Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

SEHEMU YA 202.

Karibu kuzimu.

Katika zile Skrini kubwa  zilizokuwa zimezungushwa kwenye jukwaa  kulionekana kitabu kikubwa kilichokuwa  kina maandishi kikifunguliwa kurasa zake  huku yakionekana maandishi  yalioambatana na picha. Katika kitabu hicho ulionekana wasifu  wa Gwiji namba moja  na yule mshereheshaji palepale alianza kusoma maandishi yale  kwa  namna ya kuvutia;

“Amebeba wasifu  wa jina sawa  na  la  mfalme mkuu wa mithiolojia za Kiarmenia, ambae alifunga  elementi nne za mhimili wa dunia. Uwezo wake uliibua wivu mkubwa kwa watu wote wanaotumia nguvu za ziada kwa kuwa na uwezo uliomruhusu  kuzitumia elementi kwa faida yake pekee. Hakuna anaejua jina lake halisi ni nani , mwonekano wake ni wenye kubadilika  badilika milele. Ana uwezo wa kubadilika na kuwa  hewa  na ndio maana  watu wa ulimwengu wa siri wakaamua kumbatiza jina la Air . Makofi mengi  kwa ajili ya kumkaribisha Raisi wa Adept Association, Mr Air”

Mara baada ya  mshereheshaji kuongea  watu wote walipiga makofi na kisha walitulia kwa ajili ya kumuona gwiji namba moja akiingia. Lakini sasa,  hakuna  mtu yoyote alieweza kumuona  akiingia katika njia maalumu iliotandazwa   zuria   na badala yake  watu walishangaa tu mtu kuwa tayari amekwisha kukaa katika siti iliokuwa na jina  la Air  ndani ya jukwaa la Magwiji.

Alikuwa amevaa vazi la kikale  mfano wa joho lililofungwa  na kamba kiunoni. Licha ya mwili wake kuonekana lakini  sura yake haikuweza kuonekana  moja kwa moja na kujua alikuwa ni mtu wa rangi gani. Kwa namna ambavyo alifika katika jukwaa hilo ni kama vile aliteleport na kuibukia moja kwa moja  kwenye siti yake.

Kitendo kile cha ajabu kilifanya watu   ndani ya uwanja huo kupiga makofi  mengi sana na kupiga makelele ya  kumshangilia, hususani kwa binadamu ambao ni  wanachama wa umoja huo wa watu wenye vipawa maalumu.

Mr Air alisimama na  mkono wake ulionekana kupungia watu na kisha alirudi na kukaa  kwenye kiti chake.

Regina ambae alikuwa akiangalia mlolongo wa matukio hayo alijikuta akifikicha macho yake kwa nguvu  akiwa haamini kile ambacho anaona.

“Inawezekanaje , amewezaje  kufika pale bila ya kuonekana au ni kwa mazingaombwe?”

“Hapana ule ni uwezo wake,  anaitwa hewa kwasababu  anaweza kujifananisha na hewa na asiweze kuonekana  kwa macho. Hajawahi kujulikana kwa sura moja kwasababu kila anapotokea  ana sura tofauti  na sauti tofauti , hivyo hakuna anaemfahamu  ni sura  ipi ni ya kwake halisi  au kama alishawahi kuonyesha sura yake kabisa. Kwa lugha nyepesi ni mtu ambae haonekani , na kwasababu hajawahi kuwa na ugomvi na mtu yoyote haijawahi kufahamika  uwezo wake halisi ni upi .”

Regina kama binadamu wa kawaida ilikuwa ngumu kwake kuamini  mtu anaweza  kuwa translucent  na asionekane  hewani , kitu ambacho kilikuwa nje ya mantiki za  kisayansi.

Maajabu ya ulimwengu wa siri yalikuwa  ni zaidi ya kile alichowahi kufikiria. Regina alijikuta akisahau kabisa kama ametekwa  na kumuona Helena ni kama mtu ambae  amemleta hapo kwa ajili ya matembezi.

