"Nani mimi?" Jimmy aliuliza kama vile hakuwa na uhakika kama swali ametupiwa yeye, alikuwa akijiuliza amemfanya nini bidada huyo kiasi cha kumchukia waziwazi lakini hakupata jibu
"Sophia unapaswa kushukuru ndugu zako wako hai sababu ya huyo mtu hapa, mimi sijali kama unafahamiana nae au lah na kwanini unamchukia ila ifike muda tabia yako uweke kando" aliongea mwanamama vero, alikuwa anaijua tabia ya mwanae vizuri sana kuliko mtu yeyote humo ndani
"Jimmy huyu ni Sophia dada mkubwa wa hawa ndugu zake usijali sana kuhusu tabia yake ndivyo alivyo"
Wakati anataka kujibu simu yake iliita na alipoangalia namba ya mpigaji tabasamu lilijichora usoni mwake na hakuipokea aliikata kisha kutuma ujumbe na kuirudisha mfukoni
"Samahani bi mkubwa ninahitajika mahali hivyo inabidi niwakimbie" ilibidi Jimmy aaage
"Oh sawa karibu tena" aliongea mwanamama
"Asante" alijibu kisha taratibu alianza kurmtembea akielekea mlangoni mara ghafla akakumbuka kitu
"Oh nimekumbuka" aliongea na kuingiza mkono mfukoni na kutoa mkufu mdogo wa almasi"Nadhani hii itakuwa ni mali yako uliidondosha siku ile" aliendelea kuongea akiweka tabasamu flani usoni
Sophia aliishia kutoa macho ya mshangao huku akiupokea mkufu huo ambao alikuwa akihangaika kuutafuta nyumba nzima bila mafanikio na sasa upo mbele ya macho yake
Kila mtu mule ndani alikuwa akiwaza yake kichwani walikumbuka ni kwa jinsi gani bidada huyo alivyokuwa akiwasumbua kuhusu mkufu wake uliopotea
Baada ya Ji.mmy kuondoka kimya kilitawala macho yakimuangalia Sophia na kila mmoja alipita njia yake kutoka mule subuleni huyu kaskazini, yule kusine, hawa magharibi na mwisho Cid alipitia mashariki akibakia Sophia peke yake
°°°°°°°°°°
Upande mwingine ndani ya chumba kidogo cha mahojiano chenye mwanga hafifu, meza ya chuma ikiwatenganisha watu wawili
"So Rico kama mchezaji wa man city sio? Unajua Rico Tanzania ni nchi ya amani sana sema washenzi kama nyinyi ndio mnaotuharibia sifa ya nchi yetu"
"Sikia we. Mshenzi usifanye mambo kuwa magumu niambie nina aliyekutuma?" aliongea Inspekta Sabari
"Unadhani nitatoa tasrifa kirahisi tu kwasababu ya mateso mnayonipa huh? Utakuwa mgeni katika hili inspekta"
"Ngoja nikwambie Inspekta naniliu, kuna siri zingine hazifahi kutolewa nikiongea ninauawa nisipoongea bado nitauwawa taratibu tu"
"Unadhani boss wako aliyekutuma anajali kama umeozea hapa? Tangia saa tunayokukamata tayari alishakuona takataka na pengine anapanga kuisafisha hiyo takataka"
"Unadhani najali sana kuhusu uhai? Pengine aliyeniita mpumbavu yuko sahihi, a nikwambie tu hapa unapoteza muda wako bure hutaambulia chochote"
"Damn! wewe mpumbavu!" Inspekta alipiga meza kwa hasira na kumkunja shati mtuhumiwa yule
"Ngoja tuone kama utaendelea kuwa jeuri mpaka saa ngapi" aliongea na kumtandika mtuhumiwa ngumi nzito ya pua kiasi cha kumtoa damu hakuishia hapo tu aliendelea kumshushia kipigo mpaka askari wenzaki wenzake walipoingia kumzuia
"Utaua" askari mwenzake alimtahadharisha
"Nani anajali kama akifa damu za watu wasio na hatia zimemwagwa na mikono ya hawa wapuuzi" alifoka na mtuhumiwa alianza kucheka kwa sauti, kitendo kile kilizidi kumtia hasira Inspekta
°°°°°°°°°°
"You old man... after so long, now you remember that I exist?" (We mzee leo ndo unanikumbuka baada ya kupotea kwa mda mrefu)
"Still sharp with the words, huh? I thought you'd have softened up by now" (Bado tu una mdomo eeh nilidhani labda utakuwa mpole)
"You disappeared like a ghost. No calls, no messages. I almost thought you kicked the bucket." (umepotea ghafla kama mzimu, hakuna mawasiliano kabisa nilidhani labda umekufa)
"Where were you? "(ulikuwa wapi)
