Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Mage  kwanza kabisa alishangazwa na urembo wa Najma kiasi kwamba alijiulizaje huyu Jambazi akapata pisi kama hio kwenye Maisha yake  , lakini hakukuwa na majibu sahihi yaliopatikanan katika halmashari ya kichwa chake.

“Najma usilie tena .. kaka yako alipatwa na matatizo na kwasasa yupo kalazwa anapatiwa matibabu , mimi naenda na   hawa polisi kuna jambo la kuweka sawa , hakikisha kaka yako anapatiwa matibabu sawa?”Aliongea Roma  kama mwanaume na mwanadada huyu aliekuwa ametokewa na machozi  kutingisha kichwa kwa kukubaliana nae , lakini licha ya kumuuelewa alionekana hakuwa tayari kumuachia Roma.

“Eti kuna jambo la kuweka sawa .. yaani huna aibu unamuongopea mwanamke mrembo kama huuyu  hahaha.. wewe mwambie unaenda jela na atafute  bwana mwingine”aliongea Mage kwa kebehi  na kumfanya Nama amwangalie mwanadada huyo kwa hasira.

“Wewe dada wa kitrafiki , mimi namjua Roma sio Jambazi na hayo maneno yote unayoongea   hayakai kwenye Maisha ya Roma”Aliongea Najma na kumfanya Roma amwangalie mwanamke huyu na kutabasamu.

“Hilo litajulikana mrembo eh na Ushahidi tulionao , hakuna mengi ya kuzungumza na nitahakikisha  hili Jambazi halirudi mtaani kuwarubuni Watoto wakike kama wewe , Mrembo wewe ni mhanga  huyu jamaa kakubuhu  hivyo shukuru   ninamtoa kwenye Maisha yako , nakwambia utanishukuru baadae”

Aliongea Mage na baada ya kumaliza tu  Difenda ya polisi iliingia hapo ndani na Mage  aliwaamrisha polisi wengine waendeshe gari  ya Roma na  Mage akapanda kwenye pikipiki yake  huku wakimwacha Najma anaetokwa na machozi.

“Najma nitarudi baadae sawa , usiwe na wasiwasi . hakikisha kaka  yako anapatiwa matibabu”aliongea Roma na kufanya watu waliokuwa  eneo hili la hospitali  washangazwe na Roma  maana maneno yake yalikuwa  na nguvu sana kwenye mioyo ya watu hawa.

Ni baada ya lisaa limoja tokea Roma aingizwe ndani ya kituo kikubwa cha polisi  wilaya ya Temeke  alionekana mwanamke mmoa mrembo sana  maarufu sana hapa nchini akiingia akiwa ameshikilia mkoba wake , huyu mwanadada alikuwa mrembo sio  kawaida , ila licha ya urembo wake wote hakuwa akimfikia mrembo Edna.

Mwanadada huyu hakuwa mwingine bali alifahamika kwa  jina la Nadia Alfonso  , lakini nchini na duniani   wengi walikuwa wakimuita kwa jina la ‘Goddes of law’ umaarufu wa jina hili mwanamke huyu hakupewa tu , ila yote  hayo ni kutokana na heshima aliojijengea katika ulingo wa kutafsiri sheria, usomi wa mwanadada huyu pamoja na kipaji chake  kilichangia pakubwa heshima aliokuwa nayo  .

Nsdia Alfonso ni mwanasheria  aliemaliza masomo yake ndani ya chou kikuu cha Harvard kuanzia digrii yake  ya kwanza mpaka ngazi ya juu yabisa ya PhD , unaweza ukajiuliza inakuwaje mwanamke mdogo  kama huyu kuwa na mafanikio makubwa kama hayo  , lakini yote hayo ni kutokana na juhudi binafsi  za mwanadada huyu  tokea alipkuwa mdogo , lakini pia ukijumlisha na uwezo mkubwa wa akili Mungu aliombariki nao.

