SEHEMU YA 212.
On Fire.
Hamza alishangaa mno kuona mchawi ambae alikuwa akishambuliana nae kupitia maskeletoni ni Skelidon Magus ambae alikaa nae jukwaa moja la magwiji wakati wa vikao.
“Imekuwaje..! Bro si tulimuacha ukumbini?”Aliuliza Roda kwa mshangao.
Hamza pia alikuwa katika mshangao mkubwa na hakuacha kuhisia , suala hilo linazidi kuchukua sura mpya.
“Haha.. haha..khoo..” Mr Skeleton alitoa kicheko kilichoambatana na kikohozi, “Lucifer mwili wako una nguvu mno , yaani unao uwezo wa kuruka umbali mrefu hivi bila ya kutumia nishati yoyote. Ni kwa bahati mbaya tu siwezi kuwaruhusu muondoke sasa hivi na kuvujisha taarifa”
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Hamza kusikia Skelidoni au Skeletpni akifungua mdomo na kuongea. Tokea aingie kwenye ukumbi ile jana hakuongea neno hata moja.
Hamza pale mara baada ya kuwaza ni kama akili yake iliingiwa na wazo lingine na kumfanya kukunja sura.
“Wewe..! Sio wewe uliekuwepo ukumbini bali ni..”
”Naona umegundua!”Aliongea huku akiendelea kucheka, “Yule sio mimi tokea mwanzo , ni lijimfupa linaloitikia wito wangu”
“Mr Skeletoni wewe ni moja ya Magwiji kumi wa dunia, kwanini unashirikiana na Sinagogu! Au wewe ndio wanaekuita Devasi , mfalme na kuhani wa Sinagogu, una uhusiano na makanisa ya Wabrazili?”Aliongea Hamza.
“Una maswali mengi sana na hakuna haja ya mimi kuyajibu. Wewe na huyo mwanamke mnapaswa kukaa na mimi hapa kwa muda”
Mara baada ya kuongea hivyo aliinua kile kitu alichoshikilia mkononi na mfoko wa nguvu ya kifo uliongezeka na kuwavaa Hamza na Black Fog.
“Msisimko wa kifo!”Aliongea
Hamza mara baada ya kuona vile , haraka sana alimkumbatia Black Fog na kukwepa shambulizi lile kwa kusogea pembeni.
Spidi ya Black Fog ilikuwa ndogo kuweza kuhimili nguvu ya Msisimko wa kifo.
“Bro usiwe na wasiwasi juu yangu , ukiendelea hivi utamshindwa, nitajilinda mwenyewe”Aliongea Black Fog.
Lakini Hamza hakutaka kuchukulia suala hilo kiwepesi. Na palepale aliruka mara mbili na kwenda kutua juu ya paa la kanisa na kumtua chini Rhoda.
“Wewe kaa hapa kwanza, ndio namna pekee ya kuwaeupuka wale maskeletoni na pia kuepuka uchawi wake”Aliongea Hamza.
Muda ule ndio sasa alijua Hamza amemleta hapo kwa ajili ya kuwa salama, hivyo haraka sana alitingisha kichwa.
Hamza mara baada ya kuachana na msichana huyo . aliruka kurudi chini. Alijua kama hatoweza kumshinda Skelleton , hata kama anao uwezo wa kukimbia , Black Fog anaweza asifanikiwe kuondoka akiwa hai . Hivyo njia pekee ilikuwa ni kupambana.
Hamza alijiambia ni kheri bwana huyo angekuwa mchawi wa kawaida kama wa Wican , lakini alikuwa katika daraja la kuongea na wafu hivyo ni hatari sana kushindana na msisimko wa kifo anao toa.
Hamza alitumia spidi kubwa kukimbia na kukusanya hewa nyingi kumzunguka na staili ile ilimsaidia kusukumia mbali ile nishati ya kifo na kumsogelea Skeletoni kwa spidi na kulenga kichwa chake na ngumi.
“Mfupa ngao!!”
Skelitoni palepale aliita mfupa uliobeba nguvu nyingi ya kichawi na kujikinga na Hamza.
“Bam!”
Hamza alijikuta akipambana na wimbi kubwa la nguvu ya kichawi lililokuwa kama ngao na ile analisambaratisha kwa ngumi yake aligundua Skelitoni alishaondoka aliposimama na kuelea angani kama pepo kwa kurudi nyuma nyuma. Muda ule yale maskeletoni walioyaacha mwanzo nyuma yalimsogelea Hamza kwa spidi huku yakionekana kuungua kwa moto usiokuwa wa kawaida.