“Kwahio unasema kuna watu  aina ya Mr Air  kwenye  Chama cha Adept?”Aliuliza Regina.

“Usifikirie sana, umoja wa Adept una  watu wasiopungua mia moja , licha ya kuwa na uwezo wa ajabu ila  hawana  uwezo mkubwa wa mapigano. Mr Air anaaminika sio kiumbe wa  sayari ya dunia, Asilimia kubwa ya  watu wa  jumuia ya Adept   wana vina saba vya damu ya wanyama”

 

“Damu ya Wanyama !” Regina aliishia  kutingisha kichwa kwa mshangao, “Ila inawezekana kwa namna alivyo haonekani kuwa binadamu wa kawaida”Aliongea Regina na kumfanya  Helena kucheka.

“Miss Regina  hata wewe pia unaonekana kushangaza? Yaani nimekuteka kukuleta hapa lakini naona umeshanigeuza kuwa Tour Guide wako. Huogopi nitakuuwa na kisu changu?”

“Nitafanyaje sasa?  Kwamba nikuogope mpaka kufa. Nimeona kwasababu siwezi kujiokoa ni bora nikachukulia kama fursa ya kujifunza zaidi”Aliongea Regina na  Helena alitaka kuongea  neno lakini   aliacha baada ya kusikia mshereheshaji akimtangaza Gwiji mwingine.

“Kutokana na uadilifu wake wa kiimani , aliogelea katika utukufu mkuu wa  Bwana mtakatifu na kuishi katika baraka za mbingu na ardhi. Alipofikisha miaka ishirini  na moja  alielekeza mikono yake juu na kupokea  upanga  wa kiapo, alipofikisha miaka   ishirini na tanu akaelekeza mikono yake juu na kupokea mkuki wa kulinda mbingu na ardhi. Hata baada ya  miongo kadhaa kupita  bado alisimama kileleni  kama shujaa  juu ya Jumba takatifu. Tunamkaribisha kwenu Malaika Mkuu Mika kutoka  Madhabahu takatifu ya kifalme”

Akiwa amevalia joho  refu  lililonakishiwa na nyuzi za dhahabu alionekana. Alikuwa  amevaa mkanda kiunoni   wa rangi ya dhahabu  kama shujaa. Huku akiwa ameshikilia mkuki mrefu  kwenda hewani kuzidi kimo chake uliokuwa umenakishiwa  na vito vingi vya thamani

Alikuwa na nywele za kahawia , na masharubu mengi katika uso wake. Alikuwa akitembea huku  kichwa chake  akiwa amekiinua  juu bila ya  kukipindisha kama mwanajeshi. Mwanaume huyo aliaminika kuwa na umri zaidi ya karne moja. Hakuwa mwingine bali ni  Malaika  ama kiongozi mkuu wa Mahakama takatifu Mikaeli.

Mika  mara baada ya kwenda kusimama juu ya jukwaa  wafuasi wake  kutoka  Falme ya Mahakama takatifu walisimama  na tofauti na kushangilia walianza kusali huku macho yao yakiwa  yameng’azwa na   nuru ya imani.

Lakini  hata hivyo  kulikuwa na kundi  la watu ambao walikuwa  wamekunja sura kama wamebanwa na mlango huku sura zao zikiwa zimejaa   dharau , walikuwa ni  wafuasi wa shetani wakiwakejeli wafuasi hao kwa sala zao.

Mikaeli  aliinua mkuki wake  juu  angani  na kufanya utoe mwanga wa kuumiza macho  na  kisha ukazima na haukuonekana  kwenye mikono yake bali ulionekana kusimikwa  katika mkono  wa kulia wa kiti chake.Akiwa na mwonekano wa kujiamini alikaa chini.

Mapema tu  kabla ya mshereheshaji kutangaza  Gwiji mwingine  kujitokeza  mwanaume  mwenye mwili mkubwa sana  kama kiboko alitokea katika njia ya kutokea uwanjani.