Umaarufu wake unakuja mara baada ya kusimamia kesi  ya Raisi  mstaafu wa Korea kusini , kesi ambayo ilikuwa ni gumzo sana duniani  , kesi ambayo ilikuwa ikimtuhumu  raisi huyo  kwa ufisadi , lakini kwa uwezo mkubwa wa Nadia raisi huyo  alipata haki yake na Dunia  ikatambua kuwa raisi huyo sio kama walivyomdhania  kwani alisafisha jina lake , lakini kufanikiwa huko  kunazua gumzo baada ya Raisi huyo kutoa  hotuba ya shukrani mbele ya waandishi wa habari na  kumshukuru Nadia Alfonso kama mwanasheria mkuu alisimama kidete katika kufanikisha  kwake kupata haki yake kisheria , lakini pia kusafishika kwa kile alichokiita kusingiziwa kesi ya ufisadi , kwanzia siku hio ndipo jina la Nadia  liliposambaa duniani ,umahiri wake uliotukuka aliounesha katika kesi hio , kwanzia kukusanya Ushahidi ulimpa heshima kubwa sana., umaarufu ulimfanya mwanadada huyu kutafutwa na watu wengi maarufu duniani  kwa ajili ya kusimamia kesi zao hayo ni machache kuhusu Nadia A.k.a Goddes of Law.

Polisi waliokuwa wakimjua mwanadada huyu ambaye alikuwa akipewa heshima kubwa na Taifa  kwakuwa mtanzania wa kwanza kung`ara   katika fani ya sheria , walihaha , walikuwa wakijiuliza  imekuwaje mwanasheria huyu  akaja kwenye kituo chao , na si  hao tu , hata  Mage aliekuwa  yupo kituoni hapo kuhakikisha Roma hachomoki alishangazwa  sana.

Kwanza kabisa Nadia kwake alikuwa ni Role Model , kwani katika Maisha yake Mage alikuwa akipenda sana sheria  na alipigania sana ndoto yake hio kuja kuwa mwanasheria huku  nguvu kubwa  ya kimsukumo  ikitoka kwa  Nadia ambaye  watu wengi katika sheria walimuita ‘Chain Breaker’ yaani mkata  minyororo au kwa tafsiri ya haraka haraka yaa maana hi ni kwamba mtu ambaye ameshinda vizuizi vyote yeye kama mwanamke na kuudhihirishia ulimwengu kama mshindi ,  sasa wewe jaribu kuwaza mtu ambaye ulimhudusu kwenye Maisha yako yote  akatokea mbele yako ghafla tu , basi  hio ndio namna ambavyo Mage alishituka  na hakuwa akiamini kwamba mtu aliekuwa mbele yake alikuwa ni ‘Goddes of law’ mwanamke aliekuwa akimpenda na kumpenda Zaidi ya neno lenyewe.

Mage  machozi yalianza kumtoka , alikumbuka miaka kadhaa nyuma alivyokuwa akipambania kusoma sheria , lakini kutokanana na kile alichokiita mweyewe uwezo wake mdogo  kiakili  alikuwa akifeli kila mara na kumpelekea kukata tamaa na kuachana na sheria na kujiunga   na jeshi la polisi huku akiamini kwamba polisi na wanasheria  wanafanana kwa vitu vingi ,aliamini licha ya kufeli kuwa mwanasheria  kuwa polisi  sio mbali sana na ndoto zake.

Mkuu wa kituo cha polisi  ndio wa kwanza kutoka kwa ajili ya kuonana na Nadia ili kumpa heshima zote kubwa , kwani mwanadada huyo hakuwa mdogo kabisa ndani ya taifa hili, lakini licha ya hivyo  polisi wengine wote walijipanga mstari kwa ajili ya kutoa heshima kwa Goddes of law.

“Karibu sana mheshimiwa ,, Ini furaha kwangu kufamiana na mrembo kama wewe na mtu mkubwa sana duniani  karibu kituoni kwetu”.

“Asante  sana , lakini sijaja hapa kimatembezi nipo hapa kama mwanasheria  na nina mteja wangu hapa”Aliongea Nadia kwa sauti yake tamu na kuwafanya polisi wote washangae , anachozungumza Nadia , kwanza hapo polisi hakukuwa na mtuhumiwa mwenye hadhi ya juu kama anavyoongea mwanadada huyu ,  kwani hakuwa na taarifa ya mtu wa hadhi alieshikiliwa na kituo chake Zaidi  ya vikapuku tu waliowafunga.

“Mheshimiwa Labda  umekosea  , hapa hatuna mtu tuliemshikilia ambaye  ni wa hadhi kuhudumiwa na wewe kisheria”

“Kwangu kila mtu anaehitaji sheria anapaswa kuhudumiwa na mimi na sijawahi kubagua watu kutokana na nafasi zao katika jamii”Baada ya kuongea hivyo  alimpita mkuu huyu wa kituo .

“Pumbavu nimeongea ujinga”Aliwaza mkuu huyu wakituo huku akifatisha nyuma na waliingia kwenye ofisi  ya kuonana na wageni.

