Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

 

SEHEMU YA  206.

Devil and Angel.

Watu hawakuamini  Hamza angeweza  kumpiga Gonzalez na ngumi moja tu na  kumdondosha chini,  hata wale ambao hawakushangilia mwanzo walijikuta wakishindwa kuficha hisia zao na kuanza kupiga makelele.

“Ngumi nyingine moja tu hadi chini!?”

“Nguvu aliokuwa nayo sio ya kawaida”

“Inatisha , anatisha sana  Lucifer! Yaani nashindwa kuamini kafanikisha vipi kuhimili uzito wa Gonzalez ambao ni zaidi ya tani kadhaa”

“Huyu ndio mfalme wa kuzimu sasa,ana stahili kuitwa hivyo”

“Magwiji ni magwiji tu siku zote , ingawa  Gonzalez yupo  nafasi moja nyuma kufikia daraja la Ugwiji lakini utofauti wake na magwiji ni mkubwa sana”

Watu walikuwa katika  butwaa kubwa , hata wale wa kundi la Metal tide walijihisi mioyo yao inawadondoka.

Kiongozi ambae walikuwa wakimsujudia kutokana na uwezo wake na kuamini  ni mwenye nguvu nyingi ndio huyo ambae amedondoshwa na ngumi moja tu, ilikuwa ngumu kumeza kwao.

Muda huo wanachama hao wa metal Tide  walikuwa katika hali ambazo hazielezeki , wengine walifikia  hatua ya kuweka mikono yao kwenye kichwa.

Helena macho yalimtoka , kisu alichokishikilia kilianza kumtetemeka , haikujulikana ni kwasababu ya woga ama  hasira.

Regina alikuwa  katika msisimko wa hali ya juu sana  lakini hakuonyesha, alitamani na yeye kuamka na kumshangilia Hamza kwa nguvu lakini alijitahidi kujizuia kutokana na kuwa mateka.

Hajawahi kujivunia  kuwa mke wa Hamza tokea  wafunge ndoa , lakini  siku hio namna  Hamza alivyosimama huku akishangiliwa  na jitu  zito kama Gonzalez likiwa chini  alimuona  ni shujaa mkubwa.

Gonzalez aliishia kuangalia mkono wake ambao umeharibika sana  katika hali ya kutokuamini. Hakuweza hata kufikiria  jambo kama hilo lingemtokea  tena kupitia kwa ngumi ya kibinadamu ya mkono wa Hamza.

Aliishia kujiuliza ni nguvu ya namna gani ambayo Hamza ana miliki. Haikuwa kwake tu  hata kwa Magwiji  waliosimama mbali walijikuta wakiguswa na jambo hilo.

“Nguvu alizokuwa nazo zinashangaza mno!” Aliongea Huge.

Ukweli ni kwamba bwana huyo alikuwa akijua  Hamza alikuwa na uwezo  wa juu sana wa mbinu  hio inayofahamika kwa jina la Mgawanyiko, kama  angemchukulia Hamza  mtu dhaifu kama alivyofanya Gonzalez , basi angempokonya pete  muda mrefu sana.

“Huyu mtoto anazidi kunishangaza”aliongea Silvia  huku akivuta pumzi nyingi na kuzitoa.

“Hii sio mbinu ambayo alijifunza kutoka kwa   Mr Black kwa miaka yote. Mr Black licha ya uwezo wake, ilikuwa ngumu kushambulia na ngumi yenye nguvu namna hio hata kama aunganishe na nishati zake zote za  mbingu na ardhi”Aliongea Sebastiani.

Ikumbukwe kwamba  Hamza master wake ni Mr Black , ki ufupi ni kwamba Hamza aliachana na mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi ambayo alijifunza kutoka kwa Mr Black mara baada ya kumuua.

“Hata mimi naona , inaonekana Lucifer ameamua kuachana na  mafunzo ya nishati  aliojifunza kutoka kwa Master wake baada ya kumuua. Hakika  ni kijana mwenye akili nyingi sana”Aliongea Oleg.

Mikaeli na Auland  wenyewe waliishia kutingisha  vichwa vyao pekee , ukweli ni kwamba tokea mwanzo  mpaka  mwisho  hawakuwa na wasiwasi kabisa juu ya uwezo wa Hamza

Mara baada ya kumdondosha adui yake chini, Hamza hakuchukulia kama fursa ya kumshambulia tena  na badala yake aliishia kumwangalia tu kikauzu . Ijapokuwa  mkono  mmoja wa  Gonzalez uliharibika lakini bado aliweza kusimama vyema  huku akivuta pumzi nyingi . Macho yake yalijaa hisia za kukosa hiari na woga,  lakini vilevile  alionyesha ishara ya  uovu na kukata tamaa.

