Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Jimmy alijuana na mzee kwa zaidi ya miaka kumi na katika miaka yote hiyo alijifunza mengi kutoka kwake, jimmy hakuwa na ndugu yeyote upande wa marehemu baba yake na mama yake hivyo kumchukulia mzee huyo kama ndugu pekee aliyenaye

Jimmy aligeuza shingo yake kuangalia pembeni kushoto kwake alipokaa, kulikuwa na karatasi lililokunjwa ikionyesha kuna kitu kimehifadhiwa ndani yake

Alichukua karatasi na kuikunjua na yalionekana majani yenye rangi ya ukijani iliyokauka ilikuwa ni bangi(Marijuana) haikueleweka ameitoa wapi lakini mwamba baada ya kukunjua alianza kufanya mchakato wa kusaga majani yale na kuyaweka kwenye karatasi kisha kukunja tayari kwa kuvuta.

Anakuja kugundua kilikosekana ni kiberiti tu cha kuwashia ganja hiyo hivyo mpango wake kusitisha. Alichokuwa akitaka ni utulivu wa akili na aliona pengine ganja ingemsaidia kwa asilimia kubwa lakini mpango wake haukuweza kuendelea kutokana na kiberiti kukosekana. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kutaka kuvuta ganja

Mara alikumbuka kitu na kuangalia pembeni kulia kwake kulikuwa na kitabu kidogo cha zamani sana kutokana kuchakaa kwake, kilikuwa na michoro ya sajabu ajabu isiyoeleweka ni michoro ya aina gani alikichukua na kukifungua kuanzia kurasa ya kwanza hadi mwisho lakini jambo la kushangaza ni kwamba hakukuwa na maneno yoyote zaidi ya karatasi kuwa unjano kwa mbali kuashiria ni cha muda mrefu sana

Jimmy alikigeuzageuza kitabu kukitazama ambapo mwisho wa siku alichoka na kuanza kujiuliza maswali mengi kichwani yasiyo na majibu, machache kati ya maswali aliyokuwa akijiuliza ni je kitabu hiko ni nini? Mbona hakina maandishi? Mzee myahudi alikuwa na maana gani kumpatia kitabu hiki?

Kuliko kuumiza kichwa na maswali yasiyo na majibu aliona apotezee tu na alinyanyuka kuondoka mahali hapo.

Muda mchache alionekana kwenye bar ameketi kwenye kaunta akinywa bia ya Serengeti lager kwa utulivu, hakukuwa na mteja yoyote kwa wakati huo zaidi yake, hata muhudumu pia hakuwepo. Mimi sijui kwanini yuko peke yake, ukisema ameingia kama mwizi mimi sikupingi ndugu msomaji

Wakati ametulia akisikiliza mziki laini uliokuwa ukilia kupitia simu yake ndogo aliongezeka mwanamke mmoja mzungu kwenye kaunta na kuketi

°°°°°°°°°°

Upande wa pili ndani ya gari kulikuwa na watu wawili ndani wakiwa katika hali ya ukimya

"Nadhani kuna kitu anaficha" 

"Usipoteze muda toa taarifa yote" 

"Kwa nilivyomuhoji anasema hakuachiwa chochote na yule msaliti, Vijana niliowapa kazi ya kumfatilia wamemuona ameshika kitabu kidogo" 

"Kinafananaje?" 

"Ni kama ulivyosema Sir" 

"Hahaha nadhani ni muda muafaka wa kukiweka mikononi mwetu" 

"Lakini unaweza kuniambia ni kitabu gani na kinahusu nini? Nimekuwa nikisikia tu ni hazina kubwa" 

"Jua mipaka yako" 

"Samahani  kwa kurupuka kwangu mkuu lakini sidhani yule mwanaharamu atamkabidhi hazina hiyo kijana asiye na uwezo wa kuilinda" 

"Hilo linakwenda kujulikana mda mchache mbeleni" 

......... 

"Nini kinachokuweka kwenye hali ya mawazo mkaka mzuri" aliongea mzungu yule kwa kiswahili fasaha akiachia na tabasamu

"Huna haja ya kuliongelea kama hutaki, nimeshazioona sura kama hizo hapa kabla, Inaonekana umempoteza mtu muhimu sana kwako si ndio?" aliendelea mzungu yule

"Umejuaje?" Jimmy aliuliza

"Uzoefu tu naelewa unavyojisikia"

"Sikutarajia hili lingetokea ile itoshe kusema duniani watu tunapita tu"

"Siku ndefu huh?"