“Miale ya kuzimu!”Aliongea Skelidoni
Hamza mara baada ya kusikia vile na kuona , aliishia kukunja ngumi huku akisaga meno yake na kwa spidi kubwa alianza kuyasambaratishya yale maskeletoni na ngumi na mateke.
Mara baada ya kushambulia kama mara nane hivi aliyamaliza. Lakini kitu kingine alichogundua ule moto uliokuwa ukiwaka katika miili yao haukuwa na joto na badala yake ulikuwa na hali flani ya ubaridi isiokuwa ya kawaida ambayo ni kama ilikuwa ikizuia mzunguko wa damu.
Hamza mara baada ya kuguswa na moto ule mikono yake ilijihisi ni kama imekufa ganzi , lakini hata hivyo hakukuwa na madhara makubwa.
“Unao uwezo wa kuhimili miale yangu!?”
Hamza hakuwa na muda wa kuongea nae. Aliamua kutumia faida ya spidi yake na kumsogelea Mr Skelletoni kwa spidi na kisha alirusha ngumi kulenga kichwa chake . Hata hivyo ghafla tu nyoka alichomoza katika kofia(hood) na kutaka kumng’ata Hamza.
“Hiss .. Hiss!!”
Kwa kuangalia tu nyoka hio na rangi yake , ilikuwa ni rahisi kujua ni kwa namna gani ilikuwa na sumu kali.Ilikuwa ni nyoka jamii ya Viper.
Ilikuwa ni kwa bahati nzuri , Hamza spidi yake ni kubwa kuliko mtu wa kawaida , hivyo aliweza kukwepa shambulizi lile la nyoka kwa kuondoa mkono wake.
Nyoka yule mara baada ya kufeli , alijificha ndani ya ukaya(hood) na kupotea.
Hamza kuangalia ukubwa wa koti hilo kama joho alilovalia alijiuliza kutakuwa kweli na nyoka mmoja au kuna wengi zaidi. Hamza aliona anapaswa kuwa makini maana kuna uwezekano kuna siraha nyingine alizoficha.
“Hehehehe… . hatari sana , hatari sana ila kwa bahati nzuri kipenzi changu aliwahi kushituka . Lucifer spidi na nguvu zako ni kubwa mno. Ndio maana umeweza kumuuwa Gonzalez kikatili”
“Acha maneno yako ya kimitego , najua uwezo wako sio huu unaonyesha”Aliuongea Hamza mara baada ya kuona ni kama bwana huyo hakuwa akitaka kutumia mbinu zake zote.
“Wewe na mimi tunapaswa kutumia uwezo wetu wote ili mshindi kupatikana lakini tutahitaji muda mwingi sana na kwa bahati mbaya sina muda wa kupambana na wewe mpaka mshindi apatikane”
Muda ule ghafla Black Fog aliekuwa amesimama juu ya paa la kanisa alianza kupiga makelele.
“Bro hatari ! Angalia upande wa makaburini”
Hamza alijikuta akigeuka haraka sana na kuangalia upande wa makaburini na eneo la katikati katika moja ya kaburi kubwa palionekana kuzingirwa na kiwingu kikubwa cha moshi kilichoambatana na msisimko wa kifo.
Aura iliokuwa ikitokea katika eneo lile na hisia zake , ilikuwa ni dhahiri kuna roho nyingi za wafu zimeitwa.
Palepale ghafla tu maskeletoni na watu wenye miili iliooza walianza kuibukia kutoka chini. Walikuwa wamebeba kiwango kikubwa cha roho ya umauti na kufanya kuogopesha mno.
Kwa namna maskeletoni yale yalivyoibukia katika eneo moja , Hamza alijua fika lazima yatakuwa yamefikishwa hapo na watu kwa ajili ya Skellidon kuyaamsha kwa kuyafukia na mchanga mwepesi.
Kwa haraka haraka maskeletoni hayo pamoja na maiti, idadi yao ilifikia angalau miatatu au mianne hivi.
Ile kauli ya mtu mmoja jeshi , hatimae uwezo wa Mr Skelliton wote ulianza kuonekana.
“Haha.. hahaha..” Skelidoni alitoa kicheko cha nguvu cha uovu huku akiinua kile kifaa chake alichoshikilia mkononi na kuanza kuelea kama vile anapeperushwa na upepo kurudi nyuma.
Muda ule wingu la rangi ya kijivu lilianza kusambaa na kuyafunika yale maskeletoni na miili ya wafu.
