Reader Settings

Jitu la Chuma.

The long Table au Meza ndefu ndio  kikao cha daraja la juu  katika jamii ya siri ya Inferno tokea kuanzishwa kwake. Inferno  ilitokea katika  Clubs mbalimbali za kishetani ambazo zilianzishwa hapo mwanzo katika miaka ya 70, club hizi zilipewa jina la  Hellfire  Clubs. Watu wa Hellfire club walijaribu kuvumisha jamii yao hii kwa kuingiza katika  filamu kubwa za kimataifa kama Marvel Comics , Stranger Thing  na baadhi  ya nyingine nyingi wakijaribu kuonyesha ushawishi wao  katika kila sekta  ndani ya dunia hii kwanzia katika maswala ya uchumi ,  jamii  na hata tamaduni.

Hellfire Club  walifahamika  kama watu wanaomzihaki  Mungu  nchini Ireland katika miaka hio. Hii jamii  ilikuwa ikifanana  sana na Freemason au Iluminat na iliongozwa na Black Emperor au Mr Black.

Baada ya kufa kwa jamii hii  kupitia vita takatifu ndio ikaibuka  jamii nyingine ambayo ndio hii ya Inferno.

Waasisi  wakuu walikuwa ni watu kumi na mbili  ambao  walitengeneza kikao cha hadhi ya Meza Ndefu  ya siti kumi na mbili.

Maana yake ni kwamba vikao vya juu  havikuzidi watu hao  kumi na mbili tokea kuanzishwa kwake.

Iliwachukuwa miaka miwili tu kuingia katika daraja S  katika ulimwengu wa giza  ambapo  ndio kipindi chote cha  Vita takatifu , vita ambayo  sio tu kumpa Hamza  umaarufu lakini ilimpa ushawishi mkubwa.

“Mephistopheles  hajafanikiwa kufika”Aliongea Azzle

“Sallisbury  hajasafiri kwa ajili ya kulinda kisiwa cha Toharani”Aliongea Asmuntis na Hamza palepale aliinua  juu kikombe cha mvinyo.

“Kikombe cha kwanza cha mvinyo  huu ni kwa  ajili ya kuwaenzi wale waliotuacha , Belzebuli , Abtoni , Samuel  na Roffe , Jamaa zetu hawa wa nne licha ya kutokuwepo  na sisi  leo hii lakini nafasi zao zitaendelea kuwa wazi katika vikao vyote vya  Long Table milele”Aliongea Hamza.

Katika meza hio kila mmoja  aliinua  glasi ya mvinyo wake na kisha alikunywa yote  kwa ajii ya kuwaenzi washikaji zao wengine.

Hali ile ya huzuni na  kutafakari ilipita baada ya  awamu hio ya kwanza ya mvinyo. Hamza alitaka kunywa na washikaji zake mpaka kesho , kunywa kujigalagaza kabla ya kwenda kushiriki katika baraza la maksi. Lakini muda ule simu ya Azzle ilianza kuita.

“Kuna nini na naongea na nani?” Aliuliza Azzle huku akiwa amekunja sura.

“Kapteni! Sitaki kuwasumbua katika kikao chenu na Mkuu wetu , lakini kuna kitu kimetokea hapa , watu wetu wanashambuliwa na watu wa Wimbi la chuma”

“Metal tide!” Azzle alijikuta akishangazwa na habari ile huku akiinua macho yake na kumwangalia Asmuntis

Asmuntis  hata yeye uso wake ulibadilika mara  moja baada ya kusikia mwenzake anataja Metal tide na aliishia kumwangalia Hamza kwa wasiwasi.

“Nimesikia vibaya?”Aliongea Mameni kwa sauti kubwa.

“Metal tide wanathubutu vipi kushambulia watu wetu , hawajui mtu ambae yupo nyuma ya  Barhamu ni bosi “Aliendelea kuongea Mameni.

“Mhh! Bosi inaonekana kutoonekana kwako kwa miaka mingi , hawa watu washaanza kujihisi wapo juu. Kwanini tusiwaonyeshe  kile wanachohitaji”Aliongea Leviathani na kisha akaendelea “Sasa hivi tumezidi kuwa na nguvu , tukiungana  mimi , Mhunzi  hapo   na  Mchafu na watu wake  ni swala la kufumba na  kufumbua tushalizima  kundi lote  la watu wa Wimbi La Chuma”Aliendelea kuongea Leviathani akiwa  katika hamasa kubwa sana.

