Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

SEHEMU YA 203.

Kabla ya  mc kumaliza kuongea ,  makelele mengi ya kushangilia yaliweza kusikika . Mashabiki  wengi  damu zilionekana kuwachemka . Kuna mpaka ambao walikuwa wakifuta machozi kwa furaha zao.

Yalikuwa ni makelele ya kulitaja jina la Divinirth mwanzo mwisho  huku wengine wakitamka maneno ya kiapo  yanayomtambulisha  mfalme  wa kuzimu.

Azzle na wenzake pia walisimama na kuanza kupiga makofi mengi  wakiuungana na  watu  waliokuwa wakishangilia huku macho yao yakiwa yamejaa  unyevunyevu.

Nyakasura ambae alikuwa juu ya jukwaa aliishia kupindisha midomo kwa kuchukia.

“Ana kitu gani cha upekee mpaka kuwa na mashabiki wengi hivi. Wajinga kweli”Aliongea  lakini licha ya hivyo kulikuwa na kitu kigeni kilichokuwa kikionekana katika macho yake.

Regina  alijikuta  akihisi ni kama vile nafsi yake imekuwa na shimo ghafla. Macho yake mawili  yalichanua  huku  akiwa ametoa amepanua mdomo kwa mshangao.

Alijihisi ni kama pumzi zinampotea mara baada ya kusikia jina la Lucifer likitajwa na kujua moja kwa moja jina hilo lilimhusu nani.

Ukweli siku ya kwanza aliposikia jina hilo  kutoka kwa Leibson  aliona  ni jina baya ambalo hakulipenda  kwa kuona limekaa kishetani zaidi , lakini mara baada ya maelezo ya  mshereheshaji kusikika juu ya  sifa za Hamza alijikuta kuwa katika hali ya kuchanganyikiwa.

Hakuamini mwanaume ambae alikutana nae  kwa njia  ya kuweka tangazo mtandaoni ili kuigiza kuwa ni wapenzi na uhusiano wao kubadilika na kuwa mkubwa hata kufunga ndoa.Mwanaume  ambae alijifanyisha kusoma chuo na kuishi maisha ya kimasikini  huku akifanya kila aina ya kazi kwa ajili ya kujipatia kipato. Mpaka dakika hio  Regina alijihisi   mambo mengi ambayo yametokea kuhusu Hamza yalikuwa ni ya kumfanya  apatwe na ugonjwa  wa moyo.

Hatimae wakati watu wakishangilia kwa nguvu , Hamza aliweza kuonekana akitokeza kwenye mlango na kupanda jukwaani.

Viongozi wa Set  na baadhi ya  viongozi wawakilishi kutoka nchi mbalimbali walisimama na kuanza kupiga makofi ya kumkaribisha.

Hamza mara baada ya kumulikwa na mwanga , aliishia kuinua kichwa chake juu na  kuzunguka  kuangalia watu waliokuwa wakimshangilia  na kwa jinsi watu walivyocharuka aliishia  kutoa tabasamu tu.

Ijapokuwa alijua alikuwa maarufu kwa yale ambayo amefanya katika ulimwengu wa siri , lakini kwa namna moja alijikuta akiguswa kuona kwamba alikuwa na wafuasi wengi.

Hamza alijikuta akijionea aibu  baada  ya kukumbuka alikuwa  ameamua kustaafu na sasa alikuwa akiishi nchi  ndogo  huko Afrika na kuajiriwa na mwanamke.

Hamza  hakusimama   sana katika eneo moja na badala yake alitembea na kwenda kwenye jukwaa  la magwiji.

Baada ya kukaa chini , mc alisubiri zaidi ya dakika kumi kwa ajili ya watu kutulia   na kisha  ndio akaanza taratibu za kuita mtu wa mwisho.

Mtu wa mwisho alikuwa ni  kiongozi mkuu wa  watu wa Bondeni , pamoja na  mtendaji mkuu wa  Binamu, Master  Mathias Huge.

Watu wengi hawakuwa wakimjua sana  kutokana na  aina ya sekta aliokuwa akisimamia , kuna hadi wengine ambao walionekana kutomfahamu kabisa . Hata hivyo Huge hakuonekana kujali sana na badala yake  alienda moja kwa moja kwenye jukwaa.

