Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Roma aliingia ndani ya jengo hili mapokezi na kumkuta mwanadada mmoja  alievalia tisheti nyeusi na kofia ya Chepeo ya kampuni ya Nike na mkufu  shingoni , mwanadada huyu hakuwa  mrembo sana , kwani kwanza alionekana kama wale wanawake ‘matom boy’.

“Nipo hapa kwa aili ya kuonana na kiongozi mkuu wa kampuni ya PANZ”.Yule Dada alimwangalia Roma kwa kumsanifu.

“Wewe umetokea wapi?”.

“Nimetokea  kampuni ya VEXTO na nipo hapa kwa ajili ya kuchukua marejesho ya mkopo”

“Okey nenda floor namba nne  ndio ofisi ya Chief ilipo”Aliongea  huyu mwanadada huku akitabasamu rohoni.

Wakati Roma akielekea  juu , mwanadada  huyu  alipiga simu.

“Chifu  leo kaja mwanaume kutoka VEXTO”.

“Mwache aje tumkate Ma**mbu”Yule mwanadada alijikuta akicheka   kicheko cha furaha akionekana kufurahishwa na jambo hilo.

Roma baada ya kufika ndani ya hii ofisi kwanza  alishangazwa na  sauti alizokuwa akisikia , kulikuwa na mlio  wa vimashine sio vimashine , ni kama mlio wa wadudu flani hivi.

“Ndio maana wakajiita mapanzi “Aliwaza Roma wakati akiingia ndani ya hili jengo.

Roma alishangazwa na muonekano wa Floor hii , kwanza kabisa  hakukuwa na meza kama meza ambazo ungedhania kuwa humu ndani ni kampuni bali  kulikuwa na vitanda vya Deka upande wa kulia  vitatu , na vyote vikiwa na magodoro ambayo hayakuwa yametandikwa.

Chini kulikuwa na Zulia la  rangi ya maua maua , huku wakionekana  vijana  watano waliokuwa wamekaa chini kwenye hili zulia na katikati yao kulikuwa na  kijisturi na kwa haraka haraka Roma aligundua  hii sio kampuni kama kampuni,  jina hilo la kampuni  walipewa ili kulinda kile kinachofanyika , ila hii sehemu aliweza kujua ni sehemu ya kupimia madawa ya kulevya , kwani kwa kutumia pua zake aliweza kuvuta hewa ambayo alikuwa akiitambua vyema  ,harufu ya ‘Coccaine’.

“Hey! Jombaa , nadhani mabosi wako wameamua kukutoa kafara mpaka kukuagiza  kuja hapa kutudai”Aliongea jamaa mmoja ambae alikuwa na mwili mkubwa sana uliojaa mazoezi  na kuonesha dharau mbele ya Roma na wale wengine wakacheka.

“Kino huyu leo Chief  atambadilisha jinsia”Aliongea jamaa mmoja mwenye midevu mwembamba aliekuwa akijikuna.

“Sikieni nyie wavuta bangi , nimekuja hapa kuonana na huyo chifu wenu anipe changu nisepe”Aliongea Roma na kuwafanya wale mabwana wamwangalie kwa ujasili wake , lakini waliishia kucheka tena, huku  lile jitu lenye miraba mine lilichukua unga kidogo kwenye kucha  na kunusa na alionekana kujibusti.

“Aiii .. traaaaa tatatata,,, traaaaa aiiii .. tiitiiii”Yule bwana alionekana kupagawisha na madawa yale na hapa Roma ndipo alipokuja kugundua kwanini  alikuwa akisikia sauti kama za Panzi.

Lile jamaa linaloitwa Kino baada ya kuona  ashabusti mwili alimwangalia Roma na kisha kumsogelea kwa njia ya kumpiga ngumi.

“Aaargh..”Kino alikuwa amepokea bao  la uso  lililompelekea damu kuanza kumvuja  puani , alijishika puani huku akisikia maumivu yaa ajabu na kisha akagusa zile damu kwa mshangao na kuzilamba  huku hasira zikiongezeka maradufu,wenzake walishangazwa na kitendo kile  Roma alichofanya kwa Kino

Jamaa  baada ya kuona kadhalilishwa na Roma , hasira ziliongeza na kurusha ngumi kwa pupa lakini  Roma akaudaka ule mkono na  kisha akauzungusha kwa nguvu kiasi cha kufanya  Kino azunguke kama anachezeshwa Rumba na Roma alimpiga bonge la teke mgongoni na kwenda kutua kwenye ukuta huku akitanguliza pua ile iliopata majeraha dakika chache zilizopita.

“Maaa … maaa  ..aiii”Jamaa alitoa ukulele kwani  katika maisha yake haawahi kusukumwa na nguvu kama ile  na kujigonga , maumivu yake yalikuwa sio  ya kifani kabisa , aliona nyota nyota ,Roma hakumwacha vile vile  aliendeleza kipigo na ndani ya dakika chache tu tu wale vijana wote walikuwa  wamepiga magoti  kwenye zulia hili ,huku kila mmoja akiwa na maumivu , kuna waliokuwa wakitokwa na damu puani , kuna waliokuwa wakitokwa na damu  mdomoni , kuna ambaye alikuwa ameshika jicho lake.

