Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

 

SEHEMU YA 204.

Ngumi kwa Ngumi

Ilikuwa ngumu kutafsiri hali ambayo ilitanda ghafla ndani ya  eneo hilo kutokana na mabadiliko ya Hamza, ilikuwa ni kama alikuwa ametawaliwa na kivuli ambacho hakikuwa cha kawaida na  kusababisha hali ya msisimko ambayo ilikuwa  haielezeki.

Ingawa macho yake yalikuwa katika hali ya ukawaida lakini  ki-uhalisia hayakuwa kawaida kabisa kwa namna  yalivyokuwa yakimwangalia Gonzalez.

Zaidi ya watu elfu therathini ambao walikuwa  wameshitushwa na ngumi nzito ya Gonzalez kwenda kwa Asmuntis, walijikuta wakinyamaza haraka mara baada ya kukumbwa na msisimko ambao Hamza alikuwa akisambaza.

Karibia watu wote waligeuza macho yao na kumwangalia Hamza , huku wale waliokuwa  waoga wakianza kutetemeka.

Kila mmoja alikuwa na wazo moja tu , kwamba  Kundi la Metal Tide limefikia mwisho wake.

Mabadiliko ya Hamza  yalivutia pia watu waliokuwa kando yake. Magwiji hao tisa waliokuwa katika jukwaa walionekana kuwa katika hali za kutotaka kuingilia kabisa suala hilo , wengine walionekana kuwa katika mkao wa hamu ya kuona kile kinachokwenda kutokea.

Meza za chini karibu na jukwaa lao ,  viongozi wa Baraza la Maksi  na  wawakilishi kutoka mataifa mbalimbali , walikuwa pia wamekaa wakiangalia kwa shauku kubwa.

Kanuni ya ulimwengu wa giza mara nyingi ni kwamba  dhaifu anapaswa kumheshimu  mwenye nguvu. Hata kama kuwe na sheria ili mradi  una nguvu za kutosha sheria   inaweza kukusamehe baadhi ya makosa. Hivyo kwasababu  Gonzalez ndio  alietaka kujihima na Hamza hakuna ambae alipanga kuzuia . Lakini sasa  mara baada ya Hamza kutoa msisimko  wake , watu wengi walimwangalia  Gonzalez kwa macho ya huzuni.

Gonzalez alijikuta mwili wake ukikakamaa. Alikuwa katika hali ya mshituko  na   viashiria vya woga vilevile vilimuonekana , hata hivyo mara baada ya kukumbuka Hamza hakuwa na  nishati zozote za mbingu na ardhi, ujasiri wake uliongezeka  kwa mara nyingine.

“Hatimae hasira zimekupanda! Nilishachoka kusubiria  mimi  , nilidhani  utaendelea kujificha”Aliongea  Gonzalez huku akitoa tabasamu la kumkejeli Hamza.

Hamza aliishia kutoa  pumzi nyingi  kama vile amepatwa na ahueni   lakini macho yake yaliokuwa na ukali kama kisu hayakupoa.

“Unaweza kusema kweli sina vigezo vya kukaa hapa kwasababu haujawahi kupambana na mimi  na haunijui vizuri. Lakini umekosea  kuwajeruhi  ndugu zangu”Aliongea Hamza.

Sura ya Azzle ilibadilika palepale katika hali ya hofu  na  alijikuta akiharakisha  kutaka kumzuia Hamza.

“Bosi usiwe na haraka. Huyu hana  hadhi ya kupigana na wewe”Aliongea kwa nguvu Azzle na kumfanya  Mameni aliekuwa amekaa pembeni kukunja sura.

“Unaongea ujinga gani wewe Mhunzi. Yaani mtu kamuumiza Mchafu  halafu unataka aendelee kumwangalia tu? Sio hivyo tu hata wewe jana uliumizwa pia”

“Ni kweli. Mhunzi na  Mchafu mbona siwaelewi, kwanini mnamzuia bosi kumshikisha adabu huyu mshenzi?”Aliongea Berly.

“Nadhani wanahisi wanadeni kubwa kwa bosi ndio maana, lakini hata hivyo deni letu kwa bosi ni la  maisha. Haitokuwa mbaya  akiendelea kutudai”Aliongea Leviathani  akiunga mkono.

