Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Edna ni kama  hajamuona Roma  , kwani Zaidi ya kutingisha kichwa kama salamu alimpita na alionekana alikuwa ndani ya eneo hili kwa aili ya kuonana na Abuu.

Roma hakujali sana, na yeye alichapa raba  kwani kilichokuwa kimemleta eneo hilo alikuwa ashakimaliza , aliingia kwenye lift  na  ndani ya dakika chache alikuwa  akitoka na gari yake .

Alipiga mwendo mpaka alipokuja kuibukia ndani ya Samora  ambayo  kampuni ya mke wake ilipo , lakini  muda huu kulionekana kukiwa na foleni kidogo kiasi cha kufanya magari yasimame.

“Boss nunu magazeti”Ilikuwa ni sauti ya kijana mdogo iliomshitua Roma aliekuwa akisikiliza mziki kwenye gari yake na kisha akashusha kioo na  kumhurumia kijana huyo na kuona ngoja anunue , alilipa pesa na kupata gazeti lake.

“Asante bosi” Roma aliitikia kwa kichwa na kisha alianza kufunua gazeti  hilo kwa  mbelle , na hapo ndipo alipopigwa na mshangao kwani mbele kabisa ya gazeti hili kulikuwa na picha ya Abuu na Edna na kichwa kikubwa cha habari.

“KAMPUNI YA VEXTO NA JR WASAINI MKATABA WA KUSHIRIKIANA KATIKA UJENZI  WA BARABARA YA MWENDO KASI KUTOKA MBAGALA KWENDA CHAMAZI”

Roma alisoma  kichwa hiko na kufungua ndani kupata habari kamili na hapo ndipo alipokuja kugundua kuwa mke wake Jana alikuwa na miadi na Abuu kwa ajili ya kusaini mkataba  huo , kwani ndani ya  gazeti hilo ilionesha kuwa mkataba huo ulisainiwa jana yake ndani ya hoteli  ya Serena.

“Sasa mke wangu walimteka vipi?”Alijiuliza Roma na kisha kuendelea kuendesha gari kwani magari yalikuwa yashaanza kusogea na ndani ya dakika chache alikuwa ndani ya jengo hili  la kampuni huku akiwa amechelewa sana kwani muda huo ilikuwa yapata saa tano za mchana.

“Roma!”Ilikuwa ni suati ya uchangamfu kutoka kwa mrembo Doris ndio iliomwita  Roma na kumfanya bwana huyu ageuke na hii ilikuwa ni ndani ya ofisi ambayo Roma alikuwa akifanyia kazi.

“Niambie mrembo , unaonekana kuwa mzuri Zaidi kuliko jana”

“Hahaha.. mnafiki sana wewe unanisifia huku unasema mkeo ndio mzuri kuliko wanawake wote”

“Hehe.. hilo ni kweli”Aliikuta akipigwa ngumi na Roma akajifanya kuumia na kitendo hiki kilifanya baadhi ya wafanyakazi hapa ndani washangazwe na ukaribu wa ghafla wa Roma na Doris  ila hawakutaka kuuliza kwani Dorisi alikuwa mkubwa wao kikazi na nafasi ndani ya  kampuni.

“Hawajakuumiza  popote , jana ilikuwajje?”

“Doris hayo tuyaache  tutaongea tukienda  kupeana mambo tena au unaonaje mimi niko kamili gado na nikama wameniongezea nguvu na nataka nikazitoe kwako”Huku akitabasamu na kumfanya Doris aone aibu za kike.

“Jishaue tu mwanaume nani kakuambia tutafanya tena”Aliongea na kisha akaondoka .

“Hey! Handsome  uko poa?”

“Niko poa Recho mrembo”

“Mh! Umechelewa unakua  hapa ofisni kama kwako vile?”

“Sio hvyo mrembo , nilikuwa  na Dharula”

“Mh! Haya bhana ila wewe na Doris kuna kitu kinaendelea  ila sisemi”Roma alitabasamu na  akaachana  na Recho na kisha akatafuta gemu lake la Zuma na kuanza kucheza mpaka muda wa chakula na  kuungana na Doris na Recho.

****

Usiku  Edna alirudi  mapema  sana , na kusalimiana na Roma ambae alikuwa yupo sebleni akiongea na Bi wema , baada ya kusalimiana nao moja kwa moja aliingia kwenye chumba chake.

