Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

SEHEMU YA 198.

The White Queen.

Nyakasura mara baada ya kumuona Hamza amefika , alifuta midomo palepale na kumwangalia:

“Nimesikia hapa kuna  farasi , nipeleke basi nikaendeshe?”Aliongea na Hamza kabla ya kumijibu aligida pafu la bia kwanza;

“Farasi wapo upande ule kwenye zizi. Unaweza kwenda na kuchagua mmoja na kumtoa nje , kwanini unataka nikupeleke?”

“Mimi ni mgeni hapa, si sahihi kwa mwenyeji kunipeleka?”Aliongea Nyakasura  akiwa hajaridhika.

Hamza alijiambia ni mgeni gani anajikaribisha mwenyewe , lakini kutokana na kuhofia  tabia  yake  aliamua tu kumkubalia.

“Sawa nitakupeleka ukaendeshe”

Nyakasura kusikia hivyo , furaha ilimvaa palepale na kuchukua mhindi wa kuchemsha na  kumnyooshea achukue.

“Hivyo ndio inavyotakiwa , malizia na huu muhindi kwanza”

Hamza aliangalia mhindi huo , ingekuwa afadhali ulikuwa haujaguswa ila mwanamke huyo alikuwa amekula  nusu na kuubakisha na kibaya zaidi  ulikuwa na mate ya kutosha.

“Asante ila nimeshiba sana”

“Mh! Nilikuwa nakujaribu tu , siwezi kuruhusu mtu wa kawaida kama wewe kumalizia nilichoanza kula”Aliongea.

Pembeni Leviathani , Mameni na wengine mara baada ya kuona tukio hilo waliishia  kutingisha  vichwa vyao tu , waliona  ni msichana huyo pekee ndio anaeweza kumuendesha Hamza atakavyo ila sio wao.

Ilibidi wawaache wengine kumalizia kutafuna nyama huku  wao wakiongozana mpaka kwenye zizi la farasi

“Mbona  wote ni weusi tu , hakuna mweupe?”Aliuliza Nyakasura huku akionekana kutoridhishwa na farasi hao.

“Hawa weusi ndio wazuri sasa, wana damu ya  kifalme   na ni ghali zaidi kuliko farasi wa kawaida. Wewe ni Nyakasura hivyo unapaswa kuendesha wa hivi , kwanini unataka kuendesha kulingana na rangi yake?”

Nyakasura mara baada ya kusikia hivyo , aliona ni kweli  na  aliridhika na maelezo ya Hamza.

“Upo sahihi , mimi pia nina damu ya kifalme hivyo napaswa kuendesha  farasi yenye damu ya kifalme. Leo umejua  kuniridhisha na maneno yako”

Hamza aliishia kufurahi  kisirisiri , ni kama sasa alijua namna ya kudili na mrembo huyo , ili kumfanya akubali ni kuongea kile ambacho anataka kusikia.

Hamza alimtoa  farasi mmoja mpaka nje ya zizi na kisha kumpa ishara ya kupanda.

Nyakasura  mwili wake ulikuwa mwepesi mno  kwani aliruka na kutua katika mgongo wa farasi juu ya tandiko lake  na kisha  alishikilia hatamu. Farasi ile  ilionekana kutishika na kuanza kupandisha miguu yake ya mbele hewani ikitaka kumtupia Nyakasura chini.

“Ahh! Inafanya nini hii ?”

Nyakasura yalimshinda na alijikuta akiruka kutoka kwenye  Farasi  na Hamza haraka haraka alisogelea  ile farasi na kuishikilia.

“Wewe umefanya kuirukia ulifikiria   ni bindamu huyu , kwanini usingepanda kawaida tu?”

“Sasa si ungesema , au ulitaka  kuona nikidondoka?”Aliongea huku akiwa ameweka mikono yake kiunonni.

“Sasa mimi ningejuaje kama inaogopa kurukiwa?”Aliongea Hamza akijitetea na kumfanya Nyakasura kumwangalia kwa macho ya  mashaka na kisha alipanga kujaribu tena.

