Ulinzi kwa malkia.
Regina uso wake wa kirembo ulifubaa. Hakuwahi kuona uvamizi wa viumbe wa ajabu wa aina hio. Alishawahi kuangalia filamu za mazombi, lakini muda huo kiila kitu kilikuwa ni uhalisia.
“Hamza! Kwanini hajarudi mpaka sasa hivi, yupo sawa?”Aliuliza Regina akimwangalia Asmuntis kwa wasiwasi.
Moyo wake ulikuwa ukienda mbio mno , alikuwa na wasiwasi Hamza atakuwa kwenye matatizo.
“Shemeji wewe muamini tu bosi wetu . Uwezo wake sio wa kutilia shaka. Kwa sasa tutakuchukua kukutoa hapa”
“Barhams , listen! Protect the queen”Aliongea Azzle akiwaamrisha wanajeshi wake kumlinda malkia Regina.
Asmuntis na yeye alitoa maagizo kwa maninja wake kuua kila kiumbe kitakachomsogelea Malkia.
Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Regina kuwasikia wakimuita Malkia, yaani mke wa mfalme wa kuzimu.Lakini hata hivyo hakuwa na muda wa kufurahi wala kuona haya , kwasababu muda huo akili yake ilikuwa katika hali ya kupaniki. Alikuwa na wasiwasi zaidi juu ya usalama wa Hamza na nini kilichomtokea.
*****
Ukweli ni kwamba Hamza alikwisha kujua yale maskeletoni yalishafika muda mrefu. Vita yake na Mr Skelidoni ilichukua zaidi ya dakika kumi.
Kutokana na ukali wa vita yenyewe , nguvu kubwa zilikuwa zikitumika kila dakika inapopotea.
Hamza aliweza kuhisi kabisa , mbinu ya mgawanyiko ilikuwa ikinyonya sana nguvu yake ya mwili na spidi yake kidogo ilianza kushindwa kuendana na uhiari wa fahamu zake.
Skelidoni nguvu zake za kiroho zilikuwa zimeshuka kwa kiasi na uwezo wake wa kudhibiti wafu ulishuka pia.
Hamza alichokifanya ni kutegemea mbinu yake ya mgawanyiko , kudhibiti uchawi wa kifo ambao Skelidoni anamtupia , lakini baada ya muda alianza kuathirika.
Ilikuwa ni kwa bahati nzuri Skellidoni na yeye nguvu zilikuwa zikimwishia. Mara baada ya kutoa mikondo kadhaa ya roho ya umauti , alijipeperusha angani kusogelea eneo la makaburi katikati.
“Lucifer , kama unataka kuendeleza hili pambano na mimi njoo hapa kwenye makaburi”
Hamza hakuwa mjinga , alijua bwana huyo kukaa juu ya makaburi ni kwa ajili ya kutaka kunyonya nguvu kutoka kwa wafu ili kurudisha zile alizokwisha poteza.
Lakini Hamza hakua na mpango wa kuendeleza pambano , mpango wake tokea mwanzo haukuwa kumshinda Skelidoni bali ni kuondoka katika hilo eneo.
“Tuondoke”
Aliongea Hamza mara baada ya kuona Skellidoni hana nguavu za kutosha za kumzuia haraka sana alimshika Black Fog na kuondoka nae kwa kukimbia.
Licha ya gari waliokuja nayo kuharibika , lakini miguu yao haikuwa slow kwenye kukimbia. Black Fog alijua wanapaswa kuwahi , hivyo alijitahidi kuendana na spidi ya Hamza na kukimbia kwa kasi.
Mara baada ya kuona wanakimbia , Skellidoni aliekuwa akiogelea katika nishati ya umauti alitoa cheko kubwa.
Black Foig mara baada ya kumwangalia Hamza , aligundua alisharudi katika mwonekano wake baada ya kuacha kutumia mbinu ya Mgawanyiko , lakini alikuwa akitokwa na jasho mno na kuhema kwa nguvu.
“Bro upo sawa? Unaonekana kuchoka sana” Aliuliza Black Fog akiwa na wasiwasi.
“Usiwe na wasiwasi , tuharakishe tu kurudi”Aliongea Hamza , ukweli ni kwamba hio ni mara yake ya kwanza kutumia mbinu ya Mgawanyiko kwa muda mrefu na aliweza kuhisi uhatari wake.
