CHANGE
Story by Elton Tonny
Urafiki, Familia, Mapenzi, Mahaba, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Ukatili, Mauaji, Mambo yasiyotazamiwa, Mambo yenye kuhofisha
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA SITA
★★★★★★★★★★★★
Maandalizi ya kumwondoa bwana Masoud kutoka hospitalini yakaanza haraka sana kwa madaktari kuhakikisha anasafirishwa kutoka hospitalini kwa usalama. Efraim Donald akiwa sambamba na Namouih alishughulikia mambo yaliyohusiana na gharama za usafiri, vitambulisho vya kuhama nchi, gharama ya huduma ambazo mzee huyo angepokea kutoka huku mpaka kule London kwa muda WOTE ambao angepokea matibabu hayo mpaka wakati ambapo angetakiwa kurudi tena nyumbani. Huyu mtu alikuwa na hela sana, na njia aliyozitumia ilionyesha kweli alikuwa na pendo kuu kumwelekea Namouih.
Ilkuja kwa kumshangaza kiasi bwana Masoud baada ya kuambiwa kwamba angepelekwa nje ya nchi ili kupata matibabu, lakini alijitahidi kuwa mtulivu na kutouliza mengi sana. Alijulishwa kwamba angepelekwa London ndani ya siku tatu tu, hivyo kwa muda huo watu wake wa familia wangehitaji kuwa karibu naye zaidi kabla ya kumuaga. Zakia alikuwa na furaha sana, kwa sababu Efraim Donald ndiyo alikuwa kila kitu ambacho sikuzote alitazamia binti yake angechagua kuwa nacho maishani. Mwanaume huyo aliwatendea kwa fadhili na upendo sana mpaka ingekuwa rahisi kwa yeyote kufikiri kwamba alijuana na familia hii kwa muda mrefu.
Sasa ikiwa imebaki siku moja tu kabla ya bwana Masoud kupaishwa kwa ndege, Efraim Donald alikuwa ametoka pamoja na Blandina, Zakia, na Nasma kwenda sehemu fulani kupata kama mjumuiko wa pamoja kisha ndiyo waende tena hospitali, hiyo yote ikiwa mwanzo wa kufahamiana vizuri. Aliwapeleka sehemu nzuri sana na hata kumnunulia Nasma na Zakia vitu vizuri, nao wakazidi kumpenda. Ni Namouih na Sasha ndiyo waliokuwa hospitalini wakati huo pamoja na baba yao, na sasa mzee Masoud akawa amepata nafasi nzuri ya kuzungumza na binti yake mkubwa bila uwepo wa wengine hapo.
"Sasha..." Masoud akaita.
Sasha alikuwa ameketi pembeni yake, naye akaitika, "Bee..."
"Naomba kuongea na dada yako mara moja..." Masoud akasema.
"Sawa baba..." Sasha akajibu.
Binti akanyanyuka na kuondoka sehemu hiyo, naye Namouih, aliyekuwa pembeni pia, akawa anamwangalia baba yake kwa umakini.
"Vipi baba... unataka kuniambia nini?" Namouih akamuuliza.
"Namouih... unafanya nini?" Masoud akauliza.
Namouih akatulia kidogo, kisha akauliza, "Unamaanisha nini?"
"Huyu mwanaume uliyempata ghafla-ghafla tu... mara ni mchumba wako... mara kidogo sijui naenda Marekani, sijui wapi... Namouih..."
"Baba..."
"Nilikuwa sijasema chochote kabla lakini mimi siyo mjinga. Ninakujua vizuri wewe mtoto. Unajiharibia... maisha yako kutafuta suluhisho kwa jambo lisilokuwa na faida... kwa nini?"
"Baba usirudie tena kusema hivyo. Maisha yako yana faida mara mia zaidi kuliko yangu..."
"Kwa ajili gani? Namouih... umeamua kutafuta tu mwanaume mwenye pesa bila kumjua vizuri ili.... akikunyima furaha je? Akikugeuza kuwa mtumwa wake je? Si uliniahidi usingefanya jambo lolote la kipuuzi... hivi ni nini lakini...."
Namouih akakishika kiganja chake na kusema, "Baba... usijali. Efraim namjua. Ni mchumba wangu. Usiwaze hayo kabisa. Cha muhimu zaidi wakati huu ni wewe kwenda...."
Maneno ya Namouih yakakatishwa baada ya Masoud kukitoa kiganja chake kutoka mkononi kwa binti yake. Alionyesha kukwazika sana, na jambo hilo likamwacha Namouih bila amani moyoni. Alipomwambia Blandina kwamba alitaka mambo yaende vizuri bila kuwepo kwa drama nyingi alimaanisha kama hivi, isipokuwa tu haya hayakuwa maigizo kutoka kwa baba yake; alijua amemkwaza kiukweli. Lakini akijua kabisa kwamba alifanya haya yote ili kumwokoa, ikampa nguvu ya kujihakikishia kwamba alikuwa sahihi hata kama baba yake hakupenda.
"Maamuzi nayochukua siyo kwa sababu za kibinafsi baba. Ninakupenda, na ninahitaji uendelee kuishi kwa sababu bado sisi wote tunakuhitaji. Usiwaze kuhusu mimi... Efraim ni mwanaume mzuri sana... ananipenda," Namouih akasema.
