Hamza alishangaa kidogo baada ya bwana huyo kuwasogelea.
“Ndio mkuu , kuna tatizo?”Aliuliza.
“Mimi ni mpiga picha wa jarida maarufu la mitindo hapa Paris. Jarida letu linahusisha utoaji wa ripoti juu ya watu waliopendeza zaidi kwa wiki ndani ya Paris. Nimeona huyu mwanadada mrembo mbele ya Eifell tower na kudhania macho yangu yananidanganya kwani ni kama kiumbe kilichoshushwa ghafla , hivyo nauliza kama naweza kuchukua picha zake kadhaa. Msiwe na wasiwasi picha hizi hazitotumika kwa ajili ya matangazo ya kibiashara na pia jina lako litafichwa ili tusivunje faragha yako”
Regina mara baada ya kusikia maelezo hayo alishindwa kujizuia aibu kumshika . Ingawa ameitwa sana mrembo tokea akiwa mdogo lakini sio kama kiumbe alieshushwa kutoka angani tena katika ardhi ya ugenini.
“Ni wapi picha hizi zitatumika katika jarida lenu?”Aliuliza Hamza
“Ni mbele ya jarida , lakini vilevile katika mitandao yetu ya kijamii na ofisi za maonyesho”
“Sasa kama mkichukua picha ya mke wangu si itawavutia watu wengi na maana yake mtapata trafiki kubwa , ambayo huleta hela , kuna utofauti gani na kufanya biashara?”Aliuliza Hamza akiwa hajaridhika.
“Sir kwa kusema hivyo hatuwezi kupinga pia . Lakini jarida letu linadili zaidi na wanawake warembo na hatuwezi kuchukulia swala hili kwa namna ya kujinufaisha”Aliongea na Hamza aliishia kumwangalia Regina.
“Wife , vipi unataka kupigwa picha na kuonekana kwenye jarida lao?”
Regina alikuwa na aibu sana kupiga picha ndio maana hata mtandaoni hakufahamika sana , sasa inawezekanaje apigwe picha kwa malengo ya fasheni kwa ajili ya kuonekana katika jarida.
Lakini Regina aliona kama angekubali kupigwa picha katika mazingira kama hayo itakuwa ngumu kusahaulika na pia ingekuwa nzuri zaidi.
“Sioni shida kupiga”Aliongea Regina baada ya kusita kidogo na Hamza alitingisha kichwa kukubaliana nae.
“Vipi utampatia mke wangu hela , namaanisha hela za umiliki wa picha yake?”
“Sire , tunachokifanya ni kama interview ya mtaani , itakuwa ngumu kuweza kulipa hela kila tunaeomba kumpiga picha. Kama dada atakataa kupigwa picha hatuwezi kumlazimisha pia”
“Yaani hamtaki kunipa hata shilingi , halafu mnataka kumiliki picha ya mke wangu ? Mnaniona mjinga , kwanini niwagawie mke wangu bila sababu?”
Regina alijikuta akichizishwa na maneno yake na kujiuliza huyu mtu anaongea nini ? Alishindwa kujizuia na kumfinya Hamza kiunoni.
“Wewe unaongea ujinga gani? Kupiga picha kunafanana vipi na kunigawa?”Aliongea na kumfanya Hamza kucheka.
“Ndio hivyo , sitaki mtu mwingine akuone kila siku , mimi peke yangu ndio mwenye kigezo cha kukuona wewe kila siku”Aliongea.
“Wewe , mbona unakuwa kama mtoto” Regina hakujua anune au afurahi, lakini moyo wake ulijaa utamu.
Cameraman yule aliishia kutingisha kichwa chake kwa masikitiko na kisha aliaga na tabasamu baada ya kukataliwa.
“Ipo hivyo , wewe ni wa kwangu na nitakuwa kichaa kuacha wanaume wengine waangalie picha yako kila siku”
“Yule ni msanii wa picha tu , kwanini unafikiria mbali. Jitu kubwa lakini una mawazo ya kitoto”Aliongea Regina akitingisha kichwa kama kujutia kukosa nafasi ya kupigwa picha.
