Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

TANZANIA 2013 -JULY

Ilikuwa ni mwezi July ndani ya  jiji la Dar  pilika pilika zilikuwa za hali ya juu ndani ya jiji hili , si kwa wanausalama ,sio kwa majeshi  , sio kwa wananchi  , kwa mara ya kwanza jiji la Dar linaonekana kuwa safi kuliko siku zote.lakini  haikuwa kwa swala la usafi tu , lakini pia  ulinzi ulikuwa umeimarishwa kila kona ya jiji hili, huku makachero wa kizungu pia wakionekana kulandalanda  huku na huko kuhakikisha hali ya usalama.

Naam hii yote nikutokana na ujio wa Raisi wa taifa kubwa duniani , taifa lenye ushawishi  kila kona ya dunia ,  taifa ambalo  lina uchumi mkuwa duniani , taifa ambalo linaongoza kwa teknolojia kubwa duniani,Raisi ambaye kwa mara ya kwanza anazuru ndani ya taifa la Tanzania na kufanya dunia isimame na kushangaa  tukio hili la kipekee kabisa kutokea ndani ya taifa hili.

Ni baada ya masaa kadhaa ya ndege kubwa  ya Raisi kutua ndani ya uwanja wa kimataifa wa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na mheshimiwa Raisi Kigombola raisi wa Tanzania akiongozana na viongozi wakubwa wa Tanzania walionekana kuwa katika hali ya furaha maa baada ya kumpokea raisi Barrack Mabo.

Mheshimiwa Raisi Kigombola alijisikia fahari sana , na katika Maisha yake ya uongozi alijihisi ni jambo kubwa sana ambalo amelitimiza  , kwa kumtoa raisi wa dunia  ambaye alikuwa na majukumu mengi duniani na kuja kutembelea taifa dogo  la Tanzania.

“Ndoto zangu zimetimia nina uhakika maadui zangu ndani ya  taifa hili wataelewa uwenzo na nguvu niliokuwa nao.,kumleta raisi wa Dunia Tanzania sio  jambo dogo”Aliwaza mheshimiwa huyu wakati wimbo wa Taifa ukiendelea , licha ya kwamba mzee huyu alikuwa akiimba wimbo huu lakini akili yake iilikuwa ikiwaza maadui zake na mipango yake.

“Tanzania itakuwa yangu milele na milele ,m nitaacha mizizi ambayo hakuna kiumbe yoyote ambaye ataweza  kuingoa”Aliendelea kuwaza.

Baada ya shamra shamra za aina yake  hatimae safari ya kuelekea ikulu ilianza huku asilimia tisini ya ulinzi wa raisi  huyu ulikuwa ukiratibiwa na  vikosi vyake ambavyo vilikwisha kutangulia  nchini kuhakikisha hali ya usalama.

“Karibu sana Rafiki yangu ndani ya Tanzania”Aliongea mheshimiwa  Kigombola .

“Asante sana  Kigombola  , nimefurahi na mapokezi ya watanzania”aliongea na kumfanya  mheshimiwa  Kigombola  aendelee kujiona yeye ndio yeye  na ndio Raisi wa Tanzania ambaye  ana akili nyingi kuliko raisi yoyote  yule.

Baada ya chakula   mheshimiwa Bamo alipewa ofisi yake kwa ajili ya kuendelea na majukumu ya kazi , kwani  bwana huyu hakuwa ni mwenye kupumzika kabisa ,  muda wote alikuwa macho akifanya kazi , alikuwa ni raisi wa Taifa la Marekani , lakini alikuwa akitoa maamuzi  na maelekezo yanayoenda   kutekelezwa na maraisi wa mataifa mengine   na hii yote inaifanya kazi yake kuwa ngumu sana  na kumfanya kuwa bize.

Wakati akiendelea na kazi ndani ya ikulu ya Tanzania  aliingia bwana mmoja  alievalia mavazi ya kikachero  yenye nembo ya taifa la Marekani, bwana huyu alionekana kuwa kijana mdogo , lakini alikuwa na nafasi kubwa  katika kikosi cha ulinzi cha mheshimiwa huyu.