“Wewe Farasi ole wako utake kunidondosha tena , nitakugeuza nyama”Aliongea Nyakasura bila ya kujali farasi hio ilikuwa ikielewa maneno yake au lah.

Mara baada ya kupanda , hatimae alifanikiwa kukaa bila ya  farasi ile kuleta ukinzani

“Haha.. Hamza umeona  hii farasi inaniogopa?”

“Ni kweli kabisa. Inaonekana  kuogopa nguvu zako za kifoeniksi”Aliongea Hamza kumridhisha.

“Tembea”

Nyakasura alitingisha ile hatamu ya farasi  lakini   farasi ile haikusogea hata kidogo  zaidi ya kutingisha kichwa chake kulia na kushoto.

“Hii farasi mbona imekaa kivivu vivu , kwanini haitembei?”Nyakasura alijikuta akikasirika baada ya kuona farasi hio inakataa kumtii, “Wewe farasi kimbia”

Hamza  alitamani kucheka  kuona mwanamke huyo  anataka kuendesha farasi kwa kuiamrisha na maneno.

“Hebu fanya kukandamiza miguu yako  kwa pamoja kwenye  tumbo lake  uone”Aliongea Hamza.

Nyakasura alifanya kama Hamza alivyoongea na  kweli farasi ile ilianza kutembea kwenda mbele.

“Wow! Inatembea. Vipi nikitaka itembee kwa kasi?”Aliuliza na Hamza alifikiria kidogo.

“Unaonaje tukiendesha pamoja , nitakufundisha  kidogo , ijapokuwa hio kamba ni kwa ajili ya kuongoza lakini  mwili wako ndio  unaoweza kuiongoza farasi kwa haraka”

“Sasa unabwabwaja nini , panda haraka unifundishe”Aliongea Nyakasura, muda huo hakufikiria sana alichotaka ni kujua kuendesha basi.

Hamza palepale alipanda  juu ya farasi na kwenda kukaa nyuma ya  Nyakasura. Awamu hio wawili hao walikuwa wamekaribiana mno  na  Hamza aliweza kuhisi ulaini wa mwili wa mrembo huyo.

Upande wa Nyakasura pia aliweza  kuhisi kitu cha tofauti na kufanya   uso wake kukakamaa  na mara baada ya kukandamiza lipsi zake aliishia kukaa kimya.

“Inama kidogo kwa usawa wa mwili , kisha shikilia hio hatamu vizuri. Hizi lijamu zote zinatumika  kuongoza farasi  na pia ni kama  breki  unapotaka kupunguza na kuongeza mwendo. Ukiona  spidi yake ni ndogo  tumia  mjeledi  kuichapa kwa upole  kuihimiza iongeze mwendo”

Hamza alimwelekeza kwa vitendo  Nyakasura huku akiwa ameshikilia mikono  yake  namna ya kushikilia hatamu na kisha alimshika kiuno na  kuweka sawa mwili wake.

Ni muda huo sasa Hamza aligundua  ndani ya koti jekundu alilovalia ndani alikuwa amevalia  nguo nyeusi ambayo ilikuwa imebanana na mwili wake kutokana na wepesi wake , aliweza kuona kutokana na kikoti kile kupandisha juu na kuacha kiuno wazi.

Mara baada ya farasi kuanza kutembea , miili yao ilianza  kucheza kwa kupanda na kushuka na kufanya  Hamza  mwili wake kuzidi kujisugua katika ngozi  laini ya mrembo Nyakasura. Hisia alizokuwa akipata zilikuwa za ajabu kabisa.

Hamza mara baada ya  kuona  eneo lake la mbele limemkaribia sana Nyakasura ilibidi atumie magoti yake kukandamiza makalio ya Nyakasura ili kugosea nyuma , lakini sasa mkandamizo huo  ulimwongezea msisimko  na kumfanya ashindwe kujizuia na kukandamiza tena.

Upande wa Nyakasura hakuwa akijua kinachoendelea , alikuwa akifurahia hisia za kuendesha farasi kwa spidi. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuendesha  farasi.