“Fanaka isiokoma!!”
Mara baada ya Skelliton kuongea vile , ghafla tu kile kiwingu kilianza kuvamia yale maskeletoni na kuyafanya yaanze kuchangamka kama vile yameguswa na nyaya za umeme.
Mara baada ya kutulia na kupata nguvu za kusimama vizuri ghafla yale matundu ya macho katika eneo la fuvu yalijaa miale ya kimizimu na kugeuka na kumwangalia Hamza.
Maskeletoni yale ya mwanzo hayakuwa na nguvu kama hio , hayo ya muda huo yalikuwa sio ya kawaida kabisa na mpaka mtu kuweza kuyatawala yakiwa mengi hivyo maana yake uwezo wake ni mkubwa mno.
“Go! My undead army!”
Skellidon mara baada ya kuinua kile kifaa mkononi mwake juu angani, palepale yale maskeletoni yalianza kutimua kuelekea upande mmoja, huku ikisikika sauti ya ajabu ya kibundi bundi , ilikuwa ni ngurumo ya ajabu mno.
Muda ule Hamza alijua Maskeletoni hayo yalilengwa kumshambulia yeye , lakini kilichotokea ilikuwa ni tofauti kabisa , kwani yalichukua uelekeo mwingine, na Hamza mara baada ya kupima uelekeo wake, aliweza kugundua ni upande wa Baraza la maksi linakofanyikia.
Hamza alijikuta kichwa chake kikimuwasha na kujiuliza isije ikawa huyo mshenzi anapanga kwenda kuua kila mtu ndani ya ukumbi.
Ijapokuwa kwa Magwiji isingekuwa hatari na kwa baadhi ya wanajeshi wenyewe uwezo , lakini kwa baadhi ya wanachama ambao hawakuwa na mafunzo ingekuwa hatari sana.
Hamza alijiambia kama Nyakasura angekuwepo hapo, pengine ingekuwa rahisi kuweza kuzuia maiti hizo zisiondoke katika hilo eneo kwa moto wake lakini Hamza uwezo wake haukumruhusu kushambulia maskeletoni mengi namna hio .
Kitu pekee ambacho aliona anaweza kufanya ni kurudi haraka na kwenda kuwataarifu wengine juu ya balaa linalokuja . lakini Skelidoni ndio huyo hakutaka kumpatia nafasi ya kuondoka.
“Lucifer nimekuchanganya!”
Skellitoni aliongea huku akicheka vibaya na palepale alituma tena wimbi la kifo kuelekea kwa Hamza.
Hamza kukwepa shambulizi lile ilibidi aruke juu na kwenda kutua kwenye ukuta wa kanisa na kisha akapiga sarakasi na kupiga mbizi kurudi chini kumsogelea Skelitoni.
Hata hivyo Mr Skelitoni hakuwa mzembe pia juu ya spidi yake . Mara baada ya kuona Hamza anamsogelea kumshambulia kwa mara nyingine alipeperuka na kurudi nyuma.
Hamza aliishia kutua chini huku akijizuia na mkono mmoja kwa kushika chini na kisha aliruka tena na kumsogelea Skelleton kwa spidi.
Ingawa Skelitoni hakuwa na spidi kama Hamza , lakini alikuwa na mbinu nyingi za kujilinda.
Mara baada ya kumuona Hamza anamsogelea aliita mkuki kama reki na kumrushia Hamza kwa spidi kubwa.
Hamza aliishia kusambaratisha mfupa ule hewani kabla ya kumfikia na kushidwa kumshambulia kwa mara nyingine.
“Kubali kushindwa Lucifer , huwezi kushindana na mimi , hata kama uwezo wako umeongezeka kuliko ulivyokuwa miaka mitano iliopita. Mbinu unayojifunza ni kwa ajili ya kufufua asili ya mwili pekee. Watu wa nyama kama wewe mbele yangu hamfurukuti .. hahaha.. hahaha”Skeletoni alicheka kwa nguvu.
Hamza alijawa na ukauzu mwingi usoni , ijapokuwa hakutaka kukubali lakini bwana huyo aligusa penyewe.
Kama ingekuwa ni miaka iliopita , akiwa na nishati ya mbingu na maji ya uhai pamoja na mbinu nyingine za mapigano , ingekuwa rahisi kushindana nae. Kwasababu muda huo ni sawa na kuingia katika vita ya kiroho na mwili wa kawaida, jambo ambalo ni ngumu mno kushinda.
