SEHEMU YA 208.
Because I love you.
Watu walijikuta wakishangazwa na jambo lile , kila mmoja alishangaa kuona Mr Air alikuwa akipaa.
“Anapaaa jamani!!”
Ingawa ilikuwa ni rahisi kuweza kushindana na kani mvutano kwa wale wenye mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi , lakini ni mbinu ambazo zilikuwa zikienda kinyume na kanuni za anga.
Mr Air aliifanya hewa iliokuwa chini alivyotaka na mara baada ya kujiimarisha hewani alianza kuinua matofali na vyuma na kuvifanya vielee pia angani. Kwa namna ilivyokuwa ikionekana ni kama vile kulikuwa na kamba ambazo zilikuwa zikivuta vitu hivyo.
Tukio la kushangaza liliendelea kuonekana katikati ya uwanja ule , ilikuwa ni kama vile eneo la katikati lilikuwa haliathiriwi na kani mvutano ya dunia na kufanya vitu viwe kama vile vipo ndani ya eneo lenye zero gravity na kuelea angani.
Mara baada ya Air kutingisha mkono wake hewani , alisababisha mawe na vyuma kuanza kugawanyika na kugeuka chembembe. Ilikuwa ni kama mawe yale na vile vyuma viligeuka na kuwa vumbi ambalo lilielea hewani kwa kusambaa pande zote.
“Hii ndio mbinu yake ya elemental Decomposition?”
“Itakuwa , nimesikia anao uwezo wa kutawala elementi zote za maada . ili mradi awe na muda wa kutosha anao uwezo wa kutenganisha kila kitu.Hivi vyuma na mawe vina elementi za kawaida sana kwake kutenganisha”
“Mbona hio sasa ni hatari . Kama akitumia uwezo huo kupambana si anaweza kumyeyusha adui tu?”
“Umefikiria mbali sana , ijapokuwa ni kweli uwezo wake ni wa juu na anao uwezo wa kugawanyisha vitu lakini ili kufanikisha mchakato mzima anahitaji nguvu nyingi sana za kiroho na kadri muunganiko wa vitu unavyokuwa mgumu maana yake atahitaji nguvu nyingi zaidi kufanikisha. Kwa lugha nyepesi ni kwamba ana mwisho pia wa kiasi anachoweza kutenganisha , ikiwa atakutana na mwanajeshi ambae ana nishati kubwa za mbinu na ardhi anaweza asifanikiwe”
Hayo yalikuwa maneno ya watu kadhaa waliokuwa wakielewa kuhusu uwezo wa Mr Air.
Ndani ya dakika tatu kila kitu kilikuwa kimesagwa na kuwa unga unga unaoelea hewani katikati ya uwanja.
Mara Mr Air alishuka ardhini na kukandamiza mkono wake mmoja kwenye ardhi kama vile alikuwa akiipasha ardhi moto na ghafla tu sauti kama ya tetemeko ilianza kusikika.
Wakati watu wakimaka kile kinachotokea ghafla tu zile chembechembe zilianza kujikusanya sehemu moja kwa kasi na kitu mfano wa umbo mraba lilianza kujitengeneza kwa kupanda juu hewani.
“Duuh! Uwezo wa ajabu sana huu , sidhani kama kuna mtu anaweza kuvuna nishati za mbingu na ardhi na kuja kupata ufunuo wa kutawala elementi za maada kama hivi?”Aliongea Silvia.
“Air uwezo wake ni wa asili , hata kama atokee mtu aweze kupata ufunuo hawezi mfikia”Aliongea Mikaeli.
“Kuzaliwa na Karama ni habari nyingine. Hebu fikiria tokea saa unayozaliwa unakuwa mtawala wa vitu . Hata ujitahidi vipi kuwaonea wivu na kutamani kuwa wao , hutofanikiwa”Aliongea Hamza.