Hamza alijikuta akiishiwa na usemi , aliishia kunyoosha mkono wake kwa ishara ya kuzuia pendekezo la Leviathani.

“Msiniingize mimi huko tena , nilishawaondolea  wasumbufu wote  lakini bado  tu mnataka kunichosha?”Aliongea Hamza.

Upande wa  Azzle na Asmuntis  walikuwa na hali zisizoelezeka katika nyuso zao , walifikiria  kuona Leviathani  na  wenzake hawakuwa na taarifa ya Hamza kupoteza uwezo wake wa nishati za mbingu na ardhi.

Ukweli ilikuwa tofauti kwa wenzao , walikuwa wakifahamu Hamza hakuwa na tatizo lolote kuhusu uwezo wake maana  alishawasiliana nao na hata kukutana nao  siku kadhaa zilizopita.

“Bosi timu yetu ya Barham inaonekana kupambana na watu wa Wimbi la Chuma  hapa Limour . Mimi nitaelekea huko nikadili na hili suala,sitoungana na nyie  kuendelea kunywa”Aliongea Azzle na kusimama.

“Hey! Mhunzi , hili swala limeamsha shauku yangu. Kwanini tusiende wote kuangalia. Nataka  kumuona Jitu Chuma uwezo wake ni mkubwa kiasi gani”Aliongea Mameni huku  na yeye akisimama.

“Ndio bosi , hujaonekana  kwa muda mrefu  na hawajakukaribisha  kwenye kikao cha kilele  cha  Magwiji . Ukijionyesha sasa hivi asilimia kubwa ya watu   watakuwa mashabiki zako”Aliongea Berlly.

“Mashabiki wa nini? Unadhani nimekuwa msanii?”Aliongea Hamza.

“Kwa mtazamo wangu haina haja. Bosi  huna haja ya kwenda ,kama bosi akienda si  kama tunawaheshimu sana ? Mimi na  Mhunzi peke yetu tunatosha kudili na hii hali”Aliongea Asmuntis.

Hamza aliishia kusinyaza macho baada ya kuona  Azzle na Mchafu  wanamtetea asiende kwasababu wanadhani  hana uwezo wowote. Hamza alifikiria kidogo  na palepale aliona haina haja ya kuwaambia ukweli kwanza, kwasababu alijua  anachofanya  Gonzalez ni kutaka kumtega  yeye. Gonzalez alikuwa akitafuta tu ugomvi , lakini ukweli ni kwamba  makundi yote mawili yaani  Barham na  Wimbi la Chuma walikuwa ni daraja  A  hivyo  wasingeenda mbali.

Alipanga  pale ambapo Gonzalez atakuja moja kwa moja kwake ndio atadili nae na atatumia nafasi hio kumkamata na kumshikisha adabu.

“Tutaenda wote , ila sitojitokeza. Ijapokuwa  Barham kwasasa  ipo chini yako  lakini bado nina  hisia na jina lake , nisipoonekana itawavunja moyo vijana wetu”Aliongea Hamza.

“Bosi kwasababu umeongea hivyo , basi twendeni pamoja”Aliongea Azzle

Asmuntis alishindwa kufanya lolote  mpaka hapo lakini maneno ya Hamza yalikuwa na mantiki. Kama kila  mtu yupo ndani ya Limuour na kitu kibaya kikatokea vijana wao  na Hamza hajajitokeza  itawafanya  kuvunjika moyo na pia ingeibua minong’ono.

“Twendeni , sitaki kuchelewa tena , ni bora Gonzalez akajitokeza mwenyewe nimpasue kichwa chake”Aliongea  Leviathani huku akisimama.

“Haha.. Ngisi  huna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya hilo , tupo nchi kavu  na huwezi tumia matamvua yako kirahisi. Ni kheri ukawaacha Mchafu na Mhunzi kudili na hili swala”Aliongea Mameni.

Wakati wakiwa wanaongea walitoka  ma kwenda  moja kwa moja mjini Limour  kupitia magari yao ya kifahari.