“Nipe Ripoti Chriss?”Aliongea mheshimiwa huyu na kisha akampatia mheshiwa Bahasha aliokuwa  ameishikilia mkononi na Raisi huyu aliifungua na kuangalia kilichomo ndani  , na alikuta ni picha,  alizitoa na kuanza kuziangalia na bwana huyu macho yalimtoka.

“Wanafanana kwa asiliamia kubwa na Agent no 17, Umefuatilia  ni nani baba wa mtoto huyu?”

 “Mheshimiwa tumekusanya  ripoti kadri tulivyoweza , huyo mwanadada anaitwa Edna ni mtoto wa Rahel  na Adebayo wanafamilia wanaomiliki kampuni  changa ya VEXTO”.

“Lakiini imekuwaje huyu Edna akafanana kwa asilimia mia moja na Agent 17?”.

“Hilo ndio swali lililofanya  tuendelee kufatilia kwa  ukaribu  kama kuna muunganiko wowte kati ya 17 na  Edna na katika uchunguzi tuliofanya tulibaini watu waliohusika kumfanyia matibabu Rahel kipindi cha ujauzito wake , wote walifariki  vifo visivyoleweka lakini swala hilo halikuweza kutukwamisha kupata taarifa  na kutokana  na uwepovyanzo vingi vya taarifa tulivyovipandikiza hapa nchini tumegundua Agent 17 na Edna walizaliwa mapacha wa kufanana”.

“Nini, unahakika na hio taarifa Chriss”

“Ndio mheshimiwa”.

“Sawa Chriss , kazi nzuri kaendelee na majukumu yako mengine , ila hili swala kwa sasa  nitampatia mtu mwingine ashughulike nalo , kwasasa hatupaswi kufanya jambo lolote lile”Aliongea Mheshimiwa naChriss alitoka ndani ya ofisi.

Baada ya Chriss kutoka  mheshimiwa alirudia kuangalia zile picha mezani kwake   kwa umakini  mkubwa huku akionekana kuwaza sana.

“Hapana  kwa namna yoyote ile siwezi kuruhusu  tundu lolote ambalo litafanya Operation LADO  kufichuka, Uwepo wa Edna duniani utamfanya Agent 13 na 17  kutaka kufahamu ukweli uliotokea katika Maisha yao ya nyuma kama watabahatika kumuona Edna na suluhisho la haya yote ni Edna kufa”Aliwaza mheshimiwa huyu huku akiangalia picha hizo.

Baada ya lisaa kukaa kwenye ofisi yake hatimae mheshimiwa Kigombola aliingia ndani ya ofisi hio na kukaa kwa ajili ya mazungumzo na mheshimiwa , swala la kwanza ni juu ya mipango yao , ambayo imemfanya bwana huyu mwenye madaraka makubwa duniani  kufika ndani ya taifa , lakini pia swala la pili ni  jambo binafsi alilokuwa akitaka kuomba msaada  kwa Kigombola .

“Kigombola , kuna jambo  la ziada unapaswa  kunisadia”Alianzisha maongezi.

“Jambo gani hilo mheshimiwa wewe ni Rafiki yangu na nipo tayari kukusaidia jambo lolote hata kama unataka kasehemu ndani ya hii nchi naweza kukupatia”.Alitabasamu na kisha akatoa picha na kumpa Kigombola.

“She need to die  and you as my friend  utanisaidia katika hili”Aliongea Bamo na kumfanya Raisi wa watanzania ashangae nini tatizo.

“Mheshimiwa kuna haja gani ya mtoto kama huyu kufa?”.

“Kigombola  fanya kama ninavyokuambia  huyu msichana lazima  afe  la sivyo  mafanikio yangu ambayo nimeyajenga kwa miaka na miaka yanaweza kuwa hatarini na uwepo wa huyu msichana”Aliongea  na kumfanya Kigombola kumwangalia mheshimiwa  mwenzake na kutingisha kichwa kwamba jambo hilo atalifanyia kazi.

Wakati hayo yakiendelea upande wa pili nchini Rwanda Jeremy anapokea taarifa kutoka kwa shushu wake ikulu  iliokuwa kwa mfumo wa ujumbe wa sauti.