"Some things... are better left buried, kid" .(Mambo mengine ni vyema kutoongelewa kijana)
"Then what's the point of you calling me here" (Kulikuwa kuna haja gani sasa ya kuniita)
"Maybe I just missed an old friend." (Labda nimemmisi Rafiki yangu wa kitambo)
"Come on, I know you better than that. You didn’t just disappear for no reason you're hiding something eren’t you" (Nakujua vizuri sana we mzee huwezi kupotea bila sababu kuna kitu unanificha sio)
"Take it." (chukua) alitoa kitabu kidogo cha zamani kilichochakaa sana
"What is this? "(Nini hiki)
"Something I can’t carry anymore, that's no ordinary book kid" (Kitu ambacho siwezi kukibeba tena, hiko sio kitabu cha kawaida kijana)
"What’s inside old man?"(kuna nini ndani mzee?)
"The kind of knowledge that gets people killed"(Yale maarifa ambayo hupelekea watu kuuwawa)
"Scare tactics? Thought you would be more creative" (Unaniogopesha sio? Nilifikiri utakuwa muwazi)
"You're one of the few peoples i trust in this world, guard it with your life kid and be careful, hope you won't disappoint me"(Wewe ni kati ya wachache ninaowaamini kwenye huu ulimwengu kilinde hiko kwa hali na mali pia kuwa makini nacho natumai hutoniangusha)
"Don't confuse me old man you come back out of nowhere, and hand me something like this—expecting me to just accept it?"(usinichanganye mzee yaani unarudi kusikojulikana halafu unanipatia kitu na unategemea nitakipokea?)
"Yes" (Ndio) aliitika na Jimmy alifungua hiko kitabu na kukuta kurasa zikiwa tupu hakuna neno hata moja
"I must admit it you're quite a secretive one" (Inabidi nikubali tu wewe ni msiri)
"Alright am hungry old man got any cash?" aya mzee nina njaa hapa una hela?) jimmy aliuliza na mzee huyo alitoa bakuli ambalo lilikuwa pembeni yake muda wote wanaoongea
"Haha remind me of the first time we met"(Haha unanikumbusha tulivyokutana kwa mara ya kwanza)
Maongezi hayo yalikuwa ni baina ya Jimmy na Mzee myahudi wakiwa xhimboni wamekaa kwenye benchi wakipigwa na jua la mchana lakini hakuna aliyejali. Muda haugandi masaa yalizidi kusonga na hatimae giza kuingia na siku kuishia hivyo
°°°°°°°°°°
Kesho asubuhi Jimmy alikuja kuamka saa nne asubuhi na kama kawaida yake kitu cha kwanza kufanya baada ya kuamka ni kuuchangamsha mwili kwa mazoezi, baada ya hapo alikwenda kujisafisha mwili
Ile anafungua mlango wa chumba chake kwaajili ya kutoka anakutana na sura ya dada yake
"Usiniambie ulitaka kuja kuniamsha saahizi" aliongea Jimmy
"Bro unabahati sana asee mimi dada yako nakupa salute kwa hilo" alijibu kivingine na kumuacha Jimmy katika sura ya maswali
"Unataka kusema nini?" alimuuliza na monica hakumjibu na badala yake aliishia kumpigaigapiga vingumi vya uchokozi
"Asee kuna muda nawazaga nikufunge kamba nikutupe baharani ukaliwe na papa huko unazingua sana dada yangu kila siku hukawii kuniletea vurugu... Umekunywa nini leo wewe"
"Nenda ukajionee mwenyewe bro" aliongea kwa tabasamu na kuondoka zake akimuacha jimmy akikuna kichwa chake
"Kuna muda kuwa na dada ni baraka sana ila kuna mwingine sasa........" alijiambia kichwani mwake na alielekea zake sebuleni
Hapo ndio anaelewa kwanini dada yake alikuwa vile, kulikuwa na ujio wa mtu humo ndani nae hakuwa mwingine bali ni Bianca
Bianca kumuona jimmy alisimama kutoka kwenye kochi aliloketi
"Hatimae umeamka" aliongea Bianca na sauti nyororo ya kumtoa nyoka pangoni iliyosafiri kwenye masikio ya jimmy bila ya kumuangalia usoni
Jimmy alimsogelea Bianca karibu zaidi na kumwambia akae haina haja ya kusimama isitoshe yeye ni mgeni
"Umefika muda sana?" Jimmy alimuuliza
"Hapana ni sasahivi"
"Cid yuko wapi?"