“Lucifer huna haja ya kumuonea wivu Mr Air , kwa ninavyokuona umezaliwa pia na Karama ya kuzifahamu siri za mwili , hivyo uwezo wako sio mdogo pia”Aliongea Auland na kumfanya Hamza amwangalie Auland.
“Mr Auland naona muda wote umelivaa hilo helmeti la chuma , hujisikii vibaya?”
“Sijisikii vibaya”Aliongea Auland kwa sauti kavu.
Wakati wakiongea hatimae steji ya umbo la mraba yenye upana wa mita za mraba zaidi ya mia na kimo cha mita mbili iliweza kusimama katikati ya uwanja , ila bado haikuwa imekamilika kwani kulikuwa na chembe zingine nyingi tu zilizokuwa zikielewa hewani.
Mr Air alisimama na kuanza kuzungusha mkono wake juu angani kwa kuchezesha kama anakoroga hivi na zile chembechembe zilianza kujitenga kimakundi na kisha alianza kushusha kundi baada ya kundi na kwenda kuivaa kile kifusi cha umbo la mraba kwa staili ya kufunika kama shuka. Mpaka anakuja kumaliza kundi la mwisho kufunika steji ile hatimae ilikaza na alifanikisha kumaliza kazi na upepo kutulia na sasa watu waliweza kuona eneo la steji ile likiwa imefunikwa na madini ya rangi ya silver ya kung’aa sana na kufanya ivutie kwa macho.
Watu walijikuta wakishindwa kuzuia hisia zao na kusimama na kupiga makofi mengi. Hakika walionekana kupendezwa na kile ambacho Gwiji huyo alikamilisha ndani ya muda mfupi.
“Tutumie nafasi hii kumshukuru Mr Air kwa msaada wake wa kimiujiza”Aliongea Maxim na kufanya watu wazidishe makofi na muda ule wafanyakazi maalumu wa Baraza la Maksi waliingia na viti na baadhi ya vitu vingine na kuviweka katika mpangilio uliokuwa mwanzo kabla ya jukwaa kuharibika.
Muda huo ilikuwa ni usiku sana , lakini hata hivyo Baraza hilo halikuwa la kawaida, na ni sawa tu kwa watu kutotamani kula au kulala hivyo mkutano uliendelea kama kawaida.
Siku ya kwanza ya Baraza la maksi ilikuwa ni kwa ajili ya kutoa mjumuisho wa maendeleo ya jumla ya ulimwengu wa siri au giza kwa kipindi cha miaka mitano na hio ilihusisha suala zima la kutambua wachangiaji wakubwa wa maendeleo hayo.
Na kupitia hivyo baadhi ya taasisi , makundi na watu binafsi na hata vitengo maalumu vya siri vilipandishwa vyeo na vile vilivyolega vilishushwa madaraja. Kulikuwa na hisia za furaha kwa waliopandishwa na za huzuni kwa walioshuka.
Hamza na magwiji wengine hawakuhudhuria kwa ajili ya kukaa jukwaani tu , hata wao pia walihusika katika majadiliano. Ukweli ni kwamba magwiji walikuwa ni kama viongozi na wawakilishi wa jumuiya kubwa za siri. Hamza katika muda huo aliwakilisha kitengo cha Malibu ambacho kilikuwa ni daraja A huku wengine kama Oleg waliwakilisha makundi yao ya kiharamia. Watu wa Madhabahu takatifu na ya giza ijapokuwa hawakutambuliwa kimadaraja lakini kama wangepewa wasingekuwa chini ya daraja S kama ilivyokuwa kwa jamii kama Freemason na kuendelea.
Adept Association au jamii ya watu waliozaliwa na Karama zisizo zakawaida walikuwa wakipewa heshima ya pekee pia katika Baraza hilo. Ingawa ushawishi wao ulikuwa ukiyumba na kukua vizazi na vizazi lakini uwepo wa Mr Air ambae haijulikani asili yake ilifanya jumuia hio kupewa hadhi ya juu.