“Nilitaka kupata picha moja nzuri , angalia ulizopiga zilivyo mbaya”
“Basi kama ni hivyo nitaenda kutafuta mtaalamu wa hali ya juu wa kupiga picha. Lakini mke wangu picha yako itawekwa nyumbani tu ili mimi niwe naingalia mwenyewe vinginevyo nitashikwa na wivu eti” Regina alishindwa kujizuia na kucheka.
“Wewe umekuwa mtoto kweli na vituko vyako.. nishakata tamaa sitaki picha tena”
“Haha.. mke wangu labda utakuwa hujasikia tu , Mwanaume siku zote ni kama mtoto mbele ya mwanamke anaempenda. Mwanaume akiwa hakupendi mbingo zake zitakuwa ni za kibaba baba tu. Hivyo mke wangu nipo hivi kwasababu nakupenda kutoka uvungu wa moyo wangu”
“Lione, sitaki kukusikia tena . ninunulie basi kitu chochote kitamu cha kula”
“Sawa mke wangu , ngoja nikupeleke ukale kitu utakachopenda”
Hamza alimchukua mrembo wake na kununua vitu na kisha walienda kupanda kwenye Ferris Wheel. Ijapokuwa hawakuwa na mengi ya kufanya pamoja , lakini kuwa kama hivyo , kama wapenzi wa kawaida iliwafanya ukaribu wao kuzidi kuongezeka.
Baada ya kutumia siku nzima kutembea na kucheza kama wapenzi Hamza alimuaga Regina kwamba siku tatu zitakazofuatia kuna vitu anaenda kufanya hivyo hatoweza kuwa nae.
Regina hakuhitaji maelezo mengi kujua Hamza anaenda kufanya nini , alikuwa na vitu vingi ambavyo hakuwa akijua kuhusu Hamza hivyo aliishia kumkubalia. Walikubaliana tu akisharudi huko anakoenda wataanza safari ya kurudi Tanzania.
Hamza upande wake alijua hatokuwa na muda wa kununua zawadi , hivyo aliingia mtandaoni na kuchagua vitu vingi kama zawadi na kumtumia Mzee Pino kuviandaaa kwa ajili ya Eliza, Yulia na Dina.
Wanawake hao watatu walikuwa ni warembo wake , kuhusu Prisila alimchukulia kama mdogo wake na Irene kutokana na bado kuwa mwanafunzi aliona asimpatie zawadi maana atamfanya azidi kuchizika.
Muda huo Hamza alishindwa kujizuia na ghafla tu mawazo juu ya Yonesi yalimvaa palepale. Kama bado angekuwa na mawasiliano na mrembo huyo angemnunulia pia zawadi.
*****
Ni ndani ya mji mdogo unaofahamika kwa jina la Limours , uliokuwa kusini Magharibi mwa jiji la Paris , uliozungukwa na vilima vidogo vidogo vyenye msitu.
Ni sehemu ambayo ilikuwa na utulivu mkubwa na mahali ambapo ni rahisi kuficha siri kwa watu wa ulimwengu wa nje. Hivyo Baraza la maksi lilipangwa kufanyikia katika mji huo.
Eneo la uwanja wa ndani wa mpira wa miguu , ndio mahali ambapo paligeuzwa kuwa Venue kwa ajili ya Set Conference.
Katika siku hizo , kwa watu wote ambao walifika nchini Ufaransa kwa ajili ya kushiriki baraza hilo la maksi walikuwa wamejazana katika mji huo wa Limour , karibia katika kila hoteli na gesti zote.
Kulikuwa na wanajeshi wengi pamoja na polisi ambao wametumwa na serikali kwa ajili ya kutoa ulinzi ili kuepusha machafuko.
Hamza sasa alifika ndani ya mji huo akiwa ametangulizana na Asmuntis na Black Fog kupitia gari aina ya Hummer.
