Reader Settings

Unaweza kurudi ulipoishia kupitia Maktaba.

Roma hakuwa ni mwenye kujali sana kuhusu maneno ya Edna  kwani muda huo alichokuwa anawaza ni kiwanja gani  anaweza kwenda kula bata , na angalau kujipatia kitumbua ambacho kinaweza kumtuliza  kwa siku  hio ya Wikiend.

Wakati akiwa anaingia kwenye Daraja  la  Kigambomi kuna gari aliitilia mashaka  kwani hisia zake zilimwambia kabisa gari hio ilikuwa ikimfatilia  , lakini licha ya kuwa na hisia hizo alitamani kulithibitisha hilo na ndio maanba alianza kuchukua chocho ambazo zilikuja kumfikisha  mtaa wa Chang`ombe  , lakini Gari ile bado ilikuwa nyuma yake.

“Kuna wapuuzi wananifatilia”Aliwaza Roma huku akiendelea kukumbuka kuwa gari ile ilikuwa karibu na nyumba anayoishi na kwa namna yoyote ile ni kwamba watu hao wanataarifa la eneo ambalo  anaishi  nah ii aliona ni hatari kwa yeye na kwa familia yake yaani Bi Wema na Edna.

“Ngoja kwanza niwapoteze “Aliwaza huku akiongeza spidi ya gari  na muda huu magari yalikuwa mengi barabarani  kwani ilikuwa ni muda wa jioni jioni hivi watu wakirejea majumbani , lakini licha ya magari hayo mengi haikumsumbua Roma kuendesha gari kwa spidi na kuanza kupita kila apatapo nafasi na alitumia  dakika chache tu gari iliokuwa inamfatilia  alikuwa ameipoteza  , lakini sasa alijishgaa kuona ameendesha gari umbali mrefu mpaka kufika Kawe.

“Bora niende zangu Beach”Aliwaza Roma na kuendesha gari kuelekea upande ilipo kuwepo Ufukwe wa Kawe.

Wakati anaingiza gari yake eneo maalumu la kuegeshea  magari wapo watu wengi waliokuwa wakimkodolea macho kutokana na uzuri wa gari yake.

“Bosi kuna boti  zipo hapa kama utahitaji”Aliongea kijana flani mara baada ya kumuona Roma akitoka kwenye gari, kijana huyo  alionekana kuvaa tisheti flani hivi ya kampuni iliokuwa imeanzishwa hivi karibuni ndani ya jiji la Dar es salaam ambayo ilikuwa  ikikodisha SpeedBoat , boti flani hivi  zipo kama pikipiki.

Roma alijikuta akitamani kweli kuendesha boti  na aliongozana na kijana yule mpaka upande ambao Boti hizi hukodishwa.

Baada ya kufanya malipo ya awali  , alionyeshwa upande ambao boti hizo zilikuwa zimeegeshwa  na Roma alisogea upande huo na kuchagua boti ambayo ilimvutia  na alionekana alikuwa akijua kweli boti hizo.

Baada ya kuridhika na chaguo lake alirudi   na kubadilisha nguo na kupewa mavazi ya ziada  kwani hakuwa  na mpango wa kuja ufukweni hivyo hakuwa na nguo  za fukwe.

Siku hii ndani ya eneo la fukwe kulikuwa kumechangamka mno  kiasi kwamba  kulikuwa kumependeza , kuna waliokuwa wachumba wakiwa ndani ya hili eneo , kuna  waliokuwa ndani ya  fukwe hii kama wanafamilia na pia kuna waliokuwa  wapo ndani ya  fukwe hii  wakiwa peke yao kubarizi.

Roma hakujali sana  juu ya watu hao, ila kwake muda huo ni kufurahia maji ya baharini kwa kutumia speedboat.

Upande  mwingine  kwenye maegesho ya magari , iliingia gari  aina ya Nissani nyeusi na kupaki pembeni ya  gari ya Roma na  wakashuka mwanamke mmoja  wa kizungu pamoja na mwanaume wa kizungu , wote wakiwa wamevalia Track suit  pamoa na tisheti , baada ya kushuka waliangalia gari ya Roma na kisha wakatingishiana vichwa kama ishara  na kisha walisogea upande wa fukwe.

