Edna ni kama hajamuona Roma , kwani Zaidi ya kutingisha kichwa kama salamu alimpita na alionekana alikuwa ndani ya eneo hili kwa aili ya kuonana na Abuu.
Roma hakujali sana, na yeye alichapa raba kwani kilichokuwa kimemleta eneo hilo alikuwa ashakimaliza , aliingia kwenye lift na ndani ya dakika chache alikuwa akitoka na gari yake .
Alipiga mwendo mpaka alipokuja kuibukia ndani ya Samora ambayo kampuni ya mke wake ilipo , lakini muda huu kulionekana kukiwa na foleni kidogo kiasi cha kufanya magari yasimame.
“Boss nunu magazeti”Ilikuwa ni sauti ya kijana mdogo iliomshitua Roma aliekuwa akisikiliza mziki kwenye gari yake na kisha akashusha kioo na kumhurumia kijana huyo na kuona ngoja anunue , alilipa pesa na kupata gazeti lake.
“Asante bosi” Roma aliitikia kwa kichwa na kisha alianza kufunua gazeti hilo kwa mbelle , na hapo ndipo alipopigwa na mshangao kwani mbele kabisa ya gazeti hili kulikuwa na picha ya Abuu na Edna na kichwa kikubwa cha habari.
“KAMPUNI YA VEXTO NA JR WASAINI MKATABA WA KUSHIRIKIANA KATIKA UJENZI WA BARABARA YA MWENDO KASI KUTOKA MBAGALA KWENDA CHAMAZI”
Roma alisoma kichwa hiko na kufungua ndani kupata habari kamili na hapo ndipo alipokuja kugundua kuwa mke wake Jana alikuwa na miadi na Abuu kwa ajili ya kusaini mkataba huo , kwani ndani ya gazeti hilo ilionesha kuwa mkataba huo ulisainiwa jana yake ndani ya hoteli ya Serena.
“Sasa mke wangu walimteka vipi?”Alijiuliza Roma na kisha kuendelea kuendesha gari kwani magari yalikuwa yashaanza kusogea na ndani ya dakika chache alikuwa ndani ya jengo hili la kampuni huku akiwa amechelewa sana kwani muda huo ilikuwa yapata saa tano za mchana.
“Roma!”Ilikuwa ni suati ya uchangamfu kutoka kwa mrembo Doris ndio iliomwita Roma na kumfanya bwana huyu ageuke na hii ilikuwa ni ndani ya ofisi ambayo Roma alikuwa akifanyia kazi.
“Niambie mrembo , unaonekana kuwa mzuri Zaidi kuliko jana”
“Hahaha.. mnafiki sana wewe unanisifia huku unasema mkeo ndio mzuri kuliko wanawake wote”
“Hehe.. hilo ni kweli”Aliikuta akipigwa ngumi na Roma akajifanya kuumia na kitendo hiki kilifanya baadhi ya wafanyakazi hapa ndani washangazwe na ukaribu wa ghafla wa Roma na Doris ila hawakutaka kuuliza kwani Dorisi alikuwa mkubwa wao kikazi na nafasi ndani ya kampuni.
“Hawajakuumiza popote , jana ilikuwajje?”
“Doris hayo tuyaache tutaongea tukienda kupeana mambo tena au unaonaje mimi niko kamili gado na nikama wameniongezea nguvu na nataka nikazitoe kwako”Huku akitabasamu na kumfanya Doris aone aibu za kike.
“Jishaue tu mwanaume nani kakuambia tutafanya tena”Aliongea na kisha akaondoka .
“Hey! Handsome uko poa?”
“Niko poa Recho mrembo”
“Mh! Umechelewa unakua hapa ofisni kama kwako vile?”
“Sio hvyo mrembo , nilikuwa na Dharula”
“Mh! Haya bhana ila wewe na Doris kuna kitu kinaendelea ila sisemi”Roma alitabasamu na akaachana na Recho na kisha akatafuta gemu lake la Zuma na kuanza kucheza mpaka muda wa chakula na kuungana na Doris na Recho.
****
Usiku Edna alirudi mapema sana , na kusalimiana na Roma ambae alikuwa yupo sebleni akiongea na Bi wema , baada ya kusalimiana nao moja kwa moja aliingia kwenye chumba chake.