"Ni siku ndefu ndio kiasi cha kumchanganya anyway unaweza niambia wewe na rafiki zako kwanini mlikuwa mkinifuatilia?" Jimmy aliongea huku akigida chupa ya bia

Mzungu yule aliishia kutoa tabasamu na kuongea "Kama nilivyotegemea yule msaliti lazima atafute mwanafunzi wa kurithi mambo yake" 

"Msaliti gani huyo unaemzungumzia ebu funguka itoshe kusema nishachanganyikiwa vya kutosha huna haja ya kuendelea kunichanganya" 

"Momochi Saizo" 

"Ndio nani huyo Momochi unayemzungumzia" jimmy aliuliza

"Inasikitisha sana licha ya Ukaribu uliokuwa naye hukuweza kufahamu hata jina lake" 

"Unamaanisha yule mzee aah kumbe anaitwa Momochi Saizo sikujua mana ni msiri sana yule mzee" 

"Tusipoteze muda unapaswa kunikabidhi kile ambscho si mali yako" 

"Unazungumzia mali gani sikumbuki kama niliwahi kuiba chochote" sekunde anayomaliza kutamka maneno hayo ghafla kisu aina ya "dagger" kutoka mkononi mwa yule mzungu kilikuja kwa kasi kuelekea shingoni mwa Jimmy lakini alikuwa ashastukia mchezo kwani alirudi nyuma kwa kasi na ilibaki kidogo tu kuchanwa koo yake, hakuishia kukwepa naye alimrushia chupa ya bia ambayo ilikwepwa pia

"The book you fool" alifoka yule mzungu na waliongezeka watu wengine kutoka kwenye kona za bar hio kama vivuli vilivyojificha kwenye giza

"Damn! ninyi ni maninja!" Jimmy alishangaa kwa jinsi walivyojitokeza

Licha ya kujua kwamba alikuwa akifuatiliwa tangia atoke kule mochwari lakini hakutegemea kama wangekuwa ni maninja, kuhusu namna alivyogundua kuwa ni maninja ni hiyo mbinu ya kujificha sehemu yenye ugiza pasipo kuonekana

Ni mbinu Ifahamikayo kama Shadow step ni mbinu ambayo mtumiaji hugusa kivuli na kuungana nacho kwa ufanisi ili kujificha. Akiwa ndani ya kivuli, anaweza kusafiri kati ya vivuli vilivyounganishwa kama milango ya kupita kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Ieleweke naposema kivuli namaanisha  sehemu yenye hali ya ugiza kupitiliza, jambo linalofanya iwe njia bora ya kusafiri bila kuonekana.

Mwili wake, fahamu, au nishati yake zinaungana na kivuli. anakuwa haonekani au hawezi kuguswa, kulingana na kiwango cha uwezo wake.

Mara nyingi hutumiwa kufanya upelelezi wa jambo flani mbinu hiyo inahusiana na kanuni za Taoismu na Zen ya "being formless like water, adapting seamlessly, and utilizing the natural world rather than forcing one's will upon it. The darkness is not an enemy but a tool, a medium through which one transcends visibility and perception." kwamba  kuwa bila umbo kama vile maji, kuzoea mazingira, na kutumia nguvu za asili bila ya kulazimisha. Giza si adui, bali ni chombo cha kujificha na kufanikisha malengo bila kutambulika

Jimmy katika ukuaji wake amekuwa akifundishwa mbinu za kimapigano kutoka kwa Mzee Momochi Saizo myahudi mwenye jina la asili ya kijapani akidai anatafuta mrithi kabla hajafa na uzee wake, ni mbinu nyingi ambazo nyingi tutazijua huko mbeleni

"Nimesema sijaiba mali yoyote kutoka kwenu eleweni" Jimmy alisisitiza

"Swii swiii swiiii" milio ya visu vidogo vyenye umbo la nyota vijulikanavyo kwa jina "Shuriken" vilisafiri kwa kasi hewani vikimsogelea jimmy

Alikwepa kwa kasi kwa kuruka sarakasi moja matata sana na kujivingirisha hewani kama mtaalamu na kutua chini kwa ustadi wa hali ya juu