Azzle , Asmuntis   na Black Fog wote waliishia kuangaliana kwa hali  ya wasiwasi. Walikuwa na wasiwasi wa kuongea ukweli kama bosi wao hakuwa na  nguvu yoyote ya kupambana na Gonzalez.

Hamza alimalizia  kuvuta moshi wa mwisho kutoka kwenye sigara na kisha  palepale alitupia kipisi chini na kukikanyaga  na kisha akatoka jukwaani kumsogelea Gonzalez.

Kila hatua aliokuwa akipiga  ni kama  vile mguu wake ni wa chuma  kutokana na presha aliokuwa akizalisha  na kuzidi kuugusa moyo wa Gonzalez.

Licha ya hatua za Hamza kutotoa sauti  lakini  kila akipiga  hatua moja  hatua zake zilisikika  kuwa nzito katika vichwa vya watu kama vile walikuwa wakichanganyikiwa.

Watu wote waliokuwa katika  Arena , walijikuta wakishindwa kujizuia na kumeza mate mengi huku wakijikaza  kisabuni.

Gonzalez kwa sababu ambazo hazikuwa zikielezeka  alijikuta akianza kupaniki huku jasho  la baridi likichuruzika katika  paji la uso wake.Alijiuliza nini kinaendelea? Kwanini huyu mtu ana mkandamizo mkubwa bila  ya kuwa na nishati za mbingu na ardhi?.

Gonzalez hakutaka kukubali. Aliamini yeye ndio aliekuwa akitisha  zaidi  lakini kwanini Hamza aliekuwa mfupi alikuwa akimtisha bila hata ya kuwa na nishati ya mbingu na  ardhi?.

“Mwili wa chuma!”

Gonzalez mara baada ya kuona mambo sio mazuri hakutaka kuchelewa na palepale aliongea kwa nguvu  kuita mwili wake wa chuma  na palepale mwili wake ni kama unaota magamba ya chuma na ndani ya sekunde tu ulibadilika.

Misuli katika mwili wake ilikua ,  umbo la mwili wake liliongezeka katika kimo  kingine kabisa. Alikuwa ni kama kifusi cha mtu, kama mnyama  mkali ambae  hajawahi kuonekana katika uso wa dunia.

Gonzalez  mikono yake ilitingishika mara baada ya kupiga hatua  na kukanyaga ardhi  huku akisababisha eneo hilo kutetemeka.

“Aaaahhhh!!”

Gonzalez alijikuta akibweka  kuelekea angani. Ukubwa wake wa kimwili ulionekana kumziba Hamza aliekuwa mdogo. Kwa kuangalia tu umbo lake  ilikuwa ikiogopesha sana kwa mtu wa kawaida kusogea  karibu.

“Jamani eh , ndio lenyewe  hili. Its fu*king giant, chuma chuma kweli!!”

“Kuamua kutumia   uwezo wake  wote  katika hatua ya mwanzo ya pambano. Inaonyesha ni kiasi gani Gonzalez amedhamiria kupigana na mfalme wa kuzimu”

“Nimesikia umbo lake la chuma linaweza  kuhimili kombora. Hata kama aumie anao uwezo wa  kujiponyesha kwa kunyonya  elementi za chuma tu”

“Sidhani hili pambano  litaisha vizuri. Mkumbuke pia  Lucifer uwezo wake  ulithibitishwa   na vita takatifu kati ya  The Odd ones  na  watu wa Jumba takatifu na amepigana nao kwa zaidi ya miaka miwili. Hata kama Gonzalez alitamani kuwa katika  nafasi ya ugwiji  naona angechagua mtu mwingine wa kupambana nae”

“Wewe nae umekuwa mjinga? Unadhani ni rahisi kudili na wale wataalamu wengine. Tumchukulie tu Phoenix girl ambae ndio mdogo  pale , lakini ana miliki moto , unadhani  Gonzalez  atamfanya nini? Njia rahisi alioona ni kumchagua Lucifer basi”

“Huna haja ya kuongea sana. Kati ya Adept’s,  ni Gonzalez ambae  ameweza kufikisha uwezo wake katika hatua ya juu zaidi  huku  ikichangizwa na mafanikio yake ya kuvuna nishati za mbingu    na ardhi na kufikia  daraja la ukamilifu wa mwili. Mimi naamini anatosha kushindana na gwiji yoyote pale”

“Naunga mkono hoja , hata kama  asishinde  Lucifer atapata shida sana kupambana nae na kumdhibiti”

Hadhira ilikuwa katika majabizano ya kina kuhusu pambano linalokwendqa kutokea. Wengi waliomfahamu Gonzalez walijuwa uwezo wake sio wa majisifu tu , alikuwa na uwezo haswa.

