Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Muda wa saa kumi na nusu Edna alifika nyumbani  huku mwanadada huyu  akionekana siku ya leo kuwa na furaha kuliko siku zote jambo ambalo Bi wema aliligundua , lakini hakuuliza  Zaidi , kwake  huyu mwanamke alitamani sana kumuona Edna akifurahi ndio iliokuwa ndoto yake kubwwa sana , alikuwa akiumizwa sana na tabia ya Edna muda wote kufanya kazi  kiasi kwamba kwake hakuwa na siku ya kupumzika , Edna hakuwa kama wafanya biashara wengine ambao walikuwa  wakipenda  kula bata kila ifikapo wikiendi , Edna yeye alikuwa ni aina flani ya wanawake ambao alikuwa akirudi nyumbani  ni kusomana kulala.

Ndani ya chumba cha Edna kulikuwa na mavitabu mengi sana na karibia vitabu  vyote hivyo alikuwa amevisoma  , kwa mtu wa  kawaida unaweza kushangazwa na swala hilo lakini kwa Edna  lilikuwa swala la kawaida  sana , ndio Maisha yake ambayo alikuwa amezoea , kwake kusoma vitabu ndio ilikuwa starehe yake kuliko kujichanganya na marafiki.

Edna alikuwa ni mtu wa kutabasamu mara chache sana , muda wote alikuwa  yupo siriasi   kiasi ambacho kilifanya hata wafanya kazi  wenzake wamuogope  kumsogelea, lakini leo hii mwanadada huyu anaonekana kutabasamu mbele  ya Bi Wema , mwanamama huyu aliekula chumvi nyingi alitamani kujua ni kipi kinamfanya  mwanae huyu wa kambo kutabasamu  , ila hautaka kuuliza.

“Bi Wema leo niachie jiko nitapika  mimi” aliongea Edna na kumfanya  Bi wema kutumbua macho  lakini Edna hakujali   sana , alikaa kwenye sofa huku mkononi akiwa ameshikilia kitabu   cha mapishi.

“Sawa Miss , lakini haujawahi kuingia jikoni utapika nini?”

“Bi Wema hio ni siri  , wewe utaona wakati wa kupakua”Bi Wema alijikuta akitabasamu na katika akili yake alikuwa ashajua kilichokuwa kikiendelea kwa Edna , aliamini kuna jambo ambalo lilikuwa limetokea  kazini na kusababisha mabadiliko hayo .

Saa moja kamili za jioni  Edna alikuwa bize na mapishi  huku Bi Wema akiendelea  kuangalia  tamthilia,  muda nao ulisonga lakini Roma bado hakuwa amerudi.

“Bi Wema Roma hajarudi bado?”Aliuliza mwanadada huyu aliekuwa amevalia Apron  na kumfanya apendeze sana , kiasi kwamba wewe ndio ungekuwa mume wa  Edna  na ungemuana jinsi alivyovalia Apron ni hakika ungenenepa kabla hata ya kula chakula.

“Hajarudi bado na hajatoa hata  taarifa kama atachelewa kurudi”Aliongea Bi Wema na  kumfanya Edna kuonyesha hali ya kuhuzunika.

“Ukute na hangaika hapa yupo  na mwanamke”Aliwaza Edna huku akirudi jikoni kuendelea  na upishi akitegemea Roma atarudi.

Muda wa saa tatu na nusu alionekana Bi Wema akiwa ndani ya chumba cha maliwato akitapika  huku akisukutua maji.

“Nimewahi kula chakula kibaya ila hiki cha  leo ni kiboko , Chakula kama mavi ya mtoto mchanga  khaa.. Edna ananitia aibu jamani”Aliongea   Bi Wema huku akisukutua .

“Nimekula kumridhisha tu ilia aone na yeye mwanamke , ila kile sio chakula”.

Wakati Bi Wema akiendelea kutapika huko ,Edna alikuwa amekaa kwenye sofa akimsubiria mwamba Roma arudi   huku Mabakuli ya chakula akiwa ameyapangilia kwenye Meza , na kwa jinsi yalivyopangwa  moja kwa moja utaamini kuwa kuna bonge la pishi limefunikwa.