“Haha..Huge watu hawakushangilii sio kwasababu hawakujui , bali  wewe ni muuza siri za watu , hivyo watu wanakuchukia ,  muangalie mwenzako Lucifer  namna alivyokuwa maarufu.. hahah”Aliongea Oleg Phantom.

“Phantom sisi watu  wa binamu hatuuzi tu taarifa kwa kila mtu anaetaka , tuna vipaumbele vyetu vilevile. Hata hivyo mimi kama Msomi  nishazoea kutofahamika , siwezi kujilinganisha na Bro Hamza katika swala la umaarufu”

“Ni usomi  gani uliokuwa nao , kuongea maneno yaliojaa mafumbo ndio unaita usomi. Biashara yako ya kuuza taarifa za watu haina tofauti  na biashara ya umbea ndio maana watu hawakupendi”Aliongea Nyakasura huku akivuta mdomo.

“Nyakasura kwanini unaongea kama vile  tumekuwa maadui , ilihali hatujawahi kuonana kwa zaidi ya miaka miwili?”

“Kwani ninachoongea ni uongo? Najaribu  kukuambia ukweli kama mtu ambae tunatokea ukanda mmoja”Aliongea Nyakasura.

“Tena  ni kweli nimekumbuka nyie wote watatu  mnatokea  ukanda mmoja , mnaweza msiwe  marafiki lakini  maeneo mnayoishi  yanapata faida kubwa  kupitia mafanikio yenu”Aliongea Sebastiani.

“Sebastiani naona siku hizi unajua kuongea. Hatujaonana kwa muda mrefu , vipi hali yako?”

Moja ya sababu ya Baraza la giza kuungana na Hamza katika  kushambulia watu wa mahakama ya nuru sio  kwasababu  ya ugomvi  baina yao , lakini pia ni kutokana na ukaribu wa Sebastiani na Hamza.

Hata hivyo ni Hamza  ambae  aliomba Sebastiani na watu wake kumsaidia, baada ya kuona anazidiwa  na maadui  hivyo ni sawa na kusema  Hamza alipigana vita bega kwa bega na Sebastiani.

“Baada ya vita  nilienda zangu  kwenye ngome ya kaburi kulala. Nimeamka katikati ya mwaka huu  na ndio nilipopokea mwaliko wa kuja kushiriki katika baraza la  maksi. Nikikujibu naendeleaje  ki ufupi ni kwamba bado nina usingizi”

“Mhmm! Mavampire huwa mnashida kubwa sana , yaani umelala zaidi ya miaka miwili halafu unasema bado una usingizi. Staili yenu ya kimaisha inasikitisha sana”Aliongea Oleg.

“Hehe..Mimi namuonea wivu Sebastiani ,  wao kulala ndio namna ya kurefusha maisha yao  na vilevile anao uwezo wa kuamka pale anapotaka. Sio kama sisi binadamu hatuwezi kulala muda mrefu na vilevile maisha yetu ni mafupi  kutosha kutimiza ndoto zetu”Aliongea Silvia.

“Silvia  na uwezo wako wa mafunzo ya nishati ya ufunuo wa  uponyaji , huna haja ya kuwazia sana kuhusu  miaka yao ya kuishi.”Aliongea Mikaeli.

Silvia na Madhabahu ya Nuru walikuwa na ukaribu mkubwa mno na hio yote ni kutokana na ufunuo wa mafunzo  yao ulikuwa ukishabihiana sana  licha ya kuwa na misingi  tofauti. Watu wa nuru wao walitegemea zaidi maandiko na msingi wa kisheria  kukuza nguvu za kiroho wakati upande wa  Silvia na watu wake walitegemea  maandiko pia kupanda levo katika kuvuna nishati za mbingu na  ardhi tofauti  ni kwamba tu  katika kitabu kizima cha maandiko wanaweza kuamini mstari mmoja tu. Hivyo  haishangazi kuona watu wa Silvia kuhudhuria ibada za  madhahabu ya Nuru  wakati ikiwa ni siku ya mahubiri ya mstari wanaotumia kuvunia nishati.