“Hamza angalia  inavyoenda kwa spidi.. hahaha.. kumbe kuendesha ni raha mno , nikirudi nyumbani  lazima ninue farasi”Aliongea Nyakasura  kwa fuaha huku akiona  ashagundua namna nyingine ya kupoteza muda.

Lakini Hamza aliekuwa nyuma alikuwa akifurahia hisia nyingine. Alichokuwa akifikiria muda huo ni  kama mrembo anaemkandamiza  makalio yake ni  mrembo maarufu anaefahamika kama Phoenix Girl.

Nyakasura muda huo aliweza kugundua kuna kitu  kigumu kama mti  kinachomkandamiza eneo la karibu na kiuno chake  na  bila kuwaza sana alipeleka  mkono kugusa ili kujua ni nin.

“Ah!”

Hamza aliekuwa  kwenye fantasy zake alijikuta akishituka  mara baada ya  mwanamke huyo kushika naniliu yake.

“Ni nini hichi ndani ya suruali yako?”

“Nyakasura hakugundua mara moja  na alikuja kujua mara baada ya kuminya na kuhisi joto lake.

Haraka sana  alitoa mkono wake kama vile ameshika kitu cha moto  huku  sura yake ikipatwa na moto. Alishikwa na aibu kiasi kwamba hata pumzi ilimkata.

Kubwa zaidi ni kwamba baada ya kushika  hicho kitu, kilibadilika na kuwa  kikubwa zaidi  na kwasababu farasi ilikuwa mbio  kitu kile kilizidi kujisugua katika  eneo la kiuno mpaka kwenye mgongo wake  na kumfanya ajihisi  hali ya ajabu mno.

Tokea  awe mdogo , Nyakasura hakuwahi kukutana na tukio la namna hio  kwenye maisha yake  na ndio maana  alishindwa kujua ajiweke vipi katika hali ya  ajabu iliojitokeza kama hio.

Upande wa Hamza aliishia kutabasamu kifedhuli huku akizidi kusikia raha namna  msuguano ulivyokuwa ukiendelea na alisogea karibu zaidi.

“Wewe.. mshenzi usinisogelee..”Nyakasura alijikuta akishindwa kujizuia na kuongea kwa nguvu.

“Sio kama nakusogelea , ni kwasababu  Farasi inatembea kwa kasi  na kunitingisha”

“Basi , iambie isimame”

“Sawa!” Hamza palepale alishikilia  kamba ya Farasi na kisha akapunguza mwendo.

Nyakasura  muda huo alijihisi ni kama amegeuka na kuwa mtiifu ghafla  na kujikuta akipandwa na hasira.

“Wewe mwanaharamu , kwanini unanishika?”

“Sijakushika , mimi nilikuwa  nikijaribu  kuzuia farasi isije kutudondosha”Aliongea Hamza akiwa na mwonekano wa kizembe.

“Na vipi kuhusu hapo chini , ulikuwa unafanya nini?”

“Hii ni hali ya kawaida kwa mwanaume. Nisipokuwa hivi kwa mwanamke mrembo kama  wewe  inabidi niende hospitalini nikapimwe”

Nyakasura mara baada ya kusikia neno mwanamke mrembo  hasira iliokuwa kwenye moyo wake ilipotea palepale  na alijikuta akipepesa macho na kushikilia hatamu ya  Farasi na kuifanya isimame moja kwa moja na kisha aligeuka na kumwangalia Hamza.

“Unahisi mimi ni mrembo?”

“Ndio”

Hamza hakuongea uongo , mwanamke huyo alikuwa mzuri mno ambae alikuwa na  ile hadhi ya   uanamke  Clasic na ukisasa.

“Upo sahihi , kwa  mwanamke mrembo kama mimi ni ngumu kujizuia.Lakini naomba uelewa kitu  kimoja nilipohisi  hicho kitu chako mgongoni  nilikigusa  bila  kujua , huruhusiwi  kunitania  kwa  kusema nimegusa makusudi la sivyo  nitakachokufanya hutosahau”

Hamza aliona mwanamke huyo alikuwa mwepesi kutegeka kuliko hata Regina , hivyo haraka haraka alitingisha kichwa kukubali.