“Chifu  wenu yuko wapi?”Aliongea Roma huku akikagua madawa yaliokuwa kwenye kijisturi na akachukua unga kidogo na kuvuta.

“Mnavuta mabaki mabaki, halafu nimeuliza Chifu wenu yuko wapi hamjibu, au nianze”

“Chifu yuko  chumba chake cha mapumziko m huku akinyoosha  uelekeo wa chumba  na Roma aliangalia na kuona mlango upande wa kushoto  na kuufuata, lakini kabla ya kuufungua aligeuka nyuma.

“Ole wenu mtu yoyote akimbie”Na kisha akafungua na kuingia ndani.

Roma aliangalia chumba hiki na kukuta mwanaume mmoja mwenye mwili wa wastani , akiwa amemwinamisha mwanamke Mbuzi kagoma akisindilia mpini wake.

“Nyie mafala , acheni use***nge, kwani huo upupu niliowapa  mtoe nyege zenu hautoshi”Aliongea mzee huyu pasipo kugeuka , alionekana alikuwa akikaribia mshindo na Roma aligundua hilo kwani alitembea na kupeleka mkono  kwa nyuma  na kushika Dudu  kitendo kilichomfanya bwana yule ashituke.

“Uwiiii …. Arghhh.. unaniua  wewe k*ma”Alipiga yowe huyu bwana  baada ya Roma kuminya dudu yake huku bwana huyu akilala chali kwenye kitanda na mwanamke yule ambaye alionekana kuwa mmama alishangazwa na kitendo hiko cha ghafla.

Roma hakuwa  hata na kinyaa licha ya dudu la bwana huyu kuwa na utelezi , baada ya kuona mateso hayo yamemridhisha alimuachia .

“Na wewe ondoka”Aliongea Roma huku akimfukuza yule  mwanamke na alichukua  nguo zake na kukimbilia uchi nje.

Roma baada ya kumwachia Chifu , alianza kukagua chumba hiki kikubwa kilichokuwa na kabati huku akimpa mgongo chifu ,Roma alifungua kabati moja na kutoa macho baada ya kukuta maburungutu ya hela yamepangwa kwenye kabati hili .

Chifu baada ya kuona Roma amempa kisogo na hakuwa na habari nae , alichukua chupa iliokuwakwenye kijimeza cha kitanda na kumsoglea Roma huku akiwa ni mwenye kujikaza  kwa maumivu aliokuwa akisikia .

Ni kama Roma alikuwa anamsubiria kwani ile anamkaribia aligeuka  kwa spidi na kumtwanga ngumi ya jicho na kumfanya bwana huyu aone nyota nyota  huku akitoa ukulele.

Roma aliendelea na ukaguzi wake , na kuvuta Droo na kuona bastora , aliitoa na kuitoa magazine kwa kitendo cha haraka sana na kuona kuna Risasi.

“Barreta 582 ya 1984” Aliongea  Roma aliikoki   kwa haraka na kisha akamgeukia  Chifu, na kumnyooshea na bwana yule alinwangalia kwa jicho moja  na kuanza kutetemeka.

“Unadaiwa kiasi gani na VEXTO?”

“Tulikopa  bilioni  moja ila tulitakiwa kurudisha Bilioni mbili”

“Sasa kwanini hamjarudisha mpaka sasa?”Aliongea Roma huku akiwa amekalia kiti na bwana huyu akiwa amepiga magoti akimwangalia Roma kwa woga.

“Bossi alitupa maagizo tusirudishe”.

“Bosi wenu ni nani?”Jamaa alionekana kuwa na wasiwasi sana  kutaa jina la Bosi na Roma alilijua hilo aliingiza kidole kwenye Triga.

“Naongea usiniue”

“Ongea sasa …”

“Bossi wetu ni Hassani”.

“Acha upuuzi mimi nitamjuaje Hassani , ongea vizuri Hassani ni nani  , nataka melezo ambayo  yatanifanya nimjue harakaharaka”.

“Ni kiongozi mpya wa kundi la Black Mamba”Aliongea huyu bwana na hapa ndipo alipomkumbuka Karim  aliemuua siku mbili nyuma.

“Sasa hapo nimekupata , lakini hujamalizia , huyu Hassani yukoje  na kwanini aliwazuia kutolipa hela za Kampini mlizokopa”.

“Sikupewa maagizo mengine  , Zaidi ya kuambiwa nisirudishe”Aliongea kwa woga

“Hapa ndani mna kiasi gani cha pesa?”Jamaa kimya na Roma akanyanyika kumsogelea .

“Zipo .. zipo  milioni  mia nne”.