“Kama ni hivyo nakushukuru Mikael kwa kunitoa wasiwasi”Aliongea Silvia kwa tabasamu.

Ijapokuwa macho ya hadhira yalikuwa yakiwaangalia zaidi magwiji hao , lakini haikuwazuia kuongea wao kwa wao.

Ukweli sio kwamba magwiji hao walikuwa wakipatana , walikuwa na vinyongo  lakini  waliamua kuvificha kwa wakati huo.

Regina aliekuwa kwenye  juktwaa la kundi la Metal Tide aliishia kurudi katika uhalisia mara baada ya kuhisi sio kama alikuwa akiota , bali kila alichokuwa akiangalia ni uhalisia. Aliishia kuvuta pumzi nyingi  huku akishika kifua chake kujituliza.

Regina  sasa aliona  ndio maana  Hamza alikuwa wa tofauti  katika mambo mengi , mfano  aliamini kwa uzuri wake ingekuwa rahisi  kumtuliza mwanaume yoyote lakini kwa Hamza ikawa tofauti , kumbe yote hayo   yalitokana na nguvu aliokuwa nayo.

Mwanaume siku zote akiwa katika kilele cha dunia yote , matatizo mengi ambayo watu wa kawaida wanayaona  ni makubwa kwake  ni ya kawaida  sana.

Regina alikuwa na hisia mchanganyiko wakati huo na alishindwa kujizuia baada ya kukumbuka jambo.

“Kwahio  nia yenu ya kuniteka ilikuwa ni kwa ajili ya kudili na Hamza?”

“Naona sasa umeelewa”Aliongea Helena huku akicheka.

“Mnao uwezo wa kudili nae?”Aliuliza Regina akiona ni kama watu hao wanajitafutia tu matatizo , lakini kwa Helena ilikuwa tofauti  , kwani ukauzu ulimvaa.

“Kama angekuwa  ni yule  wa mwanzo tunaemjua  tusingejaribu kufanya chochote , lakini huyu wa sasa  alichokuwa nacho ni mwonekano pekee”

“Unamaanisha nini?”

Regina alijihisi kuwa katika hali ya mshangao   na kutaka kujua lakini ghafla tu alinyamazishwa na sauti ya  Raisi wa Baraza la Maksi , ambae alianza kutumia uwezo wake wa  sauti  kuongea.

“Jamani  naombeni  tuwe kimya. Tunakwenda kuanza mazungumzo  ya kwanza rasmi”

Mara baada ya kuongea , mtu  mmoja mwenye mwili mkubwa alisimama kutoka kwenye siti yake.

“Subiri kidogo ndugu raisi. Mimi Gonzalez nina jambo la kuongea”

Mara baada ya kumuona Gonzalez , watu  zaidi ya elfu therathini waliohudhuria walijikuta wakipigwa na mshangao . Watu wachache walikuwa washasikia ugomvi uliotokea baina ya kundi la Metal tide na kundi la Barhams na pia nia ya Gonzalez kutaka kumchallenge Hamza.

Lakini watu wengi waliona  Gonzalez alikuwa akijitafutia tu kifo ,  anatubutu vipi kujaribu kushindana na mtu kama Hamza.

Licha ya kwamba  sio kawaida  kwa mtu kutaka kuingilia   kikao cha baraza hilo , lakini watu  vilevile  hawakumkasirikia na badala yake  walishikwa na shauku ya kutaka kumsikia.

“Kapteni   wa Metal Tide , ni jambo gani unataka kuongea?”Aliuliza Maxim huku akiwa na tabasamu lakini macho yake yalikuwa na ukali.

Gonzalez aliishia kutunisha kifua , huku akinyoosha shingo yake vizuri  kujiweka katika namna ya  heshima.

“Najiuliza kati ya magwiji kumi, ni wote  wanaostahili kukaa pale”

“Oh?” Maxim alijikuta akisinyaza macho yake.

Haikuwa tu kwa Maxim alieshikwa na msahngao , lakini watu wote waliosikia kauli yake walishikwa na ajabu.

“Namimi nimejiuliza  na kutamani kujua ni nani ambae unahisi hastahili kuwa pale?”Aliuliza Maxim.