Nje ya Bar moja  mjini Limour, kulikuwa kumejazana watu. Walikuwa ni wanaume na wanawake , wazee na vijana  na karibia kila mmoja amevaa  staili yake. Ndani ya eneo hilo kulikuwa na taasisi mbalimbali kutoka pande karibia zote za ulimwengu  ambazo zimetuma wawakilishi kwa ajili ya kushiriki katika baraza la Maksi.

Sasa ndani ya hii Bar, ndio vurugu ilipokuwa imetokea baina ya watu wa Wimbi la Chumba na  masenari wa kundi la Barham. Ilikuwa ni pata shika.

Kitendo cha kufanya watu wengi kusimama nje kuangalia  mapigano hayo, ilifanya watu wengi kusogelea eneo hilo.Licha ya kwamba vita ilikaribia kuisha lakini  hali ya Bar hio haikuwa ikitamanika tena , kwani  meza  na viti vilikuwa vimeharibika na kusambaa kila sehemu huku  chupa  nyingi zikiwa zimepasuka chini.

Upande mmoja katika Bar hio lilionekana kundi ambalo lilikuwa limevalia mavazi ya kijeshi  ya rangi ya kijivu na isignia za mchoro wa mawimbi kwenye vifua vyao na  mabegani.

Upande mwingine  lilikuwa ni kundi lililovaa mavazi ya kijeshi rangi ya jangwa   wakiwa na isignia za nembo ya nyota kifuani na mabegani.

Masenari hao wote walikuwa katika mavazi yao ambayo yalikuwa yamechafuka kwa damu. Na walikuwa wamesimama pande zote mbili wakiangaliana huku wakihema kwa nguvu.

“Nini kinaendelea hapa?”

Muda huo  mwanaume na mwanamke alieongozana na kundi la wanajeshi  wa kimasenari walijipenyeza katika kundi la watu waliosimama nje ya bar  na kuingia ndani.

Baada ya kusikia sauti hio  watu wa upande wa  kundi la Wimbi la chuma walikakamaa miili yao.

“Ripoti kwa  Afande Gray. Ni hili kundi la Barham limejaribu kutuletea vurugu. Kwa ajili ya kulinda hadhi ya  kundi letu  tukaamua kupigana nao”Aliongea.

Mwanaume na mwanamke alieingia hapo alikuwa ni Gray na Helena. Baada ya ripoti hio Gray aliwaangalia  Masenari saba wa kundi la pili  na kisha akatabasamu.

“Marafiki ,  Mnaweza kuwa  watawala katika peninsula ya  Uarabuni , lakini hapa ni  Ufaransa”

“Mh ! Kama sio watu wako kutuchokoza tusingekuwa na muda na nyie”Aliongea mwanajeshi wa Kimasenari wa kundi la Barham huku akitema mate chini.

“Oh! Walimuongelea vibaya Lucifer nini?”Aliongea Gray  huku akiwaangalai watu wa kundi lake.

“Sir tulikuwa tukiongelea kuhusu Lucifer kupotea  baada ya kupigana na Black Emperor . Je tumekosea wapi?”

“Mshenzi! Mlikuwa mkimuongelea vibaya bosi wetu na kusema  baada ya vita alipotea baada ya kupoteza uwezo wake ndio maana mpaka leo anaoagopa kujitokeza. Dunia nzima inajua  ni Prince aliemuua Black Empor kwa ajili ya amani ya dunia. Kwa ajili ya kuifungua katika minyororo ya giza aliamua kupigana vita takatifu na kuwaachia   huru waliofungwa gizani na Mahakama takatifu. Master ni mtu wa haki  ndio maana hata baada ya kushinda aliamua kutawanyisha watu wa Inferno ili wasijikusanyie umaarufu na ushawishi kuingilia mambo ya ulimwengu wa kawaida. Hata viongozi wetu  wa Barham ni watu wa  haki. Unatoa wapi ujasiri wa kumuongelea Master vibaya?”Aliongea  Mwarabu huyo na  kumfanya Helena kucheka.

“Nyie watu wa Barhams, siku hizi mpo sensitive sana. Tunajua mnamwabudu bosi wenu lakini  kuna haja ya kupaniki baada ya kusemwa kidogo tu?”Aliongea Helena.

