SEHEMU YA 209.
Kila mtu alimwangalia Hamza kwa namna ya mshangao , hakuna aliedhania Hamza angemsindikiza mke wake kwa ajili ya kufanya kitu kama hicho.
Walijikuta akishindwa kujizuia na kumwangalia shemeji yao Regina na mwonekano usioelezeka.
Mara baada ya kifungua kinywa , Hamza alimchukua Regina katika gari yake ile ya kifahari na kuelekea mjini.
Regina mara baada ya kukaa kwenye gari aliishia kumwangalia Hamza aliekuwa siriasi na usukani.
“Marafiki zako nadhani wananiona mimi ni mjinga kwakufanya haya yote kwa mtu alietaka kuniua”Aliongea.
“Ni kweli wewe ni mjinga, lakini ndio ninachokupendea mke wangu , nitafanyaje sasa?”
“Na umeongea hapo. Pengine siku moja utanichoka nikiwa katili na hata kuniita kama watu wanavyonisema huko mtandaoni kwa kusema mimi ni mfanyabiashara mkatili. Hata marafiki zako watakuunga mkono baada ya kuanza kunifuatilia mtandaoni na kuona watu wanavyoniita majina ya ajabu”
“Haha! Wife unachekesha , kumbe unafuatilia watu wanasema nini kuhusu wewe?”
“Unacheka nini ! Unadhani kama sina akaunti Instagram siingii kuperuzi”
“Wife huna haja ya kujali watu wanavyokufikiria na kukuongelea”
“Inamaana wewe hujali wanavyoniongelea?”
“Sijali , Nakupenda na hio inatosha”
“Lakini marafiki zako wanaweza kuniona mimi ni mtu mbaya na najaribu kuigiza tu kuwa mkarimu”
“Haha.. Wife unajua unavyoongea hivyo ni kwamba unaogopa wakiona kwamba hufai kuwa mke wangu ndio maana wasiwasi umekujaa.Naona hatimae umekubali kuwa mke wangu kabisa sasa?”
“Mimi nimeonyesha wasiwawasi wangu tu , linahusiana vipi na kuwa mke. Kwanza hata sijajua nikukubalie au nikukatalie wakati wa kunichumbia, acha kujisifia. Mimi naongea jambo la usiriasi wewe unaingiza habari nyingine”Aliongea huku akimpiga na mkono begani.
Hamza alimshika mkono Regina na kisha alimwangalia usoni kwa usirasi
“Usiwe na wasiwasi mke wangu , hawawezi kukuchukia na badala yake nina uhakika lazima sasa hivi watakuwa wanajua kwanini nimeamua kukuoa”
“Kweli?”
“Kweli kabisa”Aliongea Hamza na kumfanya Regina kufurahi.
“Ila hujaniambia kwanini umenioa. Au ni kwasababu bibi alikulazimisha?”
“Hapana bwana! Babe Regina kwanini bado unaniuliza hili swali? Nishasema nakupenda na napenda kila kitu kuhusu wewe”
Regina mara baada ya kusikia kuhusu hivyo alijikuta akiganda na kuishia tu kutoa sauti ya ‘oh’ na kuacha kuongea.
Hamza mara baada ya kumwangalia mke wake namna alivyo aliona anazidi kuwa Cute asipokuwa siriasi.
Hamza alishindwa kujizuia na alinyoosha mkono na kushika nywele za Regina kwa kuzipapasa tartibu.
Regina upande wake alihisi aibu kiasi cha kumpelekea kumzuia Hamza na mkono.
“Acha kunishika , nywele zangu zina mafuta sijaziosha”
“Wife mwili wako muda wo te unanukia , ni kama una mfumo maalumu wa kutengeneza marashi”
“Unaongea nini wewe , nimegeuka na kuwa mmea?”
“Hahaha…Wife unaonaje nikiosha nywele zako leo?”Aliuliza.
“Wewe! Sitaki , mimi mwenyewe sipendelei kuosha nywele zangu mwenyewe maana hazitoki kama ninavyotaka”Aliongea na Hamza hakubisha.
Mara baada ya kufika hospitalini , walielekea moja kwa moja katika wodi Helena aliokuwepo.
Mara baada ya kuingia alikuwa ameamka licha ya kwamba alikuwa amekwekewa mabomba ya oksijeni puani.
Mara baada ya kumuona Regina na Hamza macho yake yalionekana kucheza kwa hisia.