"Efraim Donald. Inamaanisha yeye ni mkristo... umemzoa tu huko wapi sijui unamleta eti mchumba wako... Namouih, umeshafikiria kuhusu tofauti mtakazokuwa nazo kwa sababu hiyo? Unaelewa kwamba mama yako na mimi tulitibuana mpaka ikawa shida kubwa kwa saba...."
"Baba... tafadhali acha kufikiria hivyo. Siku hizi hakuna hayo mambo sana, haijalishi dini wala nini, kikubwa ni kwamba watu wamependana na wako tayari kuwa pamoja," Namouih akamwambia.
"Unampenda huyo mwanaume Namouih?" mzee Masoud akauliza.
Namouih akabaki kimya tu na kubaki kumwangalia baba yake.
"Najua siwezi kukuamulia namna ya kuendesha maisha yako. Lakini ikiwa utaingia kwenye mikazo kwa sababu hii itakuwa ni kama mimi ndiyo nimesababisha hilo. Sijui ni kwa nini una king'ang'anizi sana we' mtoto. Nakuombea tu mazuri binti yangu, na inanifariji kuona jinsi unavyopambana kunisaidia. Ninataka tu uwe na furaha," Masoud akasema.
Namouih akakishika kiganja chake tena na kusema, "Usijali baba. Niko mwangalifu. Na huyu mwanaume sijamzoa kokote tu, ametokea mbali pamoja nami. Nachohitaji tu kwa wakati huu ni wewe kuniahidi kwamba utapambana kwenye mambo yote watakayokufanyia huko ili afya yako irudi kuwa nzuri zaidi. Niahidi."
Mzee Masoud akatabasamu na kufumba macho kwa njia iliyoonyesha kwamba amekubali kutoa ahadi hiyo.
Namouih akalaza kichwa chake karibu na bega la baba yake huku akimwimbia wimbo kwa sauti ya chini na kwa upendo sana, kama tu baba yake alivyopenda. Baada ya muda mfupi, Efraim Donald na wengine wakawa wamefika hapo na kujiunga nao, wakipata mazungumzo mengi na kutumia muda mwingi pamoja na mzee wao mpaka muda ambao wangetakiwa kumwacha. Efraim Donald akamwahidi Namouih na wadogo zake kuwa baada ya kumsafirisha baba yao wangetumia muda mwingi kutembelea maeneo mengi ambayo wangefurahia sana, hasa ukifika wakati ambao watoto wangepumzika kimasomo.
★★★
Hatimaye ilifika siku ambayo bwana Masoud alipanda ndege na kupelekwa nchini London kwa ajili ya matibabu yake. Wanafamilia na marafiki zake wengi walimuaga, na Nasma alilia sana kwa kuwa alijua baba yake alikuwa anapelekwa mbali. Masoud angekuwa chini ya uangalizi maalumu wa timu ya madaktari na wauguzi kwa muda wote ambao angekaa London, hivyo hakukuwa na haja ya yeyote kati ya watu wake wa familia kwenda huko kwa kuwa Efraim alihakikiaha kila jambo limepangiliwa vyema.
Kutokea wakati huo, Namouih na Blandina walirudi jijini kwao walikofanyia kazi, na ni huko huko ndiko Efraim Donald alitokea. Kwa hiyo mwanaume huyu alianza kumfanyia vitu vizuri Namouih kama kumpeleka matembezi, kupata milo kwenye sehemu za kifahari na kumnunulia vitu vingi vya gharama. Ingawa Namouih hakuwa aina ya mwanamke aliyehitaji mwanaume tu ndiyo amfanyie kila kitu, alivutiwa na jinsi ambavyo Efraim alijitoa kwake, naye akaendelea kujitahidi kumwingiza zaidi moyoni taratibu. Efraim Donald hata aliiboresha zaidi nyumba ya Masoud na Zakia, na alishiriki mambo mengi na mama yake Namouih hasa baada ya kumzoea kutokana na mwanamke huyo kupenda vitu vizuri-vizuri, au kwa maneno mengine, pesa.
Ikafika wakati ambao Efraim Donald alimpeleka Namouih kumwona mama yake mzazi. Aliishi mkoa mwingine tofauti na jiji hilo, naye aliitwa Halima. Mara ya kwanza kumwona Namouih, Halima alimsifia sana na kumkaribisha kwa upendo, akikazia kwa mwanaye kwamba angepaswa kumuoa mwanamke huyu haraka sana. Ndugu zake Efraim Donald walimpokea vizuri pia, na hawakuwa wengi sana mara hiyo ya kwanza kumfikisha Namouih kwao. Akiwa huku, Namouih alipata kusikia mambo fulani kuhusu familia ya Efraim Donald ambayo yalichukiza sana. Kuna ile hali fulani mtaani unakuta kwamba mtu alikuwa na maisha ya chini halafu akaja kutajirika, hivyo maneno ya wivu au fitina huwa hayakosekani, na hata Namouih aliweza kuyasikia lakini akaona ayapuuzie kwa kutojali wafitini.
Mpaka kufikia wakati huu, Namouih hakuwa amewahi kushiriki mwili wake na mwanaume huyo, kwa sababu ilikuwa wazi kwamba Efraim Donald bado alikuwa anamsubiria azielekeze hisia zake kwake kwa asilimia zote kama alivyomwahidi. Hii ilionyesha mwanaume huyu alikuwa na subira, na ni kitu kilichompendeza Namouih. Baadaye mwanamke huyu akarejea tena kazini. Alikuwa akipata taarifa kwamba hali ya mzee Masoud huko London iko kawaida (stable) baada ya taratibu za upasuaji wa mwanzo kwenda vizuri, kwa hiyo lilikuwa ni suala la muda tu na mambo mengine yangejulikana baada ya upasuaji wote kukamilika.