Unachopaswa kujua ni kwamba nguvu za kimwili za Hamza hazikuwa za kawaida kabisa. Hamza alijihisi katika historia ya binadamu pengine hakuna binadamu ambae ana mwili wenye nguvu kama zake.
Lakini kutumia tu mbinu ya Mgawanyiko , ilimchukua dakika kumi tu kuchoka mno kama vile amefanya kazi ngumu kwa muda mrefu sana. Kama isingekuwa wasiwasi wake juu ya Regina na washikaji zake. Angekaa chini na kulala kidogo.
Alishindwa kuelewa juu ya mtu ambae alitengeneza mbinu ile , alijiuliza kama mbinu yenyewe inanyonya nguvu ya mwili kiasi hicho , malengo yake ilikuwa ni nini? Au ilitengenezwa kwa ajili ya binadamu wa tofauti na yeye.
Hamza alikuwa na wasiwasi , licha ya kwamba alikuwa akikimbia kurudi ukumbini lakini alihofia kama itatokea hali ya kumtaka kutumia nguvu zaidi , je ataweza? Kwa sababu muda huo alijihisi kuchoka mno.
Lakini kwa hali yoyote ile , Hamza aling’ata meno yake na kuvumilia na waliendelea kuzichanja mbunga kupita katikati ya msitu mpaka walipokuja kuona mwanga mbele yao.
*****
Ukumbi wa Baraza la maksi uligeuka na kuwa kuzimu . Njia zote za kuingilia zilikuwa zimezibwa na nguvu kubwa ya umauti na maiti za wanajeshi. Ilishindikana kwao kutoka ndani ya eneo hilo baada ya kuumizwa.
Maiti na Maskeletoni ambayo yalikuwa chini ya utawala wa kimashambulizi , haikuwa suala tu la kuwashambulia watu , bali walikuwa pia wamebeba virusi ambavyo vilikuwa vikisambaa kwa kasi hewani.
Kila ambae alihema na kuvuta virusi hivyo, hata wale wazima walibadilishwa akili zao na kuanza kushambulia wenzao.
Kwa hali ya kusikitisha ndani ya muda mfupi tu asilimia kubwa ya watu wote waliokuwa ndani ya uwanja huo , walishaambukizwa na virusi na wengi zaidi waliendelea kuathirika.
Wanajeshi wakubwa wa ulimwengu wa giza, macho yao yalikuwa yamebadilika rangi. Wengi wao walibadilika na kuanza kung’atana.
Kadri watu walivyozidi kudondoka chini na kupoteza uhai , eneo hilo liligeuka mto wa damu.
Moto mkali ulikuwa ukiunguza makundi kwa makudi ya wale ambao wamekwisha kuambukizwa na kupandwa na wazimu.
Nyakasura mwili wake wote ulitoa mng’ao wa miale ya moto , licha ya eneo hilo kuwa na sumu nyingi na maambbukizi ya virusi , hakuathirika hata kidogo.
Watu wengi mara baada ya kuona moto wa Nyakasura ulikuwa na ufanisi mno kwenye kuwadhibiti misukule hao, wale waliokuwa hawajaambukizwa walimsogelea na kumuomba awalinde
“Nyie hebu nipisheni , mnanizuia njia nitaendelea kuwaunguza vipi?”
Yeye peke yake aliweza kuunguza zaidi ya mamia ya maskeletoni na maiti lakini kwasababu mengi yalikuwa yamesambaa kila kona pamoja na uwepo wa watu wengi , alishindwa kuyaunguza kwa haraka.
“Nyakasura , tukiendelea hivi hatuwezi kufanikiwa , tunapaswa kutengeneza njia watu wakimbie na ndio namna tunaweza kutumia uwezo wetu wote kuwadhibiti”Aliongea Huge.
“Unadhani sijafikiria hivyo? Unaona kabisa kila njia za kutokea zimejazana misukule na maiti zenye maambukizi , watu waliopo hapa hawana mafunzo yoyote , watarukaje kutoka nje?”
“Kama hakuna jia nzuri , tunaweza kuitengeneza”Aliongea Huge huku akigeuza uso wake na kumwangalia Mr Air kwa mbali , ambae alikuwa bize kuyeyusha maskeletoni.
