda mfupi nyuma, angeweza kufanya hivyo kwa kumfundisha Draxton jinsi ya kumwamini yeye Namouih, siyo tu Namouih kumwamini Draxton. Hiyo ilimaanisha nini? Ampe mapenzi kwa njia ambayo hakuwahi kumpa mwanaume yeyote kabla!
★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★
Comments