Baada ya Sasha na Nasma kuwa wamefunga masomo yao, Efraim Donald aliwachukua wote pamoja na Zakia kwa ajili ya kwenda kutembelea jijini kwao kama alivyosema kipindi kile wako hospitalini. Na akawatembeza kweli kweli. Wakati huu Namouih alikuwa akiendelea kusifika kuwa mwanasheria mzuri sana sambamba na rafiki yake, Blandina, naye alijiunga nao katika matembezi kila wakati alipopata nafasi. Efraim aliwapeleka ufukweni, kwenye mahoteli, kwenye kampuni yake, na nyumbani kwake pia; ile ile nyumba kubwa. Wakiwa hapo kwake ndiyo mwanaume huyo akatoa tangazo dogo la kutotarajiwa la kumvisha Namouih pete ya uchumba, naye akaikubali, Walifurahia sana siku hiyo, na Efraim Donald akasema asingechelewa hata kidogo kumuoa mwanamke huyu mzuri.
Efraim Donald kama kawaida alikuwa mtu wa safari za hapa na pale, lakini kila nafasi aliyopata ya kuwa jijini alijitahidi kumwonyesha upendo malkia wake kwa kumtoa matembezi, kumtambulisha kwa rafiki zake wengi, au kumnunulia zawadi. Blandina angemtania mara nyingi Namouih kwamba alitakiwa kujiandaa kwa ajili ya siku ya kumpa mwanaume huyo zawadi yake tamu, na kweli Namouih alikuwa ameshafikiria kuhusu hilo hasa kwa kuwa alikuwa ameshamzoea Efraim Donald, siyo kama mchumba kwake tu, bali kama rafiki wa muhimu sana.
★★★
Siku moja, Efraim Donald alimpeleka Namouih kwake, pale kwenye nyumba yake. Walipata mlo na maongezi, na kilichozungumziwa hasa ilikuwa ni kuhusiana na mipango ya ndoa yao. Kwa sababu ya dini kutofautiana, wote walielewa kwamba wangetakiwa kufunga ndoa kwa njia ya maandishi, yaani ndoa ya kiserikali, lakini bado Efraim alitaka sherehe ya ndoa yao iwe kubwa kupita maelezo, kwa hiyo alikuwa anapanga vitu vingi sana vya kumfanyia mrembo wake kumwonyesha jinsi alivyo wa pekee. Wakahamishia makao yao kutoka chini sebuleni na kwenda mpaka chumbani kwake Efraim, wote wakiwa na hisia nzuri sana kuelekeana na wakielewa kule ambako jambo hilo lingewafikisha.
Ilikuwa ni usiku, na Namouih alikuwa amevalia gauni fulani refu la blue lenye kuvutika na mwonekano mzito kama limelowana kwa maji, hivyo lilimbana kwa njia fulani iliyoonyesha umbo lake vyema na hasa kumchoresha nyuma vizuri sana; yaani endapo angetembea palikuwa ni mtikisiko tu. Alikuwa amezibana nywele zake kwa nyuma, huku usoni mwake akiwa amejiremba kwa kadiri, naye akasimama usawa wa kitanda kikubwa cha humo ndani akikiangalia kama vile anakitathmini. Akahisi pale ambapo Efraim Donald alimgusa kutokea nyuma yake, halafu mwanaume huyo akaibusu shingo yake taratibu.
"Napendaga unavyonukia mpenzi wangu," Efraim Donald akamwambia.
Namouih alikuwa ameanza kupandwa na hisia nyingi sana za kimahaba, lakini kwa sababu fulani, akawa anajitahidi kuzizima ili zisipitilize. Akapiga hatua nyingine mbele na kukaa kitandani, ikiwa ni kama vile amemkwepa Efraim, lakini akamtazama machoni kwa hisia.
"Sikuwahi kukuuliza. Umeshaleta wanawake wangapi hapa?" Namouih akauliza.
Efraim Donald akatabasamu na kusema, "Umechagua wakati mzuri sana kuuliza hilo swali."
Namouih akatabasamu pia.
Efraim Donald akamsogelea na kukaa naye kitandani, kisha akasema, "Sijawa na wanawake wengi sana. Maisha niliyokuwa nayo mwanzoni yalinifanya nionekane kama siwezi kummudu mwanamke, na mimi kiukweli sikuwa mtu wa kuwaza sana wanawake. Hata Mungu alipokuja kunisaidia kupata hivi vyote... nilikuwa nimezama zaidi kwenye kuboresha maisha yangu na ya familia yangu kwanza... hasa mama. Alikuwa amepitia shida nyingi mno. Kwa hiyo nilipotulia kidogo ndiyo nikaona nikutafute wewe ili nitulie zaidi."
Efraim alikuwa anasema hayo huku anasugua kiuno cha Namouih taratibu kutokea kwa nyuma, naye Namouih akatabasamu.
"Kwa hiyo sijui kama utaniamini nikikwambia kwamba sijawahi kulala na mwanamke yeyote kwenye hiki kitanda?" Efraim Donald akasema.
"Mmm... kweli?" Namouih akauliza.
"Ahahah... nataka wewe ndiyo uwe wa kwanza, na wa mwisho," Efraim akasema.
Namouih akaangalia chini kwa hisia, kisha akamtazama tena machoni.
Efraim Donald akaupandisha mkono wake uliokuwa kiunoni kwa mwanamke huyo mpaka nyuma ya shingo yake, kisha akakivuta kibanio kidogo cha nywele kilichozishikilia nywele za mrembo, nazo zikamwagika. Akazilaza upande mmoja wa bega la Namouih, halafu akamfata mdomoni na kuanza kumpiga denda taratibu. Midomo ya Namouih ilikuwa laini sana, na ulimi wake ulikuwa na ladha tamu sana iliyofanya Efraim apandishe mzuka hata zaidi. Akaanza kumtomasa kidogo sehemu ya titi lake la kulia, huku bado akimnyonya mdomo, kisha akaanza kumsukumia kitandani taratibu ili alalie mgongo. Namouih alikuwa ameshaanza kuguna kwa sauti ya chini baada ya hamu yake kuongezeka sana, naye Efraim akaanza kuivuta sehemu ya begani ya nguo ya mwanamke huyo ili ayafichue matiti yake.
Sehemu ya gauni la Namouih iliyofunika bega lake ilipovutwa chini, ilifanya sidiria aliyovaa ionekane zaidi, naye Efraim akawa analisugua titi la Namouih likiwa bado ndani ya sidiria hiyo. Alipotaka tu kulitoa ndani ya sidiria, Namouih akamshika pande za mikono yake kwa njia ya kumzuia, naye Efraim akajitoa mdomoni mwake na kumtazama kwa ufupi. Namouih akawa anamwangalia kwa njia legevu, kisha akajinyanyua na kuketi kama awali. Efraim bado alikuwa amelalia ubavu wake huku akimwangalia kwa hisia, naye Namouih akaanza kupandisha gauni lake juu ya mkono wake tena.
"Vipi?" Efraim akauliza.
Namouih akabaki kimya tu, akiinamisha uso wake kama vile kuonyesha kuna kitu kinamsumbua.
Efraim akaona akae pia, lakini wakati huu akiwa karibu zaidi na uso wa mwanamke huyu, kisha akauliza, "Uko sawa?"
Namouih akatikisa kichwa kukanusha na kusema, "Am sorry."
"Niambie tatizo nini Namouih. Kuna sehemu yoyote hujapenda nilipo...."
"No, siyo hivyo. Yaani... hhh... nisamehe Efraim... nina... sijui hata nikuelezeeje..."
Efraim akaishika shingo ya Namouih kwa wororo na kuanza kuzilaza-laza nywele zake.
"Sijawa ndani ya mahusiano kwa muda mrefu mpaka nilipokuja kukutana nawe... na hiyo ni kwa sababu kuna jambo fulani lilinipata kipindi cha nyuma lililosababisha niache... au niseme... niwachukie wanaume. Kuna mwanaume nilimpenda sana wakati nasoma chuo. Nilimpa kila kitu Efraim. Baadaye nikagundua kwamba... kila mara tulipofanya mapenzi... alikuwa anachukua video zetu... anawaonyesha watu wengine kabisa. Unajua ingekuwa bora kama nisingejua, lakini kilichoniumiza ni kwamba baada ya kumweleza kuwa sikupenda jambo hilo... akanitolea maneno machafu... kashifa nyingi sana... yaani ilikuwa ni kama vile sikumjua au.... hakunijua kabisa. Kati ya wanaume wote ambao niliwahi kutoka nao, angalau yeye ndiyo alionekana kuwa mature zaidi kwa muda wote niliodumu naye... lakini baada ya kitendo hicho... nilishindwa, yaani nilishindwa kuwaamini wanaume tena," Namouih akaeleza.
Machozi yalikuwa yameanza kumtoka alipokuwa akisema hayo, naye Efraim akamfuta kwa upendo.
"Pole sana. Sikutanii nikisema kwamba kama ningemjua huyo mwanaume ningemuua saa hiyo hiyo kabisa," Efraim akasema.
"Ahh... iliniumiza sana yaani. Sasa kwa sababu iliniathiri vibaya ndiyo maana imekuwa kama...."
"Moyo wako ni mgumu," Efraim akamalizia maneno yake.
"Am sorry Efraim... kwa mambo yote uliyonifanyia najua haustahili kabisa malipo ya namna hii."
"Namouih aliyekwambia mimi nahitaji unilipe chochote ni nani? Huyo mwanaume alikuchezea tu. Wewe sasa unaenda kuwa mke wangu. Tuna muda mwingi vya kutosha kukuruhusu uwe tayari kunionyesha upendo wako pia. Haujawahi kuniambia, lakini ninajua unanipenda..."
Namouih akamwangalia na kutabasamu.
"Kwa hiyo usiwaze. Picha zozote mbaya za mambo yaliyopita nitajitahidi kukusaidia ili uzifute... am here for you," Efraim akasema.
Namouih akakilaza kichwa chake begani kwa Efraim, na mwanaume huyu akawa anasugua bega la mrembo taratibu ili kumpa kitulizo.
"Kwa hiyo kutokea wakati huo haujawa na mwanaume yeyote kabisa?" Efraim Donald akauliza.