Wakati huo Gonzalez alikunja ngumi yake huku akiwa ameng’ata meno kana kwamba kukunja ngumi huko kulikuwa kukimsababishia maumivu.

“Lucifer  kwanini unaficha uwezo wako wa nishati za mbingu na ardhi  kufikia hatua hii?”

Hamza alitembea  mpaka kufikia mita kama kumi hivi mbele ya Gonzalez  na aliachana na  dharau zake na kuelekeza macho kwa washikaji zake.

“Msaidieni  mchafu apumzike. Siku nyingine usiwe una kurupuka”Aliongea Hamza.

“Bosi ..”Azzle alitaka kuongea baada ya kukumbuka kitu lakini aliishia kutoa macho tu asijue namna ya kuendelea.

Asmuntis aliishia kutingisha kichwa chake pekee , kama vile alikuwa akimuomba Hamza asije kufanya jambo la kijinga. Black  Fog na yeye alikuwa na wasiwasi mno kiasi kwamba alitamani kulia. Huku akimwangalia Hamza kwa macho ya kubembeleza.

Walijua fika kama Hamza atapigika  siku hio mioyo yao itavunjika vipande vipande  na ndoto zao pia zingesambaratika  pamoja na imani  waliokuwa  nayo kwa muda mrefu kuvurugika.

Hata hivyo Hamza, licha ya kuona namna walivyokuwa na wasiwasi , aliishia kutoa tabasamu hafifu na kisha alimgeukia Gonzalez palepale.

“Kudili na mtu kama  wewe sihitaji nishati za mbingu na ardhi kabisa”Aliongea Hamza lakini maneno yake yaliamsha zogo kutokana na kutokuamini  kama Hamza anaweza kupambana na  Gonzalez bila  ya kutumia nishati.

“Ni  kweli hataki  kutumia nishati za mbingu na ardhi hata kidogo au anatania?”

“Labda anapanga kutumia nguvu za mwili wake pekee  kupambana na jitu  la chuma. Huku si  kuji..”

“Sidhani, anajigamba tu , hakuna mtu ambae anaweza kufanya hivyo , hata magwiji wenzake hawawezi  kuwa na  ujasiri wa  aina hio”

“Tangu lini Lucifer akamdharau adui yake. Akiongea kitu maana yake  amekwisha mpima adui”

Makelele ya watu kujadili kauli ya Hamza yalikuwa mengi sana. Kuna waliohisi Hamza ana majigambo sana , wengine  kauli y ake iliwapelekea kuhisi damu zao kuchemka kutaka kuona kile kinachokwenda kutokea.

Regina aliekuwa katika  viti , alikuwa   na wasiwasi mno  kiasi cha kufanya mikono yake kumtoka jasho  wakati huo Helena alionekana kuwa na furaha kubwa. Alijua kwa kauli ya Hamza kutotaka kutumia uwezo wake wa nishati za mbingu na ardhi basi  kile walichootea ni sahihi. Hamza hakuwa na uwezo wowote.

Upande wa Gonzalez kusikia maneno hayo ya dharau kutoka kwa Hamza hasira yake ilimpanda maradufu. Alijihisi ni kama anachukuliwa poa.

“Haha..  kwa mtazamo wangu sio kama hutaki kutumia uwezo wako wa nishati  , bali uwezo huo huna. Vigezo vya kuendelea kuwa Gwiji huna kabisa na leo hii nipo hapa kwa ajili ya kuwaonyesha watu wote namna ulivyo dhaifu”Aliongea Gonzalez.

Magwiji tisa  waliokuwa wakisikiliza maneno hayo ukiachana na  Mathias Huge wa Binamu na  Nyakasura , wote walimwangalia Hamza kwa shauku, wakijiuliza ni jambo gani Hamza alipanga kufanya.

Kuhusu Hamza kuwa ama kutokuwa  na  nishati za mbingu na ardhi hilo halikuwaumiza sana vichwa. Kwa levo  zao walikuwa wakielewa katika mapigano  sio tu nishati za mbingu na ardhi zinazoweza kumfanya  mtu kuwa na nguvu.

 

Hamza upande wake hakuonekana kuathirika kabisa na maneno ya  Gonzalez na alikuwa amesimama tu katika eneo moja.

“Nitakupa  nafasi ya kushambulai wa kwanza”Aliongea Hamza.

“Mh! Bado unajifanya mjuaji?”

Gonzalez alijihisi   hasira huku akijiambia huyu bwana kwanini anamdharau hivi , ni muda wa kumshikisha adabu na kupanda   daraja na kuwa gwiji wa dunia. Kufikiria vile palepale  nishati za mbingu na ardhi katika mwili wake zilianza kujikusanya  kufikia katika  hatua ya juu kabisa.

Mara baada ya kusambaza wimbi  la nishati  zile ,  wawakilishi   ambao hawakuwa na  mafunzo kabisa ya nishati za mbingu na ardhi walijikuta  wakihisi mioyo yao ni kama inataka kuwatoka.

Baadhi ya magwiji pia walimwangalia  Gonzalez kwa namna ya kumkumbali.

“Yeah! Naona Gonzalez  sio wa mchezo mchezo” Aliongea  Phantom Oleg.

“Kwa mtazamo wangu  uwezo wake wa  kinishati bado  ni dhaifu”Aliongea Holy Knight, Auland, ambae muda wote alikuwa kimya.

“Auland kwa kujilinganisha na wewe unadhani ni watu wangapi  watakuwa na  uwezo wa kinishati  dhaifu?  Gonzalez  anaonekana kuwa dhaifu kwasababu ya umri wake pekee , kama angekuwa kijana angekuwa zaidi  ya pale”Aliongea Mikaeli.

“Kuna mtu kaniambia  kuwa jana  Gonzalez alihimana kwa muda mfupi na  Miss Nyakasura.  Vipi  unaonaje kuhusu uwezo wake?”Aliuliza Huge akimwangalia Nyakasura.

“Unajiita msomi lakini vilevile  ni bosi wa  Binam. Inamaana hujui uwezo halisi wa Gonzalez au unanijaribu?”Aliongea  Nyakasura akiamini kupitia teknolojia ya  jicho la Umbea ya  watu wa binamu lazima wanataarifa zote juu ya uwezo wa Hamza na Gonzalez na swali lake  limekaa  kisanifu tu.

“Tukiachana na uwezo wake wa nishati  , tuzungumzie kwanza   uwezo aliozaliwa nao  kama ni  dhaifu au   ni mkubwa. Swali hili nadhani mtu ambae anaweza kutujibu ni Raisi wake. Mr Air  unazungumzia vipi kuhusu uwezo wa Gonzalez?” Aliongea mrembo  Silvia.

Mr Air  ambae  kilichokuwa kikionekana ni koti pekee  lililojishikiza hewani sauti yake ilisikika.

“I  don’t judge  others” Alijibu akimaanisha kwamba yeye sio hakimu wa wengine.

“Haha.. Hakika wewe ni  rais wa  wasio wa kawaida. Tabia yako  ni ya tofauti sana  kuliko wengine wote hapa”Aliongea Oleg huku akicheka.

Kundi hilo la Magwiji hakuna ambae alikuwa na wasiwasi , waliongea kwa kucheka tofauti na watu wengine, lakini kwa wakati mmoja  walichokuwa wakitaka kuona ni uwezo aliokuwa nao  Gonzalez. Ni kama vile hawakuwa na wasiwasi wa  Hamza kushinda  ila walitaka kujua  kama  Gonzalez anazo nguvu za kuweza kuhimana vyema na Hamza au ni mdebwedo.

Muda huo, Gonzalez alikuwa amekamilika katika  kukusanya kila  nguvu  iliokuwa katika mwili wake  na   uwezo wake wa kimapigano ulikuwa katika kilele.

Aliishia  kukunja ngumi na kisha palepale alipiga hatua moja kwenda mbele huku akikusanya upepo.

Alikuwa ni kama  roboti  ambalo lilimsogelea Hamza kwa kasi  kutaka kumpiga. Spidi yake  na msukumo wa mwili  ilikuwa ni kama vile  ni mti  unaodondoka   kutokana na mmomonyoko wa udongo.

Ki-ufupi ni kwamba licha ya Gonzalez kuwa na mwili mkubwa ila hakuwa slow kabisa , kila hatua aliokuwa akipiga ilileta  mtetemeko.

“Ngumi ya chuma kizito!”

Gonzalez aliongea kwa nguvu huku  ngumi yake ikiwa ni kama  jiwe FATUMA wakati alipokuwa akimlenga Hamza.

“Bosi!”

Chini ya steji Asmuntis na Azzle alijikuta wakishindwa kujizuia na kupiga makelele wakiomba  Hamza kufanikiwa kuzuia ngumi ile. Hata hivyo  mwanzo mwisho Hamza mwonekano wake ulikuwa katika hali ya utulivu kabisa  na mara baada ya kuona shambulizi lile aliishia kuinua mkuno wake

Muda ule ilikuwa ngumu kwa watu kuona nini kimetokea  na hio ni kwasababu  spidi ya Gonzalez ilikuwa kubwa sana.  Karibia watu wote walijikuta wakibana pumzi  huku wengine wakifumba macho wakiamini Hamza anakwenda kugeuzwa  nyama. Lakini sasa  ndani ya sekunde, kile kilichotokea  kiliwafanya  watu kuwa katika hali  ya butwaa .

“BOOM!”

Katika hali ya kushangaza  Hamza alikuwa amenyanyua mkono wake wa kushoto na kuizuia ile  ngumi ya Gonzalez na kiganja  cha mkono kama vile  ni golikipa anaejaribu kubetua mpira.

Muda ule  ngumi ile ya Gonzalez ilipogusana na kiganja cha Hamza  sakafu iliokuwa chini ya miguu ya Hamza ilititia  na kusababisha mtikisiko mkubwa na  haikuchukuwa muda steji  ilianza kuyumba kudondoka kwenda chini.

Hamza alikuwa amesimama vilevile  , licha ya kwamba  miguu yake ilikuwa imedidimia ndani, hakuonyesha ishara za kusogea kabisa.

Mawe mazito yaliokuwa yameshikilia nguzo za jukwaa lile  yalikosa  mhimili na kuachia  na muda ule  chuma kilifyatuka  kumsogelea Hamza  kutaka kumtoboa lakini Hamza alikuwa mwepesi kwani kabla hakijamdhuru aliweza kukidaka na mkono wa kulia.

Mwanzo mwisho Hamza hakuonyesha ishara yoyote ya kutumia nishati za mbingu na ardhi , lakini amefanikiwa kuzuia shambulizi zito la Gonzalez.

Mara baada ya vumbi kutulia , Gonzalez alijikuta akimwangalia Hamza  kwa macho ya hisia mchanganyiko. Alianza kuhisi  ubaridi wa aina yake ukisambaa mgongoni.

“Hili.. inawezakana vipi?”

Gonzalez macho yalimtoka , akishindwa kuamini kile anachoona, alihisi  ukatili  wa uhalisia  na hisia za kushindwa zilimvaa palepale  na kumfanya fuvu la kichwa chake kuanza kumuwasha.

Baadhi ya  malijendi waliokuwa katika jukwaa waliishia kusinyaza macho  wakiangalia tukio hilo kwa kutokuamini , huku wengine wakiwa katika hali ya kutafakari.

Upande wa Azzle , Asmuntis na Black Fog  wote walikuwa katika hali ya bumbuwazi  huku wakiwa wameachama kwa kushindwa kuamini.

Walikuwa washaamuini  balaa linakwenda kutokea katika steji ile , lakini uhalisia uliwafanya kuwa katika hali ya  kutamani kulia  kwa  furaha kubwa.

