Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Siku;tatu zilikuwa zimepita  pasipo ya Roma kuonana na Najma  , jambo ambalo halikumshangaza kwani alikuwa akikumbuka vyema kuwa  Najma alimuona mwanamke kahaba alielala nae siku mbili zilizopita , hivyo alijua fika kuwa   mrembo huyo atakuwa na hasira kali sana juu yake , kwani alikuwa akijua  sana kwamba alikuwa akimpenda , hivyo hata yeye hakutaka kujishugulisha sana juu ya Najma , kwanza aliona ni jambo zuri kwani  angejiweka mbali na Najma.

Upande wa Juma pia jambo hilo lilimfurahisha sana , kwani aliamini kwa jambo ambalo Roma amefanya litamfanya dada yake kutomfikiria kabisa Roma na kuendelea na  maisha yake huku akimtafutia mpango wa kueoelwa na mwanamke mwenye pesa zake  na ili kuhakikisha Najma hafikiriii kabisa  kuendelea kumpenda Roma alifanya kila njia kuhakikisha  taarifa za Roma kulala  na kahaba mpaka asubuhi zinasambaa ndani ya wapangaji pamoja na  majirani.

“Mh!  Roma kabisa … siku zote nilikuwa namuona kama anamatatizo flani hivi kumbe anaonekana  na yeye anapenda wanawake . lakini alishindwa nini kumchuku Najma   mwanamke mrembo mpaka kwenda kuchukua mwanamke kahaba mtaani”

“Heheee… huenda Najma  kuna kitu anakosa katika mwili wake ambacho hakimvutii Roma” Hao walikuwa ni wapangaji waliokuwa wakiongea kishambenga wakiwa wanasukana , na yote hio ilikuwa ni kumuumiza Najma ambae alikuwa akiingia kutoka kazini  , na Najma aliwasikia vizuri tu  na kuzidi kumchukia Roma kwa kitendo cha  kuleta kahaba kwenye nyumba yao.

Najma alionekana ni mwenye mawazo , mengi mno  , lakini licha ya hayo yote ambayo yalikuwa yakiendlea kwa wapangaji ,  moyo wake ni kama umegawanyika vipande viwili , kwani kuna upande ulikuwa bado ukimpenda sana Roma na hakuwa tayari kumuacha  , lakini pia  kuna upande ambao ulikuwa  ukimchukia sana Roma, Pande zote mbili zilionekana kushindana vikali sana , huku upande unaompenda Roma ukichukua ushindi kila baada ya pambano., baada ya upande huo kushinda kila mara , hamu ya kutaka kumuona Roma ilizidi kujaa katika moyo  wake , alikuwa amemkumbuka sana  na  alipanga usiku  wa leo kumuona kwa namna yoyote ile.

Muda nao haukukawia sana   kwani ulienda kwa  haraka haraka , kwani ile Najma anakuja kushituka kutoka usingizini ilikuwa ni saa  kumi na mbili  , alinyanyuka haraka haraka na kisha alielekea gengeni kununua mboga za usiku  , na siku hio alipanga kupika  wali na Choroko , hivyo alinunua choroki na kuzichemsha na kuanza kuandaa chakula cha usiku.

“Noja leo nipike kingi , nitamuwekea Roma wangu katika chumba Chake akirudi  ale”Alijiongelesha mwenyewe wakati huo akichambua mchele.

“Vipi mwenzetu mbona leo unaonekana ni mwenye furaha hivyo”Aliuliza mama Debora moja ya wapangaji  , huku akimwangalia Najma usoni, Mama Debora ndio mpangaji pekee ambaye hakuwa na umbea mwingi na alikuwa ni Mlokole katika kanisa  flani lililokuwa mita chache kutoka nyumbani kwa  Najma  na pia ndio mpangaji pekee aliekaa kwa muda mrefu mno , kwani yeye pamoja na  mume wake walianza kupanga hapo kwao tokea wakianza kuona na mpaka sasa ambapo walikuwa na  mtoto mkubwa tuambaye alikuwa chekechea  anaefahamika kwa jina la Debora ,Mama Debora hakuwa mtu wa Nyumbani sana kwani alikuwa akifundisha  shule ya msingi  Ikwiriri , sehemu ambayo ilikuwa mbali na kumfanya kudamka sana asubhi na kurudi jioni , hivyo hakuwa akijua maswala yoyote yaliokuwa yakimuhusu Roma kuingiza kahaba.

“Hakuna  jipya mama Debo , ni ile tu leo nimejikuta kuwa ni mwenye furaha”Aliongea Najma na kumfanya Mama Debo atabasamu.

“Hehehe .. acha kunificha Roma kakutamkia  anakupenda nini?” Najma aliona aibu kwa sentensi hio na kuzidisha tabasamu .

“Nilijua tu , unaonekana kumpenda sana Roma Najma”

“Hhaha .. ndio”

“Muone sasa anavyoona aibu … nimekuja kuweka umeme mimi”Aliongea Mama Debo huku akimpita Najma na kuingia ndani  kwa ajili ya kuweka umeme kwani Luku ilikuwa kwa ndani.

Najma alidumu sebuleni kwao kwa muda mrefu sana huku akiwasubiria kaka yake na Roma kurudi  kazini  licha ya kwamba alikuwa na usingizi mzito  uliokuwa ukimnyemelea  , lakini hamu yake  ya kutaka kumuna Roma iliushinda usingizi na kuendelea kusubiri , siku hii ya leo  si kama  siku zingine kwani  walichelewa kurudi mno , kwani mpaka inafika saa tano na nusu  kaka yake hakuwa amerudi , baada ya kusubiri kwa takribani   dakika ishirini hatimae  mlango uligongwa na Najma haraka haraka alikwenda kufungua mlango.

“Najma hujalala tu , leo mbona umekua  kunifungulia  wewe”Aliongea Juma huku akiwa ni mwenye kumshangaa dada yake ,kwani siku mbili za nyuma alionekana sio mwenye kujali kuwafungulia yeye na Roma.Kwa Najma licha ya swali hilo , hakujali kabisa kwani alichokuwa akitaka kuona  ni Roma Tu , lakini  kilichomshangaza ni kwamba siku hio alimuona kaka yake  pekee jambo ambalo lilimshangaza.

“Roma yuko wapi kaka , mbona  haingii”

“Nilijua tu  unataka kumuona Roma”Aliongea Juma huku akiweka uso wa hasira na kumpita baada ya kufunga mlango , lakini Najma hakuridhika alifungua mlango na kuangalia nje lakini Roma hakuonekana , jambo ambalo lilimfanya kuwa katika hali ya maswali , alifunga mlango na kukimbilia ndani.

“Kaka Roma yuko wapi , mbona hujaja nae”.

“Bwana eeh usiniulize maswali yako mimi , kwani umeona natembea nae mfukoni”Aliongea Juma na  alikerwa sana na maswali ya mdogo wake , na  aliona kabisa   si kama alivyofikiria  kuwa Najma alikuwa ashaachana na Roma baada ya kumuingiza kahaba geto kwake, alikula chakula alichowekewa na mdogo wake huku akitabasamu kwa kuona kuwa mdogo wake anajua kupika na baada ya kushiba aliignia kwenye chumba chake na kujilaza.

“Najma akiolewa na mimi naoa , nyumba yote  inakuwa yangu na ili hili litimie sitaki Najma aolewe na Roma maana nina uhakika kwa maisha ya Roma atataka aishi na Najma hapa hapa”Alijiongelesha huku akiwa amejilaza na kukodolea macho taa mpaka pale alipopitiwa na usingizi pasipo ya kuzima taa.

Upande wa Najma  yeye hakuweza kupata usingizi kabisa , muda wote masikio yake yalikuwa kwenye geti tu , ili asikie  geti likigongwa ili akamfungulie Roma , lakini muda ulizidi kwenda , lakini alichokuwa akitegemea hakikuweza kutokea kabisa, baada ya kuona atasinzia alienda  kusbiria Sebleni  mpaka pale alipokuja kupotelea usingizini  , na  alikuja kushituka kukiwa kumekucha kabisa  na hii ni baada ya kaka yake kumkuta  Najma akiwa Sebleni, alijikuta hasira zikimpanda baada ya kuona dada yake kalala hapo sebleni  na kung`atwa na mbu huku akimsubiria fukara Roma arudi.

“Huyu mpuuzi akirudi leo na mfukuza akapange kwingine , kwa hali hii  Najma hawezi kuoelewa”Aliongea Juma na kisha alitoka mpaka vyumba vya nje vya wapangaji na  kwenda kwenye chumba cha Roma na kukifungua  na kuingia , ndani  na kitu cha kwanza alichoona  ni mabakuri  mawili makubwa ambayo alikuwa akiyafahamu yakiwa kwenye  kijimeza , aliyasogelea na kisha kufungua bakuli la kwanza na hapo nipo alipotoa macho huku sura yake ikianza kujikunja.

“Yaani huyu mpuuzi anamuwekea Roma mapaja ya kuku halafu mimi kaka yake ananiwekea  wali na Choroko, hii haiwezi kuendelea hivi”Aliongea  Juma kwa hasira huku akinyanyua yale mabakuli  na kutoka nayo nje  huku akipishana na Najma ambaye alimkata jicho , baada ya dakika chache Juma alitoka akiwa na kufuri lingine na kisha alifunga mlango wa Roma na kisha  kurudi ndani na kupasha kiporo kile na  kula.

Wakati yote hayo yakiendelea Najma ambaye alikuwa kwenye hali ya wasiwasi , alikuwa akimwangalia kaka yake tu , huku akiogopa hata ya kumuuliza chochote kuhusu Roma  alipo , baada ya kusimama nje kwa  dakika kadhaa , Juma alitoka nje  huku akionekana safari ya kwenda kazini kwake ikiw aimewaidia.

“Kaka  najua umekasirika lakini naomba uniambie Roma yuko wapi”.

“Usiniulize maswali ya kupuuzi na , kwa upendo wako wa kijinga jinga  Roma kwanzia leo   akirudi anaenda kutafuta chumba kwingine  na nisikie fyoko fyoko uone”Aliongea Juma  huku akiweka kibakrashia chake  vizuri na kutoka huku mlango wa geti ukiipigiza kwa  nguvu.

“Halafu huyu Mpuuzi kaenda wapi , tokea jana mchana  sijamuona tena  alipofuatwa na yule mtu  mwenye suti”

****

JANA YAKE  SAA SABA MCHANA

Roma mpaka kufikia muda wa Saa saba mchana alikuwa amepiga kazi kubwa sana ya kuteremsha  mizigo ya Cement , kwenye Duka kubwa la vifaa vya ujenzi la Bozi , yeye pamoja na wenzake walikuwa wamechafuka mno kiasi  kwamba hawakuwa  wakitamanika , lakini wala hawakujali sana  , kwani kwao pesa ilikuwa ndio kila kitu.

Njaa nayo haikuwaacha salama , na baada ya kupewa ujira wao , Juma aliwaongoza wenzake kuelekea upande wa pili wa barabara   ili kwenda kujipatia chakula cha mchana kwa  Mama Joshua. Kama ilivyokuwa desturi yao.

Baada ya dakika kadhaa tu  Roma alikuwa  ndio alikuwa mtu wa mwisho kunawa mikono  , alianza kunawa uso ili kutoa vumbi la Cement na kisha  alimalizia mikono , lakini ile anamaliza tu mita kadhaa kwenye barabara kuu , ilisimama gari aina ya V8 nyeupe  , gari ambayo iliwafanya baadhi ya watu kuikodolea macho .

Baada ya gari hii kusimama  , alitoka mwanadada mmoja aliekuwa  amevalia suti ya rangi ya  bluu na viatu vya rangi  ya Pink ,  mwanadada huyu alitoa picha kwenye mkoba wake na kisha aliangaza kulia na kushoto huku akitoa simu yake iliokuwa ikiita na kisha kuiweka sikio mara baada ya kuipokea na baada ya maongezi machache alikodolea upande  wa kimgahawa cha Mama Joshua  huku akikagua mtu mmoja mmoja na baada ya kuona kile alichokuwa akitafuta alisogea kuelekea upande huo wa mgahawa ,. Huku baadhi ya watu wakishangazwa na urembo na  shepu ya mwanamke huyo , lakini hakuna aliekuwa  ni mwenye kujali.

“Habari yako kaka”Aliongea mwanamke huyu kwa sauti ya kujiamini kabisa na kuwafanya wakina Juma na wenzake kushangazwa na kitendo hicho , kwani mtu aliekuwa akisalimiwa alikuwa ni Roma.

“Salama”Aliitikia Roma pasipo kujali uzuri wa mwanamke aliekuwa mbele  yake na kusogelea meza  ya plastiki ya rangi ya bluu na kuketi kwenye kiti huku  mrembo huyu kuonesha kuchukizwa na kitendo cha Roma kutokumuangalia usoni , licha ya kumsemesha  , kwake alitafsiri kama dharau kubwa ambayo ameonyeshwa kwa mwaka huo , yaani katika  maisha yake na urembo wake , hakuwahi kudharauiwa na mwanaume wa aina yoyote ile , lakini kwa Roma ilikuwa tofauti  na  hio aliingiza katika Top Ten ya dharau alizowahi kuonyeshwa katika maisha yake, lakini licha ya hivyo , mwanadada huyu bado alionekana kuwa ni mwenye shida ya kuongea na Roma kwani alisogea mpaka kwenye meza aliokuwa amekaa Roma na kumwangalia  kwa  kumshusha kwa mavazi yake  ya kimasikini na uchafu uliomjaa.

“Mama Joshua   nipe ugali mkubwa na Samaki “Aliongea Roma  na kuwafanya marafiki zake  wazidi kumshangaa Roma  kwa kitendo hicho cha kutokujali , licha ya kuongeleshwa na mwanamke mrembo kama huyo ambaye kwao , ilikuwa ni kama ndoto kupata bahati ya kuongeleshwa na mrembo kama huyo.

“kaka nimekusalimia”

“Ooh !,, sorry sister , nilikuwa bize kidogo , kumbe ulikuwa ukiniongelesha mimi”.

“Ulifikiri na muongelesha nani , au dharau tu  kaka yangu , sio vizuri”Aliongea mwanadada huyu kwa sauti yake ya kuvutia huku akionekana amekereka kweli kwa kitendo cha Roma kujifanya hakumsikia wakati wote huo aliokuwa   anamsalimia , na kilichomkera Zaidi mwanadada huyu ni kutokana na watu  waliokuwa  wakimwangalia , alichokuwa ametegemea mwanamke huyu ni Roma kumnyenyekea , lakini swala hilo likawa nje ya mategemeo yake na kumfanya yeye ndio aonekane mwanamke mwenye shobo na katika  baadhi ya watu waliamini huenda huyo mwanadada alikuwa ni demu wake.

“Ulikuwa unasemaje sista”.

“Wewe si ndio Roma”

“Ndio ni mimi”

“Basi naomba utangulizane na mimi kuna mtu muhimu sana anataka kuonana na wewe”Aliongea  mwanadada huyu na kuwafanya  watu wote waliokuwa hapo mgahawani kushangazwa na maneno hayo , ila kwa Roma hakuonekana ni mwenye kushangaa sana  , kwani alipokea chakula chake na kuanza kula.

“Sister naomba ukae , kwanza unisubirie nimalize  nipige  msosi  ndio tuongee maswala ya mtu Muhimu .. maana hii ni moja  ya starehe yangu na mara nyingi ni kila  sipendaki kusumbuliwa”Aliongea  Roma kwa kujiamini huku akianza  kumega  bonge la tonge na kulichovya kwenye mchuzi na kisha kulimeza lote , kitendo ambacho kilimshangaza sana huyu mrembo , na kumkera kwa wakati mmoja.

“Nitasubiri kwenye gari ,  ukimaliza naomba tufutatishane kama nilivyokuambia”Aliongea ule mwanadada pasipo  kusubiri jibu , na kisha kuondoka .

“Halafu we Ms**nge unapenda kuifanyisha matawi ya juu , mtoto mkali kama yule anakuongelesha unajifanya  unaongea kama hutaki  kama  vile  Mondi , vile au unatuoshea tu washikaji zako hapa”Aliongea Yusuph huku akiungwa mkono na wenzake.

“Ila jamaa nimemkubali sana , ile pia ni heshima”:Aliongea  jamaa mmoja ambaye yeye hakuwa muongeaji sana , ila siku hio alionekana kuchangia.

“Hahaha .. Mhando hata wewe leo umechangia mada , inaonekana pia  umeguswa sana na jambo hili”Aliongea Juma na kuwafanya  wengine wacheke maana ni kwa mara ya kwanza kwa Mhando kuchangia mada , yeye alikuwa ni mkimya wa hali ya juu

Baada ya Zaidi ya nusu saa ya Roma kumaliza msosi wake , alipiga maji kwenye kikombe , na kisha alijishika tumbo lake na kujiona kushiba vyema na kutoka mgahawani na moja kwa moja alielekea kweye gari  , na kugonga mlango wa kioo ulioshushwa.

“Ingia kwenye gari”Aliongea mwanadada huyu kwa  sauti iliojaa machukizo   na kwa Roma wala hakujali , baada ya  kuingia kwenye gari  ,  ilitolewa nduki  kuelekea upande wa Kongonwe na kuja kugeuzwa  na kurudi upande wa kuelekea kariakoo.

“Unanipeleka wapi Mrembo”Aliongea Roma  lakini hakujibiwa , Zaidi ya kusonywa  na Roma aliamua kutulia kwenye kiti chake  , huku akifurahia kiyoyozi kilichokuwa kwenye gari hilo, na kutokana na uchomvu aliokuwa nao  , alipitiwa na usingizi  na hata pale alipokuja kushituka alijishangaa akiwa mbele ya jengo refu  mno  maeneo ya Mawasiliano Sehemu ambayo alijua haraka kwani alikuwa  ni mwenyeji wa maeneo hayo , baada gari hii kusimama kwenye jengo hili Geti lilifunguliwa na  gari ile iliingizwa mpaka ndani  na kuegeshwa na kisha mwanamke yule mrembo alishuka .

“Karibuni Grand palace  hoteli wateja wetu”Ilisikika sauti ya muhudumu  iliowakaribisha kwa  tabasamu  na ucheshi wa hali ya juu ,Roma alimwagalia mwanamke huyo aliekuwa amevalia  sare ya hoteli hio na kisha alimkonyeza kitendo ambacho yule mwanadada aliekuja na Roma kukiona na kubetua midomo , lakini kwa  muhudumu alirudisha kwa tabasamu la kuita.

“Watu wenye pesa wanakula maisha sio poa”Aliongea Roma baada ya kuingia kwenye lift huku   akiwa si mwenye kuacha kumkonyeza mrembo huyu ambaye amenuna kama muuza sumu.

Baada ya  lift kufunguka katika  Floor namba kumi na nane , Roma alifuata nyuma nyuma mpaka walipofika kwenye  mlango wa chumba  namba 708 na kisha  huyu mrembo aligonga mlango na ndani ya dakika kadhaa  mlango ulifunguliwa  na mwanaume alievalia suti.

“Karibu  Suzzane”Aliongea mwanaume huyu alievalia suti huku akiwa  ni mwenye tabasamu   lakini pia macho yake hayakuwa mbali na uso wa mwanaume aliekuwa  nyuma ya  Suzzane , mwanaume ambaye kwa macho ya  haraka haraka alionekana kama Fukara.

“Bossi nisharudi na nimemleta”Aliongea mrembo Suzzane  kikakamavu  huku akimwangalia mwanamke aliegeukia  dirishani , akionekana kuangalia nje akiwa amewapa watu wote katika chumba hiko mgongo.

Mwanamke huyu alikuwa amependeza mno kwa vazi lake la suti alilokuwa amevaa ,suti ya rangi nyeupe

“Asante Suzzane , mnaweza kuondoka  m

paka pale nitakapowaita”

“Boss!!”Aliongea Suzzane kwa hali ya wasiwasi .

“Fanya  kama nilivyosema Suzzane”Aliongea mwanadada huyo kwa sauti ya Amri  na kumfanya Suzzane amkate  jicho Roma ambaye alikuwa akikagua uzuri  na ufahari wa chumba hiko.

Licha ya Roma kushangazwa na  ufahari wa chumba hicho , lakini pia sauti ya mwanadada aliekuwa mita kadhaa mbele yake aliempa mgongo ilikuwa ikimsisimua mno , ilionekana kama inamkumbusha mbali sana.

Baada ya Suzzane na mwanaume yule kutoka nje , mwanadada  yule aligeuka  na kumwangalia Roma , kitendo ambacho  kilimfanya  Roma atoe mshangao na   kutamka:

“Kahabaaa…!!!”

Previoua Next