“Nipo hapa kwa ajili ya  mteja wangu anaefahamika kwa jina la Roma Ramoni”Aliongea  na kumfanya Mheshimiwa ashituke na kujiuliza Roma ni nani mpaka mtu  mkubwa duniani kama huyu aje kumtoa.

“Mheshimiwa mtu unayemzungumzia ni jambazi ambalo tulikuwa tukilitafuta kwa muda mrefu sana  na  leo tumemkamata   hatuwezi  kumuachia kirahisi” Aliongea Mkuu wa kituo  na hakuwa tayari kumuachia Roma  kizembe hivyo , kwani alishuhudia yale maburungutu ya pesa  na alikuwa ashayapigia plani kabisa  wa kulipa deni ambalo alikuwa akidaiwa na anaemdai kumkalia kooni , lakini pia alikuwa akipanga kulipa kodi  ya nyumba anayoishi maana hakuwa akiishi kwenye nyumba za polisi maaruufu kama kota , lakini pia alikuwa akisumbuliwa na mchepuko wake juu ya  hela ya mtaji  na alikuwa amenyimwa  kitumbua na mchepuko huyo kwa muda wa mwezi mmoja , pia mke wake  alikuwa akidaiwa vikoba  sasa kwa matatizo hayo yote aliona kwa pesa hizo  zilizofika kwenye ofisi yake , aliona ni Mungu ndio  kaleta fursa , sasa hakuwa mzembe kiasi hicho licha ya kwamba mtu aliekuwa mbele yake alikuwa mkubwa tu  katika sheria, tamaa ya pesa ikisukumwa na matatizo aliokuwa nayo  aliona asimamie msimambo wake

“Nishatangulia kusema sipo hapa  kaa mtu maarufu , ila nimekuja kwa ajili ya mteja wangu na nina Ushahidi  wa kutosha ambao unamfanya mteja wangu kutokuwa na makosa”

Aliongea mwanadada huyu kwa upole na kujiamnini kisha akatoa Ushahidi wake  na kwa namna ambavyo mwanadada huyu alielezea  na kuoonyesha uhahidi  Mkuu wa kituo alijisemea moyoni  yes hapa kakutana na profesheno  mwenyewe.

“Naomba kwanza kuonana na mteja wangu”Aliongea Nadia na mkuu wa kituo hakuwa na  sababu ya kumzuia .

Huku upande wa nje Mage alikuwa kwenye mshangao mara baada ya kusikia  kuwa Mrembo Nadia amekuja kwa ajili ya Roma , alishangaa sana sana , inakuwaje choko kama Roma kuja kupata huduma ya kisheria kutoka kwa mwanasheria nguli duniani  na hapo hapo swali la Roma ni nani lilianza kuibuka kwenye kichwa chake.

“Pluto!” Aliita  Nadia na kumfanya Roma anyanyuie uso wake na kuangalia sauti tamu inayomwita kwa jina ambalo hajalisikia muda mrefu.

“Haha.. Nadia  unafanya nini hapa?”Roma alishangaa  sana na alionekana alikuwa akimfahamu vyema Nadia  na mrembo huyu aliachia tabasamu ambalo  ungekuwa mwanaume rijali kama Roma ungekuwa hoi.

“Za siku nyingi  The Great Pluto  nimefurahi sana kukuona tena , hujui tu nilivyokuwa nikitamani kupata nafasi ya sisi kuonana tena tokea  tulivyo achana nchini Korea Kusini”

“Nadia hayo mambo tuache kuyaongelea sasa  hivi , nataka uniambie unafanya nini hapa”Aliongea Roma kwa usiriasi na mwanadada huyu alimwangalia  na kuonekana kama hajafurahia , kwani alitamani  kumuona Roma akiwa kwenye mshangao na furaha ya wao kukutana tena baada ya miaka mingi.

“Nipo hapa   kama mwanasheria mpya wa kampuni unayofanyia kazi, na nipo kukutoa”Aliongea mwanadada huyu na kumfanya Roma ashangae.

“Okey! Basi fanya hima nitoke hapa   maana nina njaa sio poa”Aliongea  Roma huku akijigusa tumbo , yaani kwa Roma alionekana hakuwa akimchukulia  kabisa Nadia kama mtu mkubwa vile tofauti na wengi walivyokuwa wakimchukulia , kwani Nadia alikuwa akipewa heshima ya jiuu mpaka na maraisi wa Afrika , lakini kwa Roma alimuona Nadia kama wa kawaida.

“Tayari mpaka sasa upo huru”Aliongea Nadia na mlango ulifunguliwa   na akaingia mkuu wa kituo akiwa ni mwenye kutoa jasho  jingi usoni.