Mameni , Berly  , Leviathani  na wengine  ambao walikuwa wakijua Hamza hakuwa na tatizo walijikuta wakishangaa pia  maana hawakuamini kama Hamza atakuwa na uwezo  zaidi ya vile walivyokuwa wakimkadiria. Walijikuta wakishikwa na msisimko wa hali ya juu na kupiga makelele ya furaha.

Hata Asmuntis ambae alikuwa ameumizwa  alijikuta nguvu zikimrejea na kuanza kupiga makelele ya kuita jina la Hamza.

Mashabiki  wote wa Hamza walisimama na kuanza kushangilia kwa kumuita majina tofauti tofaati , wengine walitaja kwa nguvu jina la Divini-rth , wengine Lucifer ,  wengine Prince of hell.

Washikaji zake Hamza damu ziliwachemka  huku wakipata msisimko wa furaha kwa namna Hamza anavyowaheshimisha. Yale  makisio watu waliokuwa nayo yalipotea mara moja na sasa ni kama  walitegemea kuona mapigano ambayo yamebalansi.

“Oh my god! Ule sio ubinadamu , kawezaje kuzuia lile shambulizi?”

“Unadhani kwanini anaitwa Gwiji. Maana yake uwezo wake  sio kitu cha kuotea”

“Najihisi  vigoti kunilegea .. ni  hatari sana”

“Gwiji ni  Gwiji siku zote. Gonzalez alichokosa ni uzoefu  na ninavyoona hapa Lucifer alikuwa  akimpotezea kwasababu alijua  ni mdogo sana kwake la sivyo angemmaliza muda mrefu tu”

“Upo sahihi, utofauti wao wa  nguvu ni mkubwa mno , pale tu hajatumia kabisa nishati za mbingu na ardhi na ameweza kuhimili”

Mabishano   hayo yaliwafikia watu wa Metal tide na yalikuwa ni kama visu vilivyochoma mioyo yao.

Helena  na  kundi lake  walikuwa na sura mbaya sana  huku wakishindwa kuzuia hisia za kuangaliwa  na macho ya  dharau kutoka kwa watu.

Regina mara baada ya kuona   jambo lile  nafsi yake  ilitetemeka kwa sekunde. Hakuamini  mwanaume aliekuwa  juu ya steji ambae watu wanamshangilia kwa  mayowe mengi ni mume wake. Kulikuwa na hisia zisizoelezeka katika moyo wake. Baadhi zilikuwa  za furaha , baadhi zilikuwa za  kujivunia na zingine zilikuwa  ni za kuridhika. Lakini  hata hivyo  hisia nyingine  zilikuwa ni za  kupoteza ,  wasiwasi na  kujutia.

Muda ule alijihisi kitu cha baridi kikugusa kiuno chake na kumfanya Regina kugeuka na  aliweza kumuona  Helena ambe ameshatoa kisu chake na alikuwa amemuwekea kiunoni.

“Miss Regina  acha kujiona ni mwenye bahati..”Aliongea Helena akiwa na uso uliojaa usiriasi.

“Huwezi shinda”Aliongea Regina kwa kujikaza.

“Hata kama  ila wewe si upo  , mwanamke aliekuchagua na kukuoa”

“Na yeye yupo, mwanaume niliemchagua”Aliongea Regina akimwangalia Helena kwa macho makali.

Helena  kutokana na kauli ile alijikuta akishikwa na mshangao. Alikuwa na mwonekano usioelezeka  na aliishia tu kukaa kimya.

Katikati ya ukumbi huo , hali ilikuwa  patashika . Gonzalez alionekana kutojidhibiti  huku mkono wake ulionekana kutetemeka. Kama sio mwili wake wa chuma  pengine  damu ingeshamkauka.

“Wewe.. Ni shetani wa aina gani wewe?” Aliongea Gonzalez huku akimwangalia Hamza.

“Shambulizi lako limekwisha  , sasa ni zamu yangu”Aliongea Hamza.

Kabla Gonzalez hajashituka   Hamza alikuwa ashachukua hatua , mkono wake wa kulia alikunja ngumi , huku  mwili wake  ukiegamia mbele  na mkoo wake ulirudi nyuma  mara moja na kisha ukaelekea mbele.

