Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Ni5 muda wa saa moja za jioni ndani ya soko la Mbagala Rangi tatu pilika pilika zilionekana kuwa nyingi sana kwa wafanya biashara , kwani muda huu kwa  wafanya biashara wengi ndani ya soko hili ndio muda ambao walikuwa wakifunga biashara zao na kurudi majumbani , hususani wale waliokuwa wakifanya biashara za nguo na vyakula.

Kikawaida ndani ya hili soko   wafanyabiashara wengi walikuwa wakihifadhi mizigo yao sehemu salama  kwa wale ambao walikuwa na mizigo mikubwa ambayo  hawakuwa na uwezo wa kurudi nayo nyumbani ,  ambao pia  hawakuwa na maduka maalumu ya kufanyia biashara , hivyo mara nyingi  hulazimika kuhamisha mizigo yao kutoka eneo wanalo fanyia biashara mpaka sehemu ya kuhifadhia.

Kazi hii ya  uhamishaji wa mizigo ni  kubwa  kwa wafanyabiashara hivyo huomba msaada kwa waendesha  mikokoteni na wabeba mizigo kuwasaidia kuhamisha  huku wakiwalipa kwa kiasi cha mizigo wanayobeba.

“Roma  njoo  leo unisaidie kubeba mizigo yangu basi nikahifadhi muda umeenda sana” aliongea mwanamama mmoja hivi mweupe wa wastani mnene aliekuwa akifanya biashara ya kuuza   madela , vijoli pamoja na viatu vya kike ndani ya soko hili  la Rangi tatu.

“Mama Nasra wala hata usiwaze , nitakuhamishia haraka haraka maana nina  kazi pia ya kuhamisha na mzee Saidi”.

“Haya mwanangu nashukuru sana”Aliongea mwananamama huyu huku akimuonesha Roma mizigo ya kuingiza kwenye mkokoteni wake kwa ajili ya kwenda kuhifadhi sehemu husika.

Ndani ya dakiika kadhaa tu Roma alikuwa ameshamaliza kazi ya   kuhamisha mizigo yote ya kibiashara ya Mama Nasra  na  kulipwa buku lake na sasa alikuwa bize na kuhamisha mizigo ya Mzee Saidi , ambaye alikuwa ni muuza Viatu vya mtumba.

Uchapakazi  na uaminifu wa Roma ulikuwa ukiwafurahisha sana  wafanya biashara wengi sana  wa soko hili kiasi cha kupelekea mara nyingi kumtaka Roma awasaidie kila linapokuja swala la kubeba mizigo kuitoa sehemu moja kwenda nyingine , alikuwa akifanya kazi kwa haraka sana  , kiasi ambacho hata  wenzake abao aliokuwa akifanya nao kazi hio hio walikuwa wakimshangaa kwa uwezo na nguvu alizokuwa nazo Roma .

“Kijana Asante sana kwa  kuhamisha kwa haraka haraka maana nina dharula”

“Usijali mzee wangu” Aliongea Roma kwa kuweka tabasamu usoni  mwake na kisha alipokea noti yake ya shilingi elfu mbili  na kisha kuingiza mfukoni.

Mpaka kufikia muda wa saa  nne za usiku Roma alikuwa amesomba bidhaa nyingi za wafanya biashara na kwenda kuzihifadhi na sasa alikuwa amekaa kwenye moja ya meza tupu  iliokuwa  haina kitu akihesabu hela zake.

“Hatimae nimeingiza Elfu kumi na tano , ni kiasi kikubwa sana hiki kwa leo , ngoja nikale ugali na nyama ya Mbuzi kwa  mama Joshua nisepe home nikalale”Alijiongelesha Roma huku akinyanyuka mahali alipkuwa ameketi na kusogelea mkokoteni wake na kuuweka pembeni sehemu ambayo mara nyingi  anauhifadhi yeye pamoja na wenzake mpaka siku inayofuata .

“Oy mwanaa , leo umepiga kazi sio poa”.

“Kawaida tu   Juma  , japo ni kweli siku ya leo haikuwa kama jana”Aliongea Roma  akiongozana na rafiki yake Juma  wakielekea uelekeo mmoja . Juma ni rafiki yake  Roma wa muda na walikuwa wakifanya kazi pamoja , utofauti wa Juma na Roma ni kwamba Juma yeye alikuwa ni mwenyeji  wa jiji hili la Dar es salaam , akiwa amezaliwa ndani ya  jiji hili na  Roma alikuwa na muda wa miezi sita tu tokea aingie ndani ya jiji hili  la Dar es salaam kutokea  mikoani na alikuja  ndani ya jiji la Dar kama moja ya vijana wengi wanaokuja kwa kisingizio cha kutafuta maisha.