Mrembo huyu alikuwa ni mwenye mawazo ya hapa na pale lakini alichokuwa akiwaza kikubwa ni juu ya Roma , picha ya matukio yaliotokea kule kibaha hakuwa  akiyaamini kabisa kwamba mtu aliekuwa ameyafanya ni Roma , mwanaume ambae alimdhania  kuwa mbeba mizigo tu mpaka kufanya maamuzi ya kuolewa naye , huku akiamini kwamba atamfanya mwanaume huyo kuwa bwege , lakini matokeo yake yakawa tofauti.

Edna kuna vitu vingi vilikuwa vikipita kwenye kichwa chake kwa wakati mmoja , alikuwa akiwaza namna siku alivyoweza kuamka akiwa ndani ya chumba cha Roma mpaka siku ambayo alikutana na kwa mara nyingine ndani ya hoteli  kwa ajili ya kumuomba ndoa.

“Anaonekana sio mtu wa kawaida  kwa muonekano wake”Aliwaza.

Wakati akiendelea kuwaza mara simu yake ilipata uhai , aliinua na kuangalia jina na kukuta ni jina la Mheshimiwa , alipokea haraka na kisha aliweka sikioni.

“Hello Mheshimiwa habari za jioni”

“Nzuri sana Edna  , unaendeleaje ?”

“Naendelea vizuri mheshimiwa”

“Nafurahi kusikia hivyo Edna , sasa nimekupigia simu kukuomba  wewe pamoja na mume wako kuhudhuria chakula cha jioni Ikulu nina mazungumzo  pia na wewe”Edna alibabaika , hakujua kuwa mheshimiwa Raisi alikuwa akijua kuwa tayari ashaolewa , alishangaa  ila aliona Raisi ni mtu mwenye kujua mengi  hivyo swala lake lilikuwa rahisi sana kulifahamu.

“Sawa mheshimiwa , sikujua kuwa unafahamu kama nishapata mume”

“Hahaha..Edna wewe ni mtu mkubwa sana kwenye taifa hili kila unachokifanya lazima nipate taarifa zako hususani  kwa  jambo muhimu kama lako”Edna alitabasamu na kisha  waliagana na mheshimiwa huku akivuta pumzi.

Baada ya kukaa kwenye chumba chake cha kujisomea kwa muda  hatimae ilikuwa saa mbili za usiku  na alishuka kwa ajili ya chakula cha usiku baada ya kuitwa na Bi wema.

Mezani Roma alikuwepo na alikuwa tayari  ashaanza kula huku Bi Wema akiwa ameachia tabasamu akimwangalia Roma jinsi anavyokula , ilionyesha alikuwa akifurahishwa na  hamu ya kula aliokuwa nayo Roma.

“My Wife Bi Wema ni mtaalamu sana Sidhani kama unamfikia likija swala la mapishi”Aliongea Roma huku akijilamba midomo wakati huu akiwa ameshikilia paja la kuku na Edna alimwangalia mwanaume huyu kwa mtazamo wa maswali mengi.

“Huyu namtambulishaje kwa mheshimiwa kesho huyu , si ataenda kunitia aibu”Aliwaza Edna huku akianza kupakua chakula chake pasipo kumjibu Roma.

“Edna hajawahi kupika, hajui chochote kuhusu mapishi”Aliongea Bi wema  na kumfanya Roma ashangae.

“Kwa hio Bi Wema unaniambia nimeoa mke  jipu , maana mke ni upishi na mengineyo”Aliongea na kumfanya Edna akareke.

“Mr Roma  licha ya kwamba Edna hajui kupika ila yupo vizuri kwenye mambo mengi”

“Bi wema naona unamsifia mke wangu , hayo mambo mengi anayoyajua ni kama yapi?”

“Edna licha ya kuwa mkimya ila ana roho nzuri , lakini pia ni mchapakazi mzuri huoni hata kampuni imekuwa kubwa baada ya kupewa uongozi wa juu”.

“Bi wema sawa , lakini hilo swala   halihusiani na yeye kuwa mke akiwa nyumbani”

“Ndio hivyo , lakini naamini atajifunza kwani ashakuwa mke sasa”.

