Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Kwa  jinsi Roma alivyokuwa anaendesha gari , kila mtu alishangazwa na uwezo huo , Roma alikuwa akikwepa magari kama chizi  kitendo ambacho wengi  walidhania ni  kama Muvi , dakika chache mbele alikuwa  akiingia Mbagala , Roma aliendesha ndani ya mtaa huu uliokuwa na baadhi ya viwanda  na kampuni za usafirishaji , lakini ile anakaribia nyumba  anayoishi  Najma , Alimuona  Juma akiwa  nje , alisimamisha Gari na kushuka haraka haraka.

“Niambie nini kimetokea?”Aliongea Roma huku akiona baadhi ya watu wakiwasogelea na walionekana kujua nini kimetokea.

“Kuna majambazi ambayo siyafahamu  , yamekuja na kunitishia na bunduki na kisha wakamkamata Najma na kuondoka nae , huku wakiniachia maagizo kuwa nikitaka kumpata dada yangu  akiwa mzima , niwasiliane na wewe na uende  sehemu watakayo niambia”

“Sasa wamekuambia  ni sehemu gani?”.

“Hawajaniambia wamesema watapiga simu  ndani ya lisaa limoja”Aliongea Juma aliekuwa na wasiwasi huku wapangaji wakiwa wamewazunguka , kuna waliokuwa wakimwangalia Roma kwa wasiwasi ili kuona kama atakuwa na njia ya kumuokoa Najma , ila kuna wale waliokuwa wakishangaa mabadiliko ya Roma.

Baaada ya lisaa ni kweli simu ya Juma iliita na alipokea haraka haraka huku akiweka Loudspeaker na hata Roma kusikia.

“Dogo nadhani ushamwambia muhusika?”

“Ndio yuko hapa”

“Mpatie simu”Ilisikika sauti na Roma  aliinyakua kutoka kwenye mikono ya Juma na kuweka silence huku akiiingia kwenye Gari yake  na kufunga mlango.

“Ongea”.

“Roma hakikisha unakuja mahali ambapo tunakuambia kwa sasa na uje peke yako , ukifanya ujinga wa aina yoyote kama kutaarifu polisi  Najma atakufa kifo cha kikatili sana”Ilisikika sauti hio.

“Nipe simu kwanza niongee na Najma siwezi kuja kabla sijasikia sauti yake mimi sio mjinga kiasi hiko”Aliongea Roma na dakika chache  sauti ilisikika kwenye  masikio yake.

“Najma uko salama?”

“Roma usije watakuua , wana siraha usifanye wanach..”Alipokonywa simu.

“Sikia Roma eneo ni Vikindu , hakikisha unakuja peke yako”Ilisikika sauti na kumfanya Roma akasirike na hio ni baada ya simu ile kukatwa na Roma hakujiuliza sana alitoa gari eneo hilo kwa spidi kiasi cha kufanya  watu watumbue macho.

Roma alikuwa na hasira mno , kwanza kilichomkasirisha ni kwamba watu hao wamemuambia kwenda Vikindu lakini hawakuwa wameeleza Vikindu sehemu gani.

Roma baada ya kuingia ndani ya barabara ya Kongowe , alizidi kuendesha gari hio kwa spidi na ilikuwa na spidi kweli kwani zilikuwa zile gari  za gharama ya hali ya juu , alikuwa akiyapita magari  kama mwehu kiasi kilichofanya kuwanyanyua  polisi wa  barabarani.

“Shi**t huyu mpuuzi ni nani huyu anaendesha gari kwa spidi hivi kama hii nchi ya baba yake?”Alionekana  mwanamke trafiki  akiwa amekasirika mara baada ya kuisimamisha gari ya Roma lakini ilimpita  bila ya kusimama na kumuachia upepo tu.

“Huyu hanijui vizuri  ngoja nitamkamata tu”Aliongea mwanadada huyu mrembo huku wenzake wakiwa ni wenye kushangazwa na  spidi ya gari  iliowapita ndani ya eneo hili la Kongowe.

“Mage unaenda wapi?”

“Namfukuzia yule mshenzi, wasiliana na Trafiki wa mbele yetu uwape taarifa juu ya hio gari waizuie  “Aliongea mrembo huyu  mwenye kalio  kubwa huku akikimbilia Pikipiki yake kubwa ya kijapani Kawasaki Ninja H2/R hii ni  moja ya pikipiku ya kifahari sana  na ni chache sana Tanzania , inaupiga mwingi sana hii pikipiki  kwenye spidi , ina Zaidi ya 322bhp na imeingia kwenye kumi bora ya  pikipiki  zenye spidi sana duniani , thamani yake sio chini ya milioni 100 za kitanzania. .

Haikueleweka ni kivipi  mtembo huyu Trafiki  anaimiliki vipi  kwani ni ya bei kubwa mno.

“Unafikiri ataifikia ile gari?”Aliuliza Trafiki wa kiume mweupe.

“Hio pikipiki ina upiga mwingi sana hio anaweza kuifikia ila inategemea na uwezo wake wa kuendesha”Aliongea Trafiki maji ya kunde.

Ni dakika chache tu  Roma alikuwa ashafika Vikindu na kusimamisha gari huku akijiuliza ni uelekeo gani aelekee, alikuwa akiangalia daladala zilizokuwa zikiingia ndani ya  stendi , lakini ile anajiuliza simu yake ilianza kuita tena.

Simama  kwenye bango kubwa  la Tigo hapo Stendi  na kuna mtu atakufuata  hapo”Roma aliangalia mahali sahihi pakuweka gari yake na  kulisimamisha na kisha alishuka na kwenda kusimama chini ya Bango kubwa la Tigo.

“Hey! Brazaaa  mambo ni vipi , kuna wana wameniambia nije nikuchukue nadhani wewe ndio Roma”Roma aliitikia kwa kichwa huku akimwangalia huyu kijana ambaye anaonekana kuharibiwa na madawa ya kulevya.

Baada ya dakika chache za kukata kona hatimae walivuka kiwanda kimoja amacho Roma hakukitambua kilikuwa cha nini  , walipita upande wa kushoto na kusimama kwenye geti kubwa jeusi na mlango ukafunguliwa na Roma akaingia na  hapa ndipo alipojua eneo hili ni la kuhifadhia nondo  , kwani zilikuwa nyingi upande wa kulia , ni kama ghala.

Alitembea  kwa kuongozwa na kijana huyo huku akiangalia baadhi ya  mabaunsa waliokuwa wameshikilia bunduki za SMG wakilinda  eneo hili kitendo ambacho kilimshangaza Roma , inakuwaje nhi yenye Amani kama hii kuna watu wanamiliki Siraha kiholela ila hakutaka kujisumbua maaana sio kazi yake, aliingia ndani na hapa ndipo alipomshuhudia Najma aliekuwa amefungwa kwenye nguzo, na kitambaa mdomoni , alionekana kuchoka kweli kweli alikuwa akitoa  jasho  kiasi kwamba baadhi ya Sehemu za Hijabu  yake zimeloana.

Roma alimuonea huruma mrembo huyo kwa mateso aliokuwa akipitia , aligeuza macho na kuangalia mabaunsa haya Zaidi ya  matano  yakiwa na bastora na kisha  aligeuka upande mwingine akimuangalia jamaa ambae alionekana kuwa ndio bosi kwani yeye hakushika  siraha yoyote na alikuwa amekaa kwenye kiti na sigara yake mkononi.

“Roma unaonekana sana kumjali huyu mrembo, cheupe dawa mpaka ukajileta mwenyewe”Aliongea jamaa hili huku likionekana kutafuna bablishi.

“Nishafika mfungulieni Najma aondoke , ili tuongee shida  yenu na mimi”Aliongea Roma kwa hasira.

“Acha upuuzi wewe , yaani unaniona mimi  joka la kibisa , nimlete mrembo kama huyu ndani ya  hili eneo  halafu nimuache bila hata ya kumuonja”Aliongea Jambazi huyu  huku akimshia kidevu Najma na kumuangalia kisha  akaanza kumnusa usoni na shingoni.

“Kananukia vizuri na vijdomo vyake vidogo nadhani hata ka ‘K’ kake ni kadogo”Aliongea huyu jambazi mkuu na kumfanya Roma azidi kupandwa na hasira , ila hakutaka kufanya jambo lolote la kijinga kwani alihofia usalama wa Najma kwani watu hawa walikuwa wengi na wote walikuwa na siraha,Najma muda wote alikuwa mwenye kutokwa na machozi , alishindwa kuongea  ila alionekana kumhurumia Roma kwani walikuwa wamemziba na matambala.

“Mfungeni kwanza  , nataka nimfanye demu wake mbele yake”Aliamrisha na Roma alifungwa na yeye kwenye nguzo .

“Unajua kwanini nina shida na wewe fala?”.

“Wewe ndio umeniita hapa , naona unaanza kuuliza maswali ya kipuuzi”Aliongea Roma lakini alijikuta akianza kupigwa ngumi za Tumbo nyingi za haraka haraka na kisha akamaliziwa na Teke, kiasi cha kukohoa na kutema damu.

“Ulifanya kosa kubwa sana kulala na Rose,Mwanamke ambaye nimemhangaikia tokea anaingia ndani ya hili jiji , na wewe na hako kamashine kako ukajiona kidume, sasa leo nitahakikisha namto**mba huyu demu mbele yako , halafu nitahakikisha hautoki  na hiko kibolo chako  hapa ndani”Aliongea bwana huyu huku akionekana hakuwa ni mwenye utani kabisa.

“Hahaha .. sasa kama umemhangaikia ulishindwa nini  kumpata , acha kuudhihirisha ubwege wako kwangu bwana , wewe ni fala tu”Aliongea Roma kwa hasira na kumfanya bwana huyo awaambie vijana wake wamsulubu  Roma , kitendo ambacho kwa Najma kilimuumiza mno kwani ni kama  alikuwa akipigwa yeye.

Roma alitema damu kwa mara nyingine  na bwana huyu aliridhshwa na kipondo hiko na sasa kazi iliokuwa inafuata ni kukamilisha jambo lake  kwa Najma.

“Ukimgusa huyo mwanamke nakuhakikisha  nitakufanya kitu ambacho hutokisahau katika maisha yako”Aliongea Roma, kwani licha ya kupewa kichapo cha uhakika lakini alionekana kama hajapigwa vile.

“Ila lile jambazi kuu halikujali sana  alimfungua Najma na  kisha alimshika mkono kwa nguvu na akaanza kumvuta upande mwingine uliokuwa na maboksi.

“Kitendo kile kilimuuzi sana Roma kiasi kwamba  mboni za macho yake zilianza kubadilika na kuwa za kijani na hata wale  majambazi wengine walishuhudia hilo.

“Boss!”Aliita jambazi mmoja aliekuwa karibu na Roma , lakini kabla hajajibiwa alijikuta akiwa hewani na hakujua ni kwa namna gani , alipigwa na hapa Roma alikuwa amekata Kamba zote zilizokuwa zimemfunga .

“Mpige Risasi mbona mnamuangalia”Aliongea yule Jambazi  kuu , lakini katika hali ambayo hata yeye hakujua imetokea vipi , aliskia sauti ‘Shwaa.. Shwaaa  tiii …Aiii, Shwaa… Aiii..’  na mabodigai wote walikuwa chini huku wakiugulia maumivu.

Jambazi kuu alishangazwa na uwezo huo wa Roma na kuanza kutetemeka kwa woga , lakini sio yeye  hata Najma alishangaa .

Wakati Jambazi hili  kuu likiwa linashangaa , lilijikuta limefikiwa na Roma na kishikwa shingoni na kuning`inizwa hewani kwa mkono mmoja kitendo ambacho Najma ni kama alikuwa akiangalia Muvi za kihindi zile zenye uongo mwingi , yaani unakuta steringi kabeba gari na mkono mmoja.

“Sipendagi kutishiwa kwenye maisha yangu , pili Onyo mara moja  ukirudia ni kifo, tatu sipendi watu wanaotumia  watu wangu wa karibu kupambana na mimi Sababu hizo tatu zinanipa  uhalali wa kukuondoa duniani  maana wewe ni takataka”Ilikuwa sauti nzito kama ya Roboti.

“Najma Fumba macho mpaka nikwambie fumbua ”Aliongea Roma kwa sauti nzito  na Najma alifumba kweli na ndani ya dakika  mbili alimwambia fumbua na hapo ndipo Najma alipopigwa na mshangao , kwani majambazi yote manne  yalikuwa yamelala  chini huku yakiwa yamefunikwa na  maboksi kwenye uso huku Roma akilipapasa  lile jambazi kuu , lakini hakuambulia cha maana Zaidi ya pakiti ya sigara za SM na kuzichukua na kuweka mfukoni.

“Hawa wote ni maiti , ndugu zao watakuja kuchukua miili   na sijui kama wanasafirisha  au wanazika hapa hapa”Aliongea Roma bila wasiwasi na kumsogelea Najma  ili amshike mkono , lakini Najma alirudi nyuma kwani alikuwa ni mwenye kutetemeka  mno na alimuogopa Roma , hakumuona kama yule Roma aliekuwa akimjua  na kumpenda ila huyu ni Roma mwinginekabisa  mkatili na muuaji.

“Nifuate nyuma kama unaiogopa”Aliongea Roma na kuanza kupiga hatua na Najma japo alikuwa akimuogopa  Roma ila alimkimbilia kwani aliogopa  kukaa  na maiti na isitoshe ilikuwa ni usiku.

Roma baada ya kukatiza  kona ya chumba hiki alimwambia Asubiri kwa  dakika chache lakini Najma hakusubiri ,  aitoka na kuangalia nje na hapo ndipo aliposhuhudia kwani alimuona Roma akitembea kama upepo flani hivi ulioambatana na kivuli cha mtu , na alichoweza kusikia ni ‘Crak shwaa..Aiii, Crak ..   Shwaa ..Aii  Crak.. Aiii Crak Crack;’.

Majambazi yote yalikuwa chini Roma akiwa ashayavunja shingo , yaani ni kitendo cha dakika  moja tu , Roma ashamaliza kazi  na aligeuka nyuma na kumuona Najma na kumuita kwa ishara ila Najma  alizidi kumuogopa Roma.

“Najma nisamehe sana kwa kufanya mambo haya mbele yako , ila sikuwa na jinsi , sahau kabisa kilichotokea leo na nitahakikisha hakuna mtu anaekugusa tena”Aliongea Roma ila Najma hakujibu kitu aliishia kutoa machozi tu na kutangulia mbele.

Roma na yeye hakutaka kumuongelesha , alijuwa mwanake huyo  atakuwa kwenye mshituko mkubwa sana , hivyo aliona muda pekee ndio utakao weza kumuweka sawa.

Baada ya kutembea kwa dakika kadhaa hatimae , walifika barabarani, alimuona kijana ambaye alikuja kumchukua  akiendelea na upiga debe  na Roma hakumjali sana , lakini ile anakaribia gari lake , aliona matrafiki wawili watatu wameegamia gari yake wawili wakiwa wanawake na mwingine akiwa ni mwanaume.

Na wakati huu macho yake yalikuwa yasharudi kwenye hali yake ya kawaida , na alikuwa Roma  ambaye Najma alikuwa amemzoea , sio yule muaaji wa kutisha.

“Jamani habari zenu “Alisalimia Roma kama kawaida yake huku akitabasamu  na Mage polisi aliekuwa akimfukuzia , aligeuza macho yake na kumwangalia Roma juu hadi chini, kwa muonekano wa Roma hakuonesha kuweza kumiliki ndinga kama hio  na ndio maana baada ya kumuangalia kwa sekunde aligeuka na kuendelea kupiga stori  na  trafiki mwenzake wa  kike huku akimuacha trafiki wa kiume akidili na Roma.

“Jamani mmesimama kwenye gari yangu nataka nikampumzishe huyu mrembo si , mnaona jinsi  alivyochoka na pia giza kali hili”Hapo ndipo Mage aligeuka tena na kumwangalia Roma.

“Wewe ndio mwenye hii gari?”

“Ndio mrembo”

“Uko chini ya ulinzi kwanzia sasa , kwa kukiuka sheria za barabarani lakini pia kwa kuidharau serikali”.Aliongea Mage huku akiweka uso wa usiriasi.

“Mrembo nilikuwa na dharula ndio maana”

“Mpuuzi sana wewe , hata kama unadharula gani hii nchi sio ya baba yako kuendesha gari  kama kichaa , unataka kusababisha ajali na usiku huu na mipombe yako”Aliongea Mage kwa hasira.

Roma aliona hana cha kujitetea , alimwangalia Najma alivyokuwa amechoka na kumuonea huruma.

“Utaenda na sisi mpaka polisi , usituletee shida kisa unaendesha gari  la kuazima, Edwin endesha gari yake  mpaka kituoni”Aliongea   Mage na kumuamrisha trafiki wa kiume achukue funguo kwa Roma.Trafiki yule alitabasamu meno yote nje .

“Leo naenda kuonja kuendesha huu mchuma , Mungu anipe nini mimi  nikimfikisha kituoni hata nikifa nitakuwa na Amani”Alijiwazia huyu trafiki kichwani mwake baada ya kupokea ufunguo

Najma , Roma  waliingia kwenye gari na safari ya kuelekea kituoni ikaanza

Previoua Next