Misuli katika mwili wake  ilitanuka , ikifuatishana na mnyongeo  wa mwili  na kufanya nguvu  ya mikono yake kuzidi kuongezeka.

Hamza mwili wake  ulikuwa na muunganiko wa kimisuli wa kutosha mno, ilikuwa ni kama alikuwa akielekeza misuli yake namna ya  kujipanga  ili kutoa nguvu ya kutosha katika ngumi yake.

Juu ya jukwaa , Auland , Sebastian  na Mikaeli walijikuta wakiwa katika mshituko  mkubwa.

Kupitia macho yao waliweza  kuona namna misuli ya  mwili wa Hamza ilivyokuwa ikimwitikia.Ilikuwa ni tofauti na kwa watu wa kawaida ambao waliona  shambulizi la Hamza ni la kawaida sana.

Kabla ya Gonzalez kushituka ngumi ya Hamza ilitua katika eneo la tumbo lake  na ile inagusana na mwili  , Gonzalez hakujisikia vizuri hata kidogo , lakini sasa  mara baada ya nguvu  zote za mwili za Hamza kukusanyika katika ile ngumi , Gonzalez alihisi  ni kama vile ni volkano inakaribia kulipuka na kujikuta akishangaa mno.

“Bam!!”

Na sauti kubwa ya kishindo,  mwili wa Gonzalez uliokuwa mkubwa  ulipanda hewani  kwa namna ya kufyatuka kama  mpira.

Ilikuwa ikishangaza kwasababu mwili wa Hamza ulikuwa ni zaidi ya mara  tatu ya mwili wa Gonzalez , lakini kupitia ngumi yake tu alifanikisha kumfyatua Gonzalez.

Watu elfu therathini waliishia kumwangalia Gonzalez akipokea shambulizi lile na kupaa hewani  na kisha kurudi chini   kama furushi  na kutengeneza shindo nzito.

“Mmeona sasa , ngumi moja tu   jitu lipo hoi”

“Haha.. hii inathibitisha  kabisa utofauti uliopo ni sawa na  mbingu na ardhi. Hatari sana hii”

Azzle na wenzake kuona jambo  lile walijikuta wakiruka tuka kwa kushangilia

“Bosi mtu hatari sana. Hii nguvu alioonyesha ni zaidi ya  kipindi kile”Aliongea Mameni  huku akicheka kwa furaha.

Azzle , Asmuntis na  Rhoda walikuwa katika  hali  ya butwaa.

“Bosi … Inamaana bosi hakupoteza uwezo wake?”Aliongea Asmuntis kwa kiwewe.

“Mchafu usiniambie  ulikuwa hujui  lolote? Ni kweli bosi hana  nishati za mbingu na ardhi na anatumia mbinu  tofauti ya nishati?”

“Nini!”

“Kuna mbinu nyingine ya kumfanya binadamu kuwa na nguvu  isio ya kawaida tofauti na nishati ya mbingu na ardhi!?”

“Bro.. inamaana ulikuwa ukinidanganya!” Black  Fog alikuwa  hasira na furaha kwa wakati mmoja.

Azzle na Asmuntis walikosa usemi na waliishia kuangalia majeraha yao  pekee  na kuishia kutingisha vichwa  vyao  kwa masikitiko  wakiona kweli Bosi wao alijua kucheza na akili zao.

Muda huo Gonzalez ambae alikuwa amedondoka chini  alikuwa ametoboa  kwa mara nyingine eneo la steji  huku eneo la tumbo lake  kukiwa kumebonyea.

Gonzalez alijikuta akitetemeka kuanzia kichwani mpaka miguuni kama ana kifafa, wakati huo akijitahidi kujinyanyua. Hakuweza kujizuia na  aliishia kutema damu nyingi chini.

Uwezo wake wa kichuma haukumzuia kutokuumia   kwa viungo vya ndani, alichojua ni kugeuza ngozi yake  pekee kuwa chuma na sio viungo vya ndani.

Muda huo Hamza alikuwa ameshasogelea  mahali ambapo Gonzalez amedondokea  na kumwangalia.

“Ngumi niliokupiga ni kwa ajili ya kulipa  kisasi kwa ajili ya  Asmuntis , inayofuatia ni kwa ajili ya  Azzle ..”

Previoua Next