“Bi wema sitojifunza , kwanza sinampango wa kumpikia mwanaume anaekula kama mbuzi mimi”Aliongea Edna kwa hali ya kukereka ila kwa Roma ni kama hajamsikia kwani alivuta bakuli na kuongea wali kwenye sahani yake.

“Usiseme hivyo Edna ,Roma ni mumeo”.Edna hakutaka kuongezea  neon aliendelea kula.

Baada ya Roma kumaliza kula alipandisha ngazi kuelekea uu huku akiwaacha wanawake watoe vyombo , baada tu ya kuingia kwenye chumba chake alibadilisha mavazi na  kuchukua ufunguo  na kushuka chini.

“Mke wangu natoka kidogo”Aliongea Roma na  kuanza kupiga hatua  kuelekea mlangoni.

“Kesho jioni kuna mahali tunapaswa kwenda pamoja ujiandae”Aliongea Edna na Roma aligeuka na kisha kutabasamu.

“Okey my Wife Usiku mwema”Aliongea Roma na Edna hakujali Zaidi  kwani alipandisha ngazi kupanda juu chumbani kwake huku Bi wema akiwa anamuangalia.

Roma kama kawaida , alikuwa akiwaza kutafuta kitumbua cha kupunguza kichupa usiku huo  , alianza kumfikiria Rose , lakini wazo hilo alilitupilia mbali , aliendelea na kumfikiria  Dorisi na kuona pia wazo hilo sio zuri.

“Ngoja niende New Afrika hoteli  pale sikosi warembo”Alijiwazia Roma wakati akiwa anapita daraja la  kigamboni.

Dakika chache mbele alikuwa akiegesha gari yake mahali maalumu  ndani ya hoteli hii kubwa ndani ya jiji  la Dar na kisha alishuka na kuingia ndani  na moja kwa moja alienda  sehemu ya Bar iliokuwa ndani ya  hoteli hii.

Baada ya kuingia ndani ya hili eneo , kwanza alitabasamu  baada ya kuona ni sehemu iliochangamka  , lakini jambo ambalo lilimfanya kujisikia vibaya ni kwamba ndani ya hili eneo lilionekana kuwa na  watu waliokuwa wawili wawili au Zaidi , kuna waliokuwa  na wachumba zao , lakini pia kuna waliokuwa wakipiga stori wakiwa jinsia moja ,Roma aliangaza upande wa kulia kushoto na alijikuta akivutiwa na upande wa kushoto baada ya kumuona mwanamke mmoja alieonekana kuwa peke yake.

Roma alipiga hatua kuelekea upande ule na kumfikia yule mwanamke na alikiri ni mrembo mara baada ya kumuona kwa ukaribu , mwanamke huyu hakuonekana kuwa mkubwa sana kimakadirio Roma alimuona kuwa na miaka isiozidi  therethini  , alikuwa amevalia gauni  refu la maua maua   rangi ya njano na nyeupe huku   akiwa ameifunga mkanda mkubwa kwenye kiuno , alikuwa na  nywele alizokuwa amenyoa   na zikawa fupi kiasi huku zikiwa zimepakwa rangi nyeusi na kuonesha mawimbi  na kufanya kuzidi kumfanya mwanamke huyu kuzidi kiuonekana kuwa mrembo.

“Niambie mrembo , Uko peke yako?”Aliuliza Roma kabla ya  kuketi na mwanake huyu alimwangalia kwa macho yake makubwa ya gololi, wakati haya yakiendelea baadhi ya watu walikuwa wakimwangalia Roma ni kama walionekana walikuwa wakimfahamu huyu mwanamke , lakini kwa Roma hakujai Zaidi kwanza mwanamke aliekuwa mbele yake hakuwahi kumuona na pia alikuwa mrembo.

“Niko peke yangu , Unaweza kukaa”Aliongea huyu mwanamke kwa sauti Fulani hivi ya kupendeza na kumfanya  Roma Atabasamu.

“Inakuwaje mwanamke mrembo kama wewe  unakaa peke  yako?”

“Nimejisikia leo sihitaji kampani  kwani nina mengi ya kufikiria”.Aliongea huku akinyanyua glasi yake  iliojaa wine  ya gharama ya juu kabisa  iliokuwa na jina la Abreu.Roma alitabasamu huku akiangalia chupa ya Wine.

“Hio ni moja ya Wine ya bei ghali sana duniani  , imetengengezwa na  David Abreu”Aliongea  Roma na kumfanya mrembo huyu  amwangalie na kisha akatabasamu.

“Umepatia , inaonekana ni mpenzi wa hii  wine , mpaka unamjua mtengenezaji”

“Ndio  ni moja ya Wine  ninazozipenda”Aliongea Roma na  akaja mhhudumu kwa ajili ya kuchukua aina ya kinywaji  atakachotumia.

“Nipe kama  ya huyu mrembo”Aliongea Roma na kisha  mhudumu akaileta ndani ya dakika  kadhaa huku Roma akiendelea kumpigisha stori mrembo huyu , muda ulizidi kusogea kwa mrembo huyu alionekana kuanza kulewa , ila kwa Roma hakuwa  ni mwenye kuongekana kulewa

“Unamawazo gani mrembo , mpaka yakakufanya  ujitenge siku ya leo?”

“Kuna mshenzi kaniboa leo  , na sitaki hata kumsikia tena kwenye maisha yangu”

“Pole ni mume au Boyfriend?”

“Sio mume wala sio Boyfriend .. sijui haa nimuweke vipi , ila amenikera sana leo”Aliongea mrembo huyu.

“Atakuwa  mchepuko”Aliwaza Roma

“Unaonaje tukichukua chumba  mrembo  nikakuusahaulisha na  ya dunia”.

“Utaweza kunisaulisha kweli , unaonekana mdogo mno”Roma hakutaka kuongea Zaidi , aliona  hapa ni vitendo pekee ambavyo vingefanya kazi , alichokifanya ni kumuambia huyo mwanamke anyanyuke amfuate na mwanamke huyu alimwangalia Roma na kisha akanyanyuka kivivu na kumshikilia  Roma kilevi na wakatoka ndani ya hilo  eneo huku Roma akiacha Hela zilizokuwa kwa mfumo wa Dola na kuondoka.

Masaa  machache  mbele mwanamke yule mrembo alionekana kutoa  maneno ya kila aina yasio kuwa yanaelewweka na yale ambayo hayakuwa katika mpangilio mzuri ,,alionekana alikuwa kwenye ulimwengu  mwingine kabisa.

“Naomba tupumzike wewe mwanaume utaniua”Aliongea huyu mwanamke na Roma hakutaka kusikiliza Zaidi kwani  alikusanya miguu ya mwanamke huyu na kuiweka kichwani  na  kuendelea kukata kiuno na ndani ya lisaa limoja na nusu , alitua mzigo na kulala pembeni huku akihema.

Upande wa yule mwanamke  , alionekana kumwangalia Roma pasipo kummaliza  kwani magoli aliofunga usiku hio hayakuwa na idadi , alikumbuka vyema muda ambao walianza kufanya tendo hilo ni  Zaidi ya masaa mawili.

“Sijawahi kukutana na mwanaume anaeweza kuto**mba muda mrefu kama huyu”Aliongea huyu mwanamke na akapitiwa na usingizi.

Asubuhi kulivyokucha   huyu mwanamke aliangalia   pembeni na kujikuta  akiwa peke yake na Roma hakuwepo, wakati akiendelea kuwaza yaliotokea usiku , simu yake ilianza kutia mfululizo aliangalia jina na kisha akapokea .

“Kuna nini Grace?”

“Mheshimiwa Angalia mtandaoni kuna habari zako”Ilikuwa ni  sauti ya wasiwasi ya upande wa pili ikiongea.

Huyu mwanamke mrembo akiwa uchi aliangia Instagram na kuangalia kuna nini mtandano”

“MBUNGE  NA NAIBU WAZIRI WA SANAA NA MICHEZO  NEEMA LUWAZO  AONEKANA NA MWANAUME KWA MARA YA KWANZA  WAKILA BATA”Huku kichwa hiko kikiambatana na mapicha , picha ya kwanza ilikuwa ni ya Roma  japo haijaonekana vizuri , ila kwa mtu anaemjua Roma angejua ni  Roma na picha ya mpili ilikuwa ni ya   mrembo huyuy Neema Luwazo ambaye ni  Naibu wazri wa Sanaa na michezo.

Previoua Next