Gonzalez alihisi kabisa kila mtu alikuwa akimwangalia na kutokana na hali hio alijisikia vizuri  na sauti yake ilianza kusikika kwa kujiamini zaidi  huku akinyoosha kidole  chake uelekeo wa jukwaa la magwiji.

“Lucifer najua  una mashabiki wengi  lakini kundi  langu la Metal Tide haliwezi kukubali kuchokozwa kirahisi. Mimi Gonzalez nina wasiwasi na uwezo wako. Ninaamini kabisa hauna vigezo vya kukaa  kwenye jukwaa la magwiji tena”

Dakika ambayo maneno  hayo yalimtoka , uwanja  mzima ulizizima kwa mshangao.

Asmuntis , Azzle , Mameni  na wengine walisimama wote huku wakimwangalia Gonzalez  kwa macho makali.

“Gonzalez unajiona nani kuleta ukiburi wako mbele ya bosi wetu? Tushuke chini  tuone mimi mzee nisipokuua”Aliongea  Leviathani kwa sauti kubwa ya jazba.

Kundi kubwa pia la mashabiki wa Hamza lilianza kumnyooshea vidole  Gonzalez kwa  dharau zake.

Regina  ambae alikuwa amekaa  hatimae aligundua  nini kinakwenda kutokea baada ya  kuona tukio hilo na alishindwa kujizuia na  kumwangalia Helena kwa macho yaliojaa ukali.

“Nyie watu mmenileta hapa kwa ajili ya kumtishia  ili mpate umaarufu sio?”

“Ms Regina kuwa mpole, wewe ni mpango wa dharula tu . Ukweli hata tusipokutumia mume wako  hawezi kumshinda kapteni wetu”Aliongea Helena huku akicheka.

“Huna aibu wewe!” Regina aliongea kwa hasira

“Tunafanya kinachopaswa kufanywa”

Regina  uso wake ulijaa wasiwasi. Hakujua ni kitu gani  kinakwenda kutokea  na vilevile hakujua kati  ya Hamza na hilo jitu nani ana nguvu zaidi.

Alijikuta akijilaumu kwa kutotilia mkazo  mafunzo ya andiko la kimalaika. Lakini hata hivyo aliona hata kama angejifunza vipi ingekuwa ngumu kwake kutowazuia watu hao kumkamata.

Gonzalez upande wake hakujali kabisa juu ya hasira za watu  na alimwangalia Hamza  bila hofu yoyote.

“Lucifer nadhani nilikuambia jana kabisa kuwa leo  nitahitaji maelezo! Vijana wangu walishambuliwa  na watu wa kundi lako. Kama usipopiga magoti  na kuomba msamaha , siwezi kuacha hili swala lipite”

Hamza upande wake alikuwa tayari ashaa washa sigara muda mrefu tokea  Gonzalez aanze kuongea na sasa alikuwa akitoa moshi kama  tanuru kutoka kwenye pua zake, huku akitingisha kichwa chake.

“Nipo kwenye mudi nzuri  tu  kwasababu leo ni siku ambayo nitawatunikia  ndugu zangu  tuzo . kuhusu swala lako  kwanini tusiliache kwa leo na kutafuta siku nyingine?”

“Yaani unataka tubadili siku tena. Unaogopa nini kupigana na mimi mbele ya watu wa ulimwengu wa siri au   unaamua kuficha udhaifu wako kupitia sifa  ulizopewa?”

Malijendi  waliokuwa katika jukwaa waliishia kumwangalia  Gonzalez  na mwonekano wa kichokozi. Hakuna   hata mmoja ambae alikuwa na nia ya kuingilia hilo sakata.

Hamza aliishia kuipiga piga sigara yake na vidole kudondosha majivu  huku macho yake yakitoka katika  ukawaida na kuwa siriasi.

“Ulimuumiza Azzle jana nikakuacha lakini unaanza tena ,  hivi unajua  nilipaswa kukufanya nini.  Nadhani  madini yako ya chuma yamekufanya  kuwa na kichaa  ndio maana unaamua kunichokoza. Kabla ya kunichokoza  unapaswa kufikiria kuhusu wanajeshi wako , wataishije baadae”Aliongea Hamza.

Hali ya hewa ilizidi kuwa siriasi kutokana na maneno ya Hamza  na watu wengi walianza kuingiwa na wasiwasi.

