Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Wakati Roma anatoa gari kwenye Geti kuna hisia flani zilimfanya aangalie nyuma kwenye kioo , kwani alihisi kuna gari ambayo ilikuwa ikiwafatilia, hakujua ni watu gani ila hakutaka kujali sana kwani alijiamini mno .

“Nimeona ile habari kwenye gazeti Roma na nikutahadharishe tu  achana na yule mwanamke atakuingiza kwenye matatizo”Aliongea Edna wakati wakiwa wanakaribia  ndani ya Lango la ikulu wakisubiria kufunguliwa.

“Hilo lisikupe shida mke wangu”.Edna hakuongeza Zaidi  mpaka wanaegesha gari na kushuka  chini , huku wakwanza kutoka ni  Roma na akakimbilia upande wa kushoto na kumfungulia  Edna mlango huku Edna akiweka tabasamu bandia mbele ya watu waliokuwa ndani ya eneo hilo wakiwa wapo kwa ajili ya kuwapokea.

“Fatma  kutana na mume wangu anaitwa Roma , Roma huyu ni katibu muhtasi wa ikulu anafahamika kwa Fatuma Adinani”Aliongea  Edna kwa tabasamu akimtambulisha Roma mbele ya fatuma ambae alikuwa yupo eneo hilo kwa ajili ya kuwapokea .

Fatuma alikuwa ni mwanamke ambaye kwa haraka haraka umri wake haukua mkubwa sana  ni kati  ya miaka therathini kupanda , lakini alionekana kuwa na cheo kikubwa ikulu.

“Nafurahi kufahamiana na wewe Fatma”Aliongea Roma na kisha walitangulizana na Fatma  kuelekea sehemu  maalumu ndani ya eneo  hili la ikulu.

Upande wa Roma  hii ilikuwa ni mara yake ya kwanza kuingia ndani ya eneo hili la Ikulu , lakini alionekana kama mtu ambae   alikuwa mzoefu kwani hakuonesha uoga wa aina yoyote ile na hata walivyokuwa njiani pale alipoambiwa kuwa safari hio ni ya kwenda ikulu ni swala ambalo halikumshangaza sana kwani aliamini mke wake ni mtu  mkubwa hivyo ni swala la kawaida kwa yeye kualikwa na mheshimiwa kumtembelea Ikulu.

Wafanya kazi wa hii ikulu walionekana kuwa katika kazi zao , huku ulinzi ukiwa umeimarishwa kila kona , jambo ambalo kwa Roma lilimfurahisha.

“Angalau wanajitahidi , licha ya mapungufu mengi”Aliongea Roma baada ya kuongekana kukagua eneo hilo pamoja na ulinzi wake wote.

Chakula cha usiku kiliandaliwa baina ya familia ya mheshimiwa Raisi na  mualiko huo hakukuwa wa kikazi  ulikuwa ni kama wa kifamilia  , kwani hata waandishi hawakuwepo  , swala ambalo pia lilimshangaza Roma kuona mke wake  kuwa na ukaribu  sana na familia ya mheshimiwa Rais.

“Edna karibu mwanangu”Alionekana mwanamke mmoja mrembo wa  makamo  akiwasogelea wakina Roma  , huyu hakuwa mwingine bali mke wa mheshimiwa Raisi Senga afahamikae kwa jina la  Damasi Senga.

“Asante Mama”.

“Huyu ni  mume wako Doris  , jamani unatabia mbaya , umefunga ndoa hata kuniambia mama yako”Doris aliona aibu  kidogo.

“Nisamehe sana Mama  ila   ukweli swala hili lilitokea ghafla sana  na ni makubaliano yangu na mme wangu , tumefunga ndoa lakini hata sherehe hatujafanya”.

“Nimekuelewa Doris wala hata usijisikie vibaya , Karibu sana Mr Roma  Doris ni kama mwanangu maana mama yake alikuwa rafiki yangu sana  tulisoma wote”Aliongea Mama huyu kwa ukarimu wa hali ya juu na kumfanya Roma atabasamu.

“Nashukuru sana kwa kunikaribisha kwa ukarimu”

“Dorisi twendenii  tulikuwa tunawasubiri ninyi tu mfike”Aliongea mama huyu na kisha aliongoza njia na kuingia kwenye chumba kilichokuwa kushoto kilichokuwa kimetanganishwa na mlango mkubwa.