"Miaka zaidi ya kumi ya msoto wa kujifunza mbinu nyingi sasa nadhani ni muda wa kuzifanyia majaribio, uzoefu ni muhimu sana" alitamka akiachia tabasamu lisilo jema usoni mwake

Palepale jimmy kwa spidi mara tatu ya Hussein Bolt alichomoka na akisindikiza na ngumi yenye ujazo kamili alimlenga kwenye kifua mzungu huyo lakini mzungu naye alikuwa ni mtaalamu sana kwani aliweza kulipangu na jimmy alitegemea hilo, bila kutegemea mzungu alishtukia teke la shingo alilopigwa kwa staili ya "Scissor kick a.k.a kawi chagi"

KIlikuwa ni kitendo cha spidi sana na "timing" ni mbinu ya kawaida tu lakini iliyopigiwa mahesabu kisawasawa, mzungu huyo alianguka chini kutokana na uzito wa teke hilo

Jimmy hajakaa sawa maninja wengine walianza kumshambulia na alikuwa akikwepa mashambulio kama anacheza mziki vile kwa staili matata ya Capoeira akiruka na sarakasi mbili tatu kukwepa visu na mapanga

Ilikuwa ni show moja matata sana na ndani ya dakika tano Jimmy aliweza kuwadhibiti maninja sita kwa kuwazimisha na alibaki mmoja, yule mwanamke mzungu ambaye alikuwa akitazama show mwanzo mwisho bila kuingilia

"Not bad at least his effort was worth it but too bad he ain't here to witness his beloved disciple" aliongea mzungu yule akimaanisha kwamba sio mbaya juhudi zake(Mzee Momochi) Zilistahili lakini kibaya zaidi hayupo hapo kumshuhudia mwanafunzi wake mpendwa"

"So it was you fools who killed him? Who are you fools?" aliongea Jimmy akigundua kwamba hao ndio waliohusika na kifo cha mzee Momochi na kutaka kujua hao watu ni akina nani

"That old man of yours had Something very precious you know?" (Huyo mzee wako alikuwa na kitu cha thamani sana unajua?) aliongea mzungu huyo akitabasamu

"And you're going to hand it over young man by will or forxe" (Na unakwenda kunikabidhi kijana iwe kwa hiari ama kwa kutumia nguvu) aliongea mzungu huyo na kuushikilia upanga vizuri akijiandaa kufanya mashambulio

Jimmy alipandwa na hasira baada ya kugundua hao washenzi ndio wamehusika na kifo cha mzee wake. Aliinama akiokota upanga aina ya Ninjato ulionyooka wenye urefu wa sentimita arobaini na nane(48)

Alianza kutembea kulia na kushoto akinyoosha viungo vya mwili na kukaa mkao wa utayari kwa pambano

"Teng! Teng! Teng! Twing! Zzzzzz!!!" ilikuwa ni milio ya mapanga kugongana na kukwaruzana kiasi cha kutoa cheche, ilikuwa ni vita ya siraha ya ana kwa ana kati ya mbongo na mzungu

"Sikuwahi kufikiria Ipo siku nitafikia hatua hii" jimmy aliongea huku akiendelea kupambana

"Kwamba nitafikia hatua ya kutaka kumwaga damu,.... Yule mzee siku ambayo nakutana naye nilikuwa ni mpweke sana sikutarajia kama tungefika mbali kiasi kile cha kumchukulia kama mwanafamilia....."

"Shut your damn mouth and hand over the book you fool" alifoka yule ninja mzungu

"Teng! Ting! Ting! Teng!"

"Ni jana tu hapo nilipokutana nae baada ya kupotea kwa zaidi ya miaka mitano halafu......"

"..... Halafu nyinyi viroboto mmemuua...."

".......Kwa sababu ya kipuuzi sana, For a fucking book? Is that book worth much than his life?"