“Edna yupo hatarini kubaki nchini Tanzania”

“Nilitegemea swala hilo , ngoja niwasiliane na upande wa  pili wa mpango wetu”Alijibu  na simu ilikatwa.

“Fu**ck you Amerika , I must pay for what you Did , nitachimba na kuujua ukweli wote”Aliongea kwa hasira Jeremy.

****

Edna   kama kawaida yake alikuwa amekaa chumba chake cha kujisomea akiwa anafanya baadhi ya kazi  za hapa na pale  kama ilivyokuwa  kawaida ya mwanadada huyu kutokupumzika , lakini ufanyaji kazi wake wa leo mwanadada huyu haukuwa kama wa siku zote , alikuwa ni mwenye kuwaza mambo kadha wa kadha lakini kubwa lililokuw andani ya kichwa chake ni juu ya Roma.

Aliinua simu yake na kisha  kuangalia picha zilizotumwa na Suzzane zikimuonesha   Roma akiwa na Doris  siku kadhaa nyuma  wakionekana wameshikana viuno , lakini pia picha ya pili ilikuwa ikimuonesha Roma akitoka ndani ya  nyumba ya Rose , lakini picha nyingine ikimuonesha  Roma akiwa amekumbatiwa  na mwanadada ambaye sura yake haikuonekana , lakini pia picha nyingine Roma akibusiana na Nasra kwenye gari  , lakini pia picha nyingine Roma  akiingia ndani ya chumba cha hoteli na  Neema luwazo , Picha zote hizi  zilitumwa na mwanadada Suzzane mlinzi wa siri wa Edna.

“Suzzane anafanya mambo ambayo sijamwagiza , haikuwa na haja ya kumfatilia Roma  , ni mume wangu ndio lakini sio kwa mapenzi ila kwa  mkataba na ukiisha tunaachana , sitaki kuyaingilia sana Maisha yake” Aliwaza

Licha ya kuona picha hizo lakini kwa Edna hakuonyesha kukasirika alichukulia kawaida tu  lakini alionekana kuna kitu hakipo  sawa , aliona licha ya Roma kuwa mume wake kisheria ,, lakini hakuwa akiishi kama mume wake ,vitendo ambavyo aliona Roma anafanya vitamletea shida kama watu  watagundua kuwa  Roma ana mahawala wengi

Wakati akiendelea kufikiria mala mlango wake  uligongwa  na  alinyanyuka na kwenda kuufungua  na uso kwa uso na   Roma.

“Honey  Darling  Chakula tayari , twende tukale”Aliongea Roma huku akiwa ametabasamu  na Edna alimwangalia  Roma na hakummaliza.

“Sijisikii kula” Aliongea na kisha akafunga mlango kwa hasira , ila Roma hakuondoka  alisimama na kugonga tena na awamu hii mlango ukafunguliwa tena na mwanadaa huyu huku akionekana ni mwenye kuwa na hasira.

“Hivi Roma nini , si  nimekuambia sijisikii kula , unaweza kwenda kuendelea”

“Namimi siwezi kula peke yangu, na nitaendelea kugonga mlango  mpaka ushuke tukale” Edna alimwangalia Roma na kwa alivyokuwa ana muona Roma aliamini bwana huyu  alichokiongea alikuwa anaaanisha.

“Kale na Bi Wema , kama huwezi kula peke yako”

“Bi wema kasema hajisikii vizuri atakula baadae,Mke wangu mbona  huna heshima kwa  mumeo twende basi”

“Yaani Roma  wewe sijui ni mwanaume wa aina gani huelewi”Aliongea Edna huku akitoka na kufunga mlango na kuelekea chini akitangulia  huku Roma akimwangalia kwa nyuma na kuishia kutabasamu.

Bi Wema aliekuwa akiingia kutoka nje  alijikuta akitabasamu na moyo wake kuwa wa moto mara baada ya kuona Roma na Edna wakiwa  kwenye meza wakila chakula  , ilikuwa ni picha ambayo ilimvutia sana, kwake na alitamani iwe kila siku kuona wanandoa hao wanafanya mambo kwa pamoja , hakupenda namna Maisha ambayo Edna alikuwa akiyaishi , alikuwa akiamini mwanamke  hawezi kukamilika pasipo ya kuwa na mume na pia Mume hawezi kukamilika  pasipo ya kuwa na Mke.