 Baada ya kufika kwenye  fukwe walianza kuangaza macho yao kulia na kushoto   kama watu waliokuwa wakitafuta jambo Fulani  na ndani ya dakika kama mbili hivi  walijikuta wakipeana  ishara mara baada ya  kuona boti iliokuwa kwenye spidi  ikipotelea katikati ya maji.

Ni kitendo cha haraka sana mzungu yule wa kike alirudi kwenye gari na kutoa begi flani dogo na  kisha kutoka  na kuungana na mzungu wa kiume na kuelekea kwenye kampuni ambayo ilikuwa ikikodisha Speedboat na kulipia  moja  na dakika chache tu walionekana wakiwa kwenye boti ile huku wakiitoa kwa spidi kiasi kwamba watu walianza kushangaa kwa umahili wao. Na kwa  jinsi walivyokuwa wanaonekana kama ungewaangalia ungesema watu hao watakuwa ni wapenzi kwa namna yoyote ile ,kwani walikuwa wamependezana.

Roma alikuwa akiendesha mdogo mdogo huku akiwa ni mwenye kufurahia upepo  uliokuwa ukimpepea  machon kiasi cha kumpelekea kufumba macho.

“Hey! Bro , ilisikika sauti iliomwita Roma akiwa katikati ya maji kiasi cha kufumbua macho  , kwani muda wote alikuwa ameyafunga akifurahia  upepo, Na Romaa baada ya kugeuza macho yake alimuona msichana mrembo akiwa  kwenye  boat kama yake , alikuwa ni mrembo haswa kiasi kwamba  Roma pepo la ngono liliibuka  hapo hapo

Kimakadirio mwanamke aliekuwa mbele yake   alikuwa mdogo sana kiumri  kati ya miaka ishirini hivi kushuka na Roma alimkadiria mwanadada huyo kama mwanafunzi wa chuo kama tu atakuwa anasoma.

“Mambo mrembo?”

“Poa! Tunaweza kushindana?”

“Kushindana kufanya nini?”

“Kuendesha”Hapo Roma alimuelewa na kisha akatabasamu.

“Hautoweza kunishinda wewe”

“Hata mimi hautoweza kunishinda”Aliongea Mrembo na wote hawa wawili licha ya kwamba walikuwa wamekaribiana na boti zao ,lakini walikuwa wakuiongea kwa sauiti kubwa ili kusikilizana  kwani upepo ulikuwa mkali  kiasi kwamba sauti ilikuwa ikipotea.

“Sawa lakini lazima kuwe na zawadi kwa mshindi , ukiweza kunishinda nakupatia gari  yangu  niliokuja nayo”Aliongea Roma.

“Gari aina gani umekuja nayo  ambayo unaamini  ninaweza kuikubali kama sehemu ya zawadi kwa mshindi?”

“Aud Q8”Aliongea roma na kumfanya mwanadada huyu atabasamu kwani gari hio alikuwa akiijua vyema ugharama wake katika soko la magari duniani , ni gari ambayo sio chini ya milioni 200.

“Mimi ukiweza kunishinda nakupa mwili wangu leo?”Aliongea  yule mwanadada kwa kujiamini na kumfanya  Roma acheke.

“Hehe.. unaonekana unajiamini sana mremb?,o kumbuka kutimiza ahadi ”

“Ndio hakuna ambaye ashawahi kunishinda kwenye mbio za baharini , nina medali nyingi nilizopata chuoni”

“Chuo gani unasomea?”

“Yale university”Aliongea manadada huyu na kumfanya Roma atabasamu .

“Okey ! deal ule wako uende kinyume na  ahadi yako”

“Siwezi kwenda  kinyume na ahadi yangu ni moja ya sharia nilizojiwekea”

“Karembo sana haka  nitahakikisha nashinda nikakavue  nguo  nione kamebeba nini?”Aliwaza Roma  huku wakijiandaa kuanza mtanange na kuamua  mstari wa ushindi , mwanadada huyu mrembo ambaye jina bado hatumjua alionekana kujiamini mno.

“Ukute anafurahi mwenyewe atanishinda Looh!  yaani nikuvulie nguo mimi”Aliwaza mrembo huyu na  muda huo huo wakaanza kuendesha kwa spidi huku membo huyu akionekana kuwa imara kweli , kwani ni  ndani ya dakika moja tu alikuwa amemuacha mbali  kidogo Roma , lakini kwa Rroma hakuwa na wasiwasi hata kidogo ,alikuwa akiendesha kama  hataki vile.