"Cut the Crap!" mzungu aliona Jimmy anampigia makelele tu yeye alichotaka ni kitabu tu na sio ngonjera

Mpambano uliendelea kwa takribani dakika nne na katika dakika ya tano Jimmy alifanikiwa kulidondosha panga la mzungu huyo chini na kumchana baadhi ya sehemu ya mwili

(shwaaaaa!) Aaarggh!! " alipiga makelele mwanamke yule baada ya kuchanwa na upanga mkali kwenye goti na kudondoka chini akipiga goti na mguu mwingine

" Any last words miss before going six feet under? " Jimmy alimuuliza kama ana kauli ya mwisho huku akimwekea upanga karibu na koo tayari kwa kuchinja

"To be honest you really are a talent young man you have my respect but have you ever thought about your family?"(Kusema kweli una kipaji sana kijana hilo una heshima yangu lakini je umeifikiria kuhusu familia yako?) aliongea na kutabasamu mzungu yule licha kuhisi maumivu na damu kumvuja

"What did you do to my family you bitch?"(Umeifanya nini familia yangu we malaya?) Jimmy alifoka kwa hasira

"You have a pretty sister oh and your mama too"!(Una dada mzuri sana oh na mama pia)

"Niambie umewafanya nini we malaya kabla sijakutoboa macho" Jimmy aliongea kwa hasira na kumchana shavu lake na upanga na mzungu yule aliishia kuvumilia tu kwa kujikaza

"You dare hurt my face you moron?" Alilaani

"Nishakichoka kizungu chako niambie wako wapi?" Aliongea akiwa sura ya kikauzu zaidi

"Nadhani unapswa kufikiria kwa makini kati ya familia yako na hiko kitabu kipi chenye thamani" aliongea na kuzidi kumtia tu Jimmy hasira

"I think your mama didn't warn you that to never mess with someone's family"

"kama unataka kuiona familia yako ikiendelea kuishi unapaswa kunikabidhi hiko kitabu"

"Sina kwasasa" aliongea Jimmy na mzungu yule alitabasamu na kuingiza mkono wake mfukoni na kumpatia simu ndogo na kumrushia Jimmy

"Sina haraka unapaswa kwenda kukifata mahali ulipokificha baada ya masaa mawili nitakutafuta kupitia hiyo simu ukifanya ujinga nadhani unajua nini kitatokea" aliongea na kwa tabu sana alinyanyuka akiondoka mahali pale akitembea kwa kuburuza mguu mmoja

Jimmy aliishia kumwangalia mzungu huyo kwa macho yenye ukauzu bila kufanya chochote mpaka anatokomea zake mahali hapo

Alienda mpaka kwenye kaunta ambapo aliacha simu yake, aliichukua na kubonyeza-bonyeza kisha kuiweka sikioni

..........

Upande mwingine kwenye refu kwenda hewani lenye floors zaidi ya arobaini ndio makao makuu ya VELORA VROUP OF COMPANIES, kwenye floor ya ishirini na tano ndani ya ofisi kubwa iliyopambwa na vitu vya bei vhali kukiwa masofa na samani zingine kuendana na hadhi ya mwenye ofisi hiyo

Kwenye meza kubwa yenye tarakishi kampuni ya samsung alionekana mwanaume kijana mweusi aliyevalia suti nyekundu ikikosekana tai tu, mwanaume huyo alikuwa bize na tarakishi yake.

Mara simu yake aina ya Iphone ilianza kuita na alipoangalia namba ya mpigaji alikuta imeseviwa "Hero" alitabasamu na kuipokea

"Niambia bro" Cid alianza kuongea

"Upo wapi?" upande wa pili ambaye ni Jimmy aliuliza

"Nipo kazini nadili na mambo ya kampuni unashida yoyote bro?"

"Nipe Location nakuja sasahivi"

"Kuna nini kwani"

"Wewe nipe location nikifika tutaongea hukohuko"

"Poa kaka nakutumia sasahivi" aliongea na kukata simu kisha kutuma location kwa njia ya ujumbe

Dakika ishirini baadae simu ikaita tena na Cid aliipokea

"Nimeshafika uko floor ya ngapi?"

"Chukua lift mpaka floor ya ishirini na tano ukifika utakutana na dada wa mapokezi atakuleta ofisini nimeshampa taarifa tayari"

Dakika chache mbeleni mlango wa ofisi ya Cid ulifunguliwa na dada wa mapokezi akifuatiwa na Jimmy ambaye mkononi alikuwa ameshikilia kitabu kidogo

"Welcome to my workplace brother this is my office feel free" Cid alimkaribisha Jimmy kwa kingereza

ALUTA CONTINUARA........ 

Previoua Next