Watu wa kawaida walipangiwa kuishi katika hoteli kwa kipindi chote cha baraza hilo lakini ilikuwa tofauti kwa Hamza. Watu wake wasingemruhusu kukaa hotelini na watu wa kawaida hivyo walikodisha nyumba nzima kando ya shamba.
Ukweli ni kwamba Magwiji wakubwa kama wangejitokeza ama kufahamika mbele ya watu wa kawaida ingeleta msisimko na aina flani ya ukinzani. Hivyo hoteli haikuwa maeneo sahihi kwao kuishi.
Mara baada ya kufika katika nyumba iliozungukwa na shamba kubwa la Farasi , ijapokuwa eneo lilikuwa limejitenga lakini lilikuwa limeboreshwa ulinzi wake kwa teknolojia ya hali ya juu na kulikuwa na vyanzo mbalimbali vya starehe.
Ndani ya uzio wa shamba hilo kulikuwa na magari kadhaa ya kifahari yaliokuwa yameegeshwa. Ikionyesha mtu ambae sio wakawaida alikuwa ametangulia kufika.
“Bosi nasikia sauti ya kugongelea chuma”Aliongea Asmuntis wakati akitoka nje ya gari.
“Hata mimi pia , ngoja tukajionee huyu mhunzi ni kitu gani anatengeneza tena”Aliongea Hamza.
Mara baada ya kuzunguka nyuma ya banda la Farasi , waliweza kuona mwanaume akiwa ndani akigongelea chuma na nyundo kubwa.
Kipande cha juu cha mwili wa mwanaume huyo kilikuwa cha rangi ya kahawia na misuli mikubwa iliotuna iliweza kuonekana. Kila msuli ulionekana kuwa mgumu kama jiwe.
Alikuwa na nywele fupi zilizojikunja kunja, alikuwa ametoboa masikio na kuvalia heleni kubwa za dhahabu.
Dang , Dong , Clang!
Sauti hio ya kugongelea chuma , ilikuwa ni kama inatoka kwa mpangilio maalumu wa kutengeneza mziki.
Mara baada ya kumuona mwanaume huyo wa mita moja na nukta tisa , midomo ya Hamza na Asmuntis ilicheza kwa kuonyesha tabasamu.
“Uncle Azzle , kwanini kufika tu unaanza kugongelea chuma?”Aliongea Black Fog
Mwanaume huyo wa rangi ya zambarau alikuwa ni Azzle mkuu wa kundi la Kimasenari la Barhams, Maarufu kama Ares of Arabian Peninsula.
Azzle mara baada ya kugeuka na kumuona Hamza , haraka sana aliweka kile chuma kwenye dimbwi la maji.
Siziiiii! Mvuke wa maji ulipanda ukipoza chuma kile na palepale aliweka nyundo yake chini na kisha alishuka chini na goti moja huku akiweka mkono kifuani.
“My Prince!”
Alimsalimia Hamza kwa mbali na kisha akasimama na kumwangalia Asmuntis kwa macho makali.
“Wewe Mtu mchafu kwanini umechelewa kumleta bosi hapa?”
“Kwahio kama nimechelewa inakuhusu nini? Bosi alipaswa kuwa na shemeji yetu kwanza”Aliongea Asmuntis.
“Oh Tena nimekumbuka , bosi mbona simuoni shemeji?”Aliuliza Azzle.
“Wewe mzee wa Stroke , unavyoongea tu ni kama mzimu uliofufuka , halafu unataka nije na mke wangu, Unataka umtishe? Ni muda mrefu tokea tuonane mara ya mwisho nipokee hata kwa kicheko basi”Aliongea na kumfanya Azzle kutabasamu.
“Bosi nilijizuia tu , ila jana nilitaka kuja Paris kukutafuta , lakini baada ya kufikiria nikaona nije hapa mapema kuona maandalizi yakoje. Ni Berrly alieagiza hii sehemu iwe wazi kwa ajili yako , si unajua alivyo mvivu ndio maana nikaona nijihakikishie. Unapenda kuendesha Farasi ndio maana na kutengenezea viatu hapa”Aliongea.