Hasira ya Infernal king  ilikuwa ikijulikana na watu wengi  tokea kipindi kile , watu wa  Mahakama takatifu walimchokoza na  hio sababu moja tu ilimtosha Hamza kuanzisha vita . Sasa leo hii  kajikundi kadogo tu ka Metal Tide,  kama Hamza akitaka kukazima  ni  jambo jepesi sana.

Upande wa   Gonzalez yeye alihisi Hamza alikuwa akijigamba tu ila hana uwezo wowote.

“Huna haja ya kuongea kwa kujigamba , kama uwezo unao  utumie acha maneno mengi”Aliongea  Gonzalez   na kisha alimwangalia  Maxm.

“Prezdenti nadhani  kuna sababu  kubwa  ya kuitisha  mkutano mkuu wa Magwiji?  Na kama ndio,  sababu yenyewe ni kuuthibitishia ulimwengu kama  magwiji kumi tunaowatambua   wanastahili kuendelea kubaki katika nafasi zao. Si ndio”Aliongea  Gonzalez.

“Ndio , ila hio ni sababu  ndogo tu. Ni matumaini yetu kuona chini ya uongozi wa Magwiji wetu  ,  amani  na utulivu  ndani ya ulimwengu wa giza inaendelea kudumu na  kupitia ushirika wa nguvu zao ndio kitu ambacho tunahitaji”

“Haha.. upo sahihi lakini ziku zote Dhahabu halisi haigopi kusafishwa kwa moto! Leo hii mimi Gonzalez nakwenda kuwathibitishia unafiki aliokuwa nao  mfalme wenu wa kuzimu. Sijawahi  kupenda  kuwa maarufu lakini nina  mipaka yangu  vilevile. Lucifer kama usiponishambulia nitakushambulia mimi!”

Kabla hajaendelea kuongea kauli nyingine  ghafla tu kivuli cha mtu kilionekana mbele ya Gonzalez.

Shadow killer!

Watu walimaka mara baada ya kugundua  mtu mwenye  uwezo  huo alikuwa ni Asmuntis , mbinu hio  ilikuwa na uwezo wa kumpa spidi kubwa sana  katika kufanya mashambulizi.

Gonzalez alionekana kutegemea jambo lile na kabla  Asmuntis hajamshambulia na kisu chake , mkono wake uligeuka na kuwa chuma  na kukinga shambulizi lile.

“Cliiiiii!!”

Kilichosikika ni mkwaluzano wa  wa kisu kile na  mwili wa chuma wa Gonzalez , ikionekana kimeshindwa kupita kabisa katika ngozi yake.

Muda uleule Gonzalez alitumia mkono wake mwingine na kumpiga  Asmuntis na  ngumi yenye uzito wa tani za kutosha na kumfyatua.

“Bam!”

Asmuntis alipigwa ngumi nzito sana ambayo ilimfyatua na kumfanya arudi nyuma  nyuma huku akitema damu nyingi kwenye midomo  yake.

“Master!”

“Mchafuuuu!!!”

Black Fog na Azzle haraka sana waliruka na kwenda kumsaidia Asmuntis kusimama, huku kundi la watu likimwangalia Gonzalez kwa macho makali.

Asmuntis mara baada ya kusimama aliishia kutema damu  tena na kisha alitngisha kichwa kuwaonyesha kwamba alikuwa  sawa.

“Asmuntis nishawahi kukuambia hutoweza katika maisha yako kuniua mtu kama mimi , mashambulizi yako ni kama kichekesho kwangu..”

Kabla hajaendelea kuongea alijikuta akihisi msisimko  usiokuwa wa kawaida ukipita mgongoni kwake  na kumfanya ahisi mwili wake kusisimka mno kama ameshikwa na maji ya baridi sana. Haraka  sana alijikuta akigeuka  na palepale ndio alipoweza kumuona Hamza akiwa amesimama huku  macho yake ya ulegevu yakiwa yamebadilika  na kuingia ndani huku yakiwa katika hali ya ukali mno, macho yake tu lilikuwa shambulizi  lililomfanya kuhisi  anakiona kifo kinamkaribia.

 

Previoua Next