Namouih akatikisa kichwa kukubali.
"Ni miaka mingi eeh?"
"Ulikuwa mwaka wa tatu toka nilipoanza chuo... kwa hiyo... kufikia sasa imepita kama... miaka minne-mitano kufikia sita..." Namouih akasema.
"Wow. Ninajua nitafaidi sana kwako yaani..."
"Mhm... kwa nini?"
"Wewe una hali fulani hivi inayonifanya nitambue unajua sana romance... so sitakuwa na papara. Hilo jambo limekuchanganya sana naelewa, kwa hiyo si lazima iwe leo, maana kuna kesho na kesho kutwa pia... na ninajua utanipa mambo mazuri na matamu mno," Efraim akaongea hivyo na kumtekenya mbavuni.
Namouih akafurahi sana na kupitisha mkono wake kiunoni kwa Efraim. "Asante kwa kuwa na subira Efraim. Asante kwa kila kitu yaani," akasema kwa sauti ya deko.
"Kama nilivyokwambia... am here for you. Halafu kuna jambo nilitaka kukwambia. Aam... kuna hii kanpuni kubwa ya kibinafsi... CEO wake ni Edward Thomas, unampata?"
Namouih akaketi vizuri na kumwangalia usoni, kisha akauliza, "Edward Thomas... kwenye kampuni ya..."
"Ngoja nikuonyeshe kwenye simu. Ni rafiki yangu. Alikuwa amenitafuta hiyo juzi aliposikia nimekuvisha pete... alikuwa anakulenga wewe yaani. Anataka kuweka mtu awe kichwa cha masuala ya sheria kwenye kampuni yake, na amekuchagua wewe," Efraim Donald akasema.
"Kweli?" Namouih akauliza huku akitabasamu.
"Ndiyo. Namouih, ninakusihi uchukue hii kazi, ni kampuni kubwa, wanalipa vizuri sana, na wewe ukiwa kichwa pale... aisee!" Efraim akaongea kwa shauku.
Namouih akacheka kidogo na kuendelea kumsikiliza alipomwelezea mambo yote kuhusu suala hilo. Hapo ndiyo ungekuwa mwanzo sasa wa Namouih kujiingiza ndani ya kampuni ile kubwa, na alipokubali kuja kwenda huko, alitaka Blandina aendelee kuwa mwanasheria wake msaidizi hivyo naye apewe nafasi pia. Wakamtafuta huyo Edward Thomas, naye Namouih akaongea naye vizuri mpaka mipango ya yeye kwenda kuanza kazi ndani ya kampuni hiyo kubwa ikaanza mwendo. Alimshukuru sana mume wake mtarajiwa kwa kila kitu ambacho alikuwa anamfanyia, na kadiri ambavyo siku zilikwenda akawa anajitahidi kuonyesha kweli kwamba alimpenda, ingawa bado hakushiriki naye tendo la mapenzi.
Mara kwa mara Efraim Donald alijaribu sana kufanya naye mapenzi, lakini Namouih alionekana bado kuhitaji utulivu zaidi ili akija kumpa mwanaume huyo tunda, picha zote za maumivu ya nyuma ziwe zimemwondoka na ampe kwa moyo wote. Ingekuwa rahisi kusema kwamba muda mrefu vya kutosha ulikuwa umepita hivyo hakukuwa na sababu yoyote kwa mwanamke huyu kuwa mgumu bado, lakini ni kwamba tu hakuwa na moyo mwepesi sana baada ya kufanyiwa vibaya na mwanaume yule aliyempenda kipindi cha nyuma, kwa hiyo subira ya Efraim Donald bado ingeendelea kuhitajika.
★★★
Ndani ya miezi miwili hivi baada ya Namouih kuvishwa pete, tayari maandalizi ya sherehe yao ya ndoa yalikuwa yamekamilika, nao walikuwa wamealika ndugu na marafiki zao wengi kwa ajili ya kuhudhuria. Ndoa ilihalalishwa kiserikali, kisha ndiyo wangefanya sherehe yao ndani ya moja kati ya kumbi kubwa sana jijini hapo. Watu walikuwa wengi, vyakula kwa wingi, vinywaji vingi, furaha nyingi, na wanandoa hawa walipendeza sana siku hiyo.
Namouih alikuwa anatamani mno kama baba yake angekuwepo wakati huu ili kushuhudia mambo haya mazuri sana. Mzee Masoud bado alikuwa London, na kipindi hiki alikuwa amekaa tu kule baada ya upasuaji wake kufanikiwa, lakini angetakiwa kutulia kwanza ili awe na uimara kwa kutosha kuweza kurudi nchini. Ingawa hivyo, familia yake ilikuwa imemuunganisha kupitia simu kwa video aweze kuyaona mambo hapo, na alitoa baraka zake nyingi kwa binti yake na mumewe.
Basi, usiku huo baada ya wanandoa hawa wawili kuondoka sehemu ya sherehe na kwenda nyumbani wakiwa wanandoa rasmi, ilikuwa ndiyo wakati ambao Namouih alijihisi vizuri zaidi kihisia kiasi kwamba alijua utayari wa kumpa Efraim Donald haki yake alikuwa nao. Mapambo aliyowekewa mwilini mwake yalimfanya aonekane kama mhindi kabisa, hasa jinsi mikono yake ilivyopakwa yna na nguo nyekundu kama sari yenye urembo mwingi wa dhahabu kuizunguka. Efraim Donald hata akambeba kabisa mpaka chumbani ingawa ngazi zilikuwa ndefu na Namouih kuwa na uzito kiasi, na baada ya kufika chumbani akamweka kitandani taratibu ili waanze kupeana mahaba waliyosubirishiana kwa muda fulani sasa.