Alikuwa amesubiria kwa miaka mingi sana kuja kutimiza ndoto zake za kuwa sehemu ya magwiji , lakini mwisho wa siku juhudi zake zote zimeharibika , ilikuwa  ni kawaida kukumbwa na hali ya  kujisikitikia.

Chini ya kundi lote hilo la watu alikuwa amepigwa mara mbili na  Hamza. Alijihisi kudharalishwa kusikokuwa  kwa kawaida.

“Lucifer unaonekana kuwa na mbinu , lakini unadhani ndio nimefikia  mwisho?”

Gonzalez bado alikuwa na kadi yake ya hakiba ambayo hakuicheza bado  na alipanga kuitumia  katika muda   kama huo.

“Kabla ya kuzuia shambulizi langu fikiria  mara mbilimbili ..”aliongea Gonzalez huku akigeuza macho yake kuelekezea upande ambao Regina yupo. Alichokuwa akimwambia Hamza ni kwamba kama atazuia shambulizi lake tena basi  Regina atakufa. Yaani kwa lugha nyepesi  anataka Hamza asizuie na akubali  kushambuliwa.

Lakini licha ya hivyo , Hamza hakuonyesha mabadiliko yoyote kama vile kuwa na hofu.

“Nitakupa nafasi ya mwisho. Unataka kufa au  kuishi?”

Swali lile lilimfanya  Gonzalez kushituka na kuishia kukunja sura.

“Lucifer una tania? Umefikiria  mara mbilimbili kama nilivyokushauri, unadhani unaweza kuniua  kirahisi?” Aliongea huku akianza kucheka  kwa kuonyesha kiburi  na kufanya  watu kushangazwa na tabia yake.

“Mshenzi wewe  Gonzalez , unathubutu vipi kumteka shemeji yetu? Wewe ni muoga”Aliongea Mameni kwa kufoka.

“Hustahili kuwa Gwiji , kama unataka  siku nyingine  kushindana na bosi rudi kwenye  machimbo ya chuma ukajiimarishe upya”Aliongea Berly.

“Kaeni kimya! Najua mnabweka kwa kujua bosi wenu anakwenda kupoteza pambano. Endeleeni tu kuongea ujinga ila mimi Gonzalez sio mshenzi  kama mnavyofikiria”

“Hata kama  uwe mshenzi  vipi unapaswa kujiwekea mipaka. Gonzalez nilikuheshimu  sana  zamani  lakini sikutegemea utaenda mbali na kumteka shemeji yetu  kwa ajili tu ya kutaka kujipandisha hadhi . Umedhalilisha  hadhi ya  kundi lako la Metal Tide”Aliongea Asmuntis.

Mara baada ya watu wachache kusikia maneno ya watu wa Hamza , minong’ono ya chini chini ilianza kusikika  na  ni kama sasa wanaanza kupata ufahamu  kitu ambacho  Gonzalez amefanya.

“Hivi ni kweli! Kamteka mke wa Lucifer? Lakini ni lini Lucifer  akawa na mke?”

“Sidhani  kama ni kweli , Metal Tide hawawezi kufanya jambo la namna hio  maana hakutakuwa na maana ya kushinda sasa”

Watu walianza kuongea , wengi wakijizuia kuamini  kama kweli Gonzalez na watu wake wameamua kutumia mbinu ya  ajabu ya utekaji. Watu wa Metal Tide kusikia maneno mengi ya namna hio ya   walianza kukosa utulivu.

Ingawa  ulimwengu wa Giza  haukuzingatia sana sheria , lakini  hadhi na heshima ni sifa kubwa  zaidi.

“Jamani msisikilize ujinga wanao ongea. Wasiwasi wao ni kuogopa bosi wao anakwenda kushindwa pambano”Aliongea Gonzalez akijaribu kutuliza minong’ono kwa kujitetea.

“Haha .. siku zote umekuwa ukisema  mimi ni  mtu mweusi  mfanyabiashara ambae  ni fuata upepo niliekosa maadili. Lakini katika kundi letu Mhunzi  ni mtu wa heshima kubwa  na vilevile  Mchafu pia anaheshimika kwa uongozi wake . Kwanini waongee mambo ambayo hayapo?”Aliongea Mameni.

“Sina muda wa kupoteza kuongea na nyie. Lucifer tumia uwezo wako wote uliokuwa nao na mimi Gonzalez  nitakuonyesha  nini maana ya nguvu ya kweli niliokuwa nayo”

Mara baada ya kuongea hivyo  Gonzalez kwa mara nyingine  alichanua mikono yake  kwa kuisambaza  huku akipanga kunyonya elementi za chuma  za uwanja huo ili kuponyesha mkono wake. Mara  baada ya ishara za elementi za chuma kuonekana kuuvaa mkono wake ,  macho ya Hamza  ya Hamza yalionyesha nia isio nzuri  na  ghafla tu alipotea alipokuwa amesimama katika macho ya kawaida.

“What a speed!!” Auland alijikuta   akitoa mshangao wa sauti. Ukweli kwa macho ya kawaida watu wanaona Hamza amepotea ila kwa magwiji walikuwa wakimuona Hamza, ni kwamba tu alikuwa katika spidi kubwa.

Kufumba na kufumbua Hamza alikuwa mbele ya Gonzalez.  Alikuwa na kimo kirefu sana  mpaka kufikia kichwa chake  na mara baada ya kumuona Hamza akijitokeza mbele ya macho yake alihisi kitu hakipo sawa.

Hamza mwili wake ni kama ulikuwa katika slow motion kwa namna ambavyo alikuwa amegota hewani  huku akitoa ngurumo ya hasira nyingi, wakati huo akirusha ngumi kumlenga Gonzalez.

“Boom!”

Ilikuwa ni kama  ngurumo namna ngumi yake ilivyotua katika kichwa cha Gonzalez , chuma kilichokuwa kikilinda  kichwa chake kilishindwa kuhimili uzito wa ngumi ile  na kuifanya itoboe  katika paji la uso na ile Hamza anavta mkono nje ulitoka na vipande vya chuma pamoja na  uji uji mweupe na damu.

Kichwa kikubwa cha Gonzalez kilitengenezwa shimo  huku wakati huo Hamza akitua chini  ardhini na  jitu chuma mdogo mdogo likianza kuporomoka kwenda chini.

Ghafla tu  eneo lote la uwanja lilitulia tuli , huku watu wakiwa katika  hali ya mshituko usiokuwa wa kawaida, wakishuhudia mwili wa Gonzalez ukidondoka  na kutua chini.

Hakuna ambae aliamini Gonzalez ambae alikuwa akiongea sana kwa kujisifia na kuonekana kama mtu amabe angepigana na Hamza kwa raundi  kadhaa  angeweza kuuliwa na ngumi moja tu.

Mwanzo mwisho Hamza alikuwa amefanya mashambulizi matatu pekee  na kisha shambulizi alilofanya lilikuwa na madhara makubwa , lakini la mwisho ndio lilimaliza  kabisa kazi kwa kumuua palepale.

Ghafla tu watu wengi walijihisi miili yao kutetemeka huku vigoti vya miguu vikikosa nguvu , hisia waliozokuwa nazo   zilikuwa za hofu.

“Divin-rth!”

Ilikuwa ni sauti moja  tu kutoka  kwa mwanachama  wa Inferno  na sauti hio ilikuwa kama kitufe  kilichofungulia  makelele mengi ya   kushangilia.

Azzle , Asmuntis  na wengine walijikuta wakiwa katika hali ya msisimko kiasi kwamba walitamani kupiga magoti na kuanza kusujudu.

Ilikuwa ni kama vile muda umerudi nyuma  na kuwa siku ile  ya  kiumbe  aliebatizwa jina la  Ghadhabu  Takatifu  akiwa amesimama  katika uwanja wa vita huku  chini kukiwa na miili ya watu iliosambaa wa vita akiwa amemaliza kazi   kwa kujipatia ushindi.

“Bosi , Bosi.. Aah bosi…” Leviathani uchizi ulimvaa palepale  akishindwa kuelezea hisia zake.

Mapigo ya moyo ya Black Fog yalizidi kwenda mbio , mkono mmoja aliuweka  kifuani  mwake kama kwamba alikuwa akizuia moyo wake usije kuchoropoka. Macho yake yalijaa matamanio  na penzi zito.

Lakini hata hivyo licha ya watu wengi kumshangilia kama wameshikwa na ukichaa haikumfanya Hamza kujisikia furaha hata kidogo  wala kujivunia. Macho yake muda wote yalikuwa upande wa watu wa  Metal Tide  na palepale aliongea kwa nguvu.

“Jamazeni wote!”

Kauli yake ilikuwa ni kama batani  ya umeme imebonyezwa kwani  mara baada ya  sauti yake kusikika  watu walinyamaza na kumwangalia wakitaka kujua anakwenda kuongea nini.

“Watu  wa Wimbi la Chuma naomba mnisikilize , Kapteni wenu amekufa …”

Wanajeshi wa Metal Tide siti zilikuwa za moto , huku  wakati mmoja  wakihisi ubaridi usio wa kawaida ukisambaa katika kila kiungo cha miili yao.

Kifo cha Gonzalez , kilikuwa cha haraka sana , alikuwa ndio mwasisi mkuu wa kundi hilo la kimasenari  na kutokana na kifo chake kila mtu alikuwa katika hali ya kupaniki kushindwa kujua nini   hatima yao.

Ni kama uti wao wa mgogo umeshindwa kufanya kazi ghafla na sasa wapo katika hali ya kupalalaizi na kufanya wawe katika  hali ya kutojiweza.

Mshituko ambao Hamza aliwasababishia ulikuwa mkubwa mno. Picha walioweza kushuhudia ilikuwa  na athari kubwa mno kisaikolojia ambayo ilienda kushitua kila  neva ya moyo  na kulipua  homoni za uoga katika hifadhi zake na kufanya zisambae katika damu na kusafirishwa mwili mzima.

“Nitawapa machaguo mawili , mosi mwachieni mke wangu akiwa hai na kisha poteeni na nitasahau kilichotokea leo , pili  mnaweza kumuua mke wangu  lakini nyie na  kizazi chenu chote kwanzia wake zenu , wanaume wenu , watoto wenu   mpaka ndugu zenu  wa mbali , nitawaua wote”

Hayakuwa maneno tu , sauti yake pia ilisafirisha maneno hayo  na msisimko ambao ulisambaa katika  moyo wa kila mmoja  wa kundi hilo la Metal Tide.

Ilikuwa ni sawa na kusema uhai wa Regina  ulitaka kubadilishwa na maisha  ya familia zote za watu wa Metal Tide. Hakuna ambae angekubali kuona famili yake inakufa kwa ajili ya uhai wa mtu mmoja , isitoshe kama  ni kapteni wao amekwisha kufa , kuna haja gani  ya  kwenda mbali  kumchokoza mfalme wa kuzimu  kwa ajili ya   tamaa za Gonzalez?.

“Msidhani  natania ,  nawahakikishia kila ninachoongea  hapa nitakikamilisha  ipasavyo,  Nadhani wote mnajua hakuna binadamu ambae alishawahi kutafutwa na mimi dunia hii na akakosekana”

Mara baada ya kuongea hivyo  watu wake wote wa Infenro , wanajeshi wa Barhams na Maninja a  Baffodil wote walipiga saluti kuuunga mkono amri yake kuonyesha kwamba wapo tayari kwa  maelekezo kutoka kwa bosi wao.

“Helena,  unadhani ni kipi kinapaswa kufanyika?”Aliuliza Gray.

Wasingekubali tu kukubali  kumwachia Regina kwasababu , alikuwa pia ndio tiketi  ya uhai wao.  Yalikuwa maamuzi magumu kumteka mwanzo lakini vile  ni maamuzi magumu kumwachia.

Uhalisia   ulikuwa  na ukatili sana kwao, ilikuwa  ni wazi kwamba hata kama wakiamua kuchagua  chaguo la mwisho ingekuwa ngumu sana kushindana na makundi  matatu ya  Daraja A  bila ya uwepo wa Gonzalez.

Hivyo kauli ya  Hamza kusema ataua kila mwanafamilia  , haikuwa ya mkwala tu  , alikuwa na uwezo huo kwa asilimia mia moja.

Regina  mara baada ya kusikia maneno ya Hamza moyo wake ulidunda kwa nguvu. Alikuwa katika hali ya woga lakini alijua fika Hamza alikuwa akitumia kila njia kuhakikisha anakuwa salama. Alihisi pia Hamza  kauli yake ni ya kikatili sana  kwa kuona hata kama  akifa kuua familia za  watu wote hao isingekuwa  vizuri , kwani ni  watu ambao walikuwa wakitii tu  maagizo na  familia zao hazikuwa na kosa.

“Kushindwa ni kushindwa tu, ila hata kama tumeshindwa  bado tunapaswa  kusimamia  ahadi  tuliowekeana na kapteni wetu, Uhai  ni mwanzo wa wimbi na  kifo ni mwisho wa wimbi  na hatimae mwanzo  wa wimbi lingine la maisha ya kipepo”Aliongea Helena  akimalizia  na kauli mbiu ya kundi lao.

“Helena unamaanisha nini , kwahio unataka kweli kwenda kinyume na  na maneno ya Lucifer na kumuua  Regina?”Aliuliza  Gray kwa mshangao.

“Bila kufanya hivyo tutakuwa tumemsaliti  Kapteni , tumeisaliti taasisi yetu, ni nani atakubali kufanya kazi na  mwanajeshi  wa kulipwa anaevunja kiapo? Tutaondoka kwanza  na Regina hapa na kumtumia kama mateka . ili mradi tutachelewesha kifo chake  na wao pia hawatokurupuka kutushambulia”Aliongea.

“Helena wewe uko peke yako , lakini sisi wote hapa tuna wake zetu , tuna  watoto  na familia .. hebu acha  kujaribu kuwa  jasiri , Kiongozi wetu amekwisha kufa” Moja ya masenari aliongea.

“Kweli kabisa , Helena  kiongozi   wetu hajawahi kuwa na njia za kunyooka katika kufanya mambo yake. Tunapaswa kumuomba msamaha mtawala wa kuzimu. Amekwisha kusema tukimwachia mke wake hai  atasahau kuhusu  hili , ameongea kauli hii mbele ya watu wengi hivi hawezi kwenda kinyume” Jamaa aliefahamika kwa jina la Sean aliongea.

“Kaeni kimya , upo wapi ujasiri wenu? Kwanini ghafla tu mnakiogopa kifo?”Aliongea Helena.

Sean , Comb  na wengine walikuwa  na  sura zilizokuwa na hali ya uchungu.

“Helena kubali kushindwa , tunashindana na Lucifer , nguvu zake ni kitu ambacho hatuwezi kushindana nacho , mbele yake sisi hatuna tofauti na sisimizi tu”Karibia watu wote wa Metal Tide walimwangalia Helena kwa macho ya kubembeleza.

Regina mara baada ya kuona tukio hilo  , hatimae alijua  kwanini Hamza aliamuakutumia maneno ya kikatili.

Hamza alitumia ngumi tatu tu kumuua Gonzalez  na kwa wakati mmoja  alikuwa pia ameiharibu  kinga ya kundi lote la  Metal Tide  na kufanya  wanajeshi wote waliobakia kukosa kujiamini kabisa na kuwafanya wote kutaka kujisalimisha.

Lakini licha  ya yote , Regina alijikuta aishangazwa mno na mwanamke Helena, yanaweza  kuwa maamuzi mabovu kwa upande  wa Helena  kutokana na uaminifu wake  lakini  kwa wakati mmoja  ilikuwa ni sifa ya fahari kama mfuasi kwa kiongozi wake.

“Kaeni kimya  nyie wasaliti? Mnadhani kapteni alikuwa akijipambania mwenyewe? Ameamua kujitoa kwa ajili yetu wote. Sio yeye aliewaajiri na kuwafanya kupata hela nyingi? Kwanini mnataka kumsaliti  kikatili?”Aliongea Helena kwa  hasira na uchungu mwingi.

“Tuliweka rehani uhai wetu kwa ajili ya hela tulizopata! Ndio  tunamshukru kapteni kwa yale aliotufanyia lakini hatuwezi kuweka rehani  uhai wa familia zetu kwa ajili  ya kapteni aliekufa”

“Kweli kabisa! Helena hebu acha kuwa mbinafsi, unapaswa kuzingatia  maisha ya kila mtu”Aliongea Sean.

Helena alikuwa na hasira mno kiasi kwamba  mwili wake ulianza kumtetemeka. Palepale  alizungusha mkono wake katika shingo ya Regina  na kusimama  na  kisha  alitumia kisu  kukandamiza katika shingo yake.

Regina na sura yake ya kirembo  alijikuta akifubaa  huku akili yake ikiwa tupu. Hakudhania  Helena angekuwa mgumu namna hio.

“Wote kaeni kimya! Mimi Helena sipo  tayari kuwa msaliti. Natii maelekezo ya kapteni  na utii wangu kwa  Metal Tide , hivyo siwezi kwenda kinyume na kiapo changu. Nitaua kwa ajili yake sasa hivi….. Arghhh..”