Hakuna shida kabisa, siwezi kuongea. Halafu kwa  mwanamke mrembo na hatari kama wewe naanzaje kwa mfano?”Aliongea Hamza  na Nyakasura aliruka kutoka kwenye farasi na kutua chini.

“Huna haja ya kujitetea , najua  kabisa mwanaume kama wewe  huna damu ya kifalme na hadhi  ya familia yako ni ya kawaida , hivyo ni kawaida kujiona  wa hadhi ya chini kuliko mimi. Lakini angalau unajitahidi , kuna vitu vichache tu unapaswa kuvifanyia kazi  hasa kuboresha silika yako  na kujiamini kidogo , ukifanikiwa unaweza  kujaribu pengine naweza kukupa nafasi”

Hamza mara baada ya kusikia hivyo  hakujua acheke ama alie  na kujiuliza anaongea nini , mbona  imegeuka ni kama  anamfukuzia?.

“Madam  Nyakasura  kwa hadhi yako ilivyo kubwa natoa wapi ujasiri wa kujaribu kukukaribia? Isitoshe nimekwisha oa  tayari  ,  siwezi kuwa na  wazo hilo zidi yako”Aliongea  Hamza huku akicheka na muda huo Nyakasura alikumbuka Hamza alikuwa amekwisha kuoa.

“Oh tena nimekumbuka kumbe umeoa , kama ni hivyo basi kazi unayo. Lakini najua mke wako hawezi kunizidi uzuri  hivyo  huwezi kuacha kunifikiria. Nikushauri ukijihisi  umeshaanza kunipenda ili kunipata unapaswa kwanza kumtaliki mkeo , vinginevyo siwezi kukubali”Hamza mara baada ya kusikia hivyo kidogo tu atapike.

“Nyakasura  usinielewe vibaya ,ni kweli sina  mawazo hayo kabisa na wewe. Tuwe tu  marafiki na nipo hapa  kukufndisha  kuendesha farasi na kilichotokea ni bahati mbaya tu  kama mwanaume”Hamza aliona ni vizuri kujielezea.

“Unakataa nini? Si wewe ulieniita mrembo sasa hivi  na  hata kupandisha midadi yako kwasababu yangu?”

“Hamna bwana ni..” Hamza alishindwa kujua namna ya kujielezea , aliona ni kama stori nyingine sana ambayo ingekuwa na mwisho mwingine.

“Nadhani nishaanza kukuelewa sasa , unaonekana kwenye moyo wako unanitamani , lakini unaogopa nitakukataa. Kama mwanaume sioni ni ajabu  kuvutiwa na mwanamke mrembo kama mimi , hivyo usiwe na wasiwasi , siwezi kukucheka” Mara baada ya kuongea hivyo alijishika kiunoni kuonyesha umbo lake vizuri.

“Sittaki kuendesha  tena , narudi zangu  kwenye nyumba kule , Berlly amesema atanipa mvinyo mtamu , naenda kunywa”

Hamza hata yeye hakutaka kuendelea kujielezea mbele ya mwanamke huyo , maana aliona kabla atakavyoongea ndio  namna atakavyoharibu.

Mara baada ya kurudi , Hamza alimpeleka farasi yule kwenye zizi na muda huo aliweza kuhisi kuna mtu aliekuwa akiingia katika zizi hilo. Hamza hakuwa hata na haja ya kugeuka kujua ni nani kwali alishamjua kupitia hisia zake ni Asmuntis.

“Boss!!”Aliita Asmuntis huku akiwa na uso uliosawijika.

“Nini tatizo mchafu? Mbona unaonekana kuwa na huzuni namna hio, unapaswa kuwa na furaha  kwa kukutana kwetu mara nyingine”Aliongea Hamza na kumfanya Asmuntis  kushusha pumzi.

“Nilikuwa na  mazungumzo na  Azzle  na tumeona itakuwa vizuri  kutowaambia  wengine kuhusu hali yako ili  tusije kuwapanikisha , nadhani unajua Berrly na Leviathani  walivyo. Lakini  kesho hata kama usipoenda kwenye Baraza , lazima Gonzalez atataka kukuchallenge. Amekuwa akiwazia nafasi yako kwa muda mrefu. Hivyo  tumeona ni vizuri kukaa chini na  kupata suluhisho”

“Suluhisho? Nyie mnadhani ni kipi kifanyike?”

“Tumeona kwasababu huwezi  kupigana , basi itakuwa ni vizuri  ukiwaruhusu wanachama wa INFERNO kupigana , hii ndio  njia pekee ya kulinda heshima yetu. Hivyo itakuwa vizuri  kama  tukimruhusu Sally kufanya safari ya kuja hapa haraka. Kwa uwepo wake  ndio njia rahisi ya kuweza kushinda”Aliongea Asmuntis  na maneno yake yalimfanya Hamza uso wake kuongeza usiriasi.

“Roho Mchafu  nadhani utakuwa umesahau? Nilishawahi kusema mwanzo  ili mradi  ninapumua  nitamlinda Sally kwa uwezo wangu wote na kutoruhusu  mikono yake kujichafua na damu. Ukimwambia Sally aje ni kweli atakuja lakini unajua nini kitatokea akiwa uwanja wa mapambano na  kushindwa kujidhibiti,  nini matokeo yake?”

Asmuntis aliishia kupanua mdomo wake tu  akitaka kuongea kitu lakini alishindwa na kuishia kutingisha kichwa.

“Bosi , upo sahihi , kumuita Sally kuja  ni hatari zaidi”

“Usiwe na waswasi Asmuntis , nakuahidi kesho hakuna kitakachotokea”Aliongea Hamza na kisha alitembea na kumshika   bega kwa kuligonga gonga kumtuliza aondoe wasiwasi  na kisha alitoka nje ya zizi.

Dakika ambayo alitembea mpaka nje  ya  nyumba aliweza kuona  magari kadhaa  ya Mercedenz Benz rangi nyeusi yakisogelea  ueleko wa shamba  yakiwa yamewasha taa za mbele  kutokana na giza.

Kila mtu  ndani ya nyumba hio aliweza kugundua kuna  mgeni aliekuwa akifika hapo  shambani na kufanya  watoke , akiwemo Nyakasura aliekuwa ameshikilia glasi  ya Blood Mary.

“Bosi ni nani? Au ni Metal Tide wameamua  kuja  mpaka huku?”Aliuliza Mameni.

“Hapana , kwa spidi ya gari  zao, inaonyesha sio watu waliokuja kwa ajili ya kutafuta ugomvi”Aliongea Hamza.

Haikuchukua muda mrefu  gari zile zilisimama  katika  eneo la kuingilia  katika  upande wa nyumba hio  na kundi la watu  lilishuka. Watu wote walikuwa wamevalia mavazi ya suti  na mashati ya rangi nyeupe na  tai. Kulikuwa na wazungu na watu weusi  na wote walionekana  kuwa  walinzi wenye mafunzo.

Muda ule kundi lile lilitengeneza safu mbili na kumuongoza mwanaume  wa makamo hivi,  mzungu  ambae nyewele zake alikuwa amezichana vizuri. Mkononi alikuwa ameshikilia Briefcase,  na kabla ya kupiga hatua alionekana akitingisha kichwa uelekeo wa Hamza na kisha alianza kutembea  kusogea  na jumla ya walinzi nane.

Ijapokuwa ilikuwa ni usiku lakini  kila mtu aliweza kuona bango  lililokuwa katika eneo  la kifua chake karibu na mfuko wa suti , ni bango ambalo lilikuwa na nembo ya  siraha na ngao  na chini yake kulikuwa na maandihi ya ‘SETH’.

“Ni mtu  kutoka Set Association”Aliongea Asmuntis.