Kati ya Masenari hao , kuna mmoja ambae alikuwa amekaa , mwanajeshi aliekuwa na nyota  kwenye  bega lake. Alikuwa ndio kiongozi wa  kundi hilo la Barham. Mara baada ya kuona Helena anacheka kwa dharau alisimama na kusogea mbele.

“Wewe Gray na Helena  watu wa  kundi la Wimbi la Chuma nimeyasikia sana majina yenu  lakini sijawahi kudhania  watu wa sifa  zenu mtakuwa kichefuchefu namna hii. Ijapokuwa mimi Kent ni  Kiongozi wa kikosi tu  najua  heshima za msingi zidi ya   watalaamu wa daraja la  Ugwiji , nje na ndani ya kundi letu. Bosi wetu sio mtu wa kuongelewa na  mtu mwenye mdomo mchafu kama wewe. Hata kama alituacha kwa muda mfupi , yeye ndio  kiongozi wetu , mtu wa imani pekee tuliekuwa nae . Kama ujasiri unao , tangaza vita na kundi letu  hapa hapa. Nyie kumi  na mbili  mtashambuliana na sisi   saba  na hamtoweza kutushinda. Kwa uwezo wenu mdogo hata mwanajeshi wetu wa daraja la chini hamuwezi kumshinda”

“Haha.. Majigambo meengi. Kama tusingewaonea huruma  mnadhani mngeendelea kusimama?”Aliongea mwanaume wa upande wa Metal Tide.

“Eti mmetuonea huruma. Kama mmetuonea huruma mngekuwa  na nundu usoni?”Aliongea Kent.

“Nyie , mmeshinda si kwasababu mlitutega , mlikuwa na siraha na sisi hatukuwa nazo’

“Kuna chupa kibao haba ambazo mngeweza kutumia kama siraha  lakini mkashindwa , msilaumu kwa uzembe wenu. Haishangazi ndio maana kwa miaka mingi  mmebakia kuwa kundi la daraja A. Moja ya mafunzo ya mkuu wetu anatusisitizia;   kufanikiwa zaidi ni kukubali  kushindwa na  kuyatambua mapufungu yako”Aliongea Kent.

“Damn it! Sir Gray wanaendelea kutudhalilisha tu”

“Jina lako ni Kent sio? Maneno yako uliongea yametukosea sana. Piga magoti chini na uombe msamaha , la sivyo usije  kutulaumu kumdhalilisha Master wako Azzle”Aliongea Gray.

“Nipige magoti!?” Kundi lote la Barham walitunisha vifua huku wakikamamaa miili kwa kujiamini, “Hata mkuu wetu Azzle hawezi kutuambia tupige magoti. Sisi Barham ni  watiifu kwa Mfalme wa  kuzimu pekee” Mara baada ya kuongea hivyo aliwapa ishara vijana wake na kuanza  kupiga hatua kutoka katika Bar hio lakini Gray  alisogea na kusimama mbele ya Kent.

“Usipopiga magoti na kuomba msamaha , usifikirie kabisa kuondoka hapa kirahisi”

“Pisha njia” Kent alikuwa na hasira mno. Palepale alikusanya nishati ya mbingu na ardhi na kumsukuma Gray.

Ingawa hakukuwa na mabadiliko sana , lakini katika vita halisi  , tena vita mchanganyiko kama hivyo utofauti wa nishati  ya mbingu na ardhi ulikuwa  na faida kubwa. Ilikuwa ni vita ya   kifo , unapigana ukiwa na  nafasi ya kushinda  na kama hakuna  njia rahisi ni kuondoka ndio maana Kent aliongoza watu wa kundi lake kuondoka.

Gray mara baada ya kuona Kent anajitutumua  haraka sana alikunja ngumi yake na kumrushia Kent.

“Bang!

Gray alikuwa ni  mpiganaji ambae pia alifikia katika daraja la  Ukaidi wa asili na mwanzo wa ufunuo wa mwili mpya , hivyo kwa namna flani alichukuliwa kama  mbobezi.

Ngumi yake ambayo ilikuwa imeambatana na nishati ya mbingu na ardhi ilikuwa nzito kiasi kwamba  ilimfanya  Kent kutetemeka mwili.

Arghhhh!

Mfupa  katika mkono wake ulipinda  mara baada ya  kujaribu kupangua ngumi ya Gray,  uliumia na kumfanya ashindwe hata kukunja ngumi tena.