Mtu huyo alikuwa na kimo zaidi ya mita  mbili kwenda hewani  na alikuwa amevalia  Vest ya  ngozi ya mamba bila shati na kufanya mikono minene sana kuonekana , nywele zake zilikiwa ni nyeupe kama  mvi na masharubu yake pia.

Alikuwa amevalia kofia  ya kijeshi  kichwani  ilionekana kuwa ya zamani mno  na mkononi alikuwa ameshikilia kiko na alitembea  huku akivuta sigara kutoka katika kiko  kile.

Kiunoni mwake kulikuwa na  Kitara au sime  ndefu na pana, mpini wa Sime ile ulitengenezwa kwa madini ya Silver na dhahabu na vito vingine vya kuvutia. Ilionekana haikuwa Sime ambayo unaweza kuikadiria bei yake.

Bwana  huyo alionekana kujikaribisha mwenyewe huku akipunga  mkono hewani kwa kucheka.

“Nadhani sina haja ya kumtambulisha tena , kila mmoja wenu amemuona na kumfahamu”

Alikuwa ndio  mkuu wa kundi la kiharamia namba moja duniani. Inasemekana ushujaa na  ujasiri wake alirithi kutoka kwa  watangulizi wak, yaani mababu zake  maarufu kama The Vikings !. Kundi lake  la kharamia lilikuwa la Daraja   A  lililofahamika kama  Nyangumi wa Barafu(Ice Whaler).

“Ni kapteni Phantom Oleg” Sauti  za  maharamia  wa Ice Whaler zilisikika zikishangilia.

Leviathani aliekuwa amekaa, alimpigia makofi  Oleg . Ingawa walikuwa washindani lakini  Oleg alikuwa  mkubwa kwake  katika  kazi ya uharamia, kwa Lugha nyepesi ni  kwamba Leviathani alimkuta Oleg kazini.

“Maharamia pia wanaruhusiwa kushiriki katika huu mkutano , si wanawinda na serikali nyingi duniani?”Aliuliza Regina .

“Haha.. kwa nguvu waliokuwa nao hao maharamia inaweza kutishia usalama wa nchi yoyote ile wakijaribu kumkamata , kingine  katika  Mkutano mkuu wa Baraza la Maksi  hakuna mtu mzuri  wala mbaya , au mhalifu na asie mhalifu. Ukisikia sehemu ambayo  wafuasi wa mungu na shetani hupeana mkono  wa amani, basi ni hapa”

“Hili jitu  Midevu linaonekana kuwa na  msisimko mkubwa  kuliko  Mr Air na Mika  licha ya kuonekana  uwezo wake ni mdogo”Aliongea Regina.

“Regina  usimchukulie poa Phantom. Ingawa anaonekana wa kawaida lakini  ni maarufu mno katika mbinu  za kivita baharini. Ana miliki meli ya  kivita yenye upanga maarufu kama Sea God Blade,  unaovumishwa kuwa na uwezo wa kukata meli yoyote  mara  mbili.

“Sea God Blade!” Regina licha ya kutokujua  tamathali   za  kijeshi  hakutaka kuamini kama kuna meli ya kivita ambayo ina uwezo wa kutenganisha meli nyingine mara mbili kupitia upanga.

“Ndio.  Meli yake ya kivita imefungwa upanga mkubwa mbele  wenye nguvu kubwa. Phantom anajitambulisha kutokea katika kizazi cha Vikings, yaani  waliobarikiwa juu ya bahari. Anaweza asiwe na uwezo wa kupigana mkubwa akiwa nchi kavu lakini katika bahari  ni  mtu mwinginge kabisa.Anao uwezo wa kuponya majeraha yake yote kwa kugusana na maji ya bahari”

“Kweli!?”Regina aliuliza kwa kushangaa.