Mrembo huyu alikuwa ni mwenye mawazo ya hapa na pale lakini alichokuwa akiwaza kikubwa ni juu ya Roma , picha ya matukio yaliotokea kule kibaha hakuwa akiyaamini kabisa kwamba mtu aliekuwa ameyafanya ni Roma , mwanaume ambae alimdhania kuwa mbeba mizigo tu mpaka kufanya maamuzi ya kuolewa naye , huku akiamini kwamba atamfanya mwanaume huyo kuwa bwege , lakini matokeo yake yakawa tofauti.
Edna kuna vitu vingi vilikuwa vikipita kwenye kichwa chake kwa wakati mmoja , alikuwa akiwaza namna siku alivyoweza kuamka akiwa ndani ya chumba cha Roma mpaka siku ambayo alikutana na kwa mara nyingine ndani ya hoteli kwa ajili ya kumuomba ndoa.
“Anaonekana sio mtu wa kawaida kwa muonekano wake”Aliwaza.
Wakati akiendelea kuwaza mara simu yake ilipata uhai , aliinua na kuangalia jina na kukuta ni jina la Mheshimiwa , alipokea haraka na kisha aliweka sikioni.
“Hello Mheshimiwa habari za jioni”
“Nzuri sana Edna , unaendeleaje ?”
“Naendelea vizuri mheshimiwa”
“Nafurahi kusikia hivyo Edna , sasa nimekupigia simu kukuomba wewe pamoja na mume wako kuhudhuria chakula cha jioni Ikulu nina mazungumzo pia na wewe”Edna alibabaika , hakujua kuwa mheshimiwa Raisi alikuwa akijua kuwa tayari ashaolewa , alishangaa ila aliona Raisi ni mtu mwenye kujua mengi hivyo swala lake lilikuwa rahisi sana kulifahamu.
“Sawa mheshimiwa , sikujua kuwa unafahamu kama nishapata mume”
“Hahaha..Edna wewe ni mtu mkubwa sana kwenye taifa hili kila unachokifanya lazima nipate taarifa zako hususani kwa jambo muhimu kama lako”Edna alitabasamu na kisha waliagana na mheshimiwa huku akivuta pumzi.
Baada ya kukaa kwenye chumba chake cha kujisomea kwa muda hatimae ilikuwa saa mbili za usiku na alishuka kwa ajili ya chakula cha usiku baada ya kuitwa na Bi wema.
Mezani Roma alikuwepo na alikuwa tayari ashaanza kula huku Bi Wema akiwa ameachia tabasamu akimwangalia Roma jinsi anavyokula , ilionyesha alikuwa akifurahishwa na hamu ya kula aliokuwa nayo Roma.
“My Wife Bi Wema ni mtaalamu sana Sidhani kama unamfikia likija swala la mapishi”Aliongea Roma huku akijilamba midomo wakati huu akiwa ameshikilia paja la kuku na Edna alimwangalia mwanaume huyu kwa mtazamo wa maswali mengi.
“Huyu namtambulishaje kwa mheshimiwa kesho huyu , si ataenda kunitia aibu”Aliwaza Edna huku akianza kupakua chakula chake pasipo kumjibu Roma.
“Edna hajawahi kupika, hajui chochote kuhusu mapishi”Aliongea Bi wema na kumfanya Roma ashangae.
“Kwa hio Bi Wema unaniambia nimeoa mke jipu , maana mke ni upishi na mengineyo”Aliongea na kumfanya Edna akareke.
“Mr Roma licha ya kwamba Edna hajui kupika ila yupo vizuri kwenye mambo mengi”
“Bi wema naona unamsifia mke wangu , hayo mambo mengi anayoyajua ni kama yapi?”
“Edna licha ya kuwa mkimya ila ana roho nzuri , lakini pia ni mchapakazi mzuri huoni hata kampuni imekuwa kubwa baada ya kupewa uongozi wa juu”.
“Bi wema sawa , lakini hilo swala halihusiani na yeye kuwa mke akiwa nyumbani”
“Ndio hivyo , lakini naamini atajifunza kwani ashakuwa mke sasa”.
“Bi wema sitojifunza , kwanza sinampango wa kumpikia mwanaume anaekula kama mbuzi mimi”Aliongea Edna kwa hali ya kukereka ila kwa Roma ni kama hajamsikia kwani alivuta bakuli na kuongea wali kwenye sahani yake.
“Usiseme hivyo Edna ,Roma ni mumeo”.Edna hakutaka kuongezea neon aliendelea kula.
Baada ya Roma kumaliza kula alipandisha ngazi kuelekea uu huku akiwaacha wanawake watoe vyombo , baada tu ya kuingia kwenye chumba chake alibadilisha mavazi na kuchukua ufunguo na kushuka chini.
“Mke wangu natoka kidogo”Aliongea Roma na kuanza kupiga hatua kuelekea mlangoni.
“Kesho jioni kuna mahali tunapaswa kwenda pamoja ujiandae”Aliongea Edna na Roma aligeuka na kisha kutabasamu.
“Okey my Wife Usiku mwema”Aliongea Roma na Edna hakujali Zaidi kwani alipandisha ngazi kupanda juu chumbani kwake huku Bi wema akiwa anamuangalia.
Roma kama kawaida , alikuwa akiwaza kutafuta kitumbua cha kupunguza kichupa usiku huo , alianza kumfikiria Rose , lakini wazo hilo alilitupilia mbali , aliendelea na kumfikiria Dorisi na kuona pia wazo hilo sio zuri.
“Ngoja niende New Afrika hoteli pale sikosi warembo”Alijiwazia Roma wakati akiwa anapita daraja la kigamboni.
Dakika chache mbele alikuwa akiegesha gari yake mahali maalumu ndani ya hoteli hii kubwa ndani ya jiji la Dar na kisha alishuka na kuingia ndani na moja kwa moja alienda sehemu ya Bar iliokuwa ndani ya hoteli hii.
Baada ya kuingia ndani ya hili eneo , kwanza alitabasamu baada ya kuona ni sehemu iliochangamka , lakini jambo ambalo lilimfanya kujisikia vibaya ni kwamba ndani ya hili eneo lilionekana kuwa na watu waliokuwa wawili wawili au Zaidi , kuna waliokuwa na wachumba zao , lakini pia kuna waliokuwa wakipiga stori wakiwa jinsia moja ,Roma aliangaza upande wa kulia kushoto na alijikuta akivutiwa na upande wa kushoto baada ya kumuona mwanamke mmoja alieonekana kuwa peke yake.
Roma alipiga hatua kuelekea upande ule na kumfikia yule mwanamke na alikiri ni mrembo mara baada ya kumuona kwa ukaribu , mwanamke huyu hakuonekana kuwa mkubwa sana kimakadirio Roma alimuona kuwa na miaka isiozidi therethini , alikuwa amevalia gauni refu la maua maua rangi ya njano na nyeupe huku akiwa ameifunga mkanda mkubwa kwenye kiuno , alikuwa na nywele alizokuwa amenyoa na zikawa fupi kiasi huku zikiwa zimepakwa rangi nyeusi na kuonesha mawimbi na kufanya kuzidi kumfanya mwanamke huyu kuzidi kiuonekana kuwa mrembo.
“Niambie mrembo , Uko peke yako?”Aliuliza Roma kabla ya kuketi na mwanake huyu alimwangalia kwa macho yake makubwa ya gololi, wakati haya yakiendelea baadhi ya watu walikuwa wakimwangalia Roma ni kama walionekana walikuwa wakimfahamu huyu mwanamke , lakini kwa Roma hakujai Zaidi kwanza mwanamke aliekuwa mbele yake hakuwahi kumuona na pia alikuwa mrembo.
“Niko peke yangu , Unaweza kukaa”Aliongea huyu mwanamke kwa sauti Fulani hivi ya kupendeza na kumfanya Roma Atabasamu.
“Inakuwaje mwanamke mrembo kama wewe unakaa peke yako?”
“Nimejisikia leo sihitaji kampani kwani nina mengi ya kufikiria”.Aliongea huku akinyanyua glasi yake iliojaa wine ya gharama ya juu kabisa iliokuwa na jina la Abreu.Roma alitabasamu huku akiangalia chupa ya Wine.
“Hio ni moja ya Wine ya bei ghali sana duniani , imetengengezwa na David Abreu”Aliongea Roma na kumfanya mrembo huyu amwangalie na kisha akatabasamu.
“Umepatia , inaonekana ni mpenzi wa hii wine , mpaka unamjua mtengenezaji”
“Ndio ni moja ya Wine ninazozipenda”Aliongea Roma na akaja mhhudumu kwa ajili ya kuchukua aina ya kinywaji atakachotumia.
“Nipe kama ya huyu mrembo”Aliongea Roma na kisha mhudumu akaileta ndani ya dakika kadhaa huku Roma akiendelea kumpigisha stori mrembo huyu , muda ulizidi kusogea kwa mrembo huyu alionekana kuanza kulewa , ila kwa Roma hakuwa ni mwenye kuongekana kulewa
“Unamawazo gani mrembo , mpaka yakakufanya ujitenge siku ya leo?”
“Kuna mshenzi kaniboa leo , na sitaki hata kumsikia tena kwenye maisha yangu”
“Pole ni mume au Boyfriend?”
“Sio mume wala sio Boyfriend .. sijui haa nimuweke vipi , ila amenikera sana leo”Aliongea mrembo huyu.
“Atakuwa mchepuko”Aliwaza Roma
“Unaonaje tukichukua chumba mrembo nikakuusahaulisha na ya dunia”.
“Utaweza kunisaulisha kweli , unaonekana mdogo mno”Roma hakutaka kuongea Zaidi , aliona hapa ni vitendo pekee ambavyo vingefanya kazi , alichokifanya ni kumuambia huyo mwanamke anyanyuke amfuate na mwanamke huyu alimwangalia Roma na kisha akanyanyuka kivivu na kumshikilia Roma kilevi na wakatoka ndani ya hilo eneo huku Roma akiacha Hela zilizokuwa kwa mfumo wa Dola na kuondoka.
Masaa machache mbele mwanamke yule mrembo alionekana kutoa maneno ya kila aina yasio kuwa yanaelewweka na yale ambayo hayakuwa katika mpangilio mzuri ,,alionekana alikuwa kwenye ulimwengu mwingine kabisa.
“Naomba tupumzike wewe mwanaume utaniua”Aliongea huyu mwanamke na Roma hakutaka kusikiliza Zaidi kwani alikusanya miguu ya mwanamke huyu na kuiweka kichwani na kuendelea kukata kiuno na ndani ya lisaa limoja na nusu , alitua mzigo na kulala pembeni huku akihema.
Upande wa yule mwanamke , alionekana kumwangalia Roma pasipo kummaliza kwani magoli aliofunga usiku hio hayakuwa na idadi , alikumbuka vyema muda ambao walianza kufanya tendo hilo ni Zaidi ya masaa mawili.
“Sijawahi kukutana na mwanaume anaeweza kuto**mba muda mrefu kama huyu”Aliongea huyu mwanamke na akapitiwa na usingizi.
Asubuhi kulivyokucha huyu mwanamke aliangalia pembeni na kujikuta akiwa peke yake na Roma hakuwepo, wakati akiendelea kuwaza yaliotokea usiku , simu yake ilianza kutia mfululizo aliangalia jina na kisha akapokea .
“Kuna nini Grace?”
“Mheshimiwa Angalia mtandaoni kuna habari zako”Ilikuwa ni sauti ya wasiwasi ya upande wa pili ikiongea.
Huyu mwanamke mrembo akiwa uchi aliangia Instagram na kuangalia kuna nini mtandano”
“MBUNGE NA NAIBU WAZIRI WA SANAA NA MICHEZO NEEMA LUWAZO AONEKANA NA MWANAUME KWA MARA YA KWANZA WAKILA BATA”Huku kichwa hiko kikiambatana na mapicha , picha ya kwanza ilikuwa ni ya Roma japo haijaonekana vizuri , ila kwa mtu anaemjua Roma angejua ni Roma na picha ya mpili ilikuwa ni ya mrembo huyuy Neema Luwazo ambaye ni Naibu wazri wa Sanaa na michezo.
Comments