Ukiachana na Hamza kubeba kitengo cha Malibu , lakini kwa wakati mmoja pia aliwakilisha jamii yake ya siri ya Inferno. Ingawa ilionekana ni kama jamii ambayo haifanyi kazi lakini wengi hawakuona hivyo na Hamza pia hakuichukulia jamii yake kama imekufa.
Sababu ya kwanini Magwiji kumi waliketi katika jukwaa la juu kabisa chini ya viongozi wa mashirika mengine sio kwa ajili ya kuwapa watu wa kawaida changamoto za kimotisha , lakini vilevile ilikuwa ni kuonyesha heshima juu ya mafanikio yao. Kama ilivyo kanuni ya watu wa ulimwengu wa siri kwamba mwenye nguvu anapaswa kukaa juu ya wengine.
Usiku huo Hamza aliwapatia washikaji zake watatu tuzo , yaani Asmuntis , Azzle na Leviathani kwa mchango wao mkubwa katika ulimwengu wa siri.
Katika kipindi cha miaka mitano ni makundi matatu pekee yalioweza kukwea madaraja na kuingia daraja A na makundi hayo yote yalikuwa yakiongozwa na jamaa zake Hamza. Wakati wa kupokea tuzo juu ya jukwaa wote walionekana kujivunia kwa mafanikio yao.
Regina pia alishiriki katika kikao hicho na kwa bahati nzuri aliwasiliana na wafanyakazi wa kampuni yake tanzu na kuwaambia hatokuwepo mjini. Kutokana na mazingira mapya ya ulimwengu wa siri alijikuta akiwa na msisimko mwingi na hakupata hali ya usingizi hata kidogo.
Black Fog ndio aliechukuwa jukumu la kumuelezea Regina kila kitu ambacho hakuwa akielewa na kwa jinsi Regina alivyosikiliza kwa umakini ni kama vile angefanyishwa mtihani baada ya hapo.
Regina alishikwa sana na hali ya kujivunia na furaha wakati ambao alimuona Hamza akikabidhi tuzo huku watu wengi wakimshangilia.
Hatimae usiku wa saa tano Baraza lilihitimishwa kwa siku ya kwanza na kutarajiwa kuendelea siku inayofuata. Magwiji ndio waliokuwa wa kwanza kutoka ukumbini na kisha ndio wengine wangefuatia.
Hamza ile anakaribia njia ya VIP ya kutokea Khalid alikuwa tayari yupo anasubiri na alimkabidhi ufunguo wa gari yake ya Leykan.
Ile Hamza anasogelea uelekeo wa parking ya magari aliweza kukutana na mtu ambae alimfahamu , alikuwa ni Mr Air ambae alionekana kuwa hapo kwa ajili ya kuchukua ufunguo wa gari yake pia.
Hamza mara baada ya kumuona alishindwa kuzuia shauku yake na kujiuliza huyu mtu ambae anaweza kupotea na asionekane ina maana na yeye anaendesha gari na kama anaendesha gari ni ya aina gani?.
Kilichomfurahisha Hamza ni kwamba Mr Air hakuficha sura yake , ungekuwa mtu wa kawaida usingemfahamu. Ila magwiji wanatambuana.
Unachopaswa kujua Hamza alishawahi kukutana na Mr Air miaka mitano iliopita katika baraza la maksi , lakini sura ambayo alikutana nayo kipindi hicho ilikuwa tofauti kabisa na ya muda huo anayiona , ya kipindi kilichopita ilionekana ya kijana zaidi kama alikuwa na miaka ishirini na nane , lakini ya muda huo alionekana kuwa mzee hivi na mwonekano wake kwa ujumla ulikuwa tofauti.
Kulingana na taarifa zilizopo , Mr Air mara zote anapoonekana sura yake ni tofauti, akificha muonekano wake wa kawaida. Sasa muda huo Hamza ni kama alihisi amemuona Mr Air katika muonekano wake halisi.