“Inaonekana wapo hapa kwa ajili ya bosi”Aliongea  Azzle.

Sekunde chache tu  watu wale waliweza kufika mbele ya Hamza na wale walinzi  walimuonyeshea heshima Hamza na Nyakasura.

“Honorable Prince  of Hell and Phoenix Lady, I am a member of the Sytry Council. My name is Hewitt. Please forgive us for intruding and disturbing you.”Aliongea akimpa heshima Hamza kwa kumuita mtukufu Prince  wa kuzimu  na Bi Phoenix  na kujitambulisha kwamba ni mwanachama wa  Baraza la maksi  akifahamika kwa jina la Hewitt. Na anaomba radhi kwa kuwavamia usiku usiku.

Bwana huyo Hewitt alisaliamaiana na Hamza na Nyakasura tu , wakati akiwapa tabasamu wengine , ilikuwa ni ishara ya  kutoa heshima kwa  wataalamu wa mapigano wa hadhi ya Ugwiji.

“Kwanini mwanachama wa Baraza la maksi  kufika usiku usiku hapa kunitafuta?”Aliuliza Hamza na bwana yule  palepale alifungua ile Briefcase  na kisha alitoa  bahasha iliokuwa  ikimeta meta  kwa kumwagiwa madini ya almasi  na madini ya dhahabu  na kisha alifungua.

“Sir Lucifer , tuwie radhi sana , ukweli tulikuwa tukikutafuta sana kwa kipindi cha miaka miwili iliopita , lakini hatukuweza kukupata. Tumetunza  hii barua yako ya  mwaliko  kwa ajili ya kilele cha  magwiji mwaka huu , mpaka  tuliposikia kuonekana kwako leo hii, ijapokuwa tumechelewa ,  ila ni matumaini yetu utaupokea mwaliko kwa ajili ya kuhudhuria katika Baraza la maksi  mwaka huu”

Hamza aliishia kuangalia  bahasha hio ambayo ilionekana kutumia hela nyingi kwa ajili ya kuiandaa na kisha alitoa tabasamu.

“Ni mwaliko tu  kwani kuna haja  ya  kuyakuza  namna hii?”

“Kumbe hukupata mwaliko , mimi nilipewa  mwaliko mwaka jana”Aliongea Nyakasura.

“Haha.. bosi nilikuambia mimi , haiwezekani hawa watu wakakusahau? Kama usipoenda haiwezi kuwa kikao  tena”Aliongea Berlly lakini mwonekano wa  Azzle na Asmuntis ulizidi  kuwa siriasi. Kwasababu waliona kukubali kwa Hamza  kupokea mwaliko huo  maana yake aangeenda kuhudhuria.

Hamza licha ya kuona mabwana hao  walivyo na wasiwasi , lakini alipokea mwaliko ule.

“Hii bahasha mmeijua kupamba  vizuri mno , nadhani itakuwa vizuri kumpatia mke wangu”

Mara baada ya kusikia hamza akuongea hivyo ,  wenzake  walishangaa kiasi cha kuzimia.

Hewitt mara baada ya kuona mwaliko huo Hamza ameupokea , palepale alitingisha kichwa kwa ishara ya heshima.

“Wa kuheshimiwa , Prince  of hell na Phoenix Girl , barua  zetu zimepokelewa vyema   na tunatarajia ujio wenu siku ya kesho. Tumewaandalia siti  maalumu katika eneo la VIP kwa ajili ya Magwiji  wakati wa Baraza  likiendelea  na pia kutakuwa na siti hizo hizo maalumu katika kikao kikuu . Kama  mtakuwa na maswali yoyote  mnaweza kuwasiliana na  bodi ya wakurugenzi moja kwa moja. Nafasi zenu zitapatikana ndani ya  masaa ishirini na nne”

“Naona watu wa Set siku hizi mnazidi kuwa profesheno  na kufanya baraza la mwaka huu kuwa kama  sherehe ya kifahari , sio mbaya”Aliongea Hamza huku akihisi kusanyiko la mwaka huu litakuwa la kiheshima zaidi kuliko la  miaka mitano iliopita.