“Hakuna uthibitisho , ila inasemekana  anao  uwezo wa kuwasiliana na viumbe wanaoishi chini ya bahari, ikiwemo Majini bahari na Nguva na ndio wanaomsaidia kuzamisha meli na kuiba  mali. Inasemekana uwezo wake aliupata baada kufariki  akiwa baharini  na nafsi ya kiumbe wa ajabu ilimvaa  na akafufuka. Kama isingekuwa uwezo wake  mkubwa wa kupambana akiwa majini unadhani angeweza kulipa umaarufu kundi lake  la kiharamia la Ice Whalrer? Yote ni kwasababu  sio mtu wa kawaida”

Regina mara baada ya kusikia maelezo hayo aliihsi ubaridi wa mgongoni ukimpitia, kwasababu  alichosikia ni kama  Oleg hakuwa binadamu. Alijikuta akitoka mawazoni mara baada ya kumsikia mshereshaji akiongea tena;

“It is said that the real Dragon Knights will not be harmed by the dragon flames. They can bathe in the dragon flames and dance with the dragon …”

Mara baada ya kuongea hivyo  sauti zilianza kupiga mayowe ya shangwe  huku  wakiimba  kwa shangwe kwa kutamna neno; we’re burning.

“Nichukue nafasi hii kumkaribisha kwenu Aulando- Saint  Rodriguez, kiongozi mkuu wa Holy Knight na  mlinzi  mkuu wa  DSS(Dragon Slaying Sword)”

Mara baada ya kuongea hivyo palepale alitokeza  mwanajeshi alievalia vazi  la kijeshi la chuma  kuanzia miguuni  mpaka kichwani  huku akiwa na upanga mrefu kiunoni.

Vazi lake lote la chuma cha silver lilikuwa na nakshi za ajabu zilizochongwa  na kubandikiwa madini ya dhahabu  ya michoro ya nyoka. Eneo  la kifa chake kulikuwa na picha kubwa ya  Dragoni  akitema moto.

Kilichovutia zaidi ni  helmeti la kiroma alilovalia katika kichwa chake  katika  eneo la macho. Kulikuwa kumetengeneza kama vile ni miwani kubwa ya madini ya kung’aa na  kumfanya aonekane kutisha mno.

Ala ya upanga wake ilikuwa imenakshiwa na chata la Wyvern  na kuangalia  tu  mpini wa upanga huo  unaweza kugundua haikuwa siraha yenye uzito wa kawaida.

“Wanaongea nini?”Aliuuliza Regina.

“Ni Creed.  Tafsiri yake ni ‘We’re Burning’ maana yake  ni kuwaamrisha  waendesha  madragoni kuwabatiza kwa moto wa  Dragoni  bila woga. Kwa lugha  nyepesi  ni kama kauli ambazo  dini huwaamrisha  wafuasi  kuongea kama njia ya kukubali  kuwa  muumini kwa kubatizwa. Holy Dragon Knight ni umoja wa kiimani  wa  wanajeshi katika majeshi  ambao wanaamini  wana nguvu kubwa sana , si tu kiroho   lakini  kimwili pia . Ingawa Auland ndio mwanajeshi pekee alieweza kuingia katika hadhi ya Ugwiji lakini inaamnika kuna zaidi ya wanajeshi  wenye uwezo   kupita hata wa Auland , lakini yeye ametangulizwa machoni mwa watu kama mwakilishi pekee..”

Regina muda huo  aliweza kukumbuka  kauli ya Hamza kuhusu madaraja  ya  jamii za siri  na daraja la juu zaidi ni S Class.

Ikumbukwe  hata watu wa dini kubwa duniani pia  wanachukuliwa kama  jamii au  jumuia  na  huingia katika Daraja S  , hivyo   wote hao walikuwa na misemo yao maalumu ya kutamka ukitaka kujiunga nao.

Auland hakuvua helmeti lake  hata baada ya kukaa , ilionyesha ni dhahiri hakutaka kuonyesha sura yake.

“Najua wote  mmekuwa na hamu ya kumuona  Auland ambae ni mara chache sana kuonyesha sura yake. Lakini mtu anaefuatia ndio mzito zaidi” Mshereheshaji alitulia kidogo na kisha palepale akaongea.