“Ni lini nilikuambia napenda kuendesha farasi. Nakumbuka ilikuwa ni miaka sita iliopita tukiwa Argentina Pampas Height, kipindi kile niliendesha farasi sio kwasababu napaenda bali ni kwasababu nilikuwa nikifukuzia mtu nilietaka kumuua”
“Ni kwasababu bosi wewer ni tajiri tayari hivyo sijui ni kipi naweza kukupatia kama zawadi , nimeona kutengeneza horseshoes itakuwa na maana zaidi” Hamza mara baada ya kuona jitu siriasi namna hio linataka kumfurahisha aliguswa.
Washikaji zake ambao alikuwa nao kwa muda mrefu , wengi wao wanaishi kwa kuamini wana deni kubwa kwake na kila siku wanajribu kutafuta namna ya kumlipa.Lakini ukweli ni kwamba kuweza kuishi katika ulimwengu wa giza na kufanikiwa ni swala la kutegemeana.
Hivyo Hamza hakuwahi kuwaza mafanikio yake yametokana na uwezo wake pekee bali ni kwasababu ya kuwa na marafiki wengi. Hivyo hata baada ya kustaafu na kuachia maeneo aliokuwa akiongoza wayasimamie wao hakujutia wala kujisikia vibaya.
“Wewe Mhunzi nashukuru sana unaonekana kunijali lakini haijalishi kama napenda kuendesha farasi au lah . Ila kwasasa nataka tukae chini na tupate kinywaji pamoja na kupiga stori . Naamini umekuja na mvinyo mzuri , maana mpaka kuwa Mshauri mkuu wa mfalme naamini wanatumia hela zao za mafuta kukulipa vizuri”
“Bosi niseme tu ukweli sijaja na mvinyo wowote , Berly pia ni mbahiri mno sijaona mvinyo wowote hapa , ngoja nimpigie mtu simu atuletee..”Mara baada ya kuongea , sauti nyingine ilisikika kutoka chini.
“Pumbavu zako Azzle , ushaanza kunisnitch tayari kwa bosi.Mimi Berly naweza nisikupe wewe wine lakini mimi ni mtiifu kwa bosi wangu na nimemuandalia kitu roho inapenda. Huko ardhini nina chumba kizima cha mapipa ya wine kama haya, sikutaka kukuonyesha mlevi kama wewe”Aliongea huku akiwa ana kohoa mfululizo , akiwa anatoka ndani ya eneo la chini kama shimo, ilionekana eneo hilo lilikuwa na vumbi mpaka kumfanya kukohoa.
Berly alikuwa ndio mwanaume mtanashati kuliko wenzake wote , alikuwa amevalia shati la maua maua na cheni shingoni , huku nywele zake akiwa amezisuka. Muda huo alikuwa amebeba pipa la kuozeshea mvinyo na haraka sana alilitua chini na kumsogelea Hamza na kumkumbatia.
“Bosi , hatimae umefika. Nilikumisi sana. Katika miaka mitatu yote nilikuwa nikikuota wewe tu . Hatimae nimekuona tena”Aliongea huku akiwa amemkumbatia lakini Hamza aliimshia kumsukuma
“Hebu acha kuniganda kama mwanamke”Aliongea Hamza.
Berly alikuwa tofauti sana , ilikuwa ngumu kuamini alikuwa akijihusisha na ulimwengu wa giza, katika ulimwengu wa nje alikuwa ni msanii , DJ na Playboy ambae maisha bila kuzungukwa na wanawake hayaendi. Alijua sana kuhonga na kila jiji alilopita aliacha alama.
Kubwa zaidi ni kwamba alikuwa na ushawishi mkubwa sana katika tasnia ya mziki , watu wengi alikuwa akifahamiana nao na alikuwa hata na ushaiwshi wa nani apewe tuzo na nani asipewe na hio ilimfanya kuwa maarufu sana.
