Roma hakuwa ni mwenye kujali sana kuhusu maneno ya Edna kwani muda huo alichokuwa anawaza ni kiwanja gani anaweza kwenda kula bata , na angalau kujipatia kitumbua ambacho kinaweza kumtuliza kwa siku hio ya Wikiend.
Wakati akiwa anaingia kwenye Daraja la Kigambomi kuna gari aliitilia mashaka kwani hisia zake zilimwambia kabisa gari hio ilikuwa ikimfatilia , lakini licha ya kuwa na hisia hizo alitamani kulithibitisha hilo na ndio maanba alianza kuchukua chocho ambazo zilikuja kumfikisha mtaa wa Chang`ombe , lakini Gari ile bado ilikuwa nyuma yake.
“Kuna wapuuzi wananifatilia”Aliwaza Roma huku akiendelea kukumbuka kuwa gari ile ilikuwa karibu na nyumba anayoishi na kwa namna yoyote ile ni kwamba watu hao wanataarifa la eneo ambalo anaishi nah ii aliona ni hatari kwa yeye na kwa familia yake yaani Bi Wema na Edna.
“Ngoja kwanza niwapoteze “Aliwaza huku akiongeza spidi ya gari na muda huu magari yalikuwa mengi barabarani kwani ilikuwa ni muda wa jioni jioni hivi watu wakirejea majumbani , lakini licha ya magari hayo mengi haikumsumbua Roma kuendesha gari kwa spidi na kuanza kupita kila apatapo nafasi na alitumia dakika chache tu gari iliokuwa inamfatilia alikuwa ameipoteza , lakini sasa alijishgaa kuona ameendesha gari umbali mrefu mpaka kufika Kawe.
“Bora niende zangu Beach”Aliwaza Roma na kuendesha gari kuelekea upande ilipo kuwepo Ufukwe wa Kawe.
Wakati anaingiza gari yake eneo maalumu la kuegeshea magari wapo watu wengi waliokuwa wakimkodolea macho kutokana na uzuri wa gari yake.
“Bosi kuna boti zipo hapa kama utahitaji”Aliongea kijana flani mara baada ya kumuona Roma akitoka kwenye gari, kijana huyo alionekana kuvaa tisheti flani hivi ya kampuni iliokuwa imeanzishwa hivi karibuni ndani ya jiji la Dar es salaam ambayo ilikuwa ikikodisha SpeedBoat , boti flani hivi zipo kama pikipiki.
Roma alijikuta akitamani kweli kuendesha boti na aliongozana na kijana yule mpaka upande ambao Boti hizi hukodishwa.
Baada ya kufanya malipo ya awali , alionyeshwa upande ambao boti hizo zilikuwa zimeegeshwa na Roma alisogea upande huo na kuchagua boti ambayo ilimvutia na alionekana alikuwa akijua kweli boti hizo.
Baada ya kuridhika na chaguo lake alirudi na kubadilisha nguo na kupewa mavazi ya ziada kwani hakuwa na mpango wa kuja ufukweni hivyo hakuwa na nguo za fukwe.
Siku hii ndani ya eneo la fukwe kulikuwa kumechangamka mno kiasi kwamba kulikuwa kumependeza , kuna waliokuwa wachumba wakiwa ndani ya hili eneo , kuna waliokuwa ndani ya fukwe hii kama wanafamilia na pia kuna waliokuwa wapo ndani ya fukwe hii wakiwa peke yao kubarizi.
Roma hakujali sana juu ya watu hao, ila kwake muda huo ni kufurahia maji ya baharini kwa kutumia speedboat.
Upande mwingine kwenye maegesho ya magari , iliingia gari aina ya Nissani nyeusi na kupaki pembeni ya gari ya Roma na wakashuka mwanamke mmoja wa kizungu pamoja na mwanaume wa kizungu , wote wakiwa wamevalia Track suit pamoa na tisheti , baada ya kushuka waliangalia gari ya Roma na kisha wakatingishiana vichwa kama ishara na kisha walisogea upande wa fukwe.
Baada ya kufika kwenye fukwe walianza kuangaza macho yao kulia na kushoto kama watu waliokuwa wakitafuta jambo Fulani na ndani ya dakika kama mbili hivi walijikuta wakipeana ishara mara baada ya kuona boti iliokuwa kwenye spidi ikipotelea katikati ya maji.