“Kila kiza kinapoingia yeye ndio huamka na hakuna  la kumshinda kufanya . Namkaribisha kwenu  mwanachama  wa kudumu wa Madhabahu ya Giza , Mwanachama pekee wa damu ya kifalme ya Strigoi . Prince Sebastianii!!”

Mara baada ya kuongea  watu hawakushangilia kama ilivyokuwa kawaida, japo kwa mbali  yalisikika makofi , ilionyesha watu wengi walikuwa na shauku ya kumuona pekee na  hawakuwa na  ushabiki nae.

Muda ule  aliweza kuonekana  mwanaume mzungu  mwenye ngozi iliopauka , na nywele za kiblonde, aliekuwa katika makadirio ya umri wa miaka arobaini hivi akitembea kwa  kujiamini  kusogelea jukwaa, alikuwa amevaa Tuxedo  na viatu vyeusi vya  ngozi.

Sebastiani  mara baada ya kupungia mkono  watu kidogo , alisogea  kwenye  jukwaa na kuketi kwenye nafasi yake. Lakini sasa  bwana huyo aligeuza uso na kumwangalia Mikaeli  na  wawakilishi hao wa  Madhabahu ya Nuru na Madhabahu ya  Giza walionekana kukasirikiana kiasi cha kufanya  macho yao kuwaka.

“Regina  je unaweza kuamini Prince Sebastiani  umri wake ni miaka elfu tatu?”Aliongea Helena  akimwongelesha Regina.

‘Nini! Miaka elfu tatu?”

“Ndio , ijapokuwa Strigoi wanakufa  kama binadamu tu , lakini wanaishi muda mrefu sana, lakini hata hivyo ni wachache sana wa kufikisha  zaidi ya miaka elfu moja , kutokana na kwamba wengi  wao hutegemea  zaidi vipawa  vyao vya kulala muda mrefu ili kurefusha maisha.  Mfano Prince Sebastiani mpaka kufikisha umri aliokuwa nao  ni kutokana na kuwa na uwezo mkubwa sana wa kulala  muda mrefu na kupigana pale anapoamka ili kujilinda , la sivyo isingekuwa rahisi kuwa hai mpaka leo hii”

Regina aliishia kumeza mate mengi  na kujihisi mambo ambayo alikuwa akisikia muda huo yalikuwa  ni ngumu sana kuamini. Hakuamini Vampire kama huyo ameweza kuishi  miaka yote hio kwa kutegemea usingizi tu.

Ikumbukwe Strigoi  wanachukuliwa  kama  wafu , lakini  uhalisia sio wafu  bali   wanakuwa katika hali ya usingizi tu  kwa muda mrefu. Mfano Prince Sebastiani anaweza kweli kuwa na umri wa  miaka zaidi ya elfu moja lakini asilimia  themanini ya  umri wake  ameutumia kulala usingizi mzito.

“Hakuna asie na mwisho , nadhani nikiongea kauli hii wengi wataelewa  ninachomaanisha. Hatua inayofuata nakwenda kumkaribisha  mwanamke  ambae ameachiwa majukumu makubwa  na mume wake  na kujisimika katika  hadhira ya watu wengi  kupitia  uwezo wake. Kiongozi  mkuu wa The  Odd ones na mwakilishi mkuu   wa mamajusi wa nuru. The White Queen, Madam Silvia Somerset”

Hatimae muda huo alionekana mwanamke mrembo sana alievalia mavazi ya rangi nyeupe akipandisha kwenye jukwaa. Umbo lake na uzuri wake ulivutia wengi mno.

“Yule mwanamke ni mrembo mno. Mume wake amefariki?”Aliuliza Regina ambae alishindwa  kujizuia  kushangazwa  na uzuri wake.

“Ms Regina huyu  mwanamke  kwa namna moja ama nyingine  mna ukaribu..”Aliongea Helena akiwa na tabasamu la uchokozi.