Upande Nasra  alionekana akiwa nyumbani kwake jikoni akiwa bize na mapishi , alionekana kuwa mtaalamu kweli , kwani kwa namna ambavyo alikuwa  akikata kitunguuu Ungejiambia mwenyewe ndio hapa yupo mwanamke.

Bebi Nasra unajua sana kupika” Aliongea  Roma huku akiwa amejipumzisha na  pensi la kike  na haraka haraka ukimwangalia lazima ugundue  hilo  pensi ni  la Nasra  maana lilikuwa na Marinda Marinda chepete  , ila Roma hakuwa na habari  huyu bwana , yaani hakuwa na  aibu hata kidogo.

Baada ya kula na kushiba  , hakukuwa na kilichoendelea  zaidi ya kuingia kwenye mtanange .

“Bebi hii Staili inaitwaje?”Aliuliza Nasra huku akionekana kukosa pumzi maana alikuwa amelemewa na utamu.

“Mh! Mimi hata sijui  ila  umekaa kipopo popo ,, itakuwa ndio Popo kanyea Mbingu”Aliongea Roma huku  akiongeza spidi.

Muda wa  saa kumi na mbili za Asubuhi Roma aliingiza gari yake  nyumbani  bila wasiwasi kabisa na baada ya kuliegesha aliingia ndani na kumkuta Bi Wema.

Bi wema kama kawaida , alikuwa mzungu wa Roho maana alimpokea Roma na kuitikia salamu kama hakujatokea kitu ila kiukweli moyoni alikuwa na huzuniko , kwani  kwa mara ya kwanza  anamuona Edna akiingia jikoni jambo ambalo  kwake aliliona kama hatua ya kwanza ya Edna kuwa  kama mwanamke aliekamilika , lakini Roma hakuonekana nyumbani , aliona kitendo hicho kimemnyong`onyesha Edna juhudi zake , kwani Edna kwa mara ya kwanza alimsubiria Roma  kwa muda mrefu jambo ambalo sio kawaida.

“Roma jana ulikuwa wapi  , hukutoa taarifa Miss alipika na akakusubiri lakini hukutokea”Aliongea Bi wema wakati Roma akianza kupandisha ngazi kuelekea chumbani kwake , lakini baada ya kusikia maneno hayo alijikuta akisimama na kushangaa.

“Bi Wema unamaanisha Edna jana kaingia jikoni kupika?”

“Ndio chakula bado kipo mezani”Aliongea Bi Wema  na Roma hakuendela kwenda juu ,, alirudi chini na kwenda meza ya kulia chakula na kufunua mabakuli yaliopikwa.

“Bi Wema nitakula kama kiporo na chai”Aliongea Roma na kupanda ngazi kuelekea chumbani kwake  na baada ya muda alishuka kwa aili ya Chai na Edna alikuwa amejaa  mezani akinywa chai oamoja na Bi Wema.

“Wife hebu tuone leo ulichopika”Aliongea Roma na kisha alifunua mabakuli hayo  huku Edna licha ya kwamba hakuwa akimwangalia Roma usoni lakini akili yake ilikuwa ni  kusbiria nini ataongea Roma baada ya kula chakula chake.

Roma alipakuwa  chakula  na kisha alichota mtori  hhuo na kupeleka kinywani  na kula.

“Nilijua mtori kumbe ni tambi Looh! Hapa  nina jipu sio mke”Roma aliwaza moyomi  na kisha  akachota  kijiko kingine  na kula  , wakati huo Bi Wema alikuwa amekunja sura utadhani chakula kilikuwa kikiingia Tumboni  kwake.

Roma alimwangalia Edna    huku mrembo huyu akijifanyisha kunywa chai , lakini  alikuwa akisubiri Roma atamke neno.

“Wife umejitahidi sana leo, ukiendelea hivi utakuwa mpishi mzuri”Aliongea Roma na kuendelea kula bila ya wasiwasi huku nia yake ni kutokumkatisha tamaa Edna na  Bi wema alifurahishwa na maneno ya Roma na kule kukasirika kwa kutokurudi nyumbani kulipotea , lakini bado kuna kitu kilimshangaza , kwa jinsi chakula hiko kilivyokuwa na chumvi , alijiuliza  Roma amewezaje kula.

“Okey ! ngoja  nijipe adhabu  ya kumaliza  hiki chakula maana sio kwa huu utopolo”Aliwaza Roma , ila kwa Edna moyo wake ulitabasamu , licha ya kwamba hakuwa akionyesha usoni lakini alifurahia sifa hizo kutoka kwa Roma.

Roma baada ya  kumaliza kunywa chai  ya asubuhi  alipandisha chumbani kwake  kwa ajili ya kupumzika , siku hii ya leo aliona akae kidogo nyumbani , kwani tokea afike ndani ya familia  hii hakuwahi kukaa nyumbani kwa muda mrefu , muda mwingi  alikuwa  misele ya hapa na pale.

Wakati akiwa amejilaza kwenye kitanda  alijikuta akiachia tabasamu .

“Edna  mambo yake ni kama ya Seventeen  nakiri kwa asilimia kubwa wanafanana”Aliwaza Roma huku akiwa ni mwenye tabasamu.

****

1998- KIGALI RWANDA  March 8

Ilikuwa ni ndani ya  ofisi ya mheshimiwa Jeremy Paul (JP),walionekana watu wanne wakiwa  wameketi ndani ya ofisi hii   na ilionekana kuna kikao  kilichokuwa kikiendelea kati ya mheshimiwa Jeremy na   wanaume  watatu kukamilisha idadi  ya wanaume wane ndani ya ofisi hii.

Wanaiume  watatu walikuwa ni watu maarufu sana waliokuwa wakifahamika ndani ya jiji la Kigali  na moja ya sifa kubwa ambayo ilikuwa ikiwafanya watu hawa kufahamika ni kutokana na michango yao katika taifa hili dogo.

Mtu wa kwanza aliekuwa amekaa upande wa kushoto wa mheshimiwa Jrtrmy alifahamika kwa jina la  Uwimana ,huyu alikuwa ni mfanya biashara mkubwa sana ndani ya taifa hili la Rwanda na alikuwa akimiliki  visima vingi vya Mafuta , pamoja na kampuni kubwa ya usafirishaji , Mwingine alikuwa ni Jean , Wengi ndani ya taifa hili wanapenda kumuita kwa jina la Profesa J , huyu nae licha ya kuwa mfanya biashara lakini pia alikuwa  ni  mkuu wa chuo kikuu cha  Rwanda,Mtu wa tatu  hakuwa akifahamika sana ndani ya taifa la Rwanda  kama alivyokuwa akifahamika ndani ya taifa la  Tanzania ,Alikuwa akifahamika kwa ina la Aziz Mohamed huyu alikuwa ni moja ya wafanya biashara wakubwa sana kutoka taifa la Tanzania , lakini pia alikuwa ni moja ya wawekezaji wakubwa ndani ya taifa la Rwanda na ndio maana mchango wake ulikuwa ukiheshimika ndani ya taifa hili.

“Ndoto yangu yangu kubwa ni kuona Rwanda  ikiwa nchi kubwa sana kiuchumi ndani ya  bara la Afrika ,  na haya yote hayawezi kufanikiwa bila ya  uwepo wenu”Aliongea. Huku mabwana hawa  wakionekana kutingisha vichwa kuashiria kuwa wako pamoja na mheshimiwa na muheshimiwa.

“Mheshimiwa  sisi tupo tayari kukuunga mkono katika safari ya ndoto yako ya kuifanya Rwanda kuwa kubwa na tutakuwa ni wenye kushirikiana  kwa pamoja ili kuhakikisha kuinua uchumi wa taifa hili”Alingea Uwimana

Kikao hiki kilionesha dhahiri kilikuwa ni cha mipango juu  ya  kuifanya Rwanda kuwa nchi kubwa kwa miaka ishirini ijayo, mipango ambayo mheshimiwa Jeremy  aliona watu pekee wakufanikisha nao swala hilo ni  hao  mabwana watatu , haikueleweka ni kwanii Mheshimiwa akamwinginza mtu mwingine kutoka taifa la nje yaani Azizi Mohamed.

Baada ya kikao hiki kuisha Mheshimiwa huyu alionekana  kuwa na maongezi binafsi na Aziz kwani wale mabwana wengine walikuwa washatoka ndani ya ofisi hii.

“Asante sana Aziz kwa kufanikisha  kurudisha sehemu ya damu yangu mikononi mwangu”.

“Jeremy sisi ni  marafiki wa muda mrefu  sana hupaswi kunishukuru  , lakini nisingependa kuona katika Maisha yako unakosa furaha , umemkosa Rahel , lakini naamini    zawadi aliokupatia ni kubwa na angalau itakufanya usiishi kwa  kujuitia”Aliongea Azizi huku akimtaja Rahel na Jeremy alionekana kukosa furaha mara baada ya kusikia jina la Rahel.

“Ni kweli  Aziz.. lakini Maisha yangu  bado naona kama hayajakamilika kwa kumkosa Rahel , katika Maisha yangu niliamini  kwa kuwa raisi hakuna kitu ambacho ninaweza kukosa  na kunifanya nisiwe na furaha , lakini  Rahel amenifanya  nione sikuwa nikifikiria kwa usahihi”.

“Ni kweli  Jeremy, lakini kwa sasa unatakiwa kumsahau Rahel , yule mwanamke ni mke wa mtu kwa sasa na ni maamuzi ambayo aliyafanye yeye mwenyewe  na akakuacha  wewe , angalau sasa wekeza nguvu zako katika kulea kichanga alichokuachia kama zawadi”Aliongea Aziz  lakini muda huo huo  aliingia   mwanadada makamu hivi, hakuwa mrembo sana , ila alionekana  kuwa mtanashati

“Mheshimiwa kuna  taarifa mbaya?”

“Unamaanisha nini Linda , unamaanisha nini kuhusu taarifa mbaya?”

Mwanadada huyu aliefamika kwa jina la Linda alisogelea Rimoti ya Tv na kisha akawasha  Runinga  na kuweka chaneli ya BBC  .

BREAKING NEWS: NDEGE YA MALAYSIA  AIRLINE  ILIOKUWA IKISAFIRI KUTOKA  KUAL LAMPUR  KUELEKEA BEIJING CHINA YAPOTEZA MAWASILIANO.

Taarifa hii ilionekana kumshitua sana mheshimiwa  pamoja na  Aziz waliouwa wakiangalia Runinga hio lakini kati ya watu hao aliekuwa kwenye hali mbaya Zaidi ni Jeremy.

“Linda wasiliana na shirika la ndege la Malaysia  wakupe  orodha ya  majina ya  watu waliopanda kwenye hii ndege”Aliongea Mheshimiwa Jeremy huku akiwa ni mwenye wasiwasi mwingi sana.

“Jeremy  punguza  presha naamini huenda kuna tatizo la kawaida tu ambalo limetokea”

“Aziz  siwezi kutulia kabisa ,unafikiri  nitaishije kama kitu kibaya kikimkuta Lorraine ,Nitamwabia nini Rahel , hapana nitaishi kwa majuto makuU kwenye Maisha yangu yote , naomba jambo baya  lisitokee”Aliongea Mheshimiwa Jeremy  huku akishikilia kifua chake.

Ni ndani ya dakika tano Linda alirudi   na kuingia ndani ya ofisi  , huku  wasiwasi ukiwa umejaa kwenye macho yake.

“Mheshimiwa hii ndio orodha ya abiria”Aliongea lakini Azizi aliona wasiwasi uliokuwa  kwenye macho ya  Linda na kwakuwa alikuwa karibu nae alichukua ile karatasi na kuangalia  majina hayo na bwana huyu alijikuta akitumbua macho na kumwangalia Rafiki yake Jeremy.

“Azizi usiniambie Lorraine ni  sehemu ya abiria walikuwepo kwenye hio ndege?”

“Jeremy   taarifa inasema ndege imepoteza mawasiliano , lakini sio kuanguka  tusubirie taarifa kamili , Acha kufikiria mambo mabaya”Aliongea Azizi  lakini baada ya kumaliza sentensi yake…

“Mheshimiwa..!!”Aliongea linda kwa  sauti mara baada ya Mheshimiwa Jeremy kudondoka na kuzimia.

Previoua Next