Ni kitendo cha haraka sana mzungu yule wa kike alirudi kwenye gari na kutoa begi flani dogo na kisha kutoka na kuungana na mzungu wa kiume na kuelekea kwenye kampuni ambayo ilikuwa ikikodisha Speedboat na kulipia moja na dakika chache tu walionekana wakiwa kwenye boti ile huku wakiitoa kwa spidi kiasi kwamba watu walianza kushangaa kwa umahili wao. Na kwa jinsi walivyokuwa wanaonekana kama ungewaangalia ungesema watu hao watakuwa ni wapenzi kwa namna yoyote ile ,kwani walikuwa wamependezana.
Roma alikuwa akiendesha mdogo mdogo huku akiwa ni mwenye kufurahia upepo uliokuwa ukimpepea machon kiasi cha kumpelekea kufumba macho.
“Hey! Bro , ilisikika sauti iliomwita Roma akiwa katikati ya maji kiasi cha kufumbua macho , kwani muda wote alikuwa ameyafunga akifurahia upepo, Na Romaa baada ya kugeuza macho yake alimuona msichana mrembo akiwa kwenye boat kama yake , alikuwa ni mrembo haswa kiasi kwamba Roma pepo la ngono liliibuka hapo hapo
Kimakadirio mwanamke aliekuwa mbele yake alikuwa mdogo sana kiumri kati ya miaka ishirini hivi kushuka na Roma alimkadiria mwanadada huyo kama mwanafunzi wa chuo kama tu atakuwa anasoma.
“Mambo mrembo?”
“Poa! Tunaweza kushindana?”
“Kushindana kufanya nini?”
“Kuendesha”Hapo Roma alimuelewa na kisha akatabasamu.
“Hautoweza kunishinda wewe”
“Hata mimi hautoweza kunishinda”Aliongea Mrembo na wote hawa wawili licha ya kwamba walikuwa wamekaribiana na boti zao ,lakini walikuwa wakuiongea kwa sauiti kubwa ili kusikilizana kwani upepo ulikuwa mkali kiasi kwamba sauti ilikuwa ikipotea.
“Sawa lakini lazima kuwe na zawadi kwa mshindi , ukiweza kunishinda nakupatia gari yangu niliokuja nayo”Aliongea Roma.
“Gari aina gani umekuja nayo ambayo unaamini ninaweza kuikubali kama sehemu ya zawadi kwa mshindi?”
“Aud Q8”Aliongea roma na kumfanya mwanadada huyu atabasamu kwani gari hio alikuwa akiijua vyema ugharama wake katika soko la magari duniani , ni gari ambayo sio chini ya milioni 200.
“Mimi ukiweza kunishinda nakupa mwili wangu leo?”Aliongea yule mwanadada kwa kujiamini na kumfanya Roma acheke.
“Hehe.. unaonekana unajiamini sana mremb?,o kumbuka kutimiza ahadi ”
“Ndio hakuna ambaye ashawahi kunishinda kwenye mbio za baharini , nina medali nyingi nilizopata chuoni”
“Chuo gani unasomea?”
“Yale university”Aliongea manadada huyu na kumfanya Roma atabasamu .
“Okey ! deal ule wako uende kinyume na ahadi yako”
“Siwezi kwenda kinyume na ahadi yangu ni moja ya sharia nilizojiwekea”
“Karembo sana haka nitahakikisha nashinda nikakavue nguo nione kamebeba nini?”Aliwaza Roma huku wakijiandaa kuanza mtanange na kuamua mstari wa ushindi , mwanadada huyu mrembo ambaye jina bado hatumjua alionekana kujiamini mno.
“Ukute anafurahi mwenyewe atanishinda Looh! yaani nikuvulie nguo mimi”Aliwaza mrembo huyu na muda huo huo wakaanza kuendesha kwa spidi huku membo huyu akionekana kuwa imara kweli , kwani ni ndani ya dakika moja tu alikuwa amemuacha mbali kidogo Roma , lakini kwa Rroma hakuwa na wasiwasi hata kidogo ,alikuwa akiendesha kama hataki vile.