Efraim Donald alipoonyesha wazi kutaka kuanza kumpa bibie mapenzi, simu yake ikaita. Namouih akatabasamu kwa hisia baada ya Efraim kusema hiyo huwa ni lazima itokee kama kwenye tamthilia za wahindi, lakini kwake isingemzuia hata kidogo kusonga mbele. Akaichukua simu akiwa na lengo la kukata kisha aizime, lakini akatulia kwanza baada ya kuona aliyekuwa anapiga ni daktari wa huko London; mmoja wa madaktari wake mzee Masoud, akipiga kwa kutumia mfumo fulani wa simu kama "application." Efraim akamwonyesha mke wake, naye Namouih akasema aipokee ili kujua daktari alitaka nini.
Efraim Donald akapokea na kuongea na kumsikiliza, kisha akamtazama Namouih kwa njia iliyoonyesha kwamba kuna tatizo. Namouih akiwa haelewi kinachoendelea akamuuliza shida ni nini, naye Efraim akaishusha simu na kumwambia sasa alikuwa ametumiwa taarifa kwamba mzee Masoud alipoteza maisha. Namouih alibaki kumtazama Efraim kama vile hajasikia alichoambiwa. Mume wake akaanza kumfariji na kumsogelea karibu zaidi huku anamwongelesha kwa huruma, lakini Namouih hakusema lolote lile na kubaki anadondosha machozi. Jamani, si mzee alikuwa sawa kabisa mpaka wamemaliza sherehe? Nini kilikuwa kimetokea? Jambo hili liliwafanya wanandoa hawa washindwe hata kuonyeshana upendo baada ya kuingiwa na majonzi mengi.
Taarifa zaidi zilipoanza kuja kutoka London zilionyesha kwamba mzee Masoud alifanikiwa ndiyo kuokoka saratani na angerudi kuwa na afya nzuri kabisa, lakini kulikuwa na maumivu ya ndani yaliyosababisha kifo chake. Ilieleweka kwamba hiyo ilitokana na upasuaji wa kitaalamu aliofanyiwa, labda mwili wake haukuwa imara vya kutosha kuendelea kuvumilia ingawa yeye Masoud alifanya ionekane kwamba yuko sawa. Iliwaumiza sana wanafamilia wake wote, lakini mwishowe wangepaswa tu kukubali kwamba hawakuwa naye tena.
Kwa hiyo baada ya siku chache mwili wake ukawa umerudishwa nchini, naye akazikwa mkoani kwao. Ilipokuwa imeanza kuonekana kwamba furaha mpya imempata Namouih, jambo lenye kusikitisha likawa limetokea. Kwa muda fulani alikuwa kwenye huzuni sana, na Efraim Donald aliona ampe muda tu wa kutuliza hisia zake huku akiendelea kumfariji na kumwonyesha upendo wake mwingi, hivyo mwisho wa siku mwanamke huyu akaendelea tu kuchapa kazi kwa bidii. Na ilikuwa bidii yenye nguvu kweli kweli maana hakuwahi kupoteza kesi yoyote ile aliyochukua kushughulika nayo.
Ndiyo kutokea wakati huo mpaka ndoa yao inamaliza mwaka na miezi michache, wanandoa hawa hawakuwa wamewahi kupeana mahaba kabisa.......
★★★★
WAKATI ULIOPO....
Ikiwa ndiyo usiku wa siku ambayo Efraim Donald alikuwa amerudi nyumbani baada ya kutoka safarini, haikuwa imechukua muda mrefu vya kutosha kumkwaza mke wake baada ya yeye kutotaka wapeane mahaba kwa kusema amechoka. Namouih alikuwa amejifungia bafuni kwa kukasirishwa na jinsi Efraim alivyomkwepa, na mwanaume huyu akasogea mpaka mlangoni kuingilia bafuni akijaribu kumwambia kwa upole atoke ili waweze kujipumzisha; akisisitiza kwamba ni kweli alikuwa amechoka.
Namouih kiukweli hakuweza kumwelewa Efraim vizuri. Tabia hii ilikuwa imeendelea kwa muda mrefu sasa, na mwanzoni ni kweli alihitaji muda kutokana na mambo mengi magumu aliyopitia kihisia, lakini kwa wakati huu alikuwa anamwonyesha wazi kabisa kwamba anataka kumpatia mapenzi kwa kuwa vidonda vyake vimepona, ila Efraim Donald akawa anampiga chini. Ndiyo sababu alimuuliza ikiwa labda hali hii ilisababishwa na yeye kutofanya naye mapenzi kabla hawajaoana, akifikiri labda Efraim alikwazwa kipindi hicho na sasa hii ndiyo ilikuwa adhabu yake, lakini kiukweli hiyo haikuwa sababu.
