Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Saa kumi na mbili na nusu Roma alinyanyuka na kujivuta kisha akashuka chini kwenye chumba cha mazoezi  kwa ajili ya kupasha mwili   joto , wakati akiendelea kuchukua mazoezi , alikuwa akikumbuka vyEma usiku wa jana alivyoumaliza na yule mwanamke ambaye hakuwa akimjua hata jina Zaidi ya kumnyandua.

“Nadhani hatutaonana tena”Aliwaza Roma

Saa moja kamili Roma alikuwa ashamaliza kila kitu na alikuwa mezani akinywa chai  yeye pamoja na Edna kwa ajili ya kuelekea kazini.

“Wife mbona unaniangalia hivyo”

“Hivi Roma tokea  uanze kazi umefanya nini ndani ya kampuni?”

“Sina nilichofanya Zaidi ya kucheza gemu mke wangu , sijui cha kufanya  kama vipi nipe kazi hata ya ulinzi nifanye hio kuliko ya kukaa kwenye meza”Edna alishangaa ila hakuongea kitu , aliendelea kunywa chai na alimaliza wa kwanza akimuacha Roma.

“Usisahau leo kuna sehemu tunapaswa kwenda, nitamwagiza Suzzane akuletee nguo  za kuvaa”Aliongea  Edna na kumfanya Roma ashangae.

“Mke wangu nguo si ninazo kuna ulazima gani wa nguo zingine?”

“Fanya kama nilivyokuambia ,acha maswali mengi”Edna hakutaka kuongea Zaidi na Roma alimuaga Bi Wema na kisha  ndani ya Sekunde chache Roma alisikia mngurumo wa Gari  ukipotelea nje ya geti.

Roma na yeye baada ya kumaliza kunywa chai , alitoka na kuingia kwenye gari yake kuelekea kazini.

“Nikifika nipakue mtandaoni Gemu lingine lile  limenichosha sina ninachojua mimi kuhusu kazi za kukaa ofisini  najua kurudha ngumi tu na kuua”Aliwaza Roma  huku akikanyaga pedeli kuelekea kwenye kampuni.

Roma alifika na siku hii Recho alionekana kuchelewa kufika kazini kwani Roma hakumkuta,wakati Roma  anawasha Tarakishi yake kwa ajili ya kupakua gemu , mara aliingia Doris akiwa ni mweye kununa  , baada ya kumfikia  bila hara ya salamu alimpa Roma Tablet alioishika mkononi na Roma aliichukua na kuangalia baadhi ya picha zake zikiwa mtandaoni.

“Huyu mwanamke kumbe alikuwa waziri , mbona mdogo hivi”Aliongea Roma kwa sauti na kumfanya Doris azidi kufura kwa hasira.

“Usiniambie huyu ni wewe kweli?”

“Bebi Doris ni mimi ndio, si unaniaona kabisa hapo kuna kipi cha kuficha sasa”Aliongea Roma na kumfanya Dorisi azidi kushangaa inakuwaje huyu mwanaume hata kujitetea  hafanyi , maana  kwa alivyokuwa anawajua wanaume lazima wangeanza kutoa sababu ila kwa Roma yeye alikiri.

“Bebi Doris huyu mwanamke alikuwa  mrembo ila sikumdhania  ni Mbunge”Doris alimwangalia Roma kwa hasira na kisha bila ya kusema neno aliondoka na Roma hakujali , aliendelea kupakua gemu lake kwa aili ya  kuendelea kucheza.

Ndani ya ofisi ya  CEO Dorisi aliingia na kumkuta Edna akiwa  anaendelea na kama kawaida yake mwanamke huyu kwa uchapaji kazi , baada ya Dorisi kumfikia.

“Bosi umeona taarifa ya Roma inayozagaa mtandaoni?”

“Hapana sijaona”Aliongea  Edna na Doris alimkabidhi  Edna ile tablet na Edna aliangalia kwa muda huku uso wake ukijikunja kiasi.

“Kumbe alivyoniaga anatoka kidogo alienda kukutana na huyu kimada , mwanaume Malaya huyu”Alijiwazia Edna na kisha alimrudishia  Doris  Tablet yake.

“Hii sio  nzuri kwa image  ya kampuni Edna”

“Doris haya ni mambo binafsi ya Roma na wala hayahusu kampuni hivyo swala hili achana nalo na kaendelee na kazi”Aliongea Edna na Dorisi  aliondoka huku akionekana ni mwenye hasira kweli .

Baada ya Dorisi kuondoka Edna alijikuta akivuta pumzi  na kuangalia mlango aliotoka  Edna.

“Maskini hata Dorisi kashaingia kwenye mtego wa huyu mwanaume”Aliwaza na kisha akanywa kahawa kidogo na kuendelea na kazi.