“Helena unaendeleaje , Dokta kasema umevuka hali hatarishi”Aliongea Regina huku akiwa na tabasamu.
Helena aliishia kumwangalia Regina kwa sekunde na kisha akamwangalia Hamza.
“Sir Lucifer , kwanini uliniokoa?”Aliuliza na Hamza alimnyooshea Regina kidole.
“Usiniangalie mimi , ni mke wangu alietaka nikuokoe. Hivyo nilikufanyia upasuaji kwasababu aliomba na kama unataka kumshukuru basi fanya hivyo kwake”
Helena mara baada ya kusikia maelezo hayo alionekana kushangaa huku akionyesha mwonekno usio wa kawaida.
“Miss Regina kwanin.. nilitaka kukuua.. na ..”
“Ulitaka kuniua kwasababu ilikuwa ni jukumu lako kwasababu ulikubali kutii maagizo ya kiongozi wako, sijawahi kuwa na uadui wowote na wewe na siamini pia wewe ni mtu mbaya. Vinginevyo usingetumia muda wako kunielezea vitu vingi ambavyo sikuwa nikivijua wakati wa mkutano, hivyo ndio maana sikujali kukusaidua . Huna haja ya kuongea chochote na siwezi kukuomba shukrani. Maana licha ya kukusaidia najua bado ni mtiifu kwa kongozi wako”Aliongea Regina na kupozi kidogo.
“Ukweli tu ni kwamba niliguswa na uaminifu wako , hata kama ulitaka kuniua sina nia yoyote ndani yangu ya kutaka kukuchukia. Wewe ni mtu mzuri ambae ulijiunga na kumwamini mtu ambae si sahihi. Kama nafasi ipo, nipo tayari kuwa rafiki yako muda wowote”Aliendelea kuongea Regina.
Helena mara baada ya kusikia hivyo macho yake yaligeuka na kuwa mekundu , ndani ya koo alijihisi ni kama kuna kitu kilichoanza kumkaba wakati na kushindwa kulia. Aliishia kufumba macho yake na kuruhusu machozi kumtoka na kuloanisha mashavu yake.
Hamza upande wake alimwangalia Regina kwa sekunde na kisha aligeuza macho yake na kumwangalia Helena na alionekana kufikiria kitu.
“Helena utabakia hapa mpaka utakapo pona kabisa , sisi tunaondoka”
Wakati Hamza anataka kuondoka na Regina, Helena alionekana kuongea;
“Subirini kidogo ..”
Wawili hao walijikuta wakigeuka na kumwangalia .
“Unataka kuongea nini tena?” Ile wanauliza kilichotokea baada ya hapo kiliwashangaza , kwani Helena alichomoa mrija wa oksijeni na drip na kwa kuvumilia maumivu alishuka chini ya kitanda.
“Helena unafanya nini!!?” Regina alishituka.
Helena aliishia kupiga magoti chini kwenye sakafu huku akiendelea kutoa kilio cha kwikwi.
“Miss Regina . I am already someone who has died once. My life was given to me by you .. If you don’t mind , please take me away”Aliongea Helena akimaanisha kwamba yeye ni mtu ambae amekwisha kufa mara moja na uhai wake umerudishwa kwake na Regina na kama hatojali amchukue aondoke nae.
“Uhai wangu haupo tena chini ya Metal Tide , wala haupo chini ya taasisi yoyote ile . Kwanzia leo na kuendelea kama nitapata nafasi nataka kutumia sehemu ya maisha yangu yote yaliobaki kukutumikia!”Aliendelea kuongea.
Regina kusikia vile , alijikuta akiwa katika hali ya kupaniki na haraka sana alimsogelea Helena na kumsaidia ili asimame.
“Helena , usiwe hivi ,utasababisha kidonda kufunguka”Aliongea
Ukweli ni kwamba kama isingekuwa mafunzo ya nishati za mbingu na ardhi aliokuwa nayo , kidonda chake kingekuwa kishaachia muda mrefu.
“Madam! Upo tayari kunichukua niwe chini yako?”Aliongea Helena huku akiwa amemshikilia Regina mkono.
Regina aliishia kugeuza kichwa chake na kumwangalia Hamza na kisha akamgeukia Helena aliekuwa akimwangalia na macho yake ya kizungu ya kung’aa. Regina alionekana kama vile alikuwa akishindana na nafsi yake na baada ya sekunde kadhaa aliishia kutingisha kichwa.