Sasa hili jambo lingeendelea kuwa hivi mpaka wakati gani? Blandina alikuwa amemshauri azungumze naye endapo angezingua kama hivi, na ndicho Namouih alichokifanya, lakini ilikuwa ni kama masikio ya mume wake hayasikii maana ilipokuja tu kwenye suala hilo alijali zaidi kazi, safari, kupumzika. Mwanamke akaendelea tu kukaa bafuni mpaka inafika saa nane, ndiyo akatoka na kukuta Efraim akiwa ameshalala. Akamwangalia sana, sana, kisha naye akaenda taratibu kitandani na kujilaza upande wake, kukiwa na nafasi kubwa iliyowatenganisha kitandani hapo, na mioyoni mwao.
★★★
Asubuhi ikafika. Namouih kama kawaida aliamka na kujiandaa kwa ajili ya kazi, na wakati huu hakuwa amesumbuliwa na ndoto mbaya kama ile ya siku iliyotangulia. Alimwacha Efraim Donald akiwa amelala mpaka yeye alipomaliza kuvaa suti yake ya kike yenye sketi iliyoishia magotini, yenye rangi ya zambarau, viatu vyeusi na virefu chini, huku nywele zake akizibana kwa nyuma. Akashuka chini na kwenda kupata kiamsha kinywa huku akiwa na Angelo, yule paka wake, naye Esma alikuwa jikoni kushughulikia mambo mengine yaliyohitajika kwa baadaye.
Ndipo Efraim Donald akatokea huko juu chumbani Namouih alipokuwa mbioni kumalizia chai. Akafika karibu yake na kumbusu shavuni huku ameyashika mabega yake na kumsemesha kwa salamu, naye Namouih akatikisa kichwa tu kuitikia lakini akionyesha wazi kwamba bado alikuwa amekwazika. Mwanaume akakaa kwenye kiti chake mezani hapo, huku akiuliza ni mambo gani ambayo Namouih angeshughulikia leo. Yaani alifanya ionekane ni kama hakukuwa na tatizo kabisa, na kwa sababu Esma alikuwa amefika hapo kumwekea vyombo kwa ajili ya chai, Namouih akaona amjibu tu kwa ufupi, akisema anaenda kumtetea msichana kwenye kesi ya ubakaji akiwa na Blandina.
Efraim Donald akampongeza na kupendekeza kwamba wamwalike Blandina leo jioni, aje kupata chakula pamoja nao kwa kuwa alimkumbuka sana rafiki yake huyo. Angalau hii ilifanikiwa kumfanya Namouih atabasamu, naye akasema angemwambia. Mume wake akasema angekwenda mjini kutafuta mambo mengi mazuri ili Namouih akirudi atengeneze msosi wa nguvu, naye Namouih akakubali na kuaga hatimaye. Aliondoka akiwa hajihisi vizuri sana kwa sababu kuna upande wake mmoja uliofurahia sana utu wa Efraim lakini mwingine ulichukizwa na mambo kama yale yaliyotokea usiku wa jana yaliyofanya aina yao ya maisha iwe kama maigizo, lakini hakuwa na jinsi ila kubaki mtulivu; na hasa kwa sasa aelekeze nguvu zake zote kwenye kesi ya Agnes.
Akachukua gari lake aina ya Premo lenye rangi ya shaba iliyong'aa (silver) na kuanza kuelekea kwenye mahakama ambapo kesi ingesikilizwa, ikiwa imepangwa kuanza saa nne kamili asubuhi.
★★
Namouih alifika eneo la mahakama na kukuta watu kadha wa kadha wakiwa wameshafika, na Blandina tayari alikuwa hapo pia. Akamlaki rafiki yake na kuuliza ikiwa gari lake lilikuwa limepona kabisa ile sehemu iliyokunjika, naye Blandina akasema lilikuwa kwa mafundi bado likinyooshwa vyema na kupigwa rangi ili liwe kama jipya kabisa, kwa hiyo asubuhi hiyo alifika hapo kwa usafiri wa kulipia. Blandina alikuwa ameshikilia kablasha lenye karatasi za mambo kadhaa kuhusiana na kesi ya Agnes, akimwambia Namouih pia kwamba alikuwa ameshazungumza naye na mama yake kwa kuwa walifika hapo mapema, na hivyo walikuwa ndani wakimsubiri yeye Namouih.
Namouih akaanza kuvaa joho jeusi la mwanasheria alilokuwa ameliweka ndani ya gari lake, na Blandina akawa ametambua kwamba uso wake ulificha hisia ya huzuni. Akamuuliza shida ni nini, naye Namouih akasema hakukuwa na shida kabisa. Blandina akakisia kwamba mambo hayakwenda vizuri baina ya Namouih na Efraim Donald, naye akauliza ikiwa jaribio lake lilifanikiwa, na ndipo Namouih akafunguka kwa ufupi akisema alijitahidi sana lakini bado mume wake hakutaka kushiriki naye tendo la ndoa. Hii ilimshangaza Blandina kiasi, hata akauliza ikiwa labda Efraim alikuwa anatoka na mwanamke mwingine au ni shoga, lakini Namouih akasema angetakiwa tu kuliweka hilo pembeni kwanza. Akamwambia rafiki yake kuwa leo jioni anapanga kumkaribisha nyumbani kwake kwa ajili ya mlo, na lilikuwa ni wazo la Efraim, naye Blandina akafurahi na kukubali mwaliko huo.