Mwanadada aliekuwa mbele , alionekana kumdharau Roma na kuona hakuwa saizi yake , lakini ghafla wakati akiendelea na mawazo hayo , alipitwa na Roma kwa spidi ambayo haikuwa ya kawaida na kumfanya mrembo huyu ashangae na kuanza kuongeza Spidi, kwani Roma alikuwa ashamuacha hatua kadhaa mbele.
“Shi**t Atanishinda huyu”Aliongea huku akiichochea boti yake na ikaanza kusererka kiasi kwamba kulionekana povu la maji ya baharini likiwa limejitengeneza kwa nyuma.
Mchezo huu walikuwa wamewekeana umbali ambao walitakiwa kufika , kwa mbele kabisa kulionekana kukiwa na mnara ambao ndio mwanadada huyu alipendekeza , japo ilikuwa katikati ya bahari kwenye maji mengi ila hawakuongopa , lakini sasa , kadri alivyokuwa akijitahidi kuendesha hakuwa akimfikia Roma na hapa akili yake ilianza kupata moto na kujiuliza huyu mtu ni wa namna gani kwani katika Maisha yake yote hajawahi kushindwa kwenye mchezo huo na anazo medali.
Mwanadada huyu mrembo alianza kujutia maamuzi ya kuuweka mwili wake Rehani aliona kabisa dalili za kuliwa zinaenda kutimia.
Roma na yeye hakuwa na utani kabisa mbele ya kitumbua , alihakikisha anashinda na hilo alilikuwa akikaribia kulifanikisha kwani alikuwa akikaribia eneo ambalo ndio mstari wa ushindi.
Mrembo huyu alijikuta macho yakimtoka mara baada ya kumuona mwamba Roma akipita mnara kwa spidi na kuwa mshindi.
“Shi**t nishaliwa leo”Aliongea huku akipunguza mwendo lakini ghafla alimuona Roma akipiga kona ya hatari sana kuzunguka mnara ule na kuja upande ambao yupo kwa spidi ya hali ya juu sana kiasi kwamba mwanadada huyu alianza kujawa na hofu na kujiuliza ni kitu gani mwanaume huyu asiemjua anafanya , lakini alikuja kujua baada ya dakika chache , kwani ile Roma anamfikia yule mrembo aliisukuma bot ya yule mrembo kwa kutumia boat yake kwa nguvu na kuacha uwazi na hapo hapo ikapita Boat nyinngine sehemu ambayo boti ya mrembo yule alikuwa ameisimamisha na ikawa ponea ya mrembo huyu.
“Pumbavu wana siraha”Aliongea Roma baada ya kuona mwanadada wa kizungu kutoa bundiki yake kubwa na kumlenga , yule mrembo mwanzoni hakuwa akielewa kinachoendelea ila alipoangalia kwa umakini aliona bunduki na kuanza kupatwa na hofu na kujiambia leo anakufa katikati ya bahari , na eneo walilokuwepo ni kama vile watu hawa walikuwa wakiwasubiria waende mbali ili kuanza kuwashambulia wakina Roma kwani ilikuw ani mbali na fukwe.
Roma aliona yule mzungu akivuta Triga , lakini hakutaka kufa kizembe , aliipindisha Boti ile kwa upande mmoja wa kulia ina ikainama kiasi ambacho bega la Roma liligusa maji huku yeye akiinama na kichwa pia kugusa maji na boti ile kubinuka upande mmoja na kilichosikika hapo ni risasi mbili mfululizo zilizotua upande wa chini kabisa wa Boti.
Kwa jinsi Roma alivyokinga risasi ile kwa Boti ni kitendo ambacho mrembo aliekuwa pembeni hakuwahi kukishuhudia katika Maisha yake aliona kama yupo kwenye muvi.
Mzungu yule wa kike alishindwa kumlenga Roma kwani hakuwa akimuona kwa upande ambao walikuwa wapo ,kwa kitendo cha boti ya Roma kubinuka upande na nikama Roma alikuwa akifanya makusudi , baada ya wao kuona Roma amejiwekea kinga kwa kutumia boti ile , waligeuza kwa spidi kwenda upande mwingine na hapo mrembo yule alijikuta akizidi kupagawa , lakini alikuja kupiga mshangao mara ya boti ya Roma kurudi katika usawa wake , lakini kwenye boti hakukuwa na mtu na hata wale wazungu walishangaa kwa wakati mmoja na kujiuliza ni kitu gani kimetokea , walionekana kuhaha.