“Sawa! Tutaondoka wote kwenda Tanzania na nitakuruhusu ujiunge na kampuni yangu , Sawa?”Aliongea Regina na Helena alitingisha kichwa mara kibao kwa furaha.
“Vizuri! Asante sana”
“Kwanzia sasa ndio unisikilize , hakikisha unapona kwanza vizuri mwili na roho. Vinginevyo siwezi kuwa na mfanyakazi mwenye mwili uliojaa majeraha”
“Usiwe na wasiwasi . Nitakuwa sawa , nitahakikisha napona haraka. Asante sana Ms Regina , Asante sana..”
Mara baada ya kupata malengo mapya ya kimaisha , Helena ambae alikuwa katika majonzi furaha ilimrejea.
Regina alimwachia Helena namna ya kuwasiliana nae na kuahidiana wangekutana nchini Tanzania baada ya kupona kwake , kwani yeye anatangulia kuondoka mapema.
Hamza alimchukua Regina na kumpeleka hadi kwenye gari na mara baada ya kuingia , hakuwasha kwanza na kuishia kutulia.
Regina mara baada ya kuona Hamza yupo kimya na haendeshi gari aliishia kuuliza.
“Unafanya nini? Nipeleke saluni basi nikaoshe nywele”
Hamza aliishia kumwangalia tu akiwa na mwonekano usioelezeka bila ya kuongea neno . Regina kuona hivyo alianza kujisikia vibaya.
“Una matatizo gani wewe? Kwanini unaniagalia tu bila ya kuongea..”
Hamza aliishia kuvuta pumzi nyingi , huku akionekana kufikiria kwa sekunde kadha.
“Wewe.. nahisi ulitegemea Helena angefanya vile?”
“Ulitegemea nini? Kwani Helena nini amefanya?”
“Mwanzoni nilifikiri ulimuokoa kwasababu ya kuwa na roho nzuri na ulimuonea huruma kwa uaminifu wake . Lakini sasa hivi nimegundua kupitia yale maneno yako , ulivyosema amesalitiwa na watu wengi ulimaanisha wewe pekee ndio tumaini lake …”
Regina mara baada ya kusikia maneno hayo mwonekano wake ulibadilika. Ghafla tu ule pole aliokuwa nao tokea asubuhi ulipotea na alirudi katika hali yake ya kawaida ya ukauzu.
Hamza hakujali na aliishia kugeuza macho yake na kumwangalia Regina usoni kwa umakini mkubwa.
“Niambie mke wangu. Ulipanga kumuajiri Helena tokea mwanzo ndio maana ulitaka nimuokoe?”
Mara baada ya swali hio , hali ya hewa ndani ya gari ilibadilika na kuwa ya ubaridiii huku anga likiwa zito.
“Kuna utofauti kwani?” Aliongea Regina kikauzu.
“Unamaanisha nini?”
“Haijalishi nimefanya kwa roho nzuri au vipi. Ndio nilitaka awe chini yangu tokea mwanzo lakini kuhitaji kwangu angalau kumemfanya kuwa hai. Isitoshe anakwenda kuanza maisha mapya , hilo si ndio jambo zuri kwake?”Aliongea Regina.
“Ndio , kila kitu kimekuwa sawa …. Lakini kama ulifikiria tokea mwanzo kwamba kumuokoa Helena itatosha kumfanya akufuate wewe na kukutumikia kwa moyo wake wote , basi niseme tu mke wangu kweli wewe ni mke mjinga”
“Kwahio kama nimegeuka mjinga kweli ndio hunitaki tena au? Do you dislike me?, Do you think I am a b*tch? Na mtu mnafiki?”Aliongea kiswanglish.
“Sijamaanisha hivyo ..”Hamza hisia zake zilikuwa zikicheza cheza kwa kubadilika mno na alijitahidi kufosi tabasamu.
“Ila nahisi tu … ninachomaanisha ni kwamba ni kama sikujui vizuri bado.”Aliendelea
Hamza aliishia kukumbuka mwanamke aliekuwa akipiga mswaki mbele yake na kuosha uso wake alivyokuwa mrembo asubuhi na huyo wa sasa, mwanamke kauzu ambae anamfanya kuwa ngumu kwake kujua anawaza nini , moyo wake ulikuwa katika mgogoro wa kujua ni yupi moyo wake unapaswa kumpokea au apokee wote wawili.
