Masharti ya Waandishi

Writer Terms & Conditions

Tarehe ya Kuanza: Oktoba 1, 2025

Effective Date: October 1, 2025

1 Utangulizi / Introduction

Kwa kushiriki kama mwandishi kwenye FasihiNet, unakubali masharti yote yaliyoainishwa hapa. Masharti haya yanaelezea jinsi unavyoweza kuchapisha, kuuza, na kupata mapato kutoka kwa kazi yako.

By participating as a writer on FasihiNet, you agree to all terms outlined here. These terms explain how you can publish, sell, and earn from your work.

2 Umiliki wa Maudhui / Content Ownership

Maudhui yote unayochapisha kwenye FasihiNet yanabaki kuwa mali yako. Hata hivyo, unakubali kutupa ruhusa ya:

  • Kuonyesha maudhui yako kwenye jukwaa letu.
  • Kutangaza maudhui yako kupitia mitandao yetu ya kijamii na matangazo.
  • Kuuza maudhui yako kwa niaba yako kwenye jukwaa.

3 Mgawanyo wa Mapato / Revenue Share

Maudhui ya Kipekee (Exclusive Content)

Kwa vitabu vinavyopatikana pekee kwenye FasihiNet:

Ada ya Huduma / Service Fee: 20%
Mapato Yako / Your Earnings: 80%

Vitabu vya kipekee vinapata asilimia 80 ya mapato yote.

Maudhui Yasiyo ya Kipekee (Non-Exclusive Content)

Kwa vitabu vinavyopatikana kwenye majukwaa mengine pia:

Ada ya Huduma / Service Fee: 25%
Mapato Yako / Your Earnings: 75%

Vitabu visivyo vya kipekee vinapata asilimia 75 ya mapato yote.

4 Utoaji wa Fedha / Withdrawals

Kiwango cha Chini / Minimum Amount

TSH 5,000

Kiwango cha chini cha kutoa fedha

Muda wa Usindikaji / Processing Time

Ndani ya masaa 24

Siku saba za wiki

Masharti ya Utoaji Fedha:

  • Hakikisha taarifa za akaunti yako ya benki au M-Pesa ni sahihi.
  • Unaweza kuomba utoaji wa fedha mara moja tu kwa siku.
  • Ada za usindikaji zinaweza kutolewa kulingana na njia ya malipo uliyochagua.

5 Ulinzi wa Kisheria / Legal Protection

MUHIMU / IMPORTANT

Ulinzi wa kisheria unapatikana KWA MAUDHUI YA KIPEKEE PEKEE (Exclusive Content Only)

Kwa vitabu vya kipekee kwenye FasihiNet, tunatoa ulinzi wa kisheria kamili:

  • Hatua za Kisheria Dhidi ya Uvunjifu:

    Mtu yeyote atakayekamatwa kusambaza, kunakili, au kuuza maudhui yako ya kipekee bila ridhaa atafikishwa mahakamani. FasihiNet itachukua hatua za kisheria kamili dhidi ya uvunjifu wowote.

  • Ufuatiliaji wa Maudhui:

    Tunatumia teknolojia ya kisasa kufuatilia na kutambua maudhui yaliyochapiswa bila ruhusa mtandaoni.

  • Msaada wa Kisheria:

    FasihiNet itatoa msaada wa kisheria na gharama za kufikisha mahakamani waathiriwa wa uvunjifu wa maudhui ya kipekee.

  • Haki Miliki Inalindwa:

    Tunazingatia na kulinda haki miliki na usalama wa waandishi wote wa maudhui ya kipekee.

Kwa Maudhui Yasiyo ya Kipekee:

Vitabu visivyo vya kipekee (vinavyopatikana kwenye majukwaa mengine) HAVIPATI ulinzi wa kisheria kutoka kwa FasihiNet. Wewe unawajibika moja kwa moja kulinda maudhui yako kwenye majukwaa mengine.

6 Majukumu ya Mwandishi / Writer Responsibilities

  • Kuchapisha maudhui halali na yasiyokiuka haki za wengine.
  • Kusasisha sura mpya kwa wakati ili kuwafurahisha wasomaji wako.
  • Kuzingatia kanuni za jamii na kuepuka maudhui ya kuchukiza.
  • Kutoa taarifa sahihi kuhusu hali ya upatikanaji wa kitabu chako (kipekee au la).
  • Hakikisha unachapisha kazi ambayo ni yako au una haki za kisheria za kuitumia.