Mfano Hamza angekuywa na nishati ya mbingu na ardhi ya ufunuo wa maji , ambacho angefanya ni kuzingira eneo hilo na nguvu ya nishati yake na kutengeneza uzio ambao usingeruhusu maskeletoni kupita.
Sasa muda huo mafunzo ya Hamza yalikuwa ni ya nyama kwa nyama na alitegemea zaidi kufanya mafunzo makali , uvumilivu wa juu , spidi na sifa nyingine ili kuboresheka. Lakini hata hivyo mbinu yake ilihitaji mshindani ambae ni kama Gonzalez na sio yule anaetumia nguvu za kiroho.
Skellitoni hakupambana nae ana kwa ana na badala yake alitupia tu uchawi kufanya mashambulizi hivyo na kufanya mbinu za Hamza katika kushambulia kukosa nguvu.
Ilikuwa ni rahisi kupambana na Nyakasura , kwasababu Nyakasura mapigo yake ni yale yanayoonekana ambayo yalihitaji ukaribu zaidi wa kimwili ili kufanikiwa. Lakini sasa muda huo amekutana na Skellitoni ambae ni mchawi mkubwa , asingepigana kwa kusogeleana nae zaidi ya kushambulia kichawi kwa mbali na kumfanya kutokuwa na uwezo wa kumfikia.
“Kama nikiendelea hivi , hata kama sitokufa lakini nitachoka mno kiasi cha kufa”Aliongea Hamza katika moyo wake.
Eneo hilo lilikuwa la makaburi na kwa mtu kama Skeletoni ambae nguvu zake zilitegemea zaidi nguvu ya roho za umauti , angeweza kuhimili kupambana hata kwa siku kumi mfululizo lakini sio kwa Hamza. Japo ni kweli Hamza hakuathiriwa na uchawi huo wa kifo lakini hakuwa na uhakika kama anaweza kuhimili kwa muda mrefu.
Shida haikuwa kuvumilia na kupambana kwa muda mrefu , jambo lingine abalo lilikuwa likimpa wasiwasi ni juu ya mke wake Regina. Alikuwa akitaka pia kumlinda na yupo mbali,uwezo wa kukimbia kumfuata Regina alikuwa nao lakini asingeweza kumuacha Black Fog peke yake.
Muda ule Skelleton alitoa shambulizi lingine la nguvu za kichawi kumlenga Hamza.
“Shimo la Umauti!”
Kiasi kikubwa cha msisimko wa nishati ya kifo kilimzunguka Hamza. Wakati huo huo mifupa ya yale maskeletoni yaliokwisha kuharibika ardhini yaliinuka kama vile yanapeperushwa na upepo na kumvaa.
Hamza aliishia kukwepa kwa kwenda mbele na kurudi nyuma kwa ustadi wa hali ya juu lakini kwa wakati mmoja nafsi yake ikizidi kuathiriwa na roho ya umauti .
“Miale ya kuzimu!”
Skeletoni kwa mara nyingine aliona achukulie nafasi kuhangaika kwa Hamza na kuamsha maskeletoni yaliobakia yakiwa na moto ule wa baridi kumsogelea Hamza na kumgonga.
Hamza bila ya kupenda alijikuta akivuta hewa nyingi ya umauti na kwa wakati mmoja akiathiriwa na ubaridi wa miale ile ya kuzimu. Alianza kuhisi nafsi yake ikianza kujitawala nje ya hiari na kufanya mwili wake kumshinda.
Black Fog aliekuwa amesimama juu ya kanisa , ingawa aliweza kuona wapo wanajeshi wengi wa umauti ambao angeshindana nao , kumuona Hamza akiwa amezingirwa pande zote na maskeletoni yale . Alishindwa kujizuia na kujawa na wasiwasi mkubwa.
“Bro kimbia! Kimbia tu na usijali kuhusu mimi”
Makelele hayo ni kama yalimkumbusha Skeletoni kuna mtu mwingine ndani ya eneo hilo.
“Lucifer, nitamuua yule msichana kwanza na kisha nitapigana na wewe kisawa sawa”Aliongea na kisha palepale alitoa sonyo lililoambatana na tabasamu la ukatili.
Mara baada ya kugeuka alirusha, mfupa ulionekana kama wa paja la mtu kuelekea kwa Rhoda.
Black Fog alikuwa mwepesi mno na sarakasi moja tu aliweza kukwepa mfupa ule kwa namna ya kipekee , lakini hata hivyo Skelletoni alikuwa ametarajia jambo hilo , hivyo alisukumizia wimbi la upepo wa nishati ya kifo.
Kuhusu wimbi hilo lilikuwa ni kama upepo wa kawaida tu , hivyo ilikuwa ngumu kwa Black Fog kukwepa.
Mara baada ya kuona Black Fog anakwenda kumezwa na upepo ule wa kisulisuli wenye nguvu ya umauti . Hamza aliruka haraka sana na kumpiga Black Fog kikumbo na kumrushia mbali.
Black Fog aliishia kudondoka kutoka juu ya kanisa , lakini haikiwa tatizo kwake , ila sasa ile anageuka na kumuangalia Hamza . Aliweza kumuona akikakamaza misuli akishindana na nguvu ile ya uchawi wa kifo .
Hamza alivuta pumzi kwa shida , alihisi mapafu yake ni kama yanashindwa kupanuka na kuingiza hewa , huku ule uchawi wa kifo ukipelekea hali ya kulegea kwa viungo vyake vya ndani.
“Bto kwanini umeniokoa na kujiingiza kwenye matatizo”
Black Fog alishindwa kuvumilia na kupiga sarakasi mbili na kumsogelea Hamza huku machozi yakiwa yamemvaa.
“Usinisogelee! Kaa nyuma yangu” Hamza licha ya kuwa katika hali mbaya alijikamamaza na kumkemea Black Fog.
“Ni makosa yangu , kama sio mimi usingeumia.”
Kinadharia , ingawa Hamza alikuwa na wakati mgumu kushindana na Skeletoni , kama angeamua kuondoka , Skeletoni hata kwa uwezo wake asingeweza kumzuia. Lakini kwasababu yake Hamza alikosa jinsi na kupambana nae ili kumlinda na kuzidi kumpelekea kuwa na wakati mgumu kuweka umakini kwenye kupigana.
“Lucifer , hakika umenishangaza! Ni mbinu gani unajifunza mpaka kuweza kuhimili nguvu yangu kubwa ya wimbi la umauti na kuendelea kuishi?.. haha unanipa hamasa ya kutaka kukuua na kukugeuza mwanajeshi wangu , nina uhakika utanifanyia kazi kubwa kuongoza waumini wangu duniani kote”
“Bado hatujafikia mwisho wa pambano ushaanza kufikiria mbali?”
“Oh! Kwahio bado unafikiria kupambana na mimi?”
Hamza hakujisumbua kujibishana nae , aliona kama hali itaendelea kama hivyo atachoka mpaka kufa.
“Mgawanyiko!!
Hamza ghafla tu alisimama wima na kutoa sauti kwa nguvu na kwa mara nyingine aliamua kutumia mbinu ya mgawanyiko.
Ingawa Hamza alitumia mbinu hio ya mgawanyiko jana yake tu , ila hakuhisi shida yoyote, ukiachana na kwamba nguvu zake za mwili zilipungua , lakini hakuhisi tofauti yoyote mbaya.
Hivyo Hamza hakujali sana kuitumia tena, ukweli ni kwamba hakujua kuhusu madhara ya mbinu hio ni nini kwasababu ilikuwa ni nusu tu, lakini alitaka kuitumia kumdhibiti Mchawi wa misitu ya Amazoni.
Seli zote za mwili zilijikusanya na kukaa pande kwa ajili ya kupambana na sumu ya kifo iliokuwa ndani ya mwili wake.
Hamza mara baada ya kutumia mbinu hio , alihisi mwili wake ni kama unajitengeneza upya. Na kwa mara nyingine alijihisi kuwa ni mwenye bahati kuja kukutana na Yonesi na kumpatia mbinu hio.
“Asante sana Yonesi!”
Hamza aliongea katika moyo wake , hakutaka kusahau kwamba yote hayo ni Yonesi alieyawezesha na kuna muda alihisi pengine kukutana kwao si kwa bahati mbaya.
Kwa namna yoyote Hamza hakutaka kufia hapo , alipanga kumrudia mke wake na kumalizana na masuala ya Ufaransa na kurudi nyumbani.
Black Fog alijua ni muda wa Hamza kuanzisha mapigano kisawa sawa , hivyo hakutaka kuwa mzigo tena na kujificha nyuma yake.
Mr Maskeletoni alionekana kuwa makini kuliko mwanzo , aliita wimbi kubwa la upepo wa kifo wa kisulisuli na kumzingira huku kwa wakati mmoja akitumia mifupa mingi kama ngao yake.