“Unamaanisha nini?”

“Utakuja kujua baadae ukipata nafasi”Aliongea  Helena  akiacha kumuweka wazi Regina. Ukweli moja ya sababu ya  kuitishwa kwa mkutano mkuu wa Magwiji ni huyo mwanamke pia.

Ijapokuwa Silvia  alikuwa na uwezo mkubwa wa mapigano  na kuwa maarufu lakini siku zote hakuwa akionyesha uwezo wake zaidi ya kujificha nyuma ya aliekuwa  mume wake. Kwasababu ndio  kwa mara ya kwanza anasimama kama kiongozi wa The Odd ones watu wengi walitaka kuona  uwezo wake halisi.

Silvia mara baada ya kufika kwenye steji  aliishia kuwatingishia vichwa wenzake waliotangulia na kisha alienda kukaa katika nafasi yake.

“Gwiji anaefuatia anatokea ndani kabisa ya Amerika ya Kusini , gwiji mwenye uwezo wa kuicha nafsi yake kuzurura kuzunguka msitu  wote wa Amazon. Gwiji anaejitanabahisha  kutokufa milele. Nawaletea kwenu Mr Skeleton  kutoka Amazoni.Jeshi la mtu mmoja”Aliongea Mshereheshaji.

Palepale alionekana mtu alievalia mavazi ya kitamaduni ya asili ya  Red  Indiani huku kila  kiungio cha mwili  wake alikuwa amejifunga kwa kuning’iniza mifupa, ya aina mbalimabli kuanzia ya watoto mpaka wazee na pia ya wanyama na ndege mbalimbali. Mwonekano wake hakika ulitisha sana.

Haikuonekana sura yake kutokana na   rangi alizopaka usoni  na pia ngozi yake haikuwa ya kawaida , ilikuwa ni kama vile inaelekea kuoza. Regina mara baada ya kumuona mtu huyo sura yake ilikunjamana.

“Usiwe na wasiwasi, yule anafahamika kama Mchawi wa msitu wa Amazoni,  ile mifupa haijatoka katika miili ya  binadamu hai   bali  kutoka katika maiti zao”Aliongea  Helena.

“Mshereheshaji kasema  mtu huyu ni   jeshi la mtu mmoja. Anamaanisha nini?”

“Ni rahisi sana , inamaanika  kupitia uchawi wake  kupitia ile mifupa anaweza  kuamsha wafu  na  wanyama waliokufa na kupigana kwa ajili yake. Akiwa  eneo la vita kadri watu wanavyokufa ndio  namna anavyozidi kuwa na nguvu”.

“Unamaanisha kama White Walker wa  GOT?” GOT  ni filamu ya  Game of throne.

“Haha..  kumbe unaangalia  filamu! Ndio ni kama ulivyokisia”

“Kwanini hawa Magwiji kila mtu ana stori ya kuogopesha?”Aliuliza  Regina.

“Anaefuatia sio wa kuogopesha na  kubwa zaidi anatokea ukanda wa Afrika ya mashariki  mathalani nchi unayotokea”Aliongea Helena na kumfanya Regina kushikwa na shauku akitaka kujua ni nani

“Mabibi  na mabwana. Kabla ya White Queen kuingia  katika orodha ya magwiji kumi , anaefuatia alikuwa ni mwanamke pekee kushikilia hadhi  ya ugwiji. Anamiliki damu ya kifalme  yenye maajabu  ya moto. Anaweza kuunguza chochote. Moto  ni wa kuogopwa  na binadamuy wa kawaida lakini kwake ndio chanzo cha uhai. Namkaribisha kwenu binti  mdogo  kutoka Afrika mashariki . Nyakasura ,Miss Phoenix Girll”

Mara baada ya kuongea , palepale alionekana  Nyakasura aliekuwa katika mavazi    yake ya aina moja ya rangi nyekundu, hadhira haikuwa nyuma kumpokea kwa  makofi mengi na vifijo.