“Na kwenye akaunti kuna ngapi”Jamaa kimya  na Roma  alizunguka kwa nyuma yake  na kuingiza mkono upande wa kushoto wa mbavu na kumfanya bwana huyu atoe yowe.

“Kwenye akaunti kuna ngapi?”

“Bilioni .. bilioni mbili”Roma alitabasamu  na kisha alimwambia bwana huyu anyanyuke na waelekee kwenye ofisi yake ,baada ya kutoka Roma aliwakuta  watu wake wakiwa  wamekaa vile vile na kuona yes , dozi imewaingia na wamekuwa na Adabu.

Roma alitabasamu baada ya kuona kifaa kama simu cha kufanyia miamala  cha Equit bank .

“Tuma pesa zote kwenye akaunti hizi nitakazokutajia sasa hivi?”Aliongea  huku akimuonyesha Chifu kwa ishara akae  kwenye kiti chake  cha ofisi na bwana huyu  , alitamani kufanya jambo ila aliogopa”

“Bossi ataniua   nikifanya  kama anavyotaka?”

“Endelea kufikiria ujinga wako tu , nitakuua mimi sina utani, eniwei labda unaona nafanya utani ngoja nikuonyeshe kama niko siriasi”Aliongea Roma na kisha kwa haraka sana alimshika yule bwana kiganya cha mkono wa kushoto  na kilichosikika ni viungo vya Jointi  na misuli ikipishana.

Chifu alitoa ukulele wa aina yake kiasi kwamba hata  vijana wake wa kazi nje walisikia  na kuzidi kumuogopa Roma.

Chifu  hakuwa na jinsi , hakutaka kuvunjwa kiganja kingine cha mikono , na alitii haraka haraka na kufanya kama alievyoelekezwa  na ndani ya dakika chache , akaunti yake ilisoma Dollara mia nne na akatuma kiasi cha Bilioni moja na  mia sita kwenye akaunti ya VEXTO.

Baada ya zoezi hilo kuisha , Roma   alimwamuru kijana mmoja aliekuwa na nafuu  kidogo na kumwambia  aweke hela zote zilizokuwa kwenye kabati  kwenye begi  na ndani ya dakika chache  akawa ashakamilisha kazi yake.

Ila bado hakuwa ameridhika , alivuta  faili moa  lililokuwa kwenye Meza na kuangalia  na hapa akatabasamu.

“Enhe Chifu tumalizie , haya Magari  yanayoonekana hapa  kwenye hizi karatasi yako wapi?”Aliuliza Roma na Chifu kama kondoo  alimwangallia Roma.

“Kwenye Basementi chini”Aliongea  na Roma akatabasamu .

“Ongoza njia”

Roma alitoka kwenye hii ofisi na kisha akafunga mlango kwa nje  na funguo akiwafungia wale wengine na kisha wakazama kwenye lift na chifu , ndani ya dakika tu walikuwa eneo la chini kabisa ya jengo hili na kwa mtu wa kawaida usingejua kuwa chini  kuna Basementi ,tena kubwa kabisa , jambo hili pia lilimshangaza  Roma.

Aliona sehemu ambavyo ilikuwa kama Maabara na alijua kwa vyoyvyote  hapo ni sehemu ya kutengenezea madawa.

Wakati akiendelea kumfatisha Chifu aliekuwa kwenye hali mbaya ya maumivu ya kiganja na jicho , alisikia sauti ya mguno alipopita kwenye Chumba kilichokuwa kikinekana  kufungwa na mlango wa chuma , hisia za Roma hapo hapo zikamwambia kuwa hapo ndani kuna  mtu.

“Humo ndani kuna nini,Hebu fungua”Aliongea Roma na Chifu alisogelea chumba hiko na kukifungua kwa funguo iliokuwa ipo upande wa kulia  kwenye kiboksi na hapa ndipo Roma alipatwa na mshangao baada ya kumuona mtu aliekuwa  hapo ndani akiwa hatamaniki kwa majeraha, alimsogelea  mtu huyu aliefungwa kwa Kamba  akining`inia  , huku mwanga mdogo ukiwa unammulika , alimuinua kichwa chake kwa mikono yake na  hapa ndipo aliposhangaa.

“Juma!!!”Aliongea Roma kwa mshangao  na akajiuliza inakuwaje Juma akawa yupo mahali hapa , alimwangalia  Chifu na kuonekana alikuwa akitaka maelezo.

“Nini kimetokea kwanini yupo hapa?”Hapa ndipo  alipopewa mkasa wote na alikuja kugundua kumbe Juma alikuwa akihusika na  kutekwa kwa Najma , alikasirika mno na alitamani kumpiga tena Juma , lakini kwa hali ya nusu uhai aliokuwa nayo Juma aliona aache.

“Juma alijichanganya sana kufanya kazi na Karim”Aliongea  Roma huku akimkumbuka Najma , alijiuliza  mwanadada huyo atakuwa kwenye hali gani, lakini pia alijiuliza kama  atakuja kujua kuwa Juma anahusika na kutekwa kwake  ingekuwaje.

Previoua Next