6.1 Sera ya Kusasisha Simulizi / Novel Update Policy

MUHIMU: Simulizi Zinazoendelea (Ongoing Novels)

Simulizi zote zenye hali ya "Ongoing" zinahitaji kusasishwa kwa mara kwa mara.

Sheria ya Miezi Miwili (2-Month Rule)

Simulizi yenye hali ya "Ongoing" ambayo HAIJASASISHWA kwa miezi miwili (2) mfululizo itaathiriwa kama ifuatavyo:

1.
Itatangaziwa kuwa "Haijaidhinishwa" (Unapproved Status)

Simulizi yako itaondolewa kwenye orodha za simulizi zilizoidhinishwa na hazitatokea kwenye ukurasa wa nyumbani au utafutaji.

2.
Kufichwa Kwa Umma (Hidden from Public)

Wasomaji hawataweza kuona au kufikia simulizi yako mpaka utakapoisasisha.

3.
Kupoteza Msimamo wa Upatikanaji (Loss of Visibility)

Simulizi yako haitapendekeza kwa wasomaji wapya na itapoteza nafasi yake kwenye orodha za wenye mwelekeo.

4.
Mapato Yatasimamishwa (Earnings On Hold)

MUHIMU: Mapato YOTE yanayohusiana na simulizi hii yatasimamishwa na HAYATAWEZA KUTOLEWA mpaka simulizi itakapoidhinishwa tena. Hii ni pamoja na mapato ya sura zilizosomwa kabla ya kusimamishwa.

Mapato yatasimamishwa mpaka mahitaji yote ya kuidhinishwa tena yakitimizwa.

Jinsi ya Kurudisha Idhini / How to Restore Approval

Ili kurudisha simulizi yako kwenye hali ya "Approved", LAZIMA utimize MAHITAJI YOTE yafuatayo:

📋 Mahitaji ya Kuidhinishwa Tena (Re-Approval Requirements):

  • Chapisha angalau SURA 3 MPYA

    Sura hizi ni pamoja na ile uliyoikusudia kuchapisha baada ya muda wa miezi 2.

  • Jumla ya maneno: SI CHINI YA 5,000 MANENO

    Sura 3 mpya lazima ziwe na angalau maneno 5,000 kwa jumla (wastani wa ~1,667 maneno kwa kila sura).

    📊 Mfano: Sura 1 (2,000 maneno) + Sura 2 (1,500 maneno) + Sura 3 (1,800 maneno) = 5,300 maneno ✅

Baada ya kukidhi mahitaji hayo:

  • Simulizi yako itaidhunishwa moja kwa moja bila kusubiri mkaguzi
  • Itaanza kuonekana kwa wasomaji tena na kurudi kwenye orodha za simulizi zilizoidhinishwa
  • 💰 MAPATO YOTE YATAACHILIWA (All Earnings Will Be Released)

    Mapato yaliyosimamishwa yataachiliwa mara moja na utaweza kuyatoa pamoja na mapato mapya.

Mapendekezo Bora / Best Practices
  • 💡 Chapisha angalau sura moja kila mwezi ili kudumisha simulizi yako ikiwa "active"
  • 💡 Ikiwa huwezi kuchapisha kwa muda, fikiria kubadilisha hali kuwa "Complete" au wasiliana nasi
  • 💡 Wajulishe wasomaji wako ikiwa unatoa mapumziko ya muda mrefu
Kumbuka / Remember

Sera hii haiathiri simulizi zenye hali ya "Complete". Simulizi zilizokamilika zinaweza kukaa kwenye jukwaa bila masharti ya kusasisha.

8 Kusitisha Ushiriki / Account Termination

FasihiNet ina haki ya kufunga au kusitisha akaunti ya mwandishi ikiwa:

  • Unachapisha maudhui yanayokiuka haki za wengine.
  • Unatumia njia za udanganyifu kupata mapato.
  • Unakiuka masharti yoyote yaliyoainishwa hapa.
  • Unachapisha maudhui ya kuchukiza, hatari, au yasiyo halali.

Kusitisha kunaweza kufanyika bila taarifa ya awali ikiwa kuna ukiukaji mkubwa.

9 Mabadiliko ya Masharti / Changes to Terms

Masharti haya yanaweza kubadilika wakati wowote kwa kuanzishwa kwa mikataba mpya au huduma za ziada. Tutakujulisha kwa wakati kupitia:

Email

Taarifa za Dashboard

Matangazo

Wasiliana Nasi / Contact Us

Kwa maswali yoyote kuhusu masharti haya, wasiliana nasi kupitia: