Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Licha ya mzee huyu  kwa Roma kujitambulisha kama Mbeba mizigo , hakutaka kuamini kirahisi hivyo , alipiga simu mahali na kuomba  taarifa ya Roma na  ndani ya dakika chache alitumiwa na kuianza kuisoma huku akionekana ni mwenye kushangazwa na taarifa hio.

“Haiwezekani , kama   hii ni kweli kwanini  afanye kazi inayomshusha hadhi yake, hata kama  hii ripoti ni sahihi  siwezi kukubali Edna aolewe na mwanaume kama huyu  ,Edna ni mtu mkubwa haendani na huyu mpuuzi isitoshe  nikiruhusu ndoa hii nitakuwa kwenye wakati mbaya na City Master ”Aliongea mzee huyu huku akikaa chini kwenye sofa huku akiendelea kufikiria.

“Abuu alishindwa vipi kumdhibiti  Edna nilimpa kazi ya kuhakikisha anamuweka kwenye himaya yake na kumuoa ili mipando yetu iende sawa , lakini kakwama katika hili , huenda nilikosea kumchagua kama  mwanaume wa kuwa na mwanangu , Hebu ngoja nimpigie simu huenda hata hili swala halifahamu”Aliongea Baba yake Edna afahamikae kwa jina maarufu kama Mzee Adebe  kifupi cha Adebayoo.

“Abu umeshindwae kumdhibiti Edna… amekuja leo kumtambulisha  Mume wake , huo mpango uliokuwa unajigamba nao uliishia wapi, Vipi swala la City Master tunalikamilishaje?”

“Mzee naomba utulie uniambie vizuri nini kimetokea?”Aliongea Abuu  kwa pupa .

“Muda mchache Edna alikuja nyumbani kwangu na mwanaume aliejitambulisha kwa  jina la Roma anaefanya kazi kama mbeba mizigo  kutoka Rangi tatu na Edna amesema ni  Mume wake kihalali na hataki kusikia ndoa  tena na wewe ,hivi unaniambia  umezidiwa kete na  mtu kama Roma wewe”Aliongea mzee huyu kwa hasira  na upande wa pili wala haukutoa jibu Zaidi ya simu kukatwa.

“My wife , nimejitambulisha vizuri eh”Aliongea Roma huku akimwangalia Venus aliekuwa makini na usukuni , lakini baada ya kutembea hatua kadhaa , alikamata breki na kusimamisha  gari na kisha alimuamuru Roma kutoka kwenye gari yake, na Roma hakuwa mbishi alitoka , na alishangaa kurushiwa kadi  kwa kupitia dirishani.

“Hakikisha saa moja kamili upo  nyumbani  , mahali unapotakiwa kufika angalia kwenye hio kadi ole wako uchelewe ”Aliongea mwanadada huyu kwa hasira na kisha alitoa gari yake hio kwa spidi na kutokomea akimuacha Roma kwenye hali ya mshangao.

“Mwanamke  ana kisirani huyu , au bado ana hasira na mimi ya kumtoa bikra yake”Alijiongelesha huku akiangalia  saa kwenye kijisimu chake na kuona ni saa  kumi na nusu , aliangalia kadi  iliokuwa kwenye mikono yake na kuona mahali ambapo anatakiwa kwenda kwenye makazi yake mapya.

“Mwanamke anadhambi huyu yaani anataka nitembee kutoka  hapa Moroco mpaka Kigamboni”Alijisachi mfukoni na kukumbuka kuwa hakuwa na kitu  mfukoni  kwani nguo  alizokuwa amevaa ni mpya na za  kwake zilizokuwa na malipo  aliziacha kule hotelini.

“Huyu ndio mke wangu niliekubali mwenyewe kumuoa , anamuacha mume wake barabarani , kazi ninayo”Alijiongelesha huku akitembea kwa umbali mrefu mpaka pale magari  yaliposimama kwenye mataa , wakati akiwa anakagua magari hayo mara aliona mwanamke mmoja mrembo akinunua  maji akiwa ndani ya gari aina ya Aud , wakati huu magari yakiwa yamesimama.

Roma alisogelea gari hili na kisha  alisubiria biashara ile iishe atekeleze  jambo lake lililompeleka hapo.

“Hey mrembo ! mambo”Alisalimiana na mwanadada huyo na kujibiwa bila dharau na kuona yupo mahali sahihi.

“Sasa mrembo naomba unisaidie jambo , mke wangu kaniacha njiani na sina kitu mfukoni hata hea ya nauli , naomba unisaidie kiasi chochote nipate nauli ya kunifikisha Kigamboni”Aliongea Roma bila aibu na mwanadada huyo alimwangalia Roma kwa mavazi yake na kuona huenda kuna ukweli ndani yake kwani Suti na kiatu alichovaa  kilionekana cha bei ya juu na ni watu wachache sana  wana uwezo wa kumudu  aina hio ya mavazi.

“Pole kaka hela hii , hapa  nadhani  inatosha”Aliongea mwanamke huyu  na kumpatia noti ya elfu tano Roma na hapohapo  gari zilianza kuondoka na hata Roma alishindwa kutoa shukrani yake , ila alifurahi alikuwa amepata hela ya nauli.

Muda wa saa kumi na mbili na Nusu Roma alikuwa  mbele ya geti kubwa ambalo kwa  ndani  ya fensi hii lilionekana jumba kubwa  la kifahari  ndani ya mtaa huu  uliokuwa ukifahamik kwa jina la Sunlight Villa Hub , ni mtaa ambao hakukuwa na nyumba ya kizembe , majumba yote yaliokuwa yanapatikana ndani ya eneo hili yalionekana kuwa ni ya kifahari  sana na hili lililifanya eneo hili kuwa maarufu kama eneo la Matajiri ndani ya mji huu wa Kigamboni.

Roma aliminya kengere baada ya kuona yupo mahali sahihi na ndani ya dakika , alifungua bwana mmoja mweusi alievalia suti  huku sikioni akiwa na  visikilizishi.

“Wewe ni nani?”

“Mimi ni Roma na ni baba mwenye  nyumba kwanzia siku ya leo a.k.a boss wako mpya ”Aliongea Roma huku akiwa ameweka tabasamu  na kumfanya  mlinzi huuyu ashangae na kuona  chizi wa leo alikuwa wa aina yake.

“Sasa Bosi wangu mpya  kutokana na kwamba wewe ni chizi msafi leo naomba uondoke kimya kimya  kabla sijachukua  maamuzi makubwa”.Aliongea bwana huyu  huku akimwangalia Roma kwa  kumtathimi, lakini wakati  akiendelea kumwangalia  Roma ,mara  alihisi uwepo wa mtu  nyuma yake  na aligeuka .

“Madam Boss..!”Aliongea kwa hali ya mshangao baada ya kumuona Edna   alievalia gauni lililompendeza lililomfikia magotini na kumfanya aonekane kama malaika  kiasi cha mwanaume huyu  mlinzi kumeza mate ya kimatamanio.

“Nani  yupo mlangoni Derick??” Aliuliza  Edna   na kabla Derick  hajajibu alijishangaa akivutwa nje kwa spidi ambayo hakuitarajia  na Roma kuingia ndani.

“Bebi wife ni mimi mumeo nimefika ndani ya muda..hehe bebi usiniambie ulikuwa ukinisubiria??”Aliongea Roma huku akiwa ni mwenye kuweka tabasamu usoni , akinyoosha mikono kuashiria anataka  kumkumbatia , ila Edna hakumjali Zaidi ya kumkwepa.

“Derick huyu ni mume wangu Anaitwa Roma , kwanzia leo ataishi hapa na mumpe heshima yake kama mume wangu”Aliongea  Edna kwa lugha ya kiupole ila iliojaa  usiriasi kuonyesha kile anachokisema.

“Sawa  Madam bosi”Aliitika Derick kwa kubabaika kwani sekunde kadhaa alimdhania mwanaume aliekuwa mbele yake kama kichaa msafi

“Utawaambia na wenzio”Aliongea Edna kwa sauti yake nzuri  na kumfanya Roma atabasamu kwa utambulisho huo na akajiona angalau licha ya mwanamke huyu alikuwa akimdharau ,lakini afadhali alikuwa akimpa heshima yake kama mume.

Derick aliekuwa amesimama  alishangazwa sana na utambulisho huo , kilichomfanya  bwana huyu  kushangaa ni ile hali ya kutokuamini  kwamba mtu kama Roma anaweza kuwa   mume wa bosi wake , kwake Edna alikuwa mzuri  na mrembo  sana kumilikiwa na Roma hivyo matarajio yake ni kuona mtu mwenye hadhi  ya juu Zaidi kuwa mwanaume wa bosi wake , lakini  leo jambo hili lilimshangaza , lakini  hakutaka kujiuliza maswali mengi ,  Zaidi ya kutii  na alipanga kumuomba msamaha Roma pale atakapo pata nafasi ya kufanya hivyo kwa kitendo cha kumuita kichaa.

“Kuna wanaume wamezaliwa na bahati sana , yaani jamaa kama yule ndio anamsugua  bosi daah! Kweli wanawake sio wakuwaelewa kabisa”Alijiongelesha  Derick mpaka pale aliposhituliwa na mlinzi mwenzake.

Roma alikubali uzuri wa nyumba aliokuwa akiishi Edna , ilikuwa ni nyumba kubwa mno kiasi kwamba ilimfikirisha kwa wakati mmmoja kwa  kazi ambayo Edna  alikuwa akifanya  hapa mjini.

Jumba hili lilikuwa la gorofa tatu kwenda juu  , lililokuwa na mandhari  ya kuvutia sana , baada ya Roma kukaribishwa ndani  na Edna alipokelewa na  mama mmoja mtu mzima.

“Karibu sana Mister Roma ”Roma alitikia kwa heshima huku akisubiri utambulisho kutoka kwa mke wake.

“Roma huyu ni Bi Wema ni  kama mama  kwangu , ndio  alienilea tokea nikiwa mtoto  baada ya mama kufariki, Bi Wema huyu ni Roma niliekuambia , ndio mume wangu”

“Karibu sana Roma kwenye familia , jisikie huru hapa ni kwako”Aliongea bibi huyu  na Roma alitabasamu na kukubali utambulisho huo  na Edna hakuwa na maongezi mengi na Roma Zaidi ya kumwachia maagizo yote Bi wema .

“Karibu sana Roma , unaonekana ni kijana wa kipekee sana mpaka Miss Edna akakuchagua  kuwa mume wake , niseme tu mimi nimemuona Edna tokea akiwa mtoto na  hajawahi kutambulisha mwanaume yoyote kwangu  kuwa nae kimahusiano , Edna amekuwa ni mtoto mpweke sana ambae amekuwa peke yake mpaka pale aliporithishwa kampuni na marehemu mama yake, hivyo nakuomba usije ukaamuumiza”Roma alipewa nasaha hizo na bibi huyu na kuzingatia , baada ya hapo alionyeshwa chumba chake ambacho atakuwa analala.

Chumba chake kilikuwa kwenye Floor ya pili , kilikuwa ni chumba kikubwa cha kifahari kilichokuwa na kila kitu kwanzia Tv kubwa ya Inch 64 , pembeni kulikuwa na meza iliokuwa na komputa kubwa ya kamouni ya Apple , masofa na makorokoro mengine ya gharama , Roma alilirdhika na chumba hiki na kumshukuru Bi wema kwa maandalizi ya chumba chake.

Roma aliingia bafuni na kuoga na kisha alifungua kabati la nguo na kukuta nguo nyingi zinazomtosha zikiwa zimepangiliwa kwenye kabati ,  alijiuliza maswali nin muda gani nguo hizo ziliwekwa humo , ila majibu yake aliyapata kwani nguo zote zlionekana kuwa mpya.

Baada ya kupigilia tisheti iliomkaa vyma na kipensi chake ,  alijilaza kitandani mpaka pale alipopitiwa na usingizi , alikuja kushituka usiku wa saa mbili na ilikuwa ni muda wa chakula cha usiku , alishuka mpaka chini sehemu ya chakula na kuungana na Bi wema na  Mke wake  na kisha kukaa.

Jumba hilo lote lilikuwa likiishi wanafamilia wawili tu , jambo ambalo lilimshangaza sana Roma.

“Babe Edna usiniambie jumba lote hili  mnaishi wawili tu”

“Ndio Mr Roma  tupo sisi tu na Miss hana ndugu wengi zaidi ya baba yake”

“Kwa hio na baba yake kule  anaishi peke yake?”.

“Miss na mimi tulikuwa tukiishi nae wote ila baada  ya wao kugombana mara kwa mara ndio tukahamia hapa”

Roma alitikia huku  akiendelea kula bila wasiwasi kama vile ni wa siku nyingi ndani ya nyumba hio , kwani wakati wenzake walipokuwa sahani ya kwanza yeye alikuwa ameongeza Zaidi ya mara tatu na kumfanya Bi wema kutabasamu , lakini upande wa Edna alimwangalia kwa kumshangaa huku akijisemea  ndani kwa ndani kuwa Roma ni mwanaume ambaye hakuwa na aibu hata kidogo

“Bi wema unajua kupika  sana ,  mpaka miezi sita ikiisha nitakuwa na kitambi”.

“Kweli eh , kula  kabisa wala usione wasiwasi na kuna chakula kingine kimebaki jikoni”

“Asante leo ngoja nipumzike mpaka siku ya kesho”Aliongea Roma  na baada ya kula hakukuwa na stori sana na Edna kwali bado alionekana kumchunia mno  na hakutaka stori nyingi Zaidi ya mwanadada huyo kupandisha juu kabisa  kwenda kwenye chumba chake cha kujisomea.

Siku iliofuata asubuhi  Roma aliamka mapema na alionyeshwa chumba cha mazoezi na Bi wema na kuingia kuanza kufanya mazoezi , alivyomaliza chai ilikuwa tayari na Edna alievalia  gauni lililompendeza kama malaika alionekana akishuka huku akiwa na mkoba wake , aliweka kwenye sofa na kisha aliungana nao kwa   ajili ya chai.

“My wife  umeamkaje?”

“Safi”

“Niko poa  babe”aliongea Roma ila hakuzingatiwa sana , kwani Edna aliendelea kunywa chai  iliokuwa Zaidi ya chakula cha mchana kwa wingi wa vyakula , kwa Roma  hakuwa mnyonge,  kwani alikula kama hatokula tena .

“Babe Edna nikitoka hapa narudi Mbagala kazini kwangu”

“Hapana kuanzia leo ile kazi yako achana nayo, tafuta kazi nyingine yenye hazi na ufanye hapa utakaa  lakini kumbuka wewe ni mwanaume hela ya matumizi  siwezi kukupatia”Aliongea  Edna kwa msisitizo  na kisha alimuaga Bi Wema kama anaelekea kazini kwake na kuondoka.

“Ni kweli Mr unapaswa kuacha hio kazi , zipo kazi nyingi ambazo zinaendana na wewe na unaweza kufanya”.

Roma alifikira kwa muda na kuona maneno yao yana mantiki na aliona ni bora akafanya  hivyo , lakini  aliona ugumu wa kupata kazi inayoendana na hazi yake.

Baada ya kuwaza kwa muda aliona ni muda muafaka kwanza wa kurudi  Mbagala kwa ajili ya kuchukua  vitu vyake, alimuaga  Bi Wema  na kabla hajaondoka ,bibi huyu alimwambia  amfuate nyuma ya nyumba na ndani ya dakika chache walikuwa mbele ya magari yaliokuwa yamehifadhiwa , yalikuwa ni magari kumi ya kifahari ambayo yalikuwepo hapo ndani.

“Miss Edna alinipa maelekezo kama ukitaka kutoka unaweza kuchagua gari yoyote unayopenda na  itakuwa yakwako, nadhani unajua kuendesha gari”

“Ndio Bi wema niko vizuri”Aliongea kwa kutabasamu akiangalia magari hayo , kwani  moja ya Starehe pia aliokuwa akipenda Roma ni kuendesha magari .

Alilisogelea gari moja aina ya BMW X7  na kumwabia  Bi Wema atatumia gari hio kwanzia siku hio.

Basi baada ya kupewa ufunguo wake  , kwa mbwembwe zote alitoa gari nje ya geti na safari ya kuelekea  Mbagala Rangi tatu ikiwa imeanza.

“Leo watanikoma, ,Juma  na wenzake wanaongea sana”Alijiongelesha Roma  huku akikanyaga pedeli na kuongeza mwendo , huku kila alipokuwa anapita na gari lake watu walikuwa wakilikodolea macho.

Ni muda wa saa nne za asubuhi ,Roma alisimamisha Gari katika soko La mbagala Rangi  tatu na kisha alishuka , huku wengi waliokuwa wakimfahamu wakimwangalia kwamshangao kama hawakuwa wakimjua.

“Oy Roma kaka  ni wewe?”

“Nni mimi kaka , vipi mishe za hapa?”

“freshi kaka umebadilika sana  aisee”

“Hahaha.. kawaida Seif”Aliongea Roma baada ya kusalimia na Seif aliekuwa akiuza Zabibibu ndani  eneo hili la Stendi ya Rangi Tatu.

“Oya mwanaaa…!!! Aaah Romaaa .. daah ni wewe kweli?”

“Ni mimi Yusuph  , hujanifananisha , ni maisha tu haya hahaha.. unaweza ukalala masikini ukaamka tajiri ndio kilichonitokea”

Yusuph hakuwa  ni mwenye kuamini hivyo  kiharaka ,Roma alimtafuta Juma mpaka akampata  katikati ya soko akiwa anashusha mihogo kwenye  kirikuu.

“Juma!” Roma aliita na kumfanya Juma ashanagae.

“Roma!” Juma alianza kumkagua  Roma kuanzia juu hadi chini na akawa sio mwenye kuamini kama aliekuwa mbele yake ni yule aliekuwa akimdharau kiasi cha kumuita fukara na kutotaka amsogelee dada yake.

“Yes bro nimerudi , kuchukua mazaga na kumalizia  hela ya kodi unayonidai nahamia town man”Aliongea Roma na kumshangaza Zaidi Juma , ambae hakufurahi sana kumuona Roma kwenye hali kama hio kwani siku zote alikuwa akijilinganisha nae na kuona yeye ndio mwenye unafuu mkubwa wa kimaisha , lakini kwa muonekano mpya aliomuona nao Roma aliona bwana huyo sio level zake.

“Poa ngoja nije tuelekee maana nilikuwa pia na wazo hilo hilo la kukuambia utafute mahali pengine , ila kama umepata itakuwa poa sana”Aliongea Juma huku akionekana sio mwenye kufurahia mafanikio ya ghafla ya Roma   na Roma alitikia  kwa kichwa na kisha alimwambia amsubirie anakuja  na Juma alimwambia poa.

Roma alienda  na kuchukua Gari yake na kuja nayo mpaka eneo alilokuwepo  Juma , mwanzoni Juma  hakujua  nani anaendesha  gari hio, na akawa mmoja ya watu wanaoishangaa.

Roma alishusha kioo na kumuita  Juma  alizidi kushangaa Zaidi baada ya kugundua  anaendesha gari hio ni Roma.

“Roma ni wewe mwanangu??”

“Ndio ni mimi Mama Nasra”

“Hio gari ni ya kwako?”

“Ndio Mama Nasra hii nimepewa kama zawadi na mke wangu”Aliongea Roma na kuwafanya waliosikia neno ‘mke’ washangae.

“Umeoa lini Roma mbona hatujui muda wote  huo kama una mke?”

“Nimeoa jana Mama Nasra ilikuwa ghafla na nilishindwa kupata muda wa kuwaambia”Aliongea Roma na watu walishangaa  huku wakizidi kujawa na maswali ni mke gani   amekubali kuolewa na mtu kama Roma asiekuwa mbele na nyuma na mpaka kumdhawadia  gari.

“Ama kweli usimdharau mtu .. maana nyota zetu hazifanani”Alisikika mzee mmoja aliekuwa akimenya machungwa akiongea wakati huo Roma akiwa  anapitisha gari lake kwa  mbwembwe kielekea Bias.

Ndani ya gari hakukuwa na stori nyingi kati ya Juma na Roma , japo Juma muda wote macho hayakuwa yakitulia , kwenye maisha yake hakuwahi kuwaza kama atakuja kupata hata lift kwenye  gari kali kama  hii.

“Hongera kaka kwa kupata mke mwenye hela , nadhani Najma atakusahau na kuendelea na maisha yake sasa”.Roma hakujibu kitu Zaidi ya kutabasamu na kutingisha kichwa , iliwachukua dakika  tano kufika Bias.

Roma baada ya kusimamisha gari huku majirani wakiwa  wanamshangaa kwani ni siku ya jana tu habari zake za kutorudi zilikuwa zimesambaa kuwa hakurudi jana yake baada ya kuja kuchuliwa na mwanadada alievalia suti , kuna waliohisi  huenda alitekwa nyara , na kuna wengine waliokuwa wakidhania huenda Roma  alikuwa mtu mkubwa tu na alikuuwa akijifanyissha kuwa mbeba mizigo , kwani kitendo cha kufuatwa na mwanadada ambae alikuwa  mrembo , kiliwashangaza wengi na hakikua cha kawaida na cha bahati mbaya ,  kila mtu alilipa wazo lake sababu na kuwa na nguvu ndani ya kichwa chake.

Moja ya watu waliokuwa katika hali ya wasiwasi  ni mwanadada Najma , alikuwa ni mwenye mawazo kweli kiasi kwamba hata kazini hakuweza kwenda kwa  siku hio , kwani ndani ya kichwa chake alikuwa akimuwazia Roma tu , alikuwa na taarifa zote zilizokuwa zikimhusu Roma jana yake kufuatwa na  Gari la kifahari aina ya V8 jambo ambalo alipojumlisha na mawazo ya kimbea ya watu aliona huenda kuna ukweli wake, Roma hakuwa mwenzao kama walivyodhani , lakini licha ya hivyo bado aliamini  kwamba Roma alikuwa akimpenda yeye na pia yeye alikuwa akimpenda na hivyo hakukuwa na kitu ambacho kinaweza kuwatenganisha, hayo ndio mawazo aliokuwa nayo Najma karibia asubuhi yote kaka yake alipoelekea kazini.

Najma alifkiria matendo ya kikarimu ambayo Roma ashawahi kuyafanya juu yake , alikumbuka kipindi Roma alivyomsaidia  kiasi kikubwa cha pesa Zaidi ya laki nane kwa ajili ya kwenda kulipia  malipo ya nusu umiliki wa  shule aliokuwa akifundishia huku Roma akimwambia  kuwa hakupaswa kulipa kiasi hicho na achukuliea kama fedha zilizotoka kwa ndugu , alifikiria pia siku ambayo pia aligharimikia  matibabu  yake kiasi cha shilingi laki moja huku Roma akikataa malipo  , kwake aliona matendo yote hayo yalikuwa ni ya kimapenzi, aliamini Roma alikuwa akimpenda yeye na kikwazo kikubwa ilikuwa ni kaka yake, lakini licha hivyo Najma aliamini kama siku zote ataendelea kumpenda Roma basi siku moja  kaka yake atakata tamaa na kuwaruhusu wawili hao wapendane.

Najma aliendelea kukumbuka miezi sita nyuma  siku ambayo Roma alifika ndani ya nyumba yao  na kumkuta akifua nguo muda wa jioni na kumueleza shida yake kwamba alikuwa akitokea mikoani na alikuja mahali hapo kwa ajili ya kutafuta uwezekano wa kupata chumba , hio ndio siku ambayo Najma alijikuta akivutiwa mara moja na mwanaume huyo , hakujua ni nguvu gani iliokuwa ikimvuta kwa mwanaume huyo , lakini katika akili yake aliona kuwa mtu aliekuwa mbele yake hakuja hapo kwao kwa bahati mbaya  na ni Allah ndie ambae amemleta hapo kwake , na mtu aliekuwa mbele yake alikuwa ndio mume wake aliekuwa akimuota kila siku , siku hio ilichuku takribani ya madakika kadhaa kwa Najma  kuacha kumshangaa Roma na kumtathimiini mwanaume huyo  huku akiwa si mwenye kuamini kwamba  mume wake hatimae amefika na kuja kumchukua.

“Kipo chumba kaka .. karibu”Najma  aliitikia mara moja huku akiwa ni mwenye kupagawa  .. alimuonesha Roma chumba hiko huku jambo moja ambalo Roma alikosa kwa muda huo lilikuw ani godoro na Najma bila ya kujifikiria mara mbili alimwambia Roma  atamsaidia Godoro  na atalalaia bure mpaka pale atakapokuwa na uwezo wa kununua la kwake , upande wa Roma alitabasamu na kupendezwa na roho nzuri aliokuwa nayo Najma , kwani mwanamke aliekuwa mbele yake sio kuwa mzuri tu na mrembo lakini pia alionekana kuwa  mwenye kujali watu pasipo ya  muonekeano wao,  kwanzia siku hio Roma alianza kuwa na ukaribu  na mrembo Najma , na hata pale  kaka yake aliporudi kutoka kazini  na Najma kumpa  habari ya ujio wa Roma ,Juma yeye hakuwa na shida kwani alimini ujio wa Roma ni ongezeko la pesa katika walipa kodi.

Kutokana na Roma siku za mwanzoni kushinda Nyumbani  walijikuta wakiwa karibu sana  na Najma na kuzoeana  kwa haraka , kwa upande wa Najma kila  siku  alipokuwa akikaa na Roma na kupiga stori  kitu kipya kilijijenga ndani ya moyo wake.

“Huyu ndie mwanaume niliekuwa nikimuota , ni mwenyewe na sijakosea bila shaka”

Ndio sentensi aliokuwa akiongea Najma kila siku wanapokutana na Roma na kupiga Stori , mwanadada huyu alijikuta akijaa Huba ndani ya moyo wake  dhidi ya Roma, matendo yote ya Roma kwa Najma yalikuwa  yakiongeza kipande cha upando ndani ya Moyo wake.

Hata pale Roma alipoanza kuzoeana  na kaka yake na wakawa marafiki na kuanza kufanya wote kazi katika  soko la Rangi Tatu,Najma bado alisubiri muda wa kurudi kwa Roma awafungulie amuone Roma wake  moyo wake utulie ,Roma nae kila alipokuwa akirudi kwenye chumba chake alikuta chakula kitamu kikiwa kinamsubiri aliishia kutabasamu na kula chakula hiko na kisha kuacha kimemo cha Asante kwa  Najma , na mrembo huyu kila siku alipokuja kuchukua vyombo   na kukuta kikaratasi hiko cha Asante na kusifiwa kama mpishi mzuri  kiliufanya moyo wake uzidi kuloea juu ya Roma , kila  kitu kwake Najma ilikuwa ni Roma , akila chakula ilikuwa ni Roma , akioga ilikuwa ni Roma ,, ilikuwa ni Roma , Roma, Roma kila siku ,kitendo ambacho kilimfanya kaka yake Juma kugundua dada yake alikuwa amempenda Roma.

Gunduzi hio  ya mapenzi ya dada yake  juu ya Roma ndio yalioibua hali ya chuki baina ya wawili hao , upande wa Juma aliona dada yake alikuwa mzuri sana kuolewa na mwanaume Fukara kama Roma hivyo mapenzi  hayo kwake hakutakata yatokee , kila siku alijitahidi kumshawishi Roma wachelewe kurudi na kuwahi kazini , ili wawili hao wasipata nafasi ya  kuonana , lakini bado  Juma alishindwa  kuwazuia wawili hawa kutokuwasiliana  , kwani baada ya siku kadhaa Roma alinunua simu na  namba ya kwanza kumpigia katika simu yake ilikuwa namba ya mrembo Najma, walitakiana  heri kwa kila waamkapo wakielekea kazini na walitakiana heri walakati wa kulala , walishirikishana mambo mengi, mapenzi baina yao yalionekana kuwa na nguvu sana,  matendo ya Roma yalionyesha wazi alikuwa akimpenda Najma na matendo ya Najma yalioneysha  anampenda Roma ,Licha ya wawili hawa kutokuongea  kuwa wanapendana lakini  matendo yao yalikuwa ndio kila kitu kwao.

Baada ya muda mrefu wa Juma kuwa na mawazo , leo hii anajikuta moyo wake ukitulia mara baada ya Roma kupata mke , lakini mwanzo wa swala hili  linaibuka swala linguine katika moyo wake  na swala hilo lilikuwa juu ya mafanikio ya Roma , hakuamini mtu aliekuwa akimdharau leo hii alikuwa na mafanikio makubwa kuliko yake , jambo hili kwake  hakutaka litokee kabisa.

“Nitamwendea kwa mganga huyu , na siku sio nyingi anakuja kulilia hapa nimpe hiki chumba , kwanza hela sio zake akiachwa anakuwa masikini  , nitahakikisha  mke wake anamuacha huyu mpuuzi”  

Juma aliingia  ndani ya  nyumba yao na kisha alitoa ufunguo na kurudi nje na kumpatia Roma , Roma baada ya kuingia ndani ya chumba chake , alishangaa kukuta upekuzi uliokuwa umefanyika ndani ya hiki chumba,Juma nayeye alishangaa  , kwani ni asubuhi tu alifunga , lakini hali aliokuta humo ndani ilimshangaza , alifikiria ni nani anaweza kufanya jambo hilo  kwani mlango  ulikuwa umefungwa na Zaidi pia aliukuta  umefungwa kama alivyofunga, na ufunguo alikuwa akijua yeye tu  lakini hakutaka kujiuiza maswali sana , kwanza aliamini Roma hana kitu cha thamani hapo ndani kiasi cha kuwaza.

Roma yeye alishangazwa na upekuzi huo  , lakini yeye hakujali Zaidi , alisogea mpaka   lilipokuwa gororo lake  na kulinyanyua juu  na akaangalia chini na alijikuta akivuta pumzi ya ahueni.

“Inaonekana walichokuwa wakikitafuta hawajakipata”

Aliongea Roma na kisha  alichuchumaa na  kusogea mpaka sehemu ambayo ilikuwa na alama ya  mchoro wa Zero , wakati huu Juma alikuwa yupo nje akimpa nafasi Roma ya kufanya mambo yake amkabidhi hela zake .

Baada ya Roma kusogelea alama ile ya Zero  alivuta pumzi na kukunja ngumi na kwa spidi alipiga katikati ya lile eneo  na pakabaduka na kuacha uwazi , Roma alitoa mchanga na kiisha alivuta  mfuko wa Rambo na kuutoa nje  na kisha akaufungua , ndani ya mfuko huu  ulionekana kuwa  na  kiboksi flani kirefu mfano wa mstatiri , alikifungua kiboksi hiki na kuona vitu vyake vyote vipo, alitoa kiburnguti cha hela na  kutoa hela iliosomeka kwa mfumo wa Dola , ilikuwa ni Dolla Mia ambayo kwa hela za kitanzania ilikuwa ni Zaidi ya laki mbili,  baada ya  kutoa baadhi ya vitu vyake hivyo aliviingiza kwenye begi lililokuwa pembeni yake  kubwa kubwa  la kusafiria na  kisha alisimama na kuvuta pumzi huku  akionekana kama mtu  anaeonekana kuaga   chumba hiko, baada ya hapo  alitoka nje na kumkuta Juma , Alitoa ile noti ya Dola Mia na kumpatia Juma  na kumfanya  ashangae , kwani Juma pia hakuwa kilaza ashindwe kujua thamani ya dolla Mia.

“Nadhani hio italipa deni langu la Kodi , lakini pia kunasehemu nimeharibu huko ndani  so inayobaki itakuwa  fidia”

“Sawa kaka  Asante”

“Romaa..!!!”Ilisikika sauti ilioingia kwenye ngoma za masikio yake na kuitambua.

“Najma .. nilidhania upo kazini”Aliongea  Roma huku akimwangalia mwanadada aliekuwa mbele yake  , aliekuwa amesahau hata kuvaa Hijab kwa siku hii ya leo na kwa mara ya kwanza Roma anamuona mwanamke huyu akiwa hana Hijab na kuuona uzuri kamili  wa Najma.

“Najma mzuri aisee”

Previoua Next