“Mr Air , unaonaje wewe na Captain mkisaidiana? Ili mradi tukiweza kutengeneza njia ya watu kukimbilia , tutapunguza wingi wa vifo”
Oleg ambae alikuwa katikati ya kazi ya kupasua maskeletoni na ngumi na mateke, mara baada ya kusikia hivyo , alicheka kwa nguvu.
“Kweli wewe ni msomi , akili yako imewaza vyema”
Mr Air na yeye aligeuka na kumwangalia Huge na kisha alitingisha kichwa kumuelewa. Palepale alielea juu angani na kusambaza mikono yake. Wimbi kubwa la mkondo wa upepo lilijitengeneza katika uelekeo mlalo na kuwa kama kimbunga.
Upepo ule haukumuumiza mtu , bali ulisafisha njia eneo la katikati, wakati huo huo Mr Air aliita elementi za unyevunyevu wa maji kutoka pande zote na kuzielekezea katika eneo la katikati.
Ghafla tu eneo la kati lilifunikwa na maji ambayo ni kama vile hayakuwa yakiathiriwa na kani mvutano kwa namna yalivyokuwa yakielea
Oleg mara baada ya kuona maji yale macho yake yalichanua kwa furaha .
“Maji haya yananitosha kabisa , kupambana nchi kavu bila maji kunachosha mno”
Mara baada ya kuongea hivyo palepale alichomoa upanga uliokuwa kwenye kiuno chake.
Upanga ule mara baada ya kuhisi uwepo wa maji uling’aa. Ulikuwa ni kama kioo , chenye kutoa mwanga wa kufurahisha macho. Ilikuwa ni kama Dhana tofauti na siraha ya kiuungu ambayo inaweza kusabaisha watu nywele zao kusisimka.
“Upanga mzuri sana!”
“Inasemekana katika historia ya urithi wa ukoo wa Viking , upanga ule unaweza kutumiwa na mbarikiwa wa bahari pekee “
Watu walishindwa kuzuia mshangao wao , mara baada ya kuona Capteni Oleg hatimae ametoa siraha yake ya uwakilishi.
Oleg alisimama wima na kuondoa ule upanga wake mbali na maji yale yaliokuwa yakielea na kitendo kile kilifanya yale maji kusogelea ule upanga kwa kasi kwa namna ya kuvutwa kama sumaku.
Muda huo , Oleg alionekana kuwa wa kawaida tu . Alikuwa amesimama kama mwanajeshi ambae anajivunia kile anachofanya huku nywele zake na misharubu ikipeperushwa na upepo.
Ghafla tu upanga ule uliacha kuvuta yale maji na badala yake yalimvaa Oleg na kuanza kumzunguka kwa spidi , kama vile kuna kitu kimeyashikilia.
Mr Air kuona vile aliondoa utawala wake katika maji yale na sasa yakawa chini ya Oleg.
Oleg alipiga makelele kwa namna ya kunguruma na palepale upanga wake aliouelekezea angani ulianza kurefuka urefu wake huku yale maji yaliokuwa yakimzunguka yakipotea taratibu , ilionekana kama vile yale maji ndio yanayoongeza upanga ule urefu kwenda hewani.
Ndani ya dakika chache tu upanga mkubwa wa mita kadhaa ulionekana,huku ukisambaza msisimko na nguvu isiokuwa ya kawaida.
“Ghadhabu ya mungu wa habari!!”
Baada ya kuongea vile , Oleg aliupigiza chini ule upanga , upanga ule ulikuwa ni kama Nyangumi iliokuwa ikidondoka na kwenda kukandamiza vitu vilivyokuwa chini yake na kutengeneza nafasi.
Nishati iliotoka katika siraha ile na maji yalioruka ilisababisha uwanja wote kutingishika.
‘Boom!”
Majukwaa ya uwanja yalionekana kushindwa kuhimili nguvu ile ya mkandamizo na kutoboka eneo la katikati na shimo kama njia lilionekana.
Watu wengi walioshuhudia tukio lile walijikuta wakitetemeka. Ndio sasa waliweza kuamini juu ya nguvuya Sea God Blade. Mwanzoni watu waliposikia Oleg kumiliki upanga unaotengenisha meli , waliamini ni upanga wa chuma , lakini muda huo walichoweza kushuhudia ilikuwa tofauti , ulikuwa ni upanga unaoongezeka ukubwa kulingana na uwepo wa maji.
Mara baada ya shimo kubwa kuonekana , lenye kuruhusu watu wengi kupita. Rais Maxim haraka sana aliamrisha.
“Ondokeni kila mmoja . Liacheni hili eneo kwa ajili ya magwiji kupambana”
Ukweli ni kwamba watu wengi walishajua uwepo wao ulikuwa ukiwapa shida Magwiji kuonyesha uwezo wao wote. Kama isingekuwa uwepo wa watu maskeletoni hayo yasingechukua muda kudhibitiwa.
Hivyo kila mtu hakutaka kuwa mzigo ndani ya eneo hilo na kukimbia kadri awezavyo kujiokoa.
Ndani ya muda mfupi tu , watu ambao walikuwa na uwezo wa kukimbia waliweza kutoka kupitia shimo.
Muda mfupi tu watu ndani ya ukumbi huo walipungua kwa kiasi kikubwa. Nyakasura na magwiji wengine hawakuwa na kizuizi tena cha kupigana.
Maskeletioni baadhi yaliotaka kufuata shimo , waliunguzwa na moto wa Nyakasura na mwanga wa nuru wa Mikaeli.
Ndani ya dakika chache tu Nyakasura na Mikaeli waliweza kudhibiti hali kwa asilimia kubwa.
Mara baada ya kuona hali imeweza kudhibitiwa , Maxim na viongozi wengine wajuu walijikuta wakipumua kwa ahueni.
“Rais , tunapaswa kuondoka hili eneo haraka iwezekanavyo , kama kutakuwa na mlipuko , sumu yake itatuathiri vibaya” Kiongozi mmoja aliongea.
Maxim aliishia kutingisha kichwa na muda huo ile anataka kutembea aliweza kumuona mtu alievalia joho la rangi nyeusi akimsogelea
“Skellidon?!”
Maxim na wengine walionekana kushangaa . ukweli ni kwamba walijua Skellidoni kwa uwezo wake angeweza kushuhugulikia hilo suala kwa ufanisi mkubwa. Kuongea na wafu ilikuwa ni taaluma yake.
Lakini sasa tokea kuanza kwa tukio hilo , Skellidon alionekana kuwa kimya tu , jambo ambalo lilimshangaza Maxim na wengine.
Muda ule Maxun mara baada ya kuhisi kitu kisichokuwa kawaida , ghafla tu aliweza kuona moshi wa ajabu ukimtoka katika vazi lake lile na kusambaa.
“Nini hiki?”
“Msivute! Ah!”
Viongozi hao hawakutegemea kama Skellidoni angewaambukiza. Ingawa baadhi yao walikuwa wana mafunzoya nishati za mbingu na ardhi lakini hawakuwa na kinga zidi ya sumu.
Dakika ambayo Maxim alishtuka , alitoa sauti kali na kuanza kumshambulia Skellidon . Lakini hata hivyo Skellidoni alionekana kutoathiriwa na sauti yake na kuendelea kusambaza sumu ya umauti.
Maxim , alikuwa ni mzee , hakuwa kijana . Sauti yake pia ilikuwa imepungua makali yake na mwili umezeeka.
Mara baada ya kuvuta moshi mwingi wa Sumu ya umauti , sura yake ilibadilika na kugeuka nyeusi na alianza kukohoa mfululizo huku akitema damu .muonekano wake ulijawa na kutokukubali na maumivu aliosikia yalimzidia na kudondoka chini.
“Rais !”
Kundi la watu wa Set , mara baada ya kuona tukio hilo walipiga makelele kwa mshangao. Hakuna hata mmoja alieamini kwamba moja ya magwiji kumi, Mr Skellidon, angemuua Rais Maxim waziwazi.
Unachopaswa kujua ni kwamba Set organisation ilikuwa chini ya ulinzi wa mataifa mengi makubwa duniani . Kumuua kiongozi wake maana yake ni kujitengenezea uadui na mataifa hayo na sio hivyo tu kumuua pia ilikuwa ni kukiuka sheria za ulimwengu wa giza maana yake utapambana na kila mmoja wa ulimwengu huo.