Nyakasura siku hio licha ya kwamba  hakubadilisha rangi , lakini alikuwa amevalia gauni  refu lenye chata la ndege wa  maajabu. Huku akiwa ameachia nywele  zake ndefu.

Regina alishangazwa na mwonekano wa Nyakasura  kwa kiasi kikubwa.

“Huyu msichana ni mdogo mno  na yeye pia ni Gwiji?”

“Kwani humjui! Huyu  ndio mlinzi  mkubwa wa nchi yenu  chini ya kitengo cha Malibu.  Regina unaonekana kuna mambo mengi sana ya siri  ambayo huyafahamu”

Regina alijihisi kuwa mjinga , aliishia kuzungusha macho yake kuangalia watu namna walivyokuwa katika majadiliano makali.

Ukweli  kama sio uwepo wa Helena karibu yake asingewewza kufahamu lolote.

Walikaribisha jumla ya Magwiji  nane  na  ni wawili tu ambao walikuwa wamebakia kutambulishwa.

Mshereshaji, ilikuwa ni kama makusudi kwani aliacha kuongea kwa nusu dakika hivi huku akiiangalia hadhira kabla ya kumtaja mtu wa tisa. Na muda uleule aliweka maiki na kuongea.

“Mtu anaefuatia  kutambulishwa , jina lake halisi  watu wengi hamlifahamu , lakini kulingana na mtiririko wa Alfabeti anashika nafasi ya tisa. Ni mtu wa pekee sana kulingana na sifa  zake , kwasababu  kwa kipindi cha  miaka mitano ameacha doa kubwa la wino mzito ndani ya ulimwengu wa giza.

Kuonekana kwake kumebadili  muundo  wa zaidi ya miaka mia moja ya ulimwengu wa siri. Kutokana na  kughairishwa kwa Mkutano mkuu wa Magwiji katika baraza la maksi lililopita chini ya  maombi ya wanachama wa  jumuia, nitachukua nafasi hii kuelezea kwa kina  utambulisho wake  kama njia ya kuonyesha  heshima  juu ya  huyu Gwiji mwenye umri mdogo kabisa!”

Mara baada  ya maneno hayo kusikika , asilimia kubwa ya wahudhuriaji  wa mkutano huo walishamjua ni nani.  Watu wengi hususani wale ambao  ni  binadamu wa kawaida katika ulimwengu wa giza   walijawa na machozi katika macho yao na hamasa  ya juu mno. Wote macho yao yalikuwa  ni katika mlango wa kutokea kwenye juktwaa  kwa hamu kubwa ya kumuona huku  wakijiandaa kumshangilia.

“Alikuwa na miaka sita pekee  alipoletwa na kuingizwa katika  kundi la The Odd one. Alithaminiwa sana na mtawala  mkuu Mr Black  na hatimae kukidhi vigezo na kuwa  mwanafunzi wa Black Emperor wa kwanza…Aliweza kupata hadhi ya Selafi  akiwa na umri wa miaka kumi na tatu huku akiwa katika  daraja la juu sana la mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi. Katika kipindi chake cha mafunzo ya nishati  alifanikisha kuishambulia kambi ya kundi  la kimauaji   la Kichwa cha Faru  na kumuua kiongozi wao. Alipofikisha umri wa miaka kumi na sita  alivunja rekodi ya  ufanisi mkubwa  wa kuua na wingi wa watu aliowaua katika vita. Katika umri wa miaka kumi na saba alivunja  rekodi ya kuwa  Bounty Hunter aliefanikisha kuwinda watu wengi duniani na kuwapata. Watu wengi walimuona kama mwiba katika harakati zao na kumtegea kila aina ya  njama lakini hawakuweza kumzuia. Baada ya kutimiza miaka kumi na   nane aliachana  na Uanajeshi  pamoja  na uninja  na katika hali isiotegemewa akavunja tena rekodi ya kuokoa raia wengi katika maeneo ya vita . Mwaka huo huo kwa ajili  ya kupata uhuru wake alimuua  Gabriel, Mkuu wa Mahakama  takatifu  na kuamua  kujitegemea kutoka kwa Mtawala wake.