“Mheshimiwa mteja wako yupo huru”Aliongea mkuu huyu huku akionekana ni mwenye  kuhema , sijui nini kimemtokea maana ujasiri aliokuwa nao  umeisha wote.

“Daah ! Afadhali maana sio kwa njaa hii ,Nadia uko vizuri  sana kwenye  kazi yako”Aliongea Roma huku akiamka wa kwanza na kutangulia mlangoni akimuacha Nadia aliekuwa akimwangalia mwanaume huyo kwa hali ya hudhuni  inaonekana alitarajia kitu kikubwa Zaidi kutoka kwa Roma.

“Niletewe begi langu lenye pesa niondoke  nina njaa ”Aliongea Roma  huku akimwangalia Mage aliekuwa akimwangalia bwana huyu pasipo kummaliza  na alionekana ni mwenye maswali mengi sana katika kichwa chake.

“Boss begi lako hili hapa”Aliongea Afande mmoja kwa heshima na kumpatia Roma begi lake na Roma alilibeba  lakini  akasita.

“Huu uzito ni tofauti   , kuna kiasi cha pesa kimepungua”Aliongea Roma na kuwafanya mapolisi hawa wote waangaliane kama kondoo.

“Rudisheni pesa  zote zilizokuwa humu ndani  , najua kiasi kamili cha hizi pesa , mkigoma nitakaa hapa nakuhesabu zote na hakuna mtu kuondoka nikihakikisha hela ni pungufu  nitawasachi wote”

“Rudisheni pesa , acheni kuvunja sheria  la sivyo swala hili sitoliacha lipite hivi hivi”Aliongea Nadia baada ya kumuona Roma anaongea na Polisi wote walitoa jasho akiwemo mkuu wa kituo.

“Huyu jamaa mahela yote  hayo kajuaje nimepunguza vibunda viwili”Aliwaza mkuu wa kituo huku akikumbuka vibunda alivyoficha ofisini kwake,wakati akiendelea kutoa   jasho  simu yake iliingia ujumbe na kufungua  na kuangalia meseji  ilitoka kwa jina la ‘Mke Wangu’

“BABA LEAH  MWENYE NYUMBA ANAKUSUBIRI NA ANASEMA HAONDOKI MPAKA UTOE PESA YAKE ,  HALAFU  GESI IMEISHA  MPAKA SASA HATUJUI TUNAPIKA NA NINI” ilikuwa ni meseji  kutoka kwa mke wake iliandikwa kwa herufi kubwa kabisa kuonesha msisitizo , mzee huyu jasho lilizidi .

“Hapana sitoi zile  pesa nitakuwa mjinga wa karne” Uasiri uliongezeka.

“Narudia nataka pesa zangu zote  ili niondoke”Aliongea Roma akianza kuwangalia polisi mmoja mmoja  na baada ya macho yake kutua kwa mkuu wa kituo  , aliona jambo na kumsogelea.

“Nataka pesa zangu” Aliongea Roma huku akiwa amemkaribia  mkuu wa kituo karibu kabisa.

“Sijachukua pesa mimi , siwezi kuiba , mimi ni mkuu wa kituo na nachukia wezi” Aliongea kwa kujiamini na muda huo huo Simu yake iliingia ujumbe mwingine na aliinua simu yake na  kuangalia ujumbe huo ulitoka kwa  jina la “Fundi cherehani’

“ WEWE MWANAUME VIPI MBONA HUTUMI HIO HELA , AU ULIKUWA UNAJIGAMBA BURE UMEPATA PESA NYINGI LEO , KAMA HUNA HELA USEME  UACHE KUNISUMBUA MIMI  KUNA WANAUME WENZIO WANAWEZA KUNIHUDUMIA , NITUMIE HIO HELA NIKANUNUE WIGI”

Baada ya mkuu huyu wa kituo kuona  meseji  hio alikunja ngumi na kusema liwalo na liwe pesa sitoi.

Roma baada  ya kuona mkuu wa kituo anakataa , alimsukuma na kisha alimpita na kuingia kwenye ofisi yake  , baada ya kuingia tu , alivuta mtoto wa Meza na kuibuka na mabuda mawili ya pesa na  kutoka.

“Mimi siibiwi kizembe ohoo..”Aliongea huku   mkuu wa kituo akimtukana moyoni na kuona  mkeka umechanika.

“Hawa ndio majambazi ambao unatakiwa kuwakamata kama unajali sana sheria , sio  raia wema kama sisi mrembo eh” Aliongea Roma wakati akiwa amemsogelea   Mage karibu kabisa na Mage hakuwa na la kuongea kwani wakati huo alionekana kuwa  kwenye mawazo  mengi sana kwa wakati  mmoja.

Roma baada ya kutoka alifanya mawasiliano na Nasr ana kumuuliza yuko wapi na  mwanadada huyo alimjibu bado yupo ofisni , Roma alishangaa  kwani muda ulikuwa umeenda sana , lakini alijua huenda mwanadada huyo kabanwa na majukumu mengi Zaidi.

Ndani ya masaa machache Roma alikuwa  ashafika ndani ya kampuni  ,  haikueleweka waliachana vipi na mrembo Nadia ila Roma alikuwa  ni aina flani ya wanaume ambao  hawakujali sana baadhi ya mambo na ilionekana anahistoria kubwa san ana  mwanadada huyo.

******

 MASAA MACHACHE NYUMA

Kitendo cha Roma kufanikisha kazi  ya kurudisha feza kutoka PANZ  Security kilimfurahisha sana Edna, na kwa mara ya kwanza alijihisi kweli ana mume.

“Nitampikia  chakula  leo ,ananidharau sana sijui kupika ananiona sistahili kuwa mke ”Aliwaza mrembo huyu wakati akiwa ndani ya ofisi yake

“Bosi Miss Nadia amefika?” ilikuwa ni sauti ya Monica akitoa taarifa kwa bosi wake.

“Okey mruhusu aingie”

“Wow! You are beutifull Edna as the rumors”

“Asante sana Nadia , na wewe pia umrembo”

Wawili hawa walikaribishana  na kuanza mazungumzo ya kibiashara.

“Nimekubali ombi la kuwa mwanasheria wa Kampuni yako”Edna alishangaa  maana  haikuwa kazi rahisi kumfanya mwanasheria mkubwa duniani kuwa  mwanasheria wa kampuni change kama Vexto maana Nadia alikuwa akifanya kazi na makampuni makubwa kama Sumsung

“Nashukuru sana  Nadia kwa kuchagua kufanya kazi na kampuni yangu na niseme tu nitahakikisha unafurahia kufanya kazi na sisi”.

Nadia alitabasamu  huku akihusudu urembo aliokuwa nao  Edna , alikiri kuwa hakuwa akiingia kwa urembo wa mwanadada huyo hata kidogo.

Basi wawili hawa walikutana kwa ajili ya kusaini mkataba wa Nadia kusimamia  kampuni ya Edna kisheria yaani VExto.

Wakati wakiagana mara simu ya CEO Edna iliita  na alipoangalia jina aliona ni ‘Mbakaji’ na bahati mbaya ni kwamba simu ilikuwa mezani hivyo  Nadia aliona jia hilo  na kujiuta akishangaa.

“Hello!”

“Bebi nimekamatwa tena na polisi”Ilikuwa ni sauti ya Roma na Edna alishangaa.

“Ilikuwaje “

“Nina kesi ya utakatishaji fedha , nimedharau sharia za nchi”Aliongea Roma na Edna hakuongea chochote .

“Bebi mbona huongei , usiniambie mapenzi siku hizi yamepungua   kiasi  cha kutaka mumeo nikae  jela”Edna alimwangalia  Nadia.

“Natuma mwanasheria  aje kukutoa” Baada ya kukata simu  Edna alivuta pumzi.

“Nitaenda mimi” Aliongea mwanadada Nadia. Nadna alishangaa

“Lakini..”

“Usiwe na wasiwasi , najua unachofikiria lakini  nitaenda mimi  iweke kama kazi yangu ya kwanza kwa kampuni”Baada ya kuongea maneno hayo Nadia alichukua mkoba wake na kushuka  hadi kwenye maegesho ya gari na kuingia .

“Evans nipe taarifa?” Aliongea mwanadada huyu  na kupewa taarifa na mtu anaefahamika kwa jina la Evans.

“Okey ! nikusanyie   ushahidi wote  na tukutane”

“Sawa madam” ilisikika sauti upande wa pili wa simu .

Baada ya smu hio kukatwa  mwanadada huyu alifatufa jina lingine  na kupiga .

“ Ndio boss nishasaini mkataba, anaonekana kufurahia sana kwa mimi kufanya kazi ndani ya kamupini”

“Hongera sana Nadia   ni mwanzo mzuri nadhani ni wakati sasa wa kuendelea mipango yetu” ilisikika sauti nyingine  kwenye simu , sauti nzito.

Previoua Next