“Kama unahisi mimi sio mwanamke unaehitaji , muda wa kufanya maamuzi unao . Hutujatangazia watu uhusiano wetu na hatujafanya harusi , hivyo una nafasi ya kuchagua..”Aliongea Regina.
“Tuyaache hayo mke wangu , kwa vyovyote vile siwezi kukuchukia kwasababu hii , ni kwamba tu..”
“Ni kwamba nini?”
Hamza alijikuta akibakia kuwa kimya akishindwa kujua namna ya kuelezea.
“Ngoija nikupeleke saluni kwanza ukaoshe nywele”
“Haina haja”Bila ya kusubiria Hamza kuongea, aliendelea ; “Nilishaiona saluni ilipo muda mrefu pale karibu tu” Mara baada ya kuongea hivyo , palepale alifungua mlango wa gari na kutoka nje.
Hamza alijikuta akifungua mlango na kutoka nje na kweli aliweza kuona saluni iliokuwa upande wa kulia mkabala na hospitali. Muda huo Hamza alijiuliza inamaana Regina alikuwa akimwigizia kuwa mjinga hajui saluni ilipo ili ampeleke?.
Muda ule ni kama Regina alikuwa akijua Hamza alikuwa akifikiria nini nyuma yake , hivyo aligeuka na kumwangalia.
“Mimi sio wewe , sina nguvu za kutosha wala sina spidi kama yako , sina kundi la marafiki wanaoweza kunisaidia muda wowote kama wewe. Ninachotaka ni kulinda biashara zangu. Na ili kulinda kampuni yang kitu pekee ninachoweza kufanya ni kusimama mwenyewe . Kama unadhani mimi ni tofauti na mwanamke mjinga na mshamba ambae ulikuwa ukimuota na kama unaona nilikuwa nikikudanganya kwanzia mwanzo mpaka sasa endelea kufikiria hivyo hivyo. Sitaki kuelezea kile ninachofanya kwasababu mimi ni mimi na namna utakavyonifikiria hio ni juu yako. Unaweza kuondoka nikimaliza kuosha nywele zangu nitaondoka mwenyewe” Mara baada ya kuongea hivyo , Regina alivuka barabara na kusogelea Saluni iliokuwa wazi na bila kuangalia nyuma aliingia ndani.
Hamza aliishia kusimama eneo moja akiwa amekodoa macho , mara baada ya dakika kumi kupita aliishia kutoa sigara na kuiwasha na kuegamia boneti ya gari huku akivuta moshi taratibu na kuendelea kutafakari kuanzia siku aliokutana na Regina mpaka muda huo. Katika mawazo yake aliweza kugundua kulikuwa na vicheko , huzuni , utamu na migogoro . Bila kujua dakika arobaini zilipita na hatimae macho yake yalionekana kupata mwanga.
“Bado tu hujaondoka?”
Hamza mara baada ya kusikia sauti hio aliishia kugeuza kichwa chake na kumwangalia Regina ambae alishamaliza kuosha nywele.
Moja ya kitu kingine ambacho Regina alibarikiwa ni nywele , ni nywele ambazo alirithi kutoka kwa bibi yake. Zilikuwa nyeusi tii na zilizopigwa pasi na kunyooka haswa. Ilionekana hio saluni ilijua nini inafanya.
Hamza mara baada ya kuangaliwa na macho ya kirembo , alihisi moyo wake ni kama unachomwa na visindano.
“Hio staili ya nywele imekukaa vyema sana , aliekutengeneza amekuwezea, unafanana kabisa na mwanamke alieolewa”Aliongea lakini Regina mwonekano wake ulikuwa uleule.
“Kwanini tu hujaondoka?”
“Sijaondoka kwasababu nilikuwa nikikusubiri. Mke wangu kipenzi ingia kwenye gari tuondoke”
“Kwanini umenisubiri, si unanichukia?”
“Mke wangu ni saa ngapi nimesema nakuchukia?”
“Kwahio hunichukii kwa namna nilivyokufanyia , nimekuigizia mbele yako kwa kujifanyisha kuwa m’cute, nimejifanya kuwa mkarimu na mengineyo. Yote hayo nimefanya kwa ajili ya faida yangu na bado unataka kuendelea kuniamini ?”
Hamza aliishia kuvuta pumzi nyingi na kuzishusha kisha alimwangalia mwanamke huyo usoni kwa sekunde kadhaa na kisha alitingisha kichwa.
“Nakuamini”
“Nini.. Kwanini?”
“Its very simple. Because I love you”.
Comments