SEHEMU YA 213.
Katika eneo la kikao , mathalani ndani ya ukumbi ambao mkutano wa Baraza la maksi ulikuwa ukifanyika.
Ijapokuwa Hamza hakuwa amerudi bado ukumbini kwa muda mrefu , lakini vikao viliendelea kama kawaida.
Mambo mengi ya hapa na pale yanayohusiana na ulimwengu wa giza yalikuwa yakijadiliwa mpaka usiku wa kiza. Kwa washiriki wengine walijikuta wakiboreka , maana majadiliano hayo yalikuwa ni juu ya sheria mpya.
Lakini licha ya hivvo , hakuna ambae aliondoka mapema m kwasababu tukio la mwisho lilihusisha ufunguzi wa sanduku lililoachwa na mwanasayansi nguli Dokta Genesha kama alivyofahamika kwa jina lake la kawaida na Tembo wa Trishaza jina lake rasmi la ulimwengu wa Giza.
Magwiji wote waliokuwepo , macho yao yote na hamu zao zote zilikuwa ni kutaka kufahamu nini kipo ndani ya kiboksi hicho.
Tembo wa trishaza alipotea miaka miwili au mitatu iliopita na hivyo kudhaniwa kwake kufa haikuwa siri tena. Na kuhusu kilichopo ndani ya kiboksi hicho waliamini ndio urithi ambao ameuacha na pengine ikawa ni utafiti wake juu ya dawa ya kuzuia kifo.
Hatimae , baada ya saa nne za usiku kutimia , raisi wa Taasisi ya Maksi na wadumisha amani , Rais Paul Maxim alisimama juu ya jukwaa.
“Naamini kila mmoja wenu amekuwa akisubiri taarifa hii kwa muda mrefu , bila ya kuwasahau magwiji wetu kumi wa ulimwengu wa giza juu ya juktwaa. Asanteni sana kwa uvumilivu wenu”
“Hatua inayokujia tutafungua sandulu la Dokta Genesha na kuona ni kitu gani ametuachia kabla ya kupotea kwake”
Watu mara baada ya kusikia maelezo hayo ,shangwe nyingi zilisikika, ukiacha masuala ya kutangaza sheria mpya na mikakati ya kudumisha amani , suala ambalo lilisubiriwa na watu wengi kwa hamu , lilikuwa ni hilo.
Wafanyakazi kadhaa wa Set Society waliweza kuleta kiboksi cha chuma cha rangi nyeusi juu ya jukwaa.
Kisanduku hicho kilipaswa kufunguliwa kwa nywira , hakukuwa na ugumu mkubwa wa kufungua kama kutumia jicho ama kidole , bali ni herufi tu ndio zilipaswa kuingizwa
Mara baada ya kiboksi kile kuweka juu ya jukwaa katika meza maalumu , Rais Maxim , alisogea na kama kawaida yake na sauti kama ngurumo aliongea;
“Dokta Tembo mara baada ya kufika ofisini kwangu kunitembelea , alinikabidhi hiki kiboksi na kuniambia password zake . Kwa miaka yangu sitini ya uzoefu na hulka yangu , alikuwa na uhakika sitokifungua kabla ya muda. Na ni matumaini yangu kwenu wote mtaamini maneno yangu na kuona na mimi ni mara yangu ya kwanza kwenda kuona kilichopo ndani yake”
“Mzee Maxim , huna haja ya kujielezea , kila mtu anakuamini hapa”Aliongea Oleg Phantom.
“Ni kweli kabisa , kiongozi tabia yako ni kielelezo muhimu kwa kila mmoja ndani ya ulimwengu wetu”aliongea Silvia.
Watu wengi pamoja na taasisi mbalimbali hawakuwa na pingamizi na kuungana na wengine kumuamini Raisi Maxim.
Hakuaminika kwasababu ya cheo chake , bali ni kwasababu kwa muda mrefu amekuwa mtu mwenye busara sana na anaeongozwa na sheria ya uaminifu. Vinginevyo asingechaguliwa na kuwa raisi wa Set mbele ya watu wakubwa wenye nguvu kama hivyo.
“Asanteni sana kwa kuniamini , nitafungua kiboksi hiki sasa”
Aliongea na palepale chini ya macho ya maelfu ya watu aliingiza nywira zenye mkanganyiko mkubwa.
“Zii..! Ziiii!”
Hatimae kiboksi kilikubali zile nywira na Maxim alifungua mlango taratibu wa kiboksi kile.
Ndani ya kile kiboksi kulikuwa na nyaraka , hakukua na kitu kingine zaidi.
Maxim aliishia kutoa nyaraka ile , au bahasha na kuisoma pale juu kwa nguvu; “A, K , H . Hili ndio jina lililoandikwa hapa juu , jina la nyaraka” Aliongea na kuweka vizuri nyaraka ile ili kamera zipige na kuonyeshwa kwenye runinga watu waone.
Maelfu ya watu mara baada ya kuona kichwa cha nyaraka ile minong’ono iliibuka , kila mtu akionekana kuotea kitakuwa kitu gani.
Nusu ya wawakilishi waliokuwepo , pamoja na taasisi kubwa , walikuwa na uelewa kidogo juu ya dawa ya kifo na jina lake lilivyoitwa iliwafanya wawe na hali ya msisimko wa shauku katika macho yao.
“ANKH... Cross of Life… hivi ni kweli itakuwa ni taarifa za tafifi za Genesha juu ya dawa ya kifo?”Aliongea Oleg na kumfanya Silvie kumwangalia Mathias Huge wa jicho la Anga au Binamu.
“Master Huge isije ikawa kupitia jicho lenu la Anga , mlijua kilichomo ndani ya kiboksi ni Ankh !Ni kweli?”Aliuliza
“Samahani , siwezi kujibu swali lako”Aliongea Huge m hakuwa na hisia zozote katika sura yake, zaidi ya tabasamu hafifu.
“Unavyopenda kujikweza sasa , hata kama una teknolojia ya jicho la Anga huwezi kujua kila kitu. Kama mngekuwa na uwezo wa kuweza kumfuatlia mwanasayansi mwenye akili nyingi kama Dokta Genesha si mngeshamchukulia hatua tokea mwanzo?”Aliongea Mtakatifu Auland.
Auland kama kiongozi wa jamii ya siri ya wanajeshi wa zama za kale , maarufu kama Knight Templar au Dragon Knight, hajawahi kuwa na ukarimu wowote mbele ya watu wa Binamu. Kwasababu kazi yao kubwa ilikuwa ni kufuatilia mambo ya watu na kila wanapopata taarifa wanauza bila ya kujali hasara juu ya mwenye siri zake. Huge hakuongea neno zaidi ya kutingisha kichwa chake na tabasamu.
“Kama kweli kutakuwa na dawa ya kifo , binadamu ataingia katika nyakati mpya za kustaarabika”Aliongea Vampire Sebastian.
“Sebastian usiwe na wasiwasi , hata kama itokee kuwe na dawa ya kifo , binadamu hawatokuua. Isitoshe tunaweza kuwafanya wanyama wa maonyesho kwenye Zoo”Aliongea Mikaeli.
Kauli hio ilimfanya Sebastian kujawa na hasira na macho yake kuonyesha nia ya kimauaji lakini licha ya hivyo Mikaeli hakumuogopa na alimkazia macho vilevile.
Muda ule hatimae nyaraka ndani ya bahasha ilitolewa , na taarifa juu ya dawa ya kifo zilimulikwa. Muda huo magwiji wawili , yaani wa madhabahu ya Giza na ya Nuru walionekana kungurumiana.
Sababu ilikuwa nyepesi tu , kitu pekee ambacho Strigoi wanajivunia nacho ni kuishi miaka mingi. Strigoi waliamini siri ya ukuu wa binadamu imefungwa katika uchache wa miaka yake ya kuishi . Hivyo ikitokea binadamu akapata dawa ya kuvuka kiunzi na kurefusha umri wake maana yake kadri atakavyoishi ndio ataendelea kugundua nini kimejificha katika mwili wake na mwisho wa siku watakuwa na nguvu kubwa kuliko wao.
Wakati binadamu yeye akitafuta dawa ya kurefusha uhai , Strigoi wenyewe wanatafuta dawa ya kuurefusha uhai wao bila ya kulala muda mrefu.
Maana yake ni kwamba wakati binadamu wakijiendeleza , wao watakuwa wamelala pono ili kurefusha uhai na kipindi cha kulala kwao mpaka wanaamka binadamu watakuwa wamepiga hatua kubwa na kama ni hivyo maana yake ni kwamba kauli ya Mikaeli kuwageuza wanyama wa maonyesho kwenye Zoo inaweza kuwa na ukweli.
Hivyo kwa namna yoyote ile Madhabahu ya Giza hawawezi kuruhusu binadamu kupata dawa ya kuzuia kifo.
Mara baada ya kuona magwiji wawili wa madaraka makubwa tayari wapo on fire . Maxim aliona aongee kidogo ili kupoza hali.
“Tafadhari naombeni mtulize jazba! Nyie mnagombanaje bila ya kujua nini kipo ndani yake”Aliongea.
“Kama ni hivyo basi tunaomba raisi utufngulie hio nyaraka na kila mmoja kuona nini kipo ndani yake”Aliongea Prince Sebastiani , lakini moyoni alitamani nyaraka hio isifunguliwe.
“Rais Maxim huna haja ya kumsikiliza , hio ni zawadi aliotuachia Dokta Tembo kwanini turuhusu na mavampire kuangalia?”
“Mikaeli!!” Sebastiani alisimamama huku akiwa amefura mno, “Unadhani siwezi kukufanya chochote kwasababu tupo hapa?”
“Tatizo nini kwani mkubwa , mbona wasiwasi mwingi , mimi sijali kama utafanya lolote au utakaa na kutulia”Aliongea Mikaeli huku akishikilia mpini wa jambia.
“Nyie wawili , acheni basi hayo mnayofanya kwa ajili ya mimi mzee wenu. Madhabahu ya Nuru na Giza uwepo wenu ni muhimu sana kwa ulimwengu wetu na hata kwa ulimwengu wote . Kama vita ikitokea kwasababu ya hii nyaraka ambayo haijulikani kilichopo ndani ni nini , basi sidhani kuna manufaa ya kuionyesha”
“President , sio kama ni makusudi , lakini nyaraka hio pia ni muhimu sana kwetu Strigoi na ni matumaini yangu leo hii nitajua inahusiana na nini”Aliongea Sebastian.
“Nilijua tokea mwanzo kitu kisichotarajiwa kitatokea nikifungua hiki kiboksi , lakini Sebastiani nakuomba kwanza ukae chini. Hapa yapo mashirika mengi na wawakilishi wengi , kuhusu chochote kilichopo ndani ya hii nyraka tutakiangalia wote na kukaa chini kukijadili na kufikia maamuzi”
Sebastiani alisinyaza macho yake na kuangalia chini na ghaflat tu aliinua mkono juu na mwanga wa rangi nyekundu kama damu ulionekana katika ncha za vidole vyake , mwanga ule uliambatana na herufi za michoro kama runes hivi.
Ghafla tu vidole vile vilifyatua ule mwanga wa damu na kutengeneza kitu kama chupa la rangi nyekundu ambalo lilipaa angani na kutoka nje kabisa ya uwazi wa uwanja na kupasuka na kusambaza rangi za herufi angani.
“Sebastiani unafanya nini, ndio unatuma ishara kuwaita wenzako?”Aliuliza Mika.
“Kipi cha kushangaza , mimi pekee ndio strigoi hapa , sidhani kama ni ajabu kuita watu wa jamii yangu pia, au ni kosa?”
“Mh! Bado hata hajasoma nyaraka inasema nini , lakini ushaanza kuogopa vyote hivyo. Inaonekana ulichoweza ni kuishi miaka minigi tu lakini ujasiri wa kupambana mwenyewe huna” Mikaeli alikejeli.
Ilikuwa ni wazi kwamba Sebastiani alikuwa kama mwakilishi wa viumbe vyote vya giza na kama kweli binadamu wamepata dawa ya kuzuia kifo, maana yake wataweka uhai wao rehani na sio kwao wanywa damu pekee, bali mpaka kwa viumbe wengine wote wasionekana.
Baada ya kuona namna ambavyo watu hao wawili walivyochemka , magwiji wengine waliishia kubakia kimya , wakionyesha nia za kutokuingilia.
Maxim alijikuta akijutia kufungua kisanduku hicho , hata hivyo aliona kama asipokifungua siku hivo , basi angejiingiza katika matatizo ya kisanduku hicho kuibiwa kwa nguvu na pengine hata kuuliwa.
“Jamani , Muda huu nitawaita wanasayansi wetu wawakilishi kwa ajili ya kuangalia hii nyaraka inahusiana na nini na kisha tatawasikiliza kile watakachotuambia . Lazima tuweke misingi ya amani hapa”Aliongea Maxim.
Ile anamaliza sentesi yake , sauti za vilio zilianza kusikika kutoka nje na ghafla tu vilio hivyo vilipotea.
Malaika wa nuru ,Mikaeli ndie wa kwanza kushituka , huku akikunja sura na kuonyesha mshangao.
“Nahisi nguvu kubwa ya roho ya umauti”
Kauli yake ilifanya magwiji wengine wote kusimama na kuangaza kila kona.
Muda ule kundi kubwa la viumbe wafu , lilionekana likilazimisha kuingia ndani ya ukumbi huo. Viumbe hao walikuwa wakishambulia kila kilichokuwa mbele yao na kuua.
Walinzi na baadhi ya washiriki wenye uwezo mkubwa , walianza kupambana na maskeletoni yale , lakini ilikuwa ngumu kutokana na kwamba mengi yalikuwa na siraha aina ya mikuki mkononi , ilikuwa ngumu pia kuwaua na risasi kutokana na kukosa nyama, hivyo ilihitajika mapigano ya ana kwa ana na kufanya hali kuzidi kuwa ngumu.
Ghafla tu uwanja uliokuwa na ukubwa wa kutosha watu wengi uligeuka na kuwa chumba kisicho na nafasi, na msisimko wa kifo kila mtu dhaifu kiroho ulimwingia na nafsi kuanza kufurukuta na akili yake kuibiwa palepale na hata wengine kupoteza maisha kabla ya kuguswa.
“Nini kinaendelea , hawa viumbe wa wito wa kifo wametokea wapi?” Aliongea Oleg na haraka sana aligeukasna kumuangalia Mr Skeletoni
“Skeletoni , wewe ndio umewaita?”
“Captain , Skeletoni alikuwa na sisi muda wote , anawezaje kuwaita?”Aliuliza Silvia.
Skeletoni hakuongea chochote , alikuwa amesimama tu kama sananu.
“Sebastian , itakuwa ni wewe? Mbona mshenzi sana , yaani unatumia wafu kushambulia watu?”Aliongea Mikaeli huku akimnyooshea Sebastiani mkuki wake.
“Nadhani utakuwa na matatizo kwenye akili yako wewe , nimetuma ishara kuita watu wangu na hawajafika bado. Isitoshe sisi ni wa damu safi , hatuwezi kutumia mbinu chafu kama hii ya kichawi”
“Mhmh! Nyie ndio wamiliki wakubwa wa jamii ya wachawi duniani . Kama wewe hutumii uchawi haimanishi wenzako nao hawatumii”Aliongea Mikaeli.
Nyakasura mara baada ya kuona wawili hao wanagombana bila ya kufanya chochote alionekana kuchukia.
“Mnachukiza kweli! Tumalizaneni na hii dharula kwanza na ndio mwendeleze ugomvi wenu kama mnataka”
“Nyakasura yupo sahihi . Tunapaswa kwenda kuua hawa misukule kwanza”Aliongea Silvia.
“My fellow countrymen! Tafadhari naombeni msipaniki , tuna magwiji wataalamu hapa , tutafanya kazi pamoja kumzima adui yetu”Aliongea Maxim.
Kabla hata sauti yake haijapotea angani , Nyakasura alishachukua hatua na moto wake wa dhahabu kwenda kuyaadhibu yale maskeletoni.
“Haha… hayawi hayawi sasa yametokea yakukutokea , hebu na tufanye jambo na tusimuache huyu binti kujichosha mwenyewe”Aliongea Oleg na kujivingirisha kama jiwe kutoka jukwaani na kudondokea chini kama furushi.
Haraka sana Silvia na moto wake wa nuru alipaa kushuka jukwaani , Saint Auland na Huge wote waliungana na watu wao kusambaa kila kona na kutoa msaada.
Mikaeli na Sebastiani , waliishia kuangaliana kwa muda na wakaacha kupigana na kuungana na wengine.
Mara baada ya magwiji wote kushuka jukwaani kwa ajili ya kutoa msaada , Mr Skelletoni ambae amevalia kofia alitembea kuelekea njia ya kutokea. Watu mara baada ya kumuona akielekea uelekeo huo walijua anaenda kutoa msaada , hivyo hakuna aliemtilia shaka.
Watu wa Inferno , mara baada ya kuona jambo hilo , walipatwa na wasiwasi moyoni.
“Kuna mtu anapanga kuiba urithi alioacha Dokta Tembo?”Aliongea Berly.
“Nyie mpaka sasa hamuoni ajabu , kwanini bosi na Black Fog hawajarudi?”Aliongea Mameni.
“Bosi wetu atakuwa sawa , huu ni muda wa kuweka nguvu zetu kumlinda shemeji yetu asipatwe na shida yoyote na kumuondoa hili eneo”Aliongea Azzle.
Comments