Ingawa hawajawahi kuwa na ukaribu wa sana , ila Hamza aliona sio mbaya kama atamchangamkia , isitoshe wote walikuwa daraja sawa la ugwiji.
“Hey Mr Air , na wewe upo hapa kuchukua gari yako?”Aliongea Hamza na kumfanya Khalidi mara baada ya kusikia Hamza anaongea haraka sana alimsogelea yule mzee baada ya kumtambua na kumkabidhi ufunguo wa gari aina ya Volkswagen.
Hamza aliishia kukunja macho yake huku akihisi labda ameona tofauti, kwa haraka haraka aliweza kugundua ufunguo huo ni wa gari aina ya Beetle(Mende) , vigari flani hivi vya kizamani sana.
Hamza alijiuliza yaani huyo bwana ni kiongozi mkubwa wa watu wasiokuwa wakawaida na ana hadhi ya ugwiji lakini anaendesha kigari kadogo kanakofanana na mende?.
Ukiachana na swala la kuwa gari hilo lilikuwa zuri au lah suala zima lilionekana kutokuwa la kawaida.
Mara baada ya kumuona Hamza , Mr Air alionekana kushangaa pia. Hakuwa mpiganaji hivyo hisia zake hazikuwa kali sana na hio ni moja ya udhaifu wake.
Mr Air aliishia kutingisha kichwa kumuitikia Hamza na kisha alichukua ufunguo wake na kugeuka kuondoka.
Hamza alijisikia vibaya na kujiuliza anaondokaje sasa wakati anataka kumuongelesha . Lakini Hamza kuona hivyo hakutaka kulazimisha pia , kwasababu hakutaka kuongea nae hakuona haja ya kumlazimisha pia.
Wawili hao walisogea mpaka upande wa gereji na muda huo Hamza alianza kuhisi harufu hafifu ya marashi ikimtoka Mr Air na kumfanya amwangalie kwa umakini , kwa hali isio ya kawaida Hamza alihisi harufu inayomtoka ni kama alishawahi kuinusa mahali lakini hakukumbuka.
Ile Mr Air alipofikia kigari chake cha Mende cha rangi ya njano na kufungua mlango kuingia ndani, Hamza aliongea;
“Mr Air tushawahi kukutana?”Aliuliza na kumfanya Mr Air kupozi kidogo.
“Miaka mitano iliopita”Alijibu.
“Hapana , namaanisha ukiachana na baraza la maksi , tulishawahi kukutana hapo kabla?”
“Hapana”
“Oh ! Basi sawa , tutaonana kesho”
Mr Air hakujali kingine zaidi na aliingia kwenye gari yake na kuliwasha na kuliondosha ndani ya eneo hilo.
Hamza alijihisi labda ni hisia zake tu hivyo alipotezea na yeye kuingia kwenye gari yake na kuondoka ndani ya eneo hilo.
Kwasababu ilikuwa usiku tayari , Hamza aliendesha moja kwa moja kurudi Shamba. Wengine pia walikuwa wamesharudi wakiambatana na Regina.
Regina mara baada ya kufika huko alijikuta akishangaa na kujua kumbe kundi la Hamza linaisha sehemu nzuri hivyo na sio hotelini. Alishindwa kujizuia kumlalamikia Hamza kutokuja nae.
Upande wa Hamza hakujua kama mwanamke wake alikuwa akipenda mazingira ya aina hio na alimuahidi baada ya Baraza wataendesha farasi pamoja.
Saa saba za usiku meza kubwa iliandaliwa vinono na wapishi wabobevu kabisa. Hamza alimchukua Regina na kuungana na washikaji zake na kufurahia chakula cha usiku wa manane.
Kila mmoja alikuwa vizuri kwenye kudhibiti usingizi hivyo matokeo yake hawakujali muda ilikuwa ni saa ngapi na walikunywa kujigalagaza.