“Your encouragement is our motivation to move forward.”Aliongea Hewwit na kisha aliwapungia mkono kila mmoja na kisha aliongozana na kundi lake kuondoka ndani ya eneo hilo.

Mara baada ya watu wale kuondoka , Black Fog alimsogelea Hamza akiwa na wasiwasi.

“Bro , una uhakika unataka kwenda? Hata kama usiende hawawezi kusema chochote”Aliongea na  muda ule Nyakasura aliingilia.

“Wewe mtoto unajua nini? Kushiriki   katika Baraza kuu la maksi ni  raha sana  pia ni  mahali ambapo utaweza kukutana na watu wengi wazito. Au unaogopa   watakuchokoza kwasababu unaonekana mdhaifu . Usiwe na wasiwasi , kwanzia sasa hivi niite dada na nitahakikisha nakulinda”

“Miss Nyakasura , ijapokuwa  una cheo  cha Ugwiji , tafadhari naomba uniheshimu , mimi sio mtoto”

“Haijalishi unavyojiona , ila wewe ni mdogo sana kwangu .”Aliongea huku akimkagua  na kisha akaendelea , “Naona una umbo matata sana , hakika umejua kujitunza”

“Wewe..” Black  Fog hasira zilimjaa na  palepale alipeleka mkoo wake kiunoni  na kutoa  visu.

“Ah!” Asmuntis alikuwa fasta  sana kumzuia Roda kufanya  alichokusidia.

“Black Fog , umekuwa kichaa! Hebu acha kuwa mkorofi mbele ya  Miss Nyakasura, kwa uwezo wako mdogo  hustahili hata kupigana nae”

Black Fog  aliishia kupumua kwa nguvu kudhibiti hasira zake  na  aliishia kupiga piga miguu chini  na kisha alikimbilia  ueleko wa porini kwenye  shamba la chakula cha farasi. Huku Nyakasura aliishia kumtolea ulimi kwa kumuweza.

“Kwanini unamchokoza ,  anaonyesha wasiwasi wake juu yangu,. Kama wewe ni mtu mzima  kwanini usiwe kama mdogo wake kweli?”Aliongea Hamza.”

“Sio mdogo wangu, Kama ni kuwa na mdogo wangu  yupo  ila sio yeye”Aliongea Nyakasura.

“Oh!  Niambie huyo mdogo wako ni nani?”

“Wewe jua tu hivyo na  ni mtiifu kuliko  yeye, ni ..”Nyakasura alitaka kuongea lakini aligundua ni kitu ambacho hapaswi kuongea hivyo aliishia kumwangalia  tu Hamza.

“Kwani lazima nikwambie kuhusu mdogo wangu? Naenda zangu kunywa , kwaheri”

Hamza aliishia kufosi tabasamu , alitaka kumfanya aongee kidogo ili amjue zaidi lakini alionekana  kuwa  makini.

“Amekasirika kwa namna ulivyomfokea , itakuwa vizuri ukienda kumtafuta”Aliongea Hamza akimwambia Asmuntis.

“Usiwe na wasiwasi bosi , hawezi kufanya  chochote , Amefunzwa kuwa ngangari tokea akiwa mdogo”Aliongea Asmuntis na palepale  aliona aingize kitu kingine, ‘Lakini bosi  tunapaswa kufikiria mara mbili kuhusu hili suala la kesho”

“Najua unachotaka kusema ni mimi kutokwenda , ila nishakuambia  usiwe na wasiwasi. Ngoja nikamtafute mdogo wangu nimbembeleze”

Hamza mara baada ya kuongea alitembea kuingia katika shamba  la majani  kumtafuta  Chimera  na aliweza kumuona akiwa amekaa juu ya kifusi cha majani yaliokauka akiwa anaangalia juu angani.

Hamza aliishia kusimama kwa mbali akimwangalia  huku akionekana kufikiria na ni muda huo Black Fog aliweza kugundua kuna mtu aliekuwa akimwangalia.

Previoua Next