*****

Upande mwingine ndani ya  mji wa Mheshimiwa Mstaafu sehemu iliokuwa ikifahamika kama Village G alionekana mheshimiwa Raisi mstaafu bwana Kigombola Hamisi Hamisi  akiwa  ameketi kwenye sofa za bei ya hali ya juu kwenye jumba lake hili  la kifahari ndani ya kijiji hiki , muda huu   ilikuw ni asubuhi ya saa nne akiangalia runinga huku akipata chai yake taratibu.

Wakati mzee huyu mwenye mvi zilizoacha uwararaza  akiendelea kuangalia runinga mara aliingia moja ya  Sekretari wake  na kumsogelea.

“Mheshimiwa kuna taarifa  hapa  nataka kukutaarifu juu ya Madam Neema”

Mheshimiwa alichukua ile simu ya Iphone kiana huyu aliokuwa ameishikilia na kuanza kuangalia picha zilizokuwa zimetumwa kwa njia ya Watsapp , Moja ya picha hizo zilimuonesha Roma akiingia ndani ya chumba na Neema huku wakiwa wameshikana viuno.

Mzee huyu mara baada ya kuona picha hii alionekana kukunja sura kwa hasira  kali  na kisha alichukua kikombe kilichokuwa na chai mbele yake na kunywa kidogo na kisha  alimgeukia huyu bwana.

“Erick nataka taarifa zote za huyu mwanaume kwenye hizi picha  kabla ya saa saba mchana”

“Sawa mheshimiwa”

Neema Luwazo kwa wale wasio mfahamu  ni kwamba mwanamke huyu  ni moja ya wanawake maarufu sana ndani ya ulingo wa siasa , moja ya sifa kubwa iliomfanya mwanamke huyu kuwa  maarufu ni uzuri wake  aliokuwa nao.

Kabla ya neema kujiingiza katika siasa alikuwa  ni msanii na mwigizaji mkubwa sana  lakini pia ashawahi kushinda shindano la umiiss   miaka kadhaa iliopita.

Kipindi cha uongozi wa mheshimiwa Kigombola  ndio kipindi ambacho Neema kwa mara ya kwanza alipata uteuzi  na kuwa mkuu wa wilaya ndani ya jiji la Dar es salaam , uteuzi ambao ulianza  kufanya watu wahisi kuna kitu kinachoendelea kati  ya mheshimiwa Kigombola na Neema.

Licha ya  tetesi hizo zilizokuwa zikisambaa mtandaoni , hakukuwa na ushahidi wowote wa kuthibitisha taarifa hizo na hata pale Neema mwenyewe alivyoulizwa alisema.

“That is just Groundless Rumors na siwezi kuzungumza lolote  kwani sipo kama watu wanavyonifkiiria , nimefikia hapa kutokana na juhudi zangu mwenywe”Hilo ndio jibu ambalo alilitoa Neema miaka kadhaa nyuma , lakini jibu hili pia lilionekana kuwa na mashiko  kwani licha ya mwanadada huyu kuwa mkuu wa wilaya , lakini pia alisifika kwa kuwa na mali nyingi sana ambazo alirithi  kutoka kwa wazazi wake miaka kadhaa baada ya wao kufariki katika ajali ya ndege.

Utajili wa Neema ulikuwa ni kiasi cha dola za kimarekani milioni 570 wakati akiwa anarithi  mali zote za wazazi wake kama mtoto wa kipekee  alieachwa duniani.

Baada ya miaka kadhaa ya kufanya kazi Neema alizidi kujizolea umaarufu mwingi kutokana na uchapakazi wake  , lakini pia uzuri wake uliopitiliza  lakini pia utajiri aliokuwa nao ambao ulizidi kuongezeka miaka hadi miaka.

Katika kipindi chote hiko cha kuwa mkuu wa wilaya ,Neema hakuwahi  kuhusishwa na mwanaume yoyote yule kutoka nae kimapenzi jambo ambalo lilifanya mashilawadu wengi kila siku kuandika   makisio yao  ya hapa na pale , lakini   tetesi hizo zilikuja kukoma mara baada ya Neema kubeba ujauzito  na pale alipohojiwa  juu ya baba wa mtoto ndipo alipoweka wazi kuwa baba wa mtoto ni mheshimiwa Kigombola na kipindi hiki mheshimiwa kigombola alikuwa kwenye muhula wa mwisho wa uongozi wake.

Kwanzia hapo  , ndipo ilipofahamika Rasmi kuwa Neema ni chombo ya wakubwa na watu wengi walijiweka mbali na mwanamke huyo , hakuna mtu alieweza kumsogelea na kumtongoza  Neema  jambo ambalo lilimfanya mwanamke huyu kuwa mpweke kiana licha ya kuwa na mahusiano na mheshimiwa.