Mwanadada aliekuwa mbele  , alionekana  kumdharau Roma na kuona hakuwa saizi yake , lakini ghafla wakati akiendelea na mawazo hayo , alipitwa na Roma kwa spidi ambayo haikuwa ya kawaida  na kumfanya mrembo huyu  ashangae na kuanza kuongeza Spidi, kwani Roma alikuwa ashamuacha hatua kadhaa mbele.

“Shi**t Atanishinda huyu”Aliongea huku akiichochea boti yake na ikaanza kusererka kiasi kwamba  kulionekana povu la maji ya  baharini likiwa limejitengeneza kwa nyuma.

Mchezo huu walikuwa wamewekeana umbali ambao walitakiwa kufika , kwa mbele kabisa kulionekana kukiwa na mnara ambao ndio mwanadada huyu alipendekeza  , japo ilikuwa katikati ya bahari kwenye maji mengi  ila hawakuongopa , lakini sasa , kadri alivyokuwa akijitahidi kuendesha  hakuwa akimfikia Roma na hapa  akili yake ilianza kupata moto na kujiuliza huyu mtu ni  wa namna gani kwani katika Maisha yake yote hajawahi kushindwa kwenye mchezo huo na anazo medali.

Mwanadada huyu mrembo alianza kujutia maamuzi ya kuuweka mwili wake Rehani aliona kabisa dalili za kuliwa zinaenda kutimia.

Roma na yeye hakuwa na utani kabisa mbele ya kitumbua , alihakikisha anashinda   na hilo alilikuwa akikaribia kulifanikisha kwani alikuwa akikaribia  eneo ambalo ndio mstari wa ushindi.

Mrembo huyu alijikuta macho yakimtoka mara baada ya kumuona mwamba Roma akipita  mnara  kwa spidi na kuwa mshindi.

“Shi**t nishaliwa leo”Aliongea huku akipunguza mwendo  lakini ghafla alimuona Roma akipiga kona  ya hatari sana kuzunguka mnara ule na  kuja upande ambao yupo kwa spidi ya hali ya juu sana kiasi kwamba mwanadada huyu alianza kujawa na hofu na kujiuliza ni  kitu gani mwanaume huyu asiemjua anafanya , lakini alikuja  kujua baada ya dakika chache ,  kwani ile Roma anamfikia yule mrembo aliisukuma bot ya yule mrembo kwa kutumia boat yake kwa nguvu na kuacha uwazi na hapo hapo  ikapita Boat nyinngine  sehemu ambayo boti ya mrembo yule alikuwa ameisimamisha   na ikawa ponea ya mrembo huyu.

“Pumbavu wana siraha”Aliongea Roma baada ya kuona mwanadada  wa kizungu kutoa bundiki yake kubwa na kumlenga , yule mrembo mwanzoni hakuwa akielewa kinachoendelea ila alipoangalia kwa umakini aliona  bunduki na kuanza kupatwa na hofu na kujiambia leo anakufa katikati ya bahari , na eneo walilokuwepo ni kama vile watu hawa walikuwa wakiwasubiria waende mbali ili kuanza kuwashambulia wakina Roma kwani ilikuw ani mbali na fukwe.

Roma  aliona yule mzungu akivuta Triga , lakini hakutaka  kufa kizembe  , aliipindisha Boti ile  kwa upande mmoja wa kulia ina ikainama kiasi ambacho  bega la Roma liligusa maji huku yeye akiinama na kichwa pia kugusa maji na boti ile kubinuka upande mmoja   na kilichosikika hapo ni  risasi mbili mfululizo zilizotua   upande wa chini kabisa wa Boti.

Kwa  jinsi Roma alivyokinga risasi ile kwa Boti  ni kitendo ambacho mrembo aliekuwa pembeni hakuwahi kukishuhudia  katika Maisha yake  aliona kama yupo kwenye muvi.

Mzungu yule wa kike alishindwa kumlenga Roma kwani  hakuwa akimuona kwa upande ambao walikuwa wapo  ,kwa kitendo cha boti ya Roma kubinuka upande na  nikama Roma alikuwa akifanya makusudi ,   baada ya wao kuona Roma amejiwekea kinga kwa kutumia boti ile , waligeuza kwa spidi kwenda upande mwingine   na hapo mrembo yule  alijikuta akizidi kupagawa , lakini alikuja kupiga mshangao mara ya  boti ya Roma kurudi katika usawa wake , lakini kwenye boti hakukuwa na mtu  na hata wale wazungu walishangaa kwa wakati mmoja  na kujiuliza ni kitu  gani kimetokea , walionekana kuhaha.