Wawili hawa wakaanza kuelekea kule ndani ya jengo la mahakama. Lilikuwa jengo jeupe na kubwa, lenye muundo wa ghorofa pana likiwa na kumbi kadhaa, nao wakaingia moja kwa moja mpaka kule ambako kesi ingesikilizwa. Kulikuwa na mabenchi marefu yenye sehemu za kuegamia, kwa ajili ya wasikilizaji, kizimba kilichokuwa upande wa kulia kutoka pale ambapo hakimu (judge) angekaa huko mbele, upande wa kushoto kulikuwa na sehemu ambayo wangekaa waamuzi maalumu wa kesi (jury/jurors), na kulikuwa na watu wengi kiasi pande zote za kusikiliza.
Upande wa mtoa mashtaka, yaani Agnes, msichana ambaye Namouih angemtetea, ndiyo upande uliokuwa na watu wengi zaidi ya upande wa mtuhumiwa, yule kijana aliyeitwa Japheth, mwenye kesi ya kubaka. Mama yake Agnes alipomwona Namouih alianza kuongea naye, kisha akamwacha aende mpaka pale mbele kwenye meza ya kukaa mwanasheria na mtu wake wa kesi; ambako Agnes aliketi. Wakasalimiana vizuri, na Blandina alikuwa amekaa benchi la kwanza usawa wa sehemu aliyokaa Namouih pale mbele. Baadhi ya watu waliokuwepo walimwongelea sana Namouih, wakijua alisifika sana kwa kushinda kesi zote alizowahi kushughulika nazo, lakini wengine walikuwa wanaongelea zaidi urembo wake na jinsi alivyoonekana kuwa wa gharama na makini sana.
Baada ya muda fulani, Japheth akawa ameletwa hapo pamoja na mlinzi wake, yaani askari aliyetakiwa kumlinda alipokuwa amewekwa kwenye kifungo cha nyumbani, ingawa siyo nyumbani kabisa alikoishi (wanajua wenyewe wanakowapelekaga). Hii ilikuwa ni kwa sababu mwanasheria wake aliyepita aliomba apewe kifungo cha namna hiyo badala ya kumweka rumande, kwa hiyo hapo akawa amefika na kuwakuta wengine wameshatulia. Kwenye upande wake alikuwepo baba mkubwa wake, dada yake, mdogo wake wa kike, na marafiki wachache pia. Akakalishwa upande huo kwenye meza ya mbele, na askari wake akasimama pembeni. Bado, mpaka kufikia wakati huo, mwanasheria aliyetakiwa kumsimamia hakuwa amefika.
Namouih akamgeukia Blandina na kumuuliza ikiwa alikuwa ana taarifa yoyote kuhusu mwanasheria mpya wa Japheth, lakini rafiki yake akakanusha. Hivyo wakaendelea kusubiri tu mpaka wakati ambao hakimu aliingia hapo na kwenda kuketi kwenye kiti chake kule mbele, na watu wote walikuwa wamesimama mpaka alipokaa ndiyo nao wakakaa. Sasa msomaji wa kauli za mahakama (clerk) akawa amemwambia hakimu kwamba mwanasheria wa Japheth hakuwa amefika bado, na hakimu huyo akamuuliza Japheth mwanasheria wake alikuwa wapi.
Kijana huyo akasema mwanasheria wake alikuwa anakuja, hivyo wasubiri tu kidogo. Hakimu akaeleza wazi kwamba muda uliokuwa umepangwa ulitakiwa kufuatwa kwa sababu kuna kesi zingine zilihitaji kuendeshwa hapo kwa hiyo hawakuwa na muda wa kupoteza. Japheth hangeweza kujisimamia mwenyewe, kwa hiyo kama mwanasheria wake asingekuja inamaanisha kesi hii ingeamuliwa kwa kumpa hukumu kwamba ana hatia ya kubaka. Haya yote yangeepukwa kama angekuwa amekubali mwanasheria mwingine ambaye angeteuliwa mapema kwa ajili yake baada ya yule wa mara ya kwanza kupatwa na dharura, kwa hiyo huo ndiyo ungekuwa mwisho wa mambo haya yote.
Namouih akawa amekerwa sana na usumbufu wote huo alioona tokea mwanzo kabisa kwamba ungewafikisha huku. Kujiandaa kote halafu mtu anashindwa kuonyesha msimamo ni jambo lililomfanya akerwe sana, lakini mwisho wa siku ushindi ungebaki kuwa wao kwa hiyo....
"Samahani mheshimiwa... samahani kwa kuchelewa..."
Wote waliokuwa hapo wakageuka nyuma baada ya kusikia maneno hayo yakisemwa kwa sauti ya juu. Milango ya kuingilia ndani hapo ilikuwa wazi, na hapo aliingia mwanaume aliyevalia suti nyeusi huku akiwa ameshikilia begi dogo la mkononi, siyo la mgongoni. Blandina aligeuka vizuri zaidi na kubaki amemwangalia kwa umakini sana, naye Namouih alipogeuka na kumwona, akabaki kumtazama kwa umakini pia kadiri alivyoendelea kupiga hatua kuelekea mbele. Walimfahamu. Alikuwa ndiyo yule yule kijana ambaye asubuhi ya siku ya Jumapili wakati wawili hao walipotaka kwenda kumpa pole rafiki yao, yule Mwantum, Blandina alijigonga kwake na kupasua chupa, kisha mwanaume huyo akamnunulia nyingine na kuchukua namba zake; yaani Draxton!
★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★
Comments