Ndani ya mwaka mmoja na nusu  wa kujitegemea aliweza kukusanya  wafuasi  na kuingia katika vita kali na mahakama  takatifu. Mapigano yalikuwa makali   na yaliosambaa dunia nzima ya  ukubwa tofauti tofauti  bila ya kushindwa. Mwaka mmoja baadae Mahakama ya Baraza la giza wakaamua kumuunga mkono  na kulazimisha  watu wa Holy Court  kukimbia. Kwa nguvu zake  aliweza kufufua makundi ya Baffodil na Barhams na kuzima makundi mengi ya daraja A na B ili kukuza hadhi ya makundi yake….”

Wakati wote mshereheshaji akiwa anaongea , Azzle , Asmuntis , Mameni, Berly, Leviathani na wengine  waliokuwa wamekaa katika siti chini ya jukwaa  pamoja na wanachama wa  Barhams, Baffodil na  Seas Demons, macho yao yaligeuka na kuwa  mekundu kwa furaha  kubwa.

Upande wa Regina  ambae alikuwa akifuatilia tukio hilo kwa ukaribu kabisa alijikuta akitetemeka kwa sifa hizo. Ijapokuwa hakujua zaidi ya maneno yaliokuwa yakiongelezwa yalikuwa yakimaanisha nini . lakini  maelezo  hayo yalitosha kumuonyesha huyo Gwiji mwenye sifa hizo alikuwa ni hatari kiasi gani.

Alijikuta akiwa na shauku na kutaka kumjua ni Gwiji gani mwenye sifa nyingi namna hio.

Upande wa jukwaa, Mika, Silvia  na wengine  walikuwa na mwonekano usioelezeka  katika nyuso zao. Wanachama wa mahakama takatifu na watawala  wa zama zile  walionekana kutofurahia . Lakini walijua hata kama   MC asingetaja sifa hizo watu walikuwa wakizijua.

Mshindi ni mfalme na  alieshindwa ni mhalifu, hio ndio ilikuwa sheria ya ulimwengu wa siri  bila kujalisha ulikuwa ukipigania nini. Mwenye nguvu ndio mwenye haki ya kuongea. Hivyo kwa watu wenye madaraka makubwa kama hao  waliishia kuinamisha vichwa vyao chini huku wakijiambia  kushindwa kwao ni kwa muda mfupi  tu, kisasi kinakuja.

“Katika miaka miwili  yeye na wafuasi wake walitembea sehemu mbalimbali ulimwenguni na kuwakomboa watu walionyimwa haki na uhuru wao  wa kuishi. Aliharibu mashirika mengi ya giza  na kupandisha  mengi, Ari yake ya kutokukubali kujisalimisha  imewapa watu wengi motisha ya kupambania  haki zao na kuathiri  mpangilio mzima wa utendaji wa ulimwengu wa giza. Vita hii iliodumu kwa miaka miwili imebatizwa jina la Vita takatifu ya ukombozi  na kufanya watu wengi  kumkubali  lakini yeye mwenyewe  anajihisi ni mtu aliwaasi  binadamu  na anapostahili ni kuzimu pekee na kupitia  msimamo huo,Nuru ilimpotea katika uso wake na  Giza likamwangukia na kumfanya adondokee  kuzimu na  hatimae jamii ya  watu kumi na mbili wenye dhambi zisizosameheka  ikazaliwa. Jamii ya watu wa  Karibu Kuzimu  ya daraja S ikazaliwa  na kubatizwa jina la INFERNO. Nichukue nafasi hii kumkaribisha kwenu. Lucifer, kiongozi wa Karibu Kuzimu(Inferno) ambae amerudi tena. Anaefahamika  kwa jina lake maarufu na la siri,Devin-rth”

Previoua Next