“Mhunzi na Mchafu mniwie radhi kwa kutowasaidia mpaka mkaumia, nilitaka kuwaambia tokea mwanzo , lakini yule hayati mara baada ya kuona hila zake nikaona ngoja nicheze nae kwanza”Aliongea Hamza huku akiwa ameinua glasi kwa ajili ya kugongesheana na washikaji zake.
“Bosi huna haja hata ya kuelezea. Tunaelewa kabisa mbona”Aliongea Azzle.
“Ni kweli! Nadhani pia hatukupaswa kuwa na wasiwasi juu ya uwezo wako”Aliongea Asmuntis.
Hamza hata yeye alijua washikaji zake wasingemchukia kwa suala dogo kama hilo , hivyo alibadilisha mada.
“Mchafu nichagulie vijana wa moto sana kwenye kundi lako, angalau wakiwa na rangi rangi hivi za kujificha itakuwa vizuri. Nataka kuondoka nao kurudi Tanzania”
“Bosi unataka kumuwekea ulinzi shemeji yetu?”
“Ndio, na itakuwa vizuri kama watakuwa weusi na wanaojua tamaduni za waswahili ili kupunguza kushitukiwa , tunaweza pia kuwaandalia utambulisho feki”
“Bosi hilo limeisha , nitakuchagulia vijana mahili sana”
“Unataka kunilinda?” Regina aliongea kwa kumnong’oneza Hamza.
“Mke wangu kwa akili zako , siwezi kukuficha kitu”
Regina aliishia kuvimbisha mashavu bila ya kuongea kingine , alijua fika kama asingeweka watu wa kumlinda angetekwa tena na ingempa wakati mgumu. Lakini kwa namna Hamza alivyohitaji kundi la watu alijua lazima sio yeye tu ni pamoja na wengine, haikumfurahisha lakini asingeweza kumzuia.
Baada ya chakula Regina ndio aliekuwa wa kwanza kutaka chumba cha kulala , hakuwa na mafunzo ya kijeshi kama wenzake hivyo kuhimili purukushani za siku nzima bila ya kupumzika asingeweza.
Hamza upande wake alimuita Black Fog na kwenda nae kwenye majani nyuma y a banda.
“Bro umeniita , kuna tatizo?” Black Fog alijua kwasababu ya ujio wa Regina Hamza angekuwa bize na mke wake , lakini alishangaa Hamza kumuita , licha ya hivyo alishikwa na furaha.
Hamza alieshikilia sigara na mkono wa kushoto alinyoosha wa kulia na kumshika Black Fog kichwani na Black Fog kuona hivyo moyo wake ulitingishika mara baada ya kupatwa na wazo, au Hamza anataka wafanye.
Wakati Black Fog akiwa katika ulimwengu wake wa kujitakia , upande wa Hamza alikuwa akimrekebisha mkao wake kuanzia mikono , kisha na shingo, kwa namna ya kuminya , yaani alikuwa akimrekebisha na kumpima kwa wakati mmoja kwa kulenga lymph node(tezi).
Ndio muda ule Black Fog alishituka na kugundua kwamba sio kama alivyofikiria , kutokana na kuhisi hali mpya katika mwili wake.
“Naona majeraha yaliosababishwa na mbinu ya Hundred Shadows yamekwisha kupona”
“Ni kwasababu nilipata muda wa kumpumzika ndio maana”Aliongea huku akitabasamu.
“Roda kuna mafunzo nataka kukuelekeza ndio maana nimekuita , nilipanga nikuelekeze mapema lakini kwa ajili ya kuendeleza maigizo yangu kwa Metal Tide ndio maana ninakuelekeza sasa hivi”
“Bro , unataka kunifundisha mbinu ya mafunzo ya nishati ya Mbinu na Maji?”
Hamza mafunzo yake ya nishati aliyapatia kutoka kwa Mr Black na watu wengi walijua mbinu ya Mr Black ilikuwa ni ya nishati za mbingu na Maji , yaani tofauti na mbingu na ardhi. Hivyo Black Fog alijua labda Hamza anataka kumuelekeza mbinu hizo.