Kundi la nje ambalo walikuwa wakiangalia waliona  Kent alikuwa akijikadiria kwa  viwango vya juu kutaka kupigana na  mtu kama Gray  ambae hakuwa katika daraja sawa la  uwezo.

“Unadhani sisi watu wa kundi la Metal Tide hatuna uwezo? Piga magoti na omba msamaha  kabla ya kufikiria kuondoka”

Kent aliishia kusaidiwa na wenzake wawili kusimama juu  na  hakuonekana kukubali kushindwa kirahisi.

“Mwanajeshi wa  daraja la ukaidi wa asili , kushambulia mtu kama mimi ambae ni kiongozi wa kikosi  ni sawa na kujidhalilisha. Lakini  hata kama  tutakufa hapa hapa sisi Barham hatuwezi kupiga goti na kuomba msamaha  kwa watu washenzi kama nyie”

“Umeongea vyema!”Sauti ilisikika kutoka nje ikiambatana na makofi.

Muda huo kundi lilitawanyika baada ya wanajeshi waliojazia miili wa Barhampton Empire kutengeneza njia kwa ajili ya Azzle alievalia  kombati za kijeshi na Asmuntis  alievalia jacketi la kijani kibichi kupita.

Watu baada ya kuona  wanajeshi hao wawili , walijihisi ni kama miili yao imetawaliwa na  presha  kubwa na kufanya wahisi woga.

“Oneni sana , yule ndio Bwana wa Vita. Marshall wa  kundi la Barham, Kapteni Azzle mwenyewe”

“Msisimko anao toa ni wa ajabu mno. Inafanya watu  kuwa na wasiwasi  kwa kuangaliana nae usoni tu. Kama ilivyokuwa inasemekana  moja  kati ya   mashetani kumi na mbili wa  Inferno waliosalimika katika vita takatifu hawa ni moja wapo”

“Hey! Achana na  Azzle , angalia alieambatana nae , yule ndio Asmuntis mwenyewe, Assassin namba moja duniani! Bosi na mmiliki wa kundi la  wauaji la Baffodil DayDreamers! Ni adimu sana kujianika hadharani”

“Mungu wangu! Inamaana umoja wa Inferno unajikusanya upya, wanapanga kushiriki katika Baraza la Maksi au?”

“Inawezekana , Lucifer hajulikani alipo , hivyo ni kawaida kwa Baffodil na Barhampton kuja kushiriki”

Kundi lote la washiriki wa Baraza la maksi waliokuwa katika eneo hilo walikuwa wakiongea wao kwa wao kwa kile walichokuwa wakifahamu , lakini Azzle na Asmuntis  wala hawakujali kabisa

Azzle aliwapita Gray na Helena na kwenda kusimama mbele ya  Kent akimwangalia.

“Vipi  umeumia?”

Kent na wenzake mara baada ya kuona kiongozi wao amefika , walijikuta wakipatwa na ahueni na kufarijika kwa wakati mmoja.

“Report  kwa Kapteni! Ni majeraha madogo tu”Aliongea  akijikakamua na Azzle alitingisha kichwa na kisha aliwageukia Gray na Helena.

“Umemuumiza mtu wangu. Ni mkono upi ulioutumia , uvunje mwenyewe kabla sijachukua hatua”

Kauli hio ni kama vile Gray alikuwa amekuhukumiwa kifo , hakuweza kuleta ukinzani tena.

“Kiongozi Azzle nakuheshimu sana. Wewe ni mwanajeshi mwenye nguvu  na hadhi kubwa , lakini huna mamlaka ya  kuniamrisha kufanya chochote. Kundi letu ni  la daraja sawa na la kwako. Kwanini usianze kwanza kujua nini kimesababisha haya yote?”

“Haina haja  kwani vijana wangu  hawawezi kufanya kosa  kwasababu wanajua   matokeo yake ni nini  ikiwa wamekosea”

“Hapa sio  Uarabuni. Wewe ni maarufu tu kama Ares wa Peninsula  ya Uarabuni , lakini huwezi kuziba  anga  lote na mkono. Gray tuondoke , Kapteni anatusubiria”Aliongea  Helena  na Gray alitingisha kichwa kukubali

“Tuondokeni”Aliongea Gray akiwapa ishara vijana wake.

Mara baada ya agizo hilo , wanajeshi wa kundi la Metal Tide walianza kutembea kutaka kutoka , lakini Azzle na mwili wake kama wa  tembo  alienda kusimama mbele ya Gray na Helena kuwazuia.

“Kubali kupoteza mkono au ufie hapa hapa . chagua moja”Aliongea Azzle akiwa siriasi kiasi kwamba macho yake ni kama yamejaa moto wa kuzimu, kusudio lake la kuua lilikuwa limetawala Bar nzima.

Gray na Helena waliishia kuangaliana na bila kupenda walijikuta wakipiga hatua mbili kurudi nyuma. Na muda ule ghafla tu  walisogea kwa spidi  katika pande mbili tofauti na kuanza kumshambulia Azzle  kushoto na kulia.

Ukweli ni kwamba walikuwa wakijua ni ndoto ya mchana kuweza kumshinda mtu wa daraja la Azzle  kwa kupambana mmoja mmoja , hivyo  waliona angalau wakishambulia kwa wakati mmoja wanaweza kufanikisha.

Hawakutaka kukimbia pia kwani ingewafanya  watu kuwadharau. Lakini bado mtu wanaepambana nae alikuwa ni  hatari mno , mtu kuwa  moja ya sehemu ya watu wa karibu wa Hamza halikuwa swala rahisi hata kidogo.

Azzle hakuonyesha mabadiliko kabisa , mara baada ya kuona shambulizi la  Helena na Gray limekaribia shingo yake , palepale alifyatua mikono yake  yote miwili kwa wakati  mmoja na kupangua mashambulizi yale.

Bang  Bang!

Kwa wepesi kabisa aliweza kuyapangua  na kwa wakati mmoja alinyoosha mikono yake akijaribu kuwakamata wote wawili . Lakini Gray na Helena  haraka sana walifyatuka wakimkwepa baada ya kuona mashambulizi yao  hayakuzaa matunda.

Baada ya hapo wote wawili walikuwa wakishambulia kitahadhari wakimkwepa Azzle asiwakamate.

Azzle alikuwa amesimama katika eneo moja , hakuwa amesogea hata kidogo na ni mikono yake tu ndio iliokuwa ikicheza , alikuwa na nguvu za mikono  kiasi kwamba alionekana kama sio binadamuwa kawaida. Licha ya kushambuliwa,  Gray na Helena ni kama walikuwa wakigusana na chuma  kwani hawakumwathiri hata kidogo.

Asmuntis upande wake aliishia kusimama tu akiangalia  , huku akiwa hana nia ya kusaidia.

Kundi lote nje lilijawa na hamasa na shauku  katika kuangalia pambano hilo , asilimia kubwa  ni wanajeshi waliokuwa katika daraja la  chini kabisa katika mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi hivyo waliokosa ujuzi na ufunuo, hivyo kwa pambano kama hilo wasingeweza kulimudu.

Mara baada ya kumshambulia kwa dakika kadhaa , Azzle ni kama alikuwa akiwasoma muda wote na alionekana kugundua udhaifu wao . Ghafla tu  Azzle alipiga hatua kubwa  mbele na kumshika Gray mkono wake mmoja.  Gray ambae alikuwa akitaka kushambulia alijikuta akigutushwa  na shambulizi hilo  na kutaka kusogea  lakini sasa kabla haja sogea Azzle alikuwa tayari asharusha  ngumi  kwa kulenga bega lake.

Kwa namna alivyofyatuliwa ni kama alikuwa mpira , kwani alipaa hewani na kwenda kutua  mbele ya Helena ,  na mwanamke huyo hakuwa na jinsi zaidi ya kumkwepa  Gray na ile alipotua kilichosikika ni Kwacha.

“Arghhhhh!!

Gray alitoa ukulele mkubwa baada ya mkono wake mmoja kuvunjika

“Nilikuambia  vunja mkono wako au  kufa  ila hukunisikiliza”Aliongea Azzle.

Shambulizi  lile liliwafanya watu wengi kushangaa baada ya kuona  licha ya Azzle kushambuliwa na watu wawili , lakini hakupata jeraha hata moja

“Muue . haina haja ya kumuacha akiendelea kuishi”Aliongea Asmuntis  aliekuwa pembeni.

Gray na Helena walijikuta akiwa   katika mshituko mkubwa , hata Gray ambae alikuwa  katika maumivu  alijikuta yakipotea kutokana na kauli ya Asmuntis.

“Ngoja niwaache , kesho ni ufunguzi wa  baraza la maksi . Haina haja ya  kulikuza hili swala . Sitaki kuona sura zenu hapa tena , waambie watu wako wakae mbali na sisi”Aliongea  Azzle akimuonya Helena.

“Mhunzi , wapo hapa kutafuta ugomvi tu , kuwaacha  hai ni  kuwapa kiburi  cha kutuchokoza zaidi”

Azzle alikuwa sio mjinga , mara nyingi katika tukio kama hilo ilikuwa ni mtego umewekwa . Metal tide wametuma watu dhaifu ili kuibua ugomvi ili baadae  Gonzalez akiingilia mwenyewe na hata Hamza kujitokeza na kupigana , watu wa baraza wasingemhukumu kwa kusema anajitafutia sifa.

Sasa kwasababu walijua Hamza ni dhaifu kama kweli atapigwa  na Gonzalez basi moja kwa moja ingekuwa rahisi sana kwa  bwana huyo kupata hadhi ya Ugwiji.

Ki ufupi ni kwamba mtego huo alikuwa amewekewa Hamza ili aingie  kati na  Gonzalez achukue hatua.

“Kama unataka kutuua tuue tu. Sisi ni wanajeshi sio Maninja”Aliongea Gray.

“Mhunzi!” Aliita  Asmuntis  huku akijua kwa tabia ya kizamani ya Azzle asingechukua hatua ya kuwaua. Lakini  Asmuntis yeye kama muuaji hakujali watu watamfikiria nini kama atawaua  hivyo alipiga hatua kusogea.

Gray na Helena mara baada ya kuona kweli Asmuntis anasogea  walijikuta wakianza kupaniki.

Watu waliokuwa nje walijikuta pia wakishangaa , wakiwa hawaamni  kama kweli  Asmuntis  kiongozi wa  wauaji wa kundi la  Bafodili anakwenda kuua wanajeshi wa kundi la kimasenari la Metal tide.

Kama angefanya hivyo maana yake ni kwamba  kabla hata ya baraza , Baffodil ingejiingiza katika ugomvi na Metal Tide .

“Inasemekana aina ya mauaji ya King of killers ,  Asmuntis  hayajawahi kukosa sababu ..Na kama akichukua hatua huwezi hata kujua namna unavyokufa”Watu walianza kuongea wao kwa wao.

“Kwa uwezo huo si  hao watu wameisha tayari”

“Lakini  mkumbuke huyu ni muuaji wa siri, yaani Assassin , lakini hapa si  hadharani, Sidhani kama atamuua Gray na  Helena kirahisi”

Wakati maneno yakiibuka kati ya kundi hilo la watu waliokuwa wakiangalia , upande wa  Gray na Helena  ulikuwa ni  wa kutia huruma. Hisia zao zilisimama pia kwa presha kubwa  iliokuwa ikiwasogelea kutoka kwa Muuaji namba moja duniani.

Asmuntis  aliishia kusimama mara baada ya kutembea kwa hatua kadhaa huku akiwaangalia , hakuwa mrefu sana wala hakuwa na mwonekano wa kupendeza , lakini msisimko aliokuwa akitoa  ulikuwa ni wa baridi  na kufanya wahisi ni kama  wanachomwa na vichomi vya baridi mwilini.

“Uchokozi wenu ni wa kijinga sana”Aliongea Asmuntis.

Kabla ya Gray na Helena kujibu  ghafla tu walishuhudia  Asmuntis akipotea mbele yao  na ile  anatokea kwa mara nyingine kilichosikika ni;

‘Clang!!’

“Haaa !”

Kundi lote la  watu lilipiga kelele ya mshangao , waliweza kuona Asmuntis alikuwa amekwisha kumfikia Gray alipokuwa  akitaka kumchinja na kisu, lakini matokeo yake hakufanikisha baada ya  mkono uliokuwa mgumu kama chuma kuzuia shambulizi lile.

 

Previoua Next