Magwiji wengine hawakutegemea jambo hilo lingetokea . Walikuwa bize kupambana na maskeletoni, maiti pamoja na watu walioambukizwa , lakini nani angegundua Maxim ndio alikuwa shabaha na maskeletoni walikuwa chambo.
“Pisheni njia!”
Ghafla tu mwanga wa rangi nyeupe ulishika kutoka juu , Silvia ambae alikuwa amevalia gauni lake la rangi nyeupe alionekana kama malaika wakati akishuka na kwenda kutua karibu ya maiti ya Rais Maxim akiwa na macho yaliojaa ukauzu.
“Skeletoni pokea adhabu takatifu! Adhabu ya nuru ya mungu”
Silvia alifungua kiganja cha mkono wake na mpira wa nuru ulijitengeneza, ulikuwa ni kama jua na kuangaza eneo hilo wakati huo wa usiku.
Kila mmoja aliebakia eneo la tukio , aliishia kuangalia namna ambavyo mwanga ule uligeuka boriti kama mshale na kutupiwa Skeletoni na kumuunguza.
Msisimko wa nguvu ya umauti uliokuwa ukimtoka Skellidon ulipotea, mwili wake ulitingishika kidogo tu na sekunde kumi na tano mbele , mwili wote uliyeyukia hewani kama ukungu mweusi . Kitu pekee kilichobakia lilikuwa ni vazi lake la joho jeusi pekee na baadhi ya mifupa aliokuwa ameiniing’iniza.
Watu kuona shambulizi lile walionekana kushangazwa na uwezo wa Silvia, lakini kuna wengine walijawa na shaka.
“Mbona kama naona sio kawaida, yaani Gwiji aina ya Skelidoni ameuliwa na shambulizi moja tu?”
Watu wachache waliokuwepo walibung’aa mara baada ya kuona Skelidoni hayupo tena.
Ingawa ni kweli ufunuo wa nuru , mbinu anayotumia Malkia mweupe ilikuwa na nguvu juu ya aina nyingi za uchawi , lakini watu walishindwa kuelewa imekuwaje mtaalamu wa juu mwenye cheo cha ugwiji kuuliwa na shambulizi moja tu.
Magwiji walioshuhudia suala hilo , walionyesha hali ya kutokuamini pia , walikuwa na shaka kwenye nyuso zao kuona ghafla tu Skelidoni ameuliwa. Hata hivyo hakuna hata mmoja ambae alitaka kuongelea suala hilo , kwasababu baada ya kifo cha Maxim nyaraka aliokuwa ameshikilia imedondoka chini ardhini.
Sebastiani ndio aliekuwa wa kwanza , kilikuwa ni kivuli chake tu kilichoonekana kikipotea kuelekea eneo nyaraka ile ilipo kuiokota.
“Tena usijaribu !”
Mikaeli ni kama alikuwa kwenye mawazo ya Sebastiani kwani aliweza kushituka mapema sana na alirusha mkuki wake uliotawaliwa na nguvu ya nuru na kwenda kumkinga Sebastian kwa mbele.
Sebastiani hakuwa na jinsi zaidi ya kusimama , kujiepusha kugusana na nuru ya mkuki ule.
Muda huo Silvia ambae alikuwa karibu na Maxim alichukua nafasi hio na kuinama chini na kuokota ile nyaraka. Hakuishia kuiokota tu aliinamisha hata kichwa chake kuonyesha ishara ya heshima mbele ya maiti ya Maxim.
“President, everyone will remember the price you paid for the underground world.”Aliongea Silvia akiwa na hali ya majonzi usoni.
“Silvia mtawala wa siku za zama , je bado unapanga kuendelea kushirikiana na watu wa Madhabahu takatifu?”Aliuliza Sebastiani.
“Prince Sebastian kwanini unaongea hivyo? Tulikuwa na nguvu kipindi kile na sikutaka tu nyaraka hii kuangukia katika mikono ya watu wabaya. Mpaka sasa hatujajua bado nani kasababisha haya mashambulizi , kwanini tusiwe makini kwanza?”