Kabla Helena hajamalizia sentesi yake  alijikuta akitoa  mguno wa maumivu.Macho  yake   yalikodoa  na kwa uchungu mwingi aligeuza kichwa chake  na kugeuka nyuma na kumwangalia Gray.

Mkono mmoja wa Gray ulikuwa umeumia lakini mwingine ulikuwa ukifanya kazi vizuri tu na bila  ya kueleweka amefikia kisu muda gani Gray alimchoma  Helena kupitia  mgongoni  kwa kulenga moyo wake.

“Gray!”Katika macho ya  Helena  kulikuwa na viashiria vya huzuni kubwa, kutokuamini  na  masikitiko.

“Nisamehe Helena , siwezi kukuruhusu kwa ajili ya mtu aliekufa  kutuua kila mmoja”Aliongea Gray akiwa siriasi.

Mara baada ya kuona hivyo , Comb palepale alichukua hatua na kumsogelea Helena na kumpokonya kisu kilichokuwa katika mikono yake  na kumuokoa Regina.

Regina aliishia kushikwa na mshituko huku akiangalia kisu kilichotoboa kutoka nyuma na kutokea mbele katika  eneo la moyo wa Helena.Hakutarajia  hali ingegeuka na kuwa hivyo.

“Tuli.. tulifanya kazi kwa zaidi ya miaka kumi na mbili pamoja , ila umeamua kunisaliti mwishoni” Aliongea Helena akiwa na machozi  katika  macho yake huku akimwangalia Gray.

Gray upande wake alikuwa na mwonekano usioelezeka , hakujali  tena na palelae alichomoa kisu  kutoka  katika mwili wa Helena na kuusukumia  kutoka kwenye  ngazi za viti.

“Nooo!”

Regina mara baada ya kuona Helena akisukumwa chini na kuanza kuporomoka katika ngazi alijikuta akipiga yowe.

“Kwanini mmemsukuma ,  mmeshamjeruhi tayari asingeweza kuniua?”Aliongea Regina  kwa kufoka na kuwafanya Gray na wenzake kupiga magoti mbele ya Regina.

“Samahani sana Ms Regina , tumelazimishwa na Gonzalez  kukukamata, tunaomba msamaha wako tafadhari”

Regina alihisi kuchanganyikiwa , hakujua kwanini  mambo yamefikia hatua hio , ni kweli alistahili kuokolewa lakini katika  moyo  wake alihisi hali ya  chuki isioelezeka  juu ya watu waliomuokoa . Muda huo watu wote walipiga makelele kwa tukio lile.

Hamza palepale aliruka kutoka  alipokuwa amesimama  kwa mita kadhaa na kwenda kutua katika viti vya ngazi  mbele ya Regina.

“Wife , uko sawa?”

Hamza alikuwa amezima ile mbinu mgawanyiko na kufanya kile kivuri  kumpotea na kurudi katika hali ya kawaida , ile ile anayomwonyeshea Regina siku zote.

Ukweli  Hamza hakuwa na mpango wa kumuua  Gonzalez tokea mwanzo, alipanga kumshikisha tu adabu mbele ya watu , lakini mara baada ya kumteka  mke wake  aliona atumie uwezo wake wa juu  kumuua Gonzalez ili  kuvunja safu ya ulinzi ya kundi hilo na kuwatengenezea machafuko baina yao  ili iwe rahisi kumuokoa Regina.

Ijapokuwa ilikuwa njia hatari tokea mwanzo , lakini ndio alioona ipo salama zaidi   na pili hakutaka kuhatarisha usalama wa Rhoda na kutumia  uwezo wake wa spidi usiokuwa wa kawaida kujaribu kumuokoa Regina.

Hivyo ni sahihi kusema kwa asilimia mia moja kile alichopanga Hamza kilifanikiwa   lakini kwa wakati mmoja alijifunza kutoka kwenye kosa alililolifanya na alipanga baada ya hapo  anapaswa  kumtafutia Regina mlinzi  wa kumlinda  masaa ishirini na nne  na sio yeye tu  kwa kila  mtu  wake wa karibu.

Regina mara baada ya kusikia neno ‘wife’ kutoka katika sauti alioizoea alihisi ni kama  amesubiria neno hilo kwa karne nzima. Lakini kwa wakati mmoja alipoinua  macho yake na  kumwangalia aliemuita alihisi  ni kama  mtu mgeni kwake. Mrembo Regina alikuwa katika hali ya kuchanganyikiwa.

 

Previoua Next