Baada ya kuingia hapa ndani ndipo Roma aliposhangazwa na ufahari wa hili eneo , kulikuwa na mpangilio mzuri sana wa  samani zilizokuwepo hapa ndani , huku katikati kukia na meza kubwa ambayo ilikuwa imezungukwa na watu  watatu  wawili mwanaume na mmoja mwanamke.

“Oh!Doris karibuni sana  ,tulikuwa tukiwasubiri nyie tu”Aliongea mzee huyu  ambaye anafahamika kama raisi kwa waanzania ,lakini ndani ya eneo hili alionekana kama baba wa familia.

“Asante sana Mheshimiwa” huku wakisalimiana .

“Karibu sana Roma jisikie huru  kabisa”Aliongea mheshimiwa  huyu na kumfanya Roma atabasamu huku akiangaliana na mheshimiwa kiume.

“Ashley kumbe umerudi , sina taarifa zako”.

“Ndio Doris  nina siku nne tu tokea niingie nchini”Aliongea huyu mwanamke mrembo  huku macho yake yote yakimwangalia Roma , na alionekana ni mtu ambaye hakufurahishwa na uwepo wa Roma hapo ndani na Roma mwanzoni hakumuona Ashley baada ya kukutanisha macho yao  ni kama waliwasiliana  kwa macho  na Roma aliketi karibu na  mke wake.

“Ushamaliza masomo  yako ya PhD?”

“Ndio nishamaliza”

“Hongera sana ni hatua kubwa umefikia”Aliongea Doris na kumgeukia  kijana ambaye muda wote alikuwa kimya akiwa pembeni.

“Denis mbona  huwachangamkii wageni kama hujawaona”Denisi alikuwa ni kijana ambaye umri wake hakuonekana kuwa mkubwa sana , alikuwa na rika la miaka 22 hivi  na alikuwa chuo mwaka wa mwisho huko  nchini Norway.

Denis alimwangalia Edna na kisha aliweka tabasamu feki usoni  na kisha akamsalimia  Edna na  Roma , ila kwa upande wa Roma kuna ambo ambalo aliligundua katika macho ya Denis ila hakutaka kufikiria sana , aliweka kapuni swala hilo.

Basi Roma alitambulishwa   kwa mheshimiwa Senga kama mume halali wa Edna  na chakula kilifana sana kwani kilienda na stori nyingi za hapa na pale huku pongezi zikielekezwa kwa Edna kwa kupata mume kwani lilikuwa ni  jambo la kipekee sana katika maisha ya mwanamke na hakuka aliekuwa anajua kuwa wawili hao walikuwa na ndoa ya mkataba na yote waliokuwa wakifanya ni maigizo..

Mheshimiwa Raisi muda wote alikuwa akimwangalia Roma kama mtu ambaye  alikuwa na maswali mengi juu yake , ukweli ni kwamba mheshimiwa Raisi licha ya kutumia ushawishi wake na mamlaka yake kupata taarifa zilizokuwa zikimuhusu Roma lakini hakuambulia chochote .

“Mheshimiwa Taarifa  zinazomuhusu Roma zinaonekana kuwa nyeti sana  ndani ya shirkika la CIA na wamegoma kutuatia taarifa yake”.Aliongea  Kabwe baada ya kuwasilisha utafiti wake aliokuwa ameufanya juu ya Roma.

“ kwa hio unamaanisha kuna taarifa  inayomuhusu Roma  ambazo CIA hawataki kuzitoa?”.

“Ndio mheshimiwa ni Top Confidential na hata baadhi ya viongozi wa CIA hawana uwezo  kuangalia taarifa yake ni baadhi ya viongozi wakubwa tu ndio wenye  uwezo huo”Aliongea Kabwe na kumfanya mheshimiwa ashangae Zaidi na kuzidi kujiuliza maswali ya Roma ni nani kiasi cha taarifa zake kufichwa na CIA.

Baada ya kuona  swala lake limegonga mwamba  aliona njia pekee ni kumkaribisha Edna ikulu kwenye chakula cha jioni ili aweze kuoanana na Roma aweze kumfahamu  hata kwakumuangalia.

Ukweli licha ya Senga kumkaribisha Roma ikulu lakini alikuwa akikumbuka vyema kwa kitendo cha Roma kumuita babu, hivyo hakuwa akimpenda kwa dhati.

Baada ya chakula mheshimiwa  alimwita Edna kwenye ofisi yake kwa maongozi Zaidi akimuacha Roma akiongea na wanafamilia.

Edna mara baada ya kufika kwenye  ofisi ya mheshimiwa , Senga  aliingiza mkono kwenye mfuko wa suruali yake na kisha alitoa Flash disk na kumkabidhi Edna.

“Hii inahusu nini mheshimiwa?”

“Ukifika nyumbani chukua muda wako kuangalia kilichomo humo ndani kila kitu kinajieleza ni wakati wako  kujua swala hili”Aliongea Mhesimiwa na kumfanya Edna ashangae  lakini hakujiuliza maswali mengi aliichukua na  kuiweka kwenye mkoba wake.

“Umekutana kutana vipi na Roma mpaka kufikia hatua ya kufunga ndoa?”.

“Ni stori ndefu mheshimiwa, ila naweza kusema ni mwanaume wangu wa kwanza katika maisha yangu na atakuwa wa mwisho vilevile”Snga alishangazwa na jibu hilo la Edna na kisha akatabasamu.

“Unamwamini?”Edna alishangazwa na  swali hilo , ila hapo hapo akakumbuka kuwa Roma alionekana kuwa na mwanamke mwingine  kwenye mitandao hivyo alijua hueana mheshimiwa atakuwa na taarifa hizo ,ila asichokijua Edna ni kwamba Senga anajua pia uhusiano wa Roma na Edna.

“Kusema ukweli kuhusu kumuamini bado , ila moyo wangu unamuhitai Zaidi kuwa karibu  yake”Alijibu Edna.

Mheshimiwa alishangazwa  na maneno hayo na kujiuliza Roma ni mwanaume wa aina gani kiasi cha kuliliwa na kila mwanamke.

Huku upande wa Roma muda wote alikuwa akimangalia  Ashley  kwakumuibia ibia na kwa Ashley alikuwa akimwangalia  Roma kwa kuibiaibia.

Roma aliomba kuoneshwa sehemu ya maliwato na alielekezwa na mfanya kazi na hio ni kama ikawa nafasi kwa Ashley kwani na yeye alinyanyuka na kuelekea upande huo huo, huku Denis aliekuwa  akionga na mama yake wasielewe kitu baina ya hao wawili.

“Naona ushakuwa mume  wa mtu tayari?”Ilikuwa ni sauti iliosikika nyuma ya Roma aliekuwa akikojoa  na kumfanya atabasamu kifedhuli.

“Wewe unamuonaje mke wangu  chombo kile”.

“Mwanaume unaroho mbaya sana wewe , hivi unajua ni kiasi gani mimi na Profesa Clark tulivyoteseka na tunavyoendelea kuteseka  juu  yako?”.

“Juu ya Clark , mimi na wewe ni swala ambalo lilikoma nilivyoamua kurudi Tanzania na  nadhani itakuwa jambo jema mkiendelea kuheshimu uamuzi niliochukua , sasa hivi nishaoa na nitaishi kumlinda mke wangu na kuishi maisha ya kawaida”.

“Unajidanganya Ramoni Edna sio Seventeen licha ya wao kufanana  kila kitu ,Seventeen ashakufa Ramoni”

“Ashley nadhani  unakosea  sehemu moja , hakuna sehemu ambayo nimesema Edna ni Seventeen , kwangu yule mwanamke ashakufa alivyojirusha baharini kipindi kile na nishaacha kumfikiria katika maisha yangu , Edna ni Edna na nimeamua kuishi naye maisha ya  kawaida”Aliongea Roma na kisha kumpita Ashley kurudi alikowaacha wenzake.

“Clark kashapata dawa ya kukutibu Ramoni”Aliongea Ashley na Roma hakusimama alimsikia vyema , lakini aliongeza  mwendo na kurudi alikotoka.

Baada ya madakika kadhaa mheshimiwa Senga aliomba kuongea na Roma na Edna bila shida  alikubali na Roma aliitwa ofisini.

“Karibu sana Mr Roma”

“Asante sana mheshimiwa , nimeitikia wito”

“Nimekuita hapa  tuongee kidogo maana Edna kwangu ni kama mtoto wangu wa kumzaa , na mama yake nafahamiana nae vizuri tu”Roma alitingisha kichwa kukubaliana nae.

“Japo sikufahamu vyema  ulikotoka na wapi umezaliwa , ila  nataka unihakikishe kwamba Edna atakuwa salama na hataumizwa na matendo yako”.

“Mheshimiwa unaonekana umetafuta taarifa zinazonihusu mimi  tayari”aliongeaRoma.

“Ni kweli nimejaribu  na inaonekana wewe sio wa kawaida na ndio maana nataka kukupa onyo . lolote likimtokea Edna basi jua  mimi na wewe tutakuwa maadui”.

“Mheshimiwa Edna ni mke wangu na swala la kumlinda pia litakuwa juu yangu kama  mume hivyo naomba swala hili lisikuumize kichwa  , lakini pia unachojaribu kutafuta kuhusu mimi naomba uache na uendelee kuwaongoza watanzania  wazidi kupata mema ya nchi”Aliongea Roma na kumfanya Senga aone kweli anaongea na mtu  ambae  hakuwa wa kawaida , kwani Roma hakuonesha hofu yoyote ile ya woga mbele yake na alikuwa mtu wa kunyoosha maneno  tofauti na viongozi wengi walio chini yake.

“Okey ni hayo tu bwana Roma”

“Hakuna shida mheshimiwa naamini na wewe pia utaacha kufukunyua taarifa zinazonihusu” Mheshimiwa Senga aliitikia kwa kichwa na Roma alitoka.

“Fii***ck huyu Roma ni nani kwanini anajiamini hivi?” Mheshimiwa alionekana kuwa mwenye hasira kwa kutokumjua Roma ni nani.

Mheshimiwa alikuwa akitweta kwa hasira kwani katika maisha yake aliamini kama atakuwa raisi basi atakuwa na uwezo wa kuogopwa na kila mtu ndani ya taifa hili , lakini jambo hilo likawa rofauti kwani mpaka sasa amekuwa na watu wawili ambao  hawakuwa wakimuogopa ,  wa kwanza alikuwa ni The Doni na wa pili ni Roma aliejitokeza.

Uliongea nini na mheshimiwa?” Aliuliza Edna baada ya kutoka nje ya geti hili la ikulu baada ya hafla yao kuisha .

“Hehe mke wangu nadhani ushajua alichoniambia”

“Sijui ndio maana nimekuuliza”

“Aliniambia ohh yeye na wewe  ni kama mwana na baba hivyo nisije kukuumiza”

“Kama ni hivyo walausijali maana mkataba wetu wa ndoa uko pale pale , baada ya miezi  sita kuisha kila mtu atafanya mambo yake”

“Hata usijali”Aliongea Roma  huku akiendelea kuendesha gari kwa umakini na ndani ya madakika kadhaa alikuwa  mbele ya geti la nyumba , lakini kabla hajaingiza gari ,wakai huo geti likiwa limefunguliwa , mara simu yake  ilianza kuita mfululizo na kumfanya Roma  aangalie na kuona mpigaji ni  Juma , alishangazwa na upigaji huo , kwani tokea siku alivyoagana na Najma hakuwasiliana na Juma

“Juma kuna nini?”.

“Roma Wamemteka Najma ?Ilikuwa ni sauti ya wasiwasi ambayo aliisikia Roma  na alijua kuna tatizo.

“Edna naomba ushuke kwenye gari?”

“Nini?”

“Nimekuambia shuka kwenye gari kuna sehemu naenda”

“Yaani uende kwa hawara wako na gari yangu”Roma hakutaka kumsikiliza , alirudisha  gari nyuma kwa spidi akitaka kugeuza kitendo ambacho kiliwafanya hata walinzi kushangaa.

“Sawa ngoa nishuke”Aliongea Edna na kuhcukua mkoba wake na  ile anashuka tu gari ya  Roma ilitokomea kama mshale kiasi cha kumfanya atumbue  macho  kwa spidi aliotoka nayo Roma.

*****

“Erick umepata taarifa gani inayomuhusu?”Aliuliza mheshimiwa Kigombola mara baada ya Erick  kuingia ndani ya ofisi ndogo   ya mstaafu ndani ya Village G.

“Mheshimiwa kwa taarifa  niliopata inamuonesha Roma  ni  mbeba mizigo kutoka soko la Kariakoo  mpaka siku  chache zilizopita”

“Unamaanisha nini mpaka siku chache zilizopita?”

“Roma  sikuchache zilizopita alifunga ndao na CEO Edna”

“Niniii!” Mheshimiwa alijikura akishangazwa na  swala hilo.

“Ndio mheshimiwa Edna na Roma ni wanandoa”

“Nadhani kuna taarifa nyingine Zaidi ya hio Erick inawezekanaje mbeba mizigo amuoe mtu mkubwa kama Edna bila ya sababu”.

“Mkuu kuhusu hilo  sijui , ila taarifa nyingine ambayo imenishangaza inaonesha Roma ni mhitimu kutoka chuo cha Harvard  amemaliza masoko katika uongozi wa  biashara , lakini pia  katika CV yake aliowasilisha  ndani ya kampuni yetu , inaonekana  anauwezo wa kuzungumza lugha ishirini na mbili”

“Lugha ishirini na mbili , hilo sio jambo la kawaida  kwa mtu wa kawaida Erick , watu wa nmna hio huenda wakawa  majasusi wanaofanya kazi  kwa siri  au ni  Assasinators”.

“Ndio muheshimiwa nimejaribu kufatilia taarifa  Zaidi kuhusu  mahali anapotokea  na alipozaliwa inaonekana hakuna taarifa hizo”Mheshimiwa huyu alimwangalia Erick kwa muda na kisha akafikiria  jambo.

“kazi nzuri Erick unapaswa kwenda sasa , mpaka hapo nitaendelea mwenyewe”

“Sawa mheshimiwa”

Baada ya Erick kutoka  Kigombola alitafuta namba  ya simu yenye kodi ya nje ya nchi na  kisha kupiga simu.

“Mr kigombola  it`s pleasure to hear from you after long while”

“It s true mr Keneddy  and am so sorry  thar I did not contact you  for this long  but you are one of people that have special place in my life”

“It`s good  you realise that , but I presume this call  has request you want to ask me”.

“Its true kenneddy , I need all informations regarding someone who graduated at harvad”

“Just give me the name and I will  look for it in minutes”

“He is Roma Ramoni he is now living here  in Tanzania”

“Okey wait a second I will get back to you”

Mheshimiwa alikata simu akisubiria  taarifa  hio na alichokuwa anawapendea wazungu nikwamba ukiwaomba jambo hawanaga maswali mengi ,ingekuwa ni wabongo angekuwa ashakuuliza  maswali kibao kwa mfano unataka taarifa zake za nini  na ilichukuwa dakika chache tu taarifa simu yake ilianza kuita.

“ Yes Kennedy”

“I got info.. about him , it seems odd but it is true  there is information regarding him graduating  at  havard business School”.

“What is odd Kennedy?”

“He was adopted  with one of Michigan  tycoon in business Mr Robert Eglon from when he was  fourteen”.

“So what is Odd”

“There is no information  regarding where he lived before being adopted”

“You  mean there is no info .. like he was from Tanzania or anything like that?”

“Yes!,  that  which looks Odds Kigombola”.

Huyu  Roma ni nani” Ni swali pekee ambalo  liliibuka kwenye kichwa chake maada ya kupataa maelezo hayo kutoka kwa Kennedy , aliemwambia kuwa ni kweli Roma anaonekana kumaliza chuo Harvad lakini pia anaonesha kulelewa na  familia ya mfanyabiashara mkubwa  huko Michigan Marekani lakini jambo ambalo linaonekana sio kawaida ni kwamba haikuelleweka Roma aliishi wapi  kwa miaka kumi na tatu nyuma kwani alianza kulelewa akiwa na miaka kumi na nne.

“Nadhani swala pekee ni kuagiza vijana wangu wamteke  ili tumuhoji nadhani ndio njia rahisi”Aliwaza mheshimiwa

Previoua Next