Umbali ambao Roma alikuwa amesimama na umbali ambao wazungu walikuwa wamesimama ilikuwa mita kama ishirini hivi.

Mrembo  yule alikuwa kwenye hali ya mshangao na alijiambia  huenda mwanaume yule Kazama chin na Risasi ile imempata ., hakutaka kujiuliza mara mbilimbili na yeye alijitupa ndani ya bahari huku akidhamiliia kufanya jambo la kiuokozi.

Huku nje wale wazungu walishangazwa na tukio hilo , lakini pia  na wao walidhania mtu aliekuwa wakimshambulia atakuwa Kazama , lakini haikuwa hivyo kwani ile wanapunguza spidi ya boti yao   kulitokea tukio kama la Dolpin  kuruka sarakasi kwa kutokezea nje ya maji  na yule mwanamke alivutwa   kwa kushikwa kwenye mkono kwa nguvu na kuachia libunduki lake  na baada ya kuvutwa  alizamishwa kwenye maji na kukatulia tuli.

Wakati hayo yakiendelea mrembo yule mwingine alikuwa  akitokelezea kwenye maji huku akionekana kuvuta pumzi na kurudi tena kupiga mbizi , huku  akiacha kuangalia upande walikokuwa wale wazungu aliowaacha  , alirudi tena  ndani ya maji kwa ajili ya kumtafuta Roma .

Yule mzungu aliekuwa amebakia  baada ya kuona tukio lile na yeye alijitosa katika maji, huku akiwa amevalia miwani  ambayo ilionesha kumsaidia kuona  akiwa  ndani ya maji kama anavyokuwa nje , na  hapo ndipo aliposhuhudia  jambo la kutisha kabisa kwani alishuhudia  Roma akiwa amemzamisha  mwenzake  chini kabisa ya maji. Kina ambacho hata yeye mwenywe hakuwa na ujasiri wa kwenda  , kwani walikuwa wamegusa eneo la sakafu kwenye mawe .

Mzungu yule alimuona  Roma  akimvunja shingo  mwenzake na aliishia kutoa  kilio .

“Noo ..Nancy “wakati amepanua  mdogo  kumuita mwenzake , Roma alipanda kama   mshale au unaweza kusema kama zile roketi zinazoenda masafa ya juu na ni kitendo cha kufumba macho na kufumbua Roma alimfikia yule mzungu na kwakua mzungu yule hakuwa kwenye kujiandaa kutokana  na kushuduhudia tukio la mwenzake kuvunjwa  shingo. Alijikuta  ameshikwa na yeye kwa staili ya Roba shingoni na kuzamishwa chini ya maji .

Upande wa huku nje mrembo   ambaye alionekana kuwa jasiri licha ya kuona  bunduki  na majambazi yale  ya kizungu ambayo yalikuwa yanamshambulia  Roma alitokezea nje tena , lakinni awamu hii akiwa amekata tamaa kwani alikuwa amemkosa Roma chini  , lakini ile anaangalia upande wa wale wazungu hakuona mtu kwenye ile boti na kushangaa Zaidi , wakati akiendela kushangaa , aliaona mtu akitokezea kama samaki ma kuvuta boti na kuketi huku akiwa anavuja maji mwilini

Yule mrembo alipanda kwenye boti  huku akiwa ni mwenye kushangaa na akiendelea kutafuta wale wazungu wamepotelea wapi , lakini hakuwaona .

“Vipi mrembo , mbona unashangaa hivyo”Aliongea Roma kama kawaida yake utadhani hakukuwa  na  tukio lililokuwa limetokea

Yule mwanamke bado alionekana kuwa nah ofu , alikuwa akiangalia  ili wawaone wale wazungu , lakini kwake ni kama walikuwa wamepotea na alikuwa  haamini kama wale wazungu wamepotea maana ni ghafla sana.

“Unaitwa nani mrembo?”Aliuliza Roma na kumfanya yule mwanadada amwangalie Roma kwa mshangao.

“Naitwa Donyi”Aliongea mwanadada huyu na Roma akatabasamu.

“Sasa Donyi nadhani  ni muda wa kutawaza mshindi na mwenye kupata zawadi yake apate”

Previoua Next