“Roma ..!!!”Aliita Edna na  Roma alimwangalia  Edna.

“Ndio mke wangu”

“Kwanini haupo kama wanaume wengine”.

“Unamaanisha nini mke wangu , usiniambie ushaanza kunifananisha na wanauame wengine?”

“Sio kukufananisha na wanaume wengine  , lakini wewe upo tofauti kabisa , haupo siriasi na Maisha  , kazi umepata  lakini unaishai kucheza gemu  na kufanya uzinzi”Aliongea Edna  huku akionesha yupo siriasi ila Roma hakujali  kwanza alitabasamu.

“Mke wangu  nitakuwaje siriasi na pesa zote hizo ulizonazo , nani wakuzitumbua, wote tukiwa na pesa hainogi bebi , mmoja akiwa tajiri mwingine asiwe na pesa ili kuwe na  mtu wa kutumbua pesa na kula bata ,Bebi Edna tuseme wewe umeolewa na mimi na ukanikuta na mipesa kama hii yako, kwanini uanze kujihangaisha na Maisha badala ya kula  bata”

“Kwa hio  wewe kazi yako ni kutumbua pesa zangu ?”

“Halafu   mke wangu  sio pesa zako ni za kwetu , ushasahau sisi ni  mwili mmoja”Edna alimwangalia Roma kwa hasira kali mno  , alishindwa kuelewa Roma ni mtu wa aina gani yeye yupo siriasi kumwambia mambo ya maana lakini anaanza kuongea ujinga juu ya maswala ya kutumbua hela.

“Kama unawaza kutumbua pesa zangu sahau , usipo tafuta zako  hutipata chochote kutoka kwangu”

“Mke wangu kama hutaki  nikitumia pesa zako nani atazitumia ...Halafu mke wangu mbona kama  unampango wako kichwani wa sisi kutafuta mtoto  halafu huniambii nijiandae”Edna alimwangalia Roma huku akishangazwa na uroppokaji wake , ‘Neno mtoto ‘ ni swala ambalo hakuwahi kulifikiria hapo kabla .

“Nani mimi … Mtoto ,, hata kama  nitake mtoto siwezi kuzaa na mwanaume asiye siriasi na maisha  Watoto wataiga nini”.

“Bebi kama hutaki kuzaa na mimi mumeo unataka uzae nje ya ndoa ?”Edna baada ya kuona topic ambayo hakuwa akiipenda  Roma kaikomalia , alinyanyuka na kupandisha Ngazi  kuelekea chumbani kwake huku Roma akiwa ni mwenye kutabasamu.

“Huyu  mwanaume  muda wote anafikiria ujinga tu , nifanye nini ili angalau kumbadilisha ili  hata niwe na kujiamini nikimtambulisha mbele za watu”Aliwaza Edna  huku akiwa amesimama kwenye dirisha  chumbani kwake.

Ukweli ni kwamba kuna muda Edna alitamani kumuona Roma abadilishe  mfumo wake wa kimaisha ,  alitamani awe kama wanaume wengine ambao wako bize na kutafuta Maisha na kuongoza biashara  hatimae aweze kujivunia kuwa na  mume mwenye mafanikio , lakini  haikuwa hivyo , Roma alikuwa Roma kama alivyomtoa kule kwenye kazi yake ya ubeba mizigo  , hakuwa amebadilika hata kidogo ,tabia yake ilikuwa vilevile

Edna wakati akiendelea kufikiria akiwa anaangalia eno la Nje alimuona mwamba Roma akaitoka tena awamu hii akiwa amepigilia miwani ya  jua kabisa  na haikueleweka katioa wapi , alimwangalia namna ambavyo anaingia kwenye gari yake na kuwasha na mpaka lilipotokomea nje ya geti.

“Lazima anaenda kutafuta mwanamke  pale”Aliwaza Edna huku akirudi kitandani  na kukaa.

Previoua Next