“Mhm! Kwa mtazamo wangu , wewe White Queen , utakuwa ndio upo nyuma ya haya”Aliongea Sebastiani kwa kejeli.
“Prince , unao ushahidi wa kuongea hayo juu yangu?”
“Your creed of Odd Ones is ’Chos -Forvr’ which translate chaos will exist forever. Making this world fall into chaos and war , isn’t that what you’re after ?”
“Kadri ulimwengu utakavyokuwa katika machafuko ndio namna nyie wote mlivyo na furaha! Kwasasa lazima una furaha baada ya kufa kwa Rais Maxim na kuvurugika kwa ulimwengu wote wa giza. Nyie ni tofauti na sisi , ukituongelea sisi tunaishi chini ya sheria ya ‘ Avoiding the world’ kwa zaidi ya miaka elfu moja sasa. Sisi ndio kabila la watu wenye amani duniani hapa , tofauti na wewe White Queen , kushika hio nyaraka ya dawa ya kifo ni hatari zaidi , hivyo unaonaje ukinipatia mimi?”
“Kwanza kabisa, licha ya kwamba ni kweli sisi The Odd ones tunaamini ukweli wa Chaos , hio ni imani yetu tu pekee . Hatujawahi kuwa na mawazo ya kuiharibu dunia. Pili , sina mpango wa kuishikilia hii nyaraka mimi mwenyewe , tusubiri mpaka hili janga lipite na kisha tutakusanyika pamoja na kuingalia na kujadiliana namna ya kudili nayo. Si ndio vizuri zaidi kuliko mtu mmoja kuishikilia?”
“Sylvie, you don't need to speak nonsense with these heretics. If you are not of my race, your heart will definitely be different.” Aliongea Mikaeli akimaanisha kwamba Silvia aache kuongea na huyo mzushi , akiongezea kwa kusema kama sio wa kabila lao basi mioyo yao itakuwa tofauti siku zote.
Wakati huo wakati wakiendelea kuongea , Nyakasura alisogea karibu yao na kuwaangalia kwa chuki.
“Hivi nyie! Huu ni muda wa kuendelea kujadiliana kuhusu hio nyaraka? Hebu angalieni kuna maelfu ya watu wameathirika , ni kipi tunapaswa kufanya?”
Nyakasura alikuwa amechukia mno kwa namna watu wengi wasiokuwa na hatia walivyoambikizwa. Aliona sio vyema kuwaua wote kwa moto.
Viongozi muda huo ndio sasa waligundua , ijapokuwa viumbe hao wa kutisha wamekwisha kumalizika , lakini kulikuwa na watu wengi ndani ya tukio ambalo walikuwa na majeraha na kuambukizwa na virusi.
“Jamani haina haja ya kupaniki , pengine ufunuo wangu wa uponyaji unaweza kuondoa sumu ndani ya miili yao. Nisaidieni kuwakusanya wote walioumia sehemu moja”
“Kweli kabisa , nguvu ya uponyaji ya Malkia wa nuru ina uwezo wa kuondoa nguvu za kichawi”
Viongozi wa baraza hilo haraka sana waliondoka kwa ajili ya kuweka utaratibu kwa majeruhi kupelekwa katika eneo moja ili kutibiwa.
Silvia aliishia tu kumwangalia Sebastiani na macho yaliojaa ukauzu na kisha akashusha pumzi zake.
“Prince , kama hakuna kingine nadhani tutamalizia baada ya kutibia majeruhi . Sidhani kuna kitu muhimu zaidi ya kuokoa uhai wa mtu , au unasemaje?”.
Watu wengi waliosikia maneno ya Silvia walitingisha vichwa kwa kuona ameongea kwa busara sana. Sebastiani upande wake aliishia kutoa mguno tu na kisha akaondoka.
***
Nje ya ukumbi watu wa Inferno walifanikisha kumtoa Regina nje akiwa salama salimini . Hata hivyo baadhi ya masenari walikuwa pia wameambukizwa na moshi wa kifo na waliishia kudondoka chini kwa maumivu.
Wakati kila mmoja akiwaza nini hatua ya kuchukua , ndio muda ambao Hamza na Black Fog waliweza kufika.
“Bosi! Hatimae umerudi”Aliongea Mameni.
Hamza aliishia kuangalia hali ilivyo mbaya katika eneo hilo pamoja na shimo ambalo limetengezwa kutokea nje ya uwanja, aliishia tu kukunja sura kwa jinsi watu walivyokuwa wakiugulia maumivu , huku wengine wakionyesha ishara za kupandwa na wazimu.
“Wife , unaendeleaje?”
Mara baada ya kuona Hamza amerudi salama , Regina alishikwa na hali ya ahueni na kutingisha kichwa chake.
“Nipo sawa . Shukrani kwa kila mmoja hapa nimekuwa salama , ni kwamba tu baadhi ya watu wameingiwa na sumu”Aliongea Regina na Hamza alitingisha kichwa na kugeuza kichwa chake.
“Wameambukiwa na sumu ya umauti , wanapaswa kutibiwa haraka iwezekanavyo”
“Inaonekana Silvia anapanga kuwatibu watu wote walioambukizwa , anataka tuwakusanye watu wote katika eneo moja”Aliongea Azzle.
“Sawa, ufunuo wake wa uponyaji utakuwa na nguvu ya kutosha”
Mara baada ya masenari kuchukuliwa , hatimae watu walipata muda wakuongelea kile kilichotokea.
“Bosi , ulikuwa umeenda wapi? Suala kubwa limetokea hapa , kulikuwa na kundi kubwa la..”
“Najua” Hamza aliingilia na kisha akaendelea, “Nilizuiwa na Skellidoni ndio maana nilishindwa kurudi kwa wakati . Najua ameita kundi kubwa la wafu , lakini kwa bahati mbaya hakukuwa na mtandao”
Mara baada ya kila mmoja kusikia hivyo , walijikuta wakishangaa na kuona ni ajabu.
“Bosi Skeletoni ameuliwa na Silvia muda si mrefu”
“Nini!”
“Haiwezekani , Master huyo aliekufa ni feki , ni skeletoni lililokuwa chini ya akili za Skelidoni’Aliongea Black Fog.
Kila mmoja alionekana kuchanganyikiwa baada ya taarifa kutoka pande zote kukinzana.
Hamza aliona suala hilo lilikuwa na ukakasi , hivyo aliamua kusikiliza kile kilichotokea wakati akiwa hayupo.
Mara baada ya kusikia kwamba Skelidoni amemuua Rais Maxim na pia yeye kuuliwa na shambulizi moja na Silvia , alijua fika huyo ni feki. Hio ni kwasababu Hamza alishaona uwezo halisi wa Skellidon na kwa namna yoyote ile hawezi kufa kwa shambulizi moja la Silvia kirahisi.
“Bosi kwahio kwa maelezo yako unamaanisha ulikuwa ni mtego wa Skellidon na bado yupo hai?”Aliuliza Asmuntis.
“Nina uhakika hajafa , lazima sasa hivi atakuwa amejificha”
“Lakini bosi tatizo ni kwamba kama unasema hajafa na asipojitokeza , hata uwaambie watu yupo hai , hakuna atakae kuamini”Aliongea Berly.
“Shenzi! Kwanini bosi adanganye? Kwa ukubwa wa cheo chake anawezaje kufanya hivyo?”Aliongea Leviathan.
“Sisi tunaweza kumuamini bosi kwa asilimia mia moja , lakini wengine sidhani . Isitoshe kipindi cha vita takatifu tulishirikiana na Madhabahu ya Giza. Awamu hii alichofanya Prince Sebastiani kimefanya watu kumhisia kama mhusika na moja kwa moja lazima tuunganishwe”Aliongea Azzle.
Hamza alihisi kichwa chake kuanza kumuuma . Alijua kile kilichotokea ni mpango wa Skellidon lakini hakuwa na namna ya kutoa ushahidi. Na kuhusu Ankh hakuwa na uhakika kama ilikuwa kweli kwasababu hakuweza kujua ni sababu gani Dokta Genesha aliamua kuhifadhi kiboksi hicho ndani ya Baraza la maksi.
Haijalishi Dokta Tembo alimdanganya au kulikuwa na sababu nyingine, Hamza hakuweza kupata kuelewa.Muda huo akiwaza aliwez k usikia sauti ikimwita kutoka nyuma.
“Hey, Ulikuwa umeenda wapi wewe?”
Comments