“Hapana , tayari una nishati za mbingu na ardhi za kutosha kwenye mwili wako na vilevile umejifunza mbingu ya Hundred shadows , hivyo haina haja ya kuongezea na mbinu nyingine ya nishati. Ninachotaka kukufundisha ni mbinu nyingine kabisa ambayo nimeigundua mwenyewe. Sijaipa jina bado , lakini nadhani unaona uwezo wangu hautegemei nishati tofauti na nguvu pekee za kimwili. Kuna utofauti kati yetu hivyo sitakuelekeza mambo magumu sana , ila njia nyepesi ambayo itaimarisha mwili wako kwa ujumla na kama utakadhania nina uhakika ndani ya miaka mitatu ijayo utaweza kuihimili nguvu ya hundred shadows na kupanda levo zaidi”
Black Fog hakupenda mwanzo lakini mara baada ya kusikia mbinu hio ingemwezesha kuhimili nguvu ya hundred shadows alifurahi.
“Bro kweli unataka kunifundisha mbinu yako , sio kwamba ni siri na muhimu kwako?”
“Mbinu ninayokufundisha haina siri kubwa sana , siri ipo kwa anaejifunza mwenyewe kwa namna atakavyofungua vifungo vya siri ya mwili wake . Hivyo ninachokufundisha ni maelekezo ya kawaida sana , lakini namna utakavyoyachukulia na kukufaidisha ni wewe mwenyewe”
“Sawa , lakini vipi naruhusiwa kumwambia Master?”
“Inaonekana bado una heshima kubwa sana kwa Master wako. Usiwe na wasiwasi maana kabla sijafanya haya maamuzi nishaongea nae na anajua kinachoendelea”
“Basi itakuwa vizuri! Kama nitaweza kuihimili nguvu ya Hundred shadows, nina uhakika uwezo wangu utakuwa kwa viwango vingine”.
“Usiwe na wasiwasi kabisa , nitakuelekeza hatua za mwanzo na ukishazimaliza nitakuelekeza hatua inayofuata”Aliongea Hamza.
Alichopanga kumfundisha ni kile kile ambacho alimuelekeza Yonesi na Dina.
Mara baada ya kumuelekeza kutokana na uwezo wa Rhoda , ilikuwa rahisi kwake kuhimili na kuelewa kwa uharaka na kadri alivyojaribu alijikuta akianza kuhisi kitu ambacho hakuwahi kukifikiria mwanzo na macho kumtoka.
Baada ya kama masaa manne hivi , wote walikubaliana kurudi kupumzika licha ya kwamba kushapambazuka. Kwasababu watu walijua Hamza na Regina ni mume na mke waliwaandalia chumba kimoja.
Hamza mara baada ya kuingia chumbani alihakikisha hapigi kelele kwa hofu za kumuamsha Regina lakini ile anaingia alishangaa kuona Regina alikuwa macho na alikuwa akimalizia kuongea na simu.
“Wife kumbe umeamka?” Aliuliza Hamza akiwa na tabasamu.
“Nimeamka muda mrefu tu. Nilikuwa nikiongea na watu wa kampuni”
“Basi twende tukapate kifungua kinywa”Aliongea Hamza na Regina alitingisha kichwa na kushuka kitandani na kuvaa sendo.
“ Vipi na leo tunaenda kwenye mkutano?”
“Yeah, nina makubaliano ya watu wa kitengo cha Malibu. Leo nitaenda kukamilisha suala lao . Ila kwa wewe mke wangu kama umechoka huna haja ya kwenda , nitamuagiza mtu kwa ajili ya kukutembeza tembeza”Aliongea Hamza
“Hata mimi nataka kwenda kuangalia . Nataka kujua kwa undani kuhusu ulimwengu wa siri ulivyo , vinginevyo nitaendelea kujiona mjinga tu wa kutoelewa vitu”
Hamza aliishia kumwangalia mwanamke huyo na tabasamu la ridhiko, Regina alionekana kuwa tofauti sana na siku zote hakuwa kam bosi na hakuwa na ukauzu wowote , alionekana kuwa mwanamke wa kawaida mrembo.