“Njoo , Lucifer ni muda wa kuona una nguvu kiasi gani mpaka ukaweza kumuua Goliati wa Chuma , Gonzalez”Aliongea
Hamza hakuongea neno . Aliruka na kwenda kukaa usawa wa Mr Maskeletoni na muda ule wakati anasogea ni kama alianza taratibu na ghafla tu alipotea
“Bang! , Bang! , Bang!”
Mifupa mitatu ya ulinzi iliokuwa ikizunguka hewani kama kinga, ilisambaratishwa na nguvu za kinyama za Hamza .
Mr Maskeletoni , alionekana kuogopa.Hakutegemea baada ya Hamza kuchukua sura mpya angeweza kuwa na uwezo mara mbili yake.Ile anataka kujipeperusha kurudi nyuma , Hamza huyu hapa mbele yake.
Hamza macho yake yalionekana kama vile yanaungua na moto, na mwili wake uliokuwa na nguvu zaidi ya mara mbili ulifyatua ngumi nzito katika ukaribu mkubwa zaidi.
“Kufa!”
Hamza ngumi yake ilichomoza , ile nyoka ndani ya ukaya , haikuwa hata na muda wa kujichomoza tena kumng’ata Hamza , kwani ngumi ilikuwa ishawasili tayari.
“Bam!’
Hakukuwa na damu yoyote , Hamza alijihisi ni kama mkono wake umepigana na fuvu tu.
Muda ule akishangaa , ghafla tu mwili wa Mr Maskeletoni ulitoa mvuke na kujaribu kumvaa Hamza. Sio mvuke tu , nyoka wa rangi tofauti tofauti pia walichomoza kutaka kumng’ata.
Hamza mkono wake ni kama radi kwani kupitisha tu aliua nusu ya wale nyoka, huku kwa wakati mmoja akirudi nyuma na kukwepa minyororo ile ya roho ya kimauti.
Kilichomshangaza Hamza ni kwamba Mr maskeletoni mwenyewe alionekana kuwa limfupa tupu lisilo na nyama ambalo amelifunika na koti . Skeletoni lenyewe liliharibika na ni nusu yake tu ndio lilibakia baada ya kulitia ngumi.
Lakini sasa ile nguvu ya kifo iliokuwa imemzingira ilikusanya ile mifupa na kujirudisha tena na fuvu lake lilijirudisha katika hali ya kawaida.
“Shenzii! , wewe ni kitu gani?”
Hamza alishindwa kujizuia na kuishia kulaani , katika maisha yake alipigana na maadui wengi sana na washindani wa kila aina , pamoja na vita vingi. Lakini hakuwahi kushuhudia fuvu likijirudisha upya baada ya kuchanguliwa.
“Unafikiri wanaosema mimi ni wa milele na Mchawi wa Maskeletoni wanadanganya?. Mimi Skeletoni ni nafsi ya umilele , hata kama uharibu skeletoni langu naweza kuvaa lingine tu na kuzaliwa upya”
“Bullshit , wewe sio Mungu ila ni mchawi tu . Ijapokuwa najua mwili wako ni wa skeletoni lakini kama siwezi kukuua kwa shambulizi moja , kama ni unakufa kwa mashambulizi mawili au hata mia moja nitafanya hivyo”
Hamza aliishia kung’ata meno yake kwa hasira , mwili wake uligeuka na kuwa kama mshale na kwa mara ya pili alimsogelea Mr Maskeletoni. Lakini awamu hio Mr Maskeletoni , alikuwa amejiandaa . Ingawa ilikuwa ngumu kukwepa shambulizi la Hamza kwa asilimia mia lakini aliweza kuita dhoruba ya umauti ndani ya wakati kujikinga.
“Tufani ya umauti!”
Mr Maskeletoni mwili wake ulizingirwa na kimbunga cha msisimko wa kifo , kwa umbali wa mita mia moja za mraba , mchanga na vitu vyote vilivyokuwa ardhini vilianza kupanda hewani kwa namna ya kuzunguka na kumzuia Hamza.Haikuwa hivyo tu , mifupa mingi ilimsogelea Hamza kwa kasi na kuanza kumshambulia.
Ingawa Hamza alikuwa na uwezo wa kuzuia mifupa hio , ilikuwa ngumu kumsogelea Mr Skeletoni pale alipo na kumshambulia tena kama mwanzo.
Mr Maskeletoni alijitengenezea kimbunga na kujjiweka kati na Hamza alipambana na kimbunga ili kumfikia katikati na kumshambulia na ngumi.Ilikuwa patashika ya kuvutana.
Comments