Ukiachana na kuimba hakuwa na kazi maalumu , alichofanya siku nzima ni kula bata kwenye mayatcht ya kifahari na kupiga milegezo. Hakujali kabisa swala la mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi na ilikuwa ngumu kuamini mtu kama huyo alikuwa na ukaribu na Hamza.
Lakini alikuwa mtu muhimu sana kwa Hamza , anaweza asiwe na nguvu ama na uwezo kama Asmuntis , lakini kipindi alipokuwa na Hamza alikuwa ndio mtu pekee aliekuwa akiongoza kwenye vita ya maneno , alikuwa na kipaji cha kuongea na mtu yoyote na akakubali kile anachomwambia , hivyo alifanikisha mambo mengi kwa ajili ya Hamza.Lakini mbaya zaidi aliatumia uwezo wake wa ushawishi kuwakopa wenzake.Alikuwa anakula bata kwa kukopa marafiki zake.
“Bosi usinilaumu wakati wewe ndio uliniacha mwenyewe , nina picha yako nyumbani na muda wote naingalia kila nikikukumbuka . Kuna muda mwingine hadi nalia’
“Tangu lini ukawa na nyumba ya kuamkia kila siku wewe, Si unaamkia mahotelini na kwenye maboti wewe. Imepita miaka mingi lakini tabia yako ya kudanganya hujaacha tu”Aliongea Hamza huku asijue acheke ama alie.
“Bosi nilipomuambia atukodishe hili shamba , aliniambia tumlipe Euro milioni mbili. Jamaa ni mbahiri sana kwa sisi washikaji zake ila mbele ya mbususu anakuwa kama chizi kwa kuhonga tena kwa hela zetu”
“Azzle acha kunisnitch , ndio maana muda wote unanuka mafuta ya taa na petroli. Niliemkodisha shamba kaniuzia na mvinyo , kuomba Euro milioni mbili unaona nyingi sana?”
“Nakudai Dollar milioni mia moja zangu , ulizonunulia private Jet. Nakupa mwaka mmoja , usiponilipa nitayafanya maisha yako kuwa magumu”Aliongea Azzle.
“Wewe Mhunzi , kwanini unashindwa kujali ushikaji wetu. Bosi ashawahi kusema upendo na haki ni zaidi ya thamani ya dhahabu. Hela kidogo hio ila makelele meengi”Aliongea Berly kwa sauti
“Berly hata mimi nimekumbuka nakudai dolla milioni moja na hamsini, mimi nirudishie tu milioni mia , zinazobaki nimekupunguzia”Aliongea Hamza.
“Bosi mimi ni shabiki wako namba moja , kwanini unanikandia? Nyie wote naona hamtaki niwe na amani . Yaani nimewatafutia eneo zuri kama hili kwa ajili ya kukutania baada ya kunipa shukrani mnaanza kunidai madeni. Hela zote hizo natoa wapi , sijui kupigana , sijui kuuza siraha , sijui kuua watu , ninachojua ni kuwakopa tu bila kujua namna ya kulipa”Aliongea huku akijitilisha huruma na kuigiza alikuwa akilia huku amekaa chini kama mtoto.
Baada ya kuona anachokifanya Berly iliwaacha midomo wazi na walishindwa kujizuia na kucheka.
“Mnanifanya hata binamu yangu Roda ananidharau . Kuna haja gani ya mimi kuendelea kuishi , sina thamani kabisa hata ya kuwa mbele yenu na bosi ..”Aliongea kama mkiwa.
“Bosi mbona kuna makelele mengi huko ndani , mnamfanya nini huyo mwehu. Hebu tokeni kwanza huko ndani mje tucheze raundi boja la sivyo Leviathani ataniua kwa kipigo”
Mara baada ya kusikia sauti hio , kila mmoja alijua ni nani na palepale waligeuka na ndio muda walioweza kumuona mwanaume bonge kama Rickross akiingia
Boss!