Mwanzoni Hamza alikuwa akijitahidi sana kumuelewa Regina , lakini mpaka kufikia hatua hio walikuwa wakijuana. Pengine ni kwasababu ya jana hatimae Regina ameanza kumchukulia Hamza kwa uhalisia wake na sio ule wa maigizo. Alionekana kuwa na amani zaidi mbele ya Hamza kuliko siku zote.
“Wewe mbona unaniangalia tu” Aliuliza Regina ambae alikuwa akipiga nswaki na mara baada ya kuona Hamza muda wote anamwangalia alihisi aibu.
“Ni kwasababu mke wangu , nimegundua kadri ninavyokuangalia ni kama unazidi kuwa mrembo na kufanya moyo wangu kushindwa kufanya kazi yake ya kusukuma damu kwa usahihi”
“Eeh Baba! Utakuwa kipofu wa macho wewe sio bure. Uso mkavu hivi!”
“Uzuri wa mwanamke huonekana wakati wa asubuhi na kwako wewe mke wangu licha ya uso wako kuwa mkavu , lakini unavutia”Aliongea Hamza huku akicheka.
“Laiti wale mashabiki zako wanaona ulivyo hivi , nina uhakikwa kichaa kinaweza kuwashika”Aliongea Regina akitingisha kichwa.
“Mimi nina nini kwani, kwanza lazima wakubaliane na mimi kwamba mke wangu ni mzuri”
“Toka huko. Nwnda nje kwanza ataka kukojoa”Aliongea Regna huku akielekea bafuni.
Chumba hiko licha ya kuwa na choo cha ndani lakini hakikuwa na mlango ndio maana.
“Wewe kojoa tu , sitokuchungulia”
“Wewe toka bwana , la sivyo nitakasirika”
Hamza alijikuta akiwa hana jinsi na kuishia kutoka na kufunga mlango. Lakini wakati akiwa mlangoni na kuvuta picha namna Regina alivyo uchi, alijikuta akishindwa kujizuia na mwili wake kuwa wa moto.
Mara baada ya Regina kumaliza mambo yake , wawili hao walichukuana na kwenda dining kwa ajili ya kifungua kinywa , wengine pia waliweza kufika na kuungana nao.
Katikati ya kifungua kinywa , Regina alipokea simu na alionekana kusikiliza na kisha kuitikia na kukata.
“Helena ameamka. Watu wa hospitali wanasema kama unataka kwenda na kumuona unaweza kwenda”Aliongea akionekana kufurahishwa na taarifa hio.
“Shem, Licha ya Helena kutaka kukuua ila uliamua kumuokoa. Nadhani umekwisha kufanya yalio ndani ya uwezo wako. Bado tu unataka kuonana nae?”Aliuliza Azazel.
“Lakini hana ndugu yoyote , nimesikia kutoka kwa baadhi ya wanajeshi, hana ndugu wala mume , ameamka mwenyewe akiwa hospitalini nahisi kumuonea huruma”Aliongea Regina kwa kusita kidogo na kufanya watu wote kuangaliana.
“Shemeji hakika una roho nzuri sana”Aliongea Berly.
Regina aligeuza macho yake na kumwangalia Hamza aliekuwa bize na Sandwich.
“Unaonaje nikienda hospitalini kwanza na kisha nitakuja kwenye mkutanano baadae?”
“Wife unadhani upo Dar hapa kwamba unaweza kupanda taksi na kwenda unapotaka? Inabidi nikupeleke mwenyewe , hata hivyo mkutano unaanza mchana, nadhani pia itakuwa vizuri ukanunue na baadhi ya nguo na kusafisha nywele, unaonaje?”
“Sawa”
Comments