Baada ya uongozi wa Senga , Neema ndipo alipopata  ubunge wa viti maalumu na kuteuliwa kuwa naibu waziri wa Sanaa na michezo  , kipindi hiki mtoto wa Neema wa kike afahamikae kwa jina la maarufu la Donyi alikuwa na miaka   minne tayari.

Upande wa mheshimiwa Kigombola alikuwa amekufa na kuoza juu ya Neema  , alikuwa haambiwei chochocte kuhusu Neema na  kutoka na mapenzi yake juu ya mwanamke huyo  , alikuwa ameweka watu ambao walikuwa wakimchunguza mienendo yake kwa siri.

Upande wa Neema licha ya kuzaa na mheshimiwa , hakuwa na mapenzi yoyote  kwake na kuna tukio ambalo lilimtokea  Neema na kumfanya  aombe msaada wa Mheshimiwa na hapo ndipo ulipoanza mwanzo wa  kulala na   mheshimiwa mpaka  kupata mtoto Donyi na yeye alimchukulia Kigombola kama ‘stepping stone’ kwenye carear yake ya kisiasa.

Sasa hii ndio maana siku Roma wakati anamsogelea Neema watu wengi walikuwa wakimshangaa kwa ujasiri wake wa kutoogopa kuonekana na  chakula ya wakubwa , ila kwa upande wa Roma hakuwa akimjua kabisa Neema kwani hakuwahi kukaa na kuanza kufatilia siasa  za Taifa la Tanzania.

*****

Ni muda wa saa kumi na mbili na Nusu za jioni Roma alieonekana kupendeza  sana kwa suti  nyeusi ya bei ghali , iliochangamshwa na tai  , huku chini akiwa na kiatu kikali cha kampuni ya Louis Vuitton pamoa na Saaa ya Rolex  mkononi , hakika ungemuona Roma usingemdhania ni yule  wa siku kadhaa zilizopita  aliekuwa akibeba mizigo.

Dakika chache mbele za Roma kusubiri chini ya eneo hili la Sebuleni akiwa na Bi Wema  mara hatua za viatu zilisikika zikishuka kutoka  juju na hapo ndipo Roma alipogeuza macho  yake  na kumuona mwanamke mrembo kama  malaika akishuka , huyu hakuwa mwingine bali alikuwa ni mrembo Edna.

Edna alikuwa akivutia haswa , muonekano wa mavazi yake  jioni hii ulimfanya  Roma kupagawa , bwana huyu  alikuwa ameona  wanawake warembo ila kwa Edna alikiri alikuwa mzuri tena Zaidi ya mzuri , kila kiungo cha mwanamke huyu katika mwili wake kilikuwa kimepangwa kimpangilio ili kuleta radha ,Edna alikuwa amevalia  kigauni flani cheupe  cha kampuni yake  kilichokuwa na shingo ndefu  na kumuacha  shingo yake  kama ya Kinyarwanda wazi  na kumfanya apendezeshwe Zaidi na mkufu wa  madini ya Almasi  uliokuwa ukimeremeta shingoni  kuonekana vyema , kigauni hiki kilikuwa sio kirefu sana  na kumfanya  miguu yake ya bia ilionona na kuwa na michirizi flani  kuonekana vyema , kilichomfanya Edna kuzidi kuwa mzuri  ni  rangi ya sura yake iliokuwa sio nyeupe wala sio nyeusi , alikuwa na karangi flani hivi  kiasi kwamba ukimwangalia baba yake na mama yake Edna   kwenye picha ungejiuliza ilikuwaje wakawa na mtoto wa aina hio maana mzee Adebayo alikuwa ni mbaya wa sura 

“This is God Masterpiece of creation which he ever did”Aliwaza Roma huku akitabasamu   na kumeza mate kwa wakati mmoja akiwa anamwangalia mke wake.

“Mke wangu umzuri sana mpaka nayaonea wivu macho yangu”Aliongea Roma na  kumfanya Bi Wema agune na kutabasamu  na kwa Edna alionyesha hali ya aibu kwani macho ya Roma yalikuwa yakimtazama sana  kwa matamanio.

“Twende tunachelewa”Aliongea Edna na kisha Roma alitangulia mbele  kuelekea kwenye magari na kutoa V8 nyeusi ya bei ghari  na kuisogeza mpaka  katikati ya jumba hili na kisha akatoka na kumfungulia Edna  mlango.

“Kuitwa mume wa Edna ni heshima Tosha hata kama haonekani  kuwa na mpango wa kunipa kitumbua” Aliwaza Roma  na kisha  alitoa gari hio  taratibu kuelekea ikulu.

Previoua Next