Mwanaume huyo mwenye mwili mweusi alitembea huku akitawanya upepo na kwenda kumkumbatia Hamza.
Kama Hamza asingekuwa na nguvu angedondoka nae chini maana sio kwa uzito huo.
“Mameni kila ulipo unawaza kucheza kamari tu , utaacha lini?”Aliongea Hamza huku akicheka.
Mameni ukiachana na kuwa Taikuni wa kuuza siraha , lakini vilevile alikuwa ni mlevi mkubwa wa michezo ya kamari na kubeti.
“Ndio kitu kinachonipa furaha, hili eneo lilivyokauka kamari ndio starehe pekee iliobaki”aliongea huku akicheka
“Twendeni zetu tukacheze , Azzle huna haja ya kuendelea kutengeneza hicho chuma”Aliongea Hamza na Azzle alikubali.
Mara baada ya kuona kila mtu anaondoka bila kujali huzuni yake , Berly aliekaa chini alianza kulia tena.
“Bosi vipi kuhusu mimi! Unanitelekeza masikini kama mimi”
“Njoo na hio pombe”Aliongea Hamza na kumfanya Berlly furaha kumvaa na haraka haraka aliinuka na kubeba pipa lile.
Wote walitembea na kwenda kuingia katika nyumba iliokuwa katikati ya shamba hilo , kwa nje haikuwa nzuri sana , ila ndani ilikuwa imepambwa vizuri tu na kupendeza.
Katika eneo la Dining kwenye meza ndefu alionekana Leviathani akiwa amekodolea macho kararata.
Mara baada ya kumuona Hamza akiingia Leviathani haraka haraka alisimama na kumpa Hamza heshima yake.
“Wewe ngiri kwanini unang’ang’ania kucheza na Mameni! Unaishi baharini halafu unataka kumfunga?”
“Sikutaka kukubali ndio maana nikampiga, kwanini kila saa yeye ndio anashinda tu” Hamza muda ule aliweza kuona Leviathani alikuwa amenyoa kipara na alishangaa.
“Wewe Ngiri hicho kipara umekitoa wapi kwanza?”
“Haha.. binti yangu anasema rasta zangu zinamuumiza kila ninapomkumbatia ndio maana nikaamua kunyoa kipara”
“Kumbe hata shetani mkubwa wa baharini ana upande mwingine mlaini , Ajabu iliooje hii”Aliongea Berry na kauli y ake ile ilimfanya Leviathani haraka haraka amsogelee na kumkwida tai.
“Wewe takataka ni lini utanilipa milioni zangu therathini ninazokudai na dhahabu ulizochukua?”Aliongea akiwa siriasi.
“Ngisi hebu acha kuwa hivi basi , ijapokuwa tunalingana umri lakini nimekuzidi mwezi mmoja , hivyo mimi ni kaka yako na uache kuniabisha, kama ni hela nitalipa tu nikipata..”
Mara baada ya kusikia hivyo watu wote walijikua wakianza kucheka , huku Leviatahni akishangaa , maana hakujua ni kipi kimewafanya kucheka.
Mara baada ya kuongea kidogo , kila mmoja alikaa kwenye nafasi yake . Hamza alikaa katika kiti cha heshima na kumfanya awe anawaangalia kupitia pande zote mbili. Ndani hapo karibia marafiki zake wakubwa wote walikuwepo , akiwemo Azzle , Asmuntis , Mammeni, Livotani , Berly na wengine. Black Fog hakuthubutu kukaa , aliishia kuwamiminia mvinyo huku akiwa amesimama nyuma ya Asmuntis.
Muda huo wote walitulia na Hamza hakuongea neno wala Berly muongeaji sana hakuongea neno . Kila mmoja alikuwa na mwonekano mzito , wakiwa katika takafakari ya kukumbukia mambo yote yaliopita.
Mpaka dakika kumi kupita hatimae Hamza aliwaangalia mmoja baada ya mwingine na kisha akaongea.
Kunani huko kwenye Baraza la maksi?
Comments