Umbali ambao Roma alikuwa amesimama na umbali ambao wazungu walikuwa wamesimama ilikuwa mita kama ishirini hivi.
Mrembo yule alikuwa kwenye hali ya mshangao na alijiambia huenda mwanaume yule Kazama chin na Risasi ile imempata ., hakutaka kujiuliza mara mbilimbili na yeye alijitupa ndani ya bahari huku akidhamiliia kufanya jambo la kiuokozi.
Huku nje wale wazungu walishangazwa na tukio hilo , lakini pia na wao walidhania mtu aliekuwa wakimshambulia atakuwa Kazama , lakini haikuwa hivyo kwani ile wanapunguza spidi ya boti yao kulitokea tukio kama la Dolpin kuruka sarakasi kwa kutokezea nje ya maji na yule mwanamke alivutwa kwa kushikwa kwenye mkono kwa nguvu na kuachia libunduki lake na baada ya kuvutwa alizamishwa kwenye maji na kukatulia tuli.
Wakati hayo yakiendelea mrembo yule mwingine alikuwa akitokelezea kwenye maji huku akionekana kuvuta pumzi na kurudi tena kupiga mbizi , huku akiacha kuangalia upande walikokuwa wale wazungu aliowaacha , alirudi tena ndani ya maji kwa ajili ya kumtafuta Roma .
Yule mzungu aliekuwa amebakia baada ya kuona tukio lile na yeye alijitosa katika maji, huku akiwa amevalia miwani ambayo ilionesha kumsaidia kuona akiwa ndani ya maji kama anavyokuwa nje , na hapo ndipo aliposhuhudia jambo la kutisha kabisa kwani alishuhudia Roma akiwa amemzamisha mwenzake chini kabisa ya maji. Kina ambacho hata yeye mwenywe hakuwa na ujasiri wa kwenda , kwani walikuwa wamegusa eneo la sakafu kwenye mawe .
Mzungu yule alimuona Roma akimvunja shingo mwenzake na aliishia kutoa kilio .
“Noo ..Nancy “wakati amepanua mdogo kumuita mwenzake , Roma alipanda kama mshale au unaweza kusema kama zile roketi zinazoenda masafa ya juu na ni kitendo cha kufumba macho na kufumbua Roma alimfikia yule mzungu na kwakua mzungu yule hakuwa kwenye kujiandaa kutokana na kushuduhudia tukio la mwenzake kuvunjwa shingo. Alijikuta ameshikwa na yeye kwa staili ya Roba shingoni na kuzamishwa chini ya maji .
Upande wa huku nje mrembo ambaye alionekana kuwa jasiri licha ya kuona bunduki na majambazi yale ya kizungu ambayo yalikuwa yanamshambulia Roma alitokezea nje tena , lakinni awamu hii akiwa amekata tamaa kwani alikuwa amemkosa Roma chini , lakini ile anaangalia upande wa wale wazungu hakuona mtu kwenye ile boti na kushangaa Zaidi , wakati akiendela kushangaa , aliaona mtu akitokezea kama samaki ma kuvuta boti na kuketi huku akiwa anavuja maji mwilini
Yule mrembo alipanda kwenye boti huku akiwa ni mwenye kushangaa na akiendelea kutafuta wale wazungu wamepotelea wapi , lakini hakuwaona .
“Vipi mrembo , mbona unashangaa hivyo”Aliongea Roma kama kawaida yake utadhani hakukuwa na tukio lililokuwa limetokea
Yule mwanamke bado alionekana kuwa nah ofu , alikuwa akiangalia ili wawaone wale wazungu , lakini kwake ni kama walikuwa wamepotea na alikuwa haamini kama wale wazungu wamepotea maana ni ghafla sana.
“Unaitwa nani mrembo?”Aliuliza Roma na kumfanya yule mwanadada amwangalie Roma kwa mshangao.
“Naitwa Donyi”Aliongea mwanadada huyu na Roma akatabasamu.
“Sasa Donyi nadhani ni muda wa kutawaza mshindi na mwenye kupata zawadi yake apate”
Comments