Roma alikuwa ni mrefu wa wastani  , mwenye mwili uliokuwa umejengeka vyema kimazoezi  , hakuwa handsome sana  wala hakuwa mwenye sura mbaya , alikuwa ni wale wanaume ambao walikuwa wakionekana kawaida sana katika macho ya wengi  na moja ya sababu kubwa iliompa Roma umaarufu ni kutokana na uchapaji kazi wake ndani ya soko hili la  Rangi tatu.

Baada ya marafiki hawa kuvuka upande wa pili wa barabara hatimae walikuwa ndani ya mgahawa wa Mama Joshua kwa ajili ya kupata chakula cha  usiku  , waliungana na wenzao wengi waliokuwa ndani ya eneo hilo na kuagiza  chakula huku wakiendelea  kupiga stori za hapa na pale  ili mradi kunogesha maongezi yao.

“Oya Wadau leo  Club B kuna bonge la  Party ,  leo ni full bia   nusu bei”Aliongea  jamaa mmoja  mbeba mizigo aliekuwa maarufu sana ndani ye eneo hili la Rangi tatu aliekuwa akifahamika kwa jina la Yusuph.

“Tukitoka hapa lazima tukatembelee eneo hilo, ila hio parti inahusu nini?” aliuliza jamaaa mmoja mwembamba hivi.

“Mrembo Rose leo ni siku yake ya kuzaliwa na  kuna bosi anaetoka nae hapa town ndio kaamua kumfanyia bonge la sherehe”.

“Kama ni hivyo hapo ni sawa kwa sisi kwenda kutembelea , au unaonaje  Roma “ aliongea Juma akionekana ni mwenye kufurahia tukio hilo linalokwenda  kutokea kwani alikuwa ni mwenye kupenda sana kunywa bia hasa zile za ofa.

“Nyie  mtatangulia mimi nitarudi Getto kwanza nikaoge then nitaungana na ninyi”

“Ahaaa.. mzee unazingua , hapa hata sisi tutaenda kuoga kwanza ndio  turudi  kwenye Parti”aliongea Juma na kuwafanya wengine wote wamsapoti.

Naam ni  muda wa lisaa limoja tu  Juma akiwa ameongozana na Roma walikuwa mbele ya nyumba iliokuwa na  geti jekundu Mbagala Biasi pembezoni kabisa na kilipokuwepo kituo cha Tanesko , taa kubwa  za kituo hiki ziliwamulika na kufanya waonekane vyema kwa wapiti njia , kwani licha ya kwamba muda ulikuwa umeenda sana , lakini bado pilikapilika za watu wa eneo hili  zilikuwa zikiendelea.

 Baada ya kusimama kwa    madakika kadhaa  hatimae mlango mdogo wa geti hilo  ulifunguliwa na mwanadada mmoja mrembo  aliekuwa amevalia shungi  na kuwakaribisha ndani.

“Najma vipi , ulikuwa umelala mbona umechelewa kfungua mlango?”.

“Hapana nilikuwa  chumbani na hata sikusikia” aliongea mwanadada huyu kwa sauti yake iliokuwa  ikisikika vyama na kisha alimwangalia Roma na kumsalimia.

“Roma mambo”

“Poa Naj , habari za siku nzima”.

“Safi tu”

“Oya Roma kajiandae chap tuondoke   muda unakwenda wenzetu watatangulia kufika” aliongea Juma ilimradi tu akatishe maongezi  yaliokuwa yakiendelea kati ya Roma na Najma .

Najma alikuwa ni  mdogo wake  Juma , alikuwa akiishi ndani ya nyumba hio ambayo ilikuwa ni  yakwao walioachiwa  ya urithi  , ilikuwa ni nyumba kubwa tu ambayo ilikuwa  wameigawa nusu  wapangaji na nusu walikuwa wakiishi  yeye pamoja na kaka yake.

Najma alikuwa akifundisha   shule ya chekechea eneo moja lililokuwa likifahamika kwa jina la Kiramba, licha ya kwamba alikuwa akilipwa ujira mdogo , lakini alikuwa pia akionekana kuipenda kazi yake hio ya ufundishaji.

Tokea siku ambayo Roma anafika ndani ya nyumba yao na kupanga , Najma alitokea  kumpenda Roma, Najma alikuwa  si mwenye furaha asipomuona Roma  , na kutokana na shughuli za kaka yake na Roma kuwa  ni za kuwaruhusu kurudi usiku na kudamka asubuhi asubuhi , hivyo mara nyingi alikosa  muda wa kuonana na Roma , hali ambayo ilimfanya kuhakikisha  kila siku yeye ndio anaewafungulia  mlango kila wanaporudi kutoka  kazini.

Licha ya Najma kumpenda Roma kwa kaka yake ilikuwa ni tofauti , hakupenda kabisa Najma kujihusisha kimapenzi na Roma kabisa na hii yote ilisababishwa na hali ya kimaisha  aliokuwa nayo  Roma  ,Juma alimuona Roma kama mtu ambaye hakuwa  na malengo na maisha yake , hivyo aliona kitendo cha dada yake kuingia  katika mapenzi na Roma dada yake asingefika mbali kimaisha na angeendelea kuishi katika hali ya maisha duni jambo ambalo hakuwa akitaka litokee kwani aliamini kwa uzuri aliokuwa nao dada yake ,  kama ni kupata mwanume  mwenye pesa na kumuoa lisingekuwa jambo gumu , lakini asiliolijua Juma ni kwamba ni wanaume wengi sana walikuwa wakikataliwa na  Najma  licha ya kutaka kumhonga pesa nyingi na hata kumuahidi kumuoa ,mlimbwende huyu alikuwa amekufa na kuoza kwa mwanaume ambaye hakuwa na chochote cha kutishia jamii , mwanaume wa  kawaida sana  na maskinini mpangaji wao  anaenda kwa jina la Roma.

Katika akili ya mwanadada huyu mrembo Najma aliamini siku moja Roma atamtamkia  tu kuwa  anampenda na yeye pia atamkubali na watayaanza maisha yao pamoja  ,  hio ndio Imani aliokuwa nayo Najma juu ya Roma.

Kwa upande wa Roma alikuwa akijua fika kuwa Najma alikuwa akimpenda sana  kimapenzi , lakini  pia alikuwa akijua sana kwamba Juma hakuwa akitaka dada yake kutoka na yeye kimapanzi kutokana na hali yake ya kimaisha  , hivyo licha ya yeye kumuona  Najma kama mwanamke mrembo ambayey yeye kama mwanaume rijali anapaswa kuwa naye katika mahusiano , lakini alijitahidi sana kujizuia kumuonyeshea mapenzi mwanadada huyo , kwani  hakuwa ni mtu mwenye kutaka ugomzi na rafiki yake Juma , kifupi alikuwa amependa sana  chumba alichopanga   ndani ya nyumba hii ya Roma na dada yake.

Basi baada ya  Roma na  Juma kujiandaa na kubadilisha nguo hatimae walitoka kwa kupitia geti dogo na kisha kutoka ndani ya nyumba hio na kuelekea uelekeo wa Club B , kutoka Bias mpaka ilipokuwa  ikipatikana Club B hapakuwa mbali sana  , Club hii ilikuwa ikipatikana  Chalambe  nyuma kidogo kabla haujafika sehemu iliokuwa ikifahamika kama  Maji Matitu , ilikuwa ni moja ya Club kubwa sana  na ya kuvutia  iliokuwa ikipatikana ndani ya eneo hili , lakini pia ilikuwa maarufu sana kiasi kwamba ilikuwa ikitembelewa na watu waliokuwa wakiishi ndani ya  mji huu  pamoa ambao waliokuwa wakiishi nje ya eneo hili , ikiwemo Chamazi , Temeke , Kisemvule na baadhi ya meneo ya karibu.

“Wadau mmechelewa sana   tena Sanaa yaaniii ….. bia ya tatu hii”Aliongea Yusph huku akigida bia yake kwa mbwembwe iliokuwa na chapa la Safari Lager .

“Usijali Yusuph tutakufikia  tu “Aliongea Juma huku akiangaza macho huku na  kule akikagua mandhari ya hapa ndani na hata kwa upande wa  Roma hivyo hivyo.

“Siku hii ya leo watu walionekana kuwa wengi , kwani makelele yalikuwa mengi  , huku harufu ya Pombe ikiwa imetapakaa kwa hali ya juu ndani ya eneo hili.

“Handsome Boys karibuni niwahudumie”Ilikuwa ni sauti moja nyororo iliosikika kwa vijana hawa na kuwafanya wamuangalie aliekuwa akiongea  na hapo kila mmoa alitoa macho ya uchu baada ya kumuona mwanamke wa haja. Mrembo alievalia suruali ya kitambaa iliomchora vyema umbo lake namba nane , mwanamke huyu  alikuwa ni mzuri kweli  , si kujaliwa tu shepu lakini pia alikuwa  amejaliwa sura  nzuri yenye urembo wa asili ambao huwafanya  wapenda ngono wengi kummezea mate.

“Aaaaa..hhh Sister Rose sjijatarajia  kukuona leo ukihudumia bhana”Aliongea Juma kwa mshangao na kumfanya Rose kutabasamu huku macho yake yote akiwa ameyaelekeza kwa Roma ambaye alionekana kama mtu ambaye hakuwa na habari na mtu aliekuwa mbele yake kwani alikuwa ni mwenye kukagua kila mtu aliekuwepo ndani ye neo hilo kama jasusi anaetafuta adui.

“Mimi nipe Safari  kama Broo wangu yusuph hapo , nipe ya baridiii”Aliongea Juma huku akikaa vizuri kwenye viti hivyo virefu huku akiwa amechia tabasamu pana usoni mwake.

“Na wewe Roma  vipi leo” Aliongea huku akimwangalia Roma kwa madaha kiasi kwamba wenzake wote walikuwa wakimuonea wivu  kwa kuangalia na mwanamke mrembo kama Rose kwa staili hio.

“Nataka ofa  leo , nipe Heinken  gharama ni juu yako”Aliongea Roma pasipo kupepesa macho na kumfanya Rose atabasamu na kisha kumwambia asijali anamletea na atalipia kwa kila kinywajia atakachokunywa kwa siko hio , jamboa mbalo liliwafanya marafiki zake waone ni upendeleo , lakini wala Rose hakuwajali.

“Oya mwanangu Roma huyu Manzi anakukubali sana kitambo tu ,  nashangaa mzee huchangamki , au unaogopa ni  vya wakubwa”Aliongea  jamaa mmoja aliekuwa pembenni   ya yuspuh ,jamaa huyu alikuwa akifahamika kwa jina la Samia.

“Kweli kabisa Samia , Manzi anamkubali sana Mwamba hapa , lakini jamaa  anazembea  zembea , ningekuwa mimi ningekuwa nisharekebisha tayari na hapa ningekuwa nakunywa bia fulu fulu bureeee”Aliongeezea  Yusuph na muda huo huo alikuja Rose na kuweka vinywaji huku akimpatia kinywaji  Roma.

“ Bebi kuna ,mbuzi choma  nikuleteee”  wote waliangaliana kwa macho  ya kimshangao na ya kutamani kile kilichosemwa , lakini hawakuambiwa wao , mtu aliekuwa amepewa ofa hio alikuwa ni Roma.

“Kweli mama leo umezaliwa upya  , kama ni ofa  mimi sina tatizo na nipo tayari kwa kila ofa inayopatikana”Alionea Roma .

“Ofa nyingine hautaweza , siku zote umekuwa ni wa kunikimbia” aliongea Rose kwa kumnong`oneza Roma na kumfanya atabasamu  , kwani alikuwa akijua alichokuwa akimaanisha Mrembo huyu.

Huu usiku kama walivyotegemea  vijana hawa ndio kile walichopata , kwani walilewa chakalii kwa  bia za ofa ambazo zilikuwa zimetolewa na  kibosile ambaye  ilikuwa ikiaminika alikuwa akitoka kimapenzi na mwanadada Rose.

Baada ya  masaa matatu baada ya  ya keki kukatwa  na sherehe kukaribia kumalizika , huku waliokuwa wakiendelea kula mziki na kunywa bia wakiendelea , alikuja  jamaa mmoja  aliekuwa mhudumu wa hii Club na kumpa kijimemo Roma, ambaye  licha ya kunywa bia nyingi alionekana kuwa ngangari kuliko wenzake wote , baada ya kufungua  kimemo hiki , alitabasamu na kisha alinyanyuka na kuoelekea nje , na kukata kushoto na ndani ya dakika chache alikuwa nje ya chumba na kugonga  , na mlango ulifunguliwa na mrembo Rose aliekuwa amevaa khanga moja tu, alionekana  alikuwa ametoka kuoga.

“Karibu Mpenzi”Aliongea Rose kwa namna ya kudeka huku akimvuta Roma ndani  na kuzama mzima mzima .

Next