"Sijaja nae yuko busy na mambo yake ya biashara"
"Ooh kumbe ni mfanyabiashara na sijui anyway karibu vipi umekula" Jimmy aliuliza naye alitingisha kichwa kukanusha
"Okay ngoja basi nikaandae kifungua kinywa tule kwanza ndio tuendelee na maongezi" jimmy aliongea na kunyanyuka
"Subiri kwanza......" Jimmy alisimama baada ya mrembo huyo kumtaka asubiri
"Asante" aliongea Bianca akitoa shukrani ya dhati kwa sauti ya upole na Jimmy alitabasamu
"Ni jambo la kawaida kutoa shukrani hivyo usiwaze sana nimepokea shukrani" aliongea kwa sauti ya upole pia
"Japokuwa wewe na kaka yangu ni marafiki lakini haimaanishi mimi na wewe tu marafiki hivyo nataka tuwe marafiki kuanzia sasa" Bianca alikusanya ujasiri na kuongea
"Sawa natazamia urafiki wetu utakapotufikisha" aliongea maneno yenye zaidi ya maana moja
"kweli?" Aliuliza
"Sioni sababu ya kukataa urafiki na mrembo kama wewe" aliongea jimmy na kufanya mrembo huyo kuangalia chini akitabasamu
Monica alitoka jikoni akiwa amemaliza kuandaa kifungua kinywa cha asubuhi hiyo na kukiweka mezani
"Sijui umemfanya nini dada wa watu mpaka anakuonea ila nimempenda" Mony alimnong'oneza Jimmy aliyekuwa akiandaa pamoja naye
"Unadhani sijui unachokiwaza akilini mwako? Sita kama unapanga kumchuna kwa namna yoyote ile hilo sahau"
"Nimekwambia nataka kumchuna shida y....." aliishia njiani na kuweka uso wa tabasamu baada Bianca kusogea kwenye meza ya kula
°°°°°°°°°°
Baadae mchana mida ya saa saba na nusu Jimmy alionekana mitaa ya kariakoo akifanya shughuli mdogomdogo za u'day-worker kujiingizia kipato
Wakati akiendelea na shughuli zake lilionekana gari jeusi aina ya Lexus TX SUV new model likikatiza mitaa hiyo likisindikizwa na macho ya watu wengi, ilikuwa ni nadra sana kwa magari ya kifahari kama hilo kuonekana mitaa hiyo
Lilikwenda ku-park sehemu yenye uwazi na alishuka mwanaume mnene kiasi mwenye upara ung'aao juani na ndevu za mviringo, akivalia suti rangi ya kahawia mkononi akishika simu janja ambayo kwenye skrini ilionekana picha ya watu wawili jinsia moja wamekaa poz la kirafiki
Aliangalia kulia na kushoto kabla ya kuvuka barabara upande wa pili na alienda moja kwa moja mpaka kwenye duka ambalo pembeni kulikuwa na lorry dogo lenye mizigo na watu kadhaa walionekana kufanya kazi ya kuishusha na kuingiza ndani ya duka hilo
Wewe ni Jimmy sio?"
" Ndio ni mimi kiongozi una shida yoyote?" Jimmy aliitika na kuuliza
" Nina ujumbe wako" aliongea
"Ujumbe wangu? Ujumbe gani?" aliuliza tena
Mtu yule alimuonyesha picha iliyokuwa kwenye simu yake ambayo alionekana jimmy mwenyewe na mtu mwingine
"Unamjua huyu kwenye picha hii"
"Ndio ni mzee wangu huyo, amefanya nini kwani?"
"Ninasikitika kukwambia kwamba hatnaye tena"
"Nini?"
"Jana usiku ulikutwa mwili wake ambao haukuwa na uhai umetupwa kando ya ufukwe wa bahari na kitu pekee ni hii picha iliyokuwa kwenye mfuko wa wazi lake"
Jimmy palepale alisitisha kile alichokuwa anafanya na kwenda kukaa pembeni akiwa katika hali ya mawazo sana, Picha hiyo ilionekana kupigwa miaka mitano nyuma kabla ya mzee huyo myahudi kupotea na ni jana aliweza kukutana nae tena lakini cha kusikitisha ni kwamba ameuawa
"Pole sana kwa kumpoteza mzee wako kijani"
"Hakuwa tu ni mzee wangu alikuwa ni kama rafiki yangu na familia yangu, unaweza niambia nini kilichosababisha kifo chake"
"Kwasasa bado hatuna jibu, bado tupo kwenye uchunguzi"
"Vilevile nina maswali pia ya kukuuliza"
"Kabla ya hayo maswali nataka kuuona kwanza mwili wake kudhibitisha kama ni yeye" aliongea Jimmy na mtu yule alimwambia waongozane na hakupinga, walienda mpaka kwenye gari na kuingia kisha kuondoka maeneo yale kuelekea sehemu husika
Nusu saa ilitosha kwao kufika kwenye hospitali ya kuhifadhia maiti na kuingia ndani ya chumba husika
Kulikuwa na mwili umelazwa juu ya meza ndefu ya chuma ya kulazia maiti, mwili ukiwa umefunikwa na shuka jeupe
Jimmy aliusogelea taratibu mwili ule uso wake ukiwa na hisia mchanganyiko, alifunua shuka na kushuhudia mwili wenye alama za kutobolewa na kuchanwachanwa na mapanga kila mahali, mzee aliuwawa kikatili sana na aliweza kudhibitisha ni yeye kweli
Alikunja ngumi kisiri akificha hasira iliyochanganyika na maumivu na alijiambia yeyote anayehusika na kifo cha mzee huyo lazima amkamate
"Nadhani umeweza kudhibitisha kwamba ni yeye sasa ni wakati wa mimi kuuliza maswali muda wa kuomboleza upo wa kutosha" aliongea mtu yule na kauli ile ilimfanya Jimmy amusangalie kwa jicho flani hivi ambalo halikueleweka linamaanisha ni nini
"Unaweza kuuliza"
"Mara ya mwisho kukutana na mzee huyu ilikuwa ni lini"
"Sikumbuki vizuri ila nadhani ni baada ya kupiga picha kipindi kile"
"Una uhakika unachoongea ni kweli?"
"Kipi kinachokufanya utilie shaka maneno yangu?"
"Sawa mara ya mwisho ilikuwa ni kipindi mnapiga picha, je hakukupatia chochote kile kabla ya kupotea au kukwambia chochote kile chenye kutilia shaka?"
"Mimi nakumbuka mara ya mwisho tulipiga picha na kupiga story mbili tatu kabla ya kutokumuona tena na hakuna chochote cha kutilia shaka tuliomgelea kuhusu mademu jinsi ya kutofautisha pisi mbovu, pisi kali na pisi classic" aliongea jimmy na mtu yule alimtazama machoni kumsoms na hakuambulia chochote
"Nikigundua ulichoongesa ni uongo sidhani ka.ma litakuwa jambo zuri kwako"
"Ondoa wasiwasi kamanda nilichosema ni kweli
Mtu yule aliondoka mahali pale akimuacha jimmy peke yake akiutazama mwili wa mzee na kufanya ishara ya msalaba
" Pumzika kwa amani" aliongea kauli hiyo yenye uchungu ndani yake
°°°°°°°°°°
Baadae jimmy alionekana ameketi mahali palipo na utulivu, akiwa katika tafakari nzito, alikumbuka kwa mara ya kwanza alivyokutana na mzee mpaka kuwa marafiki jinsi alivyomfunza kucheza piano, mbinu mbalimbali za kujilinda na mambo mengine mengi ila huzuni kwa.mba mzee huyo ambaye hakulijua hata jina lake zaidi ya kumuita babu na mzee hayupo